The Holy See
back up
Search
riga

HALMASHAURI YA KIPAPA
KWA AJILI YA MAZUNGUMZANO NA DINI MBALIMBALI

Wakristo na Waislam: Tuungane kushinda vurugu miongoni mwa wafuasi wa dini mbalimbali

UJUMBE KWA AJILI YA MWISHO WA RAMADHAN

Id al-Fitr 1431/2010 A.D.

Jijini Vatikani

 

Wapendwa Marafiki Waislam,

1. ‘ld Al-Fitr, inayohitimisha mwezi wa Ramadhan, kwa mara nyingine, inatupa fursa nzuri, ili, kwa niaba ya Halmashauri ya Kipapa kwa ajili ya Mazungumzano na Dini mbalimbali, kuwaletea matashi ya moyoni kuwatakia utulivu na furaha.

Mwezi huu wote mlijitoa kusali, kufunga, kuwasaidia wahitaji, na kuimarisha mahusiano ya familia na undugu. Mungu hataacha kuzibariki juhudi hizo!

2. Ninayo furaha kusema kwamba waumini wa dini nyingine, kwa namna ya pekee Wakristo, wako karibu nanyi kiroho katika siku hizi, kama inavyoshuhudiwa na mikutano mbalimbali ya kirafiki, ambayo mara nyingi inawezesha mabadiliko asili ya kidini. Ni furaha yangu kufikiri kwamba hata Ujumbe huu unaweza kutoa mchango chanya kwa ajili ya tafakari zenu.

3. Mada iliyopendekezwa mwaka huu na Halmashauri ya Kipapa: Wakristo na Waislam: Tuungane kushinda vurugu miongoni mwa wafuasi wa dini mbalimbali, kwa bahati mbaya, ni suala lenye mbinyo, walau katika maeneo kadhaa ulimwenguni. Kamati ya Pamoja kwa ajili ya mazungumzano iliyoundwa na Halmashauri ya Kipapa na Kamati ya Kudumu kwa ajili ya mazunguzano miongoni mwa dini zinazomwamini Mungu mmoja ya al-Azhar zilichagua mada hii kwa ajili ya kujifunza, kutafakari, na kubadilishana mawazo wakati wa mkutano wake wa mwisho wa mwaka (Cairo, -23 - Februari 24, 2010). Mniruhusu nishiriki nanyi hitimisho lilitolewa mwishoni mwa mkutano huu.

4. Kuna sababu nyingi zinazosababisha vurugu miongoni mwa waumini wenye mapokeo mbalimbali ya dini, ikiwa ni pamoja na: kupotosha lengo la dini kwa malengo ya kisiasa au mengineyo; ubaguzi kwa misingi ya ukabila, utambulisho wadini; migawanyiko na mivutano ya kijamii. Ujinga, umasikini, maendeleo duni ni vyanzo vya moja kwa moja au visivyo wazi vya vurugu hata ndani ya jumuiya za kidini. Ni vema serikali na viongozi wa dini watoe mchango wao ili kuepusha mazingira mengi hivi kwa ajili ya manufaa ya jamii nzima. Ni vema serikali zizingatie ubora wa sheria katika kuhakikisha haki ya kweli ili kuwakomesha wazuaji na waenezaji wa vurugu!

5. Yako pia mapendekezo muhimu yaliyotolewa na matini iliyotajwa: kufungua mioyo yetu kwa ajili ya kusameheana na kupatana, kwa ajili ya kukaa pamoja kwa amani kunakoleta faida; kutambua kile tunachokuwa nacho kwa pamoja na kuheshimu tofauti, kama msingi wa utamaduni wa mazungunzano; kutambua na kujali heshima na haki za kila mwanadamu bila kuingiliwa na upendeleo wowote unaohusiana na kabila au ushirikishwaji wa kidini; lazima kuendeleza sheria za haki zinazowahakishia usawa wa msingi kwa wote; kukumbuka umuhimu wa elimu kwa ajili ya heshima, mazungumzano na udugu katika nyanja mbalimbali za uelimishaji: nyumbani, shuleni, kanisani na misikitini. Kwa namna hiyo tutaweza kuzishinda vurugu miongoni mwa wafuasi wa dini mbalimbali na kukuza amani na mapatano miongoni mwa jumuiya za dini mbalimbali. Mafundisho ya viongozi wa dini, kadhalika vitabu vya shuleni vinavyoleta dini kwa namna iliyo halisi, pamoja na ufundishaji kwa jumla, vina msukumo imara juu ya elimu na malezi ya vizazi vipya.

6. Natumaini kwamba fikra hizi, hali kadhalika na majibu ambayo yatayaibuliwa ndani ya jamii, na pamoja na marafiki zenu Wakristo, zitachangia katika kuendeleza mazungumzano, kukua katika heshima na utulivu, kwa ajili ya hayo ninasihi Baraka za Mungu.

 

Jean-Louis Kardinali Tauran
Rais

Askofu Mkuu Pier Luigi Celata
Katibu

 

 
top