Index

Back Top Print

[BEELENESFRHUIDITLVNLPLPTSQSWUKVIZH]
 

MKUSANYIKO WA MAFUNDISHO YA KANISA KUHUSU JAMII

 

YALIYOMO

 

Barua ya Angelo Kardinali Sodano
Uwasilishaji wa chapisho

 

UTANGULIZI

UTU THABITI NA ULIOKAMILIKA

a.    Mwanzoni mwa milenia ya tatu
b.    Umuhimu wa Waraka Huu
c.    Kwa Utoaji wa Huduma ya Ukweli Uliokamilika Kumhusu Mtu
d.    Kwa Ishara ya Mshikamano, Heshima na Mapendo

 

SEHEMU YA KWANZA

SURA YA KWANZA

MPANGO WA MUNGU WA UPENDO KWA WANADAMU

I.      MATENDO YA MUNGU YA UKOMBOZI KATIKA HISTORIA YA ISRAELI
a.     Uwepo wa Mungu Wenye Hisani
b.     Asili ya Uumbaji na Matendo ya Kujitoa ya Mungu

II.     YESU KRISTO ANATIMIZA MPANGO WA UPENDO WA MUNGU
a.     Katika Yesu Kristo Linatimizwa Tendo Kuu la Historia ya Mungu Pamoja na Wanadamu
b.     Ufunuo wa Upendo wa Utatu Mtakatifu

III.   BINADAMU KATIKA MPANGO WA UPENDO WA MUNGU
a.     Upendo wa Utatu Mtakatifu, Asili na Lengo la Binadamu
b.     Wokovu wa Kikristo ni kwa Watu Wote na kwa Mtu Kamili
c.      Wanafunzi wa Kristo kama Uumbaji Mpya
d.     Wokovu Hupita Ufahamu wa Binadamu na Uhuru wa Mambo ya Dunia

IV.    MPANGO WA MUNGU NA UTUME WA KANISA
a.     Kanisa, Alama na Mlinzi wa Ufahamu Ulio Juu Kabisa ya Uwezo wa Binadamu
b.     Kanisa, Ufalme wa Mungu na Kufanya Upya Mahusiano ya Kijamii
c.      Mbingu Mpya na Dunia Mpya
d.     Maria na 'Ndiyo' yake Katika Kuitikia Mpango wa Upendo wa Mungu

 

SURA YA PILI

UTUME WA KANISA NA MAFUNDISHO YA KIJAMII

I.      UINJILISHAJI NA MAFUNDISHO YA KIJAMII
a.     Kanisa, Makao ya Mungu Pamoja na Wanaume na Wanawake
b.     Injili Hupenya na Kutajirisha Jamii
c.      Mafundisho ya Jamii, Uinjilishaji na Kumuenzi Binadamu
d.     Haki na Majukumu ya Kanisa

II.     ASILI YA MAFUNDISHO YA KANISA KUHUSU JAMII
a.     Ufahamu ulioangaziwa na Imani
b.     Katika Dialogia ya Kirafiki na Matawi yote ya Ufahamu
c.      Ufafanuzi wa Utume wa Kanisa katika Kufundisha
d.     Jamii Hupatanishwa Katika Haki na Upendo
e.     Ujumbe kwa Wanangu na Mabinti wa Kanisa na kwa Ajili ya Binadamu
f.      Katika Ishara Endelevu na Kufanya Upya

III.   MAFUNDISHO YA KANISA KWA NYAKATI ZETU: MAELEZO YA KIHISTORIA
a.     Mwanzo wa Njia Mpya
b.     Kutoka Rerum Novarum Mpaka Siku ya Leo
c.      Katika Mwanga na Mvuto wa Injili

 

SURA YA TATU

MTU NAFSI NA HAKI ZA BINADAMU

I.      MAFUNDISHO KUHUSU JAMII NA KANUNI YA MTU NAFSI

II.     MWANADAMU KAMA “MFANO WA MUNGU”
a.     Viumbe kwa Mfano wa Mungu
b.     Msiba mkuu wa Dhambi
c.      Dhambi Inayowafikia Wote, na Wokovu Unaowafikia Wote

III.   SURA MBALIMBALI ZA BINADAMU

A.     UMOJA WA NAFSI YA BINADAMU

B.     WAZI KWA MAMBO YALIYO NJE YA UFAHAMU WA BINADAMU NA UPEKEE WA MWANADAMU
a.     Wazi kwa Mambo ya Juu
b.     Pekee na Asiyekaririwa
c.      Heshima kwa Hadhi ya Binadamu

C.     UHURU WA MWANADAMU
a.     Tunu na Mipaka ya Uhuru
b.     Kifungo kinachounganisha Uhuru na Ukweli na Sheria ya Maumbile

D.     HADHI SAWA KWA WATU WOTE

E.     MAUMBILE YA KIJAMII YA WANADAMU

IV.    HAKI ZA BINADAMU
a.     Tunu za Haki za Binadamu
b.     Kuziainisha Haki
c.      Haki na Wajibu
d.     Haki za Watu na Mataifa
e.     Kujaza Pengo kati ya Andiko na Roho

 

SURA YA NNE

KANUNI ZA MAFUNDISHO YA KANISA KUHUSU JAMII

I.      MAANA NA UMOJA

II.     KANUNI YA MANUFAA KWA WOTE
a.     Maana na Mielekeo ya Msingi
b.     Wajibu wa Kila Moja katika Manufaa ya Wote
c.      Jukumu la Jumuiya ya Kisiasa

III.   KIKOMO CHA MALI KWA JUMLA
a.     Chanzo na Maana
b.     Kikomo cha Jumla cha Mali na Mali ya Binafsi
c.      Kikomo cha Jumla kuhusu Mali na Upendeleo kwa Maskini

IV.    KANUNI YA AUNI
a.     Chanzo na Umaana
b.     Viashirio Halisi

V.     USHIRIKI
a.     Maana na Thamani
b.     Ushiriki na Demokrasia

VI.    KANUNI YA MSHIKAMANO
a.     Maana na Thamani
b.     Mshikamano kama Kanuni ya Jamii na Fadhila ya Maadili
c.      Mshikamano na Ukuaji wa Kawaida wa Binadamu
d.     Mshikamano katika Maisha na Ujumbe wa Yesu Kristo

VII.   TUNU ZA MSINGI ZA MAISHA YA JAMII
a.     Uhusiano kati ya Kanuni na Tunu
b.     Ukweli
c.      Uhuru
d.     Haki

VIII. NJIA YA UPENDO

 

SEHEMU YA PILI

SURA YA TANO

FAMILIA, KIINI MUHIMU CHA JAMII

I.      FAMILIA, JAMII YA KWANZA KIASILI
a.     Umuhimu wa Familia kwa Mtu.
b.     Umuhimu wa Familia kwa Jamii

II.     NDOA NI MSINGI WA FAMILIA
a.     Thamani ya Ndoa
b.     Sakramenti ya Ndoa

III.   UDHAHANIA WA DHANA YA KIJAMII JUU YA FAMILIA
a.     Upendo na Malezi ya Jumuiya ya Watu
b.     Familia ni Mahali Pa Kutakatifuza Maisha
c.      Jukumu la Kuelimisha
d.     Utu na Haki za Watoto

IV.    FAMILIA KAMA MSHIRIKI MAKINI KATIKA MAISHA YA JAMII
a.     Mshikamano katika Familia
b.     Familia, Maisha ya Kiuchumi na Kazi

V.     JAMII KATIKA HUDUMA YA FAMILIA

 

SURA YA SITA

KAZI YA MWANADAMU

I.      MTAZAMO WA KIBIBLIA
a.     Wajibu wa Kuzalisha na Kuitunza Dunia
b.     Yesu, Mtu wa Kazi
c.      Wajibu wa Kufanya Kazi

II.     NGUVU YA UNABII KATIKA BARUA RERUM NOVARUM

III    HESHIMA YA KAZI
a.     Sehemu ya Ubinadamu Katika Kazi na Matokeo ya Kazi ya Binadamu
b.     Uhusiano Kati ya Nguvu Kazi na Mtaji
c.      Kazi, na Haki ya Kushiriki Kazi
d.     Uhusiano Kati ya Kazi na Umiliki wa Mali Binafsi
e.     Kupumzika Kazi

IV.    HAKI YA KUFANYA KAZI
a.     Kazi ni Jambo la Lazima
b.     Jukumu la Serikali na Vikundi vya Kijamii Katika Kukuza Haki ya Kufanya Kazi
c.      Familia na Kazi
d.     Wanawake na Haki ya Kufanya Kazi
e.     Ajira kwa Watoto
f.      Tatizo la Uhamiaji na Kazi
g.     Ulimwengu wa Kilimo na Haki ya Kufanya Kazi

V.     HAKI YA WAFANYAKAZI
a.     Haki ya Ujira Halali na Mgawanyo wa Mapato
b.     Haki ya Mgomo

VI.    MSHIKAMANO WA WAFANYAKAZI
a.     Umuhimu wa Kuungana
b.     Aina na Njia Mpya za Mshikamano

VII.   “MAMBO MAPYA” KATIKA ULIMWENGU WA KAZI
a.     Kuweka Kipindi Kipya cha Mpito Katika Historia
b.     Mafundisho ya Jamii “na Mambo” Mapya

 

SURA YA SABA

MAMBO YA KIUCHUMI

I.      MTAZAMO WA KIBIBLIA
a.     Mtu, Umaskini na Utajiri
b.     Mali Huwapo ili Igawiwe

II.     UADILIFU NA UCHUMI

III.   JITIHADA BINAFSI NA UJASIRIAMALI
a.     Ujasiriamali na Malengo Yake
b.     Nafasi na Wajibu wa Wamiliki Biashara na Usimamizi

IV.    TAASISI ZA KIUCHUMI KATIKA KUMHUDUMIA MTU
a.     Nafasi na Wajibu wa Soko Huria
b.     Amali ya Serikali
c.      Nafasi na Wajibu wa Vyombo vya Kati
d.     Akiba na Bidhaa Zitumiwazo

V.     MAMBO MAPYA” KATIKA SEKTA YA UCHUMI
a.     Utandawazi: Fursa na Hatari
b.     Mfumo wa Kifedha wa Kimataifa
c.      Nafasi ya Jumuiya za Kimataifa Enzi za Uchumi wa Kidunia
d.     Maendeleo Kamili ya Mwanadamu Katika Mshikamano
e.     Hitaji la Elimu zaidi na Malezi ya Kiutamaduni

 

SURA YA NANE

JAMII YA KISIASA

I.      MTAZAMO WA KIBIBLIA
a.     Utawala wa Mungu
b.     Yesu na Mamlaka ya Kisiasa
c.      Jumuiya za Kikristo za Mwanzo

II.     MSINGI NA MADHUMUNI YA JUMUIYA YA KISIASA
a.     Jumuiya ya Kisiasa, Mtu Nafsi na Jamii
b.     Kutetea na Kuhamasisha Haki za Binadamu
c.      Maisha ya Kijamii Katika Msingi wa Urafiki wa Kiraia

III.   MAMLAKA YA KISIASA
a.     Msingi wa Mamlaka ya Kisiasa
b.     Mamlaka Kama Nguvu ya Kimaadili
c.      Haki ya Pingamizi kwa Kufuata Dhamiri
d.     Haki ya Kupinga
e.     Utoaji Adhabu

IV.    MFUMO WA KIDEMOKRASI
a.     Tunu na Demokrasia
b.     Taasisi na Demokrasia
c.      Vipengele vya Uadilifu Katika Uwakilishi wa Kisiasa
d.     Vyombo vya Kushiriki katika Siasa
e.     Habari na Demokrasia

V.     JUMUIYA YA KISIASA KWA KUHUDUMIA JUMUIYA YA KIRAIA
a.     Thamani ya Jamii
b.     Kipaumbele cha Jumuiya ya Kiraia
c.      Matumizi ya Kanuni ya Auni

VI.    SERIKALI NA JUMUIYA ZA KIDINI

A.     UHURU WA DINI, HAKI MSINGI YA BINADAMU

B.     KANISA KATOLIKI NA JUMUIYA YA KISIASA
a.     Kujitawala na Uhuru
b.     Ushirikiano

SURA YA TISA

JUMUIYA YA KIMATAIFA

1.     VIPENGELE VYA BIBLIA
a.     Umoja wa Familia ya Binadamu
b.     Yesu Kristo, Mfano Halisi na Msingi wa Ubinadamu Mpya
c.      Wito wa Ukristo kwa Watu Wote

II.     KANUNI ZA MSINGI ZA JUMUIYA YA KIMATAIFA
a.     Jumuiya ya Kimataifa na Tunu Zake
b.     Mahusiano katika Msingi wa Mapatano kati ya Taratibu za Kisheria na za Kimaadili

III.   MUUNDO WA JAMII YA KIMATAIFA
a.     Manufaa ya Mashirika ya Kimataifa
b.     Hadhi ya Kisheria ya Kiti cha Kitume

IV.    USHIRIKIANO WA KIMATAIFA KWA AJILI YA MAENDELEO
a.     Ushirikiano wa Kuhakikisha Haki ya Maendeleo
b.     Vita dhidi ya Umaskini
c.      Deni la nje

 

SURA YA KUMI

UTUNZAJI WA MAZINGIRA

I.      VIPENGELE VYA BIBLIA

II.     MTU NA VITU VYOTE VILIVYOUMBWA

III.   UPEO WA MGOGORO KATIKA UHUSIANO KATI YA MTU NA MAZINGIRA

IV.    UWAJIBIKAJI WA WOTE
a.     Mazingira ni ya Manufaa Kwa Watu Wote
b.     Matumizi ya Bioteknolojia
c.      Mazingira na Mgawanyo wa Kushirikishana Rasilimali
d.     Mitindo Mipya ya Namna ya Kuishi

 

SURA YA KUMI NA MOJA

UHAMASISHAJI WA AMANI

I.      VIPENGELE VYA BIBLIA

II.     AMANI: TUNDA LA HAKI NA MAPENDO

III.   KUSHINDWA KWA AMANI: VITA
a.     Kujitetea Kihalali
b.     Kulinda Amani
c.      Wajibu wa Kuwalinda Wasio na Hatia
d.     Hatua Dhidi ya Wale Wanaotishia Amani
e.     Upunguzaji wa Silaha za Vita
f.      Kuushutumu Ugaidi

IV.    MCHANGO WA KANISA KWA AJILI YA AMANI

 

SEHEMU YA TATU

SURA YA KUMI NA MBILI

MAFUNDISHO KUHUSU JAMII NA UTENDAJI WA KANISA

I.      KAZI YA KICHUNGAJI KATIKA NYANJA YA KIJAMII
a.     Mafundisho kuhusu Jamii na Utamadunisho wa Imani
b.     Mafundisho Kuhusu Jamii na Kazi ya Kichungaji ya Kijamii
c.      Mafundisho Kuhusu Jamii na Malezi
d.     Kustawisha Dialogia
e.     Wenye Kuhusika na Uendeshaji wa Kazi ya Kichungaji ya Kijamii

II.     MAFUNDISHO KUHUSU JAMII NA UWAJIBIKAJI WA WALEI
a.     Waamini Walei
b.     Maisha ya Kiroho ya Waamini Walei
c.      Kutenda kwa Busara
d.     Mafundisho kuhusu Jamii na Vyama vya Walei
e.     Huduma Katika Sekta Mbalimbali za Maisha ya Kijamii

1.     Huduma kwa Binadamu
2.     Huduma katika Utamaduni
3.     Huduma katika Uchumi
4.     Huduma katika Siasa

 

HITIMISHO

KWA USTAARABU WA UPENDO

a.     Msaada Ambao Kanisa Hutoa kwa Watu wa Leo
b.     Kuanza Upya toka Imani katika Kristo
c.      Matumaini Thabiti
d.     Kujenga “Ustaarabu wa Upendo”

Faharisi ya Nukuu


Kutoka Vatikano
29 Juni, 2004

 

Sekretariati ya Ofisi Kuu”
N. 559. 332

Mhashamu,

Katika kipindi chake chote, na hasa katika kipindi cha miaka mia moja iliyopita, Kanisa halijaacha hata mara moja kwa mujibu wa Papa Leo XIII kuyaweka bayana kabisa yale “matamshi yake” yanayotilia mkazo masuala juu ya maisha katika jamii. Akiendelea kutoa maelezo ya kina na wakati huohuo akiuboresha ule utajiri wa urithi wa mababu juu ya Mafundisho ya Kanisa Katoliki kuhusu jamii, Papa Yohane Paulo II naye kwa upande wake amewahi kuchapisha nyaraka kubwa tatu za kipapa ambazo ni – Laborem Exercens, Sollicitudo Rei Socialis na Centesimus Annus – zinazoonesha hatua muhimu za Kikatoliki za kuzingatia katika eneo hili. Maaskofu wengi kutoka kila pembe ya dunia nao kwa upande wao, wamechangia kwa mapana na marefu siku za hivi karibuni katika kuyaelewa zaidi Mafundisho hayo ya Kanisa kuhusu jamii. Wanazuoni wengi kutoka kila bara nao pia wameonesha ubingwa wao katika kutoa michango ya suala hili.

1. Ilitegemewa, kwa hiyo, kuwa yote yaliyokusanywa baada ya juhudi hizo zote yawekwe pamoja kwa mpangilio mzuri unaoonesha misingi ya mafundisho ya Kikatoliki kuhusu jamii. Ni jambo la kutia moyo sana kuwa katika miaka ya hivi karibuni, Baraza la Kipapa linaloshughulika na masuala ya Haki na Amani limepania kuichukua na kuiendeleza kazi hii.

Nimefarijika kuona kwamba Chapisho hili la “Mkusanyiko huu wa Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii” hatimaye limechapishwa. Napenda kushirikiana nanyi kwa furaha kulitoa kwa waamini na kwa watu wote wenye mapenzi mema ili liwe kama chakula kwa malezi ya kimwili na ya kiroho kwa kila mmoja wenu peke yake na kwa jumuiya zote.

2. Kazi hii inaonesha pia jinsi manufaa ya mafundisho ya Kanisa Katoliki kuhusu jamii yanavyofanya kazi ya uinjilishaji (taz. Centesimus Annus, 54) kwa kuwa inaweka mahusiano ya binadamu na ya jamii katika mwanga wa Injili. Kanuni za mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanayotokana na sheria za asili yanaonekana kuimarishwa na kukomazwa katika imani ya Kanisa kwa njia ya Injili ya Kristo.

Kwa maana hiyo, watu wote, wanaume kwa wanawake, wanaalikwa wajisikie na wajione wenyewe kuwa viumbe wenye uwezo zaidi ya ule wa kibinadamu katika nyanja zote za maisha yao pamoja na zile zinazohusisha masuala ya kijamii, kiuchumi na kisiasa. Imani inakamilisha umaana wa familia inayotokana na ndoa ya mume mmoja na mke mmoja, familia ambayo inaunda kiini cha kwanza na cha muhimu sana cha jamii. Aidha, imani inatoa mwanga unaohusiana na heshima ya kazi ambayo, kama shughuli ya kibinadamu iliyokusudiwa kwa kumkamilisha binadamu ina umuhimu wa juu zaidi ya mtaji, na inaimarisha madai yao halali ya kushiriki katika kufurahia matunda yatokanayo na kazi.

3. Katika maandishi haya tunaweza kuona umuhimu wa tunu za kimaadili zitokanazo na sheria ya asili iliyoandikwa ndani ya dhamiri ya kila binadamu, na inalazimika kuitambua na kuiheshimu sheria hiyo. Ubinadamu leo unahitaji utendaji wa haki zaidi katika kuyashughulikia matukio mengi na makubwa ya utandawazi; unajishughulisha sana na ikolojia pamoja na mbinu sahihi za usimamizi wa masuala ya dhamiri za kitaifa bila hata hivyo, kusahau utaratibu wa sheria na utambuzi wa uwepo wa familia ya binadamu. Ulimwengu uliokuwa na kazi, ambao sasa umebadilishwa kabisa na teknolojia mpya unaonesha viwango vya ubora wa pekee wa vitu. Lakini kwa bahati mbaya, teknolojia hiyo mpya lazima pia ikubali kuwa imeleta aina mpya ya hali ya kuyumbayumba na kutotengamaa kwa maisha ya watu, unyonyaji na hata hali ya utumwa katika jamii hizohizo ambazo zinadhaniwa kuwa zimefaidika na hiyo teknolojia mpya na kupata utajiri. Katika sehemu mbalimbali duniani, kiwango cha ustawi kinazidi kuongezeka, lakini pia kuna hatari ya ongezeko la idadi ya watu kuwa maskini, na kwa sababu mbalimbali tofauti kati ya nchi maskini na tajiri inazidi kuongezeka. Soko huria, mchakato wa kiuchumi na mtazamo chanya vinaonesha mipaka ya ukomo wake. Kwa upande mwingine lile chaguo la Kanisa la kuzipendelea nchi maskini ni chaguo la kimsingi kabisa, na hata kwa hiyo, Kanisa linawashauri watu wengine wote wenye mapenzi mema kufanya hivyo.

Kwa hiyo, ni wazi kwamba Kanisa haliwezi kushindwa kujifanya lisisikike mintarafu “vitu vile vipya” (Res novae) vinavyofanana na vile vya kisasa kwa sababu ni jukumu lake kuwaalika watu wote kufanya kile wanachoweza kufanya ili kuleta ustaarabu halisi na thabiti unaoelekea zaidi na zaidi kwenye ukamilifu wa maendeleo ya binadamu katika mshikamano.

4. Siku hizi waamini walei wanashughulika sana na masuala ya kijamii au ya kiutamaduni kwa kufuata maelekezo ya Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatikano unaokumbusha na kushauri kwamba walei wanaoshughulikia mashauri yanayohusu mambo ya kidunia na wajitahidi kuyaweka katika mpangilio mzuri unaokubalika kadiri ya mapenzi ya Mungu (taz. Lumen Gentium, 31). Kwa hiyo, tunaweza kwa urahisi kuelewa umuhimu mkubwa wa malezi ya walei kuwezesha utakatifu wa maisha yao na nguvu ya ushuhuda wao kuchangia katika maendeleo ya mwanadamu.

Maandishi haya yametayarishwa ili yawasaidie katika utendaji wao huu wa siku hadi siku.

Aidha, inapendeza kuona jinsi Makanisa mengine na Jumuiya za Kikristo pamoja na Dini zingine wanavyoshiriki katika masuala mengi yaliyokusanywa na kuandikwa katika kitabu hiki. Kitabu kimeandikwa kwa namna ambayo hakitakuwa na manufaa kwa wale tu walio ndani ya Kanisa husika (ab intra), yaani Wakatoliki, lakini pia walio nje ya Kanisa hili (at extra). Kwa kweli, wale wote waliobatizwa, kama tulivyo sisi na hata wafuasi wa dini zingine pamoja na watu wengine wote wenye mapenzi mema, wanaweza kupata nafasi nzuri ya tafakari kwa kuyasoma maandishi haya, na hivyo kumotishwa na kuhamasishwa kujiendeleza wenyewe na pia kuwaendeleza wengine katika masuala muhimu na ya lazima katika maisha yao.

5. Wakati akitarajia kwamba maandishi haya yatawasaidia binadamu katika harakati zao za kuyatafuta yale ambayo yana manufaa kwa wote, Papa anamsihi Mungu awabariki wale wote watakaotumia muda wao kuyatafakari yalioandikwa katika chapisho hili. Kwa heshima na taadhima, namalizia maneno yangu kwa kukutakia kila la heri na kukupongeza wewe Mwadhama na washiriki wako katika Baraza la Kipapa linaloshughulikia masuala ya Haki na Amani kwa kufanikisha kazi hii muhimu.

Wako mwaminifu katika Kristo,
Angelo Kardinali Sodano
(
Mkuu – Sekretariati ya Ofisi Kuu Vatikano)


UWASILISHAJI WA CHAPISHO

Nafarijika kuwasilisha chapisho hili la “mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii,” chapisho ambalo limetayarishwa kwa ushauri na maombi ya Papa, linalotoa kwa kifupi, lakini kwa ukamilifu unaostahili mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii.

Kuyarekebisha masuala yanayohusu jamii kwa nguvu ya Injili, masuala ambayo watu wote, wanaume kwa wanawake wamwaminio Yesu Kristo limekuwa muda wote changamoto na limebaki kuwa changamoto hadi kufikia milenia hii ya tatu ya kipindi cha Ukristo. Utangazaji wa “Habari Njema” ya wokovu, mapendo, haki na amani uliofanywa na Yesu Kristo, kwa kweli haujapokewa na ulimwengu wa leo ulioharibiwa kama mambo yanavyojidhihirisha yenyewe kwa vita, umaskini na udhalimu. Kutokana na sababu hiyo, wanaume na wanawake wa siku hii ya leo, wanahitaji neno la Injili zaidi kuliko hapo awali, imani inayookoa, matumaini yanayoangaza na sadaka inayoonesha upendo.

Kanisa ni mahiri sana katika kuyashughulikia masuala yanayowahusu binadamu na linaendelea kusonga mbele kuelekea kwenye “mbingu mpya” ya “nchi mpya” (2 Pet 3 : 13), kwa mujibu wa imani na kwa kujihusisha kimatendo, jambo ambalo Kanisa linataka liwe wazi kwa kila mtu ili kusaidia watu kuishi kwa kuzingatia upeo wa maana halisi wa maisha. “Gloria Dei vivens homo”: binadamu anayeishi kwa mujibu wa hadhi ya utu wake anatoa utukufu kwa Mungu aliyewapa watu wote, wanaume kwa wanawake, hadhi hii ya utu wa ubinadamu.

Watu wanashauriwa kuyasoma maandishi haya ili wadumishe na kuendeleza hali yao ya utendaji wa Ukristo katika sekta ya kijamii, hususani hali ya kiutendaji ya walei ambao wanahusika na eneo hili kwa namna ya pekee; maisha yao yote yanaonekana kama kazi ya uinjilishaji, kazi ambayo inazaa matunda. Kila mwamini lazima, awali ya yote ajifunze kumtii Bwana kwa nguvu ya imani akifuata mfano wa Mtakatifu Petro “Bwana mkubwa tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha tusipate kitu, lakini kwa neno lako nitashusha nyavu” (Lk 5:5). Kila msomaji wa maandishi haya ambaye ana “mapenzi mema” ataweza kuelewa kwa nini Kanisa linaingilia kati masuala ya sekta hii ya kijamii ambayo ukiangalia kijuujuu unaweza kudhani kuwa sio sekta yake (Kanisa). Hata hivyo, wasomaji haohao wataona sababu na mantiki ya kuwa na mabadiliko yanayowezesha mazungumzo na ushirikiano katika kuhudumia manufaa kwa wote.

Mwenzangu aliyenitangulia katika kushughulikia kazi hii hasa ile sehemu ya maandalizi, Mwadhama Hayati Francois – Xaver Kardinali Nguyen van Thuan na kupata bahati ya kukamilisha kutokana na afya yake kuwa mbaya na hatimaye kufariki. Kazi niliyokabidhiwa ambayo sasa nami naitoa kwa wale watakaoisoma ina mhuri wa ushahidi adhimu wa Msalaba Mwadhama Hayati Francois - Xaver Kardinali Nguyen Van Thuan ambaye alibaki shupavu katika imani yake wakati wa miaka ile ya udhalimu uliokuwa umeshamiri katika nchi ya Vietnam. Shahidi huyu ataipokea shukrani yetu kwa kazi yake nzuri na ya thamani kubwa aliyoifanya kwa mapendo na kwa kujitolea. Nina uhakika kabisa kuwa atawabariki wale wote watakaochukua muda wao mfupi kuzipitia kurasa za kitabu hiki.

Namwomba Mtakatifu Yosefu, Baba mlezi wa mwokozi wetu, mume wa mama Bikira Maria, mlezi wa Kanisa la ulimwengu na wa kazi ili ayawezeshe maandishi haya kuzaa matunda tele katika maisha ya jamii na yawe pia chombo cha utangazaji Injili kwa ajili ya upatikanaji wa haki na amani.

Jijini Vatikano, 2 Aprili, 2004, Kumbukumbu ya Mtakatifu Francis wa Paola.

 

Mwadhama Renato Raffaele Kardinali Martino
Mwenyekiti

+Giampaolo Crepaldi
Katibu

 

 

 

MKUSANYIKO WA MAFUNDISHO YA KANISA KUHUSU JAMII


UTANGULIZI

UTU THABITI NA ULIOKAMILIKA

 

a. Mwanzoni mwa Milenia ya Tatu

1. Kanisa linazidi kusogea zaidi na zaidi kuelekea kwenye milenia ya tatu ya enzi hii ya Kikristo mithili ya mahujaji, likiongozwa na Kristo “Mchungaji Mkuu” (Ebr 13:20). Yeye ni ule “Mlango Mtakatifu” (taz. Yn 10:9) tulioingilia wakati wa Jubilei Kuu ya mwaka 2000.[1] Yesu Kristo ni njia ya Ukweli na Uzima (taz. Yn 14:6): tukitafakari sura ya Bwana tunathibitisha imani na matumaini yetu kwake yeye ambaye ndiye Mwokozi na kikomo cha historia.

Kanisa linaendelea kuongea na watu wa mataifa yote kwa kuwa ni kwa kupitia jina la Yesu tu, watu wote, wanaume kwa wanawake, hupata wokovu. Wokovu ambao unapatikana kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo “kwa thamani” (1Kor 6:20. taz. Pet 1 18-19), unakamilishwa baada ya kufa katika maisha yale mapya yanayowasubiri wale wanaoshika na kufuata sheria, lakini wokovu huo hupenya na kusambaa pia hapahapa duniani na kushuhudiwa katika mambo kadhaa kama yale ya kiuchumi na kazi ya kiteknolojia, kiutamaduni, kimawasiliano, kisiasa na kiuhusiano katika jumuiya ya kimataifa. “Yesu alifika kuleta wokovu uliokamilika, wokovu unaomzunguka mtu kamili na binadamu wote kwa ujumla wao na hivyo kufungua matarajio ya ajabu ya upendo wa Mungu.”[2]

2. Mwanzoni mwa Milenia hii ya Tatu, Kanisa halichoki kuitangaza Injili inayoleta Wokovu na uhuru wa kweli, uliokamilika katika hali halisi ya masuala ya dunia hii. Linaukumbuka ule ushauri wa Mtakatifu Paulo alioutoa kwa mfuasi wake Timotheo unaosema “lihubiri neno, uwe tayari,

wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho, maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia walimu makundi makundi, wenyewe watajipatia walimu wanaofaa matakwa yao, kwa kuwa wana masikio ya utafiti; nao watajiepusha wasisikie yaliyo kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo. Bali wewe, uwe na kiasi katika mambo yote, vumilia mabaya, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiliza huduma yako (2 Tim 4:2-5).

3. Kanisa pia linatoa mafundisho yake kuhusu jamii kwa watu waliopo sasa ambao wapo katika msafara mmoja nalo. Kwa kweli, Kanisa “linapotekeleza jukumu lake la kutangaza Injili linatoa ushuhuda kwa jina la Kristo, kwa hadhi yake na kwa wito wake kwa kushirikiana na watu. Linamfundisha mtu yale yote yanayohitajika kwa kutoa haki na kwa kupata amani kwa kuzingatia hekima ya Kimungu.”[3] Mafundisho haya yana kiungo chake cha msingi sana kitokanacho na amani ya wokovu uliokamilika, matumaini yaliyojaa Haki na Upendo unaowafanya wanadamu wote wawe kama ndugu wa kweli katika Kristo. Hii ni alama dhahiri ya upendo wa Mungu kwa ulimwengu alioupenda hivi hata akamtoa Mwanae pekee” (Yn 3:16). Amri mpya ya mapendo inazijumlisha familia zote za binadamu na haina ubaguzi wa aina yoyote wala mipaka kwa sababu wokovu ulioletwa na Kristo umesambaa na kuenea “hata mwisho wa nchi” (Mdo 1:8).

4. Pale Binadamu wanapotambua kuwa Mungu anawapenda, ndipo wanapokiri kuwa si vyema kuwa na ubinafsi bali ni vizuri kushirikiana na jamii zao katika mahusiano yao ya ubinadamu. Wanaume kwa wanawake wanaofanywa waonekane “wapya” kwa mapendo ya mwenyezi Mungu wana uwezo wa kuzirekebisha sheria na hali halisi ya mahusiano kati yao. Wanaweza hata kuyageuza na kuyarekebisha maumbile ya kijamii. Watu hawa wana uwezo wa kuleta amani pale uliposhamiri ugomvi , uwezo wa kujenga na kuendeleza mahusiano ya kindugu pale penye uhasama na uwezo wa kutafuta na kupata haki

pale mtu anapomnyonya mwenzake. Ni mapendo tu ambayo yanaweza kubadili na kurekebisha kwa haraka sana uhusiano uliopo kati ya watu. Hii ni taswira inayomruhusu kila mtu mwenye mapenzi mema kufahamu marefu na mapana ya masuala ya haki na maendeleo ya binadamu katika ukweli na wema.

5. Mapendo yanakabiliana na kazi nyingi na Kanisa lina hamu ya kutoa mchango wake kwa kutumia mafundisho ya kijamii. Mafundisho haya yanamhusu mtu kwa ujumla wake kama alivyo na yanaelekezwa kwa watu wote. Kuna ndugu wengi tu wahitaji wanaosubiri msaada, kuna pia watu wengi wanaokandamizwa ambao wanahitaji kutendewa haki, kuna wale wasio na kazi wanaosubiri kuajiriwa. Pamoja na hao wote kuna watu wengine wanaongoja tu wapate heshima wanayostahili kuipata. “Inawezekanaje kwamba hadi siku hii ya leo bado kuna watu wanaokufa kwa njaa? Watu wasiojua kusoma na kuandika? Watu wanaoshindwa kupata hata yale mahitaji ya msingi tu ya dawa? Watu wanaoishi bila hata kibanda chenye paa la kufunika vichwa vyao? Mpangilio na mtiririko huu wa mambo ya umaskini ni urefu na unaweza kuendelezwa na usifikie mwisho na hasa kama unaorodhesha pia aina zile mpya za umaskini. Aina hizi mpya ni kama zile mara nyingi zinazozigusa sekta za watu matajiri na za vikundi vinavyoelekea kukata tamaa kutokana na ukweli kuwa havioni maana ya maisha na kuendelea kuishi katika maisha kama haya na hivi kujiingiza katika utumiaji wa dawa za kulevya. Wasiwasi wa vikundi vingine vya hawa waliokata tamaa unaotokana na ule ukweli kwamba pindi uzee ukiwafika au wakiumwa hawatakuwa na watu wa kuwapa huduma na pia katika hali ya uzee wanakabiliwa na tishio la kuenguliwa polepole na kutengwa na jamii. Tuendeleeje kubaki tu bila kujali yale maafa ya kiikolojia yanayoweza kutukumba, maafa ambayo yanasababisha maeneo mengi ya dunia yetu yasiweze kukaliwa na watu na hivyo kujijengea uadui na binadamu? Au kutokana na matatizo ya kutokuwa na amani ambayo mara nyingi hutishiwa na machafuko ya vita au kwa kutokuheshimu haki za kimsingi za watu wengi na hasa za watoto?”[4]

6. Mapendo ya Kikristo yanaelekezwa kwenye kujikana na kwenye kutoa ushauri, na pia kujiingiza katika uendelezaji wa miradi ya kiutamaduni na ya kijamii. Mapendo haya yanachochea utendaji wa kimaendeleo unaoamsha ari ya wale wote wenye mapenzi mema kutoa mipango yao. Ubinadamu unaelekea kuelewa vizuri zaidi kwamba ubinadamu huo umeunganishwa kwa njia moja inayohitaji makubaliano ya majukumu ya pamoja, majukumu ambayo yametiwa msukumo kwa njia ya ubinadamu ulio kamili na uliochangiwa pia. Inaonekana kwamba ubinadamu huo mara nyingi huwa na mwelekeo unaolazimishwa uwe kama ulivyo na vigezo vya kiteknolojia na vya kiuchumi na unahitaji utambuzi mkubwa zaidi wa kimaadili unaokuwa dira ya njia yake ya kawaida. Wakipigwa na butwaa na uvumbuzi mwingi wa kiteknolojia, watu wote wanaume kwa wanawake wa leo, wanatamani maendeleo haya yanayofanywa kuwa yaelekezwe kwenye manufaa halisi ya mwanadamu wa leo na wa kesho.

b. Umuhimu wa Waraka Huu

7. Mkristo anafahamu kwamba katika mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii kuna kanuni za kufanyia tafakari; vigezo vya kutolea hukumu na miongozo ya utekeleaji, vitu ambavyo huwa ndivyo vya mwanzo kwa ukuzaji wa ubinadamu wenye mshikamano na uliokamilika, kwa hiyo, kuyatangaza na kuyaweka mafundisho haya bayana ni suala kweli la kiuchungaji linalostahili kupewa kipaumbele ili watu wote, wanaume na wanawake, waelimishwe na wawezeshwe kutoa tafsiri sahihi ya maisha na wajitahidi kupata njia muafaka ya utendaji “Ufundishaji na uenezaji wa haya mafundisho ni sehemu ya ujumbe wa Kanisa wa Uinjilishaji.”[5]

Ni kutokana na hali hii kwamba chapisho la waraka huu litoalo madokezo muhimu yanayohusu mafundisho ya Kanisa juu ya jamii likionyesha uhusiano wa mafundisho haya na ile aina mpya ya uinjilishaji,[6] likionekana kuwa chapisho lenye manufaa makubwa, Baraza la Kipapa la masuala ya Haki na Amani na ambalo linawajibika kwa kila hali na yote yaliyochapishwa katika waraka huu, limeandaa maandiko ya chapisho kwa kushirikiana na Wajumbe na Washauri wa idara mbalimbali za Vatikano, Mabaraza ya Maaskofu ya nchi mbalimbali na wataalamu mabingwa wa masuala yaliyoongelewa.

8. Waraka huu unakusudia kutoa maelezo ya mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii kwa kina na kwa mpangilio muafaka hata kama ni kwa madokezo tu. Mafundisho haya ni mapato ya tafakari makini ya Majisterio na ni alama ya msimamo ambao daima Kanisa linao kwa mujibu wa uaminifu wake kwa neema ya wokovu ulioletwa na Kristo na kwa kuzingatia mapenzi ya majaliwa ya binadamu. Katika waraka huu, masuala ya kijamii yanayogusa vipengele vya theolojia, falsafa maadili, utamaduni na uchungaji yamefafanuliwa vizuri na kwa mpangilio wa kueleweka. Kwa njia hii, ushahidi wa manufaa ya makabiliano ya Injili na matatizo ambayo binadamu hukumbana nayo katika historia ya maisha yao unadhihirishwa. Kwa kusoma na kujifunza yale yalioandikwa katika maandishi haya ya Ufupisho Makini wa Mafundisho ya Kanisa Kuhusu Jamii, ni vema kukumbuka kuwa madondoo haya ya Majisterio yamekusanywa kutoka nyaraka zilizoandikwa na waandishi mbalimbali. Pamoja na nyaraka na barua za Kipapa na nyaraka zilizoandikwa na ofisi za Papa. Naomba msomaji atuvumilie tukirudia kusema kwamba Majisterio za ngazi mbalimbali zimehusishwa katika kuyaandaa maandishi haya. Waraka huu umevifafanua vipengele vile vya mafundisho ya Kanisa juu ya jamii vinavyoonekana kuwa ni vya msingi. Namna ya kuyatumia mafundisho haya na vipengele vyake yameachiwa Mabaraza ya Maaskofu ambayo yatafanya hivyo kulingana na hali halisi ya mahali husika.[7]

9. Waraka huu unatoa picha kamili ya mfumo wa kimsingi wa mkusanyo wa maandishi yote juu ya mafundisho ya Kanisa Katoliki juu ya jamii. Picha hii inaturuhusu kuyashughulikia kwa usahihi zaidi masuala ya hivi sasa yanayohusu jamii, masuala ambayo lazima yafikiriwe kwa ujumla wake kwa kuwa yanajionyesha kwa mwingiliano unaojitokeza wazi na hivyo kuwa na ushawishi kati yao unaolifanya jambo hili liwe na mvuto unaoleta wasiwasi kwa familia yote ya binadamu. Ufafanuzi wa mafundisho ya Kanisa juu ya jamii unalenga kutoa mapendekezo ya njia yenye mpangilio na utaratibu katika kupata majibu na ufumbuzi wa matatizo na kutambua kuwa maamuzi yanayochukuliwa yanalingana na hali na hali halisi ya ukweli wa mambo na ili mshikamano na matarajio viwe na matokeo kwa mujibu hali ilivyo hivi sasa. Kwa kweli kanuni hizi zina uhusiano wa karibu sana na zinasaidiana katika kutoa ufafanuzi kwa kuwa zote zinaonyesha anthropolojia za Kikristo,[8] matokeo ya ufunuo wa mapendo ya Mungu kwa binadamu. Hata hivyo, tusisahau kwamba jinsi muda unavyosonga mbele na mazingira ya kijamii yanavyozidi kubadilika, kutakuwa na haja ya kuziangalia tena fikira hizi zilizogusiwa na kuzifanya zionekane za kisasa zaidi ili zitoe ufafanuzi wa alama za nyakati.

10. Waraka huu umetolewa kama chombo cha utambuzi wa kimaadili na kiuchungaji, utambuzi ambao unahusu matukio hata ya wakati huu wetu. Umetolewa pia kama mwongozo kwa matumizi ya kila mtu peke yake au kwa matumizi ya watu kwa pamoja ili kuchochea na kusukuma mitazamo na maamuzi yatakayowahusu watu wote kuangalia hali zao za baadaye kwa imani na matumaini. Aidha, umetolewa kama msaada kwa waamini ili uwasaidie kuelewa mafundisho ya Kanisa katika maeneo ya masuala yanayohusu maadili ya kijamii. Kwa kuanzia hapo kunaweza kupatikana mikakati mipya inayoendana na matakwa yetu ya wakati huu kulingana na rasilimali na mahitaji ya binadamu. Zaidi ya yote kunaweza kutokea katika Kanisa motisha ya kuvumbua tena ule wito unaofaa kwa haiba tofauti inayokusudiwa kwa madhumuni ya uinjilishaji wa mpango wa kijamii kwa sababu “wanakanisa wote ni wanahisa katika ulimwengu huu.”[9] Kwa kifupi maandishi haya yanapendekezwa yawe kichocheo cha mazungumzo na wale wote wanaowatakia mema binadamu kwa moyo wao wote.

11. Waraka huu unakusudiwa utumiwe na Maaskofu watakaoamua mbinu zipi zinazofaa zaidi zitumiwe kwa kuufafanua na kuutangaza. Kwa kweli, waraka huu ni sehemu ya Maaskofu “manus docendi ” kwa kuwawezesha kufundisha kwamba vitu vya ulimwengu huu pamoja na taasisi zake za kidunia vimepangwa kulingana na Mipango ya Mungu Muumba wetu, kwa ajili ya wokovu wa watu na vinaweza kutoa michango mkubwa tu kwa ujenzi wa Mwili wa Kristo.[10] Mapadre, watawa wanaume na wanawake, wacha Mungu na kwa jumla wale wanaowajibika na malezi watapata katika waraka huu mwongozo wa kufundishia na kitendeakazi chao. Kwa walei wanaotafuta Ufalme wa Mungu “kwa kujishughulisha na mamlaka ya kidunia kulingana na utashi wa Mungu“[11], watakuta katika maandishi haya utaalamu unaohusu huo ujumbe wao. Jumuiya za Kikristo zitaweza kuyageukia maandishi haya kwa kutaka msaada katika kuchanganua masuala mbalimbali bila upendeleo katika kuyaeleza wazi maneno ya Injili, bila kuyabadilibadili katika kuunda kanuni za kutafakari kwa maamuzi na miongozo kwa ajili ya utendaji[12]

12. Waraka huu unapendekezwa pia utumiwe na ndugu zetu wa Makanisa mengine, Jumuiya zingine za Makanisa, wafuasi wa dini zingine pamoja na wale wote wenye mapenzi mema ambao wamejitolea kutoa huduma kwa manufaa ya watu wote. Hao wote wanaombwa waupokee kama kazi yenye manufaa iliyotokana na mikono ya binadamu, kazi ambayo ina kila dalili ya uwepo wa Roho wa Mungu. Hii ni hazina ya vitu lukuki vya kale na vipya (taz. Mt 13:52) ambavyo Mungu anapenda kutushirikisha katika kumtolea yeye mwenyewe sadaka aletaye “kila kitolewacho kilicho kamili” (Yak 1:17). Ni ukweli kwamba dini na tamaduni mbalimbali siku hizi zipo tayari na wazi kukaribisha mazungumzo na kuona kuwa kuna haja ya kuungana ili kukuza haki, undugu na amani pamoja na ukuaji wa binadamu kwa jumla.

Kanisa Katoliki linaungana na Makanisa mengine pamoja na jumuiya zingine za dini katika ngazi ya tafakari ya Mafundisho ya Kanisa ngazi ya kiutendaji. Kwa ushirikiano huo, Kanisa Katoliki linaamini kwamba kutokana na ule urithi wa pamoja wa mafundisho ya kijamii uliohifadhiwa na mapokeo hai ya watu wa Mungu, kuna uwezekano wa kuwa na motisha na pia mwelekeo wa kuwa na ushirikiano wa karibu zaidi katika ukuzaji wa haki na amani.[13]

c. Kwa Utoaji wa Huduma ya Ukweli Uliokamilika Kumhusu Mtu

13. Waraka huu ni tendo la Kanisa la huruma kwa watu wote, wake kwa waume, wa wakati huu. Kanisa linawaachia urithi wa mafundisho yake juu ya jamii kwa kufuata mtindo wa mazungumzo ambao Mungu mwenyewe kwa kumpitia mwanae wa pekee aliyejifanya mtu “asemavyo na rafiki yake” (Kut 33:11,Yn 15:14-15) na anatembea kati yao (taz. Bar 3:38).”[14] Likichukua mwongozo wa Hati ya kiuchungaji “Gaudium et Spes” waraka huu pia unamweka “mtu aliyekamilika akiwa na mwili na roho, moyo na dhamiri, akili na utashi”[15] kama ufunguo wa ufafanuzi wake kwa maana hiyo Kanisa “ halisukumwi na malengo ya kidunia, lakini linatafuta lengo moja: kuendeleza kazi ya Kristo mwenyewe kwa kuongozwa na fadhili za Roho wa Mungu kwa sababu Kristo alifika hapa duniani kutoa ushuhuda wa ukweli, kuokoa na si kuhukumu, kuhudumia na si kuhudumiwa.”[16]

14. Kwa msaada wa waraka huu, Kanisa linakusudia kuchangia katika kutoa jibu linaloonyesha ukweli wa nafasi ya mtu kwa mujibu wa hulka yake katika jamii. Mada hii inazikabili tamaduni na staarabu mbalimbali ambazo zinajitahidi kuonyesha hekima na busara katika kulishughulikia suala hili. Maswali yaliyokuwa yakiulizwa kuhusu nafasi ya mtu katika jamii ni ya karne nyingi na yamekuwa yakijitokeza kwa sura mbalimbali kama ile ya dini, falsafa na usanii wa kishairi. Watu wa tamaduni hizi mbalimbali wamekuwa wakitoa maelezo yao kuhusu ulimwengu huu na pia kuhusu jumuiya ya binadamu katika jitihada yao ya kutaka kuelewa maana ya maisha haya. Mimi ni nani? Kwa nini kuwe na mateso, maovu, vifo, wakati huohuo kuna maendeleo makubwa yaliyokwisha kufanyika? Kuna manufaa gani basi ya hayo maendeleo iwapo gharama yake imekuwa isiyoweza kuvumilika? Mambo yatakuwaje baada ya maisha haya? Haya ni maswali ya msingi ya kujiuliza, maswali ambayo yanaonyesha mwelekeo wa maisha ya binadamu.[17] Kuhusu hili tunayakumbuka yale maonyo yasemayo “Jitambue mwenyewe” yalioandikwa kwa kuchongwa kwenye lango la hekalu kule Delphi. Maonyo haya yanatoa ushahidi wa kweli wa kimsingi kwamba mtu ameumbwa kama mtu kwa sababu kwa asili yake yeye ana hulka ya kujitambua mwenyewe.

15. Majawabu yatakayopatikana kutokana na maswali yanayohusu nafasi ya mtu na maumbile yake ya asili katika jamii, ndiyo yatakayoamua uwepo wa binadamu, jamii na historia yake. Madhumuni ya maandishi haya ni kusaidia kutoa mchango wa majibu kwa maswali haya. Maana halisi ya kuwepo kwa binadamu kwa kweli kunaonekana katika uhuru wa uchunguzi unafanyika katika utafutaji wa dira hiyo ya mwelekeo. Maswali yaliyodokezwa hapo awali huifanya akili ya binadamu na utashi wake iendelee kufanya uchunguzi huo. Maswali haya ni kipimo cha kiwango cha juu sana cha maumbile ya binadamu kwa kuwa yanahitaji majibu yanayopima kiwango cha uwajibikaji wake kwa kuwepo kwake hapa duniani. Aidha, kuwepo kwake huku kumedodoswa kwa vidokezo vya maswali yanayoulizwa kwa mfano: “kwa nini kuwe na viumbe” yanapochunguzwa kwa kina na yanapounganishwa na matokeo ya utafiti wa lile jawabu la mwisho, hapa ndipo akili ya binadamu inapofikia kilele chake kwa sababu majawabu yanayopatikana yanagusa Imani ya Dini. Hali ya Imani ya Kidini inawakilisha ile maana yenyewe halisi ya ubinadamu kwa sababu huoni unapoishia upeo wa maumbile yake ya kuweza kufikiri kirazini. Hali husababishwa na hamu kubwa ya kutafuta ukweli, hamu ambayo ni huru na ni ya mtu mwenyewe binafsi anayoielekeza kwa masuala ya Kimungu.[18]

16. Maswali ya msingi ambayo yamekuwa yakifuatana na maisha ya binadamu tangu hapo awali kabisa yanaonekana kuchukua sura tofauti, kwa kuwa na umuhimu zaidi siku hizi kwa sababu ya kujitokeza kwa changamoto nzitonzito na kuwepo kwa hali na umaana wa maamuzi yanayovikabili vizazi vya sasa.

Moja ya hali ya kwanza kabisa ya changamoto hizo nzito zinazowakabili binadamu siku hizi ni ule ukweli wenyewe wa kuwepo kwa kiumbe kinachoitwa mtu. Mipaka na mahusiano kati ya hali ya asili ya maumbile, teknolojia na maadili ni masuala yanayohitajika kwa kila mtu binafsi na kwa pamoja katika kujibu maswali kama binadamu ni kiumbe wa aina gani? kiumbe huyu anaweza kufanya nini na angetazamia afanye nini zaidi ya haya anayofanya. Changamoto ya pili inaonekana katika kuelewa na kudhibiti mfumo unaotambua mawazo na misimamo ya dini mbalimbali pamoja na tofauti zao katika kila ngazi kama vile namna yao ya kufikiri, namna ya kufanya chaguzi za kimaadili, jinsi utamaduni wao ulivyo, ushirikishaji wa dini pamoja na falsafa ya ukuzaji wa jamii na ile ya binadamu. Changamoto ya tatu ni ile ya utandawazi ambayo umuhimu wake ni mpana na ni wa maana zaidi kuliko ule wa kiuchumi kwa kuwa historia imeshuhudia kuanza kwa enzi mpya inayojali lengo la ukomo wa binadamu.

17. Wafuasi wa Yesu Kristo wanajiona kuwa wanahusika na maswali haya. Wao pia wanayabeba katika mioyo yao na wanataka kuchukua jukumu pamoja na watu wengine wote, wanaume kwa wanawake, kutafuta ukweli na maana halisi ya maisha ya kila mmoja peke yake na maisha ya jamii. Wanatoa mchango mkubwa katika utafutaji huo kwa ushahidi wenye ukarimu usio na kipimo. Mwenyezi Mungu amezungumza na watu wake, wanaume na wanawake, kwa karne zote za historia ya ulimwengu huu. Kwa kweli, hata yeye mwenyewe akaja kujiingiza katika historia ili aweze kuzungumza na watu wake ana kwa ana na awafunulie mpango wake wa ukombozi wa haki na wa undugu. Kwa njia ya Yesu Kristo, Mwanae aliyejifanya mtu, Mungu ametuweka huru kutokana na dhambi na ametuonesha njia ya kufuata na pia kikomo cha kukifanyia mikakati ya kukifikia.

d. Kwa Ishara ya Mshikamano, Heshima na Mapendo

18. Kanisa husafiri likifuatana na binadamu wote katika njia yake ya kihistoria. Kanisa hilo lipo katika dunia hiihii yetu. Ingawa si la ulimwengu huu (taz. Yn 17: 14 – 16), lakini limealikwa kuuhudumia ulimwengu huu kwa kuzingatia wito wake wa ndani kabisa. Fikra hii ambayo inazungumziwa pia katika maandishi haya imekita mizizi yake katika ile imani kwamba kama kulivyo na umuhimu kwa ulimwengu huu kulitambua Kanisa kama kitu halisi cha kihistoria kuna pia umuhimu kwa Kanisa kukitambua kile lilichokipata kutokana na historia hiyo na pia kutokana na ukuzaji wa taifa la binadamu.[19] Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatikano umetoa maelezo fasaha kuhusu mshikamano, heshima na mapendo kwa familia yote ya binadamu kwa kujihusisha nalo katika mazungumzo ya pamoja juu ya migogoro mingi iliyojitokeza, “likiukaribisha ule mwanga wa Injili na hapohapo likiziweka rasilimali za ukombozi mikononi mwa taifa la binadamu, rasilimali ambazo Kanisa limekabidhiwa na Mwanzilishi wake kwa msaada wa Roho Mtakatifu. Ni mtu mwenyewe ambaye lazima akombolewe na ni jamii ya binadamu ambayo lazima ikarabatiwe ili ionekane kama mpya.”[20]

19. Kanisa ambalo katika historia ni alama ya mapendo ya Mungu na wito kwa binadamu wote wa kuungana kama watoto wa yule Baba mmoja,[21] linakusudia kwa kuutumia waraka huu unaohusu mafundisho ya jamii kutoa pendekezo kwa watu wote, ubinadamu unaolingana na viwango vya mapendo vya mpango wa Mungu katika historia, ubinadamu wa pekee na ulio kamili wenye uwezo wa kuunda utaratibu mpya wa kiuchumi, kijamii na kisiasa uliojengeka katika heshima na uhuru wa kila mtu, utaratibu ambao utaundwa kwa amani, haki na mshikamano. Ubinadamu huu unaweza kuwa ni wa kweli iwapo watu wote na jamii zao wataweza kukuza maadili ya kijamii ndani mwao na hatimaye kuyaeneza katika jamii nzima.” Halafu kwa msaada wa neema, watu wapya ambao watakuwa wajenzi wa ubinadamu mpya.”[22]

 

SEHEMU YA KWANZA

“Mtazamo wa Kitheolojia unahitajika kwa ajili ya kutafsiri na vilevile kwa ajili ya kutatua matatizo ya wakati huu katika jamii ya wanadamu.”

(Centesimus Annus, 55)

 

SURA YA KWANZA

MPANGO WA MUNGU WA UPENDO KWA WANADAMU

I. MATENDO YA MUNGU YA UKOMBOZI KATIKA
HISTORIA YA ISRAELI

 

a. Uwepo wa Mungu Wenye Hisani

20. Kila mang'amuzi ya kidini yaliyo ya kweli, katika mapokeo yote ya kiutamaduni, yanaelekeza kwenye hisia ya Fumbo, ambayo si mara chache, yaweza kutambua, walau kwa sehemu, sura ya uso wa Mungu. Kwa upande mmoja, Mungu anaonekana kuwa asili ya kila kilichopo, kama ambaye anawahakikishia wanaume na wanawake, wanaoishi kwa utaratibu katika jamii, hali ya msingi ya maisha, akiwapatia mema yote yaliyo ya lazima. Kwa upande mwingine, Yeye anaonekana kuwa kama kipimo cha kila linalotakiwa kuwa, kama yule ambaye anahoji matendo ya binadamu – yawe ya kibinafsi ama ya kijamii – kuhusiana na matumizi ya mema hayohayo, katika mahusiano na watu wengine. Kwa hiyo, katika kila mang'amuzi ya kidini, umuhimu ni katika sehemu ya zawadi na majitoleo, ambayo yanaonekana ndiyo yenye mkazo katika kung'amua kwamba binadamu huishi pamoja na wengine duniani. Hali kadhalika, yatokanayo na hali hiyo, hugusa dhamiri ya binadamu, ambayo imeitwa kutunza kwa uwajibikaji pamoja na wengine zawadi iliyopokelewa. Ukweli huo unashuhudiwa na utambuzi wa wote wa kanuni kuu "Kanuni ya Dhahabu", inayoelezea kuhusu mahusiano ya watu yaani ile amri iliyoagizwa kwa wanaume na wanawake na Fumbo [la Mungu]: "Basi yoyote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo" (Mt 7:12).[23]

21. Katika historia ya mang'amuzi ya kidini yaliyo ya wote, ambamo wanadamu hushiriki kwa namna mbalimbali, ule ufunuo wa Mungu kwa watu wa Israeli ulioendelea hatua kwa hatua, unakuwa wa pekee. Ufunuo huo unajibu kwa namna isiyotarajiwa na kwa njia inayoshangaza jitihada za mwanadamu kuchunguza juu ya umungu. Maana hutoa jibu kwa matendo na matukio ya kihistoria – yaliyo angavu na yenye kueleweka – ambayo kwayo upendo wa Mungu kwa wanadamu unadhihirika. Katika Kitabu cha Kutoka, Bwana Mungu anamwambia Musa maneno haya: "Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao. Nami nimeshuka ili niwaokoe kutoka mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, na pana, nchi ijaayo maziwa na asali" (Kut 3:7-8). Uwepo wa Mungu wenye hisani ambao unadokezwa na jina lake lenyewe, jina analomfunulia Musa, "Mimi Niko Ambaye Niko" (Kut 3.14) – hudhihirishwa katika ukombozi kutoka utumwani na katika ahadi. Na hayo yanakuwa matendo ya kihistoria, ambayo ni asili ya namna ya watu wa Mungu kujitambua wenyewe kwa pamoja, kwa njia ya kupatiwa uhuru na nchi ambayo Mungu anawapa.

22. Uhiari wa utendaji huo wa Mungu katika historia uliendana daima na wajibu wa kushika agano, lililowekwa na Mungu na kukubaliwa na Israeli. Juu ya mlima Sinai, jitihada ya Mungu inachukua sura ya matendo halisi anapofanya agano na watu wake, ambao Bwana anawapa Amri Kumi (taz. Kut 19-24). "Amri Kumi" (Kut 34:28; taz. Kum 4:13; 10:4) "zinaeleza maana ya kuwa watu wa Mungu kulikoanzishwa kwa njia ya agano. Maisha adili ni jibu kwa tendo la upendo wa Bwana. Ndiyo kukiri, kutoa uchaji na ibada ya shukrani kwa Mungu. Ni kushiriki katika mpango ambao Mungu anaushughulikia katika historia."[24]

Amri Kumi, ambazo ni dira ya pekee ya maisha na zinaonesha njia ya uhakika ya kuishi katika uhuru kutoka utumwa wa dhambi, zinabeba maelezo maalumu ya sheria ya kimaumbile. Amri Kumi "zinatufunza utu wa kweli wa binadamu. Zinafunua wajibu za lazima kwa namna isiyo ya moja kwa moja, haki za msingi zilizomo katika hali ya binadamu."[25] Zenyewe zinaeleza maadili ya kibinadamu ya popote. Katika Injili Yesu anamkumbusha yule kijana tajiri kwamba Amri Kumi (taz. Mt 19:18) "ni kanuni za lazima za maisha yote ya kijamii."[26]

23. Katika Amri Kumi hutoka wajibu ambao hauhusiani tu na uaminifu kwa Mungu mmoja aliye wa kweli, lakini pia kuhusu mahusiano ya kijamii miongoni mwa watu wa Agano. Mahusiano hayo yanarekebishwa, hasahasa, kwa [amri ile] iliyoitwa haki ya maskini: Kama akiwapo mtu maskini pamoja nawe, nduguyo mmojawapo, . usifanye moyo wako kuwa mgumu, wala usimfumbie mkono wako nduguyo maskini; lakini mfumbulie mkono wako kwa kweli, umkopeshe kwa kweli yatoshayo haja yake katika ahitajiayo" (Kum 15:7-8). Hayo yote yahusika pia na wageni: "Na mgeni akikaa pamoja nawe katika nchi yako, usimdhulumu. Mgeni akaaye pamoja nawe atakuwa kama mzalia kwenu; mpende kama nafsi yako; kwa maana ninyi mlikuwa wageni katika nchi ya Misri. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu" (Law 19:33-34). Hivyo, zawadi ya uhuru na ya Nchi ya Ahadi, na zawadi ya Agano juu ya mlima Sinai na ya Amri Kumi zimefungamana na matendo ambayo yanatakiwa kurekebisha – kwa haki na mshikamano – maendeleo ya jamii ya Waisraeli.

24. Miongoni mwa kanuni nyingi zenye kuleta sura thabiti ya mtindo wa kujitoa na kihisani na kushirikishana katika haki, ambayo Mungu anaelekeza, mna sheria ya mwaka wa sabato (inayoadhimishwa kila baada ya miaka saba) na ile ya mwaka wa Jubilei (inayoadhimishwa kila baada ya miaka hamsini)[27] Haki hizo zimekuwa kama mwongozo mkuu – ingawa haukutimizwa kamwe kikamilifu kimatendo katika historia ya watu wa Israeli – kwa maisha yao ya kijamii wala ya kiuchumi. Pamoja na kudai mashamba yapumzike bila kulimwa, sheria hizo zinadai ufutaji wa madeni pamoja na maachilio ya jumla ya watu na vitu: kila mmoja ana uhuru wa kurudi kwenye familia yake na kumiliki tena urithi wake.

Sheria hizo zina lengo la kuhakikisha kwamba tendo la wokovu lililotimizwa katika Kutoka na uaminifu kwa Agano si tu kanuni ya msingi katika kujenga maisha ya kijamii, kisiasa na kiuchumi ya watu wa Israeli, lakini pia ni kanuni ya msingi katika kukabiliana na masuala ya umaskini kiuchumi na ukosefu wa haki kijamii. Kanuni hiyo imewekwa ili kubadili, daima na kutoka kwa ndani, maisha ya watu wa Agano, kusudi maisha yao yalingane na mpango wa Mungu. Ili kuondoa kabisa ubaguzi na tofauti za kiuchumi zilizosababishwa na mabadiliko ya kijamii-kiuchumi, kila baada ya miaka saba kumbukumbu la Kutoka na Agano hutafsiriwa katika matendo ya kijamii na ya kisheria, kusudi kurudisha dhana za umiliki, madeni, mkopo na mali kwenye maana yake ya ndani kabisa.

25. Maagizo ya miaka ya sabato na miaka ya Jubilei yanabeba aina ya mafundisho kuhusu jamii kwa kifupi.[28] Maagizo hayo yanaonesha jinsi kanuni za msingi za uadilifu na mshikamano wa kijamii zinavyotokana na majitoleo ya tendo la wokovu lililotimizwa na Mungu. Pia kwamba zenyewe tu hazina maana ya kukosoa vitendo vinavyotawaliwa na maslahi na malengo ya kibinafsi; bali lazima kwamba, zaidi ya hayo, zikawe kama utabiri wa mambo yajayo, kama hoja za kikanuni za rejea ambazo kila kizazi katika Israeli kinatakiwa kuzifuata, ikiwa kinataka kuwa na uaminifu kwa Mungu wake.

Kanuni hizo zinakuwa kiini cha mahubiri ya Manabii, ambayo yanajaribu kuziweka moyoni. Roho wa Bwana, aliyemiminwa katika moyo wa binadamu – ndivyo wahubirivyo Manabii – atazifanya hisia hizohizo za uadilifu na mshikamano, zilizomo moyoni mwa Bwana Mungu, zistawishe mizizi ndani mwenu (taz. Yer 31:33; na Eze 36:26-27). Hapo mapenzi ya Mungu, yaliyoelezwa katika Amri Kumi zilizotolewa kule Sinai, yataweza kustawisha mizizi kwenye mtima wa binadamu. Mchakato wa kuweka moyoni unajenga na kuchochea zaidi kutenda kijamii kwa kina na uhalisia, kwa kuwezesha fikra za haki na mshikamano kuenea zaidi na zaidi popote, [kwa vile] watu wa Agano wanavyotakiwa kuwa nazo mbele ya watu wote, wanaume kwa wanawake wa kila taifa.

b. Asili ya Uumbaji na Matendo ya Kujitoa ya Mungu

26. Tafakari ya Manabii na ile ya Maandishi ya Kihekima, inagusia ufunuo wa kwanza na asili yenyewe ya mpango wa Mungu kwa ajili ya wanadamu wote, pale inapofikia kutamka kanuni ya msingi ya kwamba vitu vyote viliumbwa na Mungu. Katika ungamo la imani la Israeli, kutamka kwamba Mungu ni Muumba si tu kueleza imani ya kinadharia tu, lakini pia kutambua upeo halisi wa utendaji wake Mungu, uliojaa fadhili na rehema, kwa ajili ya binadamu. Maana, Mungu anavijalia viumbe vyote vilivyopo uwepo na uzima. Mwanamume na mwanamke, walioumbwa kwa sura na mfano wake (taz. Mwa 1:26-27), wanaitwa kwa sababu hiyo kuwa ishara inayoonekana wazi na chombo madhubuti cha ufadhili wa Mungu katika bustani ambapo Mungu aliwaweka kama wakulima na walinzi wa mema ya uumbaji.

27. Ni katika utendaji huru wa Mungu ndiko tunakopata maana halisi ya uumbaji, hata kama umeharibiwa na matendo ya dhambi. Kwa kweli, simulizi la dhambi ya asili (taz. Mwa 3:1-24) linaeleza jaribu lenye kurudiarudia na hali ya machafuko ambamo wanadamu wote wanajikuta wamo baada ya anguko la wazazi wa kwanza. Kumwasi Mungu ni kujiweka mbali na macho ya upendo wake na kujaribu kuendesha kila mmoja binafsi maisha na utendaji wake duniani. Kuvunja uhusiano wa ushirika na Mungu, kunasababisha kuvunjika kwa umoja wa ndani wa nafsi ya mtu, kwa upande wa mahusiano ya ushirika kati ya mwanamume na mwanamke, pia kwa upande wa mahusiano mazuri kati ya binadamu na viumbe vingine.[29] Katika mfarakano huo wa asili lazima kutafuta mizizi ya ndani ya kila ubaya unaoathiri mahusiano ya kijamii kati ya watu.  Pia kuangalia kila hali katika uchumi na katika siasa inayochezea utu wa mwanadamu, haki na kuvuruga mshikamano.

 

II. YESU KRISTO
ANATIMIZA MPANGO WA UPENDO WA MUNGU

 

a. Katika Yesu Kristo Linatimizwa Tendo Kuu la Historia ya Mungu Pamoja na Wanadamu

28. Wema na huruma ambavyo vinasukuma matendo ya Mungu na kuleta uwezo wa kuyaelewa vinakuwa karibu sana na mwanadamu, hadi kuchukua sura ya mwanadamu Yesu, ambaye ni Neno aliyejifanya mwili. Katika Injili ya Mt. Luka, Yesu anaeleza huduma yake ya kimasiya kwa maneno ya Isaya ambayo yanakumbusha maana ya kinabii ya Jubilei: "Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, na vipofu kupata kuona tena, kuwaacha huru waliosetwa, na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa" (Lk 4:18-19; taz. Isa 61:1-2). Kwa hiyo, Yesu anajiweka, katika mstari wa mbele wa utimilifu, siyo tu kwa sababu yeye hutimiza yaliyoahidiwa na kutazamiwa na Israeli, lakini pia, kwa undani zaidi, kwa sababu katika yeye tendo kuu katika historia ya Mungu na watu linatimizwa. Yeye hutangaza: "Aliyeniona mimi amemwona Baba" (Yn 14:9). Yaani, Yesu ni ufunuo wazi na halisi wa jinsi Mungu anavyotenda kwa ajili ya wanaume na wanawake.

29. Upendo unaomsukuma Yesu katika huduma yake kati ya watu ni ule upendo aliouonja katika umoja wake wa ndani na Baba. Agano Jipya linaturuhusu kuingia kwa undani katika mang'amuzi ambayo Yesu mwenyewe anaishi na kushirikisha, ya upendo wa Mungu Baba yake – "Aba" – na, kwa namna hiyo, linatuwezesha kuingia moyoni mwa uzima wa kimungu. Yesu anatangaza rehema ya Mungu yenye kuwaokoa wale wote anaowakuta kwenye njia yake, kuanzia maskini, waliotengwa, na wadhambi. Yeye huwaalika wote kumfuasa, kwa sababu yeye mwenyewe ndiye wa kwanza kuutii mpango wa upendo wa Mungu, naye hufanya hivyo kwa njia ya pekee kabisa, kama mjumbe wa Mungu duniani.

Jinsi Yesu anavyojitambua kuwa Mwana wa Mungu inaonesha wazi mang'amuzi hayo ya asili. Mwana alipewa yote na Baba, na alipewa bure: "Na yote aliyo nayo Baba ni yangu" (Yn 16:15). Naye, kwa upande wake, anao utume wa kuwafanya watu wote washiriki katika zawadi hii, na katika umwana wake: "Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki, kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu" (Yn 15:15).

Kwake Yesu, kutambua upendo wa Baba ni kuyafanya matendo yake kulingana na majitoleo na huruma ya Mungu, maana ni hayo ambayo huzaa uzima mpya. Hivyo anakuwa – kwa njia ya maisha yake – mfano na kielelezo kwa wanafunzi wake. Wafuasi wake Yesu wanaitwa kuishi kama yeye alivyoishi, baada ya Pasaka yake ya kifo na ufufuko, pia kuishi katika yeye na kwa njia yake, kwa ajili ya zawadi tele ya Roho Mtakatifu, aliye Mfariji, mwenye kutia ndani ya mioyo ya watu mtindo wa maisha yake Yesu mwenyewe.

b. Ufunuo wa Upendo wa Utatu Mtakatifu

30. Kwa mshangao usiokoma walio nao wale ambao wameng'amua upendo wa Mungu usioweza kuelezeka (taz. Rum 8:26), Agano Jipya hufumbata, katika mwanga wa ufunuo uwazi wa upendo wa Utatu Mtakatifu uliojaliwa katika Pasaka ya Yesu Kristo, maana ya msingi ya Umwilisho wa Mwana wa Mungu na ya utume wake miongoni mwa watu. Mtakatifu Paulo anaandika: "Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu? Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye?" (Rum 8:31-32). Mt. Yohane naye anatumia maneno kama hayo, akisema: "Hili ndilo pendo: si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu" (1Yoh 4:10).

31. Uso wa Mungu, uliofunuliwa zaidi na zaidi katika historia ya wokovu, hung'aa kwa ukamilifu katika uso wa Yesu Kristo msulibiwa na mfufuka kutoka kwa wafu. Mungu ni Utatu: Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, tofauti na umoja, kwa sababu Mungu ni ushirika wa upendo usio na ukomo. Upendo wa kujitoa wa Mungu kwa wanadamu hufunuliwa, kabla ya yote, kama upendo unaotokana na Baba, ambaye kutoka kwake kila kitu kinapata asili yake. Pia kama mawasiliano ya bure ambamo Mwana hufanya ya upendo wake, akijitoa tena kwa Baba, na akijitoa kwa wanadamu; kama ustawi mpya daima wa upendo wa kimungu ambao Roho Mtakatifu humimina katika mioyo ya watu (taz. Rum 5:5).

Kwa njia ya maneno na matendo yake, na kwa kikamilifu na kwa daima kwa njia ya kifo na ufufuko wake,[30] Yesu huwafunulia wanadamu kwamba Mungu ni Baba, na kwamba sisi sote tunaitwa kwa neema kuwa watoto wake katika Roho (taz. Rum 8:15; Gal 4:6), na hivyo kuwa kaka na dada miongoni mwetu. Ndiyo sababu Kanisa linaamini kwa uthabiti kwamba "ufunguo, kiini na lengo la historia yote ya mwanadamu hupatikana katika Bwana wake na Mwalimu."[31]

32. Kwa kutafakari juu ya majitoleo na wingi wa zawadi ya Mungu Baba katika Mwana, ambayo Yesu alifundisha na kuishuhudia kwa kutoa uhai wake kwa ajili yetu, Mtume Yohane anapata maana yake halisi na matokeo yake muhimu zaidi. "Wapenzi, ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana. Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wowote. Tukipendana, Mungu hukaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani yetu" (1Yn 4:11-12). Kutendeana upendo kunadaiwa na amri ambayo Yesu hutaja kama "mpya" na kama "yake": "Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo" (Yn 13:34). Amri ya kupendana inaonyesha jinsi ya kuishi katika Kristo maisha ya Kiutatu Mtakatifu ndani ya Kanisa, lililo Mwili wa Kristo, pia jinsi ya kugeuza historia hadi kwamba ifikie utimilifu wake katika Yerusalemu ya mbinguni.

33. Amri ya kupendana, iliyo sheria ya uzima kwa watu wa Mungu,[32] lazima itie msukumo, itakase na kuinua kila uhusiano wa binadamu katika jamii na katika siasa. "Ubinadamu ni wito wa ushirika kati ya watu,"[33] kwa vile sura na mfano wa Mungu wa Utatu Mtakatifu ni msingi wa "maadili ya binadamu, ambao hufikia kilele chake katika amri ya upendo."[34] Hali ya kisasa ya kutegemeana, ambayo ni ya kiutamaduni, kijamii, kiuchumi na ya kisiasa, inakazia na kudhihirisha wazi vile vifungo vinavyounganisha familia ya wanadamu wote. Hivyo inasisitiza tena, katika mwanga wa Ufunuo, "mfano mpya wa umoja wa mbari ya wanadamu, ambao unatakiwa kuhimiza mshikamano wetu. Mfano huu mkuu wa umoja, uliopo ambao huakisi mtima wa uzima wa Mungu, aliye Mungu mmoja katika Nafsi tatu, ndicho sisi Wakristo tunachokimaanisha kwa neno "ushirika".[35]

 

III. BINADAMU KATIKA MPANGO WA UPENDO WA MUNGU

a. Upendo wa Utatu Mtakatifu, Asili na Lengo la Binadamu

34. Ufunuo katika Kristo wa fumbo la Mungu kama upendo wa Utatu wakati huohuo ni ufunuo wa wito kwa binadamu wa kupenda. Ufunuo huo unamulikia kila fani ya hadhi na uhuru wa wanaume na wanawake, na pia undani wa tabia yake ya kijamii. "Kuwa mtu mwenye sura na mfano wa Mungu ni kuwepo kwa mahusiano, kuhusiana na mwingine na “mimi"[36] kwa sababu Mungu mwenyewe, aliye mmoja na Utatu, ni ushirika wa Baba, na Mwana na Roho Mtakatifu.

Katika ushirika wa upendo ambao ni Mungu, na ambamo Nafsi Tatu za Mungu hupendana na kuwa Mungu Mmoja, binadamu huitwa kupata chemchemi na lengo la kuwepo kwake na la historia. Mababa wa Mtaguso, katika Konstitusyo ya kichungaji Gaudium et Spes, walifundisha kwamba "Bwana Yesu akimwomba Baba ili ‘wote wawe na umoja, kama sisi nasi tulivyo umoja’ (Yn 17:21-22), anatuwekea upeo mpya uliofumbika kwa akili ya binadamu. Na papo hapo anatudokezea ufanano kati ya umoja wa Nafsi [tatu] za Mungu na umoja wa wana wa Mungu katika ukweli na upendo. Ufanano huo unadhihirisha kwamba binadamu, ambaye hapa duniani ni kiumbe pekee alichotaka Mungu kwa ajili yake chenyewe, mwanadamu hawezi kuvumbua kikamilifu ukweli wake, isipokuwa kwa kujitolea mwenyewe kwa moyo mweupe (taz. Lk 17:33)."[37]

35. Ufunuo wa Kikristo unatoa mwanga mpya juu ya utambulisho, wito na kikomo cha kila binadamu na cha wanadamu wote. Kila mwanadamu ameumbwa na Mungu, kupendwa na kuokolewa katika Yesu Kristo, naye hujikamilisha kwa kuunda mtandao wa mahusiano mbalimbali ya upendo, haki na mshikamano na watu wengine, huku akijishughulisha na mambo yake mbalimbali duniani. Kazi ya mwanadamu, ikiwa na lengo la kustawisha utu kamili na wito halisi wa mtu, ubora wa hali ya maisha na kukutana na watu katika mshikamano wa watu na mataifa, kulingana na mpango wa Mungu, ambaye hakosi kuonyesha upendo na maongozi yake kwa watoto wake.

36. Kurasa za kitabu cha kwanza cha Maandiko Matakatifu, zenye kueleza kuumbwa kwa mwanamume na mwanamke katika sura na mfano wa Mungu (taz. Mwa 1:26-27), zina mafundisho ya msingi kuhusu utambulisho na wito wa binadamu. Maana, zinatueleza kwamba kuumbwa kwa mwanamume na mwanamke ni tendo huru na la hiari la Mungu; kwamba mwanamume na mwanamke, kwa vile walivyo huru na wenye akili, ndio yule "wewe " aliyeumbwa na Mungu; hivyo katika uhusiano naye tu waweza kuvumbua na kutimiliza maana halisi na kamili ya maisha yao ya binafsi na ya kijamii; kwamba katika hali ya kukamilishana na kupokeana, wao ni mfano wa Upendo wa Utatu Mtakatifu katika ulimwengu ulioumbwa; kwamba kwao, kama kwa kilele cha kuumbwa kote, Mungu Muumba alikabidhi jukumu la kutawala viumbe vyote kadiri ya mpango wake (taz. Mwa 1:28).

37. Kitabu cha Mwanzo hutupatia misingi kadha wa kadha ya anthropolojia ya Kikristo: utu wa mwanadamu usioondosheka, ambao shina na dhamana yake huonekana katika mpango wa Mungu wa uumbaji; tabia ya asili ya kijamii ya binadamu, ambayo mfano wake wa awali unaonekana katika uhusiano wa asili kati ya mwanamume na mwanamke, ambao muungano wao "umeunda mtindo wa kwanza wa ushirika kati ya watu";[38] Maana ya utendaji wa binadamu katika dunia, ambao unafungamana na kuvumbua na kustahi sheria za maumbile ambazo Mungu aliandika ndani ya viumbe vyote, ili watu wapate kuishi katika ulimwengu na kuutunza kulingana na mapenzi yake Mungu. Mtazamo huo wa binadamu, wa jamii na wa historia una misingi thabiti katika Mungu, nao huonekana dhahiri pale azimio lake la wokovu linapotendeka.

b. Wokovu wa Kikristo ni kwa Watu Wote na kwa Mtu Kamili

38. Wokovu uliotolewa kwa watu kikamilifu katika Yesu Kristo, kwa azimio la Mungu Baba, na kuletwa na kuenezwa kwa kazi ya Roho Mtakatifu, ni wokovu kwa watu wote na wa mtu kamili: ni wokovu kwa wote na kamilifu. Unahusiana na binadamu katika hali zake zote: ya kibinafsi na ya kijamii, ya kiroho na ya kimwili, ya kihistoria na ya upeo wa ufahamu na akili ya kibinadamu. Nao huanza kufanywa tayari katika historia, kwa vile vilivyoumbwa ni vyema na Mungu alivitaka, na kwa vile Mwana wa Mungu alivyojifanya kati yetu.[39] Lakini ukamilifu wake uko mbele hadi hapo tutakapoitwa sisi pamoja na viumbe vyote (taz. Rum 8) kushiriki katika ufufuko wake Kristo na katika ushirika wa uzima wa milele na Baba katika furaha ya Roho Mtakatifu. Matarajio hayo yanaonesha wazi kosa na udanganyifu wa mitazamo iliyo ya kidunia tu kuhusu maana ya historia na kuhusu madai ya binadamu kuweza kujiokoa mwenyewe.

39. Wokovu ambao Mungu huwajalia watoto wake unadai jibu na ukubali huru. Ni katika kile kilichomo katika imani, na kwa njia hii kwamba "mwanadamu hujikabidhi kikamilifu na kwa uhuru mikononi mwa Mungu,"[40] na kuitikia upendo wake Mungu, aliyetupenda kwanza kwa upendo tele (taz. 1Yoh 4:10). Mwanadamu huitikia kwa kuwapenda kweli ndugu zake, na kwa kuwa na tumaini thabiti, maana yeye aliyeahidi ni mwaminifu."(Ebr 10:23). Mpango wa wokovu wa Mungu hauwaweki wanadamu katika hali ya kutotenda, au ya chini zaidi kuhusiana na Muumba wao, kwa sababu uhusiano wao na Mungu aliotufunulia Yesu Kristo na ambao ndani yake Yeye anatushirikisha kwa kazi ya Roho Mtakatifu, ni uhusiano wa mtoto kwa mzazi wake: nao ni uhusiano uleule anaoishi Yesu na Mungu Baba (taz. Yn 15-17; Gal 4:6-7).

40. Wokovu alioutenda Kristo, ulio wa wote na mkamilifu, hufanya thabiti kile kifungo baina ya uhusiano ambao kila mtu anaitwa kuwa nao na Mungu na wajibu alio nao kila mtu kwa jirani zake katika matukio ya kawaida ya historia. Hayo yanahisiwa, ingawa mara nyingine kwa wasiwasi au kutokuelewa, katika uchunguzi wa wanadamu wote juu ya ukweli na umaana, nayo yamekuwa kama jiwe la msingi la agano la Mungu na Israeli, kama inavyoshuhudiwa na Torati na mahubiri ya Manabii.

Kifungo hicho kinaelezwa wazi na dhahiri katika mafundisho yake Yesu Kristo hadi kuthibitishwa kikamilifu na ushuhuda wake mkuu wa kutoa uhai wake, kwa kuyatii mapenzi ya Baba na kuwapenda ndugu zake. Kwa yule mwandishi aliyemwuliza, "Katika amri zote ni ipi iliyo ya kwanza?" (Mk 12:28), Yesu alijibu hivi: "Ya kwanza ndiyo hii: Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja; nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote. Na ya pili ndiyo hii: 'Mpende jirani yako kama nafsi yako.' Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi." (Mk 12:29-31).

Katika moyo wa binadamu yameunganika bila kuchanganulika uhusiano na Mungu – anayefahamika kama Muumba na Baba, chemchemi na utimilifu wa uzima na wokovu – na uwazi kwa upendo unaodhihirika mbele ya watu, wanaotakiwa kutendewa kama "nafsi yangu" mwingine, hata kama ni adui (taz. Mt 5:43-44). Katika mtima wa binadamu, basi, kuna mizizi yake ya kuwajibika kwa ajili ya haki na mshikamano, kwa ujenzi wa maisha ya kijamii, ya kiuchumi na ya kisiasa yanayoendana na mpango wa Mungu.

c. Wanafunzi wa Kristo kama Uumbaji Mpya

41. Maisha ya binafsi na ya jamii, na hali kadhalika utendaji wa binadamu katika dunia, daima yanaathiriwa na dhambi. Lakini Yesu Kristo "kwa kuteswa kwa ajili yetu, alituachia kielelezo ili tufuate mfano wake, na pia alitufungulia njia ili tunapoifuata, uzima na mauti vitakatifuzwe na kupata maana mpya."[41] Wanafunzi wa Kristo huambatana, katika imani na kwa njia ya sakramenti, na Fumbo la Pasaka ya Yesu, na hivyo utu wake wa zamani, pamoja na maelekeo yake maovu, unasulubiwa pamoja na Kristo. Hapo yeye, kama kiumbe kipya, anawezeshwa na neema "kuenenda katika upya wa uzima" (Rum 6:4). "Jambo hilo haliwahusu Wakristo tu bali pia wanadamu wote wenye mapenzi mema, ambao neema ya Mungu hufanya kazi mioyoni mwao, kwa namna isiyoonekana. Maana Kristo alikufa kwa ajili ya watu wote na wito halisi wa binadamu ndio mmoja, ule wa kimungu. Kwa hiyo lazima tuwe na wazo kwamba Roho Mtakatifu anawajalia watu wote uwezekano wa kushiriki fumbo la kipasaka, kwa jinsi anayoijua Mungu."[42]

42. Ugeuzi wa moyo wa binadamu, katika kufananishwa zaidi na zaidi na Kristo, ni sharti la awali kwa ajili ya ugeuzi halisi wa mahusiano yake na wengine. "Basi ni lazima uwezo wa kiroho na kimaadili wa binadamu na hitaji la kudumu la wongofu wake wa ndani yanatakiwa ili kupata mabadiliko ya kijamii yatakayomfaa kweli. Kipaumbele kinachotambuliwa cha wongofu wa moyo hakiwezi kuondoa bali kinyume chake kinaleta wajibu wa kuleta marekebisho katika taasisi na hali za maisha, pale mambo yanapokuwa yana kishawishi cha dhambi, kusudi yalingane na kanuni za haki na kuendeleza mema badala ya kuyazuia."[43]

43. Haiwezekani kuwapenda jirani kama nafsi yako na kudumu katika mwenendo huu bila kuwa na nia thabiti na imara ya kutenda kazi kwa ajili ya mema ya watu wote na ya kila mmoja, kwa sababu sisi tunawajibika kwelikweli kwa ajili ya wote.[44] Kadiri ya mafundisho ya Mtaguso, "heshima na upendo ni lazima viwafikie pia wale wenye kufikiri au kutenda tofauti na sisi katika masuala ya kijamii, kisiasa, na hata ya kidini. Maana kadiri tutakavyozidi kupenya katika namna zao za kufikiri, kwa ukarimu na upendo mkubwa, ndivyo tutakavyofanikiwa kirahisi kuingia katika dialogia nao."[45] Njia hii inahitaji neema, ambayo Mungu humjalia binadamu ili kumsaidia kushinda mapungufu yake, kumtoa katika mfululizo wa uongo na ukatili, kumwimarisha na kumhimiza ili, kwa moyo mpya na wa utayari, atengeneze daima mtandao wa mahusiano halisi na manyofu na binadamu wenzake.[46]

44. Pia mahusiano na viumbe vyote vya ulimwengu na utendaji wa binadamu ambao kwao hulenga kuutunza na kuutengeneza, hayo matendo ambayo kila siku huhatarishwa na kiburi cha binadamu na kujipenda kwake kusikokuwa na utaratibu, lazima kusafishwa na kukamilishwa kwa msalaba na ufufuko wake Kristo. "Maana binadamu, akishaokolewa na Kristo na kuwa kiumbe kipya katika Roho Mtakatifu, anaweza na anapaswa kuvipenda pia vitu vile alivyoviumba Mungu. Anavipata kutoka kwa Mungu, anavitazama na kuviheshimu kana kwamba vinatoka wakati huohuo mikononi mwa Mungu. Anamshukuru [Mungu] Mhisani kwa hivyo; na akivitumia na kuvifurahia viumbe hivi katika umaskini na uhuru wa kiroho, huingizwa katika umiliki wa kweli kana kwamba ni mtu asiye na kitu, bali yu mwenye vitu vyote: "Maana vyote ni vyenu: nanyi ni wa Kristo, na Kristo ni wa Mungu" (1Kor 3:22-23)."[47]

d. Wokovu Hupita Ufahamu wa Binadamu na Uhuru wa Mambo ya Dunia

45. Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu aliyejifanya mwanadamu, ambaye ndani yake na kwa njia yake ulimwengu na binadamu hupatiwa ukweli wake halisi na mtimilifu. Fumbo la Mungu kuwa karibu sana na binadamu – lililotimia katika Umwilisho wa Yesu Kristo, ambaye alijitoa mwenyewe juu ya msalaba, akikubali hata kufa – linaonesha kwamba kadiri mambo ya kibinadamu yanavyozidi kutazamwa katika mwanga wa mpango wa Mungu na kuyaishi katika ushirika na Mungu, vivyo hivyo yanapata nguvu na uhuru katika utambulisho wake maalumu na katika uhuru ulio wake halisi. Kushirikishana katika maisha ya Kristo ya umwana, kulikowezeshwa na Umwilisho na zawadi ya kipasaka ya Roho Mtakatifu, mbali na kufishwa, kunasababisha kuchanua kwa sura na kwa upekee halisi na huru unaoainisha wanadamu katika hali zao zote mbalimbali.

Mtazamo huo unaelekeza kwenye kukaribia kisahihi mambo ya kidunia na kujitawala kwake, jambo ambalo linasisitizwa sana na mafundisho ya Mtaguso wa Pili wa Vatikano; "Tunaweza kuelewa kwamba suala la "kujiendesha yenyewe kwa mambo ya dunia" lina msingi kwamba vitu vilivyoumbwa pamoja na jamii zenyewe vina sheria na tunu zake; na binadamu anapaswa polepole kuzivumbua tunu hizo, kuzitumia na kuzipanga. Ikiwa tutaelewa hivyo, basi kujiendesha huku ni dai lililo halali. Tena dai hilo . linalingana pia na mapenzi yake Muumba. Maana ni kwa nguvu yenyewe ya kuumbwa kwao, kwamba viumbe vyote vinapata uthabiti wao wa pekee, ukweli na wema wao pamoja na sheria na utaratibu wao. Binadamu hupaswa kuyaheshimu hayo yote kwa kuzitambua mbinu mahususi za kila sayansi na ufundi."[48]

46. Hakuna hali ya mgongano kati ya Mungu na binadamu, bali kuna uhusiano wa upendo ambako ulimwengu na matunda ya kazi za binadamu ulimwenguni yanakuwa mada za kupeana zawadi kati ya Mungu Baba na watoto wake, pia kati ya watoto wenyewe, katika Yesu Kristo: katika Kristo na kwa njia yake ulimwengu na binadamu hupata maana yao halisi na maalumu. Katika nuru ya jumla ya upendo wa Mungu yenye kukumbatia kila kilichopo, Mungu mwenyewe hufunuliwa kwetu katika Kristo kama Baba na mtoaji wa uzima; tena binadamu [hufunuliwa] kama yule ambaye, katika Kristo, hupokea vitu vyote kutoka kwa Mungu kama zawadi, kwa unyenyekevu na kwa hiari, na anayemiliki kila kitu kama ni chake mwenyewe, akijua na kung'amua kila kitu kama ni mali ya Mungu, chenye asili katika Mungu, na kuelekea kwake. Mintarafu hayo, Mtaguso wa Pili wa Vatikano unafundisha hivi: "Ikiwa kwa usemi 'kujitawala kwa mambo ya dunia' inaeleweka kuwa vitu vilivyoumbwa havimtegemei Mungu, tena kuwa binadamu huweza kuvitumia bila ya kuvielekeza kwa Muumba, [basi ikieleweka hivyo,] wale wote wenye kumwamini Mungu wanahisi jinsi kauli hizo zilivyo za udanganyifu. Maana kiumbe bila Muumba hutoweka."[49]

47. Binadamu, kwa mwenyewe na pia wito wake, hupita upeo wa ulimwengu ulioumbwa, wa taasisi na wa historia: kikomo chake cha mwisho ni Mungu mwenyewe,[50] aliyejifunua kwa wanadamu kusudi kuwaalika na kuwapokea katika ushirika naye mwenyewe.[51] "Mwanadamu hawezi kujitolea kwa mradi ulio wa kibinadamu tu wa mambo halisi, kwa udhanifu wa kinadharia au kwa njozi ya uongo. Kwa vile ni nafsi, yeye huweza kujitoa mwenyewe kwa nafsi nyingineyo au nyinginezo, na hatimaye kwa Mungu, ambaye ndiye aliyemfanya, naye ndiye awezaye kupokea kikamilifu zawadi yake."[52] Kwa sababu hiyo, "mwanadamu hukengeuka ikiwa anakataa kujishinda mwenyewe na kuishi kwa kung'amua namna ya kujitolea na ya kujenga jumuiya iliyo na utu halisi, yenye kuelekea kwenye lengo lake la mwisho, yaani kwa Mungu. Jamii nayo hukengeuka ikiwa mbinu zake za kujiratibisha kijamii, za uzalishaji na utumiaji zinasababisha kuwa vigumu zaidi kujitolea na kujenga mshikamano kati ya wanadamu."[53]

48. Binadamu hawezi na lazima hatakiwi kumilikiwa na kuchezewa na miundo ya kijamii, kiuchumi au kisiasa, kwa sababu kila binadamu anao uhuru wa kujielekeza kwenye kikomo chake. Kwa upande mwingine, kila ufanikishaji wa kiutamaduni, kijamii, kiuchuni au kisiasa, ambamo tabia ya kijamii ya binadamu na harakati zake za kutengeneza ulimwengu zinakuwa utendaji katika historia, unatakiwa daima kuangaliwa pia katika muktadha wa hali yake tegemezi na ya mpito, "kwa maana mambo ya ulimwengu huu yanapita" (1Kor 7:31). Ni hali tegemezi ya kieskatolojia, kwa maana ya kwamba binadamu na ulimwengu huelekea lengo lake, yaani utimilifu wa kikomo chake katika Mungu; tena, ni hali tegemezi ya kitheolojia, maadamu zawadi ya Mungu, ambayo kwayo kikomo cha wanadamu na cha viumbe vyote hupatikana, yapita upeo wa mawazo na matazamio ya binadamu. Kila mtazamo wa kimabavu kuhusu jamii na dola, na kila itikadi ya maendeleo iliyo ya kidunia tu, ni kinyume cha ukweli halisi wa ubinadamu na cha mpango wa Mungu katika historia.

 

IV. MPANGO WA MUNGU NA UTUME WA KANISA

a. Kanisa, Alama na Mlinzi wa Ufahamu Ulio Juu Kabisa ya Uwezo wa Binadamu

49. Kanisa, yaani jumuiya ya wale waliokusanyika pamoja na Kristo Mfufuka na wanakubali kumfuasa, "ni alama, pia ni mlinzi, wa hali ipitayo ufahamu wa binadamu.[54]" "Katika Kristo Kanisa ni kama sakramenti au ishara na chombo cha kuwaunganisha watu kiundani na Mungu na kuleta umoja kati ya wanadamu wote."[55] Utume wake ni kutangaza na kushirikisha wokovu alioutenda Kristo, ambao Yeye aliuita "Ufalme wa Mungu" (Mk 1:15), yaani, ushirika na Mungu na kati ya watu. Lengo la wokovu, Ufalme wa Mungu, lahusu watu wote na latimizwa kikamilifu baada ya historia, katika Mungu. Kanisa limepokea "utume wa kuutangaza Ufalme wa Kristo na wa Mungu, na kuusimika kati ya mataifa. Nalo Kanisa hapa duniani ni chipukizi na chanzo cha Ufalme huo."[56]

50. Kanisa hujiweka kimatendo kwenye utumishi wa Ufalme wa Mungu hasa kwa kutangaza na kushirikisha Injili ya wokovu na kwa kuanzisha jumuiya mpya za Kikristo. Pamoja na hayo, "Kanisa linahudumia Ufalme kwa kusambaza duniani “tunu za Injili” ambazo ni matokeo ya Ufalme na zinasaidia wanadamu kupokea mpango wa Mungu. Basi ni kweli kumekuwemo na mianzo kadhaa ya Ufalme hata nje ya mipaka ya Kanisa, popote kati ya mataifa, kwa kadiri yanavyoishi “thamani za Injili” na pia kujifungulia kwa utendaji wa Roho anayevuma apendapo na apendako (Yn 3:8). Lakini lazima tuongeze kusema kuwa hali hiyo ya kidunia ya Ufalme si kamili, mpaka ulingane na Ufalme wa Kristo uliomo katika Kanisa na uelekeao kwenye ukamilifu wa kieskatolojia."[57]Hufuatana na hayo, hasa, kwamba Kanisa halichanganywi katu na jumuiya ya kisiasa, wala halifungamani na mtindo wowote wa mfumo wa kisiasa.[58] Maana, "jumuiya ya kisiasa na Kanisa zina uhuru na mamlaka kila moja katika uwanja wake. Na zote mbili zipo kwa ajili ya kutumikia wito wa binadamu, kwa mtu binafsi na katika huduma kwa jamii ya wanadamu walewale, ijapo ni kwa msingi ulio tofauti."[59] Kweli, ubainisho kati ya dini na siasa, pia kanuni ya uhuru wa dini, ni mafanikio maalumu ya Ukristo, tena ni mmojawapo wa michango yake ya msingi ya kihistoria na ya kiutamaduni.

51. Kadiri ya mpango wa Mungu uliotimizwa katika Kristo, inahusiana na upekee na utume wa Kanisa katika ulimwengu "lengo la kiwokovu na la kieskatolojia ambalo laweza kufikiwa katika maisha yajayo tu."[60] Ni hasa kwa sababu hiyo kwamba Kanisa latoa mchango wake wa pekee na usio mbadala pamoja na mahangaiko yanayolisukuma kuifanya familia ya wanadamu wote na historia yake kuwa na utu zaidi, likihimizwa kusimama kama ngome dhidi ya kila kishawishi cha kutumia mabavu, kwa kumwonesha binadamu wito wake halisi na mtimilifu.[61]

Kwa kuihubiri Injili, kwa neema ya sakramenti na kwa kuishi ushirika wa kidugu, Kanisa "linaponya na kuinua utu wa mwanadamu, linaimarisha jamii ya kibinadamu, na kutia maana ya kina zaidi na kusudi lake katika kazi za kila siku za wanadamu."[62]Kwa ngazi ya matukio ya kihistoria, kwa hiyo, ujio wa Ufalme wa Mungu hauwezi kutambulika kwa mtazamo wa utaratibu wa kijamii, kiuchumi au kisiasa ulio maalumu na wa hakika. Mbali nayo, [Ufalme] unashuhudiwa katika maendeleo ya hisia za kijamii zilizo za kiutu, ambazo kwa wanadamu wote kwa jumla ni kama chachu ya ukamilisho halisi, ya hali na ya mshikamano, kwa kuwa wazi kwa Aliye juu kabisa, anayetazamwa kama rejea kwa utimilifu wa mwisho wa kila mmoja.

b. Kanisa, Ufalme wa Mungu na Kufanya Upya Mahusiano ya Kijamii

52. Mungu, katika Kristo, hamkomboi tu mtu binafsi, lakini hukomboa pia mahusiano ya kijamii yaliyopo kati ya watu. Kama vile anavyofundisha Mtume Paulo, maisha katika Kristo yafanya kwamba upekee wa kila mwanadamu na tabia yake ya kijamii – pamoja na matokeo yake kiutendaji katika historia na jamii – vijitokeze kitimilifu na kwa namna mpya: "Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu. Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo. Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala mtu huru. Hapana mtu mume wala mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu" (Gal 3:26-28). Katika mtazamo huo, Jumuiya za Kanisa, zilizoletwa pamoja na ujumbe wa Yesu Kristo na kukusanywa katika Roho Mtakatifu kumzunguka Bwana Mfufuka (taz. Mt 18:20; 28:19-20; Lk 24:46-49) zajitokeza kama mahali pa ushirika, ushuhuda na utume, na kama mvuto kwa ukombozi na mageuzi ya mahusiano ya kijamii. Kuhubiriwa kwa Injili ya Yesu kunawasukuma wanafunzi kuwahisha yatakayokuwa kwa kufanya upya mahusiano ya kijamii.

53. Kugeuza mahusiano ya kijamii kunakotokana na matakwa ya Ufalme wa Mungu, hakubanwi ndani ya mipaka inayoeleweka mara moja kwa daima. Mbali na hayo, ni jukumu la jumuiya ya Kikristo, la kustawishwa na kutekelezwa kwa tafakari na matendo yanayochochewa na Injili. Roho wa Bwana, mwenye kuongoza watu wa Mungu na hapohapo kuujaza ulimwengu,[63] ndiye ambaye mara kwa mara huwaongoza watu katika njia mpya na za kufaa ili kutekeleza jukumu lao kwa ubunifu.[64] Msukumo huo hupewa jumuiya ya Wakristo ambao ni sehemu ya dunia na historia, na hivyo wako tayari kuzungumza na watu wote wenye mapenzi mema, katika harakati ya pamoja ya kutafuta "mbegu za ukweli na uhuru" zilizopandwa katika konde pana sana la wanadamu wote.[65] Utekelezaji wa kufanya upya huko unatakiwa kufungamana barabara na kanuni za msingi za sheria ya kimaumbile, iliyoandikwa na Mungu Muumba ndani ya kila kiumbe chake (taz. Rum 2:14-15), na kutiwa mwanga wa kieskatolojia katika Yesu Kristo.

54. Yesu Kristo anatufunulia kwamba "Mungu ni upendo" (1Yn 4:8) na kutufundisha kuwa "sheria kuu ya ukamilifu wa binadamu, na hivyo pia ya mageuzi ya ulimwengu, ni amri mpya ya upendo. Kwa hiyo wale wote wanaouamini upendo wa Mungu, wanahakikishiwa naye kuwa njia ya upendo imewekwa wazi kwa watu wote. Tena wanathibitishiwa kwamba juhudi zinazokusudia kutimiza udugu wa wote, si za bure".[66] Sheria hiyo inatakiwa kuwa kipimo na kanuni ya mwisho ya kila uhusiano wa wanadamu katika utendaji wake wowote. Kwa kifupi, ni fumbo halisi la Mungu, Upendo wa Utatu Mtakatifu, ambalo ndio msingi wa maana na thamani ya mtu, mahusiano ya kijamii, utendaji wa binadamu katika ulimwengu, kwa jinsi lilivyofunuliwa na kushirikishwa kwa wanadamu kwa njia ya Yesu Kristo, katika Roho wake.

55. Kugeuza ulimwengu ni hitaji la msingi kwa wakati wetu huu pia. Kwa hitaji hilo Majisterio ya Kanisa kuhusu jamii inadhamiriwa kutoa majawabu kulingana na mahitaji ya alama za nyakati, kwa kuelekeza kwanza kabisa kwenye mapendo kati ya wanadamu, mbele za Mungu, kama chombo chenye nguvu zaidi cha mabadiliko, kibinafsi na kijamii pia. Maana, mapendo, yanayoshiriki katika upendo wa Mungu usio na mipaka, ni lengo halisi la wanadamu, la kihistoria na la juu kabisa pia. Kwa hiyo, "ni lazima kutofautisha kwa makini maendeleo ya kidunia na ustawi wa Ufalme wa Kristo. Hata hivyo, maendeleo hayo yana umuhimu mkubwa kwa Ufalme wa Mungu, kwa kadiri yanavyoweza kuchangia kuratibisha vizuri zaidi jamii ya kibinadamu."[67]

c. Mbingu Mpya na Dunia Mpya

56. Ahadi ya Mungu na ufufuko wa Yesu Kristo huibua tumaini thabiti la Wakristo kwamba makao mapya na ya milele yameandaliwa kwa kila mtu, nchi mpya ambayo haki hukaa ndani yake (taz. 2Kor 5:1-2; 2Pet 3:13). "Hapo ndipo mauti itakaposhindwa, wana wa Mungu watafufuliwa katika Kristo, na kile kilichopandwa katika udhaifu na uharibifu kitaivaa hali ya kutokufa. Upendo na matunda yake ndivyo vitakavyobaki, na mambo yote yaliyoumbwa na Mungu kwa ajili ya binadamu yataokolewa na utumwa wa ubatili."[68] Tumaini hili, mbali na kuudhoofisha, lazima lituchochee nguvu ya kuwajibika katika kazi zinazotakiwa kufanywa kwa ajili ya mahitaji ya wakati huu.

57. Yale mema – kama vile utu wa mwanadamu, udugu na uhuru, matunda yote ya dunia na ya kazi za binadamu – ambayo yalisambazwa duniani katika Roho wa bwana na kuendana na amri yake, yakiisha kutakaswa na kila doa, kuangaziwa na kugeuzwa, yanakuwa mali ya Ufalme wa ukweli na uzima, wa utukufu na neema, wa haki, wa upendo na wa amani, ambao Kristo atamtolea Baba, na ndiko ambako sisi tutayakuta tena. Hapo ndipo maneno ya Kristo yatakaposikiwa na wote katika ukweli wake mzito: "Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu; kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha; nalikuwa uchi, mkanivika; nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia. kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi" (Mt 25:34-36,40).

58. Utimilifu kamili wa binadamu, unapatikana katika Kristo kwa kipaji cha Roho Mtakatifu, huendelea katika historia na hupiga hatua kwa kupitia mahusiano ya mtu na watu wengine; mahusiano ambayo, kwa upande wake, yanatimilika kadiri ya uwajibikaji wa kila mmoja katika kuendeleza ulimwengu katika haki na amani. Utendaji wa binadamu katika historia ni muhimu na una nguvu kwa kuweka hatimaye Ufalme wa Mungu, ijapo hilo linabaki tendo ambalo ni zawadi bure ya Mungu, iliyo nje ya ufahamu wa binadamu. Utendaji huo, ukistahi utaratibu halisi wa mambo ya kidunia na kumulikwa na ukweli na upendo, unakuwa njia ya kufanya haki na amani kuwepo zaidi na wazi duniani, na unaotarajia kwa nyakati zetu kuwepo kwa Ufalme ulioahidiwa.

Kwa kujifananisha na Kristo Mkombozi, binadamu hujitambua kama kiumbe kilichopendwa na Mungu na kuteuliwa naye tangu milele, kuitwa kupokea neema na utukufu katika utimilifu wote wa fumbo aliloshirikishwa katika Yesu Kristo.[69] Kufananishwa na Kristo na kutazama uso[70] wake kunawawekea Wakristo hamu isiyozimika ya utangulizi tangu katika ulimwengu huu, katika mazingira ya mahusiano ya kibinadamu, wa yale yatakayokuwa mambo ya kweli kabisa katika ulimwengu halisi ujao; ndiyo sababu Wakristo hujitahidi kutoa chakula, kinywaji, mavazi, makao, huduma na kumkaribisha na kuwa jirani na Bwana anayebisha mlangoni (taz. Mt 25:35-37).

d. Maria na 'Ndiyo' yake Katika Kuitikia Mpango wa Upendo wa Mungu

59. Mrithi wa tumaini la wenye haki katika Israeli na wa kwanza miongoni mwa wafuasi wa Yesu Kristo ndiye Maria, Mamaye. Kwa kukubali 'ndiyo' mpango wa upendo wa Mungu (taz. Lk 1:38), kwa niaba ya wanadamu wote, yeye apokea katika historia yule Aliyetumwa na Baba, Mkombozi wa wanadamu. Katika utenzi wa Maria hutangaza ujio wa Fumbo la Wokovu, kuja kwake "Masiha wa maskini" (taz. Isa 11: 4; 61:1). Mungu wa Agano, ambaye Bikira wa Nazareti amsifu kwa kumwimbia akifurahi rohoni, ndiye Yule anayewaangusha wakuu katika viti vyao vya enzi na wanyonge kuwakweza, awashibisha mema wenye njaa na wenye mali awaondoa mikono mitupu, awatawanya walio na kiburi na kuonyesha rehema kwa hao wanaomcha (taz. Lk 1:50-53).

Kwa kuutazama moyo wa Maria, na kina cha imani yake iliyooneshwa katika maneno ya Utenzi wa Maria, wanafunzi wake Yesu huitwa kufanya upya zaidi na wazi ndani yao utambuzi wa "kwamba ukweli juu ya Mungu anayeokoa, ukweli juu ya Mungu aliye chanzo cha kila karama, hawezi kutenganishwa na udhihirisho wa upendo wake wa pekee kwa maskini na wanyonge, upendo ule ambao hutajwa bayana katika Utenzi huo na kuelezwa baadaye katika maneno na kazi za Yesu."[71] Maria anamtegemea Mungu katika yote na anaelekezwa kwake kikamilifu na msukumo wa imani yake. Ndiyo sababu yeye ni "taswira kamili ya uhuru na ya ukombozi wa wanadamu na wa ulimwengu mzima".[72]


SURA YA PILI

UTUME WA KANISA NA MAFUNDISHO YA KIJAMII

I. UINJILISHAJI NA MAFUNDISHO YA KIJAMII

 

a. Kanisa, Makao ya Mungu Pamoja na Wanaume na Wanawake.

60. Kanisa hushiriki na wanadamu katika furaha na matumaini, wasiwasi na uchungu, linasimama pamoja na kila mwanamume na mwanamke wa kila mahali na nyakati katika kuleta habari njema ya ufalme wa Mungu, ambayo katika Yesu Kristo amekuja na kuendelea kuwepo kati yao.[73] Miongoni mwa wanadamu na katika ulimwengu yeye ni sakramenti ya upendo wa Mungu na hivyo matumaini yenye kutia moyo, kuchochea na kuendeleza ukombozi endelevu wa wanadamu unaochukua na kujitoa katika ukombozi wenye utu na msukumo wa mbele. Kanisa lipo miongoni mwa wanadamu kama hema ya kuwakutanisha watu na Mungu, “maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu” (taz. ufu 21:3), ili mtu asiwe peke yake, aliyepotea au kuogopa katika kazi yake ya kutengeneza ulimwengu, ili uwe na utu zaidi; wanaume na wanawake wasaidiwe na upendo wa wokovu wa Kristo. Ukiwa kama utumishi wa kiukombozi. Kanisa siyo kitu cha hewani wala siyo eneo la kiroho tu, bali katika eneo la kihistoria na dunia ambamo mtu anaishi.[74] Hapa binadamu anakutanishwa na upendo wa Mungu na kwa wito anashiriki mpango wa Mungu.

61. Katika Nafsi ya kila mtu ina upekee usiojirudia na uwezo wa mahusiano na wengine katika jamii. Maisha ya pamoja katika jamii, ndani ya mtandao wa mahusiano unaounganisha watu binafsi, familia, na ushirika kati ya makundi yanayokutana, kuwasiliana na kubadilishana, kuhakikisha ubora wa maisha. Manufaa ya wote yanayotafutwa na kufikiwa na jumuiya za kijamii yanahakikisha manufaa ya watu binafsi, familia na jumuiya.[75] Hizo ni sababu za chimbuko la jamii na kuchukua sura zenye miundo wazi, ya kisiasa, kiuchumi, kisheria na tamaduni zinazoiunda. Kwa binadamu, “aliyejiingiza ndani ya mtandao wa kawaida wa mahusiano katika jamii za kisasa,”[76] Kanisa linaelekeza mafundisho yake ya kijamii. Likiwa kama bingwa wa utu,[77] lina uwezo wa kumuelewa mtu katika wito na maelekeo yake, katika ufinyu na mapungufu yake, haki na wajibu wake, na kuongea neno la uhai linalojirudia katika historia na mazingira ya uhai wa binadamu.

b. Injili Hupenya na Kutajirisha Jamii

62. Kwa njia yake ya mafundisho ya jamii, Kanisa linatafuta kutangaza Injili na kuifanya iwepo kwenye mtandao wa mahusiano ya kijamii. Siyo suala tu la kumfikia mtu alipo katika jamii lakini binadamu akiwa ndiye mwenye kupokea tangazo la Injili, bali Injili hupenya na kutajirisha jamii.[78] Kwa hiyo, Kanisa linazingatia mahitaji ya binadamu na kazi yake ya kimisionari na ukombozi. Watu wanavyoishi pamoja katika jamii mara kwa mara wanaonesha kipimo cha ubora wa maisha na hivyo hali ambayo kila mwanaume na mwanamke wanaelewa na kuwekea maamuzi yanayohusu wito wao. Kwa msingi huu, Kanisa haliachi kutilia mkazo lile ambalo limeufanyia uamuzi, linalotokana na uzoefu ndani ya jamii. Kanisa liko makini kuhusu ubora wa maadili, yaani vipengele vyenye utu wa kuaminika katika maisha ya kijamii. Maisha ya kijamii: siasa, uchumi, kazi, sheria, utamaduni – siyo tu mambo ya kidunia, ambayo huwa nje au kuwa ujumbe mgeni katika mpango mzima wa wokovu. Hali halisi ya jamii pamoja na yale yote yenye kufanikisha yanamhusu binadamu. Jamii inaundwa na wanaume na wanawake ambao ndio “msingi na kiini cha mwelekeo wa Kanisa.”[79]

63. Kwa njia yake ya mafundisho ya kijamii, Kanisa linachukua jukumu la kutangaza yale yote ambayo limekabidhiwa na Bwana. Linatengeneza ujumbe wenye uhuru na wokovu ambao umeundwa na Kristo: Injili ya Ufalme wa Mungu uliopo katika historia ya mwanadamu. Katika kutangaza injili, Kanisa “linabeba ushuhuda kwa mwanadamu, kwa njia ya Kristo, na heshima yake na wito wake ni katika ushirika wa watu. Kanisa linafundisha jukumu la kutenda haki na kujenga amani kwa kuzingatia hekima ya Kimungu.”[80]

Kadiri Injili inavyorudiwarudiwa na Kanisa la leo kwa wanaume na wanawake wa leo,[81] mafundisho ya jamii yanakuwa ni neno lenye kuleta uhuru. Hii ina maana Injili ina matokeo ya uhuru na neema inayotoka kwa Roho wa Mungu, anayepenyeza mioyoni na kuendelea kuweka katika fikra na katika mtindo wa upendo, haki, uhuru na amani. Hivyo, uinjilishaji katika sekta ya jamii ina maana ya kuingiza ndani ya moyo wa binadamu nguvu ya maana ya uhuru unaopatikana katika Injili ili kuinyanyua jamii inayooana na mwanadamu kwa sababu inaendana na Kristo: ina maana kujenga mji wa binadamu wenye utu zaidi kwa sababu unaendana zaidi na ufalme wa Mungu.

64. Kwa mafundisho yake ya kijamii Kanisa haliendi kinyume na utume wake; bali linakuwa na uaminifu thabiti kwa utume wake. Ukombozi ulioletwa na Kristo na kukabidhiwa katika kazi ya ukombozi wa Kanisa kwa vyovyote vile upo katika mpango wa Mungu. Mtazamo huu hauweki mipaka ya ukombozi, bali ni kielelezo chenye kuunganisha.[82] Hali ya Kimungu isichukuliwe kama hali au mahali ambapo maumbile yanaanza, sehemu ambayo maumbile yanafikia kikomo, bali ndipo maumbile yanapopata mahali pa juu zaidi. Kwa njia hii hakuna kilichoumbwa kinachoonekana kigeni na kutengwa na Mungu, uwe utaratibu wa kibinadamu au mpango wa kimungu au mwendo wa kitheolojia ya kiimani na neema, bali vyote hupatikana ndani yake, vikiendelea na kuinuliwa au kuhuishwa Naye. “Ndani ya Yesu Kristo, dunia iliyoumbwa kwa ajili ya mwanadamu (taz. Mwa 1: 26 – 30), dunia ambamo dhambi ilipoingia ilifanywa kitu kisicho na maana (Rum 8: 20, taz. 8: 19 – 20), ikarudia hali yake ya asili inayounganika na Mungu aliye chemchemi ya hekima na upendo. Kwa hiyo, “Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanae wa pekee” (Yn 3: 16). Kwa kuwa muunganiko huu ulivunjwa na mwanadamu, na hivi ubinadamu wa Kristo uliuumbwa upya (taz. 5: 12 – 21).”[83]

65. Wokovu ulianza na Umwilisho, kwa kufanya hivyo mwana wa Mungu anafanyika mwili pasipokuwa na dhambi, kulingana na mshikamano uliowekwa na hekima ya Mungu Muumba, na kukumbatia kila kitu kama zawadi yake pendo la wokovu. Binadamu anaguswa na upendo huu katika hali yake kamili ya kuwa kiumbe: anayeishi katika hali ya kimwili na kiroho, maana yake akiwa katika mshikamano wa kuhusiana na wengine. Mtu mzima hatenganishwi na roho au kutengwa kabisa utu wake binafsi, lakini mtu na jamii za watu wanahusika katika mpango wa ukombozi wa kiinjili. Kanisa lenye kubeba dhamana ya ujumbe wa Injili wa Umwilisho na Wokovu, haliwezi kufuata njia nyingine. Mafundisho yake ya kijamii yenye matokeo ya utendaji unaoibuka kutoka katika mafundisho hayo, siyo tu linaficha sura yake au sauti yake katika utume wake, lakini linao uaminifu kwa Kristo na linaonesha lenyewe kwa wanaume na wanawake kama “sakramenti ya ukombozi.”[84] Huu ni ukweli kwa nyakati hizi zinazojidhihirisha katika ongezeko la hali ya kutegemeana na utandawazi katika masuala ya jamii.

c. Mafundisho ya Jamii, Uinjilishaji na Kumuenzi Binadamu

66. Mafundisho ya Kanisa kuhusu Jamii ni muunganiko wa utume wake wa uinjilishaji. Hakuna kitu kinachohusu jumuiya ya wanaume na wanawake, mazingira na matatizo yanayohusu haki, uhuru, maendeleo, mahusiano kati ya watu, amani ambavyo ni vigeni katika uinjilishaji, na uinjilishaji hauwezi kukamilika iwapo hautazingatia mahitaji ya Injili na hali halisi kwa mtu binafsi na kwa jamii ya wanadamu.[85] Kwa undani kabisa kuna muunganiko kati ya uinjilishaji na kumuenzi binadamu: “Hii ni pamoja na mahusiano ya utaratibu wa anthropolojia, kwa sababu binadamu anayetakiwa kuinjilishwa siyo kiumbe wa kufikirika, bali anaingia katika masuala ya kijamii na ya kiuchumi. Haya ni pamoja na muunganiko wa taratibu za kitheolojia, kwani mmoja hawezi akaacha kuwa mshiriki wa mpango wa uumbaji na mpango wa wokovu. Haya hatimaye yanagusa hali halisi ya mazingira ya kukosekana haki, hali ambayo inabidi ishughulikiwe ili haki iweze kupatikana. Hii ni pamoja na kuunganisha na nafasi ya juu katika utaratibu wa uinjilishaji ambao ni matendo ya kimapendo: “Ni kwa vipi mmoja anaweza kutangaza amri mpya bila kupindisha ukweli wa haki na amani, kumwendeleza binadamu kufikia maendeleo ya kweli?”[86]

67. Mafundisho ya Kanisa kuhusu Jamii “ni chombo kinachokubalika cha uinjilishaji”[87] na kimetokana kila mara pale ujumbe wa kiinjili unapokutana na maisha ya jamii. Ikieleweka namna hii, mafundisho haya ya jamii yanajidhihirisha kwa Kanisa linalobeba utume wa Neno na kazi ya kinabii.[88] Katika kufundisha na kueneza mafundisho yake ya kijamii ambayo ni sehemu ya utume wa kuinjilisha wa Kanisa na ni sehemu ya lazima ya ujumbe wa Kikristo, kwa kuwa mafundisho haya yanaonesha na kuelekeza matokeo ya ujumbe katika maisha ya jamii na kuyaweka katika kazi za kila siku na jitihada za kutafuta amani katika eneo la kumshuhudia Kristo Mwokozi.”[89] Hilo siyo jambo la maelekeo ya chini au shughuli na jitihada za utume wa Kanisa, bali ipo kwenye kiini cha huduma ya utumishi wa Kanisa. Kwa mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii, Kanisa “linamtangaza Mungu na fumbo la wokovu wa Kristo kwa kila binadamu, na kwa sababu hiyo humfunua mwanadamu kwa yeye mwenyewe.”[90] Huu ni utume ambao shina lake si kutangaza tu bali ni njia ya ushuhuda.

68. Kanisa halichukulii na kutimiza wajibu katika kila kipengele cha maisha ya jamii, bali linazungumzia yale ambayo ni uwezo wake yaani wa kumtangaza Kristo Mwokozi.[91] “Kristo hakulirithisha Kanisa wito kwa ajili ya siasa, uchumi au taratibu za kijamii; bali lilikabidhiwa kwa lengo la kidini. Hata hivyo, utume wa dini ndiyo chanzo cha kujitoa, kupata uelekeo na kuweka nguvu na kuimarisha jumuiya za watu kadiri ya sheria ya Mungu.”[92] Hii ina maana Kanisa haliingilii masuala ya kipekee pamoja na mafundisho yake ya kijamii, wala halipendekezi au kuanzisha miundo ya mifumo ya kijamii.[93] Hii siyo sehemu ya utume wake ulivyoaminishwa na Kristo. Uwezo wa Kanisa unatoka katika Injili: kutoka katika ujumbe unaomuweka binadamu kuwa huru, ujumbe unaotangazwa na kushuhudiwa toka mwanzo Mwana wa Mungu alipojifanya mwanadamu.

d. Haki na Majukumu ya Kanisa

69. Kwa njia ya Mafundisho yake ya kijamii, Kanisa lina lengo la kumsaidia binadamu katika njia ya ukombozi.[94] Huu ni msingi na lengo la kwanza kabisa. Hakuna nia ya kuingilia shughuli za wengine au kuweka pembeni na kuzipuuza wajibu wake; na wala kufikiria malengo ambayo ni mageni kwa utume wake. Huu ni utume wa kutumikia wenye kutoa sura ya jumla ya haki kwa Kanisa na wakati huohuo jukumu lake la kuendeleza mafundisho yake ya jamii na kuangazia jamii na mifumo yake kwa njia ya wajibu na kazi ambazo hujitokeza.

70. Kanisa lina haki ya kumfundisha mwanadamu, ni mwalimu wa ukweli wa imani: ukweli siyo mafundisho msingi rasmi tu (dogma), lakini pia maadili ambayo chimbuko lake lipo katika maumbile ya mwanadamu na katika Injili.[95] Neno la Injili, siyo tu kwamba lisikike lakini pia lionekane na kutafsiriwa kwa vitendo (taz. Mt 7: 24; Lk 6: 46 – 47; Yn 14: 21, 23 – 24; Yak 1: 22). Mtiririko wa tabia unaonesha kuwa mtu kweli anaamini na hafungwi na mambo ambayo huhusiana na Kanisa tu au ya roho peke yake, lakini wanaume kwa wanawake wanahusika katika uzoefu wa maisha ya jumla na suala la uwajibikaji. Hata hivyo, uwajibikaji wa mambo ya dunia hata ungekuwaje, unamlenga binadamu ambaye anaitwa na Mungu kwa njia ya Kanisa ili kushiriki zawadi ya ukombozi.

Wanaume na wanawake lazima wapokee zawadi ya wokovu siyo kijuujuu au kukubali kwa maneno, bali kwa maisha yote katika nyendo za mahusiano zinazotafsiri katika maisha bila kupuuza chochote, kama kuacha maeneo na malimwengu ambayo hayana maana au yanaonekana mageni kwa ukombozi. Hivyo, mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii, siyo kwa ajili ya kujinufaisha na wala siyo kuyaachia, kutafuta unafuu au kuingilia kati, bali ni haki yake kutangaza Injili katika maeneo ya jamii ili kufanya neno la Injili la ukombozi lipenye katika michakato ya uzalishaji, kazi, biashara, fedha, uchumi, siasa, sheria, utamaduni, mawasiliano ya jamii, ambamo wanaume na wanawake wanaishi.

71. Wakati huohuo, haki hii ya Kanisa ni wajibu, kwa sababu haliwezi kuacha wajibu huu bila kukana uaminifu wake kwa Kristo. “Ole wangu nisipohubiri Injili (1 Kor 9: 16). Onyo analotoa Mtakatifu Paulo yeye mwenyewe linagonga dhamiri ya Kanisa kama wito wa kutembea njia ya uinjilishaji, siyo tu kwa wale ambao wanaongozwa na dhamiri ya mtu binafsi bali pia kusukuma ndani ya taasisi za watu: kwa upande mmoja, dini lazima isifungwe na dhamiri ya “eneo la ubinafsi.”[96] Kwa maneno mengine, ujumbe wa Kikristo ni lazima usiwe ni ukombozi wa mambo ya kidunia peke yake isiyoweza kuangazia uhai wa dunia yetu.[97]

Kwa sababu ya umuhimu wa Injili na imani kwa watu, kwa sababu ya madhara ya kukosekana haki yaani, dhambi, Kanisa haliwezi kujiweka pembeni katika masuala ya jamii.[98] Kwa Kanisa wakati wote na mahali pote ni kutangaza kanuni za maadili, ikiwa ni pamoja na zile zinazoendana na taratibu za kijamii, na kutoa msimamo wa masuala yoyote yanayohitaji haki za msingi kwa wanadamu au wokovu wa roho.”[99]

 

II. ASILI YA MAFUNDISHO YA KANISA KUHUSU JAMII

a. Ufahamu ulioangaziwa na Imani

72. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii hayatokani na mawazo ya muundo wa mfumo fulani, bali yaliandaliwa kwa nyakati mbalimbali, kwa njia ya Majisterio kuingilia kati katika masuala mbalimbali ya jamii. Kilichojitokeza katika masuala haya ni wazi kwamba mambo fulani yalijitokeza kadiri ya hali yake, kanuni na muundo wa elimu fahamu (epistemolojia). Umuhimu wake uligusiwa na waraka wa Laborem Exercens,[100] na kueleza wazi zaidi katika suala hili na waraka wa Sollicitudo Rei Socialis: “Mafundisho ya Kanisa kuhusu Jamii yanahusu uwanja ambao siyo wa itikadi, bali theolojia hususani theolojia ya maadili.[101] Haiwezi ikapambanuliwa na mienendo ya uchumi wa kijamii. Hiyo siyo itikadi au nadharia ya vitendo yenye lengo la kupambanua mwenendo wa uchumi, siasa na mahusiano ya kijamii, bali ni eneo la aina yake.

Ni “maelezo sahihi ya mawazo ambayo yamefanyiwa tafakari katika masuala yasiyo wazi yanayohusu hali halisi ya uhai wa binadamu, jamii na taratibu za kimataifa kwa njia ya imani na mapokeo ya Kanisa. Lengo lake ni kutafsiri hali halisi iendane au isiwe nje ya mafundisho ya binadamu na wito wake, wito ambao ni wa kidunia na unaovuka mipaka ya binadamu - Mungu, hivyo madhumuni yake ni kuongoza tabia ya Kikristo.”[102]

73. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yana asili ya kitheolojia, hususani theolojia ya kimaadili, “kwa vile mafundisho hayo yana nia ya kuongoza tabia za watu.[103] “Mafundisho haya. yanapatikana pale maisha ya Kikristo na dhamiri ya Kikristo yanapokutana na hali halisi ya ulimwengu. Hii inaonekana katika jitihada za mtu mmojammoja, familia, watu wanaojihusisha na mambo ya kiutamaduni na kijamii, pia wanasiasa na viongozi wa serikali katika kuweka sura na utekelezaji wa mafundisho katika historia.”[104] Kwa kweli mafundisho ya kijamii yanaonesha vipengele vitatu vya mafundisho yanayohusu theolojia ya maadili: Kipengele msingi kinachohusu motisha; kipengele cha kanuni zinazoongoza maisha katika jamii na dhamiri ya makusudi, ambayo ni kiunganishi kati ya kanuni za jumla; na mazingira maalum na halisi ya kijamii. Hivi vipengele vitatu vinagusia ufafanuzi pamoja na njia sahihi na muundo maalum wa elimu fahamu (epistemolojia) ya mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii.

74. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanapata msingi katika ufunuo wa biblia na mapokeo ya Kanisa. Kutoka vyanzo hivi ambavyo vinatoka juu, Kanisa linajichotea mvuto toka ndani na mwanga katika kuelewa, kuamua na kuelekeza uzoefu wa binadamu na historia. Kabla ya kitu chochote kile na zaidi vitu ni mpango wa Mungu kwa dunia iliyoumbwa na kwa namna ya pekee kwa ajili ya maisha na ukomo wa wanaume na wanawake, ambao wanaitwa katika ushirika wa Utatu Mtakatifu.

Imani ambayo inapokea neno la Mungu na kuliweka katika vitendo, ni pamoja na kutumia akili. Kuelewa imani, hususani imani inayoelekeza katika utendaji, inajengwa na akili na inatumia mchango unaoweza kutolewa na akili. Mafundisho ya jamii kwa vile ni ufahamu unaotumika katika mazingira na historia yenye vipengele vya utendaji, inaunganisha imani na akili “fides et ratio[105] na kuonyesha uhusiano wa moja kwa moja.

75. Imani na akili ni njia mbili za mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii. Ufunuo na maumbile ya mwanadamu. “Kujua” imani ni kuelewa na kuelekeza wanaume na wanawake kadiri ya fumbo la historia ya wokovu na zawadi ya Kristo kwetu sisi. Kuelewa imani kwa namna hii ni pamoja na akili ambayo inaweka wazi na kuelewa kikamilifu ukweli uliojificha na kuunganisha ukweli wa maumbile ya binadamu, ukweli unaopatikana upande wa Mungu na kujieleza katika uumbaji.[106] Hii inafungamanisha ukweli wa mwanadamu aliye na roho na mwili na katika mahusiano na Mungu, watu na viumbe vingine.[107]

Kwa vile kiini cha fumbo ni Kristo, wajibu wa kiurazini haupungui wala kuwekwa pembeni na hivyo mafundisho ya Kanisa hayakosi mantiki na kwa hiyo yanaweza kutumika popote.. Kwa vile fumbo la Kristo linaangaza fumbo la binadamu, na linatoa ukamilifu wa maana ya heshima ya binadamu na maadili yanayohitajika. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii ni maarifa yanayoangaziwa na imani, ambayo yanaeleza uwezo wa akili kwa kiwango kikubwa. Mafundisho yanaeleza ukweli kwa watu wote, ukweli unaothibitishwa na majukumu yanayohitajika, hivyo, yanaweza kukubalika na kushirikishwa wote.

b. Katika Dialogia ya Kirafiki na Matawi yote ya Ufahamu

76. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanatoa mchango kutoka katika matawi yote ya ufahamu. Vyanzo vyovyote vile vina umuhimu katika maeneo mbalimbali ya ufahamu “ili ukweli uwekwe katika hali halisi ambayo binadamu ni tofauti na yanabadili mara kwa mara jamii, katika maudhui ya kiuchumi na kisiasa, mafundisho haya yanaingia kwenye dialogia na maeneo mbalimbali ya ufahamu yanayohusu binadamu. Yanaelezwa maeneo ya ufahamu ambayo yanapaswa kutoa mchango.[108] Mafundisho ya jamii yanatumia umuhimu wa michango ya falsafa pamoja na maelezo ya michango ya sayansi za kibinadamu.

77. Juu ya yote, mchango wa falsafa ni wa lazima. Mchango huu umeonekana unahitaji maumbile ya binadamu kama chanzo cha fahamu katika kutambua njia ya imani yenyewe. Kwa njia ya ufahamu, mafundisho ya jamii yanaisaidia falsafa katika mantiki zake, kwa maneno mengine ni hoja zinazokaa mahali pake.

Kuthibitisha kwamba mafundisho ya jamii ni sehemu ya theolojia kuliko falsafa haina maana ya kutothamini au kutotilia umuhimu mchango wa falsafa. Ukweli ni kwamba, falsafa inafaa na ni chombo cha lazima katika kufikia uelewa wa umuhimu kuhusu dhana ya mafundisho ya jamii, dhana kama: mtu, jamii, uhuru, dhamiri, sheria, haki, manufaa kwa wote, mshikamano duni na dola. Uelewa huu unaleta utulivu wa maisha katika jamii. Ni falsafa inayoonesha na kukubali mwanga wa Injili katika jamii, na kuvutia kila urazini uwazi wa dhamiri na kukubali ukweli.

78. Umuhimu wa mchango wa mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii katika kanisa unatoka katika sayansi za binadamu na sayansi za jamii.[109] Kwa mtizamo wa ukweli unaoweza kufunua, hakuna tawi la ufahamu linaloweza kuwekwa pembeni. Daima Kanisa linatambua na kupokea kila kitu kinachotambua uelewa wa binadamu kwa mapana zaidi, pia mahusiano yake ya kijamii ambayo ni yenye hali ya kubadilikabadilika zaidi, na yaliyo magumu zaidi kueleweka. Kanisa linaelewa ukweli kwamba msingi wa kuelewa mtu haupo katika theolojia tu, bila mchango wa matawi ya ufahamu ambamo theolojia yenyewe inarejea.

Umuhimu huu na uwazi wa mara kwa mara katika matawi ya ufahamu unafanya mafundisho ya jamii yaaminike, yagusike na yawe na maana. Shukrani kwa sayansi, kwani inaliwezesha Kanisa kujipatia uelewa zaidi wa mtu katika jamii, kuongea na wanaume na wanawake wa wakati wake kwa kuamini na zaidi sana kuweka majukumu ya kisayansi na ya jamii katika nyakati zetu, neno la Mungu na imani yanatiririka kutoka katika jamii.[110]

Majadiliano ya maeneo ya fahamu yanaipa sayansi changamoto ili ielewe mtazamo wenye maana, thamani, na kujitoa katika ufahamu wa jamii katika Kanisa na “kuweka wazi upeo mpana wenye nia ya kutumikia binadamu binafsi ambaye anakubaliwa na kupendwa katika ukamili wa wito wake.[111]

c. Ufafanuzi wa Utume wa Kanisa katika Kufundisha

79. Mafundisho ya jamii ni ya Kanisa kwa sababu Kanisa ndilo linalotengeneza maelezo, kuyasambaza na kuyafundisha. Siyo manufaa ya sehemu za mwili wa Kanisa bali jumuiya yote; inaeleza njia ambayo Kanisa linaelewa jumuiya na nafasi yake kuhusu miundo na mabadiliko ya jamii. Jumuiya yote ya Kanisa – mapadre, watawa na walei – inashiriki kutengeneza mafundisho ya jamii, kila moja kadiri ya kazi zake, karama na utendaji wake wa kiutume.

Michango hii mingi na namna mbalimbali ambayo inamwelezea “Mungu katika kukubalika kwa Imani (sensus fidei) kwa watu wote” [112] – zinachukuliwa, zinatafsiriwa na kuunganishwa na Majisterio, ambayo inaweka rasmi kuwa mafundisho ya Kanisa. Kwa Majisterio ya Kanisa inawahusu wale walioipokea (munus docendi) au utume wa kufundisha katika eneo la imani na maadili yaliyopokelewa kwa mamlaka kutoka kwa Kristo. Mafundisho ya jamii siyo suala la mawazo tu au kazi za utaalamu wa watu, bali ni mawazo ya Kanisa ikiwa kama kazi ya majisterio ambayo inafundisha kwa mamlaka ya Kristo aliyewapa uwezo mitume na waandamizi wake: Papa na Maaskofu katika ushirika wake.[113]

80. Katika mafundisho ya jamii, majisterio inafanya kazi katika maeneo mbalimbali na ambayo yanaelezeka. Jambo la muhimu zaidi ni ujumla wa majisterio wa Papa na Halmashauri: hii ni majisterio inayoonesha uelekeo na kupima maendeleo ya Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii. Mafundisho haya yanatumika katika majisterio ya maaskofu ambao katika uhalisi na mazingira fulani ya mahali, inatoa maana sahihi ya mafundisho, kuyatafsiri na kuyaweka katika vitendo.[114] Mafundisho ya jamii ya Maaskofu yanatoa mchango unaokubalika na yanabeba uzito wa Majisterio ya Mkuu wa Roma. Kwa njia hii, kuna mzunguko unaojieleza wa wachungaji wa Kanisa kuungana na Papa katika mafundisho ya jamii. Mafundisho halisi yanayotolewa yanaunganishwa, yaani mafundisho ya jumla ya Papa na mafundisho fulani ya Maaskofu.

Kwa kuwa mafundisho ya Kanisa ni sehemu ya Mafundisho ya maadili, hivyo mafundisho haya yana hadhi na mamlaka kama yalivyo maadili ya Kanisa. Ni Majisterio inayoaminika, ambayo inalazimisha waamini kufuata.[115] Uzito wa mafundisho mbalimbali na kukubalika yanategemea hali ya mafundisho ya fulani kwa kiwango cha uhuru kutoka katika uwepo na vipengele vinavyojitokeza mara kwa mara.[116]

d. Jamii Hupatanishwa Katika Haki na Upendo

81. Shabaha ya mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanataka lazima iwepo akili kwa kuishi kwake. Binadamu anaitwa kwenye ukombozi, na hivyo anaaminiwa na Kristo katika Kanisa linalojali na kuwajibika.[117] Kwa njia yake ya mafundisho ya jamii, Kanisa linaonesha kuwa linajali maisha ya binadamu katika jamii likizingatia thamani ya maisha ya jamii ambayo huhusiana na haki na upendo ambavyo vinaunda mfungamano wa jamii. Hii inategemea uamuzi wa kulinda kutetea na kumuinua binadamu ambaye ndiye chimbuko la kila jumuiya. Shughuli za jamii kwa kweli zinalenga utu na haki ya mtu na amani katika mahusiano kati ya watu na kati ya jumuiya za watu. Haya ni mambo bora ya jumuiya ya kijamii ambayo lazima yapatikane na yahakikishwe. Kwa mtazamo huu, mafundisho ya jamii yana jukumu la kutangaza, lakini pia kukataa yasiyotakiwa.

Jambo la kwanza ni kutangaza ambayo ni maalumu kwa Kanisa: “kutazama mtu na masuala ya binadamu kwa ujumla wake.”[118] Hili halifanywi katika kiwango cha kanuni tu, lakini pia katika utendaji. Mafundisho ya jamii, hayatoi maana, tunu na kipimo katika uamuzi peke yake, bali pia kanuni na mwelekeo wa vitendo unaojitokeza kutokana na haya yote.[119] Kwa mafundisho ya jamii, Kanisa halijaribu kuunda au kupangilia jamii, bali kuelekeza; kuongoza na kuunda dhamiri.

Mafundisho ya jamii yanahusu jukumu la kukataa, pale dhambi inapokuwepo, dhambi ya kukosa haki na vurugu ambayo kwa njia tofauti inaingia katika jamii, na jamii inashikamana nayo.[120] Kwa kukataa mambo fulani mafundisho ya jamii yanahukumu yale yasiyokubalika na ukiukwaji haki na hasa za wale maskini wadogo, na wanyonge.[121] Kadiri haki hizi zinavyopuuzwa au zinavyovunjwa, ndivyo vurugu zinavyozidi na kukosa haki. Hii inahusu watu mbalimbali na maeneo mapana kijiografia duniani, na kusababisha maswali huharibu na kuondoa mizani ambayo inapelekea mtafaruku wa jamii. Sehemu kubwa ya mafundisho ya jamii inashawishi na kupimwa na maswali ya jamii ambayo yanatakiwa kupata majibu yake yanayotakiwa yatokane na haki katika jamii.

82. Nia ya mafundisho ya jamii ni ya utaratibu wa kidini na utaratibu wa kimaadili.”[122] Nia ya kidini ni kwa sababu ya uinjilishaji na utume wa kiukombozi unakumbatia binadamu “katika ukweli kamili wa uhai wake wa maisha yake na pia jumuiya na jamii yake.”[123] Nia ya Maadili ni kwa sababu Kanisa nia yake ni “kukamilisha muundo wa binadamu,”[124] hii ina maana kujikomboa kutokana na kila kitu kinachomkandamiza binadamu”[125] na kufikia “maendeleo kamili ya binadamu wote.”[126] Mafundisho ya jamii yanaionesha jamii njia ya kufuata na kuipatanisha kwa njia ya haki na upendo, jamii yenye kutumia historia kabla ya wakati, kutayarisha na kuwakilisha “mbingu mpya na dunia mpya, ambayo haki yakaa ndani yake” (2 Pet 3: 13).

e. Ujumbe kwa Wanangu na Mabinti wa Kanisa na kwa Ajili ya Binadamu

83. Wanaopokea kwanza mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii ni wanajumuiya wote wa Kanisa, kwa sababu wote wana jukumu ambalo lazima walitimize. Dhamiri inaitwa na mafundisho haya ya jamii na kutimiza majukumu ya haki na ukarimu katika jumuiya. Mafundisho haya ni mwanga wa ukweli wa maadili yanayosukuma kukubalika kwa mwaliko kadiri ya wito na utume wa kila Mkristo. Jukumu la uinjilishaji, yaani, kufundisha, katekesi na malezi ambayo mafundisho ya jamii yanachochea, inaelekezwa kwa kila Mkristo, kila mmoja kadiri ya uwezo, karama, ofisi na utume wa kila mtu.[127]

Mafundisho ya jamii yanaleta majukumu kuhusu kujenga, muundo na jinsi jamii zinavyofanya kazi, hii ni kusema kisiasa, kiuchumi na utawala wenye kuwajibika – wajibu wa maumbile ya kiulimwengu ambayo ni ya walei waaminifu, siyo kwa mapadre au watawa.[128] Majukumu haya ni ya walei kwa namna tofauti, kwa vile hali yao ya kiulimwengu na asili ya kiulimwengu ya wito wao.[129] Kwa kutimiza majukumu haya, walei waaminifu wanayatafsiri mafundisho ya jamii katika vitendo na hivyo kuufanya utume wa Kanisa katika ulimwengu utimizwe.[130]

84. Pamoja na uwepo wa ukomo ambao kimsingi na hususani ni kwa wana na mabinti wa Kanisa, mafundisho yake ya jamii pia yana kikomo cha jumla. Mwanga wa Injili ambao mafundisho ya jamii yanaiangazia jamii inayowamulikia wanaume na wanawake wote, na kila dhamiri na akili ipo katika hali ya kuelewa undani wa maana ya binadamu na tunu zinazojieleza kwake na mawazo ya binadamu na kumfanya awe mwanadamu zaidi katika taratibu za kiutendaji. Mafundisho ya Kanisa yanalenga watu wote – jina na heshima ya binadamu ambayo ni moja na ya pekee, na katika utunzaji wa ubinadamu na kuikuza jamii. Mafundisho yanamlenga kila mtu kwa jina la Mungu mmoja, Muumba na kikomo cha kila mtu.[131] Mafundisho haya ya jamii ni mafundisho yanayoelekeza waziwazi kwa watu wote wenye mapenzi mema,[132] na kwa kweli yanawahusu wanajumuiya wa Makanisa mengine na jumuiya za kikanisa, wafuasi wa mapokeo ya dini zingine na watu ambao siyo washiriki wa kundi lolote la kidini.

f. Katika Ishara Endelevu na Kufanya Upya

85. Kanisa likiongozwa na mwanga wa Injili na kuzingatia mabadiliko ya jamii, Mafundisho yake ya jamii yana sifa endelevu na kufanyiza upya.[133]
Uendelevu wa mafundisho unatokana na tunu zinazochotwa kutoka Neno la Mungu na maumbile ya binadamu. Kwa hiyo mafundisho haya hayategemei tamaduni, itikadi na mawazo mbalimbali. Ni mafundisho endelevu yenye sifa ya “kubaki katika upekee wake, katika msingi wa mvuto na katika kanuni za tafakari, katika vigezo vya kuamua, katika maelekezo ya vitendo, na zaidi yote katika kuunganisha na Injili ya Bwana.”[134] Huu ndiyo msingi na kiini cha kudumu cha mafundisho ya Kanisa, ambacho kinapita ndani ya historia bila kubanwa na historia au kuingia hatari ya kupotea kabisa.

Kwa upande mwingine katika kudumu kuizingatia historia na kujiingiza katika matukio yanayojitokeza, mafundisho ya jamii yanaonesha uwezo, wa kuendelea kutengenezwa upya. Kusimama imara katika kanuni hakuyafanyi yawe ni mafundisho yasiyobadilika.[135] Ni mafundisho ambayo “yanaelekezwa katika mambo ya lazima na fursa ya marekebisho yanayooneshwa katika mabadiliko ya hali ya historia ambayo haikomi kumiminika kutoka mapokeo ambayo yameundwa na maisha ya watu na jamii.”[136]

86. Mafundisho ya jamii yanawasilishwa kama uwanja wa kazi ambako kazi daima inaendelea, ambako ukweli wote unapenyeza na kuingia katika mazingira mapya, kuonesha njia ya haki na amani. Imani haidhaniwi kufungwa na mabadiliko ya jamii na hali halisi za kisiasa ndani ya muundo wa kazi.[137] Bali, kinyume chake: imani huweka chachu ya ubunifu na uumbaji. Kufundisha mara nyingi kunaanza na “kuendeleza kwa njia ya tafakari inayofanyika katika mazingira yanayobadilika ya ulimwengu huu, kwa msukumo wa Injili kama chanzo cha kufanya upya.”[138]

Kanisa kama Mama na Mwalimu, halijiwekei mipaka yake lenyewe, wala halijirudishi nyuma lakini linakuwa wazi, linawafikia na kumgeukia binadamu ambaye kikomo cha wokovu ndiyo sababu ya uwepo wake. Kanisa lipo kuwajali wanaume na wanawake likiwa kielelezo cha Mchungaji mwema, anayetafuta na kumkuta binadamu pale anapoishi na katika historia ya maisha yake. Ni hapa Kanisa linakuwepo kwa ajili ya binadamu pale anapokutana na Injili, ujumbe wa ukombozi na upatanisho wa haki na amani.

 

III. MAFUNDISHO YA KANISA KWA NYAKATI ZETU: MAELEZO YA KIHISTORIA

a. Mwanzo wa Njia Mpya

87. “Mafundisho ya jamii” neno hilo limeanza kuzungumzwa na Papa Pius wa XI,[139] kama mkusanyiko wa mafundisho kuhusu masuala muhimu ya jamii kutoka katika Barua ya Rerum Novarum[140] ya Papa Leo XIII aliyeiendeleza kwa njia ya Majisterio ya Roma na katika ushirika wao wa Maaskofu.[141] Masuala yanayohusu mambo ya jamii hayakuanza na barua hiyo, kwani Kanisa halijawahi kushindwa kutimiza hamu yake katika masuala ya jamii. Hata hivyo, Rerum Novarum inaonesha njia mpya inayotokana na mapokeo ya mamia ya miaka iliyopita, ni alama ya mwanzo mpya na jambo moja la maendeleo ya Kanisa katika maeneo ya jamii.[142]

Katika kuendelea kuwa makini kwa wanaume na wanawake wanaoishi katika jamii, Kanisa limekusanya utajiri wa urithi wa mafundisho. Chimbuko lake likiwa ni Maandiko Matakatifu, hususani Injili na maandishi ya mitume. Baadaye Mafundisho yaliendelezwa na kuchukua sura na muundo kuanzia na mababa wa Kanisa na Wataalamu, Waalimu wakuu wa Karne za Kati hadi kuwa mafundisho msingi bila hata kufikia hatua ya kuwa tamko rasmi la Majisterio. Hivyo Kanisa polepole limetambua uwezo wake katika masuala ya kijamii.

88. Katika karne ya kumi na tisa, matukio ya hali ya uchumi yalileta matokeo makubwa katika jamii, kisiasa na kiutamaduni. Matukio ya Mapinduzi ya viwanda yalibadili kabisa mifumo ya kijamii iliyokuwepo katika karne za zamani na kuleta maswali juu haki na swali la kwanza la jamii kuhusu suala la ajira lililozuka kutokana na mgongano wa mtaji na nguvukazi. Katika mazingira haya, Kanisa lilionja hitaji la kujihusisha na kuingilia kati kwa namna mpya: (mambo haya mapya) res novae yalileta haya matukio yenye kuleta changamoto katika mafundisho yake na kuhamasishwa kwake na hasa kuhusu maisha ya watu. Kuchuja upya mazingira haya kulihitajika, uwezo wa kuchuja ili kutafuta majibu ya kufaa katika matatizo yasiyo ya kawaida na ambayo hayakutazamiwa kulihitajika.

b. Kutoka Rerum Novarum Mpaka Siku ya Leo

89. Katika kujibu swali kubwa la kijamii, Papa Leo XIII alitangaza Barua ya kwanza ya kijamii, Rerum Novarum.[143] Barua inachambua hali ya wafanyakazi wa mishahara na kwa namna ya pekee inawalenga wale wanaofanya kazi viwandani ambao waliishi katika hali mbaya isiyo ya kiutu. Suala la wafanyakazi limezungumziwa kwa upana wake. Barua inachambua masuala ya kijamii na kisiasa ili kuruhusu tathmini kufanyika katika mwanga wa kanuni zilizo katika msingi wa Ufunuo wa Mungu na sheria ya asili na uadilifu.

Rerum Novarum inaorodhesha dosari zinazopelekea matatizo ya jamii, kuweka pembeni itikadi ya ujamaa ikiwa ndiyo dawa na kueleza kwa kina na kwa usahihi na katika hali ya kisasa “Mafundisho ya Kikatoliki kuhusu kazi, haki ya mali, ushirikiano badala ya mapambano ya jamii, haki za wanyonge, heshima kwa maskini na wajibu wa tajiri, ukamilifu kuhusu haki kwa njia ya mapendo, haki ya kuunda vikundi vya wanataalamu.”[144]

Rerum Novarum ilikuja kuwa Barua inayochochea kazi za Kikristo katika eneo la kijamii na kuwa ndio rejea ya kazi hizi.[145] Kiini cha wazo la hati ni kuratibu jamii, kwa mtazamo ambao una majukumu na kutofautisha kigezo cha kuhukumu yale yatakayosaidia kutathmini uwepo wa jamii na mifumo ya siasa na kupendekeza mambo muhimu ya kufanya yanayoendana na mageuzi.

90. Rerum Novarum ilishughulikia suala la kazi kwa kutumia mbinu zinazoweza kuleta “mifano inayodumu[146] kwa ajili ya hatua za maendeleo ya mafundisho ya Kanisa. Kanuni zilizothibitishwa na Papa Leo wa XIII ziliweza kuchukuliwa tena na kujifunza kwa kina katika hati za jamii zilizofuatia. Mafundisho yote ya jamii yanaweza kuonekana kama vile yanafanyiwa marekebisho mapya, uchambuzi wa kina na upanuzi, chanzo chake kikiwa ni Rerum Novarum. Kwa ujasiri wa kuona mbali, alichoandika Papa Leo XIII “alilipatia Kanisa ‘hadhi ya uraia’ kwa kuliwezesha kuzungumza maisha ya umma,”[147] na kutengeneza “Tamko wazi”[148] ambalo limebaki kuwa na “vipengele vya kudumu vya mafundisho ya jamii.”[149] Alithibitisha kwamba masuala mazito ya kijamii “yangeweza kutatuliwa kwa njia ya ushirikiano kati ya nguvu zote”[150] na kuongeza kwamba, “kuhusu Kanisa, ushirikiano wake hauwezi kukosekana kamwe.”[151]

91. Mwanzoni mwa miaka ya 1930, kufuatia matatizo makubwa ya kiuchumi 1929, Papa Pius XI aliandika Barua ya Quadragesimo Anno,[152] ikiwa ni miaka arobaini ya Rerum Novarum. Papa anasema upya yaliyopita kwa mwanga wa uchumi na mazingira ya jamii inayosababisha kupanuka kwa makundi ya fedha kitaifa na kimataifa, na kuongeza madhara yaliyotokana na ukuaji wa viwanda. Ilikuwa baada ya kipindi cha vita, ambapo utawala wa mabavu ulilazimisha Ulaya kuwa na mvutano wa kitabaka uliokuwa mkali zaidi. Barua inaonya hali ya kushindwa kuheshimu uhuru wa kuunda vikundi vya ushirikiano na kusisitiza kanuni za mshikamano na ushirikiano ili kushinda migongano. Mahusiano kati ya mtaji na ajira lazima yawe na tabia ya ushirikiano.[153]

Quadragesimo Anno inathibitisha kanuni za mishahara kuwa zingelengwa na uwiano siyo tu kwa mahitaji ya wafanyakazi, lakini hata familia za wafanyakazi. Dola katika mahusiano na sekta binafsi, ingepaswa kutumia kanuni ya mshikamano, kanuni ambayo itafanywa kuwa kitu cha kudumu cha mafundisho ya jamii. Barua ilikataa uhuru, ulioeleweka kama ni ushindani wa nguvu za uchumi, na kuthibitisha tena mali binafsi, kwa kuangalia tena jamii inavyofanya kazi. Katika jamii inayohitaji uwepo tena wa kujenga misingi ya uchumi, kama jamii ambayo kwa yenyewe imekuwa ni suala la kushughulikia kikamilifu, “Pius XI alionja hitaji na wajibu wa kunyanyua zaidi uelewa, hususani tafsiri na matumizi ya haraka ya sheria zinazoongoza mahusiano yenye nia ya kushinda migongano kati ya matabaka na kufikia muundo mpya wenye misingi ya haki na huruma.”[154]

92. Papa Pius XI hakusita kutamka kupinga matumizi ya utawala wa mabavu uliokuwa umelazimishwa Ulaya wakati wa upapa wake. Tayari tarehe 29 Juni 1931 alipinga matumizi ya nguvu ya mabavu na ya kifashisti katika utawala wa mabavu wa Italia kwa barua Non Abbiamo Bisogno.[155] Alichapisha barua Mit Brennender Sorge, katika mazingira ya Kanisa Katoliki wakati wa utawala wa Hitler (Reich), tarehe 14 Machi 1937.[156] Barua ya Mit Brennender Sorge ilisomwa kwenye mimbari katika kila Kanisa Katoliki Ujerumani. Barua hii ilitolewa kufuatia matumizi mabaya ya madaraka na vurugu na Maaskofu wa Ujerumani ndio waliomwomba Papa kutoa barua hiyo baada ya Reich kuchukua hatua za kutumia nguvu na kuwalazimisha watu mwaka 1936, hasa vijana waliokuwa wanatakiwa kujiorodhesha kama wafuasi wa Umoja wa Vijana wa Hitler. Papa aliongea moja kwa moja kwa mapadre, watawa na walei akiwatia moyo, na kuwasihi kukataa mambo hayo mpaka amani ya kweli imerudi kati ya Kanisa na Dola. Mwaka 1938 hali ya kuwakataa Wasemitiki (Wayahudi) ilienea, Papa Pius XI akakazia kwa kusema “Kiroho sisi sote ni Wasemitiki.”[157]

Kwa Barua ya Divini Redemptoris,[158] kuhusu wasiomwamini Mungu wa kikomunisti na mafundisho ya Kikristo ya jamii, Papa Pius XI alikosoa kwa mpangilio ukomunisti akiuelezea kuwa “haukubaliki kwa silika”[159], na kuonesha njia nzuri ya kusahihisha uovu wa kupindukia ingeweza kuwa ni kufanya maisha ya Kikristo kuwa mapya, yaani kuishi kwa vitendo Injili ya Upendo na huruma, kutimiza wajibu wa haki katika ngazi ya mahusiano ya watu binafsi na ya jamii kuhusiana na manufaa ya wote, na kujenga taasisi za kitaaluma na ushirikiano wa makundi ya wanataaluma.

93. Katika ujumbe wa Papa Pius XII,[160] katika Redio ujumbe wa Krismasi, pamoja na kuingilia kati masuala ya kijamii, tafakari ya majisterio kuhusu utaratibu mpya wa jamii unaongozwa na uadilifu na sheria na kutazama kwa undani katika masuala ya haki na amani, kulifanyika kwa kina. Wakati wa Upapa wake ulichukua miaka ya kutisha ya Vita Vikuu ya Pili ya Dunia na kazi ngumu ya kujenga upya. Hakuchapisha barua nyingine kuhusu masuala ya jamii, lakini katika mazingira mbalimbali tofauti aliendelea kuonesha kujali utaratibu wa kimataifa, ambao ulikuwa umetikiswa vibaya. “Wakati wa vita na baada ya kipindi cha vita, kwa watu wengi wa mabara yote na kwa mamilioni ya waamini na wasio waamini, mafundisho ya jamii ya Papa Pius XII yaliwasilisha sauti ya dhamiri za wote.. Kwa mamlaka yenye hadhi kimaadili, Papa Pius XII alileta mwanga wa busara ya Kikristo kwa watu wasio na idadi wa kila kundi na kila ngazi ya kijamii.”[161]

Moja ya tabia ya Papa Pius XII ya kuingilia kati ni kitu cha “muhimu alichokifanya katika kujenga uhusiano kati ya uadilifu na sheria. Alisisitiza kuhusu sheria ya maumbile kama ni roho ya mfumo wa kujengwa katika ngazi ya kitaifa na kimataifa. Jambo lingine alilokazia Papa, lilikuwa ni matabaka ya wanataaluma na wafanyabiashara kufanya kazi pamoja kwa namna ya pekee ili kufikia manufaa kwa wote.” Kwa sababu ya kuwa kwake macho na akili ya kuelewa ‘alama za nyakati,’ Papa Pius XII angeweza kuchukuliwa kuwa ndiye aliyetoa mwelekeo wa Mtaguso Mkuu wa Pili na mafundisho ya jamii ya Mapapa waliofuata.”[162]

94. Miaka ya 1960 inaleta matumaini ya mambo: kujenga upya baada ya uharibifu ulioletwa na vita, mwanzo kuondoa ukoloni, na alama za mwanzo wa dalili zisizo nzuri za mahusiano kati ya Marekani na Urusi. Hili ni eneo ambalo Mwenye Heri Papa Yohane XXIII alisoma kwa undani kabisa “alama za nyakati,”[163] Suala la jamii linaanza kuwa la wote na kuhusisha nchi zote: Pamoja na suala la kazi na Mapinduzi ya Viwanda, likaja tatizo la kilimo, maendeleo ya mabara, ongezeko la idadi ya watu na kuhusu ushiriki wa kiuchumi duniani. Kukosekana kwa usawa kulikokuweko huko nyuma ndani ya mataifa, sasa kunazidi kuwa kwa kitaifa na hiyo inafanya hali katika Dunia ya Tatu kuwa wazi zaidi na zaidi.

Mwenyeheri Papa Yohane XXIII, katika Barua yake ya Mater et Magistra,[164] “ina lenga kuziweka upya nyaraka ambazo zimekwisha tolewa tayari na kupiga hatua mbele katika mchakato unaohusu jumuiya nzima ya Kikristo.”[165] Maneno ya msingi katika barua ni jumuiya na namna ya kujenga jumuiya.[166] Kanisa linaalikwa katika ukweli, haki na upendo kushiriki katika kujenga ushirika wa kweli na wa kuaminika pamoja na wanaume na wanawake. Kwa njia hii ukuaji wa uchumi hautabaki katika mipaka ya kuridhisha mahitaji ya watu, bali pia utakuza heshima yao.

95. Kwa Barua ya Pacem in Terris,[167] Mwenyeheri Papa Yohane wa XXIII anaweka mkazo katika matatizo ya amani yaliyo kuwepo kipindi cha kuenea kwa silaha za nuklia. Zaidi ya yote, Pacem in Terris ni ya kwanza kuwa na mambo ya ndani katika kutafakari kuhusu haki kwa upande wa Kanisa, ni Barua ya amani na utu wa mwanadamu. Inaendeleza na kukamilisha majadiliano yaliyomo katika Mater et Magistra, na kuendelea katika uelekeo uliooneshwa na Papa Leo XIII. Barua inasisitiza umuhimu wa ushirikiano wa wanaume na wanawake. Ni kwa mara ya kwanza Barua ya Kanisa inatamka na kuwalenga “watu wote wenye mapenzi mema”[168] ambao wamealikwa kwa ajili ya majukumu makubwa: “kuunda ukweli, haki, upendo na uhuru kwa njia mpya za uhusiano na wa watu katika jamii.”[169] Pacem in Terris inazama katika mamlaka ya umma katika jumuiya za ulimwengu, zinazoalikwa “kukabili na kutatua matatizo ya kiuchumi, kijamii, kisiasa au tabia za kiutamaduni zinazoletwa na manufaa kwa wote duniani kote.”[170] Katika kuadhimisha miaka kumi ya Pacem in Terris, Kardinali Maurice Roy, Rais wa Tume ya Kipapa kwa ajili ya Haki na Amani, ilituma barua kwa Papa Paulo VI pamoja na nyaraka zenye mfululizo wa tafakari kuhusu uwezekano ulioonyeshwa katika Barua ya Papa Yohane XXIII kwa vile barua ya Kardinali Maurice Roy ilileta mwanga katika matatizo mapya na suala la kuhamasisha amani.[171]

96. Hati ya Kichungaji ya Kanisa Gaudium et Spes[172] ya Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatikano ni jibu muhimu la Kanisa katika mategemeo ya Ulimwengu wa leo. Katika Hati hiyo, “ikiendana na elimu mpya ya Kanisa, wazo jipya ni kwa vipi tunaweza kuwa jumuiya inayoamini na wana wa Mungu limetafakariwa. Inaamisha kuna hamu mpya ya mafundisho yaliyomo katika Hati iliyotangulia kuhusu ushuhuda wa maisha ya Wakristo, kama njia sahihi za kufanya uwepo wa Mungu duniani uonekane.”[173] Hati kuhusu ulimwengu wa leo Gaudium et Spes inawasilisha hali ya Kanisa “inayostawisha hisia za kuwa na mshikamano wa mbari za binadamu na historia.”[174] Kanisa linatembea safari moja ya binadamu wote na kushiriki matatizo ya dunia pamoja na ulimwengu, ambayo kwa wakati huohuo ni chachu, kama ilivyokuwa, roho ya jamii ya wanadamu na kwa njia ya Kristo kuifanya upya na kuibadili iwe familia ya Mungu.”[175]

Hati ya Kanisa katika ulimwengu wa leo Gaudium et Spes inawakilisha kwa mpangilio unaofaa mada za utamaduni, uchumi, na maisha ya jamii, ndoa na familia, jumuiya za siasa, amani na jumuiya ya watu, katika mwanga wa anthropolojia ya Kikristo na utume wa Kanisa. Kila kitu kinazingatia mwanzo na kumlenga mwanadamu, “kiumbe pekee ambacho Mungu alitaka kiwepo kwa ajili yake chenyewe.”[176] Jamii, miundo na maendeleo lazima vielekezwe katika kuleta “maendeleo ya mwanadamu.”[177] Kwa mara ya kwanza, Majisterio ya Kanisa, katika kiwango cha juu, inaongea kwa mapana kuhusu vipengele vya maisha ya Kikristo duniani: “Ni lazima kutambua kwamba umakini wa Hati kuhusu mabadiliko ya jamii, kisaikolojia, kisiasa, kiuchumi, kimaadili na ya kidini vimezidi kuhamasisha. Kanisa kujali uchungaji katika matatizo ya watu na majadiliano na dunia.”[178]

97. Hati nyingine muhimu ya Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatikano Katika Mafundisho ya jamii ni Tamko Dignitatis Humanae,[179] ambamo haki ya uhuru wa dini imeelezwa waziwazi. Hati inaelezea mada hiyo katika sura mbili. Ya kwanza, ambayo ina tabia ya jumla, inakazia uhuru wa dini misingi yake ni heshima ya binadamu na ambayo lazima ichukuliwe na kusukumwa kama haki ya kiraia katika utaratibu wa kisheria kwa jamii. Sura ya pili inazungumzia katika mwanga wa Ufunuo na kufafanua matokeo yake kiuchungaji, ikionesha kuwa ni haki kutojali watu kama watu binafsi bali pia kama jumuiya mbalimbali za watu.

98. “Maendeleo ni jina jipya la amani.”[180] Papa Paulo VI anatangaza hivyo kwa unyenyekevu na umakini katika Barua Populorum Progressio,[181] ambayo inaweza kuchukuliwa kama mwendelezo wa sura inayohusu mambo ya kiuchumi na ya kijamii yaliyomo katika hati Gaudium et Spes ingawaje pia hati ina mambo mapya ya muhimu. Hususani, inawasilisha dondoo kuhusu maendeleo kamili ya mwanadamu na mshikamano wa binadamu wote: Mada hizi mbili zinachukuliwa kama ndio pande zinaunda hati. Kwa kutamani kusadikisha wapokeaji wahitaji la muhimu na la haraka la mshikamano, Papa anaelezea maendeleo kuwa ni kama mapito kutoka hali ya chini kuelekea hali ya kiutu zaidi na kuonesha tabia zake.”[182] Mapito haya hayaishii katika maeneo ya uchumi au teknolojia peke yake, bali ina maana kumpa kila mtu utamaduni, kuheshimu utu wa wengine, kukiri uwepo wa “wema wa hali ya juu, kumtambua Mungu mwenyewe aliye mwanzilishi na kikomo cha baraka hizi.”[183] Maendeleo yanayonufaisha kila mtu ni jibu la haki inayotakiwa kidunia na kuihakikishia dunia yote amani na kuleta uwezekano wa kufanikisha “ubinadamu kamili”[184] ukiongozwa na tunu za kiroho.

99. Katika hali hii, mwaka 1967, Papa Paulo VI aliunda Tume ya Kipapa “Iustitia et Pax,” hivyo kutekeleza matamanio ya Mababa wa Mtaguso ambao waliichukulia kama “fursa kubwa ambayo mfumo wa Kanisa zima unawekwa ili vyote viwili haki na upendo wa Kristo kwa maskini uweze kuendelezwa kila mahali. “Kazi ya mifumo kama hiyo itaamsha jumuiya ya Kikatoliki kukuza maendeleo katika mabara yenye uhitaji na haki ya kijamii ya kimataifa.”[185] Kutokana na msukumo wa Papa Paulo VI, kuanzia 1968, Kanisa huadhimisha siku ya kwanza ya kila mwaka kuwa ni siku ya Amani Duniani. Papa huyuhuyu alianza mapokeo ya kuandika ujumbe wa mwaka kuelezea mada zinazochaguliwa kwa ajili ya kila Siku ya Amani Duniani. Ujumbe huo unapanua na kutajirisha mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii.

100. Mwanzoni mwa miaka ya 1970, katika hali ya kuchanganya na yenye kuyumbisha pamoja na mvutano mkubwa wa kiitikadi, Papa Paulo VI anarudi tena katika mafundisho ya jamii ya Papa Leo XIII na kuyaweka upya, wakati wa maadhimisho ya miaka themanini ya Rerum Novarum, katika Barua yake ya Kichungaji ya Octogesima Adveniens.[186] Papa anaitafakari jamii baada ya viwanda pamoja na mchanganyiko wa matatizo magumu akionyesha itikadi zisivyojitosheleza katika kujibu changamoto hizi: kuibuka kwa miji, hali ya vijana, hali ya wanawake, kukosa ajira, ubaguzi, uhamiaji, ongezeko la idadi ya watu, athari ziletwazo na njia za mawasiliano ya kijamii na matatizo ya kisaikolojia.

101. Miaka tisini baada ya Rerum Novarum, Papa Yohane Paulo II alitoa Barua ya Laborem Exercens[187] katika kazi, kitu kilicho kizuri na cha msingi kwa binadamu, sehemu ya msingi mno ya shughuli ya uchumi na jibu kwa masuala yote ya jamii. Laborem Exercens inaorodhesha maisha ya kiroho na maadili ya kazi katika mazingira ya misingi ya tafakari ya theolojia na falsafa. Kazi isieleweke katika mwonekano wa vitu tu, lakini ni lazima kazi ionekane kuhusiana na mtu, hivyo kazi wakati wote imwelezee mtu. Ingawaje ni kielelezo cha maisha ya jamii, kazi inaweka mazingira ya utu katika maumbile ya watu na katika wito wao wa asili wa kimungu ambavyo lazima vikamilishwe.

102. Kwa Barua ‘Sollicitudo Rei Socialis,’[188] Papa Yohane Paulo II anaadhimisha miaka ishirini na nane ya Populorum Progressio na anaelezea kwa mara nyingine tena mada ya maendeleo kwa mitazamo muhimu miwili: “Kwa upande mmoja, mazingira yanayochanganya ya ulimwengu wa leo, chini ya kipengele cha kushindwa kufikia maendeleo katika Dunia ya Tatu, na kwa upande mwingine, maana ya hali na mahitaji kwa ajili ya maendeleo yanayomfaa binadamu.[189] Hati inawasilisha tofauti kati ya kupiga hatua na maendeleo, na inasisitiza kwamba “maendeleo hayaishii katika kuzalisha bidhaa na huduma ambavyo mtu mmoja anamiliki, lakini lazima yachangie katika uwepo wa kiumbe mtu. Kwa njia hii maumbile ya maadili kuhusu maendeleo yanatakiwa yaonekane waziwazi.”[190] Papa Yohane Paulo II akionyesha kauli mbiu ya Papa Pius XII, “opus institiae pax” (amani ni tunda la haki), anasema: “Leo, mtu angeweza kusema, kwa maneno sawa kabisa na kwa nguvu sawa ya uvuvio wa biblia (taz. Isa 32: 17; Yak 3: 18), opus solidaritatis pax (amani ni tunda la mshikamano).”[191]

103. Katika kuadhimisha miaka mia moja ya Rerum Novarum, Papa Yohane Paulo II alitangaza Barua yake ya tatu kuhusu jamii, Centesimus Annus,[192] ambayo inaonesha mwendelezo wa Majisterio ya Kanisa kuhusu jamii. Akichanganua upya kanuni za misingi za mwenendo wa Kikristo wa jamii na utaratibu wa kisiasa, ambavyo vilikuwa ndiyo kiini cha mada za hati zilizopita, Papa anaandika: “kitu ambacho leo tunakiita kanuni ya Mshikamano – mara nyingi kilielezwa na Papa Leo XIII ambaye alitumia neno urafiki . Papa Pius XI alirejea akitoa maana ambayo karibu inafanana ‘matendo ya huruma ya kijamii.’ Papa Paulo VI alipanua wazo kubeba maeneo mengi ya sasa ya masuala ya kijamii, anaongelea ustaarabu wa mapendo”.[193] Papa Yohane Paulo II ameonesha namna mafundisho ya jamii yanavyopitia mambo ya Mungu na ya binadamu: kumtambua Mungu katika kila mtu na kila mtu katika Mungu ni hali ya maendeleo ya kweli ya binadamu. Tafakari na upembuzi wa kina kuhusu “mambo mapya,” na hasa tukio kubwa la mwaka 1989 la kuanguka wa mfumo wa Kikomunisti, umeonesha kukubalika kwa demokrasia na uchumi huria, katika mazingira yasiyo na ubishi ya mshikamano.

c. Katika Mwanga na Mvuto wa Injili

104. Hati inayorejewa hapa inaonesha njia ndefu ambamo mafundisho ya jamii yamesafiri tangu wakati wa Papa Leo XIII mpaka leo hii. Muhtasari huu ungeweza kuwa mrefu zaidi iwapo tutafikiria motisha ya mambo yote yaliyoingilia kati, badala ya kuchukua mada maalumu inayohusu “kujali kichungaji katika kuwasilisha jumuiya nzima ya Kikristo na kwa watu wote wenye mapenzi mema kanuni msingi, kigezo cha jumla na mwongozo unaofaa katika kupendekeza maamuzi msingi na vitendo vinavyoambatana katika kila hali halisi ya mazingira.[194]

Katika kutengeneza na kufundisha mafundisho ya jamii, Kanisa limekuwa likiendelea kuchochewa na siyo kwa kuvutwa na nadharia bali na mahitaji ya uchungaji. Kanisa limejitokeza kwa kusukumwa na mawimbi ya jamii yanayowakabili watu, kwa mamia ya wanaume na wanawake, katika utu wa binadamu wenyewe, katika mazingira ambayo “mtu anabeba magumu na machungu kwa uvumilivu ili kutafuta dunia bora, bila kufanya kwa bidii ileile kwa faida ya roho yake mwenyewe.”[195] Kwa hoja hizi, mafundisho ya jamii yamekuja na kuendelezwa kuwa mafundisho ya kisasa ambayo yametengenezwa taratibu, kwani kama Kanisa, katika kutosheleza ufunuo wa Neno katika Yesu Kristo na kwa msaada wa Roho Mtakatifu (taz. 14: 16, 26; 13 – 15) linasoma matukio yanayotokea katika mwenendo wa historia.”[196]

 

SURA YA TATU

MTU NAFSI NA HAKI ZA BINADAMU

I. MAFUNDISHO KUHUSU JAMII NA KANUNI YA MTU NAFSI

 

105. Kanisa linaona katika wanaume na wanawake, katika kila mtu, sura hai ya Mungu. Sura hiyo hupata, na lazima ipate upya, kukua kwa kina na kwa ukamilifu katika fumbo la Kristo, aliye mfano kamili wa Mungu, yule anayemfunulia Mungu kwa mwanadamu, na mwanadamu kwa mwenyewe. Ni kwa wanaume na wanawake hawa, waliopokea heshima isiyopimika na isiyoweza kuondolewa kutoka kwa Mungu mwenyewe, Kanisa linaongea nao, likiwapa huduma ya hali ya juu sana, na ya pekee kabisa, likiwakumbushia daima wito wao maarufu sana, ili waukumbuke daima, na kuustahili. Kristo, Mwana wa Mungu, “Kwa kuutwaa mwili amejiunga kwa namna fulani na kila mtu;[197] kwa sababu hiyo Kanisa linatambua kama wajibu wake wa msingi yaani kazi ya kuona kuwa umoja huo unadumishwa daima na kuwa mpya. Katika Kristo Bwana, Kanisa linaonesha na kujitahidi kuwa wa kwanza kuchukua jukumu la kujiingiza katika njia ya binadamu,”[198] na huwaalika watu wote kutambua katika kila mmoja – walio karibu au mbali, wanaojulikana au wasiojulikana, na hasa katika maskini na wanaoteswa - kaka au dada “ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake” (I Kor 8:11; Rum 14:15).[199]

106. Maisha yote ya jamii ni maelezo yasiyokosa ya ukuu wake: mtu nafsi. Kanisa, mara nyingi na kwa njia nyingi, limekuwa mtetezi mwenye madaraka wa jambo hilo, likitambua na kukiri umuhimu, juu ya yote, wa mtu nafsi katika kila sekta na hali ya jamii. “Jamii ya watu, basi, ni sababu ya mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii, kwa sababu Kanisa haliko nje, wala juu, wala kupita watu waliounganika kijamii, bali liko hasa kati yao na, tena, kwa ajili yao.[200] Utambuzi huo hudhihirishwa katika tamko la kwamba “mbali ya kuwa mhusika au kitu kinachopokea tu maisha ya jamii” mtu nafsi “ni hasa, na anapaswa kudumu kuwa, mtendaji wake, msingi na lengo lake”.[201] Basi, asili ya maisha ya kijamii hupatikana katika mtu nafsi, na jamii haiwezi kukataa kutambua mtendaji wake mwenye kazi na wajibu; kila hali ya jamii lazima ielekee kwa mtu nafsi.

107. Wanaume na wanawake, katika hali halisi ya historia, ni moyo na roho ya fikra za kijamii Kikatoliki.[202] Mafundisho yote ya Kanisa kuhusu jamii, kweli huchukua mwanzo wake katika kanuni inayokiri utu au isiyokiuka ya mwanadamu.[203] Katika matamko mbalimbali ya ujuzi huo, Kanisa hujitahidi hasa kulinda heshima ya binadamu dhidi ya kila jaribio la kupunguza au kuharibu sura yake; zaidi liliwahi kupinga ukiukaji mbalimbali wa heshima ya binadamu. Historia husisitiza kuwa ni kutokana na muundo wa mahusiano ya kijamii kwamba huchipuka baadhi ya uwezo bora wa kuhifadhi hadhi ya mwanadamu, lakini pia upo mwelekeo mkubwa wa kukataa hadhi ya utu wa binadamu.

 

II. MWANADAMU KAMA “MFANO WA MUNGU”

 

a. Viumbe kwa Mfano wa Mungu

108. Ujumbe wa kimsingi wa Maandiko Matakatifu hutangaza kuwa mwanadamu ni kiumbe cha Mungu (taz. Zab 139:14-18), na kuona kwamba kuwa kiumbe cha Mungu ni kiini kinachomdhihirisha na kumtofautisha na viumbe vingine. “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanaume na mwanamke aliwaumba” (Mwa 1:27). Mungu anamweka binadamu kama kiini na kilele cha utaratibu ulioumbwa. Mtu (kwa Kiebrania, “adam”) alifanywa kwa mavumbi ya ardhi (adamah”) na Mungu akampulizia puani pumzi la uhai (taz. Mwa 2:7). Basi, “akiwa mfano wa Mungu, kila mwanadamu ana hadhi ya nafsi, ambaye hawi kitu tu, bali ni mtu mwenye uwezo wa kujifahamu, kuwa na mamlaka juu yake mwenyewe, na kujitoa kwa hiari na kuingia katika mahusiano na mwanadamu mwingine. Zaidi ya hayo, ameitwa kwa neema katika agano na Muumba, na kuitika kwa imani na upendo, ambayo kiumbe mwingine hawezi kwa niaba yake.[204]

109. Kuwa mfano wa Mungu kunaonesha asili na uwepo wa mwanadamu kunahusiana na Mungu katika namna ya ndani kabisa.[205] Huo ni uhusiano wa pekee kimaumbile, na kwa hiyo, si kitu kinachokuja baadaye na sio kitu kinachoongezewa kutoka nje. Maisha ya mtu kwa jumla ni hamu ya kumtafuta Mungu. Uhusiano huo na Mungu huweza kuachwa na hata kusahauliwa, au kupuuzwa, lakini hauwezi kufutiliwa mbali kamwe. Naam, kati ya viumbe vyote vinavyoonekana ulimwenguni, mtu peke yake anamuenzi Mungu “homo est Dei capax”).[206] Binadamu ni nafsi iliyoumbwa na Mungu ili iwe na uhusiano naye; mtu anapata uhai na kujitambua katika uhusiano tu, na hulka yake humwelekea Mungu.[207]

110. Uhusiano kati ya Mungu na mwanadamu hujidhihirisha katika tabia ya kiuhusiano na ya kijamii ya maumbile ya mwanadamu. Kwa kweli, mtu si kiumbe wa upweke, bali “kiumbe wa kujumuika, na asipojihusianisha na wengine hawezi kuishi wala kujiendeleza”.[208] Kwa hiyo, ukweli ni kwamba Mungu alimuumba wanadamu, wakiwa mwanamume na mwanamke (taz. Mwa 1:27) ina maana kubwa sana.[209] Jinsi ilivyo na maana hali ya kutoridhika kwa maisha ya mwanadamu bustanini Edeni wakati maelekeo yake yalikuwa ni ulimwengu wa mimea na wanyama (taz. Mwa 2:20). Wakati tu alipomwona mwanamke, kiumbe kilichokuwa nyama katika nyama yake na mfupa katika mifupa yake (taz. Mwa 2:23), na ndani yake roho ya Mungu Muumbaji ilikuwa hai pia, imeweza kuridhisha hitaji la mazungumzo na mwingine, lililo muhimu sana kwa mwanadamu. Katika jirani, awe mwanaume au mwanamke, kuna taswira ya Mungu mwenyewe, aliye lengo na hatima ya kila mwanadamu.”[210]

111. Mwanaume na mwanamke wana utu na thamani sawa,[211] sio tu kwa sababu wote wawili wameumbwa kwa mfano wa Mungu, lakini zaidi na kiundani ni kwa sababu ya uwezo wa kushirikiana unaohuisha hali ile ya “sisi” katika jozi ya wanadamu, iliyo mfano wa Mungu.[212] Katika uhusiano wa ushirikiano wa wao kwa wao, mwanaume na mwanamke wanatimiliza kwa kina, kujitambua kama nafsi kwa njia ya kuwa zawadi ya wao wenyewe.[213] Agano lao la muungano laoneshwa katika Maandiko Matakatifu kama mfano wa Agano la Mungu na mwanadamu (taz. Hos 1-3; Isa 54; Efe 5:21-33), na wakati huohuo, kama huduma ya uhai.[214] Naam, jozi ya wanadamu inaweza kushiriki katika tendo la Mungu la kuumba: “Mungu akawabariki, Mungu akawaambia, ‘Zaeni mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha” (Mwa 1:28).

112. Mwanaume na mwanamke wana uhusiano na wengine hasa wale ambao uhai wa wengine umekabidhiwa kwao.[215] “Hakika damu ya uhai wenu nitaitaka. ya mwanadamu [na] ya ndugu” (Mwa 9:5), Mungu anamwambia Nuhu baada ya gharika. Kwa mtazamo huu, uhusiano na Mungu unadai kwamba uhai wa mwanadamu uhesabiwe kama kitu kitakatifu.[216] Amri ya tano, “Usiue” (Kut 20:13; Kum 5:17), ina nguvu kwa sababu Mungu peke yake ni Bwana wa uhai na mauti.[217] Kujali ukamilifu wa uhai wa mtu kimwili hufikia kilele chake katika amri inayodai: “Umpende jirani yako kama nafsi yako” (Law 19:18), naye Yesu akaongeza sharti la kujali mahitaji ya jirani (taz. Mt 22:17-40; Mk 12:29-31; Lk 10:27-28).

113. Wakiwa na wito huu wa pekee kwa uhai, mwanaume na mwanamke wanajikuta pia mbele ya viumbe vingine vyote. Wanaweza na wanapaswa kuvitumikisha na kuvifurahia, lakini utawala wao juu ya dunia unadai kuwajibika, sio uhuru holela na wa unyonyaji. Uumbaji wote kwa kweli, una tunu ambayo ni “njema” (taz. Mwa 1:4,10,14,12,18,21,25) machoni pa Mungu aliye mwanzilishi. Mwanadamu anapaswa kutambua na kujali tunu yake. Hii ni changamoto ya ajabu ya akili yake, inayopaswa kumwinua juu kama vile juu ya mabawa[218] kuelekea kwenye ukweli wa viumbe vyote vya Mungu, yaani, kutafakari kwa undani kile ambacho Mungu anakiona kuwa “chema” ndani yao. Kitabu cha Mwanzo kinafundisha kuwa mamlaka ya mwanadamu juu ya ulimwengu yanaonekana katika kuwapa majina ya kila kiumbe hai (taz. Mwa 2:19-20). Akiwapa majina yao, mwanadamu akawatambua jinsi walivyo, na kuweka katika kila mmoja wao uhusiano wa kiuwajibikaji.[219]

114. Mtu ana uhusiano na nafsi yake mwenyewe, na ana uwezo wa kutafakari juu yake mwenyewe. Maandiko Matakatifu yanasema kuhusu moyo wa mtu. Moyo hudokeza mambo ya kiroho ya ndani, kitu kinachotofautisha mwanadamu na viumbe wengine wote. Mungu “kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake; tena ameiweka hiyo milele katika moyo wao, ili kwa jinsi mwanadamu asivyoweza kuelewa kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo hata mwisho” (Mhu 3:11). Hatimaye, moyo huonesha enzi za kiroho, zilizo za pekee kwa wanadamu, na kuwa fahari yake, kwa kuwa ameumbwa kwa mfano wa Muumba wake na akili yenye kupambanua mema na mabaya, na pia utashi.[220] Anaposikiliza uvuvio wa ndani ya moyo wake, kila mwanadamu hana budi kusema naye maneno yenye ukweli aliyosema Mt. Augustino: “Umetufanya kwa ajili yako mwenyewe, ee Bwana, na mioyo yetu haina raha, isipotulia ndani yako.”[221]

b. Msiba mkuu wa Dhambi

115. Dira hii ya ajabu ya mwanadamu kuumbwa na Mungu haitengani na tokeo lenye kushtusha vikali linalohusu dhambi ya asili. Kwa maneno wazi kabisa, Mtume Paulo anajumlisha kuanguka kwa mwanadamu kunakopatikana katika kurasa za kwanza za Biblia: “Kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na mauti kwa njia ya dhambi” (Rum 5:12). Mtu, kinyume na aliyokatazwa na Mungu, anajiruhusu kushawishiwa na nyoka, na kunyosha mkono wake kwa mti wa uzima, na kutekwa na mauti. Kwa tendo hilo, mtu anavuka mipaka yake kama kiumbe, akimjaribu Mungu, Bwana wake pekee na chemchemi ya uhai wake. Ni dhambi ya kutotii (taz. Rum 5:19) inayomtenga na Mungu.[222]

Kutokana na ufunuo tunajua kuwa Adam, mwanadamu wa kwanza, alivunja amri ya Mungu na kupoteza utakatifu na haki alizopata kwa ajili ya wanadamu wote: “Kwa kujiingiza kwa mshawishi, Adam na Hawa walitenda dhambi ya binafsi, lakini dhambi hiyo inaathiri asili ya binadamu ambayo wangepitisha katika hali ya kosa. Ni dhambi itakayorithiwa na wanadamu wote, yaani kwa kupokea asili ya mwanadamu isiyo na utakatifu wa asili na haki.”[223]

116. Kwenye mzizi wa mgawanyo wa binafsi na wa kijamii, ambao kwa ngazi mbalimbali hudhuru tunu na heshima ya nafsi ya mwanadamu, kuna donda linalopatikana ndani kabisa ya nafsi. “Katika mwanga wa imani tunaliita dhambi: kwa kuanza na dhambi ya asili, ambayo kila mmoja anairithi kwa kuzaliwa toka kwa wazazi wa kwanza, hadi dhambi ambazo kila mmoja anatenda anapotumia vibaya uhuru wake”.[224] Matokeo ya dhambi, ambayo ni tendo la kutengana na Mungu, ni mfarakano, yaani, mtu kujitenga, sio na Mungu tu, bali kwa nafsi yake yeye mwenyewe, na watu wengine, na kwa ulimwengu unaomzunguka. “Mfarakano na Mungu husababisha hali mbaya, ya mafarakano na ndugu. Kwa kusimulia ‘dhambi ya kwanza,’ mfarakano na Yahwe huvunja vilevile vifungo vya urafiki ambavyo vinaunganisha familia ya wanadamu. Hivyo, kurasa zinazofuata katika Mwanzo huonesha mwanaume na mwanamke wanaoneshana kidole kila mmoja kwa mwenzake (taz. Mwa 4:2-16). Kadiri ya simulio la Babeli, matokeo ya dhambi ni kutawanya familia ya wanadamu, iliyoanza tayari na dhambi ya kwanza, na sasa kufikia upeo kwa ngazi ya kijamii”.[225] Kwa kutafakari fumbo la dhambi, hatukosi kuchunguza uhusiano wa kutisha kati ya chanzo na matokeo.

117. Fumbo la dhambi lina donda la namna mbili, ambalo mkosefu anafungua kwa upande wake na katika mahusiano na jirani yake. Ndiyo sababu tunaweza kusema kuhusu dhambi binafsi na ya jamii. Kila dhambi ni ya binafsi kwa upande mmoja, kwa upande mwingine dhambi ni ya kijamii, hasa kwa sababu ina matokeo katika jamii. Kwa kweli, dhambi kila mara ni tendo la binafsi, kwa sababu ni tendo huru la mtu binafsi, na hatuwezi kusema dhambi ni ya kundi au jumuiya. Tabia ya dhambi ya jamii inaweza kuwa ni ya kila dhambi, kwa kuzingatia ukweli kwamba “kwa fadhila ya mshikamano wa wanadamu ulio wa fumbo na usioepukika, jinsi ulivyo wa kweli na wazi, kila dhambi ya binafsi kwa namna fulani inawagusa wengine”.[226] Haiwezekani, lakini, kwa uhalali au kukubalika, kuielewa dhambi ya kijamii kama kwamba, kwa ufahamu kamili au pungufu, husababisha kupunguza au kuweza kufuta dhambi ya mtu binafsi anayehusika kwa kukubali tu wajibu na kosa la kijamii. Mwanzoni mwa kila hali ya dhambi daima yuko mtu binafsi anayetenda dhambi.

118. Zaidi ya hayo, baadhi ya dhambi, lengo lake hasa zinaelekea kushambulia jirani. Dhambi za aina hii, kwa namna ya pekee zinajulikana kama dhambi za jamii. Dhambi za kijamii ni dhambi zinazotendwa dhidi ya haki inayopasika katika mahusiano kati ya watu binafsi, kati ya mtu na jumuiya, na pia kati ya jumuiya na mtu binafsi. Dhambi za kijamii ni kila dhambi dhidi ya haki za Binadamu, kuanzia na haki ya uhai, na pamoja na uhai ulio tumboni, na kila dhambi dhidi ya uzima wa mwili wa mtu binafsi: kila dhambi dhidi ya uhuru wa wengine wa kumwamini Mungu na kumwabudu; na kila dhambi dhidi ya heshima na utu wa jirani. Kila dhambi dhidi ya manufaa kwa wote na madai yake katika eneo zima la haki na wajibu wa raia, ni dhambi ya kijamii pia. Mwisho, dhambi ya kijamii ni ile dhambi “inayohusika na mahusiano kati ya jumuiya mbalimbali za watu. Uhusiano huo sio kila mara huwa kadiri ya mpango wa Mungu, anayekusudia kuwepo kwa haki duniani na uhuru na amani kati ya watu binafsi, vikundi na mataifa.”[227]

119. Matokeo ya dhambi yanadumisha miundo ya dhambi. Inasimikwa katika dhambi ya binafsi na hivyo, daima huhusika na vitendo vya mtu binafsi anavyotenda, inaimarika na baadaye huwa shida kuziondoa. Na hivyo, basi, hukua na kuwa yenye nguvu zaidi, huenea na kuwa asili ya dhambi nyingine, na kubana mwenendo wa wanadamu.[228] Hivi ni vikwazo na ukandamizaji unaopita matendo na muda mfupi wa maisha wa mtu binafsi, na kuingilia pia katika mchakato wa maendeleo ya watu, na kuchelewesha yale yanayopaswa kuhukumiwa katika mwanga huo.[229] Matendo na maelekeo yaliyo kinyume cha mapenzi ya Mungu na manufaa ya jirani, na vilevile miundo inayotokana na mwenendo huo, yanaonekana kuhesabiwa katika makundi mawili leo: kwa upande mmoja, tamaa inayoteketeza yote ya faida, na upande mwingine, uchu wa mamlaka, ikiwa na nia ya kushurutisha maoni yake kwa wengine. Kwa ajili ya kueleza vizuri zaidi maelekeo hayo, ingewezekana kuongeza usemi huo: kushurutisha wengine kwa gharama yoyote ile.”[230]

c. Dhambi Inayowafikia Wote, na Wokovu Unaowafikia Wote

120. Mafundisho kuhusu dhambi ya asili, yanayofundisha kuwa wote wako chini ya dhambi, yana umuhimu sana: “Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo kwetu” (Yoh 1.8). Mafundisho hayo yatia moyo kwa wanaume na wanawake wasibaki kwenye makosa wakitafuta kuwasukumia makosa yao watu wengine na kusingizia mazingira, miundo na mahusiano. Mafundisho hayo yafunua wazi udanganyifu huo.

Mafundisho ya kwamba wote wako chini ya dhambi, lakini, yasitengwe katika kutambua wokovu wa wote katika Yesu Kristo. Yakitengwa husababisha mahangaiko yasiyotakiwa ya dhambi na mtazamo mbaya wa ulimwengu na maisha, unaopelekea kudharau mafanikio ya kiutamaduni, na ya kiraia ya wanadamu.

121. Mtazamo wa Kikristo wa mambo yalivyo kweli huona vilindi vya dhambi, lakini ukiangazwa na matumaini, yanayoshinda kila dhambi, yaliyotolewa na tendo la Wokovu wa Yesu Kristo ambamo dhambi na mauti zimeharibiwa (taz. Rum 5:18-21; 1 Kor 15:56-57): “Katika yeye Mungu alimpatanisha mwanadamu naye mwenyewe.”[231] Ni Kristo, mfano wa Mungu (taz. 2 Kor 4:4; Kol 1:15), anayeangaza kabisa na kutimiliza mfano na sura ya Mungu katika mwanadamu. Neno aliyefanyika mwanadamu katika Yesu Kristo amekuwa daima nuru na uzima wa watu, nuru atiaye nuru kila mtu (taz. Yn 1:4-9). Mungu anataka katika mwombezi mmoja, Yesu Kristo Mwanae, wokovu wa wanaume na wanawake wote (taz. 1 Tim 2:4-5). Yesu ni pamoja Mwana wa Mungu na Adamu mpya, yaani, mtu mpya (taz. 1 Kor 15:47-49; Rum 5:14): “Kristo aliye Adamu mpya, akalifunua fumbo la Baba na upendo wake, hudhihirishwa kikamilifu kwa binadamu, binadamu alivyo, na kumjulisha wito wake.”[232] Katika yeye tumekusudiwa na Mungu kufananishwa na mfano wa Mwanae, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi” (Rum 8:29).

122. Hali mpya ambayo Yesu aliyotujalia haitokani na maumbile ya binadamu, wala haikuongezwa toka nje: hasa ni ushirika na Mungu Utatu, na kwake wanaume na wanawake huelekea daima toka kiini cha hulka yao kutokana na kufanana na Mungu kama viumbe. Lakini hiyo pia ni hali halisi ambayo watu hawawezi kuifikia kwa uwezo wao wenyewe. Kwa njia ya Roho wa Yesu Kristo, Mwana wa Mungu aliyejifanya mtu, ambaye katika yeye hali hiyo halisi ilikwishaletwa kwa namna ya pekee, wanaume na wanawake wanapokelewa kama wana wa Mungu (taz. Rum 8:14-17; Gal 4:4-7). Kwa njia ya Kristo, sisi tunashiriki tabia ya Mungu, anayetujalia zaidi sana upeo “kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo” (Efe 3:20). Wanadamu walichopokea tayari ni pungufu ya kuonja au ya “dhamana” (2Kor 1:22; Efe 1:14) kulingana na yale tutakayopokea katika utimilifu, lakini mbele ya Mungu mwenyewe, tutakapomwona “uso kwa uso” (1 Kor 12:13), yaani dhamana ya uzima wa milele: “Na uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee na kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma” (Yn 17:3).

123. Matumaini hayo yaliyo kwa ajili ya watu wote, yanawahusu pia, licha ya wanaume na wanawake wa mataifa yote, mbingu na nchi: “Dondokeni, enyi mbingu, toka juu, mawingu na yamwage haki; nchi na ifunuke, ili kutoa wokovu; nayo itoe haki ikamee pamoja; mimi Bwana nimeiumba” (Isa 45:8). Kadiri ya Agano Jipya, uumbaji wote, pamoja na wanadamu wote wanamngoja Mkombozi: uumbaji ukingali katika uharibifu unatamani kwa matumaini pamoja na maumivu kutaka kuwekwa huru kutoka uharibifu (taz. Rum 8:18 - 22).

 

III. SURA MBALIMBALI ZA BINADAMU

124. Yakithamini sana ujumbe wa Biblia, Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii, msingi wake mkuu usioepukika ni hali ya mtu nafsi. Hivyo yanaweza kubeba mbinu zote za fumbo na utu wa binadamu. Zamani hayakukosa maoni mbalimbali yenye upungufu kuhusu nafsi ya mtu, ambayo mengine bado kwa bahati mbaya yamo katika jukwaa la historia ya siku hizi. Hayo yana tabia ya itikadi au ni matokeo tu ya aina za desturi au mawazo yaliyoenea kuhusu wanadamu, maisha ya watu na lengo lao. Kinachounganisha hayo yote ni kujaribu kudhoofisha sura ya binadamu kwa kukaza mno sehemu moja tu ya sifa zake kwa hasara ya nyingine zote.[233]

125. Binadamu haiwezekani kuchukuliwa kama mmoja aliye kamili kwa peke yake, toka kwa mwenyewe, na ajitegemeaye barabara, asiyetegemea mwingine kamwe ila mwenyewe. Wala binadamu hawezi kufikiriwa kama chembechembe ya kiumbe hai awezaye kukubaliwa kwa kazi yake muhimu ndani ya mfumo mzima. Maoni ya upungufu wa ukweli kamili wa wanaume na wanawake yamekwisha shughulikiwa ipasavyo na Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii mara nyingi, kama kwamba halikuacha kupaza sauti yake dhidi ya hayo, kama vile dhidi ya maoni mengine ya upungufu, likijali, kinyume chake, kutangaza kuwa “watu binafsi hawaonekani kama kitu kamili peke yake mbali na vingine, kama chembe ya mchanga, bali wameunganika na nguvu ya hulka yao na kwa kusudi lililo ndani yao, katika mahusiano yanayoandamana kikamilifu.”[234] Bali limekiri kwamba binadamu hawezi kufikiriwa “kama sehemu tu, chembechembe katika mfumo wa kijamii,”[235] na hivyo, kuangaliwa kuwa binadamu ni muhimu, kusionekane katika maoni kama ya kitu peke yake au katika picha ya kijumla.

126. Imani ya Kikristo, inapokaribisha lililo jema na kustahili binadamu kwa njia yoyote ile (taz. 1 The 5:21),“yuko juu na mara nyingine kinyume na itikadi, na hapo linamtambua Mungu, aliye juu ya yote na Muumba, na ambaye, katika ngazi zote za hulka, anamwalika mwanadamu kama mmoja mwenye majukumu na uhuru.”[236]

Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanajitahidi kuonesha hali mbalimbali za fumbo la binadamu, anayepaswa kuangaliwa “katika ukweli mzima wa kuwemo kwake, na pia kama kiumbe wa jumuiya na jamii,”[237] kwa utaratibu wa pekee wa jinsi ya kutambua wazi mara moja tunu ya binadamu.

 

A. UMOJA WA NAFSI YA BINADAMU

127. Binadamu aliumbwa na Mungu katika umoja wa mwili na roho.[238] Roho iliyo ya kimungu na isiyokufa ni asili ya umoja wa kiumbe binadamu, kwa hiyo yuko kama umoja mzima - corpore et anima unus – kama nafsi. Maelezo hayo licha ya kusisitiza kuwa mwili, ulioahidiwa kufufuka, utashiriki katika utukufu. Zaidi hukumbusha kuwa akili na utashi huru zinalingana na milango yote ya maarifa ya mwili, na hisia zake. Binadamu nafsi, pamoja na mwili, yuko mikononi mwake kabisa, na ni katika umoja wa mwili na roho kwamba nafsi inadhibiti matendo yake ya kimaadili.[239]

128. Kwa njia ya kuwa mwili kweli, mtu anajumlisha ndani yake vitu asili vya ulimwengu huu: ili kwamba vitu hivyo “kwa njia yake viweze kuufikia utimilifu wake na kupata sauti ya kumsifu Muumba kwa hiari.”[240] Hali hiyo inamwezesha binadamu kuwa sehemu ya ulimwengu huu, lakini sio kama katika gereza au ugenini. Haifai kudharau maisha ya mwili; zaidi “mtu. anapaswa kuutazama mwili wake kama mwema na mwenye kustahili heshima, kwa sababu uliumbwa na Mungu, na utafufuliwa siku ya mwisho.”[241] Ijapo, kwa sababu ya hali yake ya kimwili, kwa kujeruhiwa na dhambi, huonja maasi ya mwili, na maelekeo potovu ya moyo wake; anapaswa daima kuwa mwangalifu juu ya hayo, asije kujitumikisha na kutawaliwa na mtazamo wa maisha ya kiulimwengu tu.

Kwa njia ya maisha hayo ya kiroho mtu anajimudu juu ya viumbe vingine na anajiingiza katika ukweli wa miundo ya mambo. Anapoingia ndani ya moyo wake, yaani, anapotafakari lengo lake, anatambua kuwa yuko juu ya vitu vya ulimwengu huu, kwa sababu ya adha yake pekee kama mmoja anayeweza kuongea na Mungu, na chini ya macho yake anachukua maazimio kuhusu maisha yake. Katika maisha yake ya ndani anatambua kuwa binadamu ana “roho yenye uzima wa kiroho na usiokufa” na anajua kuwa binadamu si “punje ya asili tu, au mmojawapo asiye na jina katika mji wa watu.”[242]

129. Basi binadamu ana vipaji viwili tofauti: ni kiumbe cha ulimwengu, akijiunga na ulimwengu na mwili wake, na ni kiumbe wa kiroho, wazi kwa mambo ya juu na kwa kufumbua “kweli za undani,” kwa njia ya akili, “anayoshiriki katika nuru ya ujuzi wa (nuru na fikra za) Mungu.”[243]

Kanisa latamka kwa dhati, “Umoja wa roho na mwili ni wa ndani hivi kiasi cha kuangalia roho kama “sura” ya mwili: ndiyo kusema ni kwa sababu ya mtima wa kiroho, mwili uliofanywa na vitu vinavyoonekana ni mwili wa mtu ulio hai; roho na mambo yanayoonekana katika mtu, siyo asili mbili zinazoungana, bali muungano wao unafanya asili moja tu.”[244] Wala hali ya kiroho inayobeza ukweli wa kimwili wala uchu wa mambo kiulimwengu inayofikiri hali ya kiroho ni ya ufunuo tu wa vitu yote haya hayatoi haki katika kuelewa asili ya mwanadamu kikamilifu.

 

B. WAZI KWA MAMBO YALIYO NJE YA UFAHAMU WA BINADAMU NA UPEKEE WA MWANADAMU

a. Wazi kwa Mambo ya Juu

130. Kuwa wazi kwa mambo ya juu sana yanayopita ufahamu na nguvu ya akili ni katika uwezo wa binadamu aliye nafsi: binadamu ni wazi kwa mambo yasiyo na mipaka ya upeo - Mungu - kwa sababu kwa nguvu ya akili na utashi anainuka juu ya asili yote na juu yake mwenyewe, hana shida kutegemea viumbe, yu huru katika mahusiano na vilivyoumbwa, na kuelekea kwenye ukweli mzima na wema ulio juu na wa pekee. Ni wazi kwa wengine, wanaume kwa wanawake wa duniani hapa, kwa kadiri anavyojifahamu mwenyewe mintarafu “wewe” anaweza kusema “mimi”. Anatoka nje ya mwenyewe, toka kujijali mwenyewe kwa kulinda uhai wake, na kuingia katika mahusiano ya mawasiliano na ushirika na wengine.

Nafsi ya binadamu ni wazi kwa ukamilifu wa kiumbe hai, kwa upeo usio na mipaka wa kiumbe hai. Ana ndani yake uwezo unaopita vitu vyote anavyojua, kwa njia ya kufaulu kuwa wazi kwa kiumbe kisicho na kiasi. Kwa namna fulani roho ya mwanadamu – kwa sababu ya tabia ya kufahamu – ni vitu vyote: “vitu vyote visivyo vya dunia vimekuwa havina mipaka, ikiwa vinashika yote, au kwa sababu ni kutokana na kuwa kitu cha kiroho, kinajimudu kama chapa na mfano wa kila kitu, kama ilivyo na Mungu, au kwa sababu kina mfano katika yote, au ni katika hali ya ‘kuwa’ kama malaika au ni ‘katika hali ya kuweza’ kama kwa roho.[245]

b. Pekee na Asiyekaririwa

131. Binadamu yuko akiwa pekee na asiyekaririwa. Yuko kama “Mimi” anayeweza kujifahamu, kujimiliki na kuazimia mwenyewe. Binadamu nafsi ni mwerevu na mwenye kufahamu, anaweza kujifikiria na kwa hiyo kujitambua mwenyewe na matendo yake. Ijapo sio akili, ufahamu vinavyoweza kumdhihirisha binadamu, hasa ni nafsi iliyo msingi wa matendo ya akili. Lakini sio akili, ufahamu na uhuru ambavyo vinaweza kumweleza mwanadamu, zaidi kuwa ndiye msingi wa matendo ya akili, ufahamu na uhuru. Matendo hayo yanaweza hata kukosekana, kwa vile hata bila matendo hayo, mtu haachi kuwa nafsi.

Binadamu nafsi, lazima daima afahamike kama mmoja asiyekaririwa na kukosewa upekee wake. Kweli, mtu yuko hasa kama nafsi mtendaji, kama asili ya ufahamu na uhuru, na mang’amuzi ya pekee ya maisha, yasiyofananishwa na chochote kingine yenye kukazia kwamba haiwezekani kamwe kujaribu kupunguza hali yake kwa kumshurutisha katika njia zilizokusudiwa au mfumo wa mamlaka, iwe wa itikadi au mwingine. Hiyo inadai hasa sharti sio la hadhi tu kutoka kwa wengine, hasa toka kwa taasisi za kisiasa au za kijamii na viongozi wao, kwa kujali kila mwanaume na mwanamke duniani, na zaidi sana, inamaanisha kuwa juhudi ya kila binadamu kwa wengine, na hasa taasisi hizo, lazima ziweko kwa ajili ya kumwinua mwanadamu na kwa maendeleo kamili ya mtu.

c. Heshima kwa Hadhi ya Binadamu

132. Jamii yenye haki inaweza kuwemo tu ikisimikwa juu ya heshima ya hadhi kamili ya nafsi ya binadamu. Nafsi ya binadamu inadhihirisha kikomo cha jamii, ambacho kimekusudiwa kwa ajili ya nafsi ya binadamu: “Hapo mfumo wa jamii na maendeleo yake bila kosa hufanya kazi kwa manufaa ya binadamu, kwa sababu utaratibu wa mambo unapaswa kuwa chini ya utaratibu wa watu, wala sio kinyume chake”.[246] Heshima kwa hadhi ya binadamu haiwezi kamwe kutengwa na kutii kanuni hiyo. Lazima “kumwona kila jirani, bila hitilafu, kama sawia na mwenyewe, na kujali awali ya yote uhai wake na yote, yaliyo ya lazima kwa kuishi maisha yake kwa hadhi”.[247] Kila programu, ikiwa ni ya siasa, uchumi, ya ustawi wa jamii, ya sayansi na utamaduni, lazima ichukue mwongozo kwa kutambua umuhimu wa kila mwanadamu juu ya jamii.”[248]

133. Basi, haiwezekani kabisa kutumia mwanadamu kwa malengo yasiyohusiana na maendeleo yake, ambayo yanapata utimilifu wake katika Mungu tu na katika mpango wake wa wokovu: kwa kweli, mtu katika undani wake anapita juu ya ulimwengu na yeye pekee ni kiumbe ambaye Mungu alimtaka kwa ajili yake mwenyewe.[249] Kwa sababu hiyo, wala maisha yake, wala maendeleo ya mawazo yake, wala manufaa yake, wala yale yaliyo sehemu ya utendaji wake wa kijamii, haviwezi kuzuiliwa kwa njia isiyo ya haki katika utekelezaji wa haki zao na uhuru.

Mwanadamu nafsi hawezi kuwa chombo cha kutekeleza miradi ya kiuchumi au kijamii iliyoamriwa na mamlaka fulani, hata ikiwa kwa kusingizia maendeleo ya jumuiya ya wananchi kwa jumla, au mtu mwingine yule, iwe ni kwa wakati wa sasa au wa baadaye: basi, lazima watawala wawe makini ili mambo yanayozuia uhuru au mzigo wowote uliowekwa juu ya utendaji wa mtu binafsi zisihatarishe hadhi binafsi, na hivyo kuhakikisha kweli kimatendo haki za binadamu. Zaidi hayo yote, inategemea mtazamo wa utu wa binadamu, yaani, kama mmoja anayehusika na mwenye wajibu wa kukuza mchakato wake wa kukua katika jumuiya aliyomo.

134. Mabadiliko ya kweli ya kijamii yanayofaa na ya kudumu yatakuwepo ikiwa tu yanaleta mabadiliko ya kweli katika maadili ya binafsi. Kuleta tabia ya maadili ya kweli ya maisha ya jamii haiwezekani bila kuanza na watu na kuwa na watu kama lengo la kutazamia: kweli, “kuishi maisha ya maadili hutoa ushahidi kwa heshima ya mwanadamu.”[250] Ni wazi kuwa ni wajibu watu kukuza fikra hizo za maadili zilizo msingi muhimu kwa kila jamii ambayo kweli inataka kuwa kweli ya kibinadamu (haki, uaminifu, ukweli, n.k.), na isiyowezekana kungojewa kutoka kwa wengine, au kukabidhiwa kwa taasisi. Ni wajibu ya kila mmoja, na hasa kwa wale walio viongozi katika nafasi mbalimbali za kisiasa, mahakama au wajibu wa kitaaluma, wana wajibu kwa wengine, kuwa dhamiri ya jamii, na kuwa wa kwanza kuleta katika jamii hali anayostahili binadamu.

 

C. UHURU WA MWANADAMU

a. Tunu na Mipaka ya Uhuru

135. Mtu anauelekea wema tu akiwa na uhuru, ambao Mungu amempa kama moja ya ishara iliyo kuu ya mfano wake.[251] Kwa sababu Mungu alitaka mtu kubaki katika ‘udhibiti wa maamuzi yake mwenyewe’ (Sir 15:14), hivyo anaweza kumtafuta Muumba wake kwa hiari, na kufikia ukamilifu halisi na wenye heri kwa njia ya uaminifu kwake. Hivyo, hadhi yake hudai atende kwa kujua na kuamua kwa hiari, akijitambua mwenyewe na kusukumwa kutoka ndani, wala sio kwa msukumo usiofahamika, wala kwa shuruti toka nje.”[252]

Kwa haki, mtu anathamini uhuru na kujitahidi kwa bidii: kwa haki anatamani na lazima ajenge na kuongoza, kwa nia yake huru, maisha yake binafsi na ya jamii, akipokea wajibu wake kabisa.[253] Kweli, uhuru licha ya kumruhusu mtu kubadilisha vizuri hali ya mambo yake ya nje pia unawezesha ukuzaji wa nafsi yake kwa njia ya kuchagua barabara manufaa yake ya kweli.[254] Kwa njia hii, mwanadamu anajizalisha mwenyewe, yeye ni baba wa nafsi yake,[255] na anajenga mfumo wa jamii.[256]

136. Uhuru si kinyume cha kumtegemea Mungu kama kiumbe.[257] Ufunuo hufundisha kuwa uwezo wa kuamua mema na mabaya si juu ya binadamu, bali ni ya Mungu peke yake (taz. Mwa 2:16-17). “Hakika mtu yu huru, ikiwa anafahamu na kukubali amri za Mungu. Na ana uhuru mpana sana, ikiwa anaweza kula ‘matunda ya kila mti wa bustani’. Lakini uhuru wake sio bila mipaka: husimama mbele ya ‘mti wa ujuzi wa mema na mabaya’, kwa sababu alialikwa kupokea sheria ya maadili iliyotolewa na Mungu. Naam, uhuru wa binadamu hupata utimilifu wake halisi na kamili hasa kwa kukubali sheria.”[258]

137. Utumiaji kamili wa uhuru binafsi unadai hali ya pekee ya utaratibu wa uchumi, jamii, sheria, siasa na utamaduni ambao “mara nyingi hupuuzwa na kuvunjwa. Hali za namna hii za mtu kipofu na isiyo ya haki, hudhuru maisha ya maadili na inawahusu mwenye nguvu na mdhaifu katika kishawishi cha kutenda dhambi ambayo ni kinyume cha upendo. Kwa kujitenga na sheria ya maadili mtu anakiuka uhuru wake mwenyewe, anakuwa mfungwa wa maisha yake mwenyewe, anavunja ushirikiano na majirani, na anaasi ukweli wa Mungu.”[259] Kuondoa yasiyo ya haki kunakuza uhuru wa binadamu na heshima yake: ijapo, “kitu cha kwanza cha kutenda ni kudai au kutaka uwezo wa kiroho na kimaadili wa binafsi na hitaji la daima la wongofu wa moyoni, kama tunataka kufanikisha mabadiliko ya uchumi na ya jamii yaliyo kweli kwa manufaa ya binadamu.”[260]

b. Kifungo kinachounganisha Uhuru na Ukweli na Sheria ya Maumbile

138. Katika matumizi ya uhuru wao, wanaume na wanawake, wanatenda matendo mema yanayojenga mtu binafsi na jamii yakiwa yanatii ukweli, yaani wasipojifanya kuwa Muumba, na mabwana pekee wa ukweli au ya kanuni za maadili.[261] Naam, uhuru hauna “asili yake yenyewe na bila masharti. bali katika maisha unapowekwa na ambamo unajionyesha, kwa namna ile moja, unakuwa na mipaka na pamoja na uwezekano. Uhuru wa binadamu ni mali yetu sisi kama viumbe; ni uhuru wa kupokelewa kama kipaji, wa kupokelewa kama mbegu ya kustawisha kwa wajibu.”[262] Ikitokea kinyume chake, uhuru hufa, na kuharibu mtu na jamii.[263]

139. Ukweli kuhusu mema na mabaya hutambulika kama njia ya kufaa ya kiutendaji na hukumu ya dhamiri, inayoongoza kukubali wajibu kwa mema na mabaya tunayotenda. “Kwa hiyo, kwa njia ya hukumu ya dhamiri juu ya utendaji, inayotwisha wajibu wa kutekeleza tendo fulani, kiungo kati ya uhuru na ukweli huonekana wazi. Hasa kwa sababu hiyo dhamiri inajitambulisha kwa vitendo vya ‘hukumu’ vinavyoelekea katika mema, na sio kwa ‘maamuzi’ holela. Ukomavu na wajibu wa hukumu hizo - hazipimwi na ukombozi wa dhamiri kutoka kwa ukweli halisi, kwa kupendelea kisingizio cha ubinafsi katika kuamua, lakini, kinyume chake, kwa kusisitiza kutafuta ukweli, na kutaka kukubali kuongozwa na ule ukweli katika matendo ya mtu.[264]

140. Zoezi la uhuru linadai sheria ya maumbile ya maadili, yenye tabia kwa ajili ya watu wote, inayotangulia na kuunganisha haki na wajibu. [265]Sheria ya maumbile “si nyingine ila mwanga wa akili uliyotiwa na Mungu ndani yetu. Kwa sababu hiyo tunajua kinachopaswa kufanyika na kinachopaswa kuepukwa. Mwanga huo au sheria hiyo ilitolewa na Mungu kwa hulka.”[266] Ni kushiriki sheria ya milele, iliyo Mungu mwenyewe.[267] Sheria huitwa ‘ya Maumbile’ kwa sababu akili inayoitangaza ni ya kufaa maumbile ya binadamu. Ni ya wote, inaenea kwa mataifa yote, kwa maana imesimikwa katika akili. Katika kanuni za amri zake muhimu, sheria ya Mungu na ya maumbile imetolewa na Amri Kumi za Mungu, na huonesha kanuni ya kwanza na muhimu ya kuongoza maisha ya maadili.[268] Moyo wake ni tendo la kumtamani na kujiweka chini ya Mungu aliye asili na hakimu wa kila kilicho chema, na pia tendo la kuwaona wengine sawa nasi. Sheria ya Maumbile huonyesha hadhi ya nafsi ya mwanadamu, na kusimika msingi wa wajibu za kimsingi za mtu binafsi.[269]

141. Katika tamaduni mbalimbali, sheria ya maumbile inawaunganisha watu, kwa kuunganisha kanuni zilizo sawa. Ijapo utekelezaji wake unapaswa kulingana na hali mbalimbali za maisha kadiri ya mahali, nyakati na mazingira,[270] zinadumu bila kubadilika “chini ya mkondo wa maoni na desturi na hutegemeza maendeleo yao. Hata zinapokataliwa katika misingi yake kabisa, haziwezi kuharibiwa na kuondolewa toka moyoni mwa watu. Hutokea daima tena na tena katika maisha ya watu binafsi na ya jamii.”[271]

Lakini amri zake si kwamba ni wazi na hutambulika mara na kila mmoja. Kweli za kidini na za maadili zinaweza kujulikana “na kila mmoja kwa urahisi, kwa hakika thabiti na bila kuchanganyikiwa na udanganyifu”[272] kwa msaada wa Neema tu na Ufunuo. Sheria ya maumbile hutoa msingi uliotengenezwa na Mungu kwa ajili ya sheria iliyofunuliwa na Neema, kwa kulingana kabisa na kazi ya Roho.[273]

142. Sheria ya maumbile, iliyo sheria ya Mungu, haiwezi kufutwa kwa hali ya dhambi ya binadamu.[274] Inapatikana katika msingi wa maadili kwa ajili ya kujenga jumuiya ya wanadamu na kwa kusimamisha sheria za raia inayochukua matokeo yake yanayoonekana na yenye tabia ya yamkini kutokana na kanuni za sheria ya maumbile.[275] Ikiwa sheria ya maadili imepunguka katika kutambulikana kama ya wote, watu hawawezi kujenga ushirika wa kweli na wa kudumu na wengine, kwa sababu unakosekana ulingano kati ya ukweli na mema, “iwe na kosa au la, matendo yetu yanadhuru ushirika wa watu, kwa hasara ya pande zote.[276] Uhuru tu uliosimikwa katika maumbile ya kawaida, kwa kweli, unawafanya watu kuwajibika, na kuwawezesha kuhalalisha maadili ya umma. Wale wanaojidai kuwa wao wenyewe ni kipimo cha mambo na ukweli hawawezi kuishi kwa amani katika jamii pamoja na watu wengine na kushirikiana nao.[277]

143. Uhuru katika hali ya usiri huelekea kusaliti uwazi, ukweli na wema wa watu, na mara nyingi hupendelea maovu na kujifungia ndani ya ubinafsi, kwa kujiinua katika hali ya kuwa mungu anayeumba mema na mabaya: “Ijapo ameumbwa na Mungu katika hali ya utakatifu, tangu mwanzo kabisa wa historia yake binadamu ametumia vibaya uhuru wake, kwa kusukumwa na Yule Mwovu. Mtu amesimama dhidi ya Mungu na kutafuta kupata lengo lake mbali na Mungu. Mara nyingi kwa kukataa kumtambua Mungu kama chanzo chake, mtu alivunja uhusiano wake wa pekee na pia hatima yake, na pia uhusiano na mwenyewe na wengine na viumbe vyote.”[278] Uhuru wa wanadamu, basi, unahitaji kuokolewa. Kristo kwa nguvu ya Fumbo la Pasaka, anamweka huru mtu kutoka katika upendo usio na utaratibu wa binafsi,[279] ulio asili ya kudharau jirani zake na ya mahusiano yale yanayotiliwa muhuri ya kuwatawala wengine. Kristo anaonyesha kwetu kwamba uhuru unapata hatima yake katika kuwa zawadi kwa wengine.[280] Kwa msalaba wake, Yesu anamweka mtu tena katika ushirika na Mungu na jirani zake.

D. HADHI SAWA KWA WATU WOTE

144.  “Mungu hana upendeleo” (Mdo 10:34: taz. Rum 2:11; Gal 2:6; Efe 6:9), kwa sababu watu wote wana hadhi ile sawa kama viumbe vilivyoumbwa kwa mfano na sura yake.[281] Kutwaa mwili kwa Mwana wa Mungu huonyesha usawa wa watu wote kuhusu hadhi yao. “Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala aliye huru. Hapana mtu mume na mtu mke. Maana nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu” (Gal 3:28; taz. Rum 10:12; 1 Kor 12:13; Kol 3:11).

Kwa kuwa mwangaza wa Mungu hung’aa usoni mwa kila mtu, hadhi ya kila mtu mbele ya Mungu ni msingi wa hadhi ya binadamu mbele ya wanadamu wengine.[282] Zaidi, huo ni msingi halisi wa usawa kabisa na udugu kati ya watu, bila kujali kabila, nchi, jinsia, utamaduni au tabaka.

145. Kwa kutambua hadhi ya binadamu tu, kunawezesha ukuaji wa watu wote na wa mtu binafsi (taz. Yak 2:1-9). Kwa kuchochea aina hii ya ukuaji, lazima kusaidia walau kuhakikisha kweli fursa sawa kwa wanaume na wanawake, na kuhakikisha usawa wa kweli kati ya tabaka mbalimbali mbele ya sheria.[283]

Na pia kuhusu uhusiano kati ya watu na Dola, masharti ya usawa na mgawanyo ni mwanzo wa maendeleo ya kweli kati ya jumuiya ya Kimataifa.[284] Ijapo hatua zinachukuliwa kwa lengo hilo, hatuwezi kusahau kwamba bado kuna tofauti nyingi na aina nyingi za utegemezi.[285]

Pamoja na usawa katika kutambua utu wa kila mtu, na kila nchi, lazima kujua kuwa inawezekana kulinda na kuhifadhi hadhi ya binadamu, ikiwa tu inafanyika katika jumuiya, na watu wote duniani. Kwa njia hii tu ya utendaji wa watu kibinafsi na wa watu wanaojali kweli manufaa ya wanaume na wanawake wote inawezekana kuufikia udugu wa wote ulimwenguni;[286] la, sivyo, kwa kudumisha hali ya tofauti na ngazi mbalimbali iliyo yenye nguvu, hutufanya sote kuwa maskini zaidi.

146.  “Mume” na “Mke” hutofautisha watu binafsi wa hadhi sawa, ambayo haionyeshi tofauti ya kudumu, kwa sababu hali ya pekee ya mwanamke ni tofauti na ile ya mwanamume na tofauti katika usawa ni utajirishaji kwa ajili ya maelewano katika maisha ya jamii: “Hali inayohakikisha haki ya kuwemo kwake mwanamke katika Kanisa na katika jamii ni ufahamu wa ndani zaidi na kamili wa misingi ya hali ya kuwa binadamu, kwa hali ya kuwa mume na kuwa mke kwa nia ya kudhihirisha utambulisho wa mwanamke kuhusiana na mwanaume, yaani, tofauti lakini kukamilishana, sio tu kwa ajili ya kazi, na dhima ya kutekeleza, lakini pia kwa kina zaidi inahusu umbo lake na maana yake kama nafsi.”[287]

147. Mwanamke anamkamilisha mwanaume, sawa kama mwanaume anavyomkamilisha mwanamke: mwanaume na mwanamke wanakamilishana wao kwa wao, sio upande wa mwili tu, sio tu hata kwa upande wa kiakili, lakini pia kama nafsi. Ni kwa sababu hawa wawili “mume” na “mke” ambamo kiumbe “binadamu” amekuwa uhalisia kamili. Ni “umoja wa wawili”[288] ama kwa maneno mengine, uhusiano “umoja-wawili”, unaoruhusu kila mmoja kung’amua uhusiano kati ya nafsi mbili na kila mmoja kwa mwenzake kama kipaji na pia kama utume: “kwa huo ‘umoja wa wawili’ Mungu alikabidhi sio tu kazi ya uzazi na maisha ya familia, bali kuumba historia yenyewe.”[289] “Mwanamke ni ‘msaada’ kwa mwanaume, vile kama mwanaume ni ‘msaada’ kwa mwanamke!”[290] kwa kukutana mwanaume na mwanamke huletwa wazo la umoja la nafsi ya mwanadamu, likisimama sio juu ya umuhimu wa ubinafsi, bali lile la upendo na mshikamano.

148. Binadamu mwenye vilema ni binadamu kamili, mwenye haki na wajibu: “ijapo upungufu na mateso yanayodhuru miili yao na fahamu, inaonyesha wazi zaidi hadhi ya ukubwa wa binadamu.”[291] Kwa sababu mtu mwenye vilema ni mtu mwenye haki zake zote, wanasaidiwa kushiriki katika kila hali ya familia na maisha ya kijamii katika kila ngazi inayowezekana kwao, na kadiri ya uwezo wao.

Haki ya binadamu mwenye vilema inahitaji kuhifadhiwa kwa njia zifaazo na zilizo thabiti: “Haifai kabisa kwa mwanadamu, na kukataa ubinadamu wetu wa kawaida, kwa kukaribisha kwenye maisha ya jumuiya, na hivyo kwenye kazi, wale tu walio wakamilifu. Kufanya hivyo ni kutumia njia mbaya ya ubaguzi, ya wale walio wenye nguvu na afya dhidi ya wale walio wadhaifu na wagonjwa.[292] Unatakiwa uangalifu sana sio kwa hali ya kazi ya kimwili na kiakili, kwa kupata mshahara wa haki, kwa uwezekano wa kupandishwa cheo na kuondoa vikwazo, lakini pia kwa hali ya upendo na hali ya jinsia ya mtu mwenye vilema: “Nao pia wanahitaji kupenda na kupendwa, wanahitaji huruma, ukarimu na upendo”,[293] kadiri ya uwezo wao na kwa kujali utaratibu wa maadili, ulio sawa kwa wasio walemavu na kwa walio walemavu.

E. MAUMBILE YA KIJAMII YA WANADAMU

149. Binadamu ni hasa kiumbe wa kuishi kijamii,[294] kwa sababu Mungu aliyewaumba watu, alitaka hivyo.[295] Maumbile ya kibinadamu, kweli, yanajifunua kama maumbile ya kiumbe anayekubali mahitaji yake. Hii inategemea nafsi iliyo na mahusiano, yaani, jinsi kiumbe aliye huru na mwenye wajibu anatambua shida ya kujihusisha na kusaidiana na wenzake, na ambaye anaweza kushiriki pamoja nao katika mstari wa ufahamu na upendo. “Jamii ni kundi la watu wanaojiunga pamoja na mipango fulani kutokana na kanuni ya umoja unaopita kila mmoja wao. Kama mkutano unaoonekana na usioonekana yaani wa kiroho, jamii hudumu katika wakati: na inachukua yaliyopita na kutayarisha yatakayokuja.”[296]

Basi, ni lazima kukazia kuwa maisha ya jumuiya ni tabia ya kawaida inayotofautisha mwanadamu na viumbe wengine wa dunia. Kazi katika jamii inachukua ishara ya pekee ya binadamu na ya watu kama nafsi anayefanya kazi katika jumuiya ya nafsi: hiyo ni alama inayodhihirisha sura ya ndani ya mtu na imekuwa maumbile yake halisi.[297] Tabia hii ya kuhusiana inachukua, katika mwanga wa imani, maana ya kina zaidi na ya kudumu. Aliyeumbwa kwa mfano na sura ya Mungu (taz. Mwa 1:26), na akiwa anaonekana katika ulimwengu kusudi aishi katika jamii (taz. Mwa 2:20,23) na kutumia mamlaka juu ya nchi (Mwa 1:26,2-30), binadamu, kwa sababu hiyo, anaitwa toka mwanzoni kuishi katika jamii: “Mungu hakuumba mtu aishi ‘peke yake’ bali alitaka awe ‘kiumbe wa kujumuika.’ Maisha ya jamii, basi, si kitu nje ya mtu: yanaweza tu kukua na kukamilisha wito wake katika uhusiano na wengine.”[298]

150. Tabia ya kijamii ya wanadamu haielekei kuwa ya lazima katika ushirikiano kati ya watu wenye kujitoa wenyewe. Kwa sababu ya kiburi na ubinafsi, mtu anatambua ndani yake mbegu za mwenendo wa kijamii, misukumo inayomwongoza kwenye ubinafsi na kutumia wengine.[299] Kila jamii inayostahili, ina hakika ya kusimama katika ukweli, ikiwa wanajamii wote, kwa sababu ya uwezo wa kujua yaliyo mema, wanaweza kuyachukua kwa ajili yao wenyewe na ya wengine. Ni kwa upendo kwa manufaa yao na ya wengine kwamba watu wanaunda vikundi vya kudumu kwa nia ya kupata manufaa ya wote. Jamii mbalimbali ya watu pia lazima waweke kati yao mahusiano ya mshikamano, mawasiliano na ushirikiano, kwa ajili ya kuhudumia watu na manufaa ya wote.[300]

151. Tabia ya kijamii ya wanadamu si ya namna moja bali inaoneshwa kwa njia mbalimbali. Kwa kweli manufaa ya wote hutegemea ubora wa wingi kijamii. Washiriki wa jamii hualikwa kujenga kitu kinacholingana vizuri na chenye umoja, na ndani yake inawezekana kwa kila mshiriki kulinda na kuendeleza tabia zake pekee na uhuru wake. Kila mshiriki – kama familia, jumuiya ya raia, na jumuiya ya dini – anapokea mara moja tabia ya binadamu, kumbe mengine yanatokea zaidi moja kwa moja bila kufikiri.” Kwa kuhifadhi ushirikiano wa wengi zaidi katika maisha ya jamii, kuunda vyama na taasisi za wanaojitolea hupaswa kusukumwa ‘katika mstari wa nchi na wa mataifa, zikiwa na malengo ya uchumi na kijamii, na pia ya michezo, na ufundi mbalimbali, na mambo ya siasa’. ‘Ujamiisho’ huo pia hudhihirisha tabia ya maelekeo kwa ajili ya kufikia malengo yanayopita uwezo wa watu binafsi. Hukuza sifa za mtu, hasa kuhusu jitihada na uwajibikaji, na husaidia kuhakikisha haki zake.”[301]

 

IV. HAKI ZA BINADAMU

 

a. Tunu za Haki za Binadamu

152. Kuelekea kwenye kutambua na kutangaza haki za binadamu ni moja ya majaribu ya kuhifadhi masharti yasiyoepukika ya hadhi ya wanadamu.[302] Kanisa linaona katika haki hizo nafasi maalumu inayojaliwa na nyakati zetu, kwa kukiri haki hizo, kwa kutambua vizuri zaidi hadhi ya wanadamu na kuzihifadhi ulimwenguni kwa wote kama ishara ya pekee iliyoandikwa katika kiumbe chake na Mungu Muumba[303] Majisterio haikukosea kutambua maana ya tunu ya Tamko la Haki za Binadamu iliyoazimiwa na Umoja wa Mataifa Desemba 10, 1948, ambayo Papa Yohane Paulo II alisifu kama “kiashirio katika hatua iliyofikiwa katika njia ya maendeleo kimaadili ya wanadamu.”[304]

153. Kwa kweli mizizi ya haki za binadamu inapatikana katika hadhi iliyo mali yake kila mwanadamu.[305] Hadhi iliyo yake katika maisha ya mwanadamu na sawa kwa kila mwanadamu, inatambulikana na kuelewa kwanza kabisa kwa njia ya akili. Misingi halisi ya haki inaonekana imara pale, ambapo kwa mwanga wa kimungu, hutazamwa kuwa hadhi ya wanadamu, baada ya kutolewa na Mungu na kujeruhiwa sana na dhambi, imechukuliwa na kuokolewa na Yesu Kristo katika kujifanya mtu, kufa na kufufuka.[306]

Asili hasa ya haki za binadamu haipatikani katika matakwa ya binadamu,[307]katika kuwemo kwa Dola, katika mamlaka ya serikali, bali katika mwanadamu mwenyewe, na Mungu Muumba wake. Haki hizo ni “za wote, zisizoweza kukiukwa, zisizoweza kutenguliwa.”[308] Za wote kwa sababu ziko katika kila binadamu, bila tofauti ya wakati, mahali au mhusika. Zisizoweza kukiukwa kwani “zinategemea tabia ya binadamu na hadhi ya binadamu”[309] na kwa sababu ingekuwa bure kutangaza haki, ikiwa kitu hakifanyiki kwa kuhakikisha wajibu wa kuziheshimu toka kwa watu wote, mahali pote na kwa ajili ya wote.”[310] Zisizoweza kutenguliwa kwani “hakuna mtu anayeweza kuzinyima mtu mwingine ye yote yule kisheria, kwa sababu ni kutumia nguvu dhidi ya maumbile.”[311]

154. Haki za binadamu zinapaswa kulindwa sio kwa mtu binafsi, bali kwa jumla: kwa kuzilinda kiasi kungedai namna ya kushindwa kuzitambua. Zinalingana na sharti la hadhi ya binadamu na hudai, awali ya yote, kutimiliza mahitaji ya lazima ya mtu katika mambo ya mwili na ya roho. “Haki hizo zinahusu kila hatua ya maisha na mazingira, ya kisiasa, kijamii, kiuchumi, na kiutamaduni. Pamoja zinaunda kitu kimoja bila wasiwasi kuhusu kuhifadhi maendeleo ya kila mbinu ya manufaa ya mtu pamoja na jamii. Ustawi kamili wa kila sehemu ya haki za wanadamu ni dhamana kwa heshima kamili ya haki ya kila mtu binafsi.”[312] Hali ya kuwahusu wote na ya kutogawanyika ni ishara pekee ya kudhihirisha haki za wanadamu: ni kanuni mbili zinazoongoza, ambazo pia zinadai kuwa haki za binadamu ziwe na mizizi katika kila utamaduni na sura yao ya kisheria ziimarishwe hadi kuhakikisha kwamba zinatekelezwa kikamilifu.[313]

b. Kuziainisha Haki

155. Mafundisho ya Papa Yohane XXIII,[314] Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatikano II, [315] na ya Papa Paulo VI [316] yanatoa maelekezo mengi juu ya wazo la haki za binadamu kama yanavyotoka katika Majisterio. Papa Yohane Paulo II aliandika orodha yao katika Waraka Centesimus Annus: “Haki ya kuishi, ambayo sehemu yake kwa utimilifu ni haki ya mtoto mchanga kukua katika tumbo la mama toka dakika ya kutungwa mimba; haki ya kuishi katika familia iliyounganika na katika mazingira ya maadili kwa kukuza utu wa mtoto; haki ya kukuza akili na uhuru katika kutafuta na kujua ukweli; Haki ya kushiriki kazi inayotumia kwa hekima njia ya kupata mali za dunia, na kupata malipo ya kazi yanayomwezesha yeye mwenyewe na wale wanaomtegemea kuishi; na haki ya kuanzisha familia kwa hiari, kupata watoto na kuwalea, kwa njia ya kutumia uzazi unaowajibika. Kwa namna fulani, asili na jumla ya haki hizo ni haki ya uhuru wa dini, kwa kumaanisha kama haki ya kuishi katika ukweli wa imani yake mwenyewe, na kadiri ya heshima ya hali ya juu ya utu wa mtu.”[317]

Haki ya kwanza inayopatikana katika orodha ni haki kwa uhai, toka kutungwa mimba hadi mwisho wake wa kawaida,[318] iliyo sharti la kuweza kutumia haki nyingine zote, hasa inadai kuwa kila njia ya kutaka kuharibu mimba na kusaidia kufa ni haramu.[319] Mkazo hutiliwa kwa tunu muhimu ya haki ya uhuru wa dini: “watu wote lazima waepushe kila nguvu toka kwa watu binafsi au vikundi vya jamii, kiasi kwamba hakuna asiyeshurutishwa kutenda kinyume na imani yake, iwe sirini au hadharani, akiwa peke yake au katika shirika na wengine, katika mipaka yake.”[320] Kuheshimu haki hiyo ni alama ya maendeleo halisi ya “mtu” katika kila utawala, kila jamii, mfumo au mazingira.”[321]

c. Haki na Wajibu

156. Ikiunganika kwa lazima na mada ya haki, ni suala la wajibu wanaopaswa wanaume na wanawake, inayochukua mkazo unaofaa katika mafundisho ya Majisterio. Kukamilika kwa haki na wajibu, - zinazolingana bila kuweza kutengwa – inarudi mara nyingi , hasa kuhusu mwanadamu ambaye ndiye mmiliki.[322] Kiungo hicho kina pia hali ya kijamii: “katika jamii ya watu, haki ya mtu hufuata wajibu katika watu wengine.”[323] Majisterio hukazia mgongano wa haki bila kukubali wajibu unaoendana. “Wale wanaodai haki zao, na halafu husahau au hawajali kupokea wajibu zinazotokea, ni watu wanaojenga kwa mkono mmoja na kwa mwingine wanabomoa.”[324]

d. Haki za Watu na Mataifa

157. Uwanja wa haki za wanadamu hupanuka hata kuchukua ndani yake haki za watu na mataifa:[325] kwa kweli “iliyo kweli kwa mtu binafsi, pia ni kweli kwa mataifa.”[326] Majisterio husisitiza kuwa sheria za mataifa “zinasimama juu ya kanuni ya heshima sawa kwa Dola, kwa kila nchi haki ya kujiamulia, na kwa kusaidiana kwa uhuru kwa mtazamo wa manufaa ya wote yaliyo bora zaidi.”[327] Amani hukaa juu ya heshima kwa haki za wanadamu, lakini pia kwa haki za mataifa, hasa kwa haki ya kuwa huru, kujitawala.[328]

Haki za nchi si kitu kingine ila “‘haki za wanadamu’ zilizowekwa na kuwezeshwa katika ngazi ya maisha ya jumuiya.”[329] Taifa lina “haki ya pekee ya kuwepo”, kuwa na lugha yake na utamaduni, kwani kwa njia hii taifa linadhihirisha na kustawisha. kimsingi ‘utawala wake wa kiroho,’” “kuumba maisha yake kadiri ya desturi zake, ukiacha, kila ukiukaji wa haki za binadamu na hasa kukandamiza vikundi vidogo,” “kujenga maisha ya baadaye kwa kutumia malezi yanayofaa kwa vizazi vya vijana.”[330] Utaratibu wa kimataifa unadai usawa kati ya yaliyo ya binafsi na ya wote, ambayo mataifa yote huitwa kuleta, kwa sababu, wajibu wao wa kwanza ni kuishi hali ya amani, heshima na mshikamano na nchi nyingine.

e. Kujaza Pengo kati ya Andiko na Roho

158. Tamko rasmi kuhusu haki za binadamu linapingwa na ukweli wa kusikitisha wa ukiukaji, vita na utumiaji nguvu wa kila aina, kwanza kabisa, mauaji ya halaiki na uhamishaji wa wengi, kuenea kama kwamba ni ya ulimwengu mzima, mifumo ya utumwa, kama biashara ya wanadamu, askari vijana, kuwanyonya wafanyakazi, biashara ya madawa ya kulevya kinyume na sheria, ukahaba. “Hata katika nchi zenye mfumo wa serikali ya kidemokrasia, wakati mwingine haki hizo haziheshimiwi.”[331]

Kwa bahati mbaya, kuna pengo kati ya “andiko” na “roho” ya haki za wanadamu,[332] inayosababishwa na kutambua haki hizo kwa maneno tu. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii, kwa kuzingatia upendeleo wa kiinjili inayowapa maskini, yanarudia kusema tena na tena kuwa “aliye na bahati zaidi anapaswa kujinyima baadhi ya haki zake kwa ajili ya maskini na hivyo kutumia mali zao kwa ukarimu zaidi kwa utumishi wa wengine” na kwamba kukazia usawa “kunaweza kuhifadhi ubinafsi, ambamo kila mmoja anadai haki zake bila kutaka kuitikia manufaa ya wote.”[333]

159. Kanisa linatambua kuwa utume wake wa kidini pekee unabeba pia jukumu la kulinda na kuhifadhi haki za binadamu,[334] linaheshimu sana hatua iliyofikiwa leo ya kuhifadhi popote haki hizo.”[335] Kanisa linang’amua kwa kina ulazima wa kuheshimu haki[336] na haki za binadamu[337] kati ya safu zake.

Jitihada hiyo ya kichungaji huelekea katika njia mbili: katika kutangaza asili ya Kikristo ya haki za binadamu na kulaani ukiukaji wa haki hizo.[338] Kwa vyovyote, “utangazaji daima ni wa maana zaidi kuliko kulaani, na hii ya pili haiwezi kutojali ya kwanza, ambayo inathibitisha na kutia nguvu na nia ya hali ya juu zaidi.”[339] Kwa kufaulu zaidi, jitihada hiyo ni wazi kwa ushirikiano wa kiekumeni, kwa majadiliano na dini nyingine, na mikutano inayofaa na taasisi nyingine, ya kiserikali na isiyo ya kiserikali, katika kiwango cha nchi na cha kimataifa. Kanisa linaamini juu ya yote, msaada ya Bwana na wa Roho wake, aliyemiminwa katika mioyo ya watu, kuwa ni dhamana ya kuheshimu haki na haki za wanadamu, na kutoa mchango kwa amani. “Kustawisha haki na amani katika sehemu zote za jamii ya wanadamu, kwa mwanga na chachu ya Injili imekuwa daima lengo la jitihada za Kanisa katika kutekeleza amri ya Bwana.”[340]

 

SURA YA NNE

KANUNI ZA MAFUNDISHO YA KANISA KUHUSU JAMII

I. MAANA NA UMOJA

 

160. Kanuni za kudumu za mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii[341] ndio msingi wa mafundisho ya jamii ya Kanisa Katoliki. Hizi ni kanuni za heshima ya binadamu ambazo zimehusika katika sura iliyotangulia, ambayo ni msingi wa kanuni na yaliyomo katika mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii.[342] Kanuni hizo ni manufaa kwa wote; auni; na mshikamano. Kanuni hizi, maelezo ya ukweli wote wa mtu unaojulikana kwa akili na imani, zimezaliwa na “kukutana na ujumbe wa Injili na hitaji la kuweka katika muhtasari wa amri kuu ya mapendo kwa Mungu na kwa jirani katika haki pamoja na matatizo yanayojitokeza katika maisha ya jamii.”[343] Katika mwenendo wa historia na mwanga wa Roho, Kanisa limetafakari kwa busara kadiri ya mapokeo ya imani na limeweza kutoa kwa usahihi wote msingi na sura za kanuni, na kuendelea kuzielezea katika kujaribu kujibu kadiri ya mahitaji ya nyakati na hatua za maendeleo ya maisha ya jamii.

161. Kanuni hizi za jumla na zenye tabia ya msingi, kwa kuwa zinahusu hali halisi ya jamii yote; kuanzia mahusiano ya karibu na ya papo kwa hapo yanayopatanishwa kwa siasa, uchumi, na sheria, mahusiano miongoni mwa jumuiya na vikundi na mahusiano kati ya watu na mataifa. Kwa sababu ya kudumu kwake kwa wakati na maana yao ya kijumla kidunia, Kanisa linaweka hayo kama kitu cha kwanza, cha msingi kwa vipimo vya rejea kwa ajili ya kutafsiri na kutathmini jamii zinavyoonekana. Navyo ni chanzo cha lazima cha kutafutia vigezo vya kutumia katika kupima mwelekeo wa mwingiliano wa jamii kwa kila eneo.

162. Kanuni za mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii lazima zitambulike katika umoja wake, hali yake ya kiuhusiano na maelezo yake yenye ufasaha. Mahitaji haya msingi wake ni maana ambayo Kanisa lenyewe linayaona ya mafundisho hayo kama muunganiko wa mafundisho yanayotafsiri hali halisi ya jamii ya Kisasa kwa mpangilio wa kufaa.[344] Kuchunguza kanuni hizi moja moja lazima kusielekeze katika kuzitumia kwa sehemu tu au kwa njia ya kimakosa. Kufanya hivyo ni kuona kuwa yametangazwa pasipo kuunganishwa na kuhusiana kila moja na nyingine. Uelewa wa nadharia ya kina kabisa na matumizi halisi ya hata moja tu ya kanuni hizi za kijamii inaonesha wazi, kutegemeana, kukamilishana na kuhusiana ambayo ndio sehemu ya muundo wake. Kanuni hizi ni msingi wa mafundisho ya jamii, zaidi ya hayo, zinawakilisha urithi wa kudumu wa tafakari, ambayo pia ni sehemu muhimu ya ujumbe wa Kristo, kwani zinaonesha njia zinazoweza kutumika katika kujenga maisha mazuri ya kijamii, ya kuaminika na yaliyo mapya.[345]

163. Kanuni za mafundisho ya jamii, kwa ujumla wake, yana jambo la kwanza linalouweka ukweli wa jamii waziwazi, ambao unatoa changamoto kwa kila dhamiri na kutoa mwaliko wa kuchanganyika na kila dhamiri nyingine katika ukweli, katika uwajibikaji unashirikisha kikamilifu watu wote na pia kujali watu wote. Kwa kweli, mtu hawezi kukwepa suala la uhuru na maana ya maisha ya jamii, kwa kuwa jamii ni uhalisi ambao siyo kitu cha nje wala siyo kigeni katika hali yake.

Kanuni hizi zina umuhimu mkubwa wa dhamiri kwa sababu zinarejea kwenye misingi ya ukamilifu na mpangilio wa maisha katika jamii. Kuyaelewa yote vizuri ni lazima kutenda kadiri yanavyoeleza kufuata njia ya maendeleo inayoonesha maisha yenye kufaa binadamu. Hitaji la maadili ya kanuni za muhimu zinazohusu tabia za watu binafsi – na hapo ni kwamba watu ni wa kwanza wenye wajibu usioepukika wa maisha ya jamii katika maeneo yao yote na wakati huohuo katika taasisi zinazowakilishwa kisheria, taratibu za kidesturi na uundaji wa raia, kwa sababu ya uwezo wa kuathiri na hali ya chaguzi za watu wengi kwa muda mrefu. Kwa kweli, Kanuni hizi zinatukumbusha kwamba vyanzo vya jamii inayoishi katika historia vinapatikana katika muunganiko wa uhuru wa watu wote ambao wanachanganyikana, katika uhuru huo kuchangia ama kuujenga au kuuharibu.

 

II. KANUNI YA MANUFAA KWA WOTE

 

a. Maana na Mielekeo ya Msingi

164. Kanuni ya manufaa kwa wote, katika kila eneo la maisha ya jamii lazima ihusiane, iwapo itafikia maana ya ukamilifu wake, inaanzia katika heshima, umoja na usawa wa watu wote. Kadiri ya msingi na upana unaokubalika, manufaa kwa wote inaonesha “jumla yote ya hali ya jamii ambayo inaruhusu watu, ama kama makundi au kama mtu mmojammoja, kufikia utimilifu wa kutosheleza na kwa urahisi zaidi.”[346]

Manufaa kwa wote sio jumla ya manufaa ya kila mtu katika jamii. Kuhusika kwa kila mmoja na kila mtu, inabaki “kwa ajili ya wote,” kwa sababu hayagawanyiki, na kwa sababu watu wote kwa pamoja ndipo tu wanaweza kuyafikia, kuongeza na kulinda umadhubuti wake kwa kuhusisha pia hali ya baadaye. Kama ilivyo kwa matendo ya kimaadili ya mtu mmojammoja yanavyokamilishwa kwa kufanya yaliyo mema, ni hivyohivyo matendo ya jamii yanaleta utimilifu kamili yanapoleta manufaa kwa wote. Manufaa kwa wote inaweza kueleweka katika upande wa kijamii na kijumuiya wa maadili yanayokubalika.

165. Jamii ambayo inataka na ina nia ya kubaki katika kuhudumia binadamu katika nyanja mbalimbali, hiyo ni jamii inayojali na yenye manufaa kwa wote - manufaa ya watu wote na ya mtu kamili [347] kama ndiyo lengo la msingi. Binadamu hawezi kufikia ukamilifu katika yeye mwenyewe, pamoja na ukweli kwamba anaishi “na” wengine na “kwa ajili ya” wengine. Ukweli huu hauhitaji tu kuishi na wengine katika nyanja mbalimbali za maisha ya jamii, bali hutafuta bila kuchoka kimatendo na siyo tu kwa kuwaza manufaa, yaani maana na ukweli, unaopatikana kwa njia ya jamii za watu. Hakuna kielelezo cha maisha ya jamii – kutoka katika familia hadi katika jamii ya makundi ya karibu, mashirika, wanaoshughulikia mambo ya uchumi, miji, mabara, Dola, hadi jumuiya za watu na mataifa wanaoweza kukwepa suala manufaa kwa wote kwani katika hili kuna kipengele muhimu cha umaana na sababu za kuaminika za uwepo wake huo.[348]

b. Wajibu wa Kila Moja katika Manufaa ya Wote

166. Hitaji la manufaa kwa wote linategemea hali ya jamii kwa kila kipindi cha kihistoria na iliyounganika kabisa kwa kuzingatia kumwinua na kumkuza binadamu kwa jumla na haki zake za msingi.[349] Mahitaji haya zaidi ya yote, yanahusika na kujitoa kwa ajili ya imani, mpangilio wa mamlaka ya serikali, muundo thabiti wa sheria, ulinzi wa mazingira na upatikanaji wa huduma za lazima kwa wote, ambazo kwa wakati huohuo ni haki za binadamu: chakula, malazi, ajira, elimu na uhuru wa tamaduni, usafiri, afya, uhuru wa mawasiliano na kulinda uhuru wa dini.[350] Wala mtu asisahau wajibu wa kutoa mchango wa kila taifa unaohitajika katika kujenga ushirikiano wa kweli kidunia kwa ajili ya manufaa kwa binadamu wote na kwa vizazi vijavyo pia.[351]

167. Manufaa kwa watu yanahusu wanajamii wote, hakuna anayeweza kukwepa ushirikiano kadiri ya uwezekano wa kila moja, katika kuyafikia na kuyaendeleza.[352] Manufaa kwa wote lazima yahudumiwe katika utimilifu wake, na siyo kwa mtazamo nusunusu unaoongozwa na watu waliouweka kwa faida yao binafsi, bali lazima itegemee mantiki inayochukulia uwajibikaji mkubwa. Manufaa kwa wote inaendana na silika za juu kabisa za binadamu,[353] lakini ni tunda ambalo ni vigumu kulifikia kwa sababu wakati wote unahitajika uwezo wa kudumu na nguvu ya kutafuta manufaa ya wengine kama vile ni manufaa ya mtu mwenyewe binafsi.

Kila mmoja anayo haki ya kufurahia hali ya maisha ya jamii yanayoletwa na hamu ya kutafuta manufaa kwa wote. Mafundisho ya Papa Pius XI bado yana maana: “Mgawanyo wa mali zilizozalishwa ambazo, kama kila mtu mwenye kutafakari, anavyojua leo yanafanyiwa kazi katika hali ya uovu mkubwa kutokana na tofauti kubwa kati ya watu wachache wanaozidi kuwa matajiri na watu wengi wanaobaki bila mali, lazima liangaliwe upya na kufanyiwa kazi kwa taratibu zinazozingatia manufaa ya wote, yaani, haki ya jamii.”[354]

c. Jukumu la Jumuiya ya Kisiasa

168. Wajibu wa kufikia manufaa kwa wote, licha ya kuwa ni watu binafsi, pia inahusu serikali, kwa vile manufaa kwa wote ni sababu za uwepo wa mamlaka ya kisiasa.[355] Kwa kweli, Serikali ni lazima iwahakikishie uwepo wa umoja na mpangilio wa jamii yake ya kiraia,[356] ili kwamba manufaa kwa wote yafikiwe kwa mchango wa kila raia. Mtu binafsi, familia na makundi ya karibu hayawezi kufanikisha maendeleo kamili wenyewe kwa ajili ya kuishi maisha ya kibinadamu kweli. Hivyo, ndio ulazima wa taasisi za siasa, ambazo lengo la uwepo wake ni kuwapatia watu vitu vya lazima, utamaduni, maadili na mambo ya kiroho. Lengo la maisha katika jamii kwa kweli ni kuyafikia manufaa kwa wote kwa misingi ya kihistoria.[357]

169. Kuhakikisha manufaa kwa wote, serikali ya kila nchi ina wajibu wa pekee wa kupatanisha mapendeleo ya sekta mbalimbali na mambo yanayohitajika kwa ajili ya kuzingatia masuala ya haki.[358] Kupatanisha ipasavyo mali fulani za makundi ya watu na ya mtu mmojammoja, ni moja kati ya majukumu nyeti ya mamlaka ya umma. Zaidi ya haya, ni lazima isisahaulike kwamba katika Serikali ya Kidemokrasia ambako maamuzi huwa yanafanywa na walio wengi kutoka wawakilishi wa watu waliochaguliwa na watu, wale ambao wanawajibika kwa serikali wanatakiwa kutafsiri manufaa kwa wote katika nchi na siyo kadiri ya mwongozo wa walio wengi, bali pia kadiri ya mazuri ya mahitaji ya wanajumuiya wote, pamoja na wale walio wachache.

170. Manufaa kwa wote ya jamii siyo mwisho katika yenyewe, yana thamani tu yanapolenga kufikia kikomo cha utimilifu wa mtu na manufaa ya jumla ya uumbaji wote. Mungu ni kikomo cha utimilifu wa uumbaji wake na hakuna hoja inayoweza kuondoa manufaa kwa wote katika upande wa kimungu, ambao unavuka upande wa kihistoria ambayo wakati huohuo unaitimiliza.[359] Mtazamo huu unafikia utimilifu wake kwa njia ya fadhila ya imani katika Pasaka ya Yesu aliyetoa mwanga kwa ajili ya kufikia manufaa kwa wote yaliyo kweli kwa binadamu. Historia yetu, kwa jitihada ya mtu binafsi na nguvu za pamoja kuhusu kuinua hali ya binadamu inaanza na kukomea katika Yesu: shukrani kwake, kwa njia yake na kwa mwanga wake kwa kila hali halisi, pamoja na jamii, inaweza kukamilisha utimilifu wake Mkuu. Kuwa na dira ya kihistoria na mtazamo wa mambo ya kiulimwengu tutaishia kugeuza manufaa kwa wote kuwa ustawi wa kijamii-kiuchumi tu bila kuwa na lengo la kimungu, yaani bila sababu yake ya ndani ya uwepo wake.

 

III. KIKOMO CHA MALI KWA JUMLA

a. Chanzo na Maana

171. Kati ya mambo mengi yanayopelekea manufaa kwa wote, umuhimu wa moja kwa moja unachukuliwa kama kanuni ya jumla ya kikomo cha mali: “Mungu aliweka kikomo cha dunia na vyote vilivyomo ndani yake kwa watu wote na binadamu wote ili kwamba vitu vyote vilivyoumbwa vingeweza kutumika kwa kushirikisha vizuri kwa kuongozwa na haki na mapendo.”[360] Kanuni hii msingi wake ni ukweli kwamba “Chanzo asili cha yote yaliyo mema ni tendo la Mungu, aliyeumba dunia na binadamu, aliyetoa dunia kwa binadamu ili aweze kutawala kwa kazi zake na kufurahia matunda yake (Mwa 1: 26 – 29). Mungu alitoa dunia kwa binadamu wote kwa ajili ya kuwaendeleza wote, bila kumweka pembeni au kumpendelea yeyote. Huu ni msingi wa jumla wa kikomo cha mali za dunia. Dunia kwa sababu ya hali yake ya kuzalisha na uwezo wa kuridhisha mahitaji ya kibinadamu, ni zawadi ya kwanza ya Mungu kwa ajili ya kutunza uhai wa binadamu.”[361] Binadamu hawezi bila mali zinazoendana na mahitaji ya msingi na mambo ya msingi yanayowezesha uhai na uwepo wake; mali hizi ni ulazima usioepukika, ikiwa lazima ajilishe mwenyewe, akue, awasiliane, ashirikiane na wengine, na afikie lengo la juu kabisa ambalo ndiyo wito wake.[362]

172. Haki za dunia za jumla katika kutumia mali msingi wake ni kanuni ya kikomo cha jumla cha mali. Kila mtu lazima apate kiwango cha kumwezesha katika maendeleo kamili. Haki ya matumizi ya mali kwa ajili ya wote ni “kanuni ya kwanza ya maadili na utaratibu wa jamii.”[363] na “tabia ya kanuni za Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii.”[364] Kwa sababu hii, Kanisa linaonja kubanwa na wajibu wa kudhihirisha hali na tabia ya kanuni. Kwanza kabisa, haki ya asili iliyomo ndani ya maumbile ya wanadamu na siyo tu haki chanya iliyoungana na historia ya mazingira, zaidi ya hayo ni haki ya “kurithi”[365] Ni yenye asili iliyo ndani ya binadamu na kwa kila mtu, na ni kipaumbele kuhusiana na kuingilia kati mambo ya mali, katika suala lolote la mfumo wa kisheria kuhusu hilohilo, na kwa mfumo wa kiuchumi au kijamii au kwa mbinu: “Haki nyingine zote, hata zingekuwaje ikiwa ni pamoja na haki ya mali na haki za uhuru wa biashara lazima ziwe chini ya utaratibu huu [kikomo cha jumla kuhusu mali]; ni lazima isizuie, bali ziharakishe matumizi yake. Ni lazima ziangaliwe kwa makini na kwa haraka wajibu wa kurejea haki zake za lengo la mwanzo.”[366]

173. Kuweka kanuni za jumla za kikomo cha mali katika matumizi halisi, kadiri ya mazingira ya kiutamaduni na kijamii, ina maana njia, kikomo na vitu lazima vipewe tafsiri sahihi. Kikomo cha jumla na matumizi ya mali havina maana kwamba kila kitu ni kwa ajili ya kila mtu au watu wote, au kitu hichohicho kinaweza kuwa na maana au kinahusu kila mtu au watu wote. Ni kweli kwamba kila mmoja amezaliwa na haki ya kutumia mali za dunia, vilevile ni kweli ili kuhakikisha kwamba haki hii imetumika katika hali ya usawa na utaratibu wa kufaa, kuingilia kati kunakoratibiwa ni jambo la lazima, kuingilia kati ambako ni matokeo ya makubaliano ya kitaifa na kimataifa, na utaratibu wa sheria unaamuliwa na kuwekewa bayana matumizi ya haki.

174. Kanuni ya jumla kuhusu kikomo cha mali ni mwaliko wa kuendeleza mtazamo wa uchumi unaohamasisha tunu za kimaadili zinazoruhusu watu wasipoteze hali ya kuona mwanzo au madhumuni ya mali hizi, ili kujenga ulimwengu wa kufaa wa mshikamano, ambamo vigezo vya utajiri vinaweza kufanya kazi yenye kuleta mafanikio. Utajiri, kama unavyoonekana, unawasilisha uwezekano huu wa njia mbalimbali ambazo zinaweza kujieleza kama matokeo ya mchakato wa uzalishaji ambao unafanya kazi pamoja na teknolojia na rasilimali za kiuchumi, vyote viwili yaani vya asili na vya kutengeneza. Matokeo haya yanaongozwa na rasilimali, mipango na kazi, na kutumika kama njia ya kuinua ustawi wa watu wote na mataifa yote na kuzuia wengine kuwekwa pembeni na kunyonywa.

175. Kikomo cha mali kwa jumla kinahitaji jitihada za pamoja kupata kwa kila mtu na watu wote hali ya lazima kwa maendeleo yanayounganika, ili kila mmoja aweze kutoa mchango wa kujenga dunia yenye ubinadamu zaidi, “ambamo kila mmoja anaweza kutoa na kupokea, na kwamba maendeleo ya baadhi hayatakuwa tena kizuizi cha wengine, wala hayawi uwanja wa kuwatumikisha.”[367] Kanuni hii inaendana na wito uliotengenezwa na Injili kwa watu na jamii za nyakati zote, zilizoshawishiwa kwani wakati wote wana hamu kumiliki, vishawishi ambavyo bwana Yesu alichagua kupitia (taz. Mk 1: 12 – 13; Mt 4: 1 – 11; Lk 4: 1 – 13) ili kufundisha watu namna ya kushinda hayo yote kwa neema yake.

b. Kikomo cha Jumla cha Mali na Mali ya Binafsi

176. Kwa njia ya kufanya kazi na kutumia zawadi ya akili, watu wanao uwezo wa kutawala dunia na kuifanya iwe mahali bora pa kuishi. “Kwa njia hii, anaitengeneza dunia iwe sehemu yake, na kwa vile anaipata kwa njia ya kazi, huu unakuwa ndio mwanzo wa mali ya binafsi.”[368] Mali ya binafsi na aina nyingine za kumiliki mali ya binafsi “unamhakikishia mtu ulazima wa hali ya juu katika eneo la kuishi maisha yake kwa namna ya kujitegemea yeye binafsi na familia yake na hii inafikiriwa kama ni kupanua uhuru wa mwanadamu. unaoamsha kutekeleza majukumu ambako kunahusu moja ya hali ya uhuru wa raia.”[369] Mali binafsi ni kitu cha lazima chenye kuaminika kwa jamii na sera ya kiuchumi ya kidemokrasia, na inathibitisha usahihi wa taratibu za jamii. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanataka umilikaji wa mali lazima uwepo kwa ajili ya wote [370] ili wote wawe, walau na kiasi fulani cha kumiliki, na kutokuwepo kwa hali za kusaidia “ukandamizaji unaochukuliwa kama kitu cha kawaida.”[371]

177. Mapokeo ya Kikristo hayajawahi kutambua haki za mali binafsi kama mali isiyoguswa kabisa. “Kinyume chake, daima haki hii imeeleweka kwa mtazamo mpana unaoonesha haki ya wote katika matumizi ya mali ya uumbaji wote: Haki ya mali binafsi iko chini ya haki kwa matumizi ya wote, ili kwamba mali iwe kwa ajili ya kila mmoja.”[372] Kanuni ya kikomo cha mali kwa jumla ni uthibitisho wa umiliki kamilifu na wa muda wa Mungu na yeye kama Bwana wa yote na wa mahitaji ambayo mali yote iliyoumbwa naye inabaki wakati wote kulenga utimilifu wa maendeleo ya mtu kamili na binadamu wote.[373] Kanuni hii haipingani na haki za mali ya mtu binafsi,[374] bali inaonesha hitaji la marekebisho ya kufaa. Mali ya binafsi, bila kujali marekebisho na taratibu za kisheria zinazohusika, kwa hali yake ni chombo peke yake chenye kuheshimu kanuni za jumla za kikomo cha mali, kwa uchambuzi wa mwisho kabisa, kwa hiyo, siyo mwisho, bali ni njia.[375]

178. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanatoa wito wa kutambua kazi ya jamii inayohusu aina yoyote ya umiliki mali binafsi,[376] ambao unaonesha wazi uhusiano wa lazima na manufaa kwa wote.[377] Mtu “anatakiwa kuchukulia vitu vya nje anavyomiliki kihalali kama sio vyake tu bali pia kama vya wote katika maana kwamba havitamnufaisha yeye tu bali na wengine pia.”[378] Kikomo cha jumla cha vitu kinataka wajibu katika namna ambayo vitu vinatumiwa na wamiliki halali wa vitu hivyo. Watu binafsi wanaweza wasitumie rasilimali zao bila kujali athari ambazo zinaletwa na matumizi hayo, badala yake lazima watumie kwa namna ambayo itafaidisha sio wao wenyewe tu na familia zao, lakini pia manufaa kwa wote. Hapa unakuja wajibu wa wamiliki kuruhusu mali wanayomiliki isikae bure, bali waiwekeze katika shughuli ya uzalishaji, hata kwa kuwadhamini na kuwapa wengine ambao wanahitaji na wana uwezo wa kuitumia katika uzalishaji.

179. Kipindi cha sasa cha historia kimeiletea jamii bidhaa mpya ambazo hazikujulikana kabisa mpaka nyakati za hivi karibuni. Hii inaleta hitaji jipya la kusoma kanuni ya kikomo kidunia cha mali za dunia na kuleta ulazima kupanua kanuni hii ili ihusishe maendeleo ya hivi karibuni yaliyoletwa na maendeleo ya kiuchumi na kiteknolojia. Umiliki wa bidhaa mpya – matokeo ya ujuzi, teknolojia na ufahamu – yanakuwa zaidi ndio vigezo vya maamuzi, kwa sababu “mali za mataifa yaliyoendelea, msingi wake zaidi ni katika aina hii ya umiliki kuliko rasilimali asilia”[379]

Ujuzi mpya wa kiteknolojia na kisayansi lazima uwe ni kwa ajili ya huduma kwa mahitaji muhimu ya mwanadamu, kuongezeka kwa taratibu urithi wa jumla wa mwanadamu. Kwa hiyo, kuweka kanuni ya kikomo cha mali kidunia katika utimilifu wake, kunahitaji utekelezaji katika ngazi ya kimataifa, na mipango ya programu kwa upande wa nchi. Kuna ulazima wa kuondoa vikwazo na ukiritimba ambavyo vinasababisha nchi nyingi kuwa nje ya maendeleo, na kuwajengea watu wote na nchi zote mazingira yatakayowawezesha kushiriki katika maendeleo.”[380]

180. Iwapo aina ya mali haikujulikana huko nyuma, inachukua umuhimu katika mchakato wa maendeleo ya kiuchumi na ya jamii, hata hivyo namna za mali za kimapokeo ni lazima zisisahaulike. Umiliki mali binafsi sio aina ya pekee ya umiliki halali. Mali zilizomilikiwa kijumuiya hapo zamani pia zina umuhimu wake, ingawa inaweza kuwepo katika nchi zilizoendelea kiuchumi, kwa namna ya pekee ni tabia ya muundo wa wenyeji wengi asilia wa mahali fulani. Hii ni aina ya mali yenye matokeo katika maisha ya kiuchumi, kiutamaduni na kisiasa ya watu ambao wana mambo ya msingi ya kuweza kuishi na kustawi. Kulinda na kukubali mali za jumuiya kamwe kusiweke pembeni, ukweli kwamba aina hii ya mali pia inalenga katika kuendelezwa. Iwapo hatua zinachukuliwa kwa ajili ya kutunza aina iliyopo, kuna hatari ya kufunga katika yaliyopita na kwa njia hiyo kuifanya ikubaliane na ya zamani.[381]

Mgawanyo sawa wa ardhi unabaki ni kitu cha msingi, na hasa kwa nchi zinazoendelea na nchi ambazo hivi karibuni zimebadilika kutoka mfumo wa ujima na ukoloni.[382] Katika maeneo ya vijijini, uwezekano wa kumiliki ardhi kwa njia ya fursa iliyoletwa na kazi na urahisi wa masoko ya mikopo ni hali ya lazima kwa upatikanaji wa bidhaa zingine za ziada na huduma. Pamoja na kuwemo kwa njia za kulinda mazingira, hii labda inawakilisha usalama wa jamii unaoweza kuwekwa mahali pake katika nchi zile zenye muundo dhaifu wa utawala.

181. Kwa watu, iwe mtu mmojammoja au jumuiya zinazomiliki aina mbalimbali za mali hupata maendeleo yanayokuja mfululizo: iwe hali ya maisha, usalama wa maisha ya baadaye, kuwa na mengi ya kuchukua katika kuchagua. Kwa maneno mengine, mali zinaweza pia zikaleta mfululizo wa ahadi za kidanganyifu ambazo ni kiini cha kishawishi. Wale watu na jumuiya zinazoweza kutoa jibu la mwisho kuhusu kikomo cha mali mwisho wake ni kushuhudia aina mbaya ya utumwa. Hakuna jibu la jumla la mkato la kumiliki mali ambalo linaweza kufikiriwa vinginevyo kuhusu msukumo unaoweza kuwa wa mtu binafsi na taasisi. Wamiliki ambao wanaendelea kuwa watumwa wa mali (taz. Mt 6: 24; 19: 21 – 26; Lk 16: 13) wanamilikiwa na kutumikishwa na mali.[383] Ni kwa kutambua tu kuwa mali hizo zinamtegemea Mungu Muumba na kuongoza matumizi kwa ajili ya manufaa kwa wote, na hapo inawezekana kutumia mali kama chombo cha kukua kwa watu binafsi na jumuiya kwa jumla.

c. Kikomo cha Jumla kuhusu Mali na Upendeleo kwa Maskini

182. Kanuni ya jumla ya kikomo cha mali inahitaji watu maskini, waliowekwa pembezoni, na kwa namna yoyote ile wale wanaoishi maisha ambayo ukuaji wake unaingiliwa, lazima watazamwe kwa namna ya pekee, kwa mtazamo huu, upendeleo kwa maskini lazima ukaziwe kwa nguvu zote.[384] “ Huu upendeleo au ni namna ya pekee kabisa kuishi matendo ya huruma, ambamo mapokeo yote ya Kanisa yanashuhudia. Inagusa maisha ya kila Mkristo ikiwa anatafuta kuiga maisha ya Kristo, lakini inahusu vilevile wajibu wetu kwa jamii na hivyo kuishi, na uamuzi usiopingana, uliotengenezwa kuhusu kumiliki na kutumia mali. Zaidi ya hayo, leo dunia inachukulia suala la jamii na kupewa uzito, upendo wa kupendelea maskini na uamuzi unachochea ndani yetu, haiwezekani, mpaka lazima ikumbatie wengi walio na njaa, wahitaji, wasio na malazi, wasio na afya, zaidi ya hayo, wale wote wasio na matumaini ya maisha bora ya baadaye.”[385]

183. Maumivu ya mtu ni kielelezo wazi cha hali tepetepe ya maumbile ya binadamu na hitaji lake la wokovu.[386] Kristo Mwokozi alionesha huruma katika suala hili, mwenyewe na “walio wadogo” miongoni mwa watu (taz. Mt 25: 40, 45). “Ni kwa yale ambayo watu wamewatendea maskini, ndiyo yatakayotambulisha atakaowateua. Bali aliposema ‘Maskini wamepokea habari njema iliyohubiriwa kwao.’ (Mt 11: 5), ni ishara ya uwepo wa Kristo.[387]

Yesu anasema, “Maskini mnao siku zote, lakini hamtakuwa nami siku zote” (Mt 26: 1; taz. Mk 14: 7; Yn 12: 8). Yesu anasema hayo ili kuwafanya watu wamjue kwa njia ya huduma kwa maskini. Uhalisia wa Kikristo, kwa upande mmoja kutambua jitihada nzuri zinazofanywa kuushinda umaskini, anaasa kwa upande mwingine kuhusiana na nafasi ya kiitikadi na imani ya kimasiha ambayo inaendeleza upotoshaji kwamba inawezekana kuondoa tatizo la umaskini kabisa kabisa hapa duniani. Hii itatokea tu wakati wa kurudi Kristo, atakapokuwa nasi tena daima. Kwa wakati huu, maskini wanabaki kukabidhiwa na kuaminishwa kwetu na huu ndio wajibu ambao ndio tutakaohukumiwa mwisho wa nyakati (taz. Mt 25: 31 – 46): Bwana wetu anatuonya kwamba tutatengwa naye ikiwa tutashindwa kukamilisha mahitaji muhimu ya maskini na walio wadogo ambao ndio nduguze.”[388]

184. Upendo wa Kanisa kwa maskini ni mvuto kutoka Injili ya Heri Mlimani, kwa umaskini wa Yesu na kwa kuwajali maskini. Upendo huo unahusu umaskini wa mali kivitu na pia aina nyingi zisizo na idadi za umaskini wa kiutamaduni na kiroho.[389]Kanisa “tangu mwanzo wake, na licha ya kushindwa kwa wanakanisa wake wengi, halijaacha kufanya kazi ya kuwatafutia watu maisha yenye nafuu, kulinda ukombozi kwa njia ya kazi nyingi za matendo na huruma ambayo yanabaki kuwa wajibu usioepukika kila wakati na kila mahali.”[390] Kwa kusukumwa na Injili “mmepata bure, toeni bure” (Mt 10: 8), Kanisa linafundisha kwamba mtu anatakiwa kusaidia binadamu mwenzake katika mahitaji yake mbalimbali na linazipa jumuiya zake kazi zisizo na idadi za matendo ya huruma ya kimwili na roho ya huruma. “Kati ya haya yote, kusaidia maskini ni moja kati ya ushuhuda mkubwa katika matendo ya kindugu: Pia kazi ya haki inampendeza Mungu,”[391] hata kama kutenda matendo ya huruma haifungwi katika kutoa sadaka kwa maskini, lakini pia ni pamoja na kushughulikia upande wa kijamii na kisiasa wa matatizo ya umaskini. Katika Mafundisho yake ya Kanisa kuhusu jamii mara zote linarudia uhusiano kati ya matendo ya huruma na haki. “Tunaposhughulikia wahitaji, tunawapa kilicho chao, na siyo cha kwetu. Zaidi ya kufanya kazi za huruma, tunalipa deni la haki.”[392] Mababa wa Mtaguso kwa nguvu wameonya, kwamba jukumu litekelezwe kwa usahihi, ikikumbukwa kwamba “chochote ambacho tayari ni stahili ya haki kisigeuzwe na kuitwa zawadi ya tendo la huruma.”[393] Kuwapenda maskini kwa uhakika “hakuendani na upendo usiokubalika wa tajiri au matumizi yao yaliyo katika ubinafsi.”[394] (taz. Yak 5: 1 – 6).

 

IV. KANUNI YA AUNI

a. Chanzo na Umaana

185. Kanuni ya auni ni moja ya kanuni zilizo za kudumu na tabia inayoongoza mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii, na imekuwemo toka mwanzo wa nyaraka zilizoandikwa kuhusu jamii.[395] Haiwezekani kukuza heshima ya mtu bila kujali hali ya familia, vikundi, mashirika, hali halisi ya mahali; kwa kifupi maeneo ya uchumi, jamii, utamaduni, maelekeo ya michezo, burudani, kazi za kitaaluma na kisiasa ambavyo vinaonyesha maisha ya watu moja kwa moja na kutengeneza mazingira yanayofaa kwa ajili yao ili kufanikisha kukua kwa jamii.[396] Hili ni eneo la jamii ya kiraia, inayoeleweka kama jumla ya mahusiano kati mtu binafsi na makundi ya kijamii, ambayo ndio mahusiano ya kwanza kujitokeza na ambayo yanakuwepo, shukrani katika “mang’amuzi binafsi ya raia.”[397] Mtandao huu wa mahusiano unaimarisha mfungamano wa kijamii na unajenga msingi wa jumuiya ya kweli, na kuleta uwezekano wa kutambua aina za juu za shughuli za jamii.[398]

186. Ulazima wa kutetea na kuhamasisha maelezo ya mwanzo ya maisha ya jamii umesisitizwa na Kanisa katika Barua ya Quadragesimo Anno, ambamo kanuni ya auni imeelezewa kuwa kanuni muhimu sana ya falsafa ya jamii. “Kama ilivyo ni dosari kubwa kuwanyang’anya watu kile wanachoweza kukamilisha wenyewe kwa jitihada zao katika jumuiya yao, vilevile pia ni kukosa haki, na wakati huohuo ni uovu mkubwa kuagiza ngazi ya juu mambo madogo ambayo yanaweza kufanywa katika ngazi ya chini. Kwani kila aina ya shughuli ya kijamii kwa asili yake inalenga kusaidia jamii na siyo kuharibu na kuwameza.”[399]

Kwa msingi wa kanuni hii, jamii zote za juu ni lazima zichukue mtazamo wa kusaidia (“subsidium”) – kwa hiyo, kusaidia, kukuza kuendeleza - kwa kuangalia watu wa chini katika taratibu zao kijamii. Kwa njia hii, jamii moja kwa moja zinaweza kutenda kazi zilizo ndani ya uwezo wao bila kuhitaji kuzikabidhi katika jamii zingine za ngazi ya juu, kufanya hivyo zitaishia kumezwa, mwishowe zitaonekana heshima yake inavunjwa na nafasi yake muhimu haitambuliki.

Auni kwa mtazamo chanya ina maana kusaidia mamlaka ngazi za chini kiuchumi kimuundo na kisheria. Kwa upande mwingine katika mtazamo hasi auni ina maana kuzuia mamlaka ngazi za juu kubana jitihada zinazoweza kufanywa na watu na mamlaka zao katika ngazi za chini. Jitihada, uhuru na uwajibikaji ngazi za chini lazima zisizuiwe.

b. Viashirio Halisi

187. Kanuni ya auni hulinda watu kutokana na matumizi mabaya yanayofanywa na ngazi ya juu ya mamlaka ya kijamii na inazitaka mamlaka hayohayo kusaidia mtu mmojammoja na makundi ya kati kutekeleza wajibu zao. Kanuni hii ni ya kiutendaji kwa sababu kila mtu, familia na makundi ya kati yana kitu asilia cha kuchangia katika jumuiya. Uzoefu unaonyesha kukataa au kuuwekea mipaka kwa kisingizio cha ujenzi wa demokrasia au usawa wa watu wote katika jamii, kunazuia na mara nyingine kuharibu roho ya uhuru na jitihada.

Kanuni ya auni inapinga kuweka utawala na madaraka yote ngazi ya juu, urasimu, kusaidia uwepo usio halali na unaovuka mipaka ya dola katika uendeshaji wa mambo ya umma. “Kwa kuingilia kati moja kwa moja na kuiondolea jamii wajibu wake, msaada wa dola kwa jamii husababisha kupoteza nguvu za binadamu na kuongeza nguvu ya vyombo vya umma ambazo zinatawaliwa zaidi na kufikiri kiurasimu kuliko kujali utumishi kwa wahitaji wao, na ambayo inaendana na ongezeko kubwa la matumizi.”[400] Kukosekana au upungufu katika kutambua jitihada za binafsi katika masuala ya uchumi na kushindwa kutambua kazi ya umma, inachangia kudhoofisha kanuni ya auni kama vile ukiritimba ulivyo pia.

Ili kanuni ya auni iweze kuwekwa katika vitendo, kuna mahitaji yanayoendana ya: kuheshimu na kuinua utu wa binadamu na familia; kukubali ushiriki wa mashirika na vikundi vya kati katika kuchagua mambo yao ya msingi na kwa yale ambayo hayawezi kufanyika kwa njia ya uwakilishi au kufanywa na wengine; kutia moyo jitihada za binafsi ili kila tabaka la jamii libaki kuhudumia kwa ajili ya manufaa kwa wote. Kila moja kwa tabia yake, uwepo wa wingi katika jamii na uwakilishi wa maeneo yake muhimu; kulinda haki za binadamu na haki za walio wachache; kuondoa urasimu na kugawa madaraka, kuweka uwiano kati ya mambo ya umma na binafsi, na matokeo yake kutambua kazi za jamii katika eneo la binafsi, maeneo yanaendana na njia zinazowawezesha raia kuwajibika kikamilifu wakiwa kama “sehemu ya” hali ya kisiasa na hali ya kijamii katika nchi.

188. Mazingira mbalimbali yanaweza kutengeneza ushauri kwamba Dola inaingia katika kutoa baadhi ya kazi.[401] Mmoja anaweza kufikiri kwa mfano, mazingira ambayo ni ya lazima kwa utawala wenyewe kutoa mwamko wa kiuchumi kwa sababu haiwezekani kwa jamii ya kiraia kusaidia jitihada hizo yenyewe. Mmoja anaweza kuwa na mtazamo wa hali halisi ya jamii isiyo na uwiano wa kijamii na kukosekana kwa haki ambako mamlaka ya umma yanaweza kutengeneza hali mbaya ya kukosa usawa, haki na amani. Kwa mwanga wa kanuni ya auni hata hivyo, hali hiyo ya kufanya mbadala wa kitaasisi ni lazima kusiendelee zaidi, ya kiwango cha lazima kwani kuhalalisha kuingilia kwa mtindo huu kunapatikana katika mazingira ya pekee. Manufaa kwa wote yakieleweka kwa usahihi, kamwe hayatakuwa kinyume na ulinzi na kuinua hadhi ya mtu na njia inayoelezea manufaa kwa wote ni lazima ibaki kuwa ndio kigezo cha kutoa maamuzi kuhusu matumizi ya kanuni ya auni.

 

V.   USHIRIKI

a. Maana na Thamani

189. Tabia inayoonesha auni ni ushiriki,[402] ambayo kielelezo chake ni katika mfululizo wa shughuli mbalimbali kwa njia ambazo raia, kama mtu binafsi au katika makundi na wengine, iwe ni moja kwa moja au kwa njia ya uwakilishi, inachangia utamaduni, uchumi, siasa na maisha ya jumuiya zao za kiraia walimo.[403] Ushiriki ni jukumu la kutekelezwa kwa makusudi na wote, kwa wajibu na kwa mtazamo wa manufaa kwa wote.[404]

Hii haiwezi kuwekwa ndani au kufungwa katika maeneo fulani tu ya maisha ya kijamii, ikizingatiwa umuhimu wa kukua, zaidi yoyote kukua kwa binadamu - katika maeneo kama ya ulimwengu wa kazi na shughuli za uchumi, hasa katika mwenendo unaobadilikabadilika;[405] katika sekta za habari na utamaduni, na zaidi ya yote, katika uwanja wa jamii na maisha ya kisiasa hata katika kiwango cha juu kabisa. Ushirikiano wa watu wote na ujenzi wa jumuiya ya kimataifa katika muundo wa mshikamano kutategemea eneo hili la mwisho.[406] Kwa mtazamo huu, linakuwa jambo la lazima kuhimiza na kutia moyo wa ushiriki hasahasa kwa wale ambao hawapati fursa kabisa na katika matukio ya mzunguko wa viongozi wa kisiasa ili kuzuia marupurupu yaliyojificha. Zaidi ya hayo, nguvu ya msukumo wa kimaadili inahitajika ili utawala wa maisha ya jamii uwe ni matokeo ya wajibu wa kushirikishana wa kila mmoja kuhusiana na manufaa kwa wote.

b. Ushiriki na Demokrasia

190. Ushiriki katika maisha ya jumuiya siyo tu moja ya kivutio kikubwa cha raia anayeitwa kuuishi uhuru na wajibu, jukumu la kiraia na pamoja na wengine na kwa ajili ya wengine,[407] lakini pia ni moja ya nguzo za utaratibu wote wa demokrasia na moja kati ya uthibitisho mkubwa wa kudumu wa mfumo wa demokrasia. Serikali ya kidemokrasia inatafsiriwa kwanza kama utoaji wa nguvu na majukumu kwa upande wa watu, inafanya kazi kwa jina lao, kwa ajili yao na kwa niaba yao. Kwa hiyo, ni uthibitisho wazi kwamba kila demokrasia lazima iwe shirikishi.[408] Hii ina maana kwamba watu tofauti katika jumuiya ya kiraia katika kila ngazi lazima wahabarishwe, wasikilizwe na wahusishwe katika utekelezaji wa majukumu mbalimbali.

191. Ushiriki unaweza kufanikishwa katika mahusiano yote mbalimbali kati ya raia na taasisi: kwa lengo hili, umakini fulani lazima utolewe katika historia na mazingira ya jamii ambayo ushirikiano wa kweli unaweza kuwepo. Kushinda vipingamizi vya kiutamaduni, kisheria na kijamii ambavyo mara nyingi vinakuwa vizuizi katika ushirikiano shirikishi wa raia katika kikomo chao cha maisha ya jumuiya mbalimbali kunahitajika kufanya kazi katika maeneo ya habari na elimu.[409] Kuhusu suala hili, mitazamo yote inayochochea raia wasitoe ushiriki wa kutosha na sahihi kwa vitendo au inayosababisha kupanuka katika hali ya kutoridhika na jambo lolote linalounganika na maeneo ya jamii na maisha ya kisiasa ni chanzo cha kujali na kustahili kufikiriwa kwa makini. Kwa mfano, baadhi ya raia kujaribu “kufanya ujanjaujanja” pamoja na taasisi ili kujiwekea utaratibu wenye kuleta faida kwa ajili yao, kama kwamba taasisi hizi zilikuwa kwa ajili ya mahitaji binafsi; au tabia ya raia kutoshiriki katika hatua za uchaguzi, na mara nyingi kufikia hatua ya kukataa kupiga kura.[410]

Katika maeneo ya ushiriki, chanzo kingine kinapatikana katika nchi zinazotawaliwa kwa mabavu au mfumo wa kiimla, ambamo haki za msingi za kushiriki katika maisha ya jamii haipati nafasi toka mwanzo, kwa vile hufikiriwa ni tishio kwa dola yenyewe.[411] Nchi nyingine ambapo haki zinatangazwa kinadharia, wakati katika hali halisi haiwezi kutekelezwa, wakati pia nchi nyingine kuongezeka kwa urasimu kunakosesha uwezekano wa raia kushiriki kikamilifu katika maisha ya kijamii na ya kisiasa.[412]

 

VI.  KANUNI YA MSHIKAMANO

a. Maana na Thamani

192. Mshikamano unatoa mwanga kwa njia fulani iliyoungana kabisa na maumbile ya jamii ya binadamu, usawa wa wote katika kuheshimiwa na haki na njia ya watu binafsi na binadamu wote kuelekea katika hali ya kujitoa katika umoja. Haijapata kuwepo kabla utambuzi mpana wa kifungo cha uhuru kati ya watu binafsi na binadamu wote, kinachopatikana katika ngazi zote.[413] Kupanuka haraka kwa njia na namna za mawasiliano “kwa wakati muafaka”, kama yale yanayotokana na teknolojia ya habari, maendeleo makubwa katika teknolojia ya kompyuta iliyokwenda kasi, ongezeko kubwa katika biashara na kubadilishana habari, hayo yote ni ushuhuda kwa mara ya kwanza katika historia ya binadamu, kwamba sasa inawezekana walau kwa kiteknolojia kuanzisha mahusiano kati ya watu waliotenganishwa na umbali wa masafa marefu na wasiojuana wao kwa wao.

Uwepo wa kutegemeana na kupanuka nyakati zote, hata hivyo, kunaleta katika kila sehemu ya dunia kukosa usawa kati ya nchi zilizoendelea na zinazoendelea, kukosekana kwa usawa kunakochochewa na mifumo mbalimbali ya unyonyaji, ukandamizaji na rushwa ambayo ina msukumo usiofaa kwa maisha ya ndani ya kimataifa ya dola nyingi. Kwenda kwa kasi katika kutegemeana miongoni mwa watu na binadamu wote kunahitaji kwenda pamoja na jitihada kubwa za maadili ya jamii ili kukwepa hatari zinazosababishwa na uharibifu katika kukosa haki katika kiwango cha kimataifa. Hii ingeweza kuwa na athari zisiyofaa hata kwa nchi ambazo kwa sasa zipo katika hali nzuri.[414]

b. Mshikamano kama Kanuni ya Jamii na Fadhila ya Maadili

193. Mahusiano mapya ya kutegemeana kati ya watu binafsi na binadamu wote ambao kimsingi wanatengeneza mshikamano, lazima wageuke na kuwa katika mahusiano yenye mwelekeo wa maadili yenye mshikamano wa kijamii. Hili ni hitaji la kimaadili lililoshikana kabisa na uhusiano wa binadamu. Mshikamano kwa hiyo una vipengele viwili vinavyotegemeana ambavyo ni kanuni ya jamii[415] na ile fadhila ya maadili.[416]

Mshikamano lazima uonekane kuliko jambo lolote katika thamani kama fadhila ya maadili ambayo ndiyo kigezo cha utaratibu wa taasisi. Kwa msingi wa kanuni ya “miundo ya dhambi”[417] inayotawala mahusiano kati ya watu binafsi na binadamu wote inatakiwa kuondoka. Ni lazima itakaswe na kugeuzwa kuwa miundo ya mshikamano kwa njia ya kutengeneza au kurekebisha sheria, kanuni za soko, na mifumo ya kisheria.

Mshikamano pia ni fadhila ya maadili ya kuaminika, siyo “kuonja huruma isiyo waziwazi au mahangaiko yanayojitokeza kwa bahati mbaya kwa watu wengi walioko mbali na walioko karibu. Kinyume chake, ni uimara na kuweka nia ya kuvumilia na kujitoa mtu mwenyewe kwa ajili ya manufaa kwa wote. Hii ina maana ni kwa wote na kwa kila mtu kwa sababu sisi sote tunawajibika kwa watu wote.”[418] Mshikamano unapanda juu kufikia kiwango cha msingi wa fadhila ya jamii kwani unajidhihirisha wenyewe katika eneo la haki. Ni fadhila inayoelekeza kwa yenyewe katika manufaa ya wote na inapatikana katika “kujitoa kwa ajili ya manufaa ya jirani kwa kuwa tayari, katika maana ya Injili, kutoa nafasi yake mwenyewe kwa ajili ya mwingine badala ya kumnyonya na kumtumikisha, badala ya kumkandamiza kwa faida yako mwenyewe (taz. Mt 10: 40 – 42, 20: 25; Mk 10: 42 – 45; Lk 22: 25 – 27).”[419]

c. Mshikamano na Ukuaji wa Kawaida wa Binadamu

194. Ujumbe wa mafundisho ya Kanisa kuhusu mshikamano wa jamii unaonesha wazi kwamba uwepo wa mshikamano na manufaa kwa wote, kati ya mshikamano na kikomo cha jumla cha mali, kati ya mshikamano na usawa watu na binadamu wote, kati ya mshikamano na amani duniani.[420] Neno “Mshikamano”, limetumika kwa upana na Majisterio,[421] inayoeleza kwa mtindo wa kimuhtasari hitaji la kutambua muundo unaofunga muungano wa watu na jamii ya makundi yenyewe kwa yenyewe, fursa inayotolewa kwa uhuru wa binadamu kwa ajili ya kukua kwa pamoja ambapo wote wanahusishwa na kushirikishwa. Kujitoa katika lengo kunapewa tafsiri chanya inayochangia katika kuona kwamba hakuna kinachokosekana katika jitihada za pamoja na pia katika kutafuta makubaliano yanayowezekana pale ambapo fikra juu ya utengano na kusambaratika zinatawala vipengele vinavyowezesha makubaliano ambapo mgawanyiko na mmeguko vinatawala. Ina tafsiri katika kuweka nia ya kujitoa mwenyewe kwa manufaa ya jirani yake, zaidi kuliko kujali faida yoyote ya kibinafsi.[422]

195. Kanuni ya mshikamano inahitaji wanaume na wanawake wa siku ya leo kujijengea utambuzi mkubwa kwamba wana deni kwa jamii ambayo imekuwa sehemu yao. Wana deni kwa sababu hali hizo zinawezesha uwepo wa binadamu kiuhai, na kwa sababu ya kutogawanyika na uwakilishi usioepukika na sehemu ya utamaduni, sayansi na maarifa ya teknolojia, vitu na bidhaa ambazo hali ya binadamu imeyaleta. Deni kama hili ni lazima litambuliwe kwa njia mbalimbali za mwingiliano wa jamii, na hivi safari ya binadamu haitaingiliwa, bali itabaki wazi kwa wakati uliopo na vizazi vijavyo, wote wanaitwa kwa pamoja kushiriki zawadi ileile katika mshikamano.

d. Mshikamano katika Maisha na Ujumbe wa Yesu Kristo

196. Kilele kisichofikiwa cha mtazamo hapa kinaoneshwa na maisha ya Yesu wa Nazareti, Mtu Mpya, mwenye ubinadamu hata “kufa msalabani” (Flp 2:8). Katika yeye mara zote inawezekana kutambua alama hai isiyopimika na upendo wa Mungu usio na kipimo ambao upo pamoja na sisi, isiodhalilisha watu wake, anatembea nao, anawaokoa na kuwafanya kuwa wamoja.[423] Ndani yake, na shukrani kwake, maisha ya jamii pia, pamoja na migongano na mkanganyiko, inaweza kugunduliwa kama sehemu ya maisha na matumaini, katika hili ni alama ya neema endelevu inayotolewa kwa wote kwa sababu ni mwaliko daima kwa yale ya juu kabisa na kushiriki katika mifumo yote ya kushirikishana.

Yesu wa Nazareti anaunganisha kati ya mshikamano na huruma inayong’aa mbele ya wote, kuangazia maana yote kwa muunganiko huu.[424] Kwa njia ya mwanga wa Imani, mshikamano unaenda zaidi ya kuonekana kwake, unachukua kwa namna ya pekee kipengele cha Kikristo katika kushukuru, kusamehe na upatanisho. Jirani, kwa hiyo, siyo tu binadamu mwenye haki zake na usawa wa msingi sawasawa na mtu yeyote yule, bali anakuwa sura hai ya Mungu Baba, aliyekombolewa kwa damu ya Yesu Kristo na kuwekwa chini ya utendaji wa kudumu wa Roho Mtakatifu. Hivyo, jirani lazima apendwe, hata angekuwa adui, kwa pendo lilelile ambalo Bwana anapenda na kwa ajili ya mtu huyo lazima kuwa tayari kutoa sadaka, hata ya juu sana: hata kutoa uhai wake kwa ajili ya ndugu zake (taz. 1 Yoh 3: 16).”[425]

 

VII.TUNU ZA MSINGI ZA MAISHA YA JAMII

 

a. Uhusiano kati ya Kanuni na Tunu

197. Licha ya kanuni ambazo zinaongoza kazi ya kujenga jamii ya kufaa kwa binadamu, Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii pia yanaonyesha tunu za msingi. Uhusiano kati ya kanuni na tunu bila shaka ni wa kurudiana katika hilo, tunu za kimaadili ni kielelezo katika mambo yanayokubalika na vipengele vya maadili katika kuimarisha kanuni hizi, kutumia kama rejea muhimu kwa ajili ya muundo na mpangilio wa maisha ya jamii. Tunu hizi zinahitaji, kwa hiyo, kuziishi kanuni za msingi za maisha ya jamii pamoja na kuiishi fadhila ya mtu binafsi, kwa hiyo, fikra za kimaadili zinaendana na thamani za tunu hizi.[426]

Tunu zote za kijamii zinarithiwa kwa heshima ya binadamu, ambao maendeleo yao ya kuaminika wanayasukuma. Kimsingi, tunu hizi ni: ukweli, uhuru, haki, upendo.[427] Kuziishi tunu hizi ni jambo la uhakika na njia ya lazima katika mtu kujipatia ukamilifu na uwepo wa ubinadamu wa kijamii. Hayo yote yana rejea isiyopingika katika mamlaka ya jamii, yanayotakiwa kufanya “mageuzi thabiti ya kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni na katika miundo ya kiteknolojia na mabadiliko ya lazima ya taasisi.”[428] Kuheshimu uhuru katika mambo ya duniani kunachochea Kanisa kuwa na uwezo kwa namna ya pekee katika taratibu za kiufundi na mambo ya kidunia,[429] lakini halizuiliwi kuingilia kati kuonesha namna, katika maamuzi mbalimbali yanayofanywa na wanaume na wanawake, na tunu hizi aidha zinathibitishwa ama zinakataliwa.[430]

b. Ukweli

198. Wanaume na wanawake wana kazi maalumu kwenda daima mbele kuelekea kwenye ukweli, kuheshimu na kubeba ushuhuda wa kiwajibu.[431] Kuishi katika ukweli kuna umuhimu wa pekee katika mahusiano ya kijamii. Wakati kuna uwepo wa watu ndani ya jumuiya iliyozaliwa katika ukweli, ipo katika utaratibu na ni yenye kuzaa matunda, na inawiana na heshima ya watu.[432] Watu wengi na makundi katika jamii wanapofanya jitihada zaidi kutatua matatizo ya kijamii kadiri ya ukweli, ndivyo watakavyokuwa mbali zaidi na matumizi mabaya na kutenda kadiri ya malengo yanayohitaji maadili.

Maisha ya leo yanahitaji nguvu kubwa ya elimu[433] na uwiano katika kujitoa kwa watu wote ili hamu ya kutafuta ukweli isiwe katika maelezo ya jumla au katika wazo moja au jingine – yatatiliwa mkazo katika kila sekta na yataendelea kutafuta kila jitihada ya kutimiza katika mahitaji au kuyadharau.[434] Hili ni suala linalohusu mawasiliano ya jamii na uchumi wa aina fulani. Katika maeneo haya matumizi mabaya ya fedha yanakuwa moja ya masuala mazito, ambayo yanahitaji kuwa na uwazi mkubwa na uaminifu wa mtu binafsi na shughuli za jamii.

c. Uhuru

199. Uhuru ni alama kubwa ya mtu kwa kufanywa sura ya Mungu na pia inakuja kuwa yake, ni alama ya heshima ya kila mwanadamu.[435] Uhuru unatekelezwa katika mahusiano kati ya binadamu. Kila binadamu, aliyeumbwa na Mungu, ana haki za kiasili za kutambuliwa kama kiumbe huru mwenye wajibu. Wote wanapaswa kulinda wajibu wa kuheshimiana. Haki ya kuuishi uhuru, hususani katika masuala ya kimaadili na kidini ni mahitaji yasiyopingika ya heshima ya binadamu.”[436] Maana ya uhuru lazima isibaki kufikiriwa kwa mtazamo wa binafsi na hali ya mtu kuwa huru bila mipaka. “Pamoja na kujitosheleza na kukosekana kwa mahusiano, uhuru unakuwepo kukiwa na kushikana katika kutoa na kupokea, kunakoongozwa na ukweli na haki, muunganiko wa mtu na mwingine.”[437] Kuuelewa uhuru kwa kina na upana ni pale unapolindwa, hata katika kiwango cha jamii, na katika ukubwa wake wote.

200. Thamani ya uhuru, kama kielelezo cha mtu mmoja, inaheshimika wakati kila mwanajamii anaporuhusiwa kutekeleza wito wake binafsi; kutafuta ukweli na kukiri dini, utamaduni na mawazo ya kisiasa, kutoa mawazo yake, kuchagua hali ya maisha inayowezekana, kazi yake; kuendeleza jitihada za kiuchumi, kijamii na kisiasa. Hii ni lazima itekelezwe ndani ya muundo wa sheria wenye nguvu,”[438] katika mipaka iliyotolewa kwa manufaa ya wote na utaratibu wa kijamii, na kwa hali yoyote katika namna yenye tabia ya kiuwajibikaji.

Kwa upande mwingine, uhuru lazima uelezwe kama ni uwezo wa kukataa yasiyoendana na maadili, hata kama haitajitokeza waziwazi,[439] kama uwezo wa mtu kujiweka mbali na kitu chochote kinachoweza kuzuia ukuaji wa mtu, kifamilia na kijamii. Ukamilifu wa uhuru unahusu uwezo wa kujimiliki mwenyewe katika mtazamo unaofaa kweli, katika mazingira ya manufaa ya wote.[440]

d. Haki

201. Haki ni tunu inayoendana na utekelezaji wa fadhila kuu ya maadili.[441] Kadiri ya muundo wa kiwango kikubwa, “inahusu mara kwa mara na kwa uthabiti hiari ya kutoa yanayostahili kwa Mungu na jirani.”[442] Kwa mtazamo wa binafsi, haki inatafsiriwa katika tabia ambayo msingi wake ni kumtambua mtu mwingine kama binadamu, wakati kwa mtazamo wa nje, ina vigezo vya kimaadili vinavyohusu watu binafsi na eneo la jamii.[443]

Mafundisho ya jamii ya Majisterio yanahitaji kiwango cha juu kabisa cha mifumo ya haki inayoheshimika: haki ya kubadilishana mawazo, haki ya kugawana mali na haki ya kisheria.[444] Umuhimu mkubwa umetolewa katika haki ya jamii,[445] ambayo inawakilisha maendeleo ya kweli ya jamii kwa jumla, haki inayorekebisha mahusiano ya jamii kadiri ya kigezo cha kuangalia sheria. Haki ya jamii, hitaji linayohusiana na masuala ya jamii ambayo leo limepanuka katika mtazamo, hitaji la jamii, siasa na vipengele vya kiuchumi, na zaidi ya yote, matatizo ya maeneo ya muundo na ufumbuzi wa kila tatizo.[446]

202. Haki kwa namna ya pekee ni ya muhimu katika mazingira ya leo, ambapo thamani ya mtu binafsi, heshima yake na haki zake, licha ya kutangaza nia njema, yanatishiwa kwa upana na mwelekeo wa kutengeneza kigezo cha utumiaji na umilikaji. Haki pia kwa misingi hii, ya vigezo inafikiriwa katika ufinyu wake, wakati inapata maana kamili na ya kweli zaidi katika anthropolojia ya Kikristo. Haki, kimsingi siyo tu makubaliano ya watu, kwa sababu suala la “haki” siyo tu linatambuliwa kutokana na sheria bali na upekee wa misingi ya binadamu.[447]

203. Ukweli kamili kuhusu binadamu unasababisha uwezekano wa kwenda zaidi ya hali halisi zinazopingana za mtazamo wa haki, ambao unafifisha mtazamo, na kuweka wazi pia mambo ya haki katika upeo mpya wa mshikamano na upendo. “Kwa haki yenyewe peke yake haitoshi. Kwani inaweza ikajisaliti yenyewe, isipokuwa mpaka iwe wazi katika nguvu ya ndani ambayo ni upendo.”[448] Kwa kweli, Mafundisho ya Kanisa juu ya jamii yanaweka pamoja tunu ya haki na ile ya mshikamano ambayo ni fursa katika njia ya amani. Iwapo amani ni, tunda la haki, “leo mmoja anaweza kusema, kwa uzito ule na kwa nguvu ya uvuvio wa Biblia kabisa na kwa nguvu ileile ya elimu (taz. Isa 32: 17, Yak 3: 18). (taz. Isa 32: 17; Yak 3: 18): ‘Opus Solidaritatis pax’ amani ni kama tunda la mshikamano.”[449] Lengo la amani, “kwa kweli” litafanikiwa kwa njia ya kuitekeleza haki ya kijamii na ya kimataifa, lakini pia kwa njia ya kuishi fadhila ambayo zinajenga umoja, na ambayo inatufundisha kuishi umoja, ili kujenga umoja, kwa njia ya kutoa na kupokea, jamii mpya na dunia bora.”[450]

 

VIII. NJIA YA UPENDO

204. Kati ya fadhila katika upana wake, na hususani kati ya fadhila, tunu ya jamii na upendo, kuna kifungo ambacho lazima daima kiendelee kutambuliwa kikamilifu. Upendo, mara nyingi huangaliwa kama uhusiano wa ukaribu kimwili au kuonekana katika upende wa matendo ya mtu kwa mwingine, lakini upendo lazima uangaliwe upya kiusahihi kama kigezo cha juu ya yote katika maadili kamili ya jamii. Kati ya njia zote, zikiwa hata zinazoangalia na kuchukuliwa kwa utaratibu unaoendana na namna mpya za maswali yanayoendelea ya jamii, kwa “namna nzuri zaidi” (taz. I Kor 12: 31) ni ile inaonekana kwa mapendo.

205. Ni kwa njia ya chemchemi ya ndani ya upendo ambapo tunu za ukweli, uhuru na haki zinajengwa na kukua. Maisha ya binadamu yamepangwa na kuzaa matunda yenye manufaa na kuendana na heshima ya binadamu inayopatikana katika ukweli, iwapo maisha yatakuwa ya haki, yaani, haki zionekane kuheshimika na kwa uaminifu kutekeleza shughuli zinazoendana, zikisaidiwa na roho ya kutokuwa na ubinafsi, ambayo inafanya mahitaji ya wengine yaonekane kama ya mtu mwenyewe na kuongeza umoja wa mambo ya thamani ya kiroho na kujali mahitaji ya muhimu. Yanapokamilishwa katika uhuru wenye kunufaisha wanaume na wanawake, wanaamshwa na akili ya asili inayokubaliana na wajibu katika matendo yao.[451] Tunu hizi ni nguzo zinazotoa nguvu na moja kwa moja kuimarisha nia au maisha na vitendo. Hizi ni tunu zinapima ubora wa matendo ya kijamii na kitaasisi.

206. Upendo unatanguliwa na uko juu ya haki, ambao ni “lazima upate ukamilifu wake katika matendo ya huruma.”[452] Iwapo haki kwa yenyewe inafaa katika kuamua kati ya watu wanaohusika katika kutoa na kupokea ugawaji wa mali katika hali ya usawa, upendo na ni upendo tu (ukiwa pamoja na aina ya upendo ambao ni huruma) ina uwezo wa kumfanya binadamu awe mwenyewe.”[453] Mahusiano ya binadamu yanatawaliwa tu kwa kipimo cha haki”: Mang’amuzi yaliyopita na kwa njia za nyakati zetu peke yake zinaonesha kuwa haki peke yake hazitoshi, zinaweza kurudisha nyuma na kuiharibu. Ni lazima ipate uzoefu wa kihistoria, kati ya vitu vilivyopelekea usemi huu: “Summum ius, summa iniuria.[454] Kila eneo la mahusiano katika haki, lazima isahihishwe kwa kufikiria kiwango cha upendo, ambao Mt. Paulo anatangaza, ‘una subira na ukarimu au, kwa maneno mengine una tabia ya huruma ya mapendo ambayo ndiyo hali ya Injili na Ukristo.”[455]

207. Hakuna sheria ya mfumo wa taratibu au upatanisho utakaoweza kufaulu kweli kwa kushawishi watu na nchi, kuishi maisha ya umoja, undugu na amani; hakuna namna ya kufikiri itakayozidi jitihada za kutafuta upendo. Ni upendo katika thamani yake kama “aina ya fadhila,”[456] unaoweza kuongeza na kuweka sura ya maingiliano ya jamii kuelekea kwenye amani katika mazingira ya dunia inayoendelea kuwa ya mchanganyiko. Ili yote haya yaweze kuwepo, hata hivyo umakini unaweza kuchukuliwa kuonesha upendo na siyo tu jukumu la kuamsha matendo ya binafsi, bali nguvu yenye uwezo wa kuchochea njia mpya za kukabili matatizo ya dunia ya leo, katika kufanya upya miundo ya msingi, muundo wa jamii, mfumo wa sheria kutoka ndani ya mfumo wenyewe. Kwa mtazamo huu, upendo unachukua tabia ya mtindo wa huruma kijamii na ya kisiasa: “Huruma ya jamii inafanya tupende manufaa kwa wote,”[457] inatuwezesha kikamilifu kutafuta manufaa kwa ajili ya watu wote, na siyo kama mtu binafsi bali pia vipengele vya jamii vinavyowaunganisha.

208. Jamii na huruma ya kisiasa haimalizii katika na mahusiano kati ya watu, lakini inaingia katika mtandao unaojengwa na uhusiano huu, ambao ni jamii ya kijamii na ya kisiasa, inayoingilia kati katika manufaa kwa wote. Katika mambo mengi jirani anayepaswa kuonyeshwa upendo anaishi “ndani ya jamii”, hivyo kumpenda kiuhalisi, kumsaidia katika mahitaji yake au katika umaskini wake inaweza kumaanisha kitu zaidi ya mahusiano tu kati ya watu. Kumpenda kijamii inamaanisha kuangalia mazingira, kutumia njia za mifumo ya kijamii ili kuboresha maisha yake (jirani) na kuondoa vyanzo vya kijamii vinavyoleta umaskini. Bila shaka tendo la upendo, kazi ya huruma na kwa njia hizo mtu hujibu hapa na sasa mahitaji ya jirani, lakini pia ni lazima tendo la upendo liwe katika kujipanga jamii na kuweka muundo, unaomwezesha jirani kutobaki kuishi katika umaskini. Hasa kama hali hii inakuwa ya watu wengi na nchi ama sehemu ya kundi la watu, hapo linakuwa suala la kijamii kidunia.

 

SEHEMU YA PILI

“. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii, ni chombo muhimu cha uinjilishaji. Kwa hiyo basi, Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanamtangaza Mungu na Fumbo lake la Ukombozi katika Kristo kwa kila mwanadamu. Na ni kwa sababu hiyohiyo mafundisho hayo yanamsaidia mtu kujitambua.

Kwa maongozi ya mwanga huu, na katika mwanga huu tu, mafundisho hayo yanahusiana na mambo mengine yote pia: Haki za Binadamu za kila mtu mmojammoja, na hasa zile za tabaka la wafanyakazi, familia na haki ya kupata elimu, wajibu wa Serikali, utaratibu wa jamii ngazi ya kitaifa na kimataifa, maisha ya kiuchumi, utamaduni, vita na amani, kuheshimu uhai kuanzia hatua ya kutungwa mimba mpaka kifo.”

(Centesimus Annus = Tumaini Jipya, 54)

 


SURA YA TANO

FAMILIA, KIINI MUHIMU CHA JAMII

 

1. FAMILIA, JAMII YA KWANZA KIASILI

209. Umuhimu na Ukitovu wa familia kuhusiana na mtu na jamii umeelezwa kwa mkazo na kwa kurudiarudia katika Maandiko Matakatifu. “Si vema mtu huyu awe peke yake” (Mwa 2: 18). Kutoka katika maandiko yanayoelezea uumbwaji wa mwanadamu (taz. Mwa 1: 26 – 28; 2: 7 – 24 inaonekana ni vipi katika mpango wa Mungu, wawili katika ndoa wanavyounda “aina ya jumuiya ya kwanza katika watu.”[458] Eva ameumbwa kama Adamu ambaye kwa yeye na kwa namna yake anamkamilisha Adamu (taz. Mwa 2: 18) ili kujenga pamoja naye “mwili mmoja.” (Mwa 2: 24; taz. Mt 19: 5 – 6).[459] Na wakati huohuo, wote wanajishughulisha na kazi ya kuendeleza uumbaji, kazi ambayo inawafanya wawe wafanyakazi pamoja na Muumba: “Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi” (Mwa 1: 28). Familia imewekwa katika mpango wa Muumba kama “mahala pa msingi pa ‘kuujenga utu wa mtu’ kwa ajili ya jamii” na kwa ajili ya mtu “chanzo au chimbuko la uhai na mapendo”.[460]

210. Ni katika familia ndipo mtu hujifunza upendo na uaminifu wa Mungu na sababu ya kuupokea Upendo na Uaminifu huo (taz. Kut. 12: 25 – 27; 13: 8, 14 – 15; Kum 6: 20 – 25; 13: 7 – 11; 1 Sam 3: 13). Ni katika familia ambamo watoto hupata mafundisho ya kwanza na ya muhimu juu ya kuishi hekima, ambayo kwayo maadili yote ya maisha yameunganika (taz. Mit 1: 8 – 9, 4:1 – 4, 6: 20 – 21; Sir 3: 1 – 16; 7: 21 – 28). Kwa sababu ya haya yote, Mungu mwenyewe ndiye mdhamini wa upendo na uaminifu katika maisha ya ndoa (taz. Mal. 2: 14 – 15).

Yesu alizaliwa na kuishi katika familia, akakubali hali na tabia ya familia yake[461] na akaipatia ndoa heshima ya juu kabisa, akaifanya iwe sakramenti ya agano jipya (taz. Mt. 19: 3 – 9). Ni katika mtazamo huu mpya, wawili (mke na mume) katika ndoa wanapata utimilifu wa heshima na msingi imara wa utu na familia.

211. Kwa kuangaziwa na ujumbe wa Biblia, Kanisa linaichukulia familia kuwa ni jumuiya ya kwanza katika jamii ya asili, ikiwa na haki ambazo ni sahihi kwake na kuiweka familia katika kitovu cha maisha ya jamii. Kuishusha familia na kuipa “wajibu wa usaidizi au wa ngazi ya pili, yaani kuiondoa katika nafasi yake ya haki katika jamii, ingekuwa ni kuleta hatari kubwa mno katika ukuaji halali na wa kweli wa jamii nzima.”[462] Kwa kweli, familia inatokana na ushirika na uhusiano wa karibu wa uhai na upendo ulio na misingi yake katika ndoa kati ya mwanamume mmoja na mwanamke mmoja.”[463] Familia inabeba sura ya asili, kwa hiyo familia ni mahala pakuu pa mahusiano na watu, ikiwa ndio jamii ya kwanza na kiini chenye umuhimu wa pekee kabisa katika jamii.[464] Familia ni taasisi yenye utakatifu ambayo inasimama katika msingi wa maisha ya utu wa mtu, ikiwa ndio mfano wa kwanza wa kila utaratibu katika jamii.

a. Umuhimu wa Familia kwa Mtu.

212. Familia ina umuhimu wa pekee sana kuhusiana na mtu. Ni katika chimbuko hili la uhai na mapendo ambamo watu wanazaliwa na mtoto kukua; wakati mimba inapotungwa, jamii inapokea zawadi ya mtu mpya anayeitwa “kutoka ndani kabisa ya nafsi yake kuwa katika ushirika na watu wengine na kujitoa mwenyewe kwa ajili ya wengine.”[465] Kwa hiyo, ni katika familia ambamo kujitoa mtu mwenyewe kwa ajili ya wengine kwa njia ya muunganiko wa mwanamume na mwanamke katika ndoa kunakojenga mazingira ya maisha ambamo watoto “wanakuza vipaji na uwezo wao, wanaelewa juu ya hadhi yao na wanajiandaa kukabili uelekeo wa dira pekee ya kila mmoja.”[466]

Katika hali ya kiasili ya kuonesha kutambuliwa ambayo inaunganisha wanafamilia katika familia, watu wanatambuliwa na kujifunza uwajibikaji wao kamili wa kiutu. “Muundo wa kwanza na muhimu sana kwa ajili ya hatua za ukuaji wa mwanadamu ni familia, ambamo mtu anapata mawazo ya kumjenga kimalezi kuhusu ukweli na uzuri, na anajifunza nini maana ya kupenda na kupendwa, na hivyo kujifunza nini hasa maana ya kuwa mtu.”[467] Kwa kweli majukumu ya wanafamilia hayawekewi mipaka kwa njia ya masharti ya mkataba, lakini yanatokana na chimbuko la asili la familia, msingi wake ukiwa ni agano la ndoa isiyovunjika na yenye muundo wake katika mahusiano ambayo yanajijenga ndani ya familia kufuatana na kizazi au kwa njia ya familia kupokea watoto wa kulea.

b. Umuhimu wa Familia kwa Jamii

213. Jumuiya ya asili, familia, ambamo mahusiano ya jamii ya kiutu yanastawi, inatoa mchango wa aina yake, usio na mbadala katika uzuri wa jamii. Kwa kweli, familia inajengwa na ushirika wa watu. ‘Ushirika’ unahusiana na mahusiano na watu baina ya ‘mimi’ na ‘wewe’. Kwa upande mwingine ‘Ushirika’ unakuza muundo huo na kuujenga kuelekea ‘jamii’ ambayo ni ‘sisi’. Kwa njia hii familia kama jumuiya ya watu, inakuwa ‘jamii’ ya kwanza ya watu.”[468]

Jamii iliyojengwa kwa misingi ya familia inakuwa na uwezo mkubwa wa kukwepa mkondo unaoielekeza katika madhara yatokanayo na ubinafsi au mfumo wa ujamaa ambapo nyenzo kuu za uzalishaji mali humilikiwa na umma. Hii ni kwa sababu ndani ya familia wakati wote mtu ndiye kitovu, anachukuliwa kuwa ndiye lengo kuu. Hivyo, kamwe mtu hawezi kutumika kama chombo cha kuifikia nia. Ni jambo lililo bayana kwamba mazuri ya watu na utendaji mzuri wa jamii vina uhusiano wa karibu sana “na muunganiko wa kimapendo katika ndoa na maisha ya familia.”[469] Jumuiya ambayo haina familia imara na zenye nguvu katika majukumu yake, watu wake wanakuwa dhaifu. Ni katika familia tunu za kimaadili zinafundishwa kuanzia mwanzo wa uhai. Mambo ya kiroho kutoka katika jumuiya za kidini na utamaduni wa taifa vinarithishwa kwa jamii katika familia. Ni katika familia mtu hujifunza uwajibikaji katika jamii na mshikamano.[470]

214. Vipaumbele vya familia ni lazima vitambuliwe na kukubalika kwa uwazi zaidi ya vipaumbele vya jamii na vya nchi. Kwa kweli, walau kwa kushiriki uumbaji, jukumu hili linakuwa ni sharti la uwepo wa familia. Umuhimu na thamani ya majukumu ambayo serikali na jamii wanaitwa kuyatekeleza unatokana na majukumu na mahitaji ya kila familia ambayo kwayo kila mwanafamilia ananufaika nayo.[471] Familia inayo haki za msingi na inapata uhalalisho wa haki hizo kutokana na maumbile ya mwanadamu na sio kutokana na kutambuliwa na Serikali. Familia, kwa hiyo, uwepo wake sio kwa ajili ya jamii au Serikali, bali jamii na Serikali ipo kwa ajili ya familia.

Kila mtindo wa maisha ya jamii ambao unanuia kuhudumia uzuri wa mtu, ni lazima ukazie kwamba familia ndio kiini cha jamii na suala la uwajibikaji wa familia katika jamii. Katika mahusiano na familia, jamii na Serikali wanalazimika kuwa makini kuzingatia kanuni. Kutokana na uzuri kimaadili wa kanuni hii, mamlaka ya umma pengine hayawezi kunyang’anya familia majukumu yake ambayo familia yenyewe inaweza kuyatekeleza vema au kuyakamilisha kwa kushirikiana na familia zingine; kwa upande mwingine, mamlaka hizo zina wajibu wa kudumisha familia, na kuhakikisha kwamba familia inapata kila msaada inayouhitaji kuiwezesha kutimiza vema majukumu yake.[472]

 

II. NDOA NI MSINGI WA FAMILIA

a. Thamani ya Ndoa

215. Msingi wa familia uko katika uamuzi na chaguo la hiari la wawili kuunganika katika ndoa, kwa kuzingatia maana na thamani ya taasisi hii yaani familia, jambo hili halimtegemei mwanadamu bali Mungu mwenyewe. “Kwa ajili ya manufaa ya wanandoa watoto wao na pia kwa ajili ya jamii, muunganiko huu mtakatifu hautegemei tena uamuzi wa mwanadamu peke yake. Kwa maana Mungu mwenyewe ndiye mwanzilishi wa ndoa na ameipatia ndoa faida na malengo ya aina mbalimbali.”[473] Kwa hiyo, taasisi ya ndoa ni “uhusiano wa ndani wa kimaisha na wa kimapendo.. uliowekwa na Muumba na yeye mwenyewe akaiwekea sheria zilizo sahihi.”[474] Ndoa sio matokeo ya sheria zilizotungwa na mwanadamu wala haikutokana na maagizo ya kisheria, lakini ndoa inapata uimara wake kutokana na mpango wa kimungu.[475] Ndoa ni taasisi inayoanzishwa hata mbele ya macho ya jamii na kushuhudiwa na jamii, “kutokana na tendo la mwanadamu ambamo wawili wanajuana na kupokeana na kisha kujitoa mmoja kwa mwingine,”[476] na msingi wake uko katika tendo la upendo wa kindoa ambalo ni zawadi kamili na timilifu ya mtu kwa mtu isiyoweza kufananishwa na chochote. Hii inaeleza uwajibikaji wa kimapendo unaoridhiwa na umma wa watu, na usioweza kubatilika.[477] Uwajibikaji huu unamaanisha kwamba uhusiano miongoni mwa wanafamilia unajengwa katika kuzifahamu haki na kwa kuheshimu haki na wajibu wa kila mmoja kwa mwingine.

216. Hakuna mwenye uwezo wowote wa kumwondolea mtu haki asili ya ndoa au kufanya mabadiliko katika tabia au sifa zake na lengo lake. Kwa kweli ndoa imejaliwa kwa namna yake iliyo sahihi, maumbile na sifa za kudumu. Bila kujali mabadiliko mengi (yasiyo na idadi) ambayo yamekwisha tokea katika muda wa karne kadhaa katika tamaduni na miundo mbalimbali ya kijamii na katika fikra za mambo ya kiroho, katika kila utamaduni kunakuwepo na aina fulani ya thamani ya kiutu ya muunganiko wa kindoa, ingawaje hii sio dhahiri kwa kila ushuhuda na kwa udhahiri ulio sawasawa kwa kila mahali.[478] Utu huu lazima uheshimiwe katika tabia zake maalumu na lazima ulindwe dhidi ya ushawishi au jaribio lolote la kuupunguzia hadhi na heshima yake. Jamii haiwezi kwa kujisikia na kwa urahisi kuweka sheria zinazohusiana na kifungo cha ndoa ambamo ndimo wawili wanapoahidiana uaminifu baina yao, kusaidiana na kukubali kuwapokea watoto, lakini jamii inayo mamlaka ya kurekebisha athari za kiraia kuhusiana na ndoa.

217. Sifa za kitabia za ndoa ni: ukamili ambamo wawili, mume na mke, wanajitoa mmoja kwa ajili ya mwingine katika hali zote za kiutu, kimwili, na kiroho; umoja ambao huwafanya wawe “mwili mmoja” (Mwa. 2: 24). Mambo muhimu yanayoeleza mtu kujitoa kwa tendo la ndoa ni msingi wa ndoa kutovunjika na uaminifu; na matunda yake ndio ile hali inayojionesha yenyewe kwa njia ya asili.[479] Mpango wa Mungu juu ya ndoa ni wa hekima na ni mpango ambao unaingia katika mawazo ya mwanadamu licha ya magumu yanayotokana na “ugumu wa moyo” (taz. Mt. 19: 8; Mk. 10: 5). Kupima jambo hili hakuwezi kufanyika kwa kutumia tu hali halisi na tabia zisizopingika (de facto) ambazo zinakwenda kinyume na mpango huo wa Mungu. Makatao makubwa ya mpango asili wa Mungu yanaonekana katika ndoa ya mitala, “kwa sababu mitala ni kinyume na usawa wa utu wa wanadamu, yaani wanaume na wanawake ambao katika kuoana wanajitoa wenyewe katika upendo ambao ni mtimilifu, na kwa hivyo upendo huo ni wa aina yake, usioweza kufananishwa na chochote.”[480]

218. Katika ukweli wa “fundisho hili,” mpango wa ndoa ni kwa ajili ya kuzaliana na kuelimisha watoto.[481] Muunganiko katika ndoa, kwa kweli, unatupatia utimilifu wa maisha katika zawadi ya dhati ya nafsi, ambayo tunda lake ni watoto, ambao wanakuwa zawadi kwa wazazi, kwa ajili ya familia nzima na jamii kwa jumla.[482] Hata hivyo, ndoa haikuwekwa kwa sababu ya kuzaliana tu.[483] Sifa ya kutovunjika kwa ndoa na thamani yake ya ushirika bado vinabaki hata kama wanandoa waliwataka sana watoto, lakini hawakujaliwa kuzaa. Katika hali ya jinsi hii wanandoa “wanaweza kushirikisha wengine ukarimu wao kwa kupokea watoto waliotelekezwa kwa namna moja ama nyingine au kufanya huduma ambayo ni hitaji kwa wengine.”[484]

b. Sakramenti ya Ndoa

219. Kwa Sakramenti hii kuwekwa na Kristo, wabatizwa wanaishi hali halisi ya urithi wa mwanadamu wa ndoa katika Umungu wa Sakramenti, ishara na chombo cha neema. Dhamira ya agano la ndoa, inaeleza maana ya ushirika wa kimapendo kati ya Mungu na wanadamu. Na hii ni ishara msingi ambayo imekuwepo wakati wote wa historia ya ukombozi. Ishara hii inasaidia katika kuelewa hatua mbalimbali za kuwekwa agano kuu kati ya Mungu na watu wake.[485] Katika ufunuo wa mpango wa Mungu wa upendo, kuna zawadi ya Mungu kujifanya mtu katika mwanae, Yesu Kristo, “Bwana harusi ambaye anapenda na anajitoa mwenyewe kama mwokozi wa wanadamu, akiunganisha ukombozi huo na mwili wake. Yesu Kristo anadhihirisha ukweli asili wa ndoa, ukweli wa “Chimbuko” la ndoa (taz. Mwa. 2: 24; Mt. 19: 5), na kule kumweka mwanadamu huru kutoka katika ugumu wa moyo. Mungu anamfanya mwanadamu kuwa na uwezo wa kutambua ukweli huu kwa utimilifu na ukamilifu.”[486] Ni katika upendo wa wawili, yaani upendo wa Kristo kwa Kanisa, ndipo utimilifu unapodhihirika katika kujitoa sadaka msalabani na hilo ndilo chimbuko na asili ya sakramenti ya ndoa. Neema ya sakramenti hii inaendana na upendo wa Kristo kwa Kanisa. Ndoa kama sakramenti, ni agano katika upendo kati ya mume na mke.[487]

220. Sakramenti ya ndoa inabeba uhalisia wa mwanadamu wa upendo wa kindoa katika maana kamili na “inawapatia wanandoa Wakristo na wazazi uwezo na uwajibikaji katika kuishi wito wao kama walei na kwa njia hiyo kuutafuta Ufalme wa Mungu kwa kujihusisha na mambo ya kidunia na kuyaweka katika utaratibu kulingana na mpango wa Mungu.”[488] Kwa undani na kwa uwazi ndoa imeunganika na Kanisa kwa fadhila ya Sakramenti ambayo inaifanya iwe “Kanisa la Nyumbani” au “Kanisa dogo.” Sakramenti inaiwezesha ndoa kuwa ishara ya umoja kwa ajili ya dunia na kwa njia hii kuiwezesha kutekeleza wajibu wake wa kinabii kwa kudhihirisha Ufalme wa amani ya Kristo, ambao dunia nzima inasafiri kuuendea.”[489]

Upendo wa kindoa, ambao chanzo chake hasa ni sadaka ya Kristo, ambayo imetolewa kwa njia ya sakramenti, inawafanya wanandoa Wakristo kuwa mashahidi wa dhamiri mpya ya kijamii iliyovuviwa kwa njia ya Injili na Fumbo la Pasaka. Upande wa asili wa upendo wa wanandoa unadumu kufanywa safi, kutiwa nguvu na kukuzwa kwa neema za kisakramenti. Kwa hali hii, licha ya kusaidiana wao kwa wao katika njia ya kuufikia utakatifu, wanandoa Wakristo wanakuwa ishara na chombo cha upendo wa Kristo katika dunia. Kwa maisha yao halisi wanaitwa kuwa mashahidi katika kutangaza maana ya ndoa, ambayo jamii ya sasa imefikia hali ngumu sana kuweza kuitambua. Ugumu huu unatokana hasa na jamii kukubaliana na mtazamo wa misimamo ya kimaadili inayojengwa na hisia za watu na kuchukuliwa kuwa yenyewe ndio msingi asili wa kuwepo kwa ndoa.

 

III. UDHAHANIA WA DHANA YA KIJAMII JUU YA FAMILIA

a. Upendo na Malezi ya Jumuiya ya Watu

221. Familia ni mahali ambapo ushirika ambao ni wa lazima sana kwa jamii unalelewa na kukuzwa. Pia familia ni mahali ambamo jumuiya halisi ya watu inajijenga na kukua.[490] Ni jambo la kushukuru kwa ajili ya nguvu iliyomo katika upendo ambao ndio msingi katika uzoefu wa mwanadamu na ambao unapata nafasi ya upendeleo katika familia wa kuufanya ujulikane.” Upendo unamfanya mwanadamu apate utimilifu kwa njia ya upendo wenyewe kuwa zawadi. Kupenda maana yake ni kutoa na kupokea kitu ambacho hakiwezi kununuliwa ama kuuzwa, lakini kinatolewa bure na kupokewa.”[491]

Ni jambo la kuushukuru upendo, uhalisia msingi ambao unaelezea ndoa na familia ambamo kila mtu – mwanamume na mwanamke – anatambuliwa, anakubalika na kuheshimiwa katika utu wake. Kutokana na upendo, yanaanza mahusiano yanayodumu katika kujitoa ambayo “kwa kuheshimu na kukuza utu wa kila mmoja kama ndio msingi wa thamani . yanachukua namna ya kupokeana kwa moyo, kushirikiana na mazungumzo ya mashauriano, huduma ya dhati na mshikamano imara.”[492] Kuwako kwa familia zinazoishi namna hii kunaonyesha kushindwa kwa migongano ya jamii ambayo kwa sehemu kubwa, hata kama ni ya aina yake, msingi wake ni ufanisi na utendaji. Kwa kujenga mtandao wa mahusiano ya ndani na ya nje baina ya watu kila leo, familia inakuwa “shule ya kwanza na isio na mbadala ya maisha ya kijamii, ambamo kuna mifano na vionjo kwa ajili ya mahusiano katika jumuiya pana inayotambulika kwa heshima, haki, mazungumzo na upendo.”[493]

222. Upendo pia unaonekana katika kuwajali kwa dhati wazee wanaoishi katika familia: kwani uwepo wao unaweza kusaidia kuendeleza tunu nzuri. Wazee ni mfano wa viunganishi kati ya vizazi na ni chanzo cha ustawi wa familia na jamii nzima. “Si kwamba wazee wanaonesha tu kuwa kuna kipengele cha tunu za maisha – kibinadamu, kiutamaduni, kimaadili na kijamii – ambazo haziwezi kuamuliwa kwa misingi ya ufanisi wa uchumi, lakini pia tunu hizo zinaweza kuchangia na kuleta matokeo mazuri yenye nguvu na ya kufaa katika sehemu za kazi na katika majukumu ya uongozi. Kwa kifupi hapa sio suala tu la kufanya kitu kwa ajili ya wazee, lakini pia ni kuhusiana na kuwakubali na kuwapokea katika miradi ya pamoja na kuwachukulia kama washiriki wenza kwa kutumia njia halisi zinazotekelezeka. Na hii ifanyike katika hatua ya kuchangia mawazo, kufanya mashauriano na katika utekelezaji wenyewe.”[494] Kama Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Bado wanaleta matunda hata wakati wa uzee wao” (Zab. 92: 15). Wazee wanajenga shule muhimu ya maisha, wanawezesha kurithisha tunu na tamaduni, na kulea ukuaji wa vizazi vipya, ambapo hujifunza kutafuta sio faida yao tu, lakini kujali faida na manufaa ya wengine pia. Ikiwa wazee wanaishi katika hali ambayo ni ya mateso na utegemezi, hapo si kwamba wanahitaji tu huduma ya afya na msaada sahihi kadiri ya hitaji, bali zaidi ya yote kabisa, wanahitaji kutendewa kwa upendo.

223. Mwanadamu ameumbwa katika upendo na hawezi kuishi bila upendo. Upendo unapojidhihirisha kama zawadi timilifu baina ya watu wawili katika kuheshimiana na kukamilishana, upendo hauwezi kupunguzwa thamani yake na kuchukuliwa kama mhemuko ama hisia, na kulinganishwa na hisia za kimapenzi tu. Jamii ambayo inaelekea zaidi na zaidi katika kuweka misimamo mikali ya kimaadili inayojengwa na hisia za watu na kupuuza uzoefu wake kuhusiana na upendo na mapenzi, kukuza hali ya kasi ya kuficha tunu zake msingi, kutangaza neno la Mungu kunakuwa na umuhimu na kwa uharaka na kwa njia hiyo kuonesha ushuhuda kwamba ukweli wa upendo wa kindoa na mambo ya kimapenzi vinakuwepo pale ambapo kuna ukamilifu na utimilifu wa watu, pamoja na sifa ya umoja na uaminifu.[495] Ukweli huu ndio chanzo cha furaha, matumaini na uhai, na hii inabaki kuwa kitu kisichowezekana kufikiwa ikiwa watu wanajifungia wenyewe katika misimamo mikali ya kimaadili inayojengwa na hisia na nadharia ya kushuku.

224. Kunapokuwepo na nadharia ambayo inaangalia utambulisho wa kijinsia kama ni hasa matokeo ya mwingiliano wa kiutamaduni na kijamii kati ya jumuiya na mtu binafsi, na kuchukulia utambulisho huu wa kijinsia wa mtu binafsi kama kitu kinachojitegemea, bila kuzingatia maana ya kweli ya jinsia, kunalifanya Kanisa kutochoka kurudia mafundisho yake ya kwamba: “Kila mtu, mwanamume na mwanamke, anapaswa kutambua na kukubali utambulisho wake wa kijinsia. Tofauti za watu pamoja na kuheshimiana kwa kukamilishana kimwili, kimaadili na kiroho kunaelekeza kwenye uzuri wa ndoa na kushamiri kwa maisha ya familia. Mapatano na utulivu wa wanandoa na wa jamii vinategemea kwa kiasi fulani namna ambavyo kuheshimiana na kukamilishana, kutimiza mahitaji na kusaidiana baina ya watu wa jinsia tofauti yanavyofanyika katika maisha ya watu.”[496] Kulingana na mtazamo huu ni jambo la lazima kiwajibu ya kwamba sheria zinazotungwa zikubaliane na sheria ya kimaumbile, kufuatana na namna ambayo utambulisho wa kijinsia unaruhusu, kwa sababu hili ni sharti la lazima kwa ajili ya wawili kuoana.

225. Mahusiano imara ya kindoa na sifa ya ndoa kutovunjika ni misingi asili ya upendo wa kindoa. Kukosekana kwa misingi hii kunaleta utengano, na hivyo, upendo mtimilifu ulio kifungo cha ndoa unakosekana. Matokeo yake ni mateso makubwa kwa watoto na madhara yake ni katika mfumo wa jamii pia.

Ni jukumu la jamii nzima kulinda na kukuza ndoa kwa kuwa ndio taasisi msingi kiasili, hasa kwa kuzingatia umuhimu na ulazima wake ambao ni mkubwa mno kwa jamii. Hivyo, lazima jukumu hili lisiachwe tu mikononi mwa wanandoa wenyewe. Kutokana na ndoa kuwa hitaji msingi la asili ya jamii, kuna haja kabisa ya kuipatia na kuitunzia ndoa heshima ya kitaasisi, na hii ifanyike kwa kuweka taratibu zinazotambulika kijamii na kisheria.

Kuingiza na kuruhusu talaka katika sheria za nchi, kumechochea maoni ya wenye misimamo mikali ya kimaadili inayojengwa na hisia za watu kuhusu kifungo cha ndoa, na hii imepata nguvu na kuenea hadi kufikia kuwa “Kweli ugonjwa mkubwa katika jamii.”[497] Wanandoa wanaolinda na kujenga tunu ya ndoa isiyovunjika “katika tabia ya unyenyekevu na kupeana moyo . wanatimiza wajibu walioupokea wa kuwa “ishara” - ishara ndogo na ya thamani kubwa. Ingawa wakati mwingine ndoa inaingia katika majaribu pia, lakini kila mara inafanywa mpya na hivyo inadumu katika uaminifu ambao kwayo Mungu na Kristo Yesu anampenda kila Mwanadamu.”[498]

226. Kanisa haliwatupi wale ambao wametalikiana na kuingia katika ndoa nyingine. Bali linachofanya ni kuwaombea na kuwapa moyo katika magumu ambayo wanakabiliana nayo katika maisha ya kiroho na kuwasaidia kudumu katika imani na matumaini. Watu hawa, alimradi wamebatizwa, wanaweza na kweli lazima washiriki katika maisha ya Kanisa. Watu waliotalakiana wanahimizwa kusikiliza neno la Mungu, kuhudhuria sadaka ya Misa, kudumu katika sala, kufanya matendo ya huruma na kushiriki katika miradi ya haki na amani inayoendeshwa na jumuiya zao, kuwalea watoto wao katika imani, na kujizoeza roho ya majuto na toba na kufanya malipizi ili kutafuta kila siku neema ya Mungu.

Upatanisho unaotokana na sakramenti ya Kitubio – ambayo ndio hufungua njia kwa ajili ya Sakramenti ya Ekaristi ambayo wanapewa wale tu ambao baada ya toba wanaishi aina mpya ya maisha ambamo hakuna tena mgongano na tunu ya ndoa kutovunjika.[499]

Kwa kuishi msimamo huu, Kanisa linakiri na kushuhudia uaminifu wake kwa Kristo na ukweli wa Kristo; wakati huohuo linaonesha moyo wa kimama kwa watoto wake, hasa kwa wale ambao bila makosa yao wenyewe, wameachwa na wenzi wao halali. Kwa imani iliyo imara, Kanisa linaamini kwamba hata wale ambao wamekwenda kinyume na amri za Mungu, na wanaendelea kuishi katika hali hiyo, ikiwa watadumu katika sala, toba na matendo ya huruma, wanaweza kupokea neema ya Mungu ya wokovu.[500]

227. Kuna ongezeko la kasi la miungano ya aina mbalimbali ya watu ambayo huchukuliwa kama ni ndoa, na msingi wake upo katika dhana fulani na kudai uhuru wa mtu kuchagua apendavyo[501] na hali hii inaelekeza jamii katika dira ya ubinafsi kabisa kuhusu ndoa na familia. Ndoa sio mkataba rahisirahisi wa kuishi pamoja, lakini ndoa ni mahusiano na mambo ya kijamii ambayo ni ya pekee yasiyoweza kufananishwa au kulinganishwa na mahusiano mengine yoyote yale. Hii ni kwa sababu familia inafanya kazi ya kuwalea na kuwaelimisha watoto. Kwa hiyo, familia ni chombo cha kumfanya kila mtu akue katika maeneo yote na kwa ukamilifu na kumwezesha kuhusika vema na maisha ya jamii.

Kuanzisha “Miungano isiyopingika” ambayo kisheria inawekwa sawa na familia, kutashusha hadhi ya familia. Familia haiwezi kujengwa katika mahusiano yenye mashaka na wasiwasi kati ya watu[502] bali familia hujengwa tu na muungano wa kudumu unaotokana na ndoa. Hapa inamaanisha kwamba agano kati ya mume mmoja na mke mmoja, linajengwa katika msingi wa maafikiano ya wawili na uamuzi na chaguo huru ambavyo huwezesha ushirika kamili wa kindoa, asili yake ikiwa ni kuendeleza uumbaji.

228. Pamoja na miungano isiyopingika, kuna tatizo linalohusiana hasa na msukumo wa kutaka muungano wa watu wa jinsia moja utambuliwe kisheria, tatizo ambalo linazidi kuwa kubwa na kuwa mada ya mjadala wa wazi katika jamii. Ni elimu juu ya asili ya mwanadamu inapooanishwa na ukweli juu ya mwanadamu ndio tu inaweza kutoa jibu sahihi juu ya tatizo hili, kwa kuangalia pia upande wa ngazi ya kijamii na ya kikanisa.[503] Mang’amuzi ya elimu hiyo juu ya asili ya mwanadamu yanaonyesha “ni kwa vipi matakwa hayo ya muunganiko kati ya watu wa jinsia moja hayaendani na mapatano ya hadhi ya ‘kindoa.’ Kwanza kabisa, hii inapingana na uwezekano halisi wa kuwezesha mahusiano haya yazae matunda kwa njia ya kurithisha uhai kulingana na mpango uliowekwa na Mungu tangu mwanzo kabisa wa mwanadamu. Kikwazo kingine ni kukosekana kwa hali ambazo zinaruhusu mahusiano ya mwingiliano yanayoleta mkamilishano baina ya mume na mke. Hali hizo ni za kimwili – kibiolojia na za ukuu wa kisaikolojia ambazo zimewekwa kwa matakwa ya Muumba. Ni katika muunganiko wa watu wawili wa jinsia tofauti ndipo mtu hupata ukamilifu katika umoja na katika utimilifu unaofikiwa na mahusiano ya kimkamilishano kisaikolojia.” [504]

Watu wa jinsia moja wenye kuendeleza ushoga waheshimiwe katika utu wao [505] na kuhimizwa kufuata mpango wa Mungu wakizingatia kwa makini kufanya mambo yanayoleta usafi wa moyo.[506] Wajibu wa kuheshimu watu hawa haimaanishi kukubali au kuhalalisha tabia ambazo haziendani na sheria ya maadili, na wala hakukubaliani wala kutambua haki ya ndoa baina ya watu wawili wenye jinsia moja na kuichukulia au kuitambua ndoa hiyo kuwa sawa na familia.[507]

“Kwa mtazamo wa kisheria, kama ndoa kati ya mume na mke ingechukuliwa kama ndio aina pekee ya ndoa, dhana ya ndoa ingepitia mageuzi makubwa na kuleta madhara makubwa katika manufaa kwa wote. Kwa nchi kuanzisha muunganiko wa kindoa baina ya watu wa jinsia moja na kuuhalalisha kisheria, ni kufanya jambo lisilo na msingi maalumu na hii inapingana na wajibu wake (nchi).”[508]

229. Mshikamano wa familia mojamoja ni kigezo cha ubora wa maisha ya jamii, kwa hiyo jumuiya na vikundi vya kiraia vinapaswa kupinga mambo yanayoharibu msingi wa jamii, kuanzia mzizi wake. Ingawa wakati mwingine sheria zinaweza kuvumilia au kustahimili tabia ambazo hazikubaliki kimaadili,[509] ni lazima sheria kamwe zisiruhusu kuiletea jamii udhaifu katika kutambua ndoa ya mume mmoja na mke mmoja kama ndio aina ya familia ya kweli. Kwa hiyo, ni jambo la ulazima kwamba mamlaka za umma “zinapinga mielekeo hii ambayo inaigawa jamii na kuhatarisha utu, usalama na ustawi wa raia wake, na lazima mamlaka hizo zihakikishe kwamba maoni ya umma ya jumla hayatumiki kupunguza umuhimu wa ndoa na familia”[510]

Ni wajibu wa jumuiya za Kikristo na watu wote wenye kutambua na kujali kwa moyo uzuri wa jamii, kukazia kwamba “familia inabeba maana ambayo ni zaidi ya kuchukuliwa kama kitu tu cha kisheria, kijamii na kiuchumi. Familia ni jumuiya ya upendo na mshikamano ambayo imewekwa kipekee kabisa kwa ajili ya kufundisha na kurithisha tunu za kiutamaduni, kimaadili, kijamii, kiroho na kidini, na tunu hizi ni za umuhimu mno kwa maendeleo na ustawi wa wanajamii wake na jamii kwa jumla.”[511]

b. Familia ni Mahali Pa Kutakatifuza Maisha

230. Kimaumbile upendo wa kindoa ni kwa ajili ya kupokea uhai. [512] Utu wa mwanadamu, anayeitwa kutangaza uzuri na matunda yatokayo kwa Mungu, ukuu wake unajidhihirisha katika jukumu la kuzaana: “Ubaba na Umama wa mtu, licha ya kubakia kiasili kuwa wa kufanana kibiolojia na viumbe wengine hai, ubaba na umama unabeba kitu cha muhimu na cha pekee ambacho ni ‘kufanana’ na Mungu. Ufanano na upekee huu ndio msingi wa familia kama jumuiya ya maisha ya watu, walioungana katika upendo (communion personarum).[513]

Kuzaana kunaelezea na kuendeleza dhana ya kijamii ya familia na kufanya nguvu ya upendo na mshikamano kati ya vizazi, ambayo juu yake msingi wa jamii umejengwa. Kugundua tunu ya kijamii ya manufaa kwa wote inayorithishwa kwa kila mwanadamu anayezaliwa ni jambo la ulazima. Kila mtoto “anakuwa zawadi kwa kaka na dada zake, wazazi wake na kwa familia nzima. Uhai wake (mtoto) unakuwa zawadi kwa watu haohao ambao ndio waliompa uhai. Mtoto hawezi kuwasaidia wazazi isipokuwa wazazi wanajisikia uwepo wake, kushirikishana anakokufanya katika maisha yao na mchango wake kwa ajili ya manufaa yao na kwa jumuiya ya kifamilia.”[514]

231. Familia iliyoundwa kutokana na ndoa ni kweli mahali pa utakatifu wa maisha, “mahali ambapo uhai – zawadi kutoka kwa Mungu – inapokelewa vizuri na kulindwa dhidi ya hatari nyingi zinazoizingira. Ni katika familia zawadi ya uhai inakuzwa kulingana na mambo ya kweli yanayojenga ukuaji wa mtu.”[515] Familia ina wajibu wa kujenga na kukuza utamaduni wa uhai [516] dhidi ya “njia mbalimbali za kuuangamiza, ‘zilizo kinyume na hali bora ya maisha’ kama ambavyo mitazamo na hali nyingi leo zinathibitisha uangamizi huo.”[517] Wajibu huu ni wa kimaamuzi usio na mbadala.

Kwa hivi, familia za Kikristo, kwa wema wa sakramenti, wanapokea wito wa pekee ambao unawafanya wawe mashahidi na watangazaji wa Injili ya uhai. Katika jamii, wajibu huu unaendeleza sifa za unabii ambazo ni ukweli na ujasiri. Ni kwa ajili ya sababu hii “kuhudumia Injili ya uhai inamaanisha kwamba, kwa njia ya kushirikiana ndani ya ushirika wa familia, familia inafanya kazi kuhakikisha kwamba sheria na taasisi za serikali hazina namna yoyote ya kukiuka haki ya kuishi, kuanzia hatua ya kutungwa mimba mpaka kifo cha kawaida. Zaidi ni kazi ya kuulinda na kuupa thamani zaidi uhai.”[518]

232. Familia inachangia kujenga uzuri wa kijamii kwa namna iliyo kuu kwa njia ya umama na ubaba unaowajibika na kwa ushiriki wa namna ya pekee wa wanandoa katika kazi ya Mungu ya uumbaji.[519] Ni lazima uzito wa wajibu huu usitumike kama kihalalisho cha kuufanya uwe umefungiwa na kuwa wa kibinafsi, bali ni lazima uzito huo uongoze maamuzi ya wanandoa katika kuupokea uhai kwa ukarimu. “Kwa kuhusisha hali ya kimwili, kiuchumi, kisaikolojia na kijamii, uzazi unaowajibika unatekelezwa kwa kuzingatia mambo mawili – kufikiri kwa tafakari ya kina na uamuzi juu ya ukubwa wa familia. Uamuzi huo wa kuzuia kwa muda maalumu au kwa muda usiojulikana kuzaa watoto wengine, unafanyika kwa kuangalia na kupima uzito wa sababu na umakini katika kuheshimu sheria ya kimaadili.”[520] Motisha zinazopaswa kuongoza wanandoa katika kutekeleza umama na ubaba unaowajibika asili yake ni utambuzi kamili wa wajibu wao kwa Mungu, kwao wenyewe, kwa familia na kwa jamii. Haya yafanyike kwa kuzingatia mpangilio sahihi wa tunu.

233. Kuhusu “njia” za kutumia katika uzazi wenye uwajibikaji, ya kwanza kukataliwa kabisa na kuchukuliwa kama haramu kimaadili ni ile ya kuweka ugumba, kuzuia yai kutengeneza mtoto au uzuiaji wa kuzaliwa mtoto na utoaji wa mimba.[521] Njia ya pili, licha ya kuwa haki ni uhalifu wa kuogofya na kutisha na unachukua haswa mpango ulio kinyume kabisa na maadili.[522] Utoaji mimba ni kitendo kinachofanyika katika hali ya kusikitisha na ambacho kinachangia mno kueneza fikra zilizo dhidi ya uhai, na hii inaleta tishio la hatari katika uwepo wa pamoja kijamii, kihaki na kidemokrasia.[523]

Lingine la kukataliwa ni matumizi ya njia za kisasa za aina zote za kuzuia mimba:[524] msingi wa kukataza haya ni usahihi na uelewa mkamilifu wa mtu na vitendo vya kujamiiana[525] na hii inaeleza wito wa kimaadili wa kulinda na kutetea maendeleo ya kweli ya watu.[526] Kwa upande mwingine, sababu hizohizo za elimu ya utaratibu wa mwanadamu zinahalalisha matumizi ya njia ya kujikatalia kwa muda tendo la ndoa katika kipindi cha uzazi kwa mwanamke.[527] Kukataa kuzuia mimba kwa njia za kisasa na kuruhusu kutumia njia ya asili katika kupanga uzazi, inamaanisha kuchagua kuzingatia mahusiano kati ya wanandoa katika kuheshimiana na kupokeana kiukamilifu, na kutafuta matokeo mazuri pia katika kuleta mpango ulio wa kiutu zaidi katika jamii.

234. Uamuzi kuhusu muda kati ya uzao mmoja na mwingine na idadi ya watoto ni juu ya wanandoa wenyewe. Hii ni moja ya haki yao inayomilikika, inayotekelezwa mbele ya Mungu huku wakiwa wanazingatia wajibu wao kwa wao wenyewe, kwa watoto wao ambao tayari wamekwishazaliwa, kwa familia yao na kwa jamii.[528] Mamlaka za umma zinapoingilia mambo haya ndani ya mipaka yake kiuwezo katika kuwapatia wanandoa habari na kuweka taratibu za kushughulikia yanayohusiana na idadi ya watu, lazima ifanye hayo kwa njia ambazo zinaheshimu kikamilifu watu na uhuru wa wanandoa. Katika kufanya hayo, mamlaka za umma kamwe haziwezi kuwa mbadala wa maamuzi ya wanandoa.[529] Vilevile vyombo vingine mbalimbali vinavyoshughulikia kwa bidii mambo haya, lazima viepuke kufanya hayohayo.

Programu zote za misaada ya kiuchumi ambazo malengo na nia zake ni kugharamia kampeni za kuweka ugumba, kuzuia ya kutengeneza mtoto au uzuiaji wa kuzaliwa mtoto na utoaji mimba, pamoja na zile ambazo ni programu saidizi kwa nia hizohizo, kimaadili zinalaaniwa vikali kwa kuwa zinaathiri na zinafedhehesha utu wa mtu na familia. Kuweza kupata ufumbuzi katika masuala yanayohusiana na ongezeko la idadi ya watu si vema kuchukulia kiurahisi, badala yake ni lazima kuyashughulikia na kuyatafutia ufumbuzi matatizo hayo kwa kuzingatia kwa wakati mmoja maadili ya kujamiiana na maadili ya kijamii. Kwa namna hii haki na mshikamano wa kweli vitakuzwa zaidi, na hivyo, utu utawekwa katika maeneo yote ya maisha ya kuanzia hali ya kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.

235. Kutaka na kutamani kuwa mama au baba hakuhalalishi kuwa na “haki yoyote kwa watoto,” na hapa haki ya mtoto aliye tumboni ambaye hajazaliwa ni dhahiri. Mtoto ambaye hajazaliwa ni lazima ahakikishiwe hali nzuri kabisa za uwepo wake kwa njia ya uimara wa familia iliyo na msingi wake katika ndoa, na kukamilishana kwa watu wawili, baba na mama.[530] Maendeleo ya kasi ya utafiti na matumizi ya teknolojia katika mambo ya uzazi yanaleta swali jipya na tete ambalo linahusu jamii na kanuni ambazo ndizo zinazorekebisha maisha ya jamii.

Ni lazima kukazia makatazo kimaadili ya “njia za kisasa za aina zote za uzazi - kama vile kutoa mbegu au yai, mama kubeba mimba kwa ajili ya kumzalia mama mwingine mtoto, njia mchanganyiko kijinsia za kupata ujauzito ambazo ni za bandia ambazo zinawezesha kutumia kizazi cha mwanamke mwingine au kwa kupandikizwa seli pevu za uzazi za watu wengine nje ya wanandoa, kwa kuwa njia hii inakiuka haki ya mtoto kuzaliwa na baba mmoja na mama mmoja ambao ndio baba na mama kwa maana ya kibiolojia na ya kisheria kwa pamoja. Njia nyingi zisizokubalika ambazo zinafanana na hii ni kutumia utaalam katika maabara, kama vile upandikizaji bandia wa yai la uzazi yaani kuweka kitaalam yai la mama mmoja kwa mama mwingine. Kwa namna hii mtoto anapatikana kama matokeo ya tendo la kiteknolojia zaidi kuliko kama tunda la asili la tendo la mwanadamu ambamo ndani yake kuna kujitoa kabisa na kiukamilifu kwa wanandoa wawili.[531] Ni lazima kuepuka njia zote zinazotumia teknolojia badala ya kutumia tendo la asili kwani tendo hilo huheshimu heshima ya mtu – kwa wazazi na watoto.[532] Kwa upande mwingine njia zitumikazo kwa ajili ya kutoa msaada kwa tendo la asili la ndoa au katika kufikia matokeo yake, njia hizo ni halali.[533]

236. Katika dunia leo, suala ambalo ni lenye umuhimu wake kijamii na kiutamaduni, kwa sababu ya matokeo yake mengi, makubwa na mazito kimaadili ni suala la kutengeneza kiumbe mwanadamu bila kujamiiana. Hili linamaanisha hasa tu uzalishaji wa kiumbe kibiolojia ambacho kinafanana kabisa kabisa kijenetiki na kiumbe cha kwanza. Katika wazo na jaribio hiyo imechukua maana tofauti ambayo hufuata hatua tofauti upande wa teknolojia na vilevile katika nia iliyokusudiwa. Hiyo inaweza kutumika kuelezea uzalishaji rahisi wa seli zenye kufanana au kijisehemu cha chembechembe hai za urithi (DNA) katika maabara. Lakini kwa nyakati hizi leo hiyo inamaanisha uzalishaji wa viumbe katika hatua ya mwanzo ya mimba kwa kutumia njia ambazo ni tofauti na zile za kutunga mamba kwa njia ya asili na kwa namna hiyo kiumbe kipya kinafanana kabisa kabisa kijenetiki na kile kiumbe kilichotumika kukitengeneza. Aina hii ya kuzalisha viumbe vipya bila kujamiiana inaweza kuwa na lengo la kiuzalishaji, yaani ni kuzalisha viumbe katika hatua za mwanzo (viinitete) au ijulikanayo kama nia ya kitabibu ambavyo viinitete hivyo vimekusudiwa kutumika katika utafiti wa kisayansi au hasa kwa ajili ya uzalishaji wa kikonyo cha seli.

Kwa mtazamo wa kimaadili uzalishaji rahisi wa seli za kawaida zenye kufanana au kijisehemu cha chembechembe hai za urithi (DNA) haileti tatizo la aina yake kimaadili. Hata hivyo, Kanisa lina maoni tofauti juu ya kuzalisha viumbe kwa njia tofauti na ili kujamiiana. Njia hiyo ni kinyume na utu wa uzazi wa mwanadamu, kwa sababu inatekelezwa bila kuwepo kabisa kwa tendo la kimapendo baina ya watu wawili, mke na mume.[534] Sababu ya pili, uzalishaji wa namna hii unaonesha aina ya ukandamizaji na utawala kamili unaofanywa na wale waliozalisha dhidi ya wale wanaozalishwa.[535] Ukweli ya kwamba viumbe wanaotengenezwa bila kujamiiana wanatumika kutengeneza viinitete ambavyo ni kwa matumizi ya kitabibu hiyo haipunguzi ubaya wake kimaadili, kwa sababu ili seli hizo ziweze kutengenezwa na kuchukuliwa, lazima kiinitete kwanza kitengenezwe na kisha kiangamizwe.[536]

237. Wazazi kama wahudumu wa uhai, lazima, kamwe wasisahau ya kwamba upande wa kiroho katika mambo ya uzazi unapewa uzito mkubwa zaidi ya upande mwingine wowote ule: “Ubaba na umama unawakilisha uwajibikaji ambao sio wa kuchukuliwa kiurahisi kuwa ni wa kimwili, bali asili yake ni wa kiroho; kweli, kwa njia hizi halisi hatua za unasaba za mtu zinapitiwa, ambazo zina mwanzo wake wa umilele katika Mungu na kwamba lazima zimwongoze kurudi kwake.”[537] Kuupokea uhai wa mwanadamu katika muunganiko wa upande wa kimwili na upande wa kiroho, familia zinachangia katika “ushirika wa vizazi” na kwa njia hii familia zinakuwa msaada muhimu mno na usio na mbadala kwa ajili ya maendeleo ya jamii. Kwa sababu hii “ni haki ya familia kupatiwa msaada na jamii katika kuwapata, kuwalea na kuwatunza watoto. Kwa hiyo, wanandoa wenye familia kubwa wana haki kupatiwa msaada unaotosheleza na wasiwekwe katika hali ya ubaguzi.”[538]

c. Jukumu la Kuelimisha

238. Katika kazi ya kuelimisha, familia zinamjenga mtu katika ukamili wa utu wake kulingana na hali zake zote, ukiwemo upande wa kijamii. Kwa kweli, familia zinatengeneza “jumuiya ya upendo na mshikamano, ambayo ni ya aina ya peke yake kuwezesha kufundisha na kurithisha tunu za kiutamaduni, kimaadili, kijamii, kiroho na kidini, tunu ambazo ni muhimu mno kwa maendeleo na ustawi wa wanafamilia wake na kwa jamii.”[539] Kwa kutekeleza wito huu wa kuelimisha, familia inachangia katika ustawi na manufaa ya wote na kuwa ndio shule ya kwanza ya fadhila za kijamii, ambazo jamii zote zinazihitaji.[540] Ni katika familia watu wanasaidiwa kukua katika uhuru na uwajibikaji, kuwapa uwezo wa kumudu jukumu lolote ndani ya jamii. Katika kuelimisha, tunu fulani za msingi zinapitishwa, kupokelewa na kukubaliwa katika jamii na kwa vizazi vinavyofuata.[541]

239. Katika kutunza na kulea watoto, familia zina wajibu asilia na usio na mbadala.[542] Upendo wa wazazi unaojiweka wenyewe katika huduma kwa watoto kwa kuwawezesha kujifunza kutoka kwa wazazi kile ambacho ni bora kilichomo kwa wazazi. Hii inaeleza kiukamilifu na kiufasaha wajibu wa kuelimisha. Pamoja na kuwa chanzo, upendo wa wazazi pia ndio kanuni ya kumotisha, na kwa hiyo ndio kanuni inayovutia na kutia msukumo na kuongoza shughuli yoyote maalumu na halisi ya kuelimisha, ikichochewa zaidi na tunu za wema, uaminifu, uzuri, huduma, kutopendelea, kujitoa sadaka, na haya ndio matunda ya upendo yenye thamani kubwa mno.”[543]

Haki na wajibu wa familia kuelimisha watoto wao ni wa “umuhimu mkubwa kwani inahusiana na kuendeleza na kudumisha uhai wa mwanadamu; ni kazi ya asili na ya kwanza kabisa kuhusiana na wajibu wa kielimu kwa wengine, kwa kuangalia upekee wa mahusiano ya kimapendo kati ya wazazi na watoto. Na haki na wajibu ambavyo haviwezi kupewa mtu mwingine kama msaidizi kabisa kabisa au kuchukuliwa na kutekelezwa na watu wengine.”[544] Wazazi wana haki na wajibu wa kuwarithisha watoto wao elimu ya kidini na malezi ya kimaadili,[545] haki ambayo nchi haiwezi kuwafutia badala yake lazima Serikali iheshimu na kukuza haki na wajibu huo wa wazazi kwa watoto wao. Na hii ni haki msingi ambayo wazazi hawawezi kuikataa ama kuiacha tu kwa wengine waifanye kama wasaidizi.

240. Wazazi ni walimu wa kwanza wa watoto wao, lakini sio walimu peke yao. Kwa hiyo ni juu yao wazazi kufanya kazi ya kuelimisha watoto wao kiuwajibikaji kwa kushirikiana kwa tahadhari na kwa uangalifu na mawakala wa serikali na Kanisa. “Sifa ya kijumuiya ya mtu – katika Serikali na katika Kanisa kwa pamoja – vinaleta hitaji la shughuli pana na zenye kuelezeka kiufasaha zinazotokana na ushirikiano ulio katika utaratibu mzuri baina ya mawakala mbalimbali wa elimu. Mawakala wote hawa ni wa lazima, japokuwa kila mmoja anaweza na anapaswa kuchukua nafasi yake na kutimiza wajibu wake kulingana na uwezo wake katika ushindani na mchango wake sahihi kwa wakala mwenyewe husika.”[546] Ni haki ya wazazi kuchagua njia ya kimalezi ambayo inaendana na ushawishi wao na kutafuta njia ambayo itawasaidia vizuri sana kutimiza wajibu wao kama waelimishaji, bila kusahau mambo ya kiroho na ya kidini. Mamlaka za umma zina wajibu wa kutoa uhakikisho wa haki hii na kuhakikisha hali zote halisi na maalumu za ulazima kwa haki hiyo kutendeka zinakuwepo na katika ukamilifu wake.[547] Katika muktadha huu na mafunzo, ushirikiano kati ya familia na taasisi za kitaaluma unachukua umuhimu wa kwanza na wa msingi.

241. Wazazi wana haki ya kupata taasisi ya elimu na kusaidiwa nayo. Mamlaka za umma lazima zione kwamba “ruzuku za umma zinagawanywa kuwezesha wazazi kutimiza wajibu huu kiukweli na kiuhuru bila kubeba mizigo isiyo ya haki kwao. Wazazi kwa njia ya moja kwa moja ama vinginevyo, hawapaswi kuendelea kudaiwa gharama za ziada ambazo zinawanyima ama kuwawekea mipaka isiyo ya kihaki katika kutekeleza uhuru huu.”[548] Ni jambo lisilo la haki kukataa kutoa misaada ya umma ya kiuchumi kwa shule zisizo za Serikali ambazo zinatoa huduma kwa jamii ya kiraia wakati msaada huo unahitajika. “Wakati wowote Serikali inapodai ukiritimba wa kielimu, hapo inavuka mipaka ya haki zake, na kufanya hivyo, itakuwa inakiuka haki . Serikali itakuwa haitendi haki ikiwa itazipokea shule za binafsi kama kitu cha kuvumilia ama kwa ustahimilivu tu. Shule hizo zinatoa huduma kwa umma, na kwa hiyo, zina haki ya kupata msaada wa kifedha.”[549]

242. Familia ina wajibu wa kutoa elimu katika ujumla na ukamilifu wake. Elimu ya kweli “inaelekezwa katika malezi ya kumjenga mtu kwa mtazamo wa ukomo wake na kwa ajili ya maslahi ya jamii yake ambamo anaishi na kwa ajili ya majukumu ambayo atakapokuwa mtu mzima atakuwa na sehemu yake ya kutekeleza.”[550] Ujumla na ukamilifu huu vinahakikishwa wakati watoto – kwa ushuhuda wa maisha na kwa mafundisho ya maneno –wanaelimishwa kwa mazungumzo, ushirikiano kijamii, kisheria, mshikamano na amani kwa njia ya kujijengea tunu msingi za haki na kimapendo.[551]

Wajibu wa baba na wa mama ni wa lazima sawia katika kuwaelimisha watoto.[552] Kwa hiyo, wazazi lazima wafanye kazi hii pamoja. Lazima watekeleze mamlaka yao kwa heshima na uungwana, lakini pia, inapokuwa lazima watumie uimara, ukali na nguvu. Na lazima hii ifanyike kwa njia yenye kuleta faida, iliyo ya kudumu na ifanyike kwa namna moja, kwa hekima na kila wakati itekelezwe kwa kulenga uzuri ukamili wa watoto katika ujumla wake.

243. Hivyo, wazazi wana wajibu maalumu katika elimu inayohusu kujamiiana. Kwa ajili ya uwiano katika ukuaji wa watoto, kuna umuhimu wa msingi kwamba wanafundishwa kwa namna yenye utaratibu na yenye mwendelezo maana ya kujamiiana na ya kwamba wanajifunza kutambua na kuheshimu tunu za kiutu na kimaadili zinazohusiana na mambo ya kujamiiana. Kwa kuangalia uhusiano wa karibu kati ya mambo ya mtu ya kimapenzi na mambo yake kuhusiana na tunu za kimaadili, elimu ni lazima iwafikishe watoto katika ufahamu wa kuheshimu kanuni za kimaadili na kuwawezesha kuziheshimu kanuni hizo wakielewa kwamba ni jambo lenye ulazima na uhakikisho wenye thamani ya juu kabisa kwa ajili ya kuwajibika kwa ukuaji wa kiashiki wa mtu mwenyewe.”[553] Ni wajibu wa wazazi kutafuta kujua mbinu na njia zinazotumiwa na taasisi za elimu kufundisha elimu ya jinsia na ashiki, hii itawezesha wazazi kuhakikisha kwamba mada hiyo ambayo ina umuhimu na ni nyeti inafundishwa vizuri.

d. Utu na Haki za Watoto

244. Mafundisho msingi ya Kanisa kuhusu jamii yamedumu katika kukazia hitaji la kuheshimu utu wa watoto. “Katika familia ambayo ni jumuiya ya watu, ni lazima ijitoe kwa makini, uangalifu na kwa madhumuni maalumu kwa ajili ya watoto. Familia ichukulie utu wa watoto kuwa ni wa maana sana na hivyo ijali na kuheshimu sana haki zao. Huu ndio ukweli kwa kila mtoto, lakini inaleta ulazima na umakini zaidi kwa kadiri ya umri wa mtoto, na kwa yule mwenye hitaji kwa kila kitu, hasa kwa mtoto aliye mgonjwa, mwenye mateso au mlemavu.”[554]

Haki za watoto lazima zilindwe kisheria ndani ya mifumo ya kisheria. Ni jambo la lazima kukazia kwamba tunu za kijamii za utoto zitambuliwe na umma katika nchi zote: “Hakuna nchi duniani wala mfumo wowote wa kisiasa wanaoweza kufikiri juu ya wakati wake ujao mpaka kwanza iangalie taswira yake katika vizazi vyake vipya ambavyo vitapokea kutoka wazazi wao urithi wa aina nyingi wa tunu, matamanio ya taifa walimo na kwa familia nzima ya watu.”[555] Haki ya kwanza ya mtoto ni “kuzaliwa katika familia ya kweli,”[556] haki ambayo haiheshimiwi kila wakati, na kwa sasa inaingia dosari ya ukiukwaji mpya kwa sababu ya maendeleo katika teknolojia ya jenetiki.

245. Hali ya watoto wengi duniani iko mbali mno katika kufikia ukamilifu, hii ni kutokana na ukosefu wa mazingira yanayofaa kwa ajili ya ukuaji wao kijumla na kiukamilifu licha ya kuwepo kwa chombo maalumu cha kisheria cha kimataifa kilichowekwa kwa ajili ya kulinda haki za watoto,[557] chombo ambacho kina uwezo wa kubana au kushurutisha kiutendaji wanajumuiya wote wa jumuiya ya kimataifa. Mapungufu haya ni yale yanayohusiana na ukosefu wa huduma ya afya, chakula kisichotosheleza, uhaba au kutokuwa na uwezekano wa kupata malezi ya kitaaluma japo katika kiwango cha chini, au malezi yasiyofaa na yasiyotosheleza. Zaidi ya hayo matatizo mengine yanabaki bila ufumbuzi: kuwatorosha watoto, kuwafanyisha kazi, hali ya ajabu ya kuwepo “watoto wa mitaani,” matumizi ya watoto katika mapigano ya kutumia silaha, kuwaozesha watoto kwa nguvu au wakati bado wanasoma, kuwatumia watoto katika biashara za picha au maandishi kama vile ya ngono na katika matumizi ya vyombo vya kisasa kabisa vya mawasiliano ya kijamii. Ni jambo lenye umuhimu mkubwa kupambana katika ngazi ya kitaifa na kimataifa kupinga ukiukaji wa haki za wavulana na wasichana kunakosababishwa na unyonyaji wanaofanyiwa katika mambo ya kujamiiana. Pia kukataa kuwaingiza watoto katika vitendo vya kuwavutia kimapenzi na kwa aina zote za utumiaji nguvu zinazowalenga binadamu hao wasio na uwezo wa kujitetea.[558] Vitendo hivi ni vya kihalifu ambavyo ni lazima vipigwe vita huku kukiwekwa njia za kuvizuia, na utoaji adhabu kwa wanaothibitika kuhusika. Kazi hii ifanywe kwa moyo wa dhati na mamlaka zote zinazohusika.

 

IV. FAMILIA KAMA MSHIRIKI MAKINI KATIKA
MAISHA YA JAMII

 

a. Mshikamano katika Familia

246. Sifa ya kijamii ya familia, iwe familia moja ama familia nyingi kwa pamoja, inaelezewa vizuri kwa kuonesha mshikamano na kushirikishana, na hiyo sio miongoni mwa familia zenyewe kwa zenyewe tu, bali pia katika aina mbalimbali za ushiriki katika maisha ya kijamii na ya kisiasa. Jambo hili linapatikana pale ambapo uhalisia wa familia umejengwa juu ya msingi wa upendo: Mshikamano unazaliwa na kukua katika familia ambayo imejengeka kimuundo na kimfumo.

Mshikamano unaozungumziwa hapa, ni ule unaoweza kuwa wa kuhudumia na kuwajali wale wanaoishi katika umaskini na wenye kuhitaji: yatima, walemavu, wagonjwa, wazee, wale wanaoomboleza, wenye mashaka, wanaoishi katika upweke, au wale waliotekelezwa. Ni mshikamano unaoweza kuwakubali na kuwapokea wahitaji hao kuwaongoza, kupokea na kulea (kama vile watoto wa kuwazaa wenyewe), mshikamano huu unaoweza kugeuza hali zote za shinikizo na kukata tamaa kwa kuzishughulikia hali hizo. Familia huweza kufanya hayo kulingana na uwezo wake wa pekee, wa kuingilia na kushughulikia mambo.

247. Mbali ya kwamba familia ni vyombo vya mambo ya kisiasa, familia zinaweza na ni lazima ziwe tegemeo, zikifanya kazi “kuona kwamba sheria na taasisi za nchi zinasaidia na kuunga mkono vizuri wajibu wa kulinda haki na wajibu za familia badala ya kuzikiuka. Kwa mtazamo huu familia zinapaswa kuongeza ufahamu wake katika kuziwezesha kuwa ‘mwongozaji na mhusika mkuu’ wa kile kinachojulikana kama ‘siasa za familia’ na kuchukua wajibu wa kurekebisha jamii.”[559] Kuweza kufika hapo lazima vikundi vya kushirikishana vya familia vikuzwe na kuimarishwa. “Familia zina haki ya kujiunga na familia nyingine na pia taasisi ili kuweza kutimiza wajibu wake wa kifamilia vizuri na kikamilifu, na vilevile kulinda haki zao, kuhimiza yaliyo mazuri na kuweza kuwakilisha panapohusika matakwa ya familia. Majukumu ya haki ya familia na vikundi vya familia lazima yazingatiwe katika mipango na katika kutengeneza programu ambazo zinagusa maisha ya familia kiuchumi, kijamii, kisheria na kiutamaduni.”[560]

b. Familia, Maisha ya Kiuchumi na Kazi

248. Uhusiano uliopo baina ya familia na mambo ya kiuchumi ni wa muhimu kabisa. Kwa upande mwingine, kwa kweli, uchumi (“oiko-nomia,” usimamizi wa mambo ya nyumbani) umeanzia na kazi za nyumbani. Kwa muda mrefu na hata mpaka leo katika sehemu nyingine bado nyumbani kumekuwa ni mahali pa uzalishaji na chimbuko la maisha. Kwa upande mwingine, hali ya kubadilikabadilika ya maisha ya uchumi inaletwa na msukumo wa watu na inafanyika katika namna ya mzunguko, ambayo daima iko katika mtandao mpana wa uzalishaji na kubadilishana bidhaa na huduma, mtandao ambao unahusisha familia zaidi na zaidi kila wakati. Ni haki kabisa kwa hiyo, familia ichukuliwe kama ni wakala muhimu mno kwa maisha ya uchumi, ambayo hayaongozwi tu na fikra za kisoko, bali yaongozwe na mpango mahususi wa kushirikishana na mshikamano miongoni mwa vizazi.

249. Familia na kazi vimeunganishwa na uhusiano wa aina ya pekee kabisa. “Familia inabeba moja ya marejeo muhimu katika kutengeneza sura ya utaratibu wa kijamii na kimaadili wa kazi ya mwanadamu.[561] Uhusiano huu una mizizi yake katika uhusiano uliopo kati ya mtu na haki yake ya kumiliki matunda ya kazi yake, na haihusu tu mtu binafsi kama mtu mmoja, bali pia kama mtu mwanafamilia, anayejulikana kama “jamii ya nyumbani.”[562]

Kazi ni muhimu na inayowezesha kuanzishwa familia, ni kwa njia ya kazi, familia zinaanzishwa na kutunzwa. Kazi pia ni sharti la maendeleo ya mtu, kwa kuwa familia inayokabiliwa na kukosa kazi inaingia katika hatari ya kushindwa kufikia nia yake.[563]

Mchango unaoweza kufanywa na familia katika uhalisia wa kazi ni wa thamani kubwa, na mara nyingi hauna mbadala. Ni mchango unaoweza kuelezewa kiuchumi na kama rasilimali ambapo familia inakuwa chanzo kikubwa cha mshikamano na hivyo kila mara huwa msaada mkubwa kwa wale waliomo katika familia, lakini hawana kazi au wale wanaotafuta kazi. Zaidi ya yote, na lililo la msingi kabisa ni mchango unaofanywa na familia wa kuelimisha maana ya kazi na kutoa maelekezo au ushauri na msaada katika kufanya maamuzi au katika kuchagua taaluma ya kusomea.

250. Ili kuweza kulinda uhusiano huu baina ya kazi na familia, kitu ambacho lazima kitambuliwe na kuheshimiwa na pia kulindwa ni suala la mshahara au mapato ya familia, uwe ni mshahara unaoiwezesha familia kumudu mahitaji yake na kuishi maisha mazuri.[564] Mshahara huo lazima uruhusu pia kuweka akiba ambayo itasaidia kununua mali kuiwezesha familia kujihakikishia uhuru wake. Haki ya kumiliki au kuwa na mali ina uhusiano wa karibu sana na uwepo wa familia, ambapo ni kama ulinzi na usalama wa familia kwa mahitaji na kuweka akiba na kujiendeleza katika upande wa mali zake.[565] Kunaweza kukawepo na njia mbalimbali za kuwezesha mshahara wa familia kuwa kitu halisi kama vile aina mbalimbali za mafungu ya misaada muhimu, mfano ruzuku kwa ajili ya familia na michango mingine kwa ajili ya wanafamilia tegemezi. Vilevile kuhakikisha malipo kwa ajili ya kazi za nyumbani zinazofanywa hapo nyumbani na mmojawapo wa wazazi.[566]

251. Katika uhusiano kati ya familia na kazi ni lazima kuangalia kwa namna ya pekee suala la kazi ya wanawake katika familia. Kijumla ni kutambua kazi ijulikanayo kama “matunzo ya nyumba,” ambayo ni jukumu pia la wanaume kama waume na mababa. Kwa kuanzia na mama, kazi ya kutunza familia na nyumba kiufasaha kwa sababu ni huduma inayolenga katika kutunza ubora wa maisha inakuwa aina ya kazi ambayo ni ya mtu na ni kuu na inayompa mtu heshima na kwa hiyo lazima itambuliwe na kuthaminiwa na jamii.[567] Kazi hiyo ipate malipo ya kiuchumi kwa kulinganisha na malipo ya kazi nyingine.[568] Wakati huohuo, lazima uangalifu utumike katika kuondoa vikwazo vyote vinavyozuia mume na mke kufanya maamuzi yao kwa uhuru kuhusu wajibu wao wa uzazi na hasa wajibu ule ambao hauruhusu wanawake kutimiza kikamilifu jukumu lao la umama.[569]

 

V. JAMII KATIKA HUDUMA YA FAMILIA

252. Hoja nzuri ya kuanzia na yenye kujenga uhusiano kati ya familia na jamii ni kutambua tegemeo na kipaumbele cha jamii kwa familia. Uhusiano wa ndani unahitaji kwamba “jamii kamwe isishindwe kutimiza jukumu lake la msingi la kuheshimu na kuhimiza kukua kwa familia.”[570] Jamii na hasa taasisi za Serikali, kwa kuheshimu kwanza kuwa familia ni “kipaumbele cha kwanza” zinahimizwa kutoa uhakikisho na kulea au kuendeleza utambulisho wa kweli wa maisha ya familia na kupinga mambo yote yanayoiharibu na kuvuruga familia. Kulinda thamani ya familia zinahitajika hatua za kisiasa na kisheria kuanzia katika kukuza mahusiano ya ndani na maelewano ndani ya familia katika kuheshimu uhai wa watoto walio tumboni ambao hawajazaliwa na kufikia uhuru kamili katika kuchagua elimu ya watoto wao. Kwa hiyo si jamii wala serikali wanaoweza kuchukua, kuwa mbadala au kupunguza mambo ya kijamii ya familia. Zaidi, wanatakiwa waithamini, waitambue, waiheshimu na kuikuza kulingana na kanuni ya auni.[571]

253. Huduma ya jamii kwa familia inaonekana kiudhabiti na bayana katika kutambua, kuheshimu na kukuza haki za familia.[572] Hii inamaanisha kwamba lazima kuwekwe sera madhubuti na za kweli huku kukiwa na namna ya kuingilia kati ambazo zinaweza kutimiza mahitaji yanayotokana na haki hizo. Kwa maana hii, kuna hali moja ya lazima inayopaswa kuwepo kwanza ambayo ni ya muhimu mno na haina mbadala: Hali hiyo ni Utambuzi na inabeba mambo haya – kulinda, kutambua na kuheshimu na kukuza – utambulisho wa familia, jamii asilia iliyojengwa katika ndoa. Utambuzi huo unawakilisha utenganisho ulio bayana kati ya familia, inayoeleweka kiusahihi na aina nyingine zote za ukimada ambazo, kwa asili yake kabisa, hazina ustahili wa jina lolote wala hadhi ya familia.

254. Kwa upande wa vikundi vya kiraia na Serikali kutambua kuwa familia ndio kipaumbele zaidi ya jumuiya nyingine yoyote ile, inamaanisha kuishinda dhana ya ubinafsi na kuikubali familia kama ndio mtazamo wa kiutamaduni na kisiasa kuhusiana na watu. Hii haiwekwi kama mbadala, bali zaidi kama msaada na ulinzi wa haki yoyote ile ambayo watu wanazo kama watu binafsi. Mtazamo huu unaleta uwezekano wa kuweka vigezo vya ufumbuzi sahihi wa matatizo mbalimbali ya kijamii, kwa sababu ni lazima watu wasichukuliwe tu kama watu binafsi, bali pia wachukuliwe kwa kuhusishwa na kiini, yaani familia ambamo wanatoka, zikiwemo tunu maalumu na mahitaji ambayo ni lazima yaendane nao.

 

SURA YA SITA

KAZI YA MWANADAMU

I. MTAZAMO WA KIBIBLIA

 

a. Wajibu wa Kuzalisha na Kuitunza Dunia

255. Agano la Kale linamwelezea Mungu kama Muumba Mwenyezi mwenye kudra (taz. Mwa. 2: 2, Ayub 38 – 41; Zab 104; Zab 147) ambaye alimuumba mtu kwa mfano wake na kumwalika kufanya kazi katika ardhi (taz. Mwa. 2: 5 – 6), na akamweka katika bustani ya Edeni ailime na kuitunza (taz. Mwa. 2: 15). Kwa wazazi wa kwanza – Adamu na Eva aliwakabidhi jukumu la kuitiisha dunia na kutawala kila kiumbe chenye uhai (taz. Mwa. 1: 28). Hata hivyo, katika kutawala viumbe vyote vyenye uhai, mwanadamu hatakiwi kufanya udhalimu wala uzembe na kutojali, badala yake anatakiwa “alime na kutunza” (taz. Mwa. 2: 15) vitu vilivyoumbwa na Mungu. Vitu hivyo havikuumbwa na mwanadamu, bali amekabidhiwa na Muumba, jukumu hili ambalo ni zawadi yenye thamani kubwa. Kuilima ardhi hakumaanishi kuitelekeza. Kuitawala maana yake ni kuitunza, kama vile mfalme mwenye busara atunzavyo watu wake na mchungaji achungavyo kondoo wake.

Katika mpango wa Muumba, mema yote yaliyoumbwa ni kwa ajili ya matumizi ya mwanadamu. Kwa mshangao wa ajabu wa watu kupewa heshima hii kubwa, mzaburi anasema: “Mtu ni kitu gani hata umkumbuke, na binadamu hata umwangalie? Umemfanya mdogo mno kuliko Mungu; umemvika taji ya utukufu na heshima; umemtawaza juu ya kazi ya mikono yako; umevitia vitu vyote chini ya miguu yake” (Zab 8: 4-6).

256. Kazi ni sehemu ya hali ya asili ya mwanadamu iliyofuata baada ya anguko lake, hivyo kazi sio adhabu wala laana.

Kwa sababu ya dhambi ya Adamu na Eva ambao walivunja uhusiano wa uaminifu na maelewano na Mungu, kazi imekuwa taabu, suluba na maumivu (taz. Mwa. 3: 6 – 8). Makatazo ya kula “matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya” (Mwa 2: 17) yanamkumbusha mwanadamu kwamba yeye amepokea yote kama zawadi na anaendelea kubaki kuwa kiumbe na sio Muumba. Ni sahihi kabisa kwamba kishawishi hiki “mtakuwa kama Mungu” ndicho kilichochochea dhambi ya Adamu na Eva (Mwa. 3: 5). Wao walitaka utawala kamili kabisa katika vitu vyote pasipo kukabidhi yote katika mapenzi na matakwa ya Muumba. Kuanzia wakati huo, ardhi ikawa ya taabu na suluba na mateso, isiyotoa mazao kikamilifu, iliyo hafifu (taz. Mwa 4: 12). Pia ni kwa jasho la mtu ndipo itawezekana kuvuna matunda ya nchi (taz. Mwa 3: 17, 19). Kwa hiyo, licha ya dhambi ya mababu zetu, maana na nafasi ya viumbe wake – miongoni mwao akiwemo mtu ambaye ameitwa kuilima nchi na kuitunza, inabaki hivyohivyo bila kubadilika.

257. Kazi inayo nafasi yenye heshima kubwa kwa sababu kazi ni chanzo cha utajiri, au walau ni sharti la mtu kuwa na maisha mazuri, na kimsingi ni njia pekee inayoweza kuleta mafanikio katika jitihada dhidi umaskini (taz. Mithali 10: 4). Lakini ni lazima kutokubali kushindwa na kishawishi cha kuabudu kazi, kwani hatimaye maana ya maisha na namna ya kuelezea maisha haviwezi kupatikana katika kazi. Ingawaje kazi ina umuhimu wa pekee kabisa, lakini kazi sio asili ya mwanadamu na wala sio kusudio la mwisho kabisa la mwanadamu. Asili ya mwanadamu na kusudio lake la mwisho ni Mungu mwenyewe. Kanuni ya msingi ya hekima ambayo ni ya kukazia sana ni kumcha Mungu. Haki ambayo hutokana na kumcha Mungu, na ndiyo inahitajika, na ndiyo ya kujali kwanza kabla ya kufikiria faida: “Kuwa na mali chache pamoja na kumcha Bwana ni bora kuliko mali nyingi pamoja na taabu” (Mit 15: 16). “Afadhali mali kidogo pamoja na haki, kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu” (Mit 16: 8).

258. Kilele cha Mafundisho ya Biblia kuhusu kazi ni amri ya kupumzika siku ya Sabato. Kwa mtu, anayejihusisha na kazi kama kitu chenye ulazima, mapumziko hayo yanampa uhuru kamili, ambao ni Sabato ya milele (taz. Ebr 4: 9 – 10). Mapumziko yanawapa watu – wanawake kwa wanaume wajibu wa kukumbuka na kuiishi upya kazi ya Mungu, kuanzia Uumbaji mpaka Ukombozi, kujitambua kuwa wao wenyewe ni kazi yake (taz. Efe 2: 10), na kumtolea shukrani Muumba wao kwa zawadi ya uhai na kwa riziki anazowajalia.

Kuikumbuka na kuiishi Sabato kunatuzuia kuwa watumwa wa kazi, iwe kwa hiari ama kwa kulazimishwa. Pia Sabato hutusaidia kushinda aina yoyote ile ya unyonyaji, uwe wa dhahiri ama uliofichika. Licha ya mapumziko ya Sabato kuwezesha watu kushiriki katika kumwabudu Mungu, kwa kweli, Sabato iliwekwa kwa ajili ya kuwalinda maskini. Sabato pia inatoa fursa ya kuwaweka watu huru kutokana na tabia zinazopingana na mambo ya kijamii kuhusu kazi ya mwanadamu. Mapumziko ya Sabato yanaweza kuchukua hata mwaka mzima. Muda huu unaweza kutumika kushinikiza uwezekano wa kuwanyang’anya wamiliki wa matunda ya nchi kwa niaba ya maskini na kuwaondolea kwa muda haki ya mali wale wenye kumiliki ardhi. “Utapanda mbegu katika nchi yako muda wa miaka sita na kuyavuna maongeo yake; lakini mwaka wa saba utaiacha nchi ipumzike na kutulia, hao maskini miongoni mwa watu wako wapate kula; na hicho watakachosaza wao, wapate kula wanyama wa kondeni. Utafanya hivyo katika shamba lako la mzabibu, na katika shamba lako la mizeituni” (Kut 23: 10 – 11). Desturi hii inaendana na imani pana na ya ndani inayoeleza ya kwamba: kujilimbikizia mali kunakofanywa na baadhi ya watu huwafanya wengine wakose mali.

b. Yesu, Mtu wa Kazi

259. Katika mahubiri yake, Yesu anafundisha kwamba lazima tuiheshimu na kuithamini kazi. Yeye mwenyewe aliyekuwa “amefanana nasi katika kila kitu, alitolea miaka mingi zaidi sana ya maisha yake katika dunia kufanya kazi ngumu na ya jasho katika benchi la seremala”[573] ndani ya karakana ya Yosefu (taz. Mt. 13: 55; Mk 6: 3) ambaye alimtii. Yesu analaani juu ya mtumishi asiye na faida, anayeficha vipaji vyake (taz. Mt. 25: 14 – 20) na kumsifia mtumishi mwaminifu na mwenye akili ambaye Bwana wake anamkuta akiwa anafanya kazi yake kwa bidii kutimiza majukumu aliyokabidhiwa (taz. Mt 24: 46). Yesu anauelezea wito wake kwamba ni kufanya kazi: Akawajibu, “Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi,” (Yn 5: 17). Yesu anawaelezea wanafunzi wake kama wafanyakazi ya kuvuna katika shamba la Bwana, kazi ambayo ni kuinjilisha binadamu (taz. Mt. 9: 37 – 38). Wafanyakazi hawa wanastahili malipo, kulingana na maelezo ya kanuni ya jumla “Kwa kuwa mtenda kazi amestahili kupewa ujira wake” (Lk 10: 7). Kwa hiyo, wanafunzi wake wamepewa idhini ya kubakia katika nyumba ambayo wamekaribishwa, wakila na kunywa kile wanachopewa (taz. Lk 10: 7).

260. Katika mafundisho yake, Yesu anamfundisha mwanadamu kwamba asiwe mtumwa wa kazi. Lililo muhimu zaidi ya yote ni kushughulikia na kujali roho yake; Yesu anakazia kuwa maana na lengo la maisha sio kuupata ulimwengu wote (taz. Mk 8: 36). Pia Yesu anafundisha kwamba kwa kweli hazina ya duniani inatumika, wakati ile ya mbinguni haiharibiki kamwe. Ni katika hazina ya mbinguni ndipo lazima watu, wanawake na wanaume, waweke mioyo yao (taz. Mt 6: 19 – 21). Hivyo, kazi lazima isiwe ndio chanzo cha shauku na kututia wasiwasi katika maisha. Watu wanapokuwa na wasiwasi, mashaka na kutotulia kwa sababu ya mambo mengi, hapo wanaingia katika hatari ya kudharau na kuweka pembeni vitu ambavyo ndivyo wanavihitaji kweli kwani ni Ufalme wa Mungu na haki yake. Vitu vingine vyote kazi ikiwa ni mojawapo, vitapata nafasi yake sahihi, maana na thamani yake ya kweli ikiwa tu vinaelekezwa katika kitu hiki kimoja ambacho ni cha lazima na ambacho kamwe hawataondolewa (taz. Lk 10: 40 – 42).

261. Yesu alifanya kazi ya kuchosha wakati wa huduma yake hapa duniani, akatimiza nia yake kwa tendo la kishujaa lililo na uwezo wa kuwaweka huru watu, wanawake kwa wanaume, kutokana na magonjwa, mateso na kifo. Sabato ambayo Agano la Kale limeiweka kama siku ya ukombozi, pale ilipochukuliwa kama siku rasmi tu, ilipoteza maana yake ya kweli inayoelezwa upya na Yesu, akikazia maana na Sabato: Akawaambia “Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, si mwanadamu kwa ajili ya Sabato” (Mk 2: 27). Kwa kuwaponya watu katika siku ya mapumziko (taz. Mt 12: 9 – 14; Mk 3: 1 – 6; Lk 6: 6 – 11; 13: 10 – 17; 14: 1 – 6), Yesu alitaka kuonesha kwamba Sabato ni yake, kwa sababu yeye ni mwana wa Mungu kweli, na ya kwamba Sabato ndiyo siku ambayo watu lazima wajitoe kwa Mungu na kwa wengine. Kuwaweka watu huru kutokana na uovu, kutendeana kindugu na kushirikishana: haya ndiyo mambo yanayoipatia kazi maana yake ambayo ina thamani kubwa. Maana hii ya kazi inauruhusu utu kupitia njia itakayoufikisha katika Sabato ya milele, wakati ambapo itafanyika sherehe ambayo watu, wanaume kwa wanawake, kwa ndani wanaitamani. Maana yake kiufasaha ni kuuongoza utu kuelekea uzoefu huu wa Sabato ya Mungu na undugu katika ushirika wake wa maisha ambamo kazi ilianzisha uumbaji mpya duniani.

262. Kazi ya mwanadamu inayolenga kuzidisha kuongeza nguvu na kugeuza ulimwengu ni lazima ifungue minyororo na kuachia huru ukamilifu mtimilifu ambao unapata asili yake na mfano wake katika Neno ambaye hakuumbwa. Kwa kweli, maandiko ya Paulo na Yohane yanatupa mwanga katika kufahamu upande wa Utatu katika uumbaji, hasa muunganiko na uhusiano uliopo kati ya Mwana – Neno na uumbaji (taz. Yn 1: 3; 1 Kor 8: 6; Kol 1: 15 – 17). Ulimwengu wote umeumbwa katika yeye na kwa njia yake na kukombolewa naye. Sio mkusanyiko wa vitu uliotokea kwa bahati, bali ni “ulimwengu” uliopangwa.”[574] Ni wajibu wa mwanadamu kugundua utaratibu uliomo katika ulimwengu na kushauri utaratibu huo, ili kuuwezesha ufikie utimilifu na ukamilifu “katika Yesu Kristo ulimwengu unaoonekana ambao Mungu aliuumba kwa ajili ya mwanadamu na ambao ulipoingia katika dhambi ‘uliwekwa katika hali ya uharibifu’ (Rum 8: 20); rejea waraka huohuo wa Mt. Paulo kwa Warumi (8: 19 – 22). Ulimwengu unarudishiwa hali yake tena kwa njia ya uhusiano wa asili na chanzo cha umungu cha Hekima na Upendo.”[575] Njia hii huleta mwanga kwa kiasi ambacho hakijawahi kutokea katika “Utajiri wa Kristo usiopimika” (Efe 3: 8), ambapo katika uumbaji kazi ya mwanadamu inakuwa huduma itolewayo kwa ajili ya ukuu wa Mungu.

263. Kazi inaeleza upande wa uwepo wa mwanadamu ulio wa muhimu kabisa wa ushiriki na sio tu katika tendo la uumbaji, bali pia katika tendo la Ukombozi. Wale wanaopokea ugumu wa kazi kwa kuunganisha na Yesu wanashiriki kwa namna fulani na Mwana wa Mungu katika kazi yake ya Ukombozi na kuonesha kwamba ni wanafunzi wa Yesu, ndio wanaochukua msalaba wake, kila siku, kwa njia ya kazi waliyoitwa kuifanya. Katika mtazamo huu, kazi inaweza kuchukuliwa kama njia ya kutakatifuza na kuchochea mambo halisi ya kidunia kwa njia ya Roho wa Kristo.[576] Kwa kueleweka hivi, kazi inaelezea utu kamili wa mwanadamu, katika hali ya kihistoria na katika mtazamo wa theolojia ya mambo ya kifo na hukumu ya mwisho. Vitendo vya kiuwajibikaji na kiuhuru vya mwanadamu vinaonyesha uhusiano wake wa asili na wa ndani na Mungu na uwezo wake wa uumbaji. Wakati huohuo, kazi ni msaada wa kila siku katika kukabiliana na aibu na uharibifu wa dhambi, hata kazi inapokuwa ni kwa njia ya jasho mtu anapata riziki yake.

c. Wajibu wa Kufanya Kazi

264. Kutambua neno hili “mambo ya ulimwengu huu yanapita” (1 Kor 7: 31) haimaanishi kuacha kujihusisha na mambo ya dunia, au hata kuacha kufanya kazi (taz. 2 The 3: 7 – 15), kwa kuwa kazi ndiyo inayojumuisha na kukamilisha hali ya mwanadamu japokuwa kazi sio lengo peke yake katika maisha.  Hakuna Mkristo yeyote ambaye kwa kuwa yumo katika jumuiya yenye umoja na ya kindugu anayo haki ya kutofanya kazi na anaishi kwa jasho la wengine (taz. 2 The. 3: 6 – 12). Badala yake, kulingana na mafundisho ya Mtume Paulo ni jambo la heshima kubwa kwa Wakristo kufanya kazi kwa mikono yao wenyewe hivyo kwamba: “hawawi wategemezi kwa mtu yeyote” (1 The 4: 12). Paulo anahimiza kuishi katika mshikamano ambao unaleta maana katika kushirikishana matunda ya kazi yao na “walio wahitaji” (Efe 4: 28). Barua ya Paulo kwa Yakobo anatetea haki ya wafanyakazi iliyokandamizwa na kudhulumiwa: “Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliozuia kwa hila, unapiga kelele; na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi (Yak. 5: 4). Waamini wanapaswa kufanya kazi yao kwa mtindo wa Kristo na kutumia nafasi hiyo kwa ajili ya ushuhuda wa Kristo, anayeamuru “kwa namna hiyo mtajipatia sifa nzuri kutoka kwa wale wasio Wakristo”  (1 The 4: 12).

265. Mababa wa Kanisa hawaichukulii kazi kama “kazi ya utumwa” japokuwa utamaduni wa nyakati zao ulishikilia kwa dhati kwamba hivyo ndivyo kazi ilivyoeleweka, lakini wakati wote kazi ni “kazi ya kiutu” (opus humanum) na hivyo mababa wanabaki kushikilia maelezo ya aina yoyote kuhusu kazi kwa heshima sana. Kwa njia ya kazi mwanadamu anautawala ulimwengu kwa kushirikiana na Mungu: hii inamaanisha kwamba mwanadamu akiwa pamoja na Mungu anakuwa ndiye mmiliki na mtawala mkuu na anakamilisha mambo mazuri kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya wengine. Kukaa bure bila kazi kunamhatarisha mtu, kwani kujishughulisha na kazi ni jambo zuri kwa mwili wake na kwa roho yake.[577] Wakristo wanaitwa kufanya kazi si kwa ajili tu ya kujipatia wao wenyewe riziki, lakini pia kwa ajili ya kuwapokea na kuwasaidia jirani zao walio maskini zaidi, ambao Mungu ameamuru kuwapa chakula, cha kunywa, mavazi, kuwakaribisha na kuwatunza na pia kuwafanya wenzi kindugu[578] (taz. Mt. 25: 35 – 36). Kwa kauli aliyoshikilia Mt. Ambrose, kila mfanyakazi ni mkono wa Kristo ambao unaendelea kuumba na kutenda mema.[579]

266. Kwa kazi na kwa kuchapa kazi kwa bidii, mwanadamu ambaye ana sehemu yake katika sanaa na hekima ya Mungu anafanya uumbaji, katika ulimwengu ambao umekwishaumbwa na Baba. Na kwa kazi, mwanadamu anaufanya ulimwengu uwe mzuri zaidi.[580] Mwanadamu anakusanya nguvu za kijamii na za kijumuiya ambazo zinaongeza manufaa kwa wote,[581] na zaidi ya yote kabisa kwa wale ambao ndio wahitaji zaidi ya wengine wote. Kazi ya mwanadamu inayoelekezwa katika huduma ya kimapendo na huruma kama ndio lengo kuu la kukamilisha inakuwa ni tukio la tafakari ya kina yenye kufikirisha sana, pia inakuwa ni sala ya moyoni. Kazi yenye nia hii humsaidia mtu kupata tumaini katika hamu ya kuifikia siku ambayo haitakuwa na mwisho. “Kwa dira hii kuu, kazi ni adhabu na wakati huohuo ni zawadi au malipo kwa mwanadamu, na hii ina uhusiano mwingine, ambao hasa ni wa kidini, ambao umeelezewa kwa furaha katika Kanuni ya Wabenediktini; kazi na sala! (ora et labora)! Ukweli wa kidini unalingana na kazi ya mwanadamu inayochochea na kukomboa mambo ya kiroho. Uhusiano huo kati ya kazi na dini unaleta tafakari ya ajabu, lakini ni muungano au ushirikiano halisi ambao una namna ya kuingilia kati matendo ya mwanadamu na matendo ya Mungu.”[582]

 

II. NGUVU YA UNABII KATIKA BARUA RERUM NOVARUM

267. Kwa kuangalia historia kuna nyakati zilizokuwa na mabadiliko makubwa na mafanikio makubwa yaliyojaa matumaini sana katika masuala ya kazi. Lakini pia kumekuwa na unyonyaji waliofanyiwa wafanyakazi wengi sana pamoja na ukiukwaji wa utu wao. Kwa Kanisa, mapinduzi ya viwanda yameliwezesha kupata changamoto kubwa ambapo Majisterio ya kijamii yamejibu kwa nguvu na kiunabii. Mafundisho hayo yamekazia umuhimu na umaana ya kanuni kidunia kwa wakati wote na kwa muda wa vipindi katika kuunga mkono wafanyakazi na haki zao.

Kwa karne nyingi ujumbe wa Kanisa ulikuwa unalenga jamii ya wakulima ukiwa kwa kawaida unatolewa mfululizo. Kwa wakati huo na matukio ya zahama na mchanganyiko ndani ya jamii iliyokuwa katika hali ya mabadilikobadiliko, yakizingatia ugumu wa kuzifahamu hali mpya za mabadiliko yasiyoweza kufikirika yaliyoletwa na matumizi ya mashine katika kazi ilibidi kuiishi na kuihubiri Injili katika “namna mpya.” Katika kiini cha Kanisa kujali kichungaji, daima kulikuwa na ulazima na uharaka sana wa kuangalia suala la kazi, yaani kulishughulikia tatizo la unyonyaji kwa wafanyakazi lililosababishwa na mpango mpya wa wafanyakazi viwandani uliokuwa na mwelekeo wa kibepari. Tatizo lingine ambalo halikuwa la kudharau ni lile la itikadi ya ujamaa na ukomunisti katika kuendesha na kutawala mambo, madai yakiwa ni hali tu ya maendeleo katika ulimwengu wa kazi. Tafakari na tahadhari au maonyo yaliyomo katika barua ya Rerum Novarum ya Papa Leo wa XIII yameingia katika muktadha wa historia hii.

268. Barua ya Rerum Novarum zaidi ya yote kabisa ni utetezi wa utu wa wafanyakazi, haki ambayo hawawezi kuondolewa kamwe. Haki hii inahusiana na umuhimu wa haki ya kumiliki mali, kanuni ya kushirikiana miongoni mwa tabaka za kijamii, haki ya wanyonge na maskini. Bila kusahau wajibu wa wafanyakazi na waajiri na haki ya kujiunga pamoja.

Mwelekeo wa mawazo yaliyoelezwa katika barua hiyo yameimarisha uwajibikaji katika kutia nguvu na kuyapa tumaini maisha ya Kikristo ya jamii. Haya yalionekana katika kuanzishwa na kuimarisha jitihada nyingi za hali ya juu za kiraia. Jitihada hizi ni pamoja na kuundwa vikundi na vituo vya mafunzo ya kijamii, kujiunga pamoja, kuundwa vikundi na vyama vya wafanyakazi, ushirika, benki za vijijini, vikundi kwa ajili ya huduma ya bima na vikundi kwa malengo ya misaada. Yote haya yaliongeza kasi ya kutungwa kwa sheria zinazohusiana na utetezi wa wafanyakazi, hasa watoto na wanawake. Sheria zilizotungwa zililenga kutoa miongozo na katika maboresho ya mishahara na usalama na usafi wa mazingira ya kazini.

269. Tangu Barua ya Rerum Novarum, kamwe Kanisa halijaacha kushughulikia tatizo la wafanyakazi katika muktadha wa kuliona tatizo hilo kuwa ni tatizo la kijamii ambalo limeendelea kugusa maeneo mengi katika dunia nzima.[583] Barua Laborem Exercens imeimarisha dhamira juu ya utu ambayo ndiyo imeongoza barua nyingine zilizotangulia. Barua imeonesha hitaji la kuelewa kwa undani maana na jukumu ambalo ni hitaji au matakwa ya kazi. Kanisa linafanya hivi kwa kuzingatia kwamba kwa kweli, “matatizo na maswali mapya kila wakati yanatokea, na kila wakati kuna matumaini mapya. Lakini pia kuna hofu na vitisho vipya. Haya yote yanaendana na suala hili la msingi la uwepo wa mwanadamu ambamo maisha yake yanajengwa kila siku na kupata utu wake maalumu kutokana na kazi. Wakati huohuo lakini, kazi inabeba sura ya kutokuwa jambo rahisi, kazi ni taabu na mateso na vilevile kazi inaleta madhara na kutotendewa haki, mambo ambayo yanazama ndani kabisa katika maisha ya jamii ngazi ya kitaifa na kimataifa”[584] Kwa kweli, kazi ni “ufunguo muhimu mno”[585] katika suala zima la jamii na kazi ni sharti, sio tu kwa maendeleo ya kiuchumi, bali pia kwa ajili ya maendeleo ya watu kiutamaduni na kimaadili. Pia kazi ni sharti kwa maendeleo ya familia, jamii na kwa jumuiya nzima ya wanadamu.

 

III HESHIMA YA KAZI

a. Sehemu ya Ubinadamu Katika Kazi na Matokeo ya Kazi ya Binadamu

270. Kazi ya mwanadamu ina umuhimu katika sura mbili: Sehemu ya ubinadamu na matokeo ya kazi. Katika upande wa matokeo, kazi ni mkusanyiko wa shughuli, rasilimali, vifaa na teknolojia vinavyotumiwa na watu – wanaume kwa wanawake kutengeneza vitu au bidhaa, kutimiza agizo la kuitawala na kuitiisha nchi kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Mwanzo. Kwa upande wa sehemu ya ubinadamu katika kazi, kazi ni shughuli ya mwanadamu ambaye ni kiumbe anayeendelea kubadilika, mwenye uwezo wa kufanya mambo mbalimbali ambayo ni sehemu ya mchakato wa kazi ambao unalingana na wito wake (mwanadamu). “Mtu anapaswa kuitiisha na kuitawala nchi, kwa sababu ya “kuumbwa katika sura na mfano wa Mungu” yeye ni mtu, na hii ina maana kwamba mtu ni kiumbe aliye na uwezo wa kufanya mambo katika namna iliyo katika mpango, mantiki na kufikiri ili kubaini sababu. Mtu ana uwezo wa kutoa maamuzi yake mwenyewe na ana hali ya kuweza kujipambanua mwenyewe. Kwa hiyo, mwanadamu, kama mtu, amekuwako kwa lengo la kazi.”[586]

Kwa maana ya matokeo, kazi inabeba upande wa ziada bila kutegemea kitu kingine kwa shughuli ya mwanadamu, ambayo imedumu kuwa na tofauti katika kuielezea kulingana na mabadiliko ya hali ya kiteknolojia, kiutamaduni, kijamii na kisiasa. Hata hivyo, kwa upande mwingine kazi kama sehemu ya ubinadamu inaelezea namna yake ya kuwa katika uimara pasipo mabadiliko kwa kuwa kwa upande huu kazi haitegemei ni vitu gani watu wanatengeneza au wanazalisha au ni aina gani ya kazi inafanywa, bali kazi inategemea tu utu wa watu kama viumbe wanadamu bila kutegemea au kufananishwa na chochote. Kutofautisha hapa ni kwa hali ya juu na ni katika kuelewa nini msingi wa hatima ya thamani ya utu wa kazi na kuhusiana na magumu katika kupanga mifumo ya kiuchumi na ya kijamii inayoheshimu haki za binadamu.

271. Mtazamo huu wa ubinadamu katika kazi, unaipa kazi heshima maalumu, ambao hairuhusu kazi ichukuliwe kama bidhaa rahisi au kama kitu kilichomo ndani ya mtu kinachoweza kutumika kama chombo cha uzalishaji. Kuiweka kazi katika thamani ya lengo la chini zaidi au la juu zaidi, kazi ni kielelezo muhimu cha mtu, ni “actus personae.” Aina yoyote ya mafundisho kuhusu mali au uchumi ambayo yanajaribu kumpunguzia hadhi mfanyakazi na kumweka kama chombo tu cha uzalishaji, yaani kama nguvukazi rahisi tu, na kuacha thamani yake kuwa katika mali tu, mafundisho ya namna hiyo yataishia katika kupotosha asili ya maana ya kazi na kuiondoa katika msingi wake wa kiutu na wenye thamani na heshima kubwa kiutu ambayo ndio hatima ya mwanadamu. Utu wa mwanadamu ndicho kipimo cha heshima ya kazi: “Hapana shaka kwa kweli ya kwamba kazi ya mwanadamu ina thamani ya aina yake ya kimaadili ambayo kwa dhahiri na kwa moja kwa moja inabaki kuunganishwa na ukweli kwamba anayeitenda au anayeifanya kazi ni mwanadamu.”[587]

Ni lazima upande wa ubinadamu wa kazi uchukue uzito kuliko upande wa matokeo kwa sababu unamhusu mtu mwenyewe ambaye ndiye anayeshughulika na kazi, ndiye anayewezesha kiwango cha ubora wa kazi na thamani ya kuitimiza au kuikamilisha. Ikiwa ufahamu huu utakosekana au kama mtu anaamua kutotambua na kuzingatia ukweli huu, kazi inapoteza ukweli wake na maana yake pana na ya kina. Katika hali hii ambayo kwa bahati mbaya imekuwa ikitokea mara nyingi na katika sehemu nyingi, shughuli ya kazi na teknolojia inayotumika vinachukua nafasi na kuonekana ndio muhimu zaidi kuliko mtu mwenyewe. Na wakati huohuo mambo haya yanabadilishwa na kuwa adui za utu wa mtu.

272. Kazi ya mwanadamu sio tu kwamba inatokana na mtu, bali kazi pia hasa kimpangilio lengo lake la mwisho kabisa ni mtu. Bila kutegemea maudhui ya kazi kimatokeo, kazi lazima ielekeze katika yule anayeifanya. Hatima ya kazi ya aina yoyote ile, kila wakati, inabaki kuwa ni mtu. Hata kama hawezi mtu kudharau kipengele cha matokeo ya kazi kuhusiana na ubora wake, kipengele hiki ni lazima kwa vyovyote vile kiwe chini ya ile hali ya mtu kujitambua mwenyewe na huu ndio upande wa ubinadamu. Jambo la kushukuru kuwa linawezekana kukaziwa ni kwamba kazi ni kwa ajili ya mwanadamu, na si mwanadamu kwa ajili ya kazi. “Kila wakati mwanadamu ndiye lengo la kazi, na hii ni kwa kazi yoyote inayofanywa na mwanadamu, hata kama kipimo cha kawaida cha viwango vya kazi ni kama kutoa ‘huduma’ tu na kama ni kazi ileile daima kiasi cha kuchosha na kudharaulika, na hata kazi iliyo ngeni mno.”[588]

273. Kazi ya mwanadamu ina pia asili yake kimaumbile katika upande wa kijamii. Kwa kweli kazi ya mtu mmoja imeunganika kiasili na kazi za watu wengine. Kwa sasa, “zaidi ya siku zote ambavyo imewahi kutokea, kazi ni fanya kazi pamoja na wengine na fanya kazi kwa ajili ya wengine. Kazi hasa ni kufanya kitu fulani kwa ajili ya mtu mwingine fulani.”[589] Matunda ya kazi yanatoa fursa kwa ajili ya kubadilishana mawazo, kujenga mahusiano na vilevile kwa ajili ya kukutana bila kutegemea. Kwa hiyo, bila kuzingatia asili ya kazi ya kijamii, kazi haiwezi kufanyiwa tathmini kiusahihi: “Kwa maana nguvu ya mwanadamu ya uzalishaji haiwezi kuzaa matunda yake mpaka mfumo wa kijamii na wa mwili wake viwepo. Pili ni mpaka utaratibu wa kisheria na wa kijamii uwe makini kuangalia kazi inavyofanyika. Tatu ni mpaka shughuli nyingine mbalimbali zinazojitegemea zishirikishwe na kazi husika na zikamilishane moja kwa nyingine. Na nne na lililo muhimu zaidi ni mpaka akili, vitu na kazi viungane na kutengeneza kitu kizima kamili kama vile kila kimoja kilivyokuwa kitu kamili. Kwa hiyo, pale ambapo asili ya kazi kijamii na kama kazi moja husika inadharauliwa, hapo inakuwa haiwezekani kutathmini kazi kwa haki na kuilipia ujira wake unaostahili.”[590]

274. Kazi pia ni “wajibu na hii inamaanisha kuwa kazi ni wajibu kwa upande wa mtu.”[591] Mtu ni lazima afanye kazi kwa sababu Muumba amemuamuru mwanadamu kufanya kazi na pia kazi ni jambo la lazima ili kuweza kujipatia mahitaji na katika kutunza na kuendeleza utu wa mwanadamu. Kazi inaelezewa kama wajibu wa kimaadili kuhusiana na mtu mmoja na jirani yake ambaye wa kwanza kabisa ni familia, lakini pia jamii alimo mhusika na taifa ambamo mhusika ni mwana au binti wa taifa hilo, kwa familia nzima ya watu. Sisi ni warithi wa kazi ya vizazi vilivyotutangulia, na wakati huohuo sisi tunafanya kazi kuwaandalia watakaokuwepo baada ya sisi.

275. Kazi inakazia utambulisho mpana wa wanadamu – wanaume na wanawake, walioumbwa katika sura na mfano wa Mungu: “Kwa kuwa mtu kwa njia ya kazi anakuwa zaidi na zaidi mtawala wa dunia, na kwa kuthibitisha utawala wake juu ya viumbe vinavyoonekana, kwa njia ya kazi yake tena bado anabaki katika hali zote na nyakati zote katika mchakato ulio ndani ya utaratibu asili wa Mungu. Na utaratibu huu unabaki kuwa wa lazima na usiobatilika ukiwa unahusishwa na ukweli kwamba mtu ameumbwa kama mwanamume na mwanamke, “katika sura na mfano wa Mungu.”[592] Hii inaeleza kazi ya mwanadamu katika dunia yote: wanaume na wanawake dunia sio mali yao, bali wao ni wale waliokabidhiwa na kuaminiwa, wanaitwa kutafakari katika namna yao ya kufanyia kazi sura yake ambayo kwayo wao wameumbwa.

b. Uhusiano Kati ya Nguvu Kazi na Mtaji

276. Kazi kwa sababu ya sifa yake ya kiutu, mtu ni juu kabisa ya rasilimali zote nyingine zinazohusika katika uzalishaji; na kanuni hii inahusu hasa mtaji.” Katika ulimwengu wa leo neno “mtaji” lina maana mbalimbali. Wakati mwingine mtaji ni vitu vinavyotumika katika shughuli yoyote kwa ajili ya uzalishaji au katika kununulia bidhaa kwa ajili ya soko. Mwingine anaweza kuzungumzia “mtaji mtu” ikimaanisha rasilimali zitokanazo na binadamu. Hapa ni kuchukulia mtu mwenyewe katika uwezo wake wa kufanya kazi, kutumia ujuzi na ubunifu, kuhisi mahitaji ya wafanyakazi wenzake, na kuelewana na wengine waliopo hapo kazini. Neno “Mtaji jamii” pia linatumika kuelezea uwezo wa watu kufanya kazi pamoja katika kundi, matokeo ya uwekezaji pamoja unaofungamanishwa na uaminifu. Maana hizi mbalimbali za kazi zinatupatia mambo ya kufanyia tafakari juu ya uhusiano kati ya kazi na mtaji katika ulimwengu wa leo.

277. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii hayajashindwa bado kusisitiza uhusiano kati ya nguvukazi na mtaji. Mafundisho hayo yameweka dhahiri kuwa kipaumbele ni nguvu kazi na pia kueleza namna mtaji na nguvukazi vinavyokamilishana.

Nguvukazi ina kipaumbele cha kiasili zaidi ya mtaji. “Moja kwa moja kanuni hii inahusu mchakato wa uzalishaji: ambapo nguvukazi ndio msingi katika kuwezesha uzalishaji, wakati mtaji ambao ni mkusanyiko wa vitu vyote vinavyotumika katika uzalishaji unabaki tu chombo cha uzalishaji. Kanuni hii ni ukweli dhahiri ambao umetokana na historia nzima ya uzoefu wa mwanadamu.”[593] Hii ni “sehemu ya urithi wa kudumu milele wa mafundisho ya Kanisa.”[594]

Ni lazima pawepo uhusiano wa kukamilishana kati ya kazi na mtaji: urithi wa mtiririko wenye mantiki katika mchakato wa uzalishaji unaonesha kwamba haya mawili yanashirikishana kisambamba moja kwa jingine na ya kwamba kuna hitaji la lazima na la haraka kutengeneza mifumo ya kiuchumi ambayo inaweza kuuondoa na kuushinda ushindani au ukinzani kati ya kazi na mtaji.[595] Wakati “Mtaji” na “nguvukazi ya kukodisha” katika mfumo wa uchumi ambao haukuwa mgumu kueleweka hayakutambuliwa kama tu rasilimali ya uzalishaji, bali kama pia na hasa zaidi ya yote kama matabaka maalumu na halisi katika jamii, hapo Kanisa lilikazia[596] ya kwamba yote mawili yalikuwa halali. “Mtaji hauwezi kuwepo bila nguvukazi na wala nguvukazi bila mtaji.”[597] Huu ni ukweli ambao bado upo hata leo, kwa sababu “kuelezea mtaji peke yake au nguvukazi peke yake na kilichofikiwa na kukamilishwa na kazi ya pamoja ya yote mawili ni uongo. Sio haki kabisa kwa kimoja kujikweza chenyewe katika kilichofanyika na kudharau kazi iliyoleta matokeo mazuri ya kingine.”[598]

278. Katika kuangalia uhusiano kati ya nguvukazi na mtaji, zaidi ya yote kabisa kuhusiana na mabadiliko ya kuvutia ya wakati wetu wa sasa, lazima tukazie misimamo ya kwamba “rasilimali kuu” na “rasilimali yenye nafasi ya pekee[599] mbele ya mwanadamu, ni mwanadamu mwenyewe na ya kwamba maendeleo kamili ya mtu yanayopatikana kwa njia ya kazi hayaishushii hadhi kazi badala yake yanakuza uzalishaji na ufanisi wa kazi yenyewe.”[600] Ulimwengu wa kazi, kwa kweli, unaendelea kugundua zaidi na zaidi thamani ya “Mtaji mtu” na sasa maelezo yanakuwa katika dhamiri ya wafanyakazi, katika bidii yao ya kazi kwa ajili ya kujiendeleza, katika uwezo wao wa kidhamiri katika kukabiliana na hali nyingi mpya, kufanya kazi pamoja kuweza kufikia malengo ya pamoja. Hizi ni sifa za kiutu ambazo peke yake zimo katika ubinadamu wa kazi zaidi kuliko matokeo ya kazi, ufundi au upande wa utendaji katika utekelezaji wa kazi yenyewe. Mambo yote haya yanaleta mtazamo mpya katika uhusiano kati ya kazi na mtaji. Tunaweza kukazia kwamba, kinyume na ambayo yamekwisha tokea katika mipango ya kazi ambamo ubinadamu katika kazi ungebaki kuwa na umuhimu mdogo kuliko matokeo, zaidi ya mchakato wa kimakenika, kwa nyakati zetu leo, upande wa ubinadamu katika kazi unaelekea kuwa na nguvu zaidi na muhimu zaidi kuliko upande wa matokeo.

279. Uhusiano kati ya kazi na mtaji mara nyingi kunaonesha tabia ya kimgongano ambayo inachukua sura mpya katika mantiki ya mabadiliko ya kijamii na kiuchumi. Nyakati zilizopita, chanzo cha mgongano kati ya nguvukazi na mtaji kilionekana “kwa kweli kwamba wafanyakazi wanatoa uwezo wao kwa ajili ya wajasiriamali, na hii kufuatana na kanuni ya kulenga faida ya juu, ilijaribu kuweka uwezekano wa ujira wa chini kabisa kwa kazi iliyofanywa na waajiriwa.”[601] Kwa siku hizi, mgongano huu unaonesha mwelekeo mpya wenye unyamazaji kutokana na maendeleo ya kisayansi na kiteknolojia pamoja na utandawazi wa masoko, ambayo haya ndio chanzo cha maendeleo, kunawaweka wafanyakazi katika hatari ya kunyonywa na mambo ya kiutendaji ya uchumi na kwa njia ya kutobana kiu ya tija katika uzalishaji.[602]

280. Inafaa mtu kutoingia katika kosa la kufikiria kwamba mchakato wa kushindana na utegemezi wa kazi katika vitu, wenyewe tu unaweza kushinda utengano katika sehemu ya kazi ama utengano katika kazi. Suala hapa sio tu maeneo au makundi ya watu wasio na kazi, kazi zilizofutwa, ajira ya watoto, kazi inayolipwa chini ya kiwango, unyonyaji wa wafanyakazi – ambayo yote yapo hadi leo, lakini pia yapo katika namna mpya na mbaya za unyonyaji kwa njia ya chanzo kipya cha kazi. Hapa unyonyaji unakuwa katika kuwafanyisha kazi saa nyingi, kazi kama ajira ambavyo mara nyingi vinachukua umuhimu zaidi ya upande mwingine wa kiutu na ulio muhimu. Kuwafanyisha watu kazi mno kunayumbisha familia na wakati mwingine kufanya mambo yasiwezekane katika mtindo wa muundo wa kazi ambayo inaleta hatari ya matokeo ya kuhatarisha mtazamo wa kiumoja wa uwepo wa mtu na umadhubuti wa mahusiano ya familia. Kama watu wanadharauliwa na njia na lengo vinageuzwa, mambo yanayodhalilisha yanaweza kupatikana katika muktadha mpya wa kazi, yaani kuzalisha visivyoshikika, urahisi, ubora zaidi kuliko wingi, “aidha kwa njia ya kuongeza ushirikiano katika jumuiya au kuongeza utengano wakati kuna watu wengi na kuna hali ya kushindwa katika ushindani na kujisikia ugenini.”[603]

c. Kazi, na Haki ya Kushiriki Kazi

281. Uhusiano kati ya nguvukazi na mtaji unaweza kuelezwa pia wakati wafanyakazi wanaposhiriki katika umiliki, usimamizi na faida. Jambo hili linasahaulika mno kila wakati, na hivyo, linapaswa kuzingatiwa zaidi. “Kwa misingi ya kazi kila mtu anastahili kabisa kujichukulia kama yeye ni mmiliki mmojawapo wa sehemu ya pale anakofanyia kazi pamoja na wengine wote pia. Njia inayowezesha azma hii kufikiwa ni kuwepo kwa namna ya kushirikisha au kuhusisha kazi na umiliki wa mtaji katika namna nyingi kadiri inavyowezekana. Pamoja na njia hii, viundwe vyombo vya aina mbalimbali vinavyounganisha watu katika masuala ya kiuchumi, kijamii na kiutamaduni. Vyombo hivi vingepata kufurahia uhuru wa kujitawala na kujiendesha vyenyewe kuhusiana na uhuru wa umma, huku vikitimiza nia yake maalumu ambayo kwayo viliundwa. Na hii ifanyike kwa ushirikiano wa kiuaminifu na kila mmoja na kwa kujali pia hitaji la manufaa ya wote. Kwa mtindo wake na pia kwa kiini chake, vyombo hivyo vingekuwa jumuiya zinazoishi, kwa kila mshiriki wa kila chombo kuangaliwa na kutendewa kama mtu na kutiwa moyo kushiriki kikamilifu katika uendeshaji wa chombo husika.”[604] Njia mpya zilizo katika mpango mzuri ambapo ujuzi unachukua nafasi zaidi kuliko umiliki wa rasilimali za uzalishaji ndizo zinazofanya kazi vizuri. Hii inaonesha dhahiri kwamba kazi; kwa sababu ya tabia yake ya dhana, inawapa watu haki ya kushiriki. Ni lazima uelewa huu uwe katika nafasi na mpangilio wake ili kuweza kutoa tathmini sahihi ya nafasi ya nguvukazi katika mchakato wa uzalishaji na kutafuta njia shirikishi ambazo zinaendana na ubinadamu katika kazi kwa asili yake na kulingana na hali halisi na dhahiri.”[605]

d. Uhusiano Kati ya Kazi na Umiliki wa Mali Binafsi

282. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanatoa maelezo pia ya uhusiano kati ya kazi na mtaji katika kuwepo kwa mali ya binafsi, na hii ipo katika haki ya kumiliki na kutumia mali binafsi.  Haki hii inafuata baada ya kukamilishwa haki ile ya kikomo cha mali kidunia na ni lazima haki ya kumiliki mali binafsi isikwamishe kazi au maendeleo ya wengine. Cha muhimu kwanza ni kwamba mali iliyopatikana kutokana na kazi lazima iwekwe katika kuhudumia kazi. Huu ndio ukweli hasa kuhusiana na umiliki wa rasilimali za uzalishaji, lakini kanuni hiyohiyo pia ijali vitu na mali ambazo ni sahihi katika ulimwengu wa fedha, teknolojia, ujuzi na watumishi. Lazima ieleweke kwamba rasilimali za uzalishaji “haziwezi kumilikiwa dhidi ya kazi, na haziwezi hata kumilikiwa kwa ajili ya umiliki tu basi.”[606] Ni jambo lisilo halali kumiliki mali “ambayo haitumiki au inasaidia kukwamisha kazi ya wengine. Hapo jitihada zinakuwa ni kupata faida ambayo sio matokeo ya maelezo kamili ya kazi na utajiri wa jamii, bali zaidi ni matokeo ya kuzuia ama kuharamisha unyonyaji, biashara ya kubahatisha au kuvunjika kwa mshikamano miongoni kwa jamii ya wafanyakazi.”[607]

283. Mali ya umma na mali binafsi, pamoja na mfumo wa uendeshaji uchumi lazima iongoze uchumi katika kumhudumia mtu, hivyo kwamba vinachangia katika kutekeleza kikamilifu kanuni ya kikomo cha vitu kidunia. Suala la umiliki na matumizi ya teknolojia za kisasa na ujuzi – vitu ambavyo katika ulimwengu wetu wa sasa ni aina ya pekee ya mali ambayo ni muhimu kama ilivyo umiliki wa ardhi au mtaji,[608] hivyo hayo lazima yalenge kumhudumia mwanadamu. Rasilimali hizi kama ilivyo kwa vitu vyote zina kikomo kidunia. Kwa hiyo, navyo lazima viwekwe katika muktadha wa kanuni za sheria na taratibu za jamii ambazo zinahakikisha kwamba rasilimali hizi zitatumika kulingana na vigezo vya haki, usawa na kuheshimu haki za binadamu. Ni jambo la kushukuru nguvu zenye kuwezesha mambo mengi zilizomo katika ugunduzi mpya na teknolojia, ambazo zinaweza kutoa mchango mkubwa katika kukuza maendeleo ya jamii. Lakini ikiwa nguvu hizo zitaendelea kubakia na kutumika katika nchi tajiri zaidi au katika mikono ya makundi machache ya wenye uwezo, hii inazihatarisha na kuzifanya ziwe chanzo cha ukosefu wa ajira na kuongezeka kwa tofauti kati ya maeneo yaliyoendelea na yale ambayo hayajaendelea.

e. Kupumzika Kazi

284. Kupumzika kazi ni haki [609] “Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya” (Mwa. 2: 2), hivyo pia watu – wanaume kwa wanawake, walioumbwa kwa sura na mfano Wake, wanapaswa kufurahia mapumziko ya kutosha na kuwa na muda wao huru ambao utawawezesha kuhudumia familia zao, kushiriki mambo ya kiutamaduni, kijamii na kidini.[610] Kuwekwa siku ya Mungu kumetokana na agizo hili.[611] Siku ya Jumapili na sikukuu nyingine za Amri, waamini ni lazima waache “kushughulika na kazi au shughuli ambazo zinawazuia kumwabudu Mungu, kupata furaha kamili ya siku ya Mungu, kufanya mambo ya matendo ya huruma na kupata mapumziko kamili yanayostahili ya mwili na akili.”[612] Mahitaji ya familia na huduma zilizo na umuhimu mkubwa kwa jamii, haya yanamhalalishia mtu kukosa mapumziko ya Jumapili. Lakini ni lazima kutoruhusu mambo haya kumjengea mtu tabia ya kushiriki mambo ambayo yanakengeusha dini, maisha ya familia au afya.

285. Jumapili ni siku ambayo inafanywa takatifu kwa kufanya matendo ya huruma, kuutoa muda huo kwa ajili ya familia na jamaa, vilevile kwa wagonjwa, kwa watu dhaifu na wazee. Ni lazima mtu asimsahau “ndugu ambaye ana mahitaji na haki sawasawa naye, na bado ndugu huyo hawezi kupumzika kazi kwa sababu ya umaskini na taabu.”[613] Zaidi ya hayo, Jumapili ni muda unaofaa kwa ajili ya tafakari, ukimya, kujisomea na taamali ambayo inajenga na kukuza ukuaji wa ndani wa maisha ya Kikristo. Pia waamini wanapaswa kujitofautisha wenyewe siku ya Jumapili kwa kufanya mambo kwa kiasi huku wakiepuka kuzidisha mambo na kupita kiasi, na hakika kuepuka vitendo vya kutumia nguvu au vya unyanyasaji ambavyo vinatokea katika sehemu za mikusanyiko ya starehe na burudisho.[614] Siku ya Bwana, kila wakati inabidi tuiishi kama siku ya ukombozi ambayo inatupa nafasi kujumuika katika “mikusanyiko ya sherehe kuwakumbuka wanaopokelewa mbinguni” (taz. Ebr. 12: 22 – 23), na hii ni kushiriki kwa kutumainia Pasaka ya kweli katika utukufu wa Mbinguni.[615]

286. Ni wajibu wa mamlaka za umma kuhakikisha kwamba, kwa ajili ya tija katika uchumi, wananchi wanapatiwa muda wa kupumzika na kumwabudu Mungu. Kwa jambo hili, waajiri wana wajibu usioweza kulinganishwa na wajibu mwingine wowote ule kwa waajiriwa wao.[616] Kuhusiana na uhuru wa kuabudu na manufaa kwa wote, Wakristo wanapaswa kuipigania Jumapili na Sikukuu nyingine za Kanisa, zitambulike kama siku za sikukuu kisheria. “Wakristo wanapaswa kuonyesha mfano kwa njia ya sala, kuheshimu, furaha na kutetea tamaduni zao kama mchango wenye thamani kubwa katika maisha ya kiroho ya jamii.”[617] Kila Mkristo anapaswa kuepuka kudai wengine mambo yasiyo ya lazima ambayo yanawazuia kuadhimisha siku ya Bwana.”[618]

 

IV. HAKI YA KUFANYA KAZI

a. Kazi ni Jambo la Lazima

287. Kazi ni haki ya msingi na ni jambo zuri kwa mwanadamu,[619] kazi inamsaidia na kumpa thamani mtu kwa sababu ndiyo njia ya kumwelezea mwanadamu na kumpa utu. Kanisa linafundisha thamani ya kazi, sio kwa sababu tu kila mara kazi ni ya mwanadamu, bali pia ni kwa sababu ya asili ya kazi kama kitu cha lazima.[620] Kazi ndiyo inayowezesha familia kuanzishwa na kutunzwa,[621] kuwa na haki ya kumiliki mali,[622] na kuchangia manufaa ya wote katika familia ya wanadamu.[623] Kwa kuzingatia upande wa maadili kuhusiana na suala la kazi katika maisha ya jamii, Kanisa haliwezi kuacha kulitaja tatizo la kukosa ajira kama “kweli janga la jamii”[624] na zaidi ya yote kwa vijana wa kizazi kipya.

288. Kazi ni nzuri kwa watu wote kuwa nayo na ni lazima kazi zipatikane kwa watu wote walio na uwezo wa kufanya kazi. Kwa hiyo “Ajira kamili” inabaki kuwa lengo la lazima kwa kila mfumo wa uchumi ambao unalenga haki na manufaa kwa wote. Jamii ambamo haki ya kufanya kazi inakiukwa au inadharauliwa katika mtindo wa mfululizo, na ambapo sera za kiuchumi haziruhusu wafanyakazi kufikia hali ya kuridhika na ajira, “jamii hiyo haiwezi kukubalika kwa mtazamo wa kimaadili, wala jamii hiyo haiwezi kupata amani ya jamii.”[625] Jukumu la muhimu na ambalo ni kubwa mno linawaangukia wale “waajiri wasio wa moja kwa moja”[626] ikimaanisha wale ambao ni watu binafsi au taasisi za aina mbalimbali – walio katika nafasi ya kuongoza kazi ya kutengeneza sera zinazohusiana na kazi na uchumi katika ngazi ya kitaifa au kimataifa.

289. Uwezo wa kuweka mipango ya jamii inayolenga kufikia manufaa kwa wote na kuangalia maisha ya mbele, unapimwa zaidi ya yote na msingi wa matarajio ambayo jamii hiyo inaweza kuyatoa. Kuwepo kwa kiwango kikubwa cha kukosa ajira, mifumo ya elimu iliyopitwa na wakati na kubakia katika magumu ya kupata mafunzo na malezi ya kitaaluma na tatizo la soko la ajira hasa kwa vijana, mambo haya yanaleta kikwazo kikubwa katika jitihada za watu kufikia ukamilifu wa kibinadamu na kitaaluma. Kwa kweli wale ambao hawana ajira ama ajira yao ni ya kiwango cha chini wanapata mateso yanayoletwa na hali hiyo katika utu na wanaingia katika hatari ya kutengwa ndani ya jamii na hivyo kuwa waathirika wa kutengwa na jamii.[627] Kwa jumla tatizo hili haliwahusu watu vijana tu, lakini pia wamo wanawake, wafanyakazi wasio wahitimu katika ujuzi maalumu, watu wenye ulemavu, wahamiaji, wafungwa walioachiwa huru, wasio na elimu, na wengine wote wanaokutana na magumu makubwa kila wanapojaribu kutafuta nafasi yao katika ulimwengu wa ajira.

290. Kwa mtu kuendelea kubakia katika ajira inategemea zaidi na zaidi uwezo wake kitaaluma.[628] Kwa hiyo ni lazima mifumo ya elimu na ya maelekezo wasidharau malezi na mafunzo ya kiutu na kiteknolojia, jambo ambalo ni la lazima kumwezesha mtu kutimiza kikamilifu wajibu wake. Hali ya kuendelea na kuenea zaidi na zaidi ya ulazima wa watu kubadili kazi mara nyingi katika maisha ya mtu, inaleta hitaji la haraka na muhimu kuifanya mifumo ya elimu iwe ni ya kuwatia moyo watu kuwa na upana wa kuangalia mambo yalivyo leo na kurudiarudia kushiriki mafunzo. Vijana wanapaswa kufundishwa kushughulika na ubunifu wao wenyewe, kupokea majukumu ya kuwawezesha kuwa na uwezo wa kutosheleza kuingia katika ushindani. Hii inasaidia kwani kuna hatari inayohusiana na muktadha wa uchumi unaobadilibadilika ambao kila mara namna yake ya kubadilika haiwezi kutabirika.[629] Sawa na jukumu hilo, lingine lisilokwepeka ni kutoa fursa ya kozi zifaazo kwa watu wazima wanaotafuta kupata mafunzo upya tena na kwa wale ambao hawana ajira. Kwa jumla zaidi, watu wanahitaji njia madhubuti kuwasaidia wanapoelekea katika ulimwengu wa kazi, kuanzia na mifumo ya kimalezi na hivyo itawapunguzia ugumu katika kukabiliana na nyakati za mabadiliko, zisizo na uhakika na hali zinapokosa uimara.

b. Jukumu la Serikali na Vikundi vya Kijamii Katika Kukuza Haki ya Kufanya Kazi

291. Matatizo ya ajira yanatoa changamoto katika wajibu wa Serikali, ambayo wajibu wake ni kukuza sera za ajira thabiti, ikimaanisha sera ambazo zinawezesha upatikanaji wa fursa za ajira ndani ya nchi na kuimotisha sekta ya uzalishaji iweze kufikia lengo hili. Wajibu wa Serikali kuwahakikishia raia wake wote haki ya kufanya kazi, haimaanishi kwamba serikali ihusike mno tena moja kwa moja katika kutekeleza jukumu hili na kufanya mambo ya uchumi yasiweze kuruhusu jitihada huru za watu binafsi. Serikali inao wajibu wa “kuendeleza shughuli za kibiashara kwa kuweka mazingira ambayo yatahakikisha kuwepo fursa za ajira, kuchochea shughuli hizo pale zinapokosekana au kuzisaidia shughuli hizo pale zinapokumbwa na matatizo au migogoro.”[630]

292. Kwa sababu ya maendeleo ya haraka katika mahusiano ya uchumi na fedha pamoja na suala la soko la kazi, kuna haja ya kukuza ushirikiano thabiti kimataifa miongoni mwa nchi. Ushirikiano huo inafaa ujengwe kwa njia ya mikataba, makubaliano na mipango ya pamoja ya utekelezaji ambayo inalinda haki ya kazi, na hii ifanyike hata wakati hali ya uchumi kitaifa na kimataifa inapokuwa katika hali mbaya mno. Ni lazima kuelewa ukweli kwamba haki ya mtu ya kufanya kazi ni haki ambayo moja kwa moja ndiyo inayotegemewa katika kukuza haki ya jamii na usalama wa raia. Kuhusu haki hii mashirika ya kimataifa na vyama vya wafanyakazi wana jukumu kubwa. Jitihada za pamoja ambazo zinatumia njia zifaazo kabisa, ni lazima zijibidishe kwanza kabisa kujenga “mfungamano wenye nguvu zaidi ambao haujawahi kuwepo wa taratibu na kanuni za kisheria ambazo zinalinda kazi za watu wote – wanaume, wanawake na vijana na kuwahakikishia ujira wanaostahili.”[631]

293. Kama ilivyokuwa wakati wa Barua Rerum Novarum, kukuza haki ya kazi, bado ni muhimu leo, ya kwamba kuwe na “mchakato ulio wazi kwa jamii kujipanga yenyewe.”[632] Kuna mifano na shuhuda nyingi zenye maana ya namna jamii ilivyoweza kujipanga. Mifano hiyo ni jitihada nyingi zinazofanywa, zikiwa na sifa ya ushiriki, ushirikiano na usimamizi wa watu wenyewe ambayo inabainishwa na kuunganisha nguvu na mshikamano katika biashara na kijamii. Haya yote yamejengwa kwa ajili ya soko kama sekta iliyo na sura nyingi na umuhimu katika shughuli ya kazi ambayo alama yake katika kufikia lengo ni uzingatio wa pekee wa upande wa kimahusiano wa vitu vilivyozalishwa na huduma za aina nyingi zinazotolewa: ujenzi, kutunza afya, huduma muhimu za jamii na utamaduni. Jitihada hizi zijulikanazo kama “sekta ya tatu” zinawakilisha fursa ya muhimu kwa maendeleo ya kazi na uchumi ambayo haijawahi kutokea.

c. Familia na Kazi

294. Kazi ni “msingi wa malezi ya maisha ya familia, na hii ni haki ya asili na jambo ambalo ni wito kwa mtu.”[633] Kazi inawezesha familia kuanzishwa na kuwepo, na inasaidia kuihakikishia jamii uwezo wa kutunza watoto wao.[634] Kwa uzoefu wa watu wengi familia na kazi vina uhusiano wa karibu sana. Hatimaye, uhusiano huu unastahili kuchukuliwa katika ufahamu halisi, mpana zaidi, kwa kujali na kutafuta kuyaelewa haya mawili kwa pamoja, bila kuweka mipaka katika mtazamo wa familia ya mhusika tu au kwa kujali tu upande au maoni ya kiuchumi juu ya kazi. Kwa mtazamo huu, ni lazima shughuli za biashara, vyama vya kitaaluma, vyama vya wafanyakazi wa kuajiriwa na Serikali watengeneze na kukuza sera ambazo, katika suala la ajira haziumizi familia bali zaidi zinazisaidia na kuziunga mkono. Na kwa kweli, maisha ya familia na kazi yanaathiriana kwa njia nyingi na kwa namna moja ama nyingine. Yapo mambo mengi ya kazi yanayompunguzia mtu muda kwa ajili ya familia: kusafiri umbali mrefu sana kwenda kazini, kuajiriwa sehemu mbili, uchovu wa kimwili na kisaikolojia.[635] Wakati huohuo, hali ya kukosa ajira inaleta madhara ya kimali na kiroho kwa familia, kama vile ilivyo kwa wasiwasi na migongano ya familia inavyoathiri vibaya fikra ya mtu na tija katika kazi yake.

d. Wanawake na Haki ya Kufanya Kazi

295. Vipaji vya kike vinahitajika katika maisha yote ya jamii, kwa hiyo ni lazima kuhakikisha kuwa kuna wanawake katika sehemu za kazi. Hatua ya muhimu na ya lazima isiyokwepeka katika kuelekea kufikia lengo hilo, ni kuweka njia thabiti za kuwezesha wanawake kupata mafunzo ya kitaaluma. Kutambua na kulinda haki ya wanawake katika muktadha wa kazi kwa jumla kunategemea namna kazi ilivyowekewa mpangilio ambao lazima ujali heshima na wito wa wanawake, ambao “kuwaendeleza kwa kweli.. kunahitaji kwamba kazi inapaswa iwe katika muundo ulio katika namna ambayo haiwazuii wanawake katika kutekeleza yale yaliyo ya pekee na maalumu kwao.”[636] Suala hili ni kipimo cha ubora wa jamii na utetezi dhabiti wa haki ya wanawake ya kufanya kazi.

Kudumu kwa aina nyingi za ubaguzi wa heshima na wito wa wanawake katika suala la kazi ni kutokana na mfululizo mrefu wa hali zinazoumiza wanawake, ambao wameonekana “haki yao kutowakilishwa vema” na wao wenyewe “kushushwa hadhi katika jamii na hata kufikia hali ya utumwa.”[637] Kwa bahati mbaya magumu haya hayajaweza kukabiliwa na kuyashinda. Hali hii inadhihirika pale palipo na hali ambazo zinawakatisha tamaa wanawake na kuwafanya watumike kama vyombo vya unyonyaji huu kweli. Kutambua kwa dhati haki za wanawake mahali pa kazi kunakoonekana hasa katika mambo ya malipo, bima na usalama kijamii ni hitaji la lazima na la haraka.[638]

e. Ajira kwa Watoto

296. Kufanyisha kazi watoto, katika namna ambayo haiwezi kuvumilika, ni aina ya unyanyasaji ambao sio dhahiri kuliko mwingine lakini sio kwa sababu hii unyanyasaji huu unapungua katika kuogofya.[639] Huu ni unyanyasaji ambao zaidi ya kuwa na madhara ya kisiasa, kiuchumi na kisheria, unabaki haswa kuwa tatizo la kimaadili. Papa Leo wa XIII aliandika na kuonya “Kuhusiana na watoto, uangalifu mkubwa lazima utumike kuepuka wasiwekwe katika karakana, na viwanda vikubwa mpaka hapo miili na akili zao zitakapokua kikamilifu. Kwa kuwa kama hali ya hewa mbaya inavyoangamiza machipukizi majira ya kuchipua vivyo hivyo, uzoefu unaopatikana mapema mno katika maisha ya mtu ya taabu na ugumu unaharibu matazamio ya mtoto na kusababisha jitihada za kumpatia elimu ya kweli kuwe jambo lisilowezekana.”[640] Bado hata baada ya zaidi ya miaka mia moja, tatizo sugu la ajira kwa watoto halijakwisha.

Hata pamoja na kuelewa kwamba walau kwa sasa katika baadhi ya nchi mchango katika familia unaotokana na ajira ya watoto na kwa uchumi wa taifa ni kwa kiwango kisichoweza kupingika, na ya kwamba katika matukio mengine aina ya kazi ya ziada inaweza kuwasaidia watoto wenyewe kiuhakika, bado Mafundisho ya Kanisa yanalaani “Unyonyaji wa watoto katika sehemu za kazi na kuuweka unyonyaji huo katika hali dhahiri ya utumwa.”[641] Unyonyaji huu unaonesha ukiukaji mkubwa wa heshima ya mtu, ambao kila mtu amejaliwa” bila kujali mtu huyo ni mdogo kiasi gani au kuonekana sio mtu wa muhimu kwa mtazamo wa namna atumikavyo mtu huyo.”[642]

f. Tatizo la Uhamiaji na Kazi

297. Uhamiaji unaweza kuchukuliwa kuwa ni jambo linalowezesha maendeleo, badala ya kuonekana kama kikwazo. Katika ulimwengu wa leo, ambapo bado kuna ukosefu mkubwa wa usawa kati ya nchi tajiri na maskini, na ambamo maendeleo ya mawasiliano yanapunguza haraka umbali, uhamiaji wa watu wanaotafuta maisha bora unaongezeka. Wahamiaji wanatoka katika nchi ambazo zina maisha duni na wanapoingia katika nchi zilizoendelea, kila mara wanaonekana kama tishio katika ustawi mkubwa uliofikiwa katika nchi hizo kutokana na kukua kwa uchumi wao kwa muda mrefu. Kwa matukio mengi tu, bado wahamiaji wanaziba mapengo ya mahitaji ya wafanyakazi ambayo kama wahamiaji wasingalifika yangebakia wazi katika sekta na nchi ambazo wafanyakazi wazalendo hawatoshelezi au hawako radhi kufanya kazi hiyo.

298. Taasisi katika nchi ambazo wahamiaji wanaingia, lazima ziangalie kwa makini kuenea kwa kishawishi cha kunyonya wafanyakazi wageni kwa kuwanyima haki ambazo wanawapatia wazalendo na ni haki ambayo ni stahili inayopaswa kuhakikishiwa wote bila ubaguzi. Kuweka uwiano wa uhamiaji kulingana na vigezo vya usawa na uwiano[643] ni moja ya masharti ambayo hayakwepeki katika kuhakikisha kwamba wahamiaji wanashirikishwa na kuingizwa katika jamii pamoja na uhakikisho unaohitajika katika kutambua utu wao. Wahamiaji wanapaswa kupokelewa kama watu na kusaidiwa, wao wenyewe pamoja na familia zao, kuwawezesha wawe sehemu ya maisha ya jamii.[644] Kwa mantiki hii, haki ya kuwaunganisha wahamiaji na familia zao, lazima iheshimiwe na kukuzwa.[645] Wakati huo hali zinazosukuma ongezeko la fursa za kazi katika nchi au maeneo walikotoka wahamiaji hao, lazima ifanyiwe kazi kwa jitihada zote.[646]

g. Ulimwengu wa Kilimo na Haki ya Kufanya Kazi

299. Kazi ya kilimo inastahili kuangaliwa kwa makini, kwa sababu ya nafasi na umuhimu wake kijamii, kiuchumi na kiutamaduni, na kwamba kilimo kinaendelea kuwa sehemu ya mifumo ya kiuchumi katika nchi nyingi. Na pia kwa sababu ya kuzingatia matatizo mengi ambayo inabidi yashughulikiwe katika uchumi wa leo ambao umekuwa wa kidunia na vilevile ni kwa sababu ya ongezeko la umuhimu wa kulinda mazingira asili. Kwa hiyo, mabadiliko ya haraka na makubwa yanahitajika katika kukijenga upya kilimo na kwa watu wa vijijini kuwapa thamani ya haki na kuchukulia kama ndio msingi wa uchumi bora ndani ya maendeleo ya jumuiya ya jamii nzima.”[647]

Mabadiliko makubwa yanayoendelea katika mambo ya kijamii na kiutamaduni yakiwemo mabadiliko katika kilimo yanayopanuka zaidi katika ulimwengu wa vijiji, yanaleta hitaji la kupima vizuri na katika mambo mbalimbali maana ya kazi ya kilimo. Hii ni changamoto yenye umuhimu mkubwa ambayo lazima ishughulikiwe na sera za kilimo na mazingira ambazo zina uwezo wa kushinda maoni ya ustawi wa kizamani na kujenga mitazamo mipya kwa ajili ya kilimo cha kisasa ambacho kinaweza kuchukua nafasi na kutoa mchango muhimu katika maisha ya kijamii na kiuchumi.

300. Katika baadhi ya nchi mgawanyo mpya wa ardhi kama sehemu ya sera zenye nguvu katika mabadiliko ya umilikaji ardhi ni jambo lisilokwepeka. Na hii inasaidia katika kuondoa vikwazo ambavyo mifumo isiyozalisha ya mashamba ya kibepari - iliyolaaniwa na mafundisho ya Kanisa[648] yanaweka mambo katika njia ya maendeleo ya kweli ya kiuchumi.” Nchi zinazoendelea zinaweza kufanikiwa kushughulikia mchakato wa sasa ambamo umilikaji wa ardhi unawekwa zaidi na zaidi mikononi mwa wachache. Hali hii inaweza kukua na kuwa tatizo la kimuundo kwa mfano mapungufu katika sheria na ucheleweshaji katika kutambua hati miliki za ardhi na kuhusiana na soko la mikopo. Mengine ni hali ya kutojali suala la kufanya utafiti na kutoa mafunzo ya kilimo, kudharau huduma za jamii na miundombinu katika maeneo vijijini.[649] Kwa hiyo, mabadiliko katika umiliki ardhi yanakuwa ni wajibu wa kimaadili zaidi ya ulazima wa kisiasa, kwa kuwa kushindwa kufanya mabadiliko hayo ni kuzuia nchi hizo kunufaika na mambo yanayotokana na upana wa masoko, na kwa ujumla ni kukosesha kunufaika na fursa nyingi sana zinazopatikana kutokana na mchakato wa utandawazi.[650]

 

V. HAKI YA WAFANYAKAZI

301. Kama ilivyo kwa haki nyingine zote, haki ya wafanyakazi zina msingi wake katika asili ya mwanadamu na katika utu aliourithi ambao unaovuka mipaka ya mwanadamu. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yameona inafaa kuorodhesha baadhi ya haki hizo, kwa matumaini kwamba haki hizo zinaweza kutambuliwa na kuingizwa katika mifumo ya kisheria. Kuna haki ya kupata ujira wa haki;[651] haki ya kupumzika;[652] haki ya “mazingira mazuri ya kazini na hali nzuri ya mazingira katika viwanda vya kutengeneza bidhaa. Haki hii inadai mazingira ambayo hayahatarishi afya ya mwili ya wafanyakazi na maadili yao katika ujumla wake.”[653] Haki nyingine ni kulinda utu au nafsi ya mtu mahali pa kazi “pasiwepo na mateso au hali ya kufedhehesha dhamiri au utu wa mtu;”[654] haki ya mgao sahihi wa ruzuku ambayo ni ya lazima kwa matunzo ya wafanyakazi ambao hawana ajira pamoja na familia zao.[655] Pia kuna haki ya kupata mafao ili kumhakikishia mtu mahitaji yake ya uzeeni, haki na malipo katika ugonjwa na panapotokea ajali inayohusiana na kazi.[656] Vilevile kuna haki ya usalama wa jamii kuhusiana na uzazi;[657] haki ya kukutana na kujiunga katika vikundi au vyama.[658] Haki hizi zinakiukwa kama ambavyo inathibitishwa na ukweli wa masikitiko ya wafanyakazi ambao wanalipwa kiasi kidogo kuliko stahili yao na wala hawana utetezi au uwakilishi unaoweza kuwasaidia. Inatokea mara nyingi kwamba mazingira ya kazi kwa watu: wanaume, wanawake na watoto hasa katika nchi zinazoendelea yako katika hali isiyo ya kiutu kiasi kwamba hali ilivyo ni kukiuka haki ya utu wao na kuathiri na kuhatarisha afya zao.

b. Haki ya Ujira Halali na Mgawanyo wa Mapato

302. Ujira ni njia muhimu mno katika kufikia haki ndani ya mahusiano kazini.[659] Suala na “mshahara wa haki ni matunda halali ya kazi.”[660] Wale wanaokataa kulipa mshahara wa haki au wale wanaochelewesha mshahara, au kulipa mshahara usiowiana na kazi iliyofanyika, hawa wanatenda kinyume na haki kabisa (taz. Law 19: 13; Kum 24: 14 – 15; Jos. 5: 4). Mshahara ndio unaomwezesha mfanyakazi kujipatia mahitaji hapa duniani. “Ujira wa mfanyakazi unapaswa uwekwe hivyo kwamba unakuwa njia ya kumwezesha mtu na wategemezi wake kupata thamani yake kutokana na mali na maisha yake kijamii, kiutamaduni na kiroho. Mshahara unapaswa ulingane na kazi na tija ya kila mmoja, hali ya karakana ama kiwanda anakofanyia kazi, na suala zima la ustawi na manufaa kwa wote.”[661] Mkataba tu baina ya mwajiriwa na mwajiri, kuhusiana na kiasi cha malipo hautoshelezi kuwa “mshahara wa haki,” kwa sababu mshahara wa haki” lazima usiwe chini ya kiwango cha kumwezesha mfanyakazi kuishi.”[662] Hivyo, haki ya asili ni zaidi kabisa ya uhuru wa mkataba ama yale yaliyomo katika mkataba.

303. Ustawi wa uchumi wa nchi haupimwi kwa kuangalia tu wingi wa vitu vinavyozalishwa, lakini pia kuangalia namna ambayo vitu hivyo vimezalishwa, vilevile kuzingatia usawa katika mgawanyo wa mapato. Mgawanyo huo unapaswa uruhusu kila mmoja kupata vitu anavyohitaji kwa maendeleo yake binafsi na kwa kuboresha zaidi maisha yake. Mgawanyo sawa wa mapato utaonekana ikiwa vigezo msingi vitazingatiwa na sio tu haki katika mkusanyiko wa jumla. Vigezo hivyo ni haki ya kijamii, ikimaanisha kujali thamani ya lengo katika kazi iliyofanywa, kujali utu wa mtu kama ambaye ndiye amefanya kazi hiyo. Ustawi wa kweli wa uchumi unapatikana pia kwa njia ya sera za kijamii zinazofaa katika kugawana mapato, ambapo hali ya jumla inazingatiwa bila kusahau stahili na vilevile hitaji la kila raia.

c. Haki ya Mgomo

304. Mafundisho ya Kanisa yanatambua uhalali wa kugoma pale ambapo mgomo hauwezi kuepukika, au walau inapokuwa kwamba mgomo ni wa lazima katika kupata kile kilicho sahihi,”[663] na ufanyike pale tu ambapo njia nyingine zote za ufumbuzi wa mgogoro zimeshindikana.[664] Mgomo, ukiwa moja ya ushindi mgumu wa kishujaa unaopatikana kwa vyama vya wafanyakazi unaweza kuelezwa kuwa ni nguvu ya pamoja ya wafanyakazi kukataa kuendelea kutoa huduma yao, kwa lengo la kushinikiza mwajiri, Serikali au kwa maoni ya umma waweze kupatiwa maboresho katika mazingira ya kazi au kuboresha hadhi yao kijamii. Mgomo “kama aina ya tahadhari ya mwisho,[665] lazima ufanyike kwa njia ya usalama, nia ikiwa ni kueleza hitaji na kupigania haki ya mtu. Mgomo unakuwa haukubaliki kimaadili ikiwa utaandamana na vitendo vya kutumia nguvu, au malengo yake yanapokuwa hayahusiani moja kwa moja na hali ya kazi au kuwa kinyume na manufaa ya wote.[666]

 

VI. MSHIKAMANO WA WAFANYAKAZI

 

a. Umuhimu wa Kuungana

305. Majisterio wanatambua wajibu msingi uliotimizwa na vyama vya Wafanyakazi, ambavyo kuundwa kwake kunahusiana na haki ya kujiunga pamoja au katika vyama ili kulinda na kutetea maslahi makubwa na muhimu ya walioajiriwa katika taaluma mbalimbali. Vyama “vimeundwa kutokana na mapambano ya wafanyakazi kwa jumla, lakini hasa wafanyakazi wa viwandani kutetea haki zao dhidi ya wamiliki wa rasilimali za uzalishaji.”[667] Mashirika haya, wakati wanaendelea kutimiza malengo yao maalumu, kufuatana na manufaa ya wote, wanaweza kuleta athari chanya katika utaratibu wa jamii na mshikamano, na kwa hivyo kuwa kitu kisichokwepeka kwa maisha ya jamii. Kuzitambua haki za wafanyakazi, limekuwa kila wakati jambo gumu kulitatua kwa sababu utambuzi huu unafanyika katika mchakato mgumu kueleweka kihistoria na kitaasisi. Na hata bado leo tatizo linabaki bila ufumbuzi kamili. Hii inasababisha kuunda mshikamano ulio sawa na wa kweli miongoni mwa wafanyakazi kwa ajili ya mapambano kuwa lazima kuliko ambavyo imewahi kutokea.

306. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii, yanafundisha kwamba mahusiano katika ulimwengu wa kazi lazima yawe ya kiushirikiano: Chuki na kujaribu kuondoa wengine ni mambo ambayo hayakubaliki kabisa.

Na hii ndivyo inavyopaswa kuwa kwa sababu katika mfumo wowote wa jamii “nguvukazi” na “mtaji” vyote kwa pamoja ni sharti viwepo ili uzalishaji uweze kufanyika. Kwa kuelewa hivi, mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii “hayachukulii ya kuwa kuungana kwa wafanyakazi na kuunda vyama ni kuonyesha muundo wa ‘tabaka’ wa jamii, lakini hii inawasaidia wafanyakazi kueleza mapambano ya tabaka ambayo ni jambo lisilokwepeka katika kuongoza maisha ya jamii.”[668] Kwa kueleza jambo hili vizuri, vyama ya wafanyakazi ni wakuzaji wa mapambano ya kutafuta haki za kijamii, na haki za wafanyakazi wa taaluma maalumu. Jitihada hizo za wafanyakazi kupambana kwa ajili ya haki yapasa zieleweke kuwa ni juhudi za kawaida kwa ‘ajili ya’ jambo zuri tu. na hivyo yasichukuliwe kama ni mapambano dhidi ya wengine.”[669] Vyama vya wafanyakazi, kwa kuwa kwanza kabisa ni vyombo vya mshikamano na haki, visitumie vibaya kama vyombo vya ugomvi na ushindani. Vilevile, kwa sababu ya lengo ambalo kwalo vimeundwa, ni lazima vishinde kishawishi cha kuamini kwamba wafanyakazi wote wanapaswa kuwa wanachama, ni lazima viwe na uwezo wa kujiwekea namna ya kujirekebisha au kujidhibiti vyenyewe na viwe na uwezo wa kutathmini matokeo katika manufaa kwa wote yatokanayo na maamuzi yao.[670]

307. Zaidi ya jukumu la kulinda na kuthibitisha vyama vya wafanyakazi, vina wajibu wa kutenda kama wawakilishi wanaofanya kwa ajili ya “mpangilio sahihi na unaofaa wa maisha au mambo ya uchumi” na kuelimisha dhamiri ya jamii ya wafanyakazi, hivyo kwamba watajisikia wana nafasi na wajibu muhimu kulingana na uwezo wao na vipaji vyao, katika jukumu zima la kufikia maendeleo ya kiuchumi na kijamii na katika kufikia manufaa na ustawi wa wote kidunia.[671] Vyama vya wafanyakazi na vinginevyo, vinapaswa kufanya kazi kwa ushirikiano na vyombo vingine na lazima vijali na kupendelea kushiriki katika usimamizi wa mambo ya umma. Vilevile wanao wajibu wa kuleta athari nzuri katika uwanja wa siasa, na hivyo kuifanya siasa iwe na ufahamu wa kutosha katika matatizo ya wafanyakazi na kuvisaidia vyama kufanya kazi hivyo kwamba haki za wafanyakazi zinaheshimiwa. Hata hivyo, vyama vya wafanyakazi havina sifa ya “vyama vya kisiasa” ambapo kuna kushindania madaraka, na pia havipaswi kulazimishwa kujiweka katika maamuzi ya vyama vya kisiasa na wala kuwa na uhusiano wa karibu mno navyo.” Vyama vya Wafanyakazi vikiingia hali hiyo vinapotea katika wajibu wake maalumu, ambao ni kuwapatia na kudumisha haki za wafanyakazi zilizo ndani ya manufaa kwa wote na kwa jamii nzima, na badala yake vinakuwa “chombo kinachotumika kwa malengo mengine.”[672]

b. Aina na Njia Mpya za Mshikamano

308. Muktadha wa kisasa wa kijamii - kiuchumi, wenye tabia ya mchakato wa haraka daima katika utandawazi wa mambo ya kiuchumi na kifedha, unalazimisha na kusukuma vyama vya wafanyakazi kushughulikia mambo yake kwa namna mpya. Leo vyama vya wafanyakazi vinapaswa kutenda kwa namna mpya na kwa kutumia njia mpya,[673] vikipanua pia wigo wa shughuli zake za mshikamano hivyo kwamba utetezi na ulinzi unaweza kufanyika sio tu katika makundi ya wafanyakazi yaliyokuwa yamezoeleka, lakini pia kwa wafanyakazi wasio “katika kiwango” au wale wa mkataba wa muda maalumu wa kazi, waajiriwa ambao kazi zao zinatishiwa na wafanyabiashara wanaoungana, jambo ambalo linatokea katika ongezeko la kudumu na la mara nyingi hata katika ngazi ya kimataifa. Vyama vya wafanyakazi leo vinapaswa pia kushirikisha wale wasio na kazi, wahamiaji, wafanyakazi wa misimu, na wale ambao kwa sababu hawajaifanya taaluma yao iwe ya kisasa wametupwa nje ya soko la kazi na hawawezi kupokelewa tena kazini bila kupata mafunzo sahihi upya.

Kwa kuangalia mabadiliko ambayo yametokea katika ulimwengu wa kazi, mshikamano unaweza kujengwa upya na pengine uwe na msingi imara zaidi ikilinganishwa na wakati uliopita. Na hii itafanyika ikiwa jitihada zitafanyika kugundua upya thamani ya ubinadamu katika kazi.” Hapa ni lazima kuwe na mwendelezo katika kujifunza lengo la kazi na hali ambamo ndimo watu wanaishi.” Kwa sababu hii “kuna haja ya kuwa na misukumo mipya ya mshikamano wa wafanyakazi na pamoja na wafanyakazi na hiyo iwe ni ya kudumu.”[674]

309. Kufaulu kupata “aina mpya za mshikamano[675] miungano ya wafanyakazi lazima ilenge jitihada zake katika kukubali na kupokea uwajibikaji mkubwa zaidi, na sio tu katika uhusiano na uendeshaji wa kizamani katika usambazaji mpya, lakini pia katika uhusiano na uzalishaji wa mali na kutengeneza hali za kijamii, kisiasa na kiutamaduni ambazo zitaruhusu wote walio na uwezo na hiari ya kufanya kazi watekeleze au watimize haki yao ya kufanya kazi wakiwa wanaheshimika kikamilifu katika utu wao kama wafanyakazi. Hali inayoendelea kupitwa na wakati kwa vigezo vya uundwaji wa mtindo ambao msingi wake ulikuwa ni wafanyakazi wa mshahara katika biashara kubwa inaleta sababu ya kutengeneza upya kanuni na mifumo ya usalama wa jamii ambayo hapo zamani iliwalinda wafanyakazi na kuwahakikishia haki zao za msingi.

 

VII. “MAMBO MAPYA” KATIKA ULIMWENGU WA KAZI

 

a. Kuweka Kipindi Kipya cha Mpito Katika Historia

310. Hali ya utandawazi ni moja ya vyanzo muhimu vya mabadiliko makubwa yanayoendelea katika mfumo wa kazi. Hali hii imeleta njia mpya za uzalishaji ambapo viwanda vinajengwa mbali na mahali mikakati ya uzalishaji inapoamuliwa na pia mbali na masoko ambapo ndipo walipo watumiaji na walaji wa bidhaa. Yapo mambo mawili yanayosababisha hali hii: kasi ya ukuaji usio wa kawaida katika mawasiliano ambayo sasa haiwekewi mipaka na umbali wa mahali ama muda.  Ya pili ni urahisi wa kusafirisha watu na kusafirisha bidhaa kutoka sehemu moja ya dunia hadi nyingine. Hii inaleta matokeo ya msingi kwa ajili mchakato wa uzalishaji kwa kuwa bidhaa zinakaa mbali zaidi na hakuna kuangalia athari za kijamii zinazotokana na uamuzi uliofikiwa. Kwa upande mwingine, ikiwa ni kweli kwamba utandawazi wenyewe sio mzuri wala mbaya, bali inategemea namna unavyotumika,[676] ni lazima kukazia kwamba utandawazi wa kulinda haki za watu zilizo muhimu sana na usawa ni lazima.

311. Moja ya sifa muhimu ya mfumo mpya wa kazi ni mgawanyiko wa majukumu ya uzalishaji, ambao unakuzwa ili kupata ufanisi na faida zaidi. Katika mtazamo huu, uratibu uliokuwepo wa mahali na muda ambamo ndimo mzunguko wa uzalishaji wa awali ulivyokuwa unafanyika, sasa uko katika mabadiliko ambayo hayajawahi kutokea ambayo ndiyo yanayoongoza mabadiliko katika mfumo na muundo wa kazi yenyewe. Mambo haya yote yanaleta matokeo ambayo ni muhimu katika maisha ya mtu mmojammoja na ya jamii ambayo yanaingia katika mabadiliko makubwa kuhusiana na mali na katika utamaduni na tunu. Hali ya utandawazi kwa sasa inawahusu mamilioni ya watu bila kujali taaluma zao, hadhi zao kijamii au maandalizi kiutamaduni katika ngazi ya kidunia na ngazi za chini. Mpangilio wa muda, kuuwekea viwango na mabadiliko yanayotokea sasa katika kutumia sehemu au mahali ikilinganishwa na kiwango kilichokuwepo wakati wa Mapinduzi ya Viwanda kwa kuwa yanahusu kila sekta ya uzalishaji, katika mabara yote bila kujali kiwango cha maendeleo yao. Kwa hiyo, mambo haya yapasa yachukuliwe kama ni changamoto kubwa pia katika mambo ya kimaadili na kiutamaduni katika maeneo ya kuelezea mifumo mipya iliyopo kwa ajili ya kulinda haki ya kazi.

312. Utandawazi wa uchumi, pamoja na soko huria, kuongezeka kwa ushindani, kuongezeka kwa biashara maalumu katika kuwafikishia watu bidhaa na huduma, haya yanahitaji hali yenye tabia ya kubadilikabadilika zaidi ya soko la kazi na katika kupangilia na kusimamia hatua zinazotumika katika uzalishaji. Kuweza kutathmini suala hili nyeti, inaonekana ni sahihi kuwa makini katika maadili, utamaduni na mipango ili kuweza kuongoza shughuli ya kijamii na kisiasa kuhusiana na masuala yanayohusiana na utambulisho na yaliyomo katika kazi mpya, katika soko na uchumi ambavyo vyenyewe pia ni vipya. Kwa kweli mabadiliko katika soko la kazi kila mara ni kutokana na athari za mabadiliko ambamo na kazi imo, lakini mabadiliko hayo hayasababishwi na kazi yenyewe.

313. Zaidi ya yote, ndani ya mfumo wa uchumi wa nchi zilizoendelea zaidi, kazi inapitia awamu ya kipindi ambacho kinaweka alama ya mpito kutoka uchumi wa kiviwanda kwenda katika uchumi ambao hasa msingi wake ni huduma na ugunduzi wa kiteknolojia. Kwa maneno mengine, kinachotokea ni kwamba huduma na shughuli pamoja na maudhui ya habari ambayo yamedumu sasa inaonesha ukuaji katika kasi kubwa zaidi kuliko ilivyokuwa katika sekta ya uzalishaji bidhaa za msingi na za kati. Hii inaleta mlolongo wa matokeo kwa ajili ya mpangilio wa uzalishaji na ubadilishanaji bidhaa, ikieleza hitaji la kazi na kuweka njia zifaazo za ulinzi wa jamii.

Ni jambo la kushukuru ugunduzi wa kiteknolojia ambao ulimwengu wa kazi umenufaika na taaluma mpya wakati taaluma nyingine zimepotea. Kwa kweli, kwa wakati huu wa mpito, kuna hali inayoendelea ya wafanyakazi kuhama kutoka katika sekta ya viwanda kwenda sekta ya huduma. Kwa kuwa mfumo wa kiuchumi na kijamii inayohusiana na viwanda vikubwa na tabaka la wafanyakazi wa kufanana kote wanakosa mahali pao, matazamio ya ajira katika sekta ya tatu yanaboreka. Hasa kuna ongezeko katika shughuli za kazi katika eneo la huduma itolewayo na watu katika mtindo wa kazi ya muda wa saa, muda mfupi (isiyo ya kudumu) na ajira “isiyo ya kizamani.” Hii inamaanisha kazi ambayo haistahili kuwekwa katika kundi ambalo ingepasa kumweka mwenye kazi kama mwajiriwa au aliyejiajiri mwenyewe.

314. Mpito ambao unaendelea unaonesha mabadiliko ya kazi na kuiondoa katika mtindo wa kuwa kazi ya kumtegemea mwingine bila kikomo cha muda, ikieleweka kama kazi ya kuaminikana kuelekea katika aina ya kazi yenye sifa ya kubadilisha shughuli. Hii inaonekana katika ulimwengu ulio mmoja, unaoeleweka na dhana inayotambuliwa ya kazi kwa dunia nzima ambapo kuna aina nyingi na mbalimbali za kazi, kazi inayoweza kubadilishika kwa urahisi na yenye matarajio ya utajiri. Bado kuna maswali mengi ya kuangalia, hasa kuhusiana na ongezeko la kukosa uhakika wa kazi, kudumu kuwepo kwa ukosefu wa ajira ulio kimuundo na mifumo isiyotosheleza hitaji la mifumo na hifadhi au usalama wa jamii ya sasa. Hitaji la ushindani, ugunduzi wa kiteknolojia na ugumu wa kuelewa mtiririko wa fedha, lazima haya yawekwe katika hali inayofanya mambo haya yakubaliane na suala la kulinda wafanyakazi na haki zao.

Hali hii isiyo na uhakika na uimara inahusu sio tu hali ya kazi ya wafanyakazi katika nchi zilizoendelea zaidi, lakini inaathiri pia, na zaidi ya yote, hali halisi za uchumi duni katika nchi zinazoendelea na nchi zilizo na uchumi ulio katika mpito. Kundi hili la mwisho, licha ya kuwa na matatizo magumu kueleweka yakiunganishwa na mabadiliko ya muundo wa uchumi na uzalishaji, lazima yashughulikie kila siku marekebisho magumu, yanayohitajika katika hali hii ya sasa ya utandawazi. Hali ilivyo ni kama hasa ngumu zaidi kwa ulimwengu wa kazi, huku ikiathiriwa na mambo makubwa ya kiutamaduni na mabadiliko makubwa katika maudhui ambayo mara nyingi hayaungwi mkono na sheria na kukosekana programu za mafunzo ya kitaaluma na msaada kijamii.

315. Uzalishaji usiowekwa sehemu moja ambapo kampuni ndogo zinapewa kazi au majukumu ambayo awali yalikuwa yanafanywa na uzalishaji mkubwa, inaipa umuhimu na nguvu kubwa biashara ndogo na za kati. Kwa njia hii pamoja na sanaa ya jadi, kukaanza biashara mpya iliyo na sifa ya uzalishaji mdogo katika sekta mpya ya uzalishaji au shughuli zinazosambazwa za makampuni makubwa. Shughuli nyingi ambazo siku zilizopita zilihitaji kukodisha waajiriwa, leo zinatumia njia mpya ambazo zinasukuma kazi ya kujitegemea, na kwa hiyo, zina hatari kubwa na uwajibikaji mkubwa.

Kazi katika biashara ndogo na za kati, kazi ya sanaa na ya kujitegemea zinaweza kuwakilisha tukio la kufanya uzoefu wa kazi halisi uwe wa kiutu zaidi, katika uwezekano wa kujenga mahusiano mazuri zaidi katika jumuiya zilizo na watu wachache na hivyo kuepuka kutotendewa haki kwa kupokea ujira mdogo na zaidi ya yote kukosa uhakika wa kazi.

316. Katika nchi zinazoendelea, na zaidi katika miaka ya hivi karibuni, kumekuwa na hali ya kupanuka kwa shughuli za uchumi zisizo rasmi na “zisizo wazi,” hii inaonesha alama ya matarajio mazuri ya kukua kwa uchumi na maendeleo. Lakini hii inaleta matatizo mengi ya kimaadili na kisheria. Kwa kweli ongezeko muhimu la fursa za kazi katika muktadha wa shughuli hizo unaleta ukosefu wa kazi katika taaluma maalumu na sehemu kubwa ya wafanyakazi wa sehemu moja na vilevile katika ukuaji usio katika utaratibu wa sekta rasmi ya uchumi. Hivyo idadi kubwa ya watu wanalazimika kufanya kazi katika hali ya shinikizo isiyo na utaratibu muhimu unaowezesha heshima ya wafanyakazi kulindwa. Viwango vya tija, mapato na kiwango cha kuishi ziko chini mno na kila mara hazitoshelezi kuwahakikishia wafanyakazi na familia zao kiwango cha chini cha kuwawezesha kuishi.

b. Mafundisho ya Jamii “na Mambo” Mapya

317. Baada ya kupata “mambo mapya” ya kuvutia katika ulimwengu wa kazi, mafundisho ya Kanisa yanapendekeza kwanza ya yote kuepuka makosa ya kusisitiza na kukubali kwamba mabadiliko ya sasa yanatokea katika namna iliyodhamiriwa. Kigezo cha uamuzi na mwamuzi wa kipindi hiki kigumu kueleweka cha mabadiliko bado ni mtu ambaye lazima abakie mhusika mkuu wa kazi yake. Mtu anaweza na lazima aendelee katika mtindo wa ubunifu na uwajibikaji ambao unaonesha ugunduzi na mifumo mipya, hivyo kwamba inaongoza katika ukuaji wa mtu, familia yake, jamii na familia nzima ya wanadamu.[677] Mwanga wa haya yote unaweza kupatikana katika mwito wa kusisitiza upande wa dhana ya kazi, ambao kulingana na mafundisho ya Kanisa, ni lazima upewe kipaumbele kwa sababu kazi ya mwanadamu inaendeleza moja kwa moja watu kwa kuwa wameumbwa katika sura na mfano wa Mungu na kuitwa kuendeleza kazi ya uumbaji na kuitiisha dunia.”[678]

318. Kuelewa kazi ya uzalishaji kwa namna ya teknolojia na ya kiuchumi licha ya kuwa muhimu sasa umeshapitwa na wakati kwa sababu ya uchambuzi wa kisayansi wa matatizo yanayohusiana na kazi leo. Zaidi leo kuliko siku zilizopita, namna hii ya kuelewa inaonekana kutosheleza kabisa katika kutafsiri yakinifu ambazo kila siku zinaonesha zaidi na zaidi maana ya kazi kama shughuli huru na ya ubunifu ya mwanadamu. Mambo dhahiri inapasa yawe kichocheo kwa ajili ya kuandaa haraka mitazamo ya kinadharia na inayowekea mipaka vigezo vya utendaji usiotosheleza katika nyakati za leo zenye kubadilikabadilika. Na hii inathibitisha kukosa uwezo kiasili katika kutambua kiukamilifu mahitaji maalumu, halisi na ya haraka ya mwanadamu ambayo yanakuwa na uzito zaidi, na hivyo hayawezi kuwekwa katika kundi moja na mahitaji ya kiuchumi. Kanisa linaelewa vema jambo hili na ndio maana kila wakati limekuwa likifundisha watu wanaume kwa wanawake ya kwamba wao ni tofauti na viumbe wengine, wanadamu wana mahitaji ambayo hayawezi kuwekwa katika hali ya “kuwa na” tu[679] kwa sababu asili yao na wito wao hauna uhusiano wa kutochanganyishika na ule wa kurithishana unaovuka mipaka ya upeo wa ufahamu wa mwanadamu, wa Kimungu. Mwanadamu anakabiliana na tukio lisilo la kawaida la mabadiliko ya mambo kwa njia ya kazi ili kumwezesha kujitosheleza mahitaji ambayo kwanza kabisa ni mahitaji ya vitu. Lakini mwanadamu anafanya hivyo kwa kutii hamu inayomsukuma daima kupata zaidi ya kile ambacho amekwisha pata. Na hii ni kutaka kufikia yale yatakayolingana mno na mahitaji yake muhimu mno ya ndani.

319. Mtindo wa kihistoria ambao hutumika kupima au kueleza kazi ya mwanadamu unabadilika, lakini mahitaji yake ya kudumu hayabadiliki. Mahitaji haya yanaweza kujumuishwa pamoja kuhusiana na haki ya wafanyakazi isiyokwepeka. Kwa kukubaliana na hatari ya kukiukwa haki hizi, aina mpya za mshikamano ziwekewe dira za kufikiwa kwa kuzingatia mahusiano ambayo yanaunganisha wafanyakazi miongoni mwao wenyewe kwa wenyewe. Mabadiliko yanayozidi kuwa makubwa hali kadhalika maamuzi ya uwajibikaji wa kiakili na kiuchumi katika kulinda heshima ya kazi yanahitajika ili kuimarisha katika ngazi mbalimbali muundo unaohitajika. Mtazamo huu unawezesha kuelekeza mabadiliko ya sasa yawe kwa ajili ya uzuri zaidi na zaidi, na katika mwelekeo ambao ni wa lazima wa kukamilishana kati ya upande wa uchumi mahalia na uchumi wa kidunia. Haya ni katika kuangalia yale ya “zamani” na “mapya” katika uchumi, ugunduzi wa kiteknolojia na hitaji la kulinda kazi ya mwanadamu na vilevile ukuaji wa uchumi na maendeleo yanayojali kikamilifu masuala ya mazingira.

320. Ni wito kwa watu wote – wanaume kwa wanawake wa sayansi na utamaduni kuchangia katika utatuzi wa matatizo makubwa mno na yenye ugumu katika kueleweka yanayohusiana na kazi. Katika maeneo mengine matatizo haya yanachukua sehemu kubwa. Kwa hiyo, mchango huo ni wa muhimu mno katika kufikia ufumbuzi sahihi. Jukumu hili ambalo linahitaji kutambua matukio na hatari zilizopo katika mabadiliko yanayoendelea kutokea, na zaidi ya yote, wapendekeze njia za utekelezaji katika kuongoza mabadiliko ili yawe mabadiliko ambayo yanasaidia zaidi na zaidi maendeleo ya familia nzima ya watu. Katika jitihada hizi unakuja umuhimu wa kujua kusoma na kutafsiri ili kuelewa hali ya kijamii kwa kutumia hekima na kupenda ukweli na kuacha kujali mambo yanayoletwa na mapendeleo maalumu au ya mtu binafsi. Kwa sababu hasa mchango wao una asili ya kinadharia, unakuwa ndipo mahali muhimu mno pa marejeo kwa ajili ya utekelezaji halisi na maalumu unaooneshwa na sera za kiuchumi.[680]

321. Mpangilio wa sasa wa mabadiliko makubwa katika kazi ya mwanadamu unatoa wito hata kwa uharaka zaidi kwa ajili ya maendeleo ya kweli duniani, ya mshikamano ambao una uwezo wa kuhusisha kila upande duniani wakiwemo wale waliowekwa pembeni zaidi na hivyo kutonufaika vya kutosha. Kuhusiana na maeneo haya yasiyonufaika kuanza mchakato wa kupata aina nyingi za maendeleo katika mshikamano ambao sio tu unawakilisha uwezekano wa kuongeza fursa za kazi bali pia inachukuliwa kama ni hali kweli inayohitajika kwa ajili ya watu wote kumudu kuishi. “Hivyo mshikamano nao pia lazima uwe ni wa kiutandawazi.”[681]

Kukosekana uwiano kati ya mambo ya kiuchumi na kijamii katika ulimwengu wa kazi, ni lazima jambo hili lishughulikiwe kwa kuweka hiarikia ya haki ya tunu, na kuuweka utu wa mwanadamu mfanyakazi kuwa kitu cha kwanza kuliko mengine yote. “Hali halisi mpya ambazo zina uwezo huo unaoweza kuleta matokeo ya mshindo wenye nguvu katika mchakato wa uzalishaji, kama vile kufanya masuala mbalimbali yawe ya kiutandawazi kama ya fedha, uchumi, biashara, kazi. Na haya kamwe yasiwe yanakiuka utu na ukitovu wa mtu mwanadamu, wala uhuru na demokrasia ya watu. Ikiwa mshikamano, ushiriki na uwezekano wa kutawala mabadiliko haya makubwa sio ufumbuzi, basi ni wazi hili, ni jambo la lazima kuhakikisha maadili kwamba watu binafsi na watu kwa jumla hawawi vyombo, bali wanakuwa ndio wahusika wakuu katika kuongoza siku zijazo. Kwa kuwa yote haya yanawezekana kufikiwa, basi hili linakuwa ni jukumu la kufanyia kazi.”[682]

322. Daima lipo hitaji ambalo ni kubwa la kuzingatia, hali mpya ya kazi katika muktadha wa zama hizi za utandawazi, kwa mtazamo ambao unathamini hali asili ya mwanadamu katika kuweka mahusiano. Kwa hiyo lazima kukazia kwanza kwamba dunia kwa jumla ni mambo ya kibinadamu na sio ya vitu. Teknolojia inaweza kuwa chombo cha kusababisha utandawazi, lakini dunia kwa jumla na katika familia ya wanadamu ndicho chanzo kikuu. Kwa sababu hii, kazi pia ina upande wa dunia kwa jumla kwa kuwa msingi wa kazi ni mahusiano ya asili ya wanadamu. Teknolojia hasa ya elektroniki, imeruhusu mambo ya mahusiano ya kazi kuenea kote duniani na kuupa utandawazi ukuaji wa kasi. Hatima yake, msingi wa mabadiliko ni watu wanaofanya kazi ambao kila mara wao ni watendaji na si vyombo. Kwa hiyo, utandawazi katika kazi pia unatoka katika msingi wa elimu ya mwanadamu katika upande wa uhusiano wa kurithi kazi. Upande ulio hasi wa utandawazi kuhusu kazi lazima usiangamize wala usiharibu uwezekano wa kuwa wazi kwa ajili ya watu wote: ambao ni kuelezea utu wa kazi katika kiwango cha dunia katika mshikamano ndani ya ulimwengu wa kazi katika kiwango hichohicho, hivyo kwamba kufanya kazi katika muktadha wa kufanana, kunaenea duniani kote na kuwahusianisha watu. Na hapo watu watauelewa vema wito wao mmoja ambao wanaoushiriki wote.

 

SURA YA SABA

MAMBO YA KIUCHUMI

I. MTAZAMO WA KIBIBLIA

 

a. Mtu, Umaskini na Utajiri

323. Katika Agano la Kale mitazamo miwili inajidhihirisha mintarafu bidhaa na mali. Kwa upande mmoja, mwelekeo wa kutambua vema kuwa matunda ya kiuchumi ni muhimu kwa maisha. Kuwepo kwake tele - sio utajiri au anasa - mara kwa mara kunaonekana kwamba ni baraka kutoka kwa Mungu. Katika mtazamo wa Hekima, umaskini unaelezwa kuwa ni matokeo mabaya ya uvivu na ukosefu wa jitihada (taz. Mit 10: 4), lakini pia ni ukweli kimaumbile (taz. Mit 22: 2). Kwa upande mwingine vitufaa na utajiri havikulaaniwa isipokuwa katika matumizi yake mabaya. Mapokeo ya kinabii yanalaani vitendo vya udanganyifu, kukopesha fedha kwa riba, unyonyaji na udhalimu dhahiri, hasa vikitendwa dhidi ya walio maskini (taz. Isa 58: 3 -11; Yer 7: 4 - 7; Hos 4: 1 - 2; Amo 2: 6 - 7; Mik 2:1-2). Mapokeo haya, lakini, ingawaje huuona umaskini wa wale wanaokandamizwa, wanyonge na fukara kuwa ni uovu, aidha huona katika hali ya umaskini ishara ya hali halisi ya binadamu mbele ya Mungu, aliye chimbuko na mwanzo wa kila jema likiwa ni tunu ipasayo kusimamiwa vema na kugawiwa kwa haki.

324. Wale wanaotambua hali yao ya upungufu mbele ya Mungu, pasipokutilia maanani hali yao kimaisha, Yeye huwaangalia kwa makini sana: maskini atafutapo, Bwana humjibu; alalamapo, Bwana humsikiliza. Ahadi za kimungu wamepewa maskini: watakuwa warithi wa Agano kati ya Mungu na watu wake. Wokovu wa mwanadamu kutoka kwa Mungu utakuja kwa njia ya Daudi mpya (taz. Eze 34: 22 – 31), ambaye kama alivyo Mfalme Daudi – Yeye akiwa mkuu zaidi atakuwa mtetezi wa maskini na mdhamini wa haki; atafanya Agano jipya na ataandika sheria mpya katika mioyo ya waamini (taz. Yer 31: 31 – 34).

Umaskini ukitafutwa au kupokewa kwa njia ya imani, humwezesha yule autafutaye kutambua na kukubali mpango wa uumbaji. Kwa taswira hii, “tajiri” ni yule anayeweka tegemeo lake katika mali zake badala ya kumtegemea Mungu, ni yule anayejiimarisha kwa kazi za mikono yake na kutegemea nguvu zake pekee. Umaskini huchukua hadhi ya maadili pale unapokuwa na mwelekeo ulio radhi na nyenyekevu ukijiweka wazi kwa Mungu, ukimtegemea yeye. Mwelekeo huu huwawezesha watu kutambua uwiano wa jitihada na mazao ya shughuli za kiuchumi na hivyo kuviona kama tunu za kimungu zinazopaswa kusimamiwa vema na kugawiwa kwa haki, kwa sababu Mungu ndiye mmiliki wa kwanza wa mema yote.

325. Yesu anakubaliana kwa dhati kabisa na mapokeo ya Agano la Kale yakiwemo pia yahusuyo vitufaa, utajiri na umaskini, na yeye anatoa ufafanuzi mkuu na mkamilifu (taz. Mt. 6: 24, 13: 22; Lk 6: 20 – 24; 12: 15 – 21; Rum. 14: 6 – 8; 1 Tim 4: 4). Kwa njia ya kipaji cha Roho wake na kwa uongofu wa nyoyo, anakuja kuanzisha “Ufalme wa Mungu”, ili mahusiano mapya ya kijamii yawezekane, katika haki, udugu, mshikamano na ushirikishanaji. Ufalme uliosimikwa na Kristo unatimiliza ule wema asili katika mpango wa uumbaji na uzuri wa jitihada za binadamu, ambavyo vilipotezwa kwa dhambi. Binadamu akiwa amewekwa huru kutoka uovu na kuwekwa tena katika ushirika na Mungu, anaweza kuendelea na kazi ya Yesu, kwa msaada wa Roho wake. Katika hili, mwanadamu anatakiwa kutenda haki kwa maskini, kuwafungulia waliokandamizwa, kuwatuliza wanaoteswa. Hapo anashiriki katika kujenga mfumo mpya wa kijamii ambamo ufumbuzi wa kutosha wa matatizo ya umaskini wa vitu unapatikana na ambamo masharti yanayopinga jitihada za wanyonge kujikomboa katika mateso na utumwa yanadhibitiwa kwa ufanisi. Hali hii ikiwepo, Ufalme wa Mungu tayari unakuwapo hapa duniani, ingawaje si wa kidunia. Ni katika Ufalme huu ambamo ahadi za Manabii zinapata ukamilisho wa mwisho.

326. Katika mwanga wa ufunuo, jitihada za kiuchumi zizingatiwe, na kutendwa kwa mwitikio uliosheheni shukrani kwa wito wake Mungu anaomjalia kila mtu.
Mtu amewekwa katika bustani apate kuilima na kuitunza, akiitumia kwa kufuata viwango na kiasi kilichowekwa (taz. Mwa 2: 16 – 17) na akiwa na sharti la kuiboresha (taz. Mwa 1: 26 – 30; 2: 15 – 16; Hek 9: 2 – 3). Akitoa ushuhuda wa utukufu na wema wake Muumba, anasonga mbele kuelekea kule kwenye ukamilifu wa uhuru ambako Mungu anamwita. Utawala mzuri wa vipaji alivyopewa pamoja na mali ni kujitendea haki mwenyewe na wengine pia. Kila kitu alichojaliwa mwanadamu sharti kitumiwe istahilivyo, kihifadhiwe na kiongezwe kwa kadiri inavyopendekezwa na mfano wa talanta (taz. Mt. 25: 14 – 30; Lk. 19: 12 – 27).

Jitihada za kiuchumi na maendeleo katika vitufaa lazima vielekezwe katika kumhudumia mtu na jamii. Laiti watu wangejitolea kutenda haya kwa imani, matumaini na mapendo kama ya wale wafuasi wa Kristo, hata uchumi na maendeleo vingegeuzwa kuwa mahali pa wokovu na utakatifuzaji. Katika nyanja hizo inawezekana pia kudhihirisha upendo na mshikamano unaozidi ule wa kiutu, na kuchangia kukua kwa utu mpya unaotarajiwa katika ulimwengu ujao.[683] Ufunuo wote Yesu anaujumlisha katika maneno machache kwa kumwalika mwamini kuwa tajiri mbele ya Mungu (taz. Lk 12: 21). Kwa madhumuni hayo, uchumi nao una nafasi yake, iwapo tu kutumika kwake kama nyenzo ya kupatikana maendeleo ya mwanadamu na jamii, hali bora ya maisha ya watu, havitasalitiwa.

327. Imani katika Yesu Kristo inawezesha kuwa na uelewa sahihi wa maendeleo ya jamii katika muktadha wa ukamilifu na uthabiti wa ubinadamu. Kuhusu suala hili, mchango wa tafakari ya kitheolojia unaotolewa na Majisterio juu ya mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii ni wa manufaa sana: “Imani katika Kristo Mkombozi, huku ikiwa inatuangazia kutokana na uhalisia wa maendeleo yenyewe, inatuongoza pia katika wajibu wa kushiriki. Katika Waraka wa Mt. Paulo kwa Wakolosai, tunasoma kwamba Kristo ni ‘mzaliwa wa kwanza wa vyote vilivyoumbwa,’ na kwamba ‘vitu vyote viliumbwa katika yeye’ na kwa ajili yake (Kol 1: 15 – 16). Kwa kweli, ‘vitu vyote vinaungana katika yeye’, kwa kuwa ‘katika yeye ilipendeza utimilifu wote wa Mungu ukae, na kwa yeye kuvipatanisha vitu vyote na nafsi yake’ (v. 20). Sehemu ya mpango huu wa Mungu, ambao huanzia umilele yote katika Kristo, aliye ‘sura’ kamilifu ya Baba, na unaofikia kilele chake katika yeye, ‘mzaliwa wa kwanza kutoka katika wafu’ (v. 15 – 18), katika historia yetu wenyewe, unadhihirishwa na juhudi zetu binafsi na za pamoja za kuboresha hali ya maisha ya binadamu na kuvishinda vikwazo vinavyoendelea kujitokeza katika safari yetu. Imani hii hutuandaa kushiriki utimilifu ule ‘ukaao katika Bwana’ na ambao huushirikisha ‘mwili wake, ambao ni Kanisa’ (v. 18; taz. Efe 1: 22 – 23). Kwa wakati huohuo dhambi, ambayo kwa nyakati zote hujaribu kutunasa na kuhatarisha mafanikio yetu, inashindwa na kukombolewa kwa ‘upatanisho’ uliofanywa na Kristo (taz. Kol 1: 20).”[684]

b. Mali Huwapo ili Igawiwe

328. Mali, hata iliyopatikana kwa njia halali, siku zote imekusudiwa kwa watu wote; ulimbikizaji wowote usiofaa wa mali ni ufisadi, kwa sababu unapingana dhahiri na makusudio ya Muumba. Wokovu wa Kikristo ni ukombozi kamilifu wa binadamu, ikimaanisha kuwa uhuru si tu kutokana na dhiki, lakini vilevile katika umilikaji mali. “Kwa kuwa kupenda fedha ni mzizi wa maovu yote; ni kutokana na uchu huu wengine wamefarakana na imani” (1 Tim 6: 10). Mababa wa Kanisa wanasisitiza zaidi juu ya ulazima wa uongofu na mabadiliko ya dhamiri za waamini kuliko ulazima wa mabadiliko ya miundo ya kijamii na kisiasa ya wakati uliopo. Wanawaalika wote wanaofanya kazi ya kushughulikia mambo ya uchumi na wamiliki wa mali kujiona wao wenyewe kama wasimamizi na waendelezaji wa mema yote aliyowakabidhi na kuwaaminisha Mungu.

329. Utajiri hukamilisha wajibu wake wa kumhudumia mtu pale tu unapolengwa kuwanufaisha wengine na jamii.[685] “Tunawezaje kumtendea mema jirani yetu, anauliza Mt. Klementi wa Alexandria, “iwapo miongoni mwetu hayupo aliye na chochote?”[686] Kwa taswira ya Mt. Yohane Krisostomo, utajiri huwa mikononi mwa watu fulani tu ili wajipatie mastahili kwa kugawana mali zao na wengine.[687] Mali ni wema utokao kwa Mungu na inapaswa kutumiwa na mmilikaji pia kuisambaza kwa madhumuni ya kuwanufaisha hata wale walio katika dhiki. Uovu unaonekana katika kushikamana na mali kusiko na kiasi na tamaa ya kuhodhi. Mt Basili Mkuu anawaalika matajiri kufungua milango ya maghala yao na kuwashawishi akisema: “Mbubujiko mkubwa waja, katika mikondo elfu kwa maelfu, kupitia katika ardhi iliyojaa rutuba: na hivyo, kwa njia elfu mbalimbali hakikisheni utajiri wenu unazifikia nyumba za maskini.”[688] Mali, anafafanua Mt. Basili, ni kama maji yabubujikayo kutoka katika, chemchemi: kwa kadiri yatakavyochotwa kwa wingi, ndivyo yatakavyokuwa safi zaidi, lakini chemchemi ikibaki bila kutumika maji yake hunuka.[689] Tajiri Mt. Gregori Mkuu atasema hapo baadaye - ni msimamizi tu wa mali anayomiliki; kuwapa wahitaji kinachotakiwa ni kazi inayopaswa kufanywa kwa unyenyekevu kwa sababu mali husika si za huyo anayezigawa. Yeyote anayehodhi mali kwa ajili yake tu si mtu asiye na hatia; kuwapa fadhila walio katika dhiki ni kulipa deni.[690]

 

II. UADILIFU NA UCHUMI

 

330. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanasisitiza umuhimu wa uadilifu katika nyanja za uchumi. Papa Pius XI, katika kifungu kimojawapo cha waraka wake Quadragesimo Anno, anazungumzia juu ya uhusiano uliopo kati ya uchumi na uadilifu. Ingawaje taaluma ya uchumi na sayansi ya maadili kila moja hutumia misingi tofauti katika nyanja zake, ni kosa, hata hivyo, kusema kwamba taratibu za uchumi na zile zihusuzo maadili ni tofauti kabisa na zina utengano usiotegemeana. Dhahiri sheria za uchumi, kama zinavyoitwa, zikiwa zinatokana na hulka ya vitufaa na katika uwezo wa mwili na akili ya mwanadamu, hubainisha ukomo wa tija ya mtu, na kiasi kinachoweza kufikiwa katika uzalishaji kwa kutumia nyenzo sawia. Lakini ni fikra yenyewe ndio hudhihirisha, ikizingatia hulka ya kijamii iliyomo katika kila kitu na watu, makusudio ambayo Mungu aliazimia katika shughuli za kiuchumi. Hata hivyo, ni sheria ya kimaadili tu ambayo kama vile inavyotuagiza kutafuta kilicho bora kwetu, na ukomo wetu katika mpango wote wa shughuli zetu, hutuamuru pia kutafuta moja kwa moja katika jitihada zetu yale makusudio tunayojua kwamba maumbile, au tuseme Mungu aliye Asili ya maumbile, aliyaweka katika hali husika, na katika mahusiano yaliyo katika utaratibu ili kuziweka azma za wakati huu chini ya kilicho bora kwetu na ukomo wetu.[691]

331. Uhusiano baina ya Uadilifu na Uchumi ni wa lazima, kwa kweli ni wa asili: Shughuli za kiuchumi na mienendo adilifu vimeunganika kwa undani sana. Tofauti ya lazima baina ya uadilifu na uchumi si kutenganisha fani hizi mbili bali, kinyume chake ni kuziweka katika hali ya kutegemeana kuliko muhimu. Kama ilivyo lazima kuhusisha mantiki na masharti ya kiuchumi katika masuala ya uadilifu, vivyo hivyo lazima kuwa radhi kwa madai ya uadilifu katika fani ya uchumi: “Pia, katika nyanja za uchumi na jamii, hadhi na wito kamili wa mtu nafsi na maslahi ya jamii kwa jumla ni lazima kuyaheshimu na kuyaenzi. Kwa kuwa mtu ni chanzo, kiini, na kusudio la maisha ya kiuchumi na kijamii.”[692] Kuyapa masuala yahusuyo uchumi umuhimu na uzito ufaao, hakumaanishi kukana na kuona kuwa hakuna mantiki katika dhana yote ya utengamano wa kiuchumi. Ieleweke kwamba kusudio la uchumi halipatikani katika uchumi wenyewe, bali uchumi unapolengwa kwa ubinadamu na kwa jamii.[693] Uchumi, kwa kweli, katika ngazi ya kisayansi au katika hali ya utendaji wa kawaida haujaaminishiwa kusudio la kumkamilisha mtu au kumletea maisha ya pamoja yaliyo ya kibinadamu. Jukumu la uchumi bado si kamili: ni uzalishaji, usambazaji na utumiaji wa vitufaa na huduma mbalimbali.

332. Mtazamo adilifu katika maisha ya kiuchumi unaonyesha kwamba uchumi fanisi na jitihada za maendeleo ya watu vikihimizwa kwa pamoja si malengo mawili tofauti au mbadala, bali ni ukomo mmoja usio na utengano. Uadilifu, kitu kilicho lazima katika shughuli za kiuchumi, haupingani wala si kusema hauna sifa zinazobainika kuhusiana na uchumi: ikiwa umevuviwa na haki pamoja na mshikamano, unawakilisha kipengele cha jamii fanisi iliyomo katika uchumi husika. Uzalishaji wa bidhaa unapaswa kuendeshwa kwa ufanisi, vinginevyo ni uharibifu wa rasilimali. Kwa upande mwingine, haitokubalika kufanikiwa kufikia hatua ya kukua kwa uchumi kwa gharama ya watu, huku jamii nzima au makundi ya jamii, wakitoswa kuishi katika ufukara. Kuongezeka kwa mali, kunakoonekana katika wingi wa bidhaa na huduma, na madai ya kimaadili yanayotaka mgawanyo wa haki ni lazima vichochee mtu na jamii yote kuishi kwa kadiri ya tunu ya mshikamano,[694] Hiyo ni kwa madhumuni ya kupambana, katika fikra ya haki na upendo, dhidi ya “miundo ya kidhambi”[695] kokote inakopatikana na ambayo inasababisha na kudumisha umaskini, kukosa maendeleo na kushusha hadhi ya watu. Miundo hii ya kidhambi inajengwa na kuimarishwa kwa matendo mengi dhahiri ya ubinafsi wa mtu.

333. Ili shughuli za kiuchumi ziwe na sifa za uadilifu, ni lazima ziwalenge watu wote na jamii zote. Kila mmoja ana haki ya kushiriki katika maisha ya kiuchumi na ana wajibu wa kuchangia, kwa kadiri ya nafasi yake, kwa maendeleo ya nchi yake na yale ya familia nzima ya watu.[696] Iwapo, kwa kiwango fulani, kila mmoja anawajibika kwa ajili ya mwingine, basi kila mtu ana wajibu wa kujitolea binafsi kwa maendeleo ya kiuchumi kwa ajili ya wote.[697] Huu ni wajibu katika mshikamano na haki, hakuna shaka, ndiyo njia bora kushinda zote katika kuleta maendeleo ya kiuchumi kwa watu wote. Iwapo zitaendeshwa kiadilifu, shughuli za kiuchumi zinakuwa zimetokana na uzalishaji wa bidhaa pamoja na upatikanaji wa huduma zinazofaa kwa maendeleo ya kila mtu, pia zinakuwa ni fursa ya kila mmoja kuunganika katika mshikamano na kuishi wito wa ushirika na wengine kwani Mungu alimuumba mtu kwa madhumuni hayo.[698] Jitihada za kubuni na kutekeleza miradi ya huduma za kijamii na za kiuchumi ambazo zinahimiza manufaa kwa wote katika jamii na ulimwengu ulio wa utu zaidi ni changamoto ngumu, lakini pia inachochea wajibu kwa wote wanaofanya kazi katika nyanja ya uchumi na wanaohusika na sayansi za kiuchumi.[699]

334. Kusudi la shughuli za kiuchumi ni kupata maendeleo ya mali na kuendelea kuongezeka na sio kuongezeka tu kwa bidhaa, lakini pia ubora wake; hili linakubalika kimaadili iwapo litaelekezwa katika maendeleo ya kweli ya mtu katika mshikamano na jamii ambamo watu wanaishi na kufanya kazi. Maendeleo, kwa kweli, haimaanishi mchakato wa ulimbikizaji tu wa bidhaa na huduma mbalimbali. Kinyume na hilo, ulimbikizaji wenyewe tu, hata kama ungelikuwa kwa manufaa ya walio wengi, si sharti la kutosha kuleta furaha ya kweli miongoni mwa binadamu. Ni kwa uelewa huu, mafundisho ya Kanisa kuhusu Jamii yanaonya dhidi ya udanganyifu uliofichika katika maendeleo ya wingi wa vitu, kwani uwepo wa “ziada pindukia wa kila aina ya vitu kwa manufaa ya wachache ndani ya jamii, huwafanya hao kuwa watumwa wa mali na kujiona bora zaidi ya wengine. Hali ya jinsi hii huitwa ustaarabu wa ufujaji mali.”[700]

335. Kwa mtazamo wa maendeleo yaliyo kamili na ya mshikamano, inawezekana kufikia uelewa sahihi wa tathmini kadiri ya mpango wa maadili utolewao na mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yahusuyo uchumi wa soko huria: “Iwapo ‘ubepari’ ni kumaanisha mfumo wa kiuchumi unaotambua kimsingi nafasi chanya ya biashara, soko, umilikaji binafsi na kutokana na hivyo wajibu wa kuwa nyenzo za uzalishaji, pamoja na kipaji huru cha ubunifu katika nyanja ya uchumi, basi jibu lake ni hakika kukubaliana na ilivyoainishwa, ingawaje ingekuwa sahihi zaidi kusema ‘uchumi wa biashara,’ ‘uchumi wa soko,’ au ‘uchumi huria’. Lakini ikiwa ‘ubepari’ ni kumaanisha mfumo ambamo uhuru katika nyanja za uchumi haukuwekewa mipaka imara ya taratibu za kisheria zinazodai uchumi kuhudumia uhuru wa mwanadamu katika ujumla wake, na uchumi wenyewe ukiwa kwa namna yake ni kipengele cha uhuru huo, ambao kiini chake ni mpango wa kimaadili na kidini, basi jibu lake ni hakika kutokubaliana nalo.”[701] Kwa njia hii, mtazamo wa Kikristo unaainishwa mintarafu shughuli za kiuchumi katika hali za kijamii na kisiasa, siyo tu kanuni zake bali pia uadilifu wake na maana yake.

 

III. JITIHADA BINAFSI NA UJASIRIAMALI

336. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanazingatia uhuru wa mtu katika mambo ya kiuchumi kuwa ni tunu msingi na haki ya mtu asiyoweza kuondolewa ambayo inapaswa kuenziwa na kulindwa. “Kila mmoja ana haki katika ubunifu wa kiuchumi; kila mtu atumie kihalali vipaji vyake katika kuchangia kuneemesha yale yatakayowanufaisha wote, na kupata matunda ya haki ya kazi yake.”[702] Mafundisho haya yanatuasa dhidi ya matokeo hasi iwapo haki ya ubunifu wa kiuchumi yatadhoofishwa au kunyimwa kabisa: “Uzoefu unatuonyesha kwamba iwapo haki hii itanyimwa kabisa, au ikizuiliwa kwa kisingizio cha ‘usawa’ wa wote katika jamii, hufifisha moyo. Katika hali halisi huangamiza kabisa moyo wa ubunifu, yaani ukosefu wa uhuru wa ubunifu wa raia.”[703] Kwa mtazamo huu, ubunifu huru na unaobeba wajibu wa uchumi unaweza kuainishwa kuwa ni shughuli kwazo utu wa wanaume na wanawake hudhihirika kuwa mbunifu na wenye kuweza kufikiria kimantiki. Hivyo, ubunifu wa namna hiyo sharti upewe uhuru mkubwa wa kufikiri na kutenda tofauti. Serikali ina wajibu wa kimaadili wa kuweka taratibu na mipaka madhubuti kwa shughuli za kiuchumi ili ziendane na lengo la kupata manufaa kwa wote.[704]

337. Kipawa cha ubunifu ni cha msingi katika shughuli za binadamu, na hata katika mambo ya biashara, hujidhihirisha hasa katika maeneo ya mipango na ugunduzi. “Kuratibu jitihada za uzalishaji, kupangilia muda na kuhakikisha kwamba mali inafika kwa wakati muafaka na kwa kiasi kitakiwacho, pamoja na kuchukua tahadhari za lazima – yote hayo ni chanzo cha utajiri katika jamii ya kisasa. Kwa namna hii, dhima ya kazi ya mwanadamu iliyotendwa kwa nidhamu na ubunifu na, vikiwa kiungo muhimu katika kazi, ari na ujasiriamali inadhihirika waziwazi na kuonyesha uwezo wa kuamua.”[705] Katika msingi wa mafundisho haya inadhihirika ile imani isemayo “rasilimali kuu ya mtu ni mtu mwenyewe. Akili yake inamwezesha kutambua uwezo wa kiuzalishaji ulimo ardhini na njia mbalimbali zinazoweza kutumiwa kukidhi mahitaji ya binadamu.”[706]

a. Ujasiriamali na Malengo Yake

338. Biashara sharti zionyeshe uwezo katika kuhudumia jamii kwa manufaa ya wote kwa kuzalisha vitufaa na kutoa huduma bora. Katika jitihada za kuzalisha mali na kutoa huduma kwa kadiri ya mpango wenye lengo la ufanisi na kutosheleza mahitaji ya vikundi mbalimbali husika, biashara hutengeneza utajiri kwa ajili ya jamii yote, siyo tu kwa ajili ya wamiliki wa biashara zenyewe bali kwa ajili ya wadau wengine waliomo katika shughuli ya biashara hizo. Licha ya wajibu huo wa kiuchumi, biashara hutekeleza pia majukumu ya kijamii, zikiunda fursa za kukutana, kushirikiana, na kukuza uwezo wa washiriki.  Katika shughuli za kibiashara, kwa hiyo, upeo wa kiuchumi ni sharti la kufikia, siyo tu malengo ya kiuchumi, bali pia malengo ya kijamii na kimaadili ambayo yanatafutwa kwa pamoja.

Lengo la kibiashara sharti lipatikane katika matakwa ya kiuchumi na kwa kufuata vigezo vya kiuchumi, lakini thamani halisi ziletazo maendeleo thabiti ya mtu na jamii zisipuuzwe. Katika mtazamo huu wa kiutu-nafsi na wa kijamii, “biashara haiwezi kuchukuliwa kuwa ni tu kama jamii ya mali kimitaji,” lakini pia ni ‘jamii ya watu kwa nafsi zao’ ambamo watu wanashiriki katika njia mbalimbali wakiwa na wajibu mahususi, iwe wanaleta mitaji inayotakiwa kwa shughuli za kampuni au wanashiriki moja kwa moja katika kazi za uzalishaji.”[707]

339. Wale wote wanaothubutu kuwekeza katika biashara waelewe kwamba jamii wanamofanyia biashara huwakilisha lililo jema kwa kila mmoja na si tu muundo unaoruhusu kufikia matakwa ya mtu binafsi. Utambuzi huu peke yake huwezesha kujenga uchumi wenye mtazamo wa kweli wa kuhudumia jamii na kuandaa programu za ushirika wa kweli baina ya wadau mbalimbali katika uzalishaji.

Mfano muhimu na wa maana kuhusu suala hili unapatikana katika shughuli za ushirika, biashara ndogondogo na za kati, na biashara za sanaa za kazi za mikono na mashamba ya wastani ya familia. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanasisitiza sana juu ya mchango unaotolewa na shughuli za aina hii katika kuongeza thamani ya kazi, kukuza hisia ya uwajibikaji kwa mtu binafsi na kwa jamii, maisha ya kidemokrasia na tunu za utu ambazo ni muhimu katika maendeleo ya soko na ya jamii.[708]

340. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanatambua dhima stahiki ya faida kwamba ni kiashirio cha biashara inayoendeshwa vema: “Kampuni ikipata faida, inamaanisha kuwa rasilimali na nyenzo za uzalishaji vimetumika vema.”[709] Hilo lakini halilifumbi macho Kanisa kutambua uwezekano wa biashara kupata faida huku ikiwa haihudumii jamii ipasavyo.[710] Kwa mfano; “uwezekano wa kuwa na mahesabu yaliyo sahihi, lakini ikawa watu ambao ndio rasilimali kuu – wanadhalilishwa na kukosewa katika utu wao.”[711] Hili hutokea pale ambapo biashara inakuwa sehemu ya mfumo wa kijamii na utamaduni unaowanyonya watu na kuelekea kukwepa jukumu la kutenda haki kwa jamii na kukiuka haki za wafanyakazi.

Ni muhimu katika biashara, sambamba na kutafuta faida halali, ilinde hadhi ya wafanyakazi wa ngazi zote katika kampuni. Malengo mawili haya si kinzani, kwani kwa upande mmoja, ni kitu kisichowezekana kuhakikisha kuendelea kuwepo kwa biashara bila ya kuzalisha kwa faida mali na huduma zifaazo, ambavyo ni tunda la shughuli yoyote ya kiuchumi. Kwa upande wa pili, kuruhusu wafanyakazi kujiendeleza kunakuza tija na ufanisi katika kazi yenyewe. Ujasiriamali wowote lazima uwe ni wa kijamii yenye mshikamano,[712] yaani usijikite katika maslahi yake tu. Lazima uwe na mwelekeo wa “mfumo wa ikolojia ya kijamii”[713] wa utendaji na uchangie katika manufaa kwa wote huku ukilinda mazingira asilia.

341. Ingawaje kutafuta faida halali katika shughuli za kiuchumi na za kifedha kunakubalika, njia ya kukopesha fedha kwa riba kunashutumiwa kwa sheria ya maadili:” Wale ambao shughuli zao za riba na ubahili zinapelekea njaa na vifo vya ndugu zao katika familia ya binadamu wanafanya mauaji, ingawaje si moja kwa moja, na hawana budi kushutumiwa.[714] Shutuma hii inaelekezwa vilevile kwa mahusiano ya kiuchumi baina ya mataifa, na hasa mintarafu hali ya nchi zinazoendelea, ikitakiwa kubadili mifumo mibaya ya kifedha, kama pia ya riba na mahusiano mabaya ya kibiashara kati ya mataifa.”[715] Hivi karibuni Majisterio yamezungumzia kwa ukali na kwa udhahiri yakizieleza shughuli za riba kuwa “ni baa lililo waziwazi katika wakati wetu huu na linatishia maisha ya watu wengi.”[716]

342. Biashara za wakati huu zinaendeshwa katika muktadha za kiuchumi zinazoendelea kupanuka tu na ambazo serikali za nchi zinaonyesha kukosa uwezo wa kudhibiti mabadiliko hayo ya kasi yanayoathiri mahusiano ya kimataifa ya kiuchumi na kifedha. Hali hii hupelekea biashara kubeba majukumu mapya na makubwa zaidi ikilinganishwa na wakati uliopita. Dhima ya biashara haijawahi kuwa muhimu kama ilivyo katika wakati wa sasa kuhusiana na maendeleo ya kweli ya binadamu katika mshikamano. Muhimu pia katika maana hii ni uelewa mkubwa unaooneshwa na biashara zenyewe kwamba “maendeleo sharti yawe ya kushirikishana kati ya sehemu mbalimbali za dunia, vinginevyo huchukua mwelekeo wa kuzorota hata katika zile sehemu zinazofahamika kuwa na maendeleo endelevu, hilo linatufundisha jambo muhimu kuhusu hulka ya maendeleo ya kweli: ama mataifa yote yanashiriki au hayatakuwa maendeleo ya kweli.”[717]

b. Nafasi na Wajibu wa Wamiliki Biashara na Usimamizi

343. Jitihada za kiuchumi ni maelezo ya werevu wa mwanadamu na ulazima wa kuwajibika katika kutafuta kukidhi mahitaji ya watu kwa mtindo wa ubunifu na ushirikiano. Ubunifu na ushirikiano huo ni ishara ya fikra halisi ya mashindano ya biashara: “cumpetere,” maana yake kutafuta kwa pamoja utatuzi ulio sahihi kushinda mwingine wowote unaokidhi mahitaji kadiri yanavyojitokeza. Moyo wa uwajibikaji utokanao na ari huru katika uchumi ni fadhila, siyo tu ya mtu mmoja itakiwayo kwa ustawi wa mtu binafsi, bali pia ni kipaji cha kijamii kilicho cha lazima kwa maendeleo ya jamii katika mshikamano. “Fadhila mbalimbali muhimu zinazohusika katika mchakato wote huu, kati ya hizo ni umakini, uchapakazi, busara katika kuchukua tahadhari mambo ya uhakika yanayoweza kutegemewa na uaminifu katika mahusiano. Pia ujasiri katika utekelezaji wa maamuzi ya lazima ingawaje yanaweza kuwa magumu na ya kuumiza wakati mwingine kwa madhumuni ya kuendeleza biashara na kuondoa vipingamizi.[718]

344. Dhima za wafanyabiashara na menejimenti zina umuhimu mkuu kwa jamii, kwa sababu ni kitovu cha mtandao wa ufundi, biashara za kimataifa, usimamizi wa fedha na mikataba ya kitamaduni ambazo ni sifa bainifu za hali halisi ya biashara za kisasa. Kutokana na kuongezeka kwa mchangamano wa shughuli za kibiashara, maamuzi yanayofanywa na makampuni yanaleta athari kubwa zenye kuhusiana katika maeneo ya kiuchumi na kijamii. Kwa sababu hiyo, utekelezaji wa majukumu ya wenye biashara na menejimenti unapaswa zaidi ya kuangalia upya masuala mahususi likiwa ni lengo la jitihada za kudumu – daima ufikirie na kuhamasishwa na maadili yanayowaongoza kufanya maamuzi yao.

Wamiliki biashara na menejimenti wasiangalie tu malengo ya kiuchumi ya kampuni, viwango vya mafanikio kiuchumi na kutopoteza “mitaji” kama ndivyo vigezo muhimu pekee kwa uzalishaji. Ni wajibu wao pia kuheshimu kwa dhati hadhi ya wote wanaofanya kazi katika kampuni.[719] Wafanyakazi hawa ni “rasilimali muhimu kuliko zote katika kampuni”[720] iliyo na uwezo wa kutoa maamuzi katika uzalishaji.[721] Yafanywapo maamuzi muhimu kuhusu mikakati na fedha, kununua au kuuza, kupunguza au kuongeza, kufunga au kuunganisha biashara, masuala ya fedha na biashara visiwe ndio vigezo pekee katika kufikia uamuzi.

345. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanawasisitizia wamiliki biashara na menejimenti kupania kuweka muundo wa kazi ambao unaendeleza familia, hasa akinamama katika utekelezaji wa wajibu zao;[722] wamiliki waridhie katika mwanga wa maendeleo kamili ya mtu, dai la ubora “wa bidhaa zinazozalishwa na kutumiwa, ubora wa huduma zitolewazo, ubora wa mazingira na maisha kwa ujumla.”[723] Pia kuwekeza, iwapo mazingira yatakiwayo ya kiuchumi yanaruhusu na utengamano wa kisiasa ukiwapo, katika maeneo na sekta za uzalishaji zinazotoa fursa kwa watu binafsi na makundi ya kijamii kutumia nguvukazi yao wenyewe.”[724]

 

IV. TAASISI ZA KIUCHUMI KATIKA KUMHUDUMIA MTU

346. Mojawapo ya masuala yanayopewa kipaumbele katika uchumi ni utumiaji wa rasilimali,[725] yaani wa bidhaa zozote zile na huduma ambazo wale wazitegemeao – wazalishaji na watumiaji wawe wao binafsi au jamii – huzipa thamani kwa sababu ya manufaa yao katika uzalishaji na matumizi. Rasilimali ulimwenguni ni adimu, ikimaanisha kuwa kila mtu na kila jamii, lazima na ni sharti ijiandalie mpango wa matumizi mazuri ikizingatia mantiki ya “kanuni kubana matumizi.” Utatuzi wa kufaa wa matatizo ya kiuchumi yahusuyo watu wote na yale ya kimsingi, tatizo la kiuchumi la uhaba wa mapato ukilinganishwa na mahitaji ya mtu pekee na jamii - binafsi na jamii – pamoja na muundo mzima wa utendaji wa kufaa wa mfumo wote wa kiuchumi unategemea uzingatiaji wa kanuni hii. Ufanisi huu huhusisha moja kwa moja uwajibikaji na uwezo wa watendaji na wadau husika, kama vile soko, serikali na asasi mbalimbali za kijamii.

a. Nafasi na Wajibu wa Soko Huria

347. Soko huria ni taasisi muhimu ya kijamii kwa sababu ya uwezo wake wa kuhakikisha kunakuweko matokeo ya kufaa ya uzalishaji na utoaji wa huduma. Kihistoria, soko limejidhihirisha kuwa na uwezo wa kuanzisha na kuhimili kukua kwa uchumi kwa vipindi virefu. Ziko sababu nzuri tu za kukubaliana na hilo, katika mambo mengi “soko huria limekuwa chombo chenye ufanisi katika matumizi ya rasilimali na kutosheleza mahitaji kuliko mifumo mingine yote.”[726] Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanatambua vema faida za hakika zitokanazo na utaratibu wa soko huria unaowezesha matumizi bora ya rasilimali na kurahisisha ubadilishanaji bidhaa na mali. Taratibu hizi zaidi ya yote. zinatoa nafasi kubwa ya kukidhi matakwa na uchaguzi wa mtu mwingine.”[727]

Soko lenye ushindani wa kweli ni chombo cha kufaa kufikia malengo muhimu ya haki: likidhibiti faida kupita kiasi cha biashara husika, likikidhi mahitaji ya walaji, likihakikisha kuwepo kwa matumizi fanisi na hifadhi ya rasilimali, likiwatuza wajasiriamali na wabunifu, kuwepo taarifa zinazowezesha kulinganisha bei na ubora wa bidhaa na hivyo kuwezesha kufanya manunuzi katika mazingira mazuri ya ushindani.

348. Soko huria haliwezi kupimwa isipokuwa kwa kutumia malengo linalotaka kufanikisha na kwa tunu za kijamii zitokanazo na mwenendo wa soko lenyewe. Kwa kweli si kutoka ndani yake lenyewe kwamba soko laweza kubaini kanuni msingi za uhalali wake; ni dhamiri za watu na wajibu wa jamii kuanzisha mahusiano ya haki kati ya mapato na hatma ya jamii.[728] Faida binafsi ya biashara, ingawaje ni halali, kamwe lisiwe ndio lengo pekee. Pamoja na lengo hili, lipo lengo jingine, ambalo ni la msingi pia, lakini lililo kuu zaidi: Manufaa kwa jamii lazima lifikiwe si kiukinzani bali katika kuambatana na mantiki ya soko. Endapo soko huria litatekeleza shughuli muhimu zilizotajwa hapo juu, linakuwa na huduma kwa manufaa ya wote na kwa maendeleo kamili ya mwanadamu. Lakini, kupindua kwa mahusiano baina ya mapato na hatma ya jamii, kunaweza kusababisha kuyumba kwa maadili na kulifanya soko kuwa taasisi ya kinyama na ya kibaguzi yenye matokeo hasi na yasiyodhibitika.

349. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yakiwa yanafahamu kwamba soko ni chombo kisicho na mbadala katika kurekebisha shughuli mbalimbali zinazoendelea ndani ya mfumo wa uchumi, linalielekeza soko kuwa thabiti katika malengo yake ya kimaadili, ambayo yanahakikisha na kuweka sawia mipaka, maeneo ambamo soko lenyewe linaweza kuendesha shughuli zake kwa uhuru.[729] Nadharia ya kwamba soko peke yake linaweza kukabidhiwa kazi ya kukidhi mahitaji ya kila aina ya bidhaa haikubaliki, kwa sababu nadharia ya namna hiyo inatokana na mtazamo fasiri wa mtu na jamii.[730] Yakiwa yanakabiliwa na hatari halisi ya ‘imani’ kwa soko, Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanatahadharisha juu ya mapungufu yake yaliyo dhahiri kwa kushindwa kukidhi mahitaji muhimu ya kibinadamu “ambayo kwa asili yake sio na hayawezi kuwa bidhaa,”[731] mahitaji yasiyoweza kununuliwa na kuuzwa kwa kadiri ya kanuni ya “kubadilishana vilivyo linganifu” na kwa mantiki ya mikataba ilivyo ya kibiashara hasa.

350. Soko hubeba shughuli muhimu ya kijamii katika umma, kwa hiyo ni lazima kubainisha mazingira yatakayowezesha utekelezaji wake ipasavyo. Waendeshaji wa soko sharti wawe huru kulinganisha, kutathmini na kuchagua kutoka miongoni mwa yale yanayowezekana. Hata hivyo, Uhuru katika sekta ya uchumi, lazima udhibitiwe na kanuni zifaazo ili uweze kutumika kupata uhuru kamilifu wa binadamu. Uhuru wa kiuchumi ni sehemu moja tu ya uhuru wa mwanadamu. Ukijiendesha wenyewe tu, na endapo mtu anaonekana kuwa mzalishaji tu au mlaji wa bidhaa kuliko kuwa yeye ni lengo azalishaye na kutumia ili apate kuishi, basi uhuru wa kiuchumi unapoteza uhusiano muhimu wa lazima na binadamu, na kuishia katika kumtenganisha na jasho lake na kumkandamiza.”[732]

b. Amali ya Serikali

351. Amali ya Serikali na mamlaka nyinginezo za jamii hazina budi kuendana na kanuni ya auni na zijenge mazingira ya kufaa ya kuendeshea shughuli za kiuchumi kwa uhuru. Kazi hizo pia ziongozwe na msukumo wa kanuni ya mshikamano na pawepo na mipaka ya kujitawala kwa wahusika kwa madhumuni ya kuwakinga wanyonge.[733] Mshikamano pasipo auni, kwa urahisi kunaweza kwa kweli, kupotosha na kujenga “Ustawi wa Dola“ wakati auni bila mshikamano kwaweza kuhimiza aina za makundi ya watu wanaojifikiria wenyewe tu. Ili kanuni asili hizi ziheshimike, mkono wa Serikali katika mazingira ya uchumi usiwe wa kivamizi au wa kushtukiza na pia usikosekane, bali ulingane na mahitaji ya jamii. “Serikali ina wajibu wa kuhimili shughuli za kibiashara kwa kujenga mazingira yanayowezesha kuhakikisha nafasi za kazi, kwa kuchochea juhudi pale zinapokosekana, au kuzitegemeza kwa kuzisaidia pale zinapokumbwa na migogoro na kuingia hatarini. Serikali ina haki ya ziada ya kuingilia kati iwapo ukiritimba utasababisha ucheleweshaji au utajenga vikwazo dhidi ya maendeleo. Zaidi ya kuweka ulinganifu na kuongoza maendeleo, katika mazingira maalumu, Serikali inaweza kuchukua nafasi na kufanya kazi mbadala.”[734]

352. Kazi msingi ya Serikali katika mambo ya kiuchumi ni kuweka mfumo wa kisheria unaofaa kudhibiti shughuli za kiuchumi, kwa madhumuni ya kuikinga hapatakuwepo “kanuni ya uchumi huria ambayo inabeba dhana ya uwepo wa usawa baina ya wahusika, na kwamba hapatakuwapo na mmoja aliye na uwezo mkubwa zaidi hata kusababisha mwingine kuwa mtumishi tu.”[735] Shughuli za kiuchumi na haswa katika muktadha wa soko huria, haziwezi kuendeshwa katika mazingira yasiyo ya kitaasisi, ya kisheria na ya kisiasa. Kinyume chake inatakiwa pawepo mazingira ya kufaa kuhakikisha uhuru wa mtu na uhuru wa kuwa na mali binafsi, na pia kuwepo uthabiti wa fedha ya nchi na ufanisi wa huduma za jamii.”[736] Kutimiza kazi hiyo, Serikali sharti iridhie sheria zenye kufaa, lakini wakati huohuo, lazima ielekeze sera za kiuchumi na za kijamii ili zisitumike vibaya zinapojihusisha na shughuli mbalimbali za masoko, kwani zinapaswa na ni lazima ziendeshwe bila kuingiliwa na mamlaka – au mbaya zaidi kuwa za kiimla – miundo iliyo bora na vizuizi.

353. Ni sharti kwa soko na Serikali kutenda kwa mashauriano na kwa kukamilishana baina yao. Kwa kweli soko huria laweza kuwa na ushawishi wa kufaa kwa jamii iwapo tu Serikali imejipanga katika mtindo wa kutoa ufafanuzi na mwelekeo wa maendeleo ya kiuchumi, ikiimarisha uzingatiaji wa kanuni za haki na uwazi, na hata kuingilia kati - pale inapolazimu[737] - yaani ikitokea kuwa soko limeshindwa kupata ufanisi uliokusudiwa na inapobidi kusimamia upya mgao. Kuna sekta kadhaa ambamo soko, kwa kutumia taratibu zake za kawaida, haliwezi kuhakikisha mgawanyo sawa wa bidhaa na huduma muhimu kwa makazi bora ya raia. Katika kadhia ya namna hii, kukamilishana baina ya Serikali na soko kunahitajika zaidi kuliko wakati mwingine wowote.

354. Serikali inaweza kuwatia moyo raia na taasisi za kibiashara kukuza manufaa kwa watu wote kwa kutengeneza sera zinazokuza ushiriki wa raia wote katika shughuli za uzalishaji. Kuheshimu kanuni ya auni lazima kuchochee mamlaka za jamii kufikia mapatano na raia, mapatano yanayowapa nguvu raia kukuza uwezo wao wa jitihada binafsi, kujitawala na kujenga uwajibikaji wa raia, wakiepuka kuingilia kati shughuli za wengine.

Kwa nia ya manufaa kwa wote, ni lazima kufuatilia siku zote na kwa bidii bila kuchoka lengo la ulinganifu sahihi kati ya uhuru binafsi na amali ya jamii, ikieleweka kuwa kwa njia moja ni kuingilia kati masuala yahusuyo uchumi na pili kama kazi ya kutegemeza maendeleo ya uchumi. Katika hali yoyote ile, Serikali inapoingilia kati lazima ifanye hivyo kwa uwiano, busara na kwa nia ya kuleta matokeo yanayotakiwa. Katika hilo, Serikali ifanye bila ya kutenda badala ya watu wenyewe, ambavyo ingekuwa ni kinyume na haki yao ya uhuru wa kujituma katika shughuli za kiuchumi. Kwa jinsi hiyo, huleta madhara kwa jamii: kuingilia mno masuala ya wajibu wa raia kwa kukuza zaidi taasisi za jamii zinazoongozwa zaidi kirasimu na mantiki ya kiukiritimba kuliko kuongozwa na lengo la kukidhi mahitaji ya watu.[738]

355. Mapato yatokanayo na kodi na matumizi ya Serikali huwa na umuhimu mkubwa kiuchumi kwa kila jamii na jumuiya ya kisiasa. Lengo la kufikiwa ni kuwa na mfumo wa usimamizi wa fedha za umma wenye uwezo wa kuwa chombo cha maendeleo na mshikamano.  Usimamizi wa fedha za umma ulio wa haki, wenye ufanisi utakuwa na athari chanya kwa uchumi, kwa sababu utakuza ajira na kuhimili biashara hata kazi zisizo za kuzalisha faida na kusaidia kuongeza kuaminika kwa serikali kama mdhamini wa mifumo ya bima ya kijamii na akiba ambayo imeanzishwa kwa madhumuni ya kuwakinga hasa walio dhaifu kiuchumi katika jamii.

Matumizi ya Serikali yanakuwa na lengo la kujali manufaa kwa wote iwapo kanuni msingi zimezingatiwa: ulipaji wa kodi[739] ukiwa ni sehemu ya wajibu wa mshikamano; utozaji kodi ya kiasi na ya haki;[740] na kufuata utaratibu ulio sahihi na adilifu katika usimamizi wa mgao wa rasilimali za jamii.[741] Katika mgawanyo wa rasilimali matumizi ya serikali sharti yazingatie kanuni ya mshikamano, usawa na matumizi ya karama. Inalazimu pia kuziangalia familia kwa makini kwa kutenga kiasi cha kutosha kwa madhumuni hayo.[742]

c. Nafasi na Wajibu wa Vyombo vya Kati

356. Mfumo wa kijamii – kiuchumi sharti udhihirishwe na uwepo kwa wakati mmoja wa kazi za umma na shughuli binafsi, zikiwemo shughuli binafsi zisizo za kujitengenezea faida. Kwa jinsi hii, kunaibuka vyanzo mbadala vya kufanya maamuzi na kupangilia shughuli. Matumizi ya aina fulani za bidhaa, bidhaa zinazomilikiwa kwa pamoja, au zile zinazopaswa kutumika kwa pamoja, haziwezi kutegemea utaratibu wa soko,[743] na hata matumizi ya bidhaa za namna hii hazihodhiwi na mamlaka za Serikali peke yake. Wajibu wa Serikali mintarafu bidhaa na huduma za aina hiyo ni kutumia jitihada zote za kiuchumi na kijamii zinazohamasishwa na vyombo vya kati ambavyo huleta matokeo kwa watu. Jamii ya kiraia iliyojiunga katika vyombo vya kati inaweza kuchangia katika kufikia manufaa kwa wote kwa kushirikiana na kukamilishana kati ya serikali na soko. Kutegemeana kwa namna hii kunatia moyo wa kukuza demokrasia ya kiuchumi inayofaa. Kwa mtazamo huu uingiliaji kati wa serikali lazima udhihirishwe na mshikamano thabiti, usiotengana kamwe na kanuni auni.

357. Asasi binafsi zisizo za kutengeneza faida zina dhima mahususi katika medani ya uchumi. Asasi hizi zinadhihirishwa na jitihada zisizo na woga wowote za kuunganisha ufanisi katika uzalishaji mali na mshikamano. Kwa ujumla zimejengeka juu ya makubaliano ya kushirikiana na kudhihirisha mtazamo wa pamoja wa wanachama walioamua kuungana. Serikali inahimizwa kuheshimu hali za asasi hizo na itumie vema hali halisi inayoziunda taasisi hizo kwa kuzitendea ipasavyo kwa kufuata kanuni auni, ambayo inaamrisha kwamba hadhi na uhuru wa wajibu wa chombo kidogo sharti uheshimiwe na kuimarishwa.

d. Akiba na Bidhaa Zitumiwazo

358. Watumiaji, ambao mara nyingi huwa na uwezo wa ziada kupita kiwango kile cha kujikimu tu, huathiri sana mwenendo wa uchumi kwa maamuzi yao huru, kwa ama kutumia fedha yao kununulia bidhaa za kutumia au kuweka akiba. Kwa hakika, uwezekano wa ushawishi wa uchaguzi katika sekta ya uchumi umo mikononi mwa wale wanaopaswa kuamua wapi wawekeze fedha yao. Leo, hata kupita wakati mwingine wowote, inawezekana kutathmini uchaguzi mbadala katika uwekezaji sio tu kwa kulinganisha mapato tarajiwa yatokanayo na kuthubutu huku bali pia kwa kukadiria manufaa ya miradi mbalimbali ambamo rasilimali zingelitumika, kwa kuelewa kwamba “uamuzi wa kuwekeza katika eneo moja kuliko jingine, katika sekta hii kuliko ile, siku zote huwa ni uchaguzi wa kimaadili na kitamaduni.”[744]

359. Uwezo utokanao na mapato, lazima utumike katika muktadha wa madai ya kimaadili ya haki na mshikamano, na kwa kuzingatia uwajibikaji kwa jamii. Kamwe mtu asisahau “wajibu wa hisani.., yaani, wajibu wa kutoa kutokana na ‘tele’ aliyonayo, hata wakati mwingine kutoka katika yake yaliyo mahitaji yake, ili kumpatia maskini kilicho cha lazima kwa maisha yake.”[745] Wajibu huu unawapa uwezekano walaji. Ni jambo la kushukuru usambazaji mpana wa taarifa, kwa kuongoza tabia za wazalishaji, kwa njia ya kuchagua vipaumbele vya – kibinafsi au kimakundi – kwa bidhaa kutoka makampuni fulanifulani kuliko nyinginezo, kwa kuzingatia sio bei tu na ubora wa bidhaa zinunuliwazo, isipokuwana uwepo wa masharti na mazingira bora ya wafanyakazi na pia ulinzi wa kutosha wa mazingira asili ambamo kampuni zinaendeshea shughuli zao.

360. Mwenendo wa ufujaji bidhaa zitumikazo unajenga mwelekeo wa kudumu wa kutamani “kumiliki vitu” kuliko “kuwa”. Hili hupotosha “vigezo vya kubainisha kwa usahihi baina ya njia mpya na bora zaidi za kukidhi mahitaji ya binadamu na zile bandia zinazopinga malezi ya mtu kuelekea kuwa na nafsi adilifu.”[746] Kuushinda mwenendo huu sharti kubuni mtindo wa maisha ambamo nia ya kupata ukweli, uzuri , wema na mawasiliano na wengine kwa ajili ya kufikia maendeleo ya pamoja vitakuwa ndivyo vigezo vya kubaini bidhaa za kuzalisha, uwekaji akiba na uwekezaji.”[747] Ni ukweli usiopingika kwamba njia za maisha zinaathiriwa kwa kiwango kisichodharaulika na muktadha mbalimbali za kijamii. Kwa sababu hiyo, changamoto ya kiutamaduni itokanayo na mwenendo wa ufujaji, lazima zikabiliwe kwa ushupavu, na hasa kwa kufikiria vizazi vya baadaye vitakavyotakiwa kuishi katika mazingira yaliyokwisha porwa pasi kipimo na huo ufujaji usio na mpangilio.[748]

 

V. “MAMBO MAPYA” KATIKA SEKTA YA UCHUMI

 

a. Utandawazi: Fursa na Hatari

361. Zama zetu za kisasa zinadhihirishwa na mwenendo usio wazi kueleweka wa utandawazi wa kiuchumi na mambo ya fedha, mchakato ambao hatua kwa hatua unafungamanisha uchumi wa mataifa katika ngazi ya shughuli za kibiashara. Katika mchakato huu, wahusika ambao muda wote wanaongezeka, wanalazimika kufuata mtazamo wa kimataifa katika maamuzi yao kuhusu ukuaji na faida katika siku zijazo. Mahusiano mapya ya jamii ya kiulimwengu hayaangalii tu kuwepo kwa mikataba ya kiuchumi na kifedha baina ya taasisi husika za nchi mbalimbali, mikataba ambayo imekuwapo wakati wote, bali katika kuonekana duniani kote na katika namna ambayo haijawahi kutokea kwa kuibuka mitandao mbalimbali ya mahusiano. Dhima ya masoko ya fedha inategemewa sana sasa na ni muhimu kwa biashara. Kufuatia ulegezaji masharti ya ubadilishanaji mitaji na mzunguko wa pesa, wigo wa masoko umepanuka kwa kasi ya kushangaza, hata kufikia mahali ambapo mawakala wanaweza katika “wakati mfupi tu,” kuhamisha mitaji mikubwa kutoka sehemu moja ya dunia kwenda sehemu nyingine. Hii ni hali halisi yenye sura nyingi ambazo ni vigumu kuzitambua, kwa sababu inatanda katika ngazi mbalimbali na imo katika kubadilikabadilika kuelekea pale ambako hakuwezi kutabirika kwa wepesi.

362. Utandawazi unaamsha matumaini mapya na wakati huohuo unaibua maswali ya kutatanisha.[749] Utandawazi unaweza kubuni maendeleo ya manufaa kwa jamii yote ya binadamu. Baada ya kupatikana maendeleo ya kushangaza katika nyanja za mawasiliano, ukuaji wa mahusiano katika nyanja za uchumi na fedha kimataifa unaleta mambo mawili kwa pamoja ambayo ni kupungua kwa kiasi kikubwa cha gharama za mawasiliano na teknolojia mpya za mawasiliano, na kuongeza kasi ya mchakato ambao unawezesha biashara na uhamishaji fedha kunapanuka sana duniani. Kwa msemo mwingine, mienendo miwili hii ya utandawazi wa kiuchumi – kifedha na ya maendeleo katika teknolojia imeimarishana vema, na hivyo kuwezesha mchakato wote wa kipindi hiki cha mpito kuwa wa kasi kubwa mno.

Katika kuchanganua muktadha wa wakati huu, zaidi ya kutambua fursa zilizowekwa wazi katika zama za utandawazi wa kiuchumi, kunaonekana hatari zinazoambatana na wigo mpya wa mahusiano ya kibiashara na fedha. Kwa kweli kuna viashirio vingi vikitahadharisha kuwepo kwa mwelekeo wa kuongezeka kwa kutokuwapo usawa, kwa upande mmoja baina ya nchi zilizoendelea na zinazoanza kuendelea, na upande wa pili baina ya nchi zenye viwanda zenyewe. Ukuaji wa mali nyingi katika uchumi unaotokana na mchakato ulioelezwa hapo juu unaendana na ongezeko wianifu la umaskini.

363. Kujali manufaa ya wote kunamaanisha kutumia fursa mpya kwa kugawanya upya rasilimali kati ya maeneo mbalimbali duniani, kwa faida ya walionyimwa haki za kimsingi za kijamii ambao mpaka sasa wamekuwa wanatengwa au kutupwa kando ya mkondo wa maendeleo ya jamii na uchumi.[750] “Changamoto, kwa kifupi, ni kuhakikisha utandawazi unaofanyika katika mshikamano, yaani utandawazi usioacha wengine pembeni.”[751] Kuna hatari pia kwa maendeleo yenyewe ya teknolojia kutosambazwa kwa haki miongoni mwa nchi. Kwa kweli uvumbuzi wa teknolojia unaweza kupenya na kusambaa katika jamii husika iwapo tu walengwa wana kiwango kitakiwacho cha ujuzi na mtaji wa kutosha. Ni dhahiri kwamba, kutokana na tofauti kubwa zilizopo baina ya nchi hususani fursa ya kufikia elimu na maarifa ya kisayansi na teknolojia na bidhaa za kisasa za teknolojia hizo, mchakato wa utandawazi unaishia katika ongezeko la tofauti za kiuchumi na ustawi wa jamii baina ya nchi badala ya kupungua. Kutokana na mikikimikiki ya wakati huu mzunguko huria wa mtaji pekee hautoshelezi kuziba pengo lililopo baina ya nchi zinazoendelea na zile zenye viwanda.

364. Biashara inawakilisha sehemu muhimu ya mahusiano ya kimataifa na ya kiuchumi, ikitoa mchango thabiti katika maamuzi ya uzalishaji bidhaa mahususi na kukua kwa uchumi katika nchi mbalimbali. Leo kuliko zama zilizopita, biashara ya kimataifa – ikielekezwa vema – inakuza maendeleo na kuongeza ajira na kuwa chanzo cha rasilimali muhimu. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii mara kwa mara yametahadharisha uwepo wa kasoro za mitazamo katika biashara ya kimataifa,[752] ambayo mara nyingi kutokana na sera za kujilinda dhidi ya ushindani wa kutoka nje ya nchi zao, zinabagua bidhaa na mazao kutoka nchi changa na hivyo kuzuia ukuaji wa shughuli za kiviwanda na jitihada za kujipatia teknolojia za kisasa kwa nchi hizo.[753] Kuendelea kupungua kwa thamani ya mazao ghafi na kuongezeka kwa pengo baina ya nchi tajiri na zile maskini kumeyasukuma Majisterio kuhimiza umuhimu wa kuzingatia vigezo vya uadilifu kuwa vya msingi katika mahusiano ya kimataifa ya kiuchumi. Kutafuta manufaa kwa wote na kwamba mema ya dunia hii ni kwa wote; usawa katika mahusiano ya kibiashara; kujali haki na mahitaji ya walio maskini wakati wa kuandaa sera za kibiashara na ushirikiano wa kimataifa. La sivyo, “mataifa maskini yatabakia siku zote maskini wakati yale tajiri, utajiri wake utaendelea kuongezeka.”[754]

365. Mshikamano barabara katika zama za utandawazi unadai kwamba haki za binadamu zilindwe. Kuhusu suala hili, Majisterio inatahadharisha kwamba si tu “haijapatikana mamlaka ya kufaa ya kimataifa kusimamia utekelezaji wa haki za binadamu, uhuru na amani, bali pia kuna kusitasita sana katika jumuiya ya kimataifa kuhusu wajibu wa kuheshimu na kutekeleza haki za binadamu. Wajibu huu unagusa kila haki iliyo ya msingi, isipokuwa uteuzi na uchaguzi usiofuata taratibu zinazokubalika - mambo ambayo yanaweza kuipelekea jamii kukubaliana na mitindo ya kibaguzi na isiyo na haki. Vivyo hivyo, kumeanza kujitokeza pengo la kutisha baina ya orodha ya “haki” mpya zinazotetewa katika jamii zilizoendelea ambazo ni matokeo ya ustawi mkubwa na teknolojia – na haki msingi za binadamu ambazo hazijatekelezwa, hasa katika mazingira ya nchi zinazoendelea. Hapa zinafikiriwa, kwa mfano, haki ya kupata chakula na maji safi na salama ya kunywa, makazi na usalama, kujiamulia mambo yao wenyewe na uhuru wa masuala ambayo hawajaweza kuhakikishiwa na kufanikishiwa.”[755]

366. Kwa kadiri utandawazi unavyoenea, lazima ufuatane na uelewa mpevu wa taasisi za kiraia kuhusu kazi mpya ambazo taasisi hizo zinapaswa kufanikisha katika ngazi ya kimataifa. Tunashukuru kutokana na hatua thabiti zilizokwisha kuchukuliwa na taasisi hizi, itawezekana kuongoza mchakato huu wa ukuaji wa uchumi na fedha unaoendelea sasa duniani na kuuweka katika mfumo utakaohakikisha kwamba heshima ya haki za binadamu na haki binafsi zinatekelezwa, na pia kunakuwepo na mgawanyo wa rasilimali unaozingatia haki ndani ya nchi zenyewe na baina ya nchi mbalimbali: “Uhuru wa kibiashara unakuwa wa haki iwapo tu unaendana na madai ya haki.”[756]

Sharti pawepo na uangalifu mahususi kwa mazingira ya mahali na tofauti za kiutamaduni zinazotishiwa na mchakato wa kiuchumi na kifedha unaoendelea: “Utandawazi usiwe ukoloni mamboleo. Sharti uheshimu michepuko ya kitamaduni ambayo, katika upatanifu wa watu duniani, ni funguo za ufafanuzi wa kinachobakia kwao kuwa na thamani kubwa, ni pamoja na imani yao ya dini na taratibu zake, kwa sababu imani za kweli katika dini ni vielelezo bayana vya uhuru wa mwanadamu.”[757]

367. Katika zama za utandawazi, mshikamano kati ya vizazi lazima uhimizwe kwa nguvu: “Zamani, katika sehemu nyingi, mshikamano kati ya vizazi ulikuwa mtazamo asili wa kifamilia; ilikuwa pia ni wajibu wa jamii.”[758] Ni vema kwamba mtazamo huo unaendelezwa katika jumuiya za kisiasa za kitaifa, lakini tatizo hilo leo liko hata katika jumuiya za kisiasa za kimataifa, kwa madhumuni ya kuepusha athari mbaya za utandawazi kuwapata wale walio wahitaji na wasio na nguvu za kiuchumi. Mshikamano kati ya vizazi unahitaji mipango ya kimataifa kufanyika kwa kufuata kanuni ya mali za dunia ni kwa wote, zikiashiria kwamba ni haramu kimaadili na ni kukosa tija kiuchumi kuvibebesha vizazi vijavyo gharama za maendeleo ya wakati huu: Ni haramu kimaadili kwa sababu itakuwa ni kukwepa wajibu; ni kutokuwa na tija kiuchumi kwa sababu kurekebisha lililoharibika ni aghali kuliko kuzuia uharibifu. Kanuni hii itumike kwa makini zaidi – ingawaje si katika eneo hilo tu – kwa rasilimali zipatikanazo ardhini na kukinga dunia, na hili la mwisho ni suala nyeti kwa sababu ya utandawazi, kwani inahusisha dunia nzima kama mfumo mzima wa kiikolojia.[759]

b. Mfumo wa Kifedha wa Kimataifa

368. Masoko ya fedha si uvumbuzi wa leo: kwa muda mrefu sasa, na katika mitindo mbalimbali, yamekuwa yakijaribu kukidhi mahitaji ya kifedha katika sekta ya uzalishaji. Uzoefu wa historia unatufundisha kwamba bila mifumo ya kifedha kutosheleza, kukua kwa uchumi hakungekuwepo. Uwekezaji mkubwa wa uchumi wa soko wa kisasa haungewezekana bila ya dhima msingi ya upatanisho uliowezeshwa na masoko ya kifedha, ambayo kati ya mengi yaliyoibuliwa ni kuthamini mchango mwema wa uwekaji akiba katika mfumo mzima wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Iwapo kuanzishwa kwa kile kinachojulikana kama “soko la mitaji la kimataifa” kumeleta manufaa, shukrani kwa ukweli kwamba uwezekano mkubwa wa kuhamisha mitaji unawezesha sekta ya uzalishaji kufikia rasilimali, ingawaje kwa upande mwingine umeongeza hatari za kuwepo migogoro mikubwa ya kifedha. Sekta ya kifedha iliyokwisha shuhudia shughuli kubwa za kifedha zilizoendeshwa zikizidi shughuli halisi za uzalishaji, iko katika hatari ya kukua, kwa kadiri ya fikra zitokanazo na dhana zake yenyewe, bila ya yenyewe kuhusika kwenye misingi ya uchumi.

369. Uchumi wa kifedha unaokomea katika kujipatia fedha tu unakabiliwa na kukinzana na malengo yake yenyewe kwa kuwa umetengana na mizizi yake na kuacha kuona kusudio lake la asili. Kwa maneno mengine, umetekeleza dhima yake ya awali na ya lazima ya kuhudumia uchumi halisi na, hatimaye, kuchangia katika maendeleo ya watu na jumuiya ya binadamu. Katika mwanga wa kutokuwapo ulinganifu wowote wa uwezeshaji kunakofanywa na mifumo ya kifedha ya kimataifa, taswira nzima ni ya kutia wasiwasi bado: mchakato wa kuondoa vikwazo kwenye masoko ya fedha na uvumbuzi unapelekea kujiimarisha katika sehemu fulani tu za dunia. Hiki ni chanzo kikubwa cha ukiukaji wa maadili, kwa kuwa nchi zilizotengwa kwenye mchakato huo hazifaidiki, bali zimo hatarini kukumbwa na migogoro katika mifumo yao ya kiuchumi iliyosababishwa na mifumo ya kifedha kukosa uthabiti, na hasa iwapo nchi hizo ni dhaifu au zikiwa zinasumbuliwa na maendeleo duni.[760]

Kuongezeka ghafla kwa kasi ya michakato hii, ikiwamo ongezeko kubwa sana la thamani ya watawala wa taasisi za kifedha na kuenea upesi na kwa mtindo wa pekee sana kwa vyombo vipya na vya kisasa vya kifedha, kunatakiwa kwa haraka sana kupata suluhisho la kitaasisi litakaloweza kufanikisha kupatikana utengamano katika mfumo huu bila ya kupunguza uwezo na ufanisi wake. Kwa hiyo, ni lazima kuanzisha mfumo wa usanifu na urekebishaji utakaolinda utengano wa mfumo wa fedha iwapo utatanishi wowote utajitokeza, utakaokuza ushindani miongoni mwa asasi nyingine za kati na kuhakikisha uwazi mkubwa kwa faida ya wawekezaji.

c. Nafasi ya Jumuiya za Kimataifa Enzi za Uchumi wa Kidunia

370. Kutokana na serikali kupoteza muhimili wa uchumi, jumuiya ya Kimataifa sharti ioneshe utashi mkubwa katika kuongoza mwenendo wa uchumi duniani. Kwa kweli, moja ya matokeo muhimu ya mchakato wa utandawazi ni kwa Serikali za nchi kupoteza hatua kwa hatua usimamizi wa mwenendo wa mfumo wa uchumi wa kifedha nchini. Madola ya nchi mbalimbali yanalazimika wakati wa kufanya maamuzi ya kiuchumi na kijamii kuzingatia matarajio ya masoko ya fedha ya kimataifa na kulazimika kuaminika kwa taasisi za kifedha za kimataifa. Kwa sababu ya mikataba mipya ya kutegemeana baina ya taasisi za kifedha duniani, jitihada za asili za serikali kulinda masoko yao ya ndani zinaelekea kushindwa na, kutokana na kuibuka maeneo mapya ya ushindani, wazo la kuwapo kwa soko la kitaifa linatoweka.

371. Kwa kadiri mfumo wa kiuchumi – kifedha wa kimataifa unavyokomaa katika kujiratibu na kwa jinsi mchangamano wa shughuli zake unavyoongezeka, ni muhimu kuweka kipaumbele katika wajibu wa kudhibiti michakato hii, kuiongoza kwenye malengo ya kufikia kupata manufaa ya wote kwa familia ya binadamu. Na hapo linajitokeza hitaji la waziwazi si kwa serikali za nchi tu, bali kwa jumuiya ya kimataifa kubeba kazi ya kutoa maamuzi magumu ya kila siku kwa kutumia vyombo sahihi na fanikishi vya kisiasa na kisheria.

Kwa hiyo, ni muhimu kwa taasisi za kiuchumi na kifedha za kimataifa kutambua ufumbuzi wa kitaasisi unaofaa na kuoanisha mpango wa utendaji unaofaa kwa madhumuni ya kuleta mabadiliko ambayo, iwapo hali hii ingekubalika na kuachwa kuendelea kuwapo inavyotaka, ingelileta matukio yasiyo ya kawaida yenye kudhuru mno wale walio katika tabaka la wadhaifu wasio na uwezo wa kujitetea wenyewe.

Katika vyombo vya kimataifa, ni muhimu ukawepo uwakilishi wa kutosha wa watu wa hali na tabaka zote. Ni muhimu zaidi ya hayo kwamba “katika kutathmini matokeo ya maamuzi yao, vyombo hivyo siku zote vifikirie kwa makini wale watu wa nchi zisizo na umuhimu mkubwa katika soko la kimataifa, lakini ambazo zinaelemewa na mzigo wa mahitaji ya lazima, na hivyo ni tegemezi kwa maendeleo yao.”[761]

372. Uwanja wa siasa pia, kama ulivyo ule wa uchumi, hauna budi kupanua shughuli zake na kutoka nje ya mipaka ya kitaifa, hima ukiingia katika wigo wa utendaji wa kiulimwengu ambao pekee utaiwezesha kuongoza mchakato unaoendelea sio tu kwa vigezo vya kiuchumi, lakini pia kwa kadiri ya vigezo vya maadili. Lengo msingi ni kuongoza mchakato wa kiuchumi kwa kuhakikisha kwamba hadhi ya binadamu na maendeleo yake vinafikiwa kikamilifu na kwamba mtu anaheshimika, katika muktadha wa manufaa kwa wote.[762] Ili kutekeleza jambo hili inatakiwa kuharakisha kuunganisha taasisi zilizopo na kuunda mpya zitakazoweza kuwajibika kwa hilo.[763] Maendeleo ya kiuchumi, kwa kweli, yatakuwa ya kudumu iwapo tu yatafanyika katika uwanja unaoeleweka, ulio na kanuni za dhati na katika mpango mpana unaozingatia malezi ya kimaadili, kiraia na kiutamaduni ya familia yote ya binadamu.

d. Maendeleo Kamili ya Mwanadamu Katika Mshikamano

373. Mojawapo ya kazi zilizo za msingi kwa wale wanaohusika na masuala ya kiuchumi wa kimataifa ni kufanikiwa kupata maendeleo kamili ya mwanadamu katika mshikamano, ndio kusema, “kujali ubora wa kila mtu na wa mtu kamili.”[764] Kufanikiwa katika kazi hii, kunataka mtazamo wa kiuchumi, katika ngazi ya kimataifa unaohakikisha mgawanyo wa haki wa rasilimali zote na unaoonyesha kuelewa kuwapo kwa kutegemeana – kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni – ambako wakati huu kunawaunganisha watu na kuwafanya wajione wameunganika katika ukomo mmoja tu.[765] Matatizo ya kijamii yanazidi kuchukua sura ya kidunia. Hakuna serikali inayopambana nayo na kuyapatia ufumbuzi peke yake. Vizazi vya sasa vina uzoefu dhahiri wa hitaji la mshikamano na vina uelewa wa ulazima wa kuondokana na utamaduni wa kibinafsi.[766] Kuna uelewa mkubwa zaidi juu ya hitaji la kuwa na mitindo ya maendeleo inayotaka kubeba wajibu sio tu “wa kuinua maisha ya watu kufikia yale yanayopatikana katika nchi tajiri, ila wa kujenga maisha ya kufaa kwa nguvu za pamoja, kukuza kihalisia utu na ubunifu wa kila mtu, na pia kukuza uwezo wake katika kuuishi wito wake, na hivyo kuitikia wito wa Mungu.”[767]

374. Maendeleo yaliyo ya kibinadamu zaidi katika mshikamano yataleta pia manufaa kwa nchi tajiri zenyewe.  Katika nchi hizi zilizoendelea “kunaonekana kuwapo kwa maisha ya kufadhaisha, kutoweza kuishi na kufurahia vema maana ya uhai, ingawaje wamezingirwa na mali tele za kutumia. Hisia za mfarakano na kupoteza utu wao kumewafanya watu kujihisi kama kwamba wao ni sehemu tu ya mashine ya kuzalisha na kutumia wakiwa hawana namna ya kudhihirisha hadhi yao kama nafsi, walioumbwa katika sura na mfano wake Mungu.”[768] Nchi tajiri zimeonyesha uwezo wa kuleta hali bora za maisha, lakini mara nyingi kwa kumdhulumu binadamu na tabaka la jamii isiyoweza kujitetea. Haiwezekani kupuuza ukweli kwamba mipaka ya utajiri na umaskini inakutana katika jamii zenyewe, ziwe zilizoendelea ama zinazoendelea. Kwa kweli, kama vile tofauti za kijamii – hata kufikia hali ya maisha ya mateso na umaskini – zinavyoonekana katika nchi tajiri, vivyo hivyo, katika nchi zilizo nyuma katika maendeleo tunakutana uso kwa uso na vielelezo vya ubinafsi na jeuri ya utajiri ambako kunatia wasiwasi na kuzusha kashfa.”[769]

e. Hitaji la Elimu zaidi na Malezi ya Kiutamaduni

375. Kwa mtazamo wa Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii, uchumi ni kipengele kimoja tu na wigo mmoja katika shughuli nyingi za binadamu. Iwapo maisha ya kiuchumi tu ndio lazima kwa uhai, iwapo uzalishaji bidhaa na matumizi yake kungekuwa ndio kitovu cha maisha na tunu pekee ya jamii, ikishinda tunu nyingine zote, itakuwa si kutokana na mfumo wenyewe wa uchumi bali ni kutokana na mfumo mzima wa kijamii na kiutamaduni, ambao kwa kupuuzia wigo wa kimaadili na kidini, umedhoofishwa, hata kuishia na kujihusisha na uzalishaji mali na huduma pekee.”[770] Maisha ya binadamu, kama yalivyo maisha ya ushirikiano ya jamii, yasigeuzwe kuwa ya mtazamo wa kuwa na vitu, ingawaje mali ni muhimu sana kwa kuendelea kuishi na kwa kustawisha hali ya maisha. Kujijenga na kuongezeka kwetu katika kumtambua Mungu na kujitambua sisi wenyewe ni kwa msingi katika kufikia maendeleo kamili ya jamii ya binadamu.”[771]

376. Majisterio ikiwa inakabiliwa na maendeleo ya haraka ya teknolojia na uchumi, na mageuzi sawia ya michakato ya uzalishaji na utumiaji, inapambanua hitaji na kupendekeza elimu zaidi na malezi katika tamaduni, Kanisa linajua kwamba “kuhimiza kuwa na maisha yaliyo ya hali ya kuridhisha kiuhalali, lakini hakuzuii kutahadharisha uwepo wa wajibu mpya na hatari pia zihusikazo na awamu hii ya historia.. Katika kuainisha mahitaji mapya na njia mpya za kukidhi hayo, lazima kuongozwa na taswira ya kueleweka ya mtu inayoheshimu wigo zote za utu wake ikitanguliza na kuzipa umuhimu mkubwa zile za ndani na za kiroho zikifuatiwa na za tamaa za mwili na za mali .. Mfumo wa kiuchumi, kwa utashi wake tu, hauna vigezo vya kupambanua kwa usahihi baina ya njia mpya na adilifu za kukidhi mahitaji ya mwanadamu na mahitaji mapya potofu yanayozuia malezi ya busara. Hivyo, kazi kubwa ya uelimishaji na utamadunisho inatakiwa haraka, ikiwamo elimu kwa walaji katika kuchagua kwa busara, kujenga moyo imara wa uwajibikaji miongoni mwa wenye viwanda na hasa kati ya watu wa vyombo vya habari, na pia ulazima wa mamlaka za kijamii kuingilia kati pale inapobidi.”[772]

 

SURA YA NANE

JAMII YA KISIASA

1. MTAZAMO WA KIBIBLIA

a. Utawala wa Mungu

377. Mwanzoni mwa historia yake watu wa Israeli ni tofauti na watu wengine kwani hawana mfalme, na wanatambua utawala wa Yahwe pekee. Ni Mungu anayeingilia kati kwa niaba ya Waisraeli kwa kupitia watu wenye karama kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Waamuzi. Watu wanamwendea aliyekuwa wa mwisho wa hao, Samweli, nabii na mwamuzi, wakimwomba awateulie mfalme (taz. 1 Sam 8 :5; 10: 18-19). Samweli anawaonya Waisraeli kuhusiana na athari za utawala dhalimu (taz. 1 Sam 8:11-18). Hata hivyo, mamlaka ya Mfalme yanaweza kuonekana kama zawadi ya Yahwe anayekuja kuwasaidia watu wake (taz. 1 Sam 9:16). Mwishowe, Sauli anapata mpako na kuwa mfalme (taz. 1 Sam 10: 1-2). Matukio haya yanadhihirisha fadhaa iliyowafanya Waisraeli kuelewa ufalme kwa namna tofauti na vile ulivyokuwa ukieleweka kwa jirani zao. Mfalme, aliyeteuliwa na Yahwe (taz. Kum 17: 15; 1 Sam 9 :16) na aliyewekwa wakfu naye (taz. 1 Sam 16:12-14), anaonekana kama mtoto wa Mungu (taz. Zab 72). Mfalme, kwa hivyo, anakuwa mlinzi wa walio dhaifu na mdhamini wa haki kwa watu wake. Shutuma za manabii zinalenga haswa katika wafalme kushindwa kutekeleza wajibu hizo (taz. 1 Fal 21; Isa 10:14; Amo 2:6 – 8:48, Mik 3:1-4).

378. Mfano wa kwanza wa mfalme aliyechaguliwa na Yahwe ni Daudi ambaye mwanzo wake wa kiunyenyekevu ni mada inayopendelewa katika simulizi za kibiblia (taz. Sam 16: 1 – 13). Daudi ni mpokeaji wa ahadi (taz. 2 Sam 7 : 13 – 16; Zab 89: 2 – 38, 132; 11- 18), inayomweka mwanzoni mwa desturi maalumu ya kifalme, desturi ya “Kimasiha”. Bila ya kuangalia madhambi yote na uzinzi wa Daudi na warithi wake, desturi hii inafikia upeo wake katika Yesu Kristo, ambaye ni “mkamilifu” mpaka kwa Yahwe (yaani “ aliyewekwa wakfu na Bwana” (taz. 1 Sam 2 :35, 24:7, 11, 26:9, 16; Kut 30:22 – 32), Mwana wa Daudi (taz. Mt 1:1 – 17; Lk 3: 23 – 38; Rum 1:3).

Kushindwa kwa ufalme katika ngazi ya kihistoria hakusababishi kutoweka kabisa kwa mfano bora mfalme ambaye, katika uaminifu wake kwa Yahwe, atatawala kwa hekima na kutenda katika haki. Matumaini haya yanajitokeza mara kwa mara katika zaburi (taz. Zab 2,18,20,21,72) katika utabiri wa Masiha, mfano wa mfalme aliyejaliwa Roho wa Bwana, mwenye wingi wa hekima mwenye uwezo wa kuleta haki kwa maskini, anayengojewa katika wakati wa mwisho (taz. Isa 11:2 – 5, Yer 23:5 – 6). Akiwa mchungaji wa kweli wa watu wa Israeli (taz. Eze 34: 24,37:24) ataleta amani kwa mataifa (taz. Zek 9:9 – 10). Katika kitabu cha Mithali, mfalme anatambulishwa kama yule mwenye kutoa hukumu za haki na anayechukia sana udhalimu (taz. Mit 16:12),anayewahukumu maskini kwa usawa (taz. Mit 29:14) na ni rafiki wa walio na moyo safi (taz. Mit 22:11). Kuna udhihirisho wa taratibu wa tangazo ambalo Injili na maandiko mengine ya Agano Jipya yanaona kutimilika katika Yesu wa Nazareti, aliye mwisho katika utabiri uliotabiriwa katika Agano la Kale juu ya mfano wa mfalme.

b. Yesu na Mamlaka ya Kisiasa

379. Yesu anayakataa mamlaka dhalimu na ya kiimla ya watawala wa mataifa (taz. Mk 10:42) anakataa wao kujifanya waitwe wafadhili (taz. Lk 22:25), ingawaje hawapingi moja kwa moja watawala wa wakati wake. Katika maelezo yake kuhusu ulipaji wa kodi kwa Kaisari (taz. Mk 12:13 – 17; Mt 22:15 – 22; Lk 20: 20 –26), anathibitishwa kwamba ni lazima tumpe Mungu yaliyo ya Mungu, akiwa na maana ya kulaani kila jaribio la kuufanya uwezo wa kilimwengu kuwa wa Kimungu na wa kiimla: Mungu peke yake ana uwezo wa kudai kila kitu kutoka kwa mtu.

Yesu Masiha aliyeahidiwa alipigana na kushinda kishawishi cha umasiha wa kisiasa, ulio na sifa ya ukandamizaji wa mataifa (taz. Mt 4:8 – 11; Lk 4:5 – 8). Yeye ni mwana wa mtu aliyekuja “kutumikia na kutoa uhai wake” (taz. Mk 10:45; Mt 20:24 – 28; Lk 22:24 – 27) wanafunzi wake wakiwa wanajadiliana kati yao kujua aliye mkubwa, Yesu aliwafundisha kwamba wanapaswa kujifanya wadogo na watumishi wa wote (taz. Mk 9:33 – 35), akiwaeleza wana wa Zebedayo, Yakobo na Yohane, wanaotaka kuketi mkono wake wa kulia, njia ya msalaba(taz. Mk 10:35 – 40; Mt 20 – 23).

c. Jumuiya za Kikristo za Mwanzo

380. Utii, usio wa woga bali “kwa sababu ya dhamiri” (taz. Rum 13: 5), kwa mamlaka halali unaendana na mpango uliowekwa na Mungu. Mtakatifu Paulo anafafanua mahusiano na wajibu anaopaswa Mkristo kuwa nao kwa wenye mamlaka (taz. Rum 13:1 – 7). Anasisitiza juu ya wajibu wa kiraia kulipa kodi: “Wapeni wote haki zao; ulipaji kodi muda unapowadia; na ushuru kwa wanaohusika; astahiliye hofu, astahiliye heshima” (taz. Rum 13: 7). Mtume hakika kadhamiria kuhalalisha kila mamlaka iliyo kwa ajili ya kuwasaidia Wakristo kwa “ kuwa waangalifu kwa yaliyo mema machoni pa watu” (taz. Rum 12: 17) ikiwa ni pamoja na mahusiano yao na wenye mamlaka kwa kuwa walio na mamlaka wako katika kumtumikia Mungu kwa ajili ya mema ya mtu (taz. Rum 13:4; 1 Tim 2:1 –2; Tit 3:1) na “Kutekeleza ghadhabu (ya Mungu) kwa watenda mabaya “ (Rum 13: 4).

Mtakatifu Petro anawasihi Wakristo asemapo “tiini kila kiamriwacho na watu kwa ajili ya Bwana” (1 Pet 2:13). Mfalme na watawala wake wana wajibu “wa kuwaadhibu watenda mabaya na kuwasifu watenda mema” (1 Pet 2:14). Mamlaka yao hayo sharti “yaheshimiwe” (taz. Pet 2:17), yaani, yatambuliwe kwa sababu Mungu anadai mwenendo sahihi” utakaowanyamazisha ujinga wa watu wapumbavu” (1 Pet 2:15). Uhuru usitumike kwa kusisitiza ubaya, bali kumtumikia Mungu (taz. 1 Pet 2:16). Inahusu utii ulio huru wa kuwajibika kwa mamlaka iwezeshayo haki kuheshimika, ikihakikisha manufaa kwa wote.

381. Kuwaombea watawala, Mtakatifu Paulo alipendekeza hata alipokuwa akiteswa, kunadhihirisha kile kinachopaswa kuhakikisha kuwapo na maisha ya kisiasa yaliyo tulivu na ya amani yakiongozwa kwa uchaji wa Mungu na heshima ya utu (taz. 1Tim 2:1 – 2). Wakristo lazima “wawe tayari kwa kila kazi njema” (Tit 3:1), wakionesha “upole wote kwa watu wote” (Tit 3:2) katika utambuzi kwamba wameokolewa siyo kwa matendo yao wenyewe isipokuwa kwa huruma yake Mungu. Pasipo “kuoshwa kwa kuzaliwa kwa mara ya pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu, ambaye alitumwagia kwa wingi, kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu” (Tit 3: 5 – 6), watu wote ni wapumbavu, tukiwa waasi, tumedanganywa, huku tukitumikia tamaa na anasa za namna nyingi, tukiishi katika uovu na husuda, tukichukiza na kuchukiana (Tit 3:3). Hatupaswi kusahau hali yetu duni ya ubinadamu iliyochafuliwa na dhambi, lakini iliyokombolewa kwa upendo wa Mungu.

382. Itokeapo mamlaka ya mwanadamu kuvuka kikomo kilichowekwa na Mungu, hujikuza na kujifanya Mungu na kudai utii kamili; hapo mamlaka huwa mnyama kadiri ya Ufunuo, mfano wa mtesaji mwenye uwezo wa kifalme “aliye lewa damu ya watakatifu na damu ya mashahidi wa Yesu” (Ufu 17:6). Huyo mnyama anatumikiwa na “nabii wa uwongo” (Ufu 19: 20) ambaye kwa kutumia ishara za kughilibu hushawishi watu kumwabudu. Maono haya ni ashirio la kinabii likionesha mitego aitumiayo shetani kutawala watu, akiangalia kuingia rohoni mwao kwa udanganyifu. Lakini Kristo ni Mwanakondoo mshindi ambaye, katika nyakati zote za historia ya mwanadamu, anashinda kila uwezo unaojifanya kutokuwa na kiasi wala mipaka. Mbele ya uwezo wa namna hiyo, Mtakatifu Yohane anapendekeza upinzani wa mashahidi; kwa njia hii, waamini washuhudie kwamba uoza na uwezo wa shetani unashindwa, kwa sababu hauna tena mamlaka juu yao.

383. Kanisa linatangaza kwamba Kristo, mshindi wa kifo anatawala juu ya ulimwengu ambao yeye mwenyewe ameukomboa. Ufalme wake unajumlisha hata nyakati za sasa na utakwisha pale kila kitu kitakapokuwa kimekabidhiwa kwa Baba na historia ya mwanadamu itakapokuwa imefikia mwisho wake katika hukumu ya mwisho (taz. 1 Kor 15: 20 – 28). Kristo anadhihirisha kwamba mamlaka ya kibinadamu, wakati wote, hamu yake ya kutawala katika maana yake ya kweli na kamili ikichukuliwa kama ni huduma, wakati wote huingia katika kushawishiwa. Mungu ni mmoja aliye Baba, na Kristo ni mwalimu mmoja, wa watu wote, na watu wote ni ndugu. Enzi ni mali ya Mungu. Hata hivyo, “Bwana hakutaka kujilimbikizia mwenyewe mamlaka yote. Anakiaminisha kila kiumbe kazi ambazo kinaweza kuzifanya kadiri ya mawazo ya hali yake. Mtindo huu wa utawala unatakiwa kufuatwa katika maisha ya kijamii. Anavyofanya Mungu katika kuutawala ulimwengu kunatoa ushuhuda mkubwa sana wa heshima kubwa ya uhuru wa binadamu ambao unatakiwa uwavuvie hekima wale wanaozitawala jumuiya za wanadamu. Hawa wanatakiwa kuwa kama wahudumu wa maongozi ya Mungu”.[773]

Ujumbe wa Biblia umetupatia maongozi yasiyo na mwisho kwa ajili ya tafakari juu ya mamlaka ya kisiasa, tukikumbuka kwamba yanatoka kwa Mungu na ni sehemu ya utaratibu alioumba yeye. Mpango huu unatambulikana na dhamiri ya mwanadamu na katika maisha ya jamii, unapata ukamilifu wake katika ukweli, haki, uhuru na mshikamano uletao amani.[774]

 

II. MSINGI NA MADHUMUNI YA JUMUIYA YA KISIASA

 

a. Jumuiya ya Kisiasa, Mtu Nafsi na Jamii

384Mtu nafsi ndiye msingi na lengo la maisha ya kisiasa.[775] Akiwa amejaliwa hulka ya kufikiri, mtu mwenyewe anawajibika kwa maamuzi yake na ana uwezo wa kufuatilia mambo yaliyo ya maana kwa maisha yake binafsi na kwa jamii. Akiwa mrithi kwa Mwenyezi na kwa wengine katika sifa na tabia zimtambulishazo. Ni katika mahusiano tu na Mwenyezi na wengine ndipo mtu anafikia ukamilifu wake wote. Hii inamaanisha kwamba mtu aliye kwa hulka yake kiumbe wa kijamii na wa kisiasa “maisha ya kisiasa sio kitu cha ziada”[776] isipokuwa ni sehemu ya wigo muhimu na usioweza kufutika.

Jumuiya ya kisiasa asili yake ni katika maumbile ya mwanadamu ambaye dhamiri yao “inawadhihirisha na kuwaunganisha kutii [777] mpango ambao Mungu ameuandika katika viumbe wake wote:” mpango wa kimaadili na wa kidini. Na ni mpango huu na si fikira isiyofungamana, ni utaratibu wa mali ulio na uhalali mkubwa katika kupata suluhisho la matatizo yahusuyo maisha yao kama watu binafsi na wanajamii, na matatizo baina ya mataifa na mahusiano yao.[778] Mpango huu sharti ugunduliwe taratibu na uendelezwe na binadamu wenyewe. Jumuiya ya kisiasa, ukweli wa asili katika mwanadamu, ipo ili kukamilisha yale ambayo yasingeliweza kupatikana: maendeleo kamili ya kila wanajamii, anayealikwa kushiriki kwa dhati katika kuleta manufaa kwa wote,[779] kwa msukumo wa asili wa kupenda yaliyo ya kweli na mema.

385. Jumuiya ya kisiasa inang’amua wigo wake halisi inapojihusisha na watu. “kwa hakika jumuiya ya kisiasa inakuwa mfumo na chombo cha kuratibu umoja wa watu haswa.”[780] Neno “watu” halina maana ya kundi lisilo na muundo wowote, umma usiojimudu uliopo kuendeshwa na kutumiwa tu, isipokuwa ni jamii ya watu, kila mmoja wao “akiwa kwake na katika namna yake”[781] anaweza kuchangia maoni yake kuhusu mambo ya umma na ana uhuru wa kueleza maoni yake ya kisiasa na kuyawezesha yasaidie katika kufikia manufaa kwa wote. Watu “wapo katika utimilifu wa maisha ya wanawake na wanaume wanaounda jamii hiyo; kila mmoja wao. ni nafsi atambuaye wajibu wake na ushawishi wake.”[782] Wale waliomo katika jumuiya ya kisiasa, ingawaje kimfumo wameungana na wengine, kama watu, wanabakia ni nafsi huru katika ngazi ya uwepo binafsi na kwa malengo ya kufanyia kazi.

386. Ishara msingi ya watu ni kushirikishana maisha na tunu, jambo lililo chimbuko la ushirika wa kiroho na maadili. Jamii ya binadamu sharti kimsingi itambulike kuwa ni ya kiroho. Kwa utambuzi huo na katika mwanga wa ukweli, watu hawana budi kushirikishana ujuzi wao, watiwe moyo kujitafutia karama za kiroho, kwa pamoja wajipatie furaha itokanayo na mazuri ya ulimwengu, wakati wote wawe radhi kurithisha kwa wengine urithi wao mwema na wajitahidi kupokea na kuishi mafanikio ya kiroho ya wengine. Fadhila hizi sio tu zinashawishi, bali pia zinaonesha lengo na upeo kwa yote yahusuyo sura za tamaduni, taasisi za kiuchumi na kijamii, mifumo ya kisiasa, kisheria, na taratibu nyingine zote ambazo kwazo zinaidhihirisha jamii na daima kuistawisha.[783]

387. Kila jamii ya watu kwa kawaida huendana na kuwepo kwa taifa lake, lakini kwa sababu mbalimbali mipaka ya taifa haiendani na mipaka ya makabila mbalimbali.[784] Hivyo, suala la wachache katika jamii hujitokeza, na kihistoria limekua ni chanzo cha mapigano ambayo siyo machache. Majisterio inakazia kwamba wachache ni kundi la watu wenye haki na wajibu, zaidi ya yote wana haki ya kuwapo, ambayo “inaweza kupuuzwa kwa namna nyingi ikiwemo ile inayovuka mipaka ambayo ni kuwakataa, kuwatendea vitendo vya wazi na vya kisiri kama vile mauaji ya halaiki.”[785] Zaidi ya hayo, walio wachache wanayo haki kushiriki utamaduni wao unaojumuisha lugha yao, kudumisha imani ya dini zao, ikiwemo ile ya huduma za kuabudu. Katika kutaka kihalali kuheshimiwa kwa haki zao walio wachache wanaweza kusukumwa kudai madaraka hata ikibidi kutaka uhuru wao kamili. Katika hali hiyo nyeti inayohitaji uangalifu mkubwa, mazungumzo na majadiliano ndio njia muafaka kufikia amani. Katika hali yoyote ile, njia ya kigaidi si halali na ni dhalimu kwa kusudio linalotafutwa. Watu walio wachache nao wana wajibu zao ikiwamo, kufanya kazi kwa lengo la manufaa kwa wote katika Nchi wanamoishi. Ikumbukwe walio wachache wana wajibu wa kukuza uhuru na hadhi ya kila mmoja wa watu wao na kuheshimu maamuzi ya kila mtu hata ikiwa mmoja wao angeamua kutumia desturi za walio wengi.”[786]

b. Kutetea na Kuhamasisha Haki za Binadamu

388. Kuweka maanani kwamba mtu mwenyewe ndiye mwanzishaji na kusudio la jumuiya ya kisiasa, kunamaanisha awali ya yote, kutambua na kuheshimu hadhi ya mtu kwa kutetea na kukuza haki za msingi za binadamu zisizoweza kuondolewa kwa vyovyote: “Katika nyakati zetu hizi manufaa kwa wote yanahakikishwa iwapo haki binafsi na wajibu vinatekelezwa.”[787] Haki na wajibu za mtu zinabeba muhtasari kamili wa matakwa msingi ya kimaadili na kisheria yanayopaswa kuongoza uundaji wa jumuiya ya kisiasa. Masharti haya yanafanya taratibu halisi ambazo ni msingi wa sheria chanya na haziwezi kupuuzwa na jumuiya ya kisiasa kwa sababu katika uhalisia wa uwepo na katika kusudio la mwisho mtu mwenyewe ni zaidi ya jumuiya ya kisiasa. Sheria chanya sharti ihakikishe kwamba mahitaji msingi ya binadamu yanapatikana.

389. Jumuiya ya kisiasa inatafuta manufaa ya wote inapojitahidi kuweka mazingira mazuri yenye kuwezesha wananchi kuishi haki zao na kutekeleza kwa ukamilifu wajibu wao. Uzoefu umetufundisha kwamba mamlaka isipochukua hatua zifaazo za kiuchumi, kisiasa na za kiutamaduni, tofauti baina ya raia zinaelekea kuongezeka zaidi na zaidi, hasa katika ulimwengu wa kisasa, na matokeo yake ni ukiukaji wa haki za binadamu na utekelezaji wa wajibu wao kushindikana.”[788]

Ili kuwezekana kufikia kikamilifu lengo la kupata manufaa kwa wote kunatakiwa jumuiya ya kisiasa kubuni utekelezaji ambao unatetea haki za binadamu na wakati huohuo unazihamasisha na kuzikuza. Isitokee kwamba watu fulanifulani au makundi maalumu yanapata faida kutokana na ukweli kwamba maslahi yao yalipata utetezi wa upendeleo. Pia isitokee kwamba serikali katika jitihada zake za kutetea haki hizi zinakuwa ni kikwazo kwa wananchi kuziishi na kuzidhihirisha haki hizo.”[789]

c. Maisha ya Kijamii Katika Msingi wa Urafiki wa Kiraia

390. Maana ya kina ya maisha ya kijamii na kisiasa haitokani moja kwa moja na orodha ya haki na wajibu za mtu. Maisha katika jamii yanachukua maana yake yote yakiwa yamejikita katika urafiki na undugu wa kijamii.[790] Eneo la haki kwa kweli ni mle ambamo maslahi yanatetewa, kutoingiliwa kati, kulinda bidhaa na usambazaji wake kwa kuzingatia kanuni zilizowekwa. Eneo la urafiki, kumbe ni kutojipendelea, kutoambatana na mali, kutoa kwa moyo na kujali mahitaji ya wengine.[791] Urafiki wa kijamii[792] ukieleweka hivyo, unakuwa njia ya kweli ya kutimiza kanuni ya udugu, isiyoweza kutengana na uhuru na usawa.[793] Kwa sehemu kubwa, kanuni hii haijatekelezwa katika hali halisi ya jamii ya kisiasa ya sasa kwa sababu ya ushawishi wa ubinafsi na itikadi za umiliki wa pamoja.

391. Jumuiya inakuwa na misingi imara ikijieleza katika kumjali mtu kamili na manufaa ya wote. Katika hali hiyo, sheria inafafanuliwa, inaheshimika na kutekelezwa kwa kuzingatia mwelekeo wa mshikamano na kujitolea kwa ajili ya jirani. Haki inataka kuwa kila mtu aweze kufurahia mali yake na haki zake; na hii inaweza kufikiriwa kuwa ndicho kipimo cha chini kabisa cha upendo.[794] Maisha ya kijamii yanaelekea kuwa ya kiutu zaidi kwa kadiri yanavyodhihirishwa na uwepo wa jitihada za kukuza uelewa wa lengo linalotafutwa, ambalo ni “ustaarabu wa upendo”[795]

Mwanadamu ni nafsi, si tu mmoja wapo.[796] Neno “nafsi” linaonyesha “asili ya mtu aliyojaliwa, akili na utashi.[797] Kwa hiyo, mtu ni halisi, aliye bora kuzidi kitu chochote ambacho hufuata sifa na mahitaji yake tu. Mwanadamu, kwa kweli ingawaje anashiriki kwa vitendo katika miradi iliyotumiwa kukidhi mahitaji yake katika familia yake na katika jumuiya ya kijamii na kisiasa, hawezi kupata ukamilifu wake mpaka anavuka nje ya hisia yake ya mahitaji na kuingia katika wigo wa kukirimiwa na hutumikiwa, ambao unaendana vema na asili yake na wito wa jumuiya.

392. Amri ya Upendo ya Injili inawaangazia Wakristo maana ya kina ya maisha ya kisiasa. Ili kuyafanya maisha kuwa ya kiutu kweli, “hakuna njia bora iliyoko kuliko kukazia dhamira ya haki, ukarimu na nia ya kuhudumia ili kupata manufaa ya wote, na kuimarisha imani msingi kuhusu asili ya kweli ya jumuiya ya kisiasa juu ya matumizi sahihi na mipaka ya mamlaka ya umma.”[798] Lengo wanalopaswa kujiwekea waamini liwe ni la kujenga mahusiano ya kijumuiya baina ya watu. Mtazamo wa Kikristo wa jamii ya kisiasa unaipa umuhimu mkubwa thamani ya Jumuiya, ikiwa ni kielelezo cha mpangilio wa maisha katika jamii na vilevile mtindo wa maisha ya kila siku.

 

III MAMLAKA YA KISIASA

 

a. Msingi wa Mamlaka ya Kisiasa

393. Kanisa limefikiria daima namna tofauti ya kuyaelewa mamlaka, uangalifu ukiwa ni kutetea na kupendekeza mfano wa mamlaka yatokanayo na asili ya kijamii ya mtu mwenyewe. “Kwa kuwa Mungu aliwafanya watu wanajamii kwa asili na kwa kuwa hakuna jamii inayoweza kushikamana pamoja isipokuwa mmoja wao anakuwa juu ya wote akiwaongoza katika jitihada za dhati kupata yaliyo bora kwa ajili ya manufaa ya wote. Kila jamii iliyostaarabika lazima iwe na mamlaka tawala na mamlaka hii si kwa kiwango pungufu ya kile cha jamii yenyewe, ina chanzo chake katika asili, hivyo ina Mungu akiwa muumbaji wake.”[799] Kwa hiyo, mamlaka ya kisiasa ni lazima yawepo[800] kihalali na hayana mbadala katika maisha ya kijamii.[801]

394. Mamlaka ya Kisiasa haina budi kuhakikisha kunakuwepo taratibu na uadilifu katika maisha ya kijamii, bila kuingilia shughuli huru za watu binafsi na makundi, bali uhuru huo yapasa kuongoza na kuujengea nidhamu, kwa kuheshimu na kutetea uhuru wa mtu binafsi na wa wanajamii kwa madhumuni ya upatikanaji wa manufaa ya wote. Mamlaka ya kisiasa ni chombo cha uratibu na uongozi ambacho kwa walio wengi pamoja na asasi za ushirika watakuwa na maisha ya kutegemeana, ambapo taasisi na taratibu vitatumika kwa ustawi wa mwanadamu kamili. Mamlaka ya kisiasa kwa kweli, ikiwa katika jumuiya au katika taasisi za kiserikali, lazima yatumike ndani ya mipaka ya maadili na kwa niaba ya maamuzi endelevu ya manufaa kwa wote kwa kuzingatia taratibu za kisheria zilizo halali. Hali ikiwa hivyo wananchi wanabanwa na dhamiri zao kutii.”[802]

395. Watawala wa mamlaka ya kisiasa ni watu katika ujumla wao wakiwa wao wenyewe ndio wenye enzi. Katika namna mbalimbali, watu hawa hukabidhi mamlaka yao kwa wawakilishi wao waliowachagua kwa uhuru, lakini hujibakizia haki yao ya kutetea enzi hii kwa kutathmini utendaji wa wale waliowapa wajibu wa kutawala na kwa kuwabadilisha iwapo utendaji wao si wa kuridhisha. Ingiwaje haki hii itatumika katika kila mfumo wa kisiasa, utawala wa kidemokrasia, kutokana na taratibu zake za uthibitisho, unawezesha na kuhakikisha matumizi yake kamili.[803] Ridhaa pekee ya watu, kwa hali yoyote, si kigezo cha kutosheleza kuridhia kwamba ni “haki” namna mamlaka ya kisiasa yanavyotumika.

b. Mamlaka Kama Nguvu ya Kimaadili

396. Mamlaka sharti yaongozwe kwa sheria ya kimaadili. Heshima yake inatokana na kutekelezwa kwake katika muktadha wa taratibu ya kimaadili,[804]” ambao unaotokana na Mungu aliye asili na mwisho wake.”[805] Kwa sababu ya ulazima wake wa kutegemea taratibu za kimaadili, ambazo zinatangulia na ndio msingi wake kwa sababu ya madhumuni yake na watu inayopaswa kuwatumikia, mamlaka hayawezi kuchukuliwa kama uwezo uliobainishwa kwa vigezo vyenye asili ya kijamii na kihistoria peke yake. “Kuna wengine ambao hukana kuwepo kwa utaratibu unaopita ufahamu wa binadamu, uliyo kamili, ulio na enzi na kuwafungamanisha wote sawa kwa ahadi zake. Na pale ambapo sheria ya haki haizingatiwi na wote, watu wasitegemee kufikia makubaliano ya wazi katika masuala muhimu.”[806] Daraja hili “halina uwepo, isipokuwa katika Mungu, likitenganishwa na Mungu lazima lisambaratike.”[807] Ni kutokana na taratibu za kimaadili mamlaka hupata uwezo wake wa kuamuru na kuwajibisha[808] na uhalali kimaadili,[809] si kutokana na utashi usio na taratibu zinazokubalika au kutokana na kiu au uchu wa madaraka,[810] na ina wajibu wa kutafsiri na kuhuisha daraja hii katika matendo halisi ya kupata manufaa kwa wote.[811]

397. Mamlaka sharti yatambue, yaheshimu na kukuza tunu muhimu za kiutu na kimaadili. Hizi ni za asili na zinatiririka kutoka katika ukweli kamili wa mwanadamu zikidhihirisha na kulinda heshima ya nafsi, ni tunu ambazo hakuna mtu, wala umma, au Serikali inayoweza kuzitengeneza, kuzibadilisha au kuziangamiza.”[812] Hizi tunu hazina chimbuko lake katika maoni ya muda au yanayobadilikabadilika ya “wengi”, isipokuwa sharti yakubalike tu, yaheshimiwe na kutetewa kama sehemu asili ya lengo la sheria ya kimaadili, sheria asili iliyoandikwa katika moyo wa mwanadamu (taz. Rum 2:15) na kanuni rejea ya sheria za nchi.[813] Iwapo kutokana na kiwingu cha kusikitisha kinachopotosha dhamiri kingefanikiwa kutia mashaka juu ya misingi ya sheria ya kimaadili,[814] mfumo wa kisheria wa Serikali wenyewe ungetikisika hadi kwenye mizizi yake, na kugeuzwa kuwa si chochote, bali kuwa taratibu za udhibiti wa utendaji wa makundi yenye mivuto mbalimbali na kinzani.[815]

398. Mamlaka hayana budi kutunga sheria zenye haki, yaani, sheria zinazoendana na heshima ya mwanadamu na yanayohitajiwa kwa fikira sahihi. “Sheria za kibinadamu ni sheria, iwapo zitaafikiana na fikira sahihi na hivyo zinatokana na sheria ya milele. Endapo, kwa hali yoyote, sheria inapingana na mantiki, inaitwa sheria dhalimu; katika hali hiyo, inakoma kuwa sheria na badala yake huwa ni kitendo cha ukatili.”[816] Mamlaka inayotawala kwa urazini haiwaongozi wananchi katika mahusiano ya kila mtu kuwajibika kwa mwingine bali kwa mahusiano ya kuheshimu taratibu za kimaadili na, hivyo, kwa Mungu mwenyewe aliye chanzo cha utaratibu huo.[817] Hivyo anayemwasi mwenye mamlaka, “hushindana na agizo la Mungu” (Rum 13: 2).[818] Kwa mantiki hiyo, iwapo mamlaka ya umma – iliyo na mwanzo wake katika asili ya mwanadamu na iliyo katika daraja lililowekwa na Mungu tokea mwanzoni[819] – inaacha kufuatilia yaliyo ya manufaa kwa wote, huwa inatelekeza kusudio la uwepo wake na hivyo kupoteza uhalali wake.

c. Haki ya Pingamizi kwa Kufuata Dhamiri

399. Raia analazimika katika dhamiri kutofuata sheria za serikali zinapokuwa kinyume cha mpango wa maadili, haki za msingi za binadamu au mafundisho ya Injili.[820] Sheria dhalimu husababisha matatizo ya kutatanisha ya dhamiri kwa watu walio adilifu: Wanapotakiwa kushiriki katika matendo maovu kimaadili ni lazima wakatae.[821] Baki ya kwamba ni wajibu wa kimaadili, kukataa kwa namna hiyo ni haki msingi ya binadamu ambayo, hivyo ilivyo, Sheria za nchi zinatakiwa kuitambua na kuitetea. “Wale wenye kukimbilia njia ya pingamizi kwa kufuata dhamiri, lazima watetewe siyo tu dhidi ya adhabu za kisheria, bali pia dhidi ya athari hasi katika uwanja wa sheria, nidhamu, uchumi na taaluma.”[822]

Ni wajibu mkubwa wa dhamiri kutoshiriki, hata ukitakiwa rasmi, katika mambo ambayo, ingawaje yameruhusiwa kwa kadiri ya sheria za nchi, ni kinyume cha Sheria ya Mungu. Ushiriki wa namna hiyo kwa kweli hauwezi kuhalalishwa kwa njia yoyote, hata kwa visingizio vya kuheshimu uhuru wa wengine wala kwa utetezi kwamba ilikuwa halali kwa sheria za nchi. Hakuna awezaye kukwepa kuwajibika kwa matendo yake, na yote yatahukumiwa na Mungu mwenyewe kwa kadiri ya wajibu huu (taz. Rum 2: 6: 14: 12).

d. Haki ya Kupinga

400. Kwa kufahamu kwamba sheria ya maumbile ndiyo msingi wa sheria ya Serikali, na kwamba ndiyo iwekayo mipaka yake, kunamaanisha ni kukubali kuwa ni halali kupinga mamlaka iwapo itafanya uvunjaji mkubwa au wa mara kwa mara wa misingi muhimu ya sheria ya maumbile. Mtakatifu Tomaso wa Akwino anaandika kwamba “mtu analazimika kutii. kama itakiwavyo na mpango wa haki.”[823] Sheria ya maumbile kwa hiyo ndio msingi wa haki ya kupinga.

Kunaweza kuweko njia nyingi tofauti za haki hii kuweza kutumiwa; vivyo hivyo, kunaweza kuweko malengo mbalimbali ya kufuatilia. Pingamizi kwa mamlaka ni kwa madhumuni ya kuthibitisha uhalali wa uwepo wa mtazamo tofauti wa mambo, iwapo nia ni kufanikisha mabadiliko kiasi, kwa mfano, kurekebisha sheria fulani, au kupigania mabadiliko ya kimsingi katika hali husika.

401. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanadokeza vigezo vya kutumia haki ya kupinga: “Kupinga ukandamizaji wa mamlaka ya kisiasa kwa kutumia silaha si halali, isipokuwa kama hali zifutazo zinakuwepo: (1) kwamba kuna uvunjaji wa hakika, mkubwa na ulioendelezwa wa haki za msingi; (2) kwamba njia nyinginezo za kutatua tatizo lililopo zimejaribiwa bila mafanikio; (3) kwamba upingamizi wenyewe hautachochea ghasia mbaya zaidi; (4) kwamba kuna tumaini thabiti la mafanikio; (5) kwamba haiwezekani kwa kweli kuona mbele jawabu bora zaidi.”[824] Kimbilio la kutumia silaha linaonekana kuwa ni njia ya mwisho ili kukomesha “udhalimu uliojidhihirisha kwa muda mrefu ambao ungeleta madhara mabaya kwa haki msingi za watu na kuhatarisha jitihada za kufikia hali ya kupata manufaa ya wote nchini.”[825] Kutokana na ukubwa wa hatari inayoweza kusababishwa na uamuzi wa kutumia silaha wakati wa sasa inapendekezwa upinzani baridi utumiwe, ambao “ni namna inayokubaliana na taratibu za maadili na iliyo matarajio mazuri ya kufanikiwa.”[826]

e. Utoaji Adhabu

402. Kwa madhumuni ya kutetea mema ya wote, Serikali halali lazima itumie haki yake na wajibu wa kutoa adhabu kwa kufuatana na uzito wa uhalifu uliotendeka.[827] Serikali ina wajibu mara dufu kusitisha tabia potofu dhidi ya haki za binadamu na kanuni msingi za maisha ya kijamii, na kurekebisha, kwa kutumia mfumo wa adhabu, madhara yaliyosababishwa na uhalifu. Katika utawala wa kisheria, uwezo wa kutoa adhabu imepewa Mahakama: “katika kuainisha mahusiano ya kufaa baina ya mamlaka ya kutunga sheria, serikali na mahakama, Katiba za mataifa ya kisasa zinayahakikishia mahakama uhuru kamili katika wigo wa sheria.”[828]

403. Adhabu si kwa madhumuni ya kulinda utaratibu wa umma tu na kuhakikisha usalama wa watu; ni chombo cha kumrekebisha mhalifu pia, urekebishaji unaochukua uadilifu wa kufidia iwapo mhalifu kwa hiari yake mwenyewe anaipokea adhabu yake.[829] Kuna azma mbili katika hili. Kwa upande mmoja, kuhimiza moyo wa kumrejesha katika jamii aliyekuwa amefungwa; kwa upande wa pili, kukuza haki ya upatanisho, haki yenye uwezo wa kurejesha katika mahusiano ya kijamii yaliyovurugwa na uhalifu uliotendwa.

Kuhusu suala hili, shughuli wanayopaswa kutenda wahudumu wa kiroho magereza ni muhimu, siyo tu katika uwanja wa dini bali pia katika kutetea hadhi ya walio kifungoni. Jambo la kusikitisha, mazingira ambamo wafungwa wanaishi hayawezeshi kuwepo heshima ya utu wao; mara nyingi, magereza pamekuwa mahali ambamo uhalifu mpya unatendeka. Hata hivyo, mazingira ya vyombo vya adhabu yanaleta fursa ya kutoa ushuhuda wa Kikristo wa kuonyesha kujali masuala ya kijamii: “Nilikuwa. kifungoni, mkanijia” (Mt 25: 35 – 36).

404. Utendaji wa wale walio na dhamana ya kuthibitisha uhalifu wa watu, ambao siku zote ni jukumu la mtu binafsi, lazima ujitahidi kuwa na uchunguzi wa makini sana wa ukweli na lazima uendeshwe kwa kuheshimu haki za binadamu; hii inamaanisha kuhakikisha kunakuwepo haki za wahalifu sambamba na za wasio na kosa. Kanuni ya kisheria inayozuia kutolewa adhabu kabla ya kuthibitishwa kwa uhalifu sharti izingatiwe.

Katika kufanya upelelezi, sheria inayozuia matumizi ya mateso, hata katika uhalifu mkubwa, sharti ifuatwe: Mfuasi wa Kristo anakataa kutumia njia za namna hii, ambazo hakuna chochote kinachoweza kuzihalalisha, na ambamo heshima ya mtu inadhalilishwa kwa mtesaji kama ilivyo kwa mhanga wa mateso hayo.”[830] Vyombo vya kisheria vya kimataifa vinavyojihusisha na haki za binadamu vinakataza kwa usahihi kabisa matumizi ya mateso na kuielezea kanuni hiyo kuwa kamwe isivunjwe kwa sababu zozote. Kadhalika imekataza “matumizi ya kuwekwa kizuizini au mahabusu kwa madhumuni ya kupata taarifa muhimu za kuendeshea mashtaka.”[831] Zaidi ya hayo, ihakikishwe kuwa “mashtaka yanaendeshwa haraka: mashtaka ya muda mrefu hayavumiliki kwa wananchi na kwa kweli ni kutotenda haki.”[832]

Watumishi wa Mahakama wanatakiwa kuwa waangalifu sana katika upelelezi ili wasivunje haki za mtuhumiwa za usiri na kutokiuka kanuni ya uwezekano wa mtuhumiwa kutokuwa na hatia. Kwa sababu hata mahakimu wanaweza kukosea, ni vema sheria ikaweka kipengele cha wahanga wa namna hiyo, kufidiwa ikidhihirika kwamba kumefanyika makosa ya kisheria.

405. Kanisa linaona kuwa ni ishara ya matumaini “kuongezeka kwa upinzani dhidi ya adhabu ya kifo katika jamii, hata ingawaje adhabu yenyewe inaonekana kuwa ni ‘utetezi halali’ kwa jamii. Kwa kweli leo, serikali ina nafasi ya kuweza kufaulu kudhibiti uhalifu, na kwa aliyetenda kosa asiweze kuleta madhara bila kumwondolea kabisa fursa ya kujirekebisha.”[833] Inapotokea kuwa kuna uthibitisho wa hakika wa mtuhumiwa, mapokeo ya mafundisho ya Kanisa hayaondoi matumizi ya adhabu ya kifo “isipokuwa kama hiyo ndiyo njia pekee ya kulinda maisha ya watu dhidi ya mkosaji.”[834] Njia zisizo za umwagaji damu na adhabu ni nzuri zaidi kwani” zinaoana zaidi na masharti halisi ya manufaa kwa wote na zaidi yanaendana na heshima ya mtu.[835] Kuongezeka kwa nchi zinazoridhia mipango ya kufuta adhabu ya kifo au kusimamisha matumizi yake ni uthibitisho wa ukweli kwamba kesi ambazo kumuua mkosaji ni lazima kabisa “ni chache sana na kwa kweli karibu haziko kabisa.”[836] Kuongezeka kwa chuki dhidi ya adhabu ya kifo katika maoni ya watu, na mpango wenye lengo la kuifuta au kusitisha matumizi yake kunadhihirisha kuongezeka kwa utambuzi wa maadili.

 

IV. MFUMO WA KIDEMOKRASI

406. Barua ya Centesimus Annus ina maoni dhahiri na fasaha kuhusu demokrasia: “Kanisa linathamini mfumo wa kidemokrasia kwa sababu unawahakikishia wananchi ushiriki wao katika maamuzi ya kisiasa, huwahakikishia watawaliwa uwezekano wa kuwachagua na kuwawajibisha wawatakao, na kuwabadilisha kwa njia za amani wakati ukiwadia. Hivyo, haliwezi kupendelea uwepo wa vikundi vidogo vya watawala vinavyoweza kujichukulia uwezo wa Kiserikali kwa madhumuni yao binafsi au kwa kuendeleza itikadi zao. Demokrasia halisi inawezekana tu katika Serikali inayotawala kwa mujibu wa sheria, na kwa misingi ya dhana sahihi ya mtu nafsi. Ni sharti pawepo na mazingira ya lazima kwa maendeleo ya mtu binafsi kwa njia ya elimu na malezi katika maadili ya kweli, na ya ‘sehemu ya ubinadamu’ katika jamii kupitia miundo ya uumbaji ya ushiriki na ushirikianaji wa majukumu.”[837]

a. Tunu na Demokrasia

407. Demokrasia halisi haitokani na kufuata orodha ya kanuni zilizowekwa, bali ni tunda la kuridhia zile tunu zitiazo msukumo wa kuishi taratibu za kidemokrasia: hadhi ya kila binadamu, heshima ya haki za mtu, kujitolea ili kupata manufaa ya wote hilo likiwa ndio kigezo cha madhumuni na dira ya maisha ya kisiasa. Endapo kutakosekana makubaliano katika tunu hizo, maana kamili ya demokrasia inapotea na uthabiti wake unahatarishwa.

Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanatahadharisha dhidi ya misimamo ya kimaadili inayotegemezwa na hisia za watu tu, misimamo inayopinga kuwepo vigezo halisi au vya nyakati zote na kwa watu wote vinavyoweza kuwa vyanzo vya mpangilio sahihi wa vipaumbele vya tunu za maisha, kuwa ni tishio kubwa kwa nchi za kidemokrasia za sasa. Kumejitokeza mielekeo siku hizi ya kudai kwamba kutojali kumjua Mungu na misimamo kwa kadiri ya hisia za watu tu ndio falsafa na namna msingi ya fikra inayoendana na mifumo ya kidemokrasia ya maisha ya kisiasa. Wale wanaoamini kwamba wanaujua ukweli na kuufuata kwa dhati hawaaminiki kwa wenye mtazamo wa kidemokrasia, kwa sababu hawakubali kwamba ukweli unaweza kubainishwa na kuainishwa na wingi wa watu tu au kwamba hubadilika kufuatana na mwelekeo wa kisiasa. Kuhusu suala hili, ifahamike kwamba iwapo hakuna ukweli halisi, basi mawazo na misimamo vyaweza kuchezewa kwa faida ya mamlaka. Kama historia inavyodhihirisha, demokrasia isiyo na tunu huweza kugeuka mara kuwa udikteta wa chinichini au waziwazi.”[838] Kimsingi demokrasia “ni ‘mfumo’ na hivyo ni nyenzo na siyo hatima. Tunu yake ya ‘kimaadili’ haijitokezi yenyewe, bali inategemea utiifu wa sheria ya maadili, inayobainisha mienendo yote ya binadamu: kwa maneno mengine, uadilifu wake unategemea uadilifu wa malengo inayofuatilia na nyenzo inazotumia.”[839]

b. Taasisi na Demokrasia

408. Majisterio inakiri uhalali wa kanuni ihusuyo mgawanyo wa madaraka katika nchi: “ ni vema zaidi kila chombo cha dola kudhibitiwa na kingine na wigo mwingine wa madaraka ili kuwekana katika mipaka itakiwayo. Huu ndio msimamo wa ‘utawala wa sheria’ ambamo sheria ndiyo muhimili, na siyo utashi wa watu binafsi usio na taratibu zozote.”[840]

Katika mfumo wa kidemokrasia, mamlaka ya kisiasa yanawajibika kwa watu. Taasisi za uwakilishi sharti ziwe chini ya usimamizi thabiti wa jamii. Usimamizi huu unaweza kutekelezwa mahususi katika chaguzi huru zinazowezesha uteuzi na kubadilisha wawakilishi. Jukumu la waliochaguliwa kutoa maelezo ya kazi zao ambalo linadhaminiwa na kuheshimiwa kwa taratibu za uchaguzi – ni kipengele muhimu katika uwakilishi wa kidemokrasia.

409. Katika maeneo yao mahususi ya kiuwajibikaji (uandishi wa rasimu ya sheria, utawala, uundaji mifumo ya udhibiti wa matumizi ya madaraka), viongozi waliochaguliwa sharti wajitahidi kutafuta na kufikia hilo litakalochangia katika kufanya maisha ya wananchi yawe bora na ya ustawi katika kila hali.[841] Watawala wanawajibika kutoa maelezo kwa wale wanaowaongoza, lakini hili halimaanishi kwamba wawakilishi ni mawakala wa wananchi wasio na hisia wala maoni yao binafsi. Udhibiti wa wananchi kwa kweli hauwaondolei viongozi wa kuchaguliwa uhuru wao wanaopaswa kuutumia katika kutekeleza wajibu wao mintarafu malengo yanayopaswa kufikiwa. Haya hayategemei matashi mahususi ya watu maalumu, bali kwa sehemu kubwa zaidi kuunganisha na kupatanisha mambo yenye kuleta manufaa kwa wote, moja ya malengo ya lazima ya mamlaka ya kisiasa.

c. Vipengele vya Uadilifu Katika Uwakilishi wa Kisiasa

410. Wale walio na dhamana ya kisiasa sharti wasisahau au wasipuuzie maadili katika uwakilishi wa kisiasa, unaojumuisha kujitoa mhanga kuchangia kikamilifu katika kufikia majaliwa ya watu na kupata ufumbuzi wa matatizo ya kijamii. Katika mtazamo huu, mamlaka inayowajibika ina maana pia ya utawala wenye fadhila zinazouwezesha kutumia uwezo wake kama huduma[842] (uvumilivu, staha, kiasi, mapendo, jitihada za kushirikishana), mamlaka ya watendaji walio na utashi wa kupata manufaa ya wote, na siyo ufahari au kujipatia maslahi binafsi, ikiwa ndilo lengo la kweli la kazi yao.

411. Kati ya vilema vya mfumo wa kidemokrasia, rushwa ya kisiasa imebobea kwa kiwango kikubwa[843] kwa sababu unazisaliti kwa pamoja misimamo ya kimaadili na kanuni za haki za kijamii. Huujengea kashfa utendaji wa Serikali, ukisababisha mahusiano yasiyo mema kati ya watawala na wanaongozwa. Husababisha pia kuongezeka kwa kutoaminiwa kwa taasisi za Serikali, kunakopelekea wananchi kutopenda siasa na wawakilishi wake, na kuleta udhoofu wa taasisi. Rushwa hupotosha kabisa dhima ya taasisi za uwakilishi, kwa sababu panakuwa mahali pa kushindania kati ya maombi ya watu na huduma za kiserikali. Matokeo yake ni kwamba matakwa ya kisiasa yanapendelea maamuzi ya wale walio na uwezo wa ushawishi kwa maamuzi hayo yanakuwa kikwazo katika kufikia manufaa ya wananchi wote.

412. Kikiwa ni chombo cha Serikali, utawala wa umma katika ngazi yoyote – taifa, mkoa, jumuiya – unatakiwa kutoa huduma kwa wananchi: “Serikali ikiwapo kwa ajili ya kuhudumia wananchi wake, ndiyo msimamizi wa rasilimali za watu, ambazo zinatakiwa zitawaliwe kwa mtazamo wa kufikia manufaa kwa wote.”[844] Urasimu uliokithiri ni kinyume na mtazamo huo na hujitokeza pale ambapo “taasisi zinakuwa na miundo changamano na kujidanganya kuendesha kila eneo lililopo. Mwishowe, zinashindwa kutekeleza yaliyotarajiwa kutokana na kutokuwapo uwajibikaji binafsi, urasimu usio na kikomo, matashi binafsi yasiyo halali, na mzahamzaha hujenga tabia ya kupoteza uwajibikaji.”[845] Nafasi na wajibu wa wale wanaofanya kazi katika utumishi wa umma usieleweke na kuonekana kama kazi tu ama au iliyo kiurasimu tu, bali uonekane kuwa ni tendo la kusaidia raia linalotendwa kwa moyo wa huduma.

d. Vyombo vya Kushiriki katika Siasa

413. Vyama vya kisiasa vina kazi ya kuhamasisha ushiriki wa watu wengi na kuyaweka wazi majukumu ya umma ili yaweze kufikiwa na wote. Vyama vya siasa vinatakiwa kufafanua mategemeo ya jamii, vikiyaelekeza katika kupata manufaa ya wote,[846] vikiwadhihirishia wananchi uwezekano wa kuchangia katika kutengeneza sera na kufanya maamuzi ya kisiasa yenye kutekelezeka. Lazima viwe vya kidemokrasia katika miundo yake ya ndani na vyenye uwezo wa kutengeneza mipango ya kisiasa iliyo na ubunifu wa kuunganisha yaliyo mema katika jamii.

Namna nyingine ya ushiriki katika harakati za kisiasa ni kura ya maoni, ambayo kwayo maamuzi ya kisiasa yanafanywa moja kwa moja. Mfumo wa uwakilishi kwa kweli hauzuii uwezekano wa kuwauliza raia moja kwa moja kuhusu maamuzi yaliyo na umuhimu mkubwa katika maisha ya jamii.

e. Habari na Demokrasia

414. Habari ni kati ya vyombo msingi vya ushiriki kidemokrasia. Ushiriki pasipo uelewa wa hali ya jumuiya ya kisiasa, vipengele na ufumbuzi uliopendekezwa kwa matatizo yaliyopo hauwezekani na haufikiriki. Ni lazima kuhakikisha mfumo unaokubali washiriki wa mitazamo tofauti kushiriki katika wigo huu wa maisha ya kijamii, ikihakikishwa kwamba kunakuwepo miundo mingi na vifaa vya habari na mawasiliano. Ni lazima vilevile kurahisisha masharti ya usawa katika kumiliki na kutumia vifaa hivi kwa njia ya sheria zinazofaa. Kati ya vikwazo vinavyozuia matumizi kamili ya haki ya kutokuwa na upendeleo katika habari,[847] uangalifu makini uwepo kwa jambo linalojitokeza sana la vyombo vya habari kumilikiwa na watu wachache au vikundi. Hili lina athari ya kuhatarisha mfumo mzima wa kidemokrasia iwapo jambo hilo litaambatana na mahusiano ya karibu sana baina ya amali ya serikali na taasisi za kifedha na habari.

415. Vyombo vya habari sharti vitumike kuijenga na kuihimili jumuiya ya watu katika sekta zake mbalimbali: kiuchumi, kisiasa, kitamaduni, kielimu na kidini.[848] “Habari zinazotolewa na vyombo vya habari zipo kwa ajili ya kuhudumia kwa manufaa ya wote. Jamii ina haki kupata habari zilizo na asili ya ukweli, uhuru, haki na mshikamano.”[849]

Swali la msingi ni je mfumo wa sasa wa habari unachangia katika kumboresha mwanadamu mwenyewe; hii ni sawa na kuuliza, mfumo huo unawafanya watu wakamilifu zaidi kiroho, waelewa zaidi hadhi ya utu wao, wawajibike zaidi au wawe wazi kwa wengine, na haswa kwa wahitaji na wadhaifu mno. Kipengele cha ziada na kilicho na umuhimu mkubwa ni hitaji la teknolojia mpya kuheshimu tofauti halali za kitamaduni.

416. Katika ulimwengu wa vyombo vya habari, matatizo halisi ya mawasiliano yanazidiwa na itikadi, tamaa ya kupata faida na uongozi wa kisiasa, ushindani na mapigano baina ya makundi, na maovu mengineyo ya kijamii. Tunu za kimaadili na kanuni zake zinavihusu pia vyombo vya habari. “Uwanda wa maadili unahoji si tu ujumbe uliobebwa na mchakato wa mawasiliano (jinsi mawasiliano yanavyowezeshwa) bali pia muundo msingi na masuala yahusuyo mfumo, yenye kuibua maswali makubwa ya sera ya kudadisi jinsi gani usambazaji wa teknolojia ya kisasa na bidhaa zake unavyofanyika (nani atakayekuwa tajiri katika mawasiliano na nani ataendelea kuwa maskini wake).”[850]

Katika maeneo yote matatu – ujumbe wenyewe, mchakato, na masuala ya kimuundo – kanuni moja msingi inahusika: mtu mwenyewe na jumuiya ya wanadamu ndio hatma na kipimo cha matumizi ya vyombo vya habari. Kanuni ya pili inakamilisha ile ya kwanza: lililo la manufaa kwa wanadamu haliwezi kupatikana bila ya kutegemea lililo la manufaa kwa jumuia waliyomo.[851] Ni lazima kwamba raia wanashiriki katika mchakato wa kufanya maamuzi yahusuyo sera za vyombo vya habari. Ushiriki huu, ambao unapaswa kuwa wazi, sharti uwe thabiti usio na upendeleo kwa makundi mahususi iwapo vyombo vyenyewe vya habari ni vya kibiashara.[852]

 

V. JUMUIYA YA KISIASA KWA KUHUDUMIA
JUMUIYA YA KIRAIA

 

a. Thamani ya Jamii

417. Jumuiya ya kisiasa imeanzishwa kwa madhumuni ya kuhudumia jamii iliyo asili yake. Kanisa limechangia vema katika kutofautisha baina ya jumuiya ya kisiasa na jamii hasa kwa mtazamo wake wa mtu, anayetambulika kuwa huru, aliye na mahusiano na aliye wazi kwa Mwenyezi. Mtazamo huu unapingwa na itikadi za kisiasa zenye asili ya ubinafsi na zile zenye tabia ya udikteta, zinazojumuisha jamii katika wigo wa Serikali. Msimamo wa Kanisa wa kujitosa kwa ajili ya mfumo wa wingi wa kijamii una nia ya kuwezesha kupatikana kwa ubora zaidi kwa manufaa ya wote na demokrasia zenyewe, kwa kadiri ya kanuni za mshikamano, auni na haki.

Jamii ni jumla ya mahusiano na rasilimali, tamaduni na mengine yanayounganisha watu, ambayo kwa kiwango fulani hayahusiani na mambo ya kisiasa na hayamo katika sekta ya kiuchumi. “Madhumuni ya jamii ni ya kilimwengu, kwa kuwa yanahusu manufaa ya wote, ambamo kila mwananchi ana haki kwa kiasi chake.”[853] Hili linadhihirishwa kwa uwezo wa kupanga wenye lengo la kuwezesha maisha ya kijamii yaliyo huru na yenye haki zaidi, ambamo makundi mbalimbali ya raia yanaweza kujiundia asasi, kufanya kazi, kustawisha na kuonyesha hiari yao kwa madhumuni ya kukidhi mahitaji yao msingi na kutetea upendeleo wao halali.

b. Kipaumbele cha Jumuiya ya Kiraia

418. Jumuiya ya kisiasa na jamii, ingawaje wana uhusiano na kutegemeana, hawako sawa katika kipaumbele cha hatima. Kimsingi jumuiya ya kisiasa ipo kwa ajili ya kuhudumia jamii na, katika uchambuzi wa kina, ni watu wenyewe na makundi yanayounda jamii.[854] Kwa hiyo, jamii haiwezi kufikiriwa kuwa ni nyongeza au sehemu inayobadilika daima ya jumuiya ya kisiasa; kwa hakika, jamii inapewa kipaumbele kwa sababu ni katika yenyewe ndimo jumuiya ya kisiasa inajipatia uhalali wake.

Serikali lazima iandae mfumo wa kisheria unaojitosheleza kuwawezesha raia kujihusisha katika shughuli zao kwa uhuru, na sharti iwe tayari kusaidia ipasavyo kwa kadri ya kanuni ya auni, ili mahusiano baina ya asasi huru na maisha ya kidemokrasia yaelekezwe kupata manufaa kwa wote. Jamii kwa kweli ina sura nyingi na zisizo za aina moja kila wakati; haikosi utata na migongano. Ni mahali pia ambapo mapendeleo tofauti hugongana, kukiwa na hatari dhahiri kwamba aliye na nguvu zaidi atashinda.

c. Matumizi ya Kanuni ya Auni

419. Jumuiya ya kisiasa ina wajibu wa kurekebisha mahusiano yake na jamii kwa kufuatana na kanuni ya auni.[855] Ni muhimu kwamba ustawi wa maisha ya kidemokrasia unaanza ndani ya mfumo wa jamii. Shughuli za jamii – hasa za vyama vya wenye kujitolea na shughuli za ushirika katika sekta ya jamii – binafsi, zote hizo zikijulikana kama “sekta ya tatu” katika kuitofautisha na zile za serikali na soko – zinawakilisha njia bora zifaazo kustawisha uwanda wa kijamii wa mtu mwenyewe, anayegundua katika shughuli hizo mahali pa lazima kujieleza kikamilifu. Kuendeleza upanuzi wa jitihada za kijamii nje ya wigo unaodhibitiwa na Serikali kunawezesha kugundulika maeneo mapya ya uwepo hai na ushiriki wa moja kwa moja wa raia, wakiunganisha na kazi za Serikali. Hali hii muhimu, imejitokeza mara kwa mara kupitia njia zisizo rasmi na imeibua namna mpya na halali za kutumia haki binafsi, ambazo zimeleta ustawishaji mzuri wa maisha ya kidemokrasia.

420. Ushirikiano, hata ukiwa katika muundo usio rasmi, unajidhihirisha kutoa ufumbuzi wa kufaa kwa mitazamo ya ukinzani na ushindani usio na kikomo unaoonekana kuenea sana siku hizi. Mahusiano yanayojengeka katika hali ya ushirikiano na mshikamano yanashinda migawanyiko ya kiitikadi yakihamasisha watu kutafuata yale yanayowaunganisha kuliko yanayowatenganisha.

Uzoefu mwingi katika kazi za kujitolea ni mifano ya thamani kubwa inayowataka watu kutazama jamii kama mahali ambapo panawezekana kujenga maadili ya juu ya msingi wa mshikamano, ushirikiano thabiti na mazungumzo ya kidugu. Wote wanaalikwa kuangalia kwa uhakika yale yanayowezekana na kisha watoe nguvu zao kwa manufaa ya jumuiya kwa ujumla na kwa namna ya pekee, kwa manufaa ya wanyonge na wahitaji wakubwa. Kwa njia hii, kanuni ya “uwajibikaji wa jamii” inathibitishwa pia.[856]

 

VI. SERIKALI NA JUMUIYA ZA KIDINI

A. UHURU WA DINI, HAKI MSINGI YA BINADAMU

421. Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatikano ulilipa Kanisa Katoliki wajibu wa kukuza Uhuru wa dini. Tamko Dignitatis Humanae linaeleza katika kichwa kidogo chake kwamba linakusudia kutangaza “haki ya mtu na ya jumuiya kuwa na uhuru wa kijamii na kiraia katika mambo ya kidini.” Ili uhuru huu uliowekwa na Mungu na kuandikwa katika maumbile ya watu uweze kutumika ipasavyo kusiwekwe kikwazo chochote cha kuuzuia kwa kuwa ukweli hauwezi kulazimishwa isipokuwa kwa fadhila ya ukweli wenyewe”.[857] Hadhi ya mtu mwenyewe na hulka ya kumtafuta Mungu vyataka kwamba wote waume kwa wake wawe huru bila ya kizuizi chochote katika masuala ya dini.[858] Jamii na Serikali isimlazimishe mtu kutenda dhidi ya dhamira hiyo.[859] Haki ya uhuru wa dini sio leseni ya kimaadili ya kuambatana na kosa, wala sio haki inayotakiwa kwa kosa.[860]

422. Uhuru wa dhamiri na dini “unamhusu mwanadamu katika hali yake binafsi na kama mwanajumuiya.[861] Haki ya uhuru wa dini lazima itambulike kisheria na iidhinishwe kama haki ya raia;[862] hata hivyo, ina mipaka yake. Ukomo halali wa matumizi ya uhuru wa dini lazima uamuliwe ndani ya jamii kwa kutumia busara za kisiasa, kwa kuzingatia matakwa ya kufikia yaliyo mema kwa wote, na uidhinishwe na serikali kupitia kawaida ya kisheria kulingana na lengo la mfumo wa maadili. Tunu hizo zinapaswa kukamilishwa “kwa madhumuni ya kuzikinga itakiwavyo haki za wananchi wote na kwa ajili ya usuluhishi katika migongano ya haki hizo kwa amani, na pia kuwapo kwa hitaji la kuwa na tahadhari ya kutosha ya amani kamili kwa jamii, ambayo hujiri wakati wananchi wanaishi pamoja kwa taratibu njema na haki ya kweli, na mwisho kwa matakwa ya misingi murua ya malezi thabiti ya maadili ya jamii.”[863]

423. Kwa sababu za mfungamano wa kihistoria na wa kiutamaduni baina ya taifa na jumuiya fulani ya kidini, jumuiya husika inaweza kutambuliwa mahususi na Serikali. Utambuzi huo usisababishe ubaguzi na upendeleo kwa dini husika dhidi ya makundi mengine ya kidini.[864] Mtazamo wa mahusiano baina ya Serikali na mashirika ya kidini unaohimizwa na Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatikano unaokubaliana na matakwa ya Serikali za utawala wa kisheria na taratibu za Sheria ya Kimataifa.[865] Kanisa linajua vema kwamba mtazamo huo haukubaliki kwa wengine; haki ya uhuru wa dini, kwa bahati mbaya, inakiukwa na Serikali nyingi, hata kufikia hatua kwamba atakayefahamika kuendesha mafundisho ya katekesi, kuruhusu yafundishwe au kuyapokea ni kosa linalostahili kuadhibiwa kwa mujibu wa sheria.”[866]

 

B. KANISA KATOLIKI NA JUMUIYA YA KISIASA

a. Kujitawala na Uhuru

424. Ijapokuwa Kanisa na Jumuiya ya kisiasa kila mmoja inajidhihirisha kwa muundo unaoonekana wazi, kwa hulka ni tofauti kwa sababu ya wasifu wao na hatima wanazofuatilia. Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatikano kwa heshima ulisisitiza kwamba, “katika maeneo ya mamlaka zao, jumuiya ya kisiasa na Kanisa wote wawili ni huru na wanajitawala.”[867] Kanisa limejipanga katika namna inayofaa kukidhi mahitaji ya kiroho ya waamini wake, wakati jumuiya mbalimbali za kisiasa zinaanzisha mahusiano na taasisi za kuhudumia kila kitu kilicho sehemu ya malimwengu kwa manufaa ya wote. Kujitawala na uhuru wa taasisi hizi halisi ni dhahiri hasa kuhusiana na hatima zao.

Wajibu wa kuheshimu uhuru wa dini unaitaka jumuiya ya kisiasa kulihakikishia Kanisa wigo unaohitajika kutekeleza wito na ujumbe wake. Kwa upande wake, Kanisa halina uwezo wala uhalali kisheria kuhusiana na miundo ya jumuiya ya kisiasa: “Kanisa linaheshimu utawala halali wa taratibu za kidemokrasia na halina haki kuonyesha upendeleo katika maamuzi ya kitaasisi au ya kikatiba,”[868] na si mwenendo wake kujihusisha na masuala yahusuyo programu za kisiasa, isipokuwa zinapokuwa na athari za kuhatarisha dini au maadili.

b. Ushirikiano

425. Kujitawala kwa kila mmoja wao Kanisa na jumuiya ya kisiasa hakusababishi utengano wa kutokuwepo ushirikiano. Wote wawili, ingawaje kwa majina tofauti, wanahudumia wito wa mwanadamu kibinafsi na ule wa kijamii wa mwanadamu yuleyule. Kanisa na jumuiya ya kisiasa, kwa kweli, zinajidhihirisha zenyewe katika mifumo iliyo na taratibu ambayo si hatima ya taasisi hizo, lakini iliyokusudiwa kwa kumhudumia mwanadamu, kumwezesha kuishi haki zake kikamilifu, zile zilizo za asili katika uhalisia wake kama mwananchi na Mkristo, na kutimiza kwa usahihi wajibu wake husika. Kanisa na jumuiya ya kisiasa zinaweza kutoa huduma hii kwa ufanisi zaidi “kwa mema ya wote iwapo kila mmoja wao atawajibika zaidi kwa ushirikiano wa jumla katika njia stahili kufuatana na mambo yalivyo ya wakati na mahali.”[869]

426. Kanisa lina haki ya kukubalika kisheria kwa utambulisho wake sahihi. Kwa sababu utume wake hujumuisha uhalisia wote wa mwanadamu, Kanisa, likifahamu kwamba “limeungana kwa kweli na kwa undani sana na wanadamu na historia yao,”[870] linadai haki ya uhuru wake kudhihirisha busara yake adilifu kuhusu uhalisia huu, wakati wowote litakapotakiwa kutetea haki msingi za mtu mwenyewe au kwa ajili ya wokovu wa roho.[871]

Kanisa kwa hiyo linatafuta: Uhuru wa kujieleza, kufundisha na kuinjilisha; uhuru wa kuabudu; uhuru wa kujipanga na kuwa na utawala wake wa ndani; uhuru wa kuchagua, kuelimisha, kuwapa majina na kuwahamisha wachungaji wake; uhuru wa kujenga majengo ya kidini, uhuru wa kupata na kumiliki rasilimali kwa ajili ya kuendeshea shughuli zake; na uhuru wa kuunda jumuiya siyo tu kwa madhumuni ya kidini bali pia kwa elimu, utamaduni, afya na kwa ajili ya malengo ya hisani.[872]

427. Ili kuzuia au kupunguza uwezekano wa kuhitilafiana baina ya Kanisa na jumuiya ya kisiasa, uzoefu wa kisheria wa Kanisa na ule wa Serikali umeainisha mifumo thabiti ya mawasiliano na vyombo vya kufaa vya kuhakikisha uwepo wa mahusiano yenye mapatano. Uzoefu huu ni kipengele cha marejeo muhimu kwa kesi zote ambamo Serikali imekuwa na ufedhuli wa kuvamia maeneo ya shughuli za Kanisa, kudhoofisha uhuru wa utendaji wake hata kudiriki waziwazi kulitesa au, kinyume chake, kwa kesi ambamo taasisi za kikanisa hazitendi ipasavyo kuhusiana na Serikali.

 

SURA YA TISA

JUMUIYA YA KIMATAIFA

1. VIPENGELE VYA BIBLIA

 

a. Umoja wa Familia ya Binadamu

428. Maelezo ya Biblia kuhusu uumbaji yanaonesha umoja wa familia ya binadamu na yanafundisha kwamba Mungu wa Israeli ni Bwana wa kihistoria na ni Bwana wa Ulimwengu. Tendo lake la uumbaji linajumuisha ulimwengu wote pamoja na familia nzima ya binadamu iliyokusudiwa na kazi ya Mungu ya uumbaji. Maamuzi ya Mwenyezi Mungu ya kumuumba mtu kwa mfano wake (taz. Mwa 1: 26 – 27) yanampa mwanadamu hadhi ya pekee inayoenea na kuvigusa vizazi vyote vya ulimwengu huu (taz. Mwa 10). Kitabu cha Mwanzo kinaonesha pia kwamba binadamu hakuumbwa akae peke yake bali awe katika mazingira yenye maeneo yanayoulinda uhuru wake. Mazingira hayo ni kama yale yenye miti na nyasi ambayo yanaweza kumpatia chakula akiyatumia kwa kufanya kazi. Mungu alimpa pia zawadi ya mwenza anayefanana naye (taz. Mwa 2: 8 – 24) ili waishi pamoja kwa kusaidiana. Katika Agano lote la Kale hali inayodhihirisha ukamilifu wa maisha ya binadamu ndiyo madhumuni ya baraka ya kimungu. Mungu anataka kuhakikisha kuwa binadamu anapata mahitaji yake yote muhimu ili aweze kujiendeleza na awe na uhuru wa kujieleza na apate pia mafanikio katika kazi yake na awe na mahusiano mema ya kijamii.

429. Baada ya uharibifu uliosababishwa na gharika, agano alilolifanya Mungu na Nuhu (taz. Mwa 9: 1 – 17) na pia alilolifanya na jumuiya nzima ya binadamu kwa kupitia kwa Nuhu, inaonekana kuwa Mungu anataka kudumisha hali nzuri ya ulimwengu kwa ajili ya jumuiya nzima ya binadamu. Anataka pia kuudhibiti uumbaji pamoja na hadhi na heshima ya maisha ya binadamu iliyokuwa imeoneshwa wazi kwa ule uumbaji wa kwanza. Haya ni matakwa ya Mungu licha ya dhambi, uhasama na udhalimu vitu vilivyokuwa vimeadhibiwa na Mungu kwa gharika ambavyo vilikuwa vimeingia katika uumbaji. Kitabu cha Mwanzo kinaonesha kwa kustaajabu jinsi kila mtu alivyo tofauti na mwenzake kutokana na tendo la Mungu la ubunifu (taz. Mwa 10: 1 – 32). Wakati huohuo kinakemea ukaidi wa binadamu wa kuukataa ubinadamu wake, ukaidi ambao ulisababisha mtafaruku wa Mnara wa Babeli (taz. Mwa 11: 1 – 9). Kwa mujibu wa Mpango wa Kimungu, watu wote walizungumza “lugha moja yenye maneno ya kufanana” (taz. Mwa 11: 1). Hata hivyo, binadamu waligawanyika wakimgeuzia Muumba migongo yao (taz. Mwa 11: 4).

430. Ahadi aliyokuwa ameiweka Mungu na Abraham ambaye alikuwa ameteuliwa kuwa “Baba wa Mataifa mengi” (Mwa 17. 4), inafungua milango ya familia ya binadamu ya kumrudia Mungu muumba wao. Historia ya ukombozi inawafanya Waisraeli waamini kuwa kitendo cha Mungu kiliishia kwenye mipaka ya nchi ya Israeli tu. Lakini sasa binadamu wanaanza kuamini kidogokidogo kuwa kazi ya Mungu inavuka mipaka ya Israeli na kuendelea kuenea kwenye mataifa mengine (taz. Isa 19: 18 – 25). Manabii wangetangaza wakati ule wa nyakati za kutabiri vifo na hukumu ya mwisho, hija ya mataifa kwenye hekalu la Bwana na kuwe pia na kipindi cha amani kati ya watu (taz. Isa 2: 2-5; 66: 18-23). Wana wa Israeli waliotawanyika kama wakimbizi, wazi kabisa wangekuwa na wajibu wa kufahamu kuwa wao ni mashahidi wa yule Mungu Mmoja (taz. Isa 44: 6 – 8) ambaye ni Bwana wa ulimwengu mzima na wa historia ya mataifa (taz. Isa 44: 24 – 28).

b. Yesu Kristo, Mfano Halisi na Msingi wa Ubinadamu Mpya

431. Bwana wetu Yesu Kristo ni mfano na msingi wa ubinadamu mpya. Katika Yeye “Aliye sura yake Mungu” (2 Kor. 4: 4) mtu – aliyeumbwa kwa mfano wa Mungu anapata ukamilifu wake. Katika ushahidi halisi wa mapendo ambayo Mungu ameyafunua kwa njia ya msalaba wa Kristo, vipingamizi na aina yote ya uadui vimekwisha ondolewa (taz. Efe 2: 12 – 18) na kwa wale wanaoishi maisha mapya katika Kristo, tofauti za utaifa na utamaduni si tena sababu za kutengana (taz. Rum 10: 12; Gal 3: 26 – 28; Kol 3: 11).

Kanisa linaufahamu mpango wa Kimungu kuhusu umoja unaohusu jamii yote ya binadamu (taz. Mdo 17: 26), Roho ashukuriwe kwa hilo. Mpango huu ni mahususi wa kuunganisha tena ulimwengu katika fumbo la wokovu uliofanyika kwa njia ya ukombozi wa Kristo (taz. Efe 1: 8 – 10). Kuanzia siku ile ya Pentekoste, ufufuko unapotangazwa kwa watu wa mataifa yote, ambao kila mmoja anasikia na kuelewa kwa lugha yake mwenyewe (taz. Mdo 2: 6), Kanisa linakamilisha ile kazi yake ya kurejesha uhusiano uliokuwa umetiwa dosari na linakuwa shahidi wa umoja uliokuwa umepotea kule Babeli. Kutokana na kazi hii ya kitume, familia ya binadamu inapaswa kuutafuta tena umoja wake na kumtambua pamoja na kuukiri utajiri uliomo katika tofauti ambazo zipo ili kuufikia “umoja uliokamilika katika Kristo.”[873]

c. Wito wa Ukristo kwa Watu Wote

432. Ujumbe wa Ukristo unatoa mwanga kwa maisha ya watu na jamii nzima hapa ulimwenguni.[874] Mwanga huu unawafanya waukiri ule umoja wa familia ya wanadamu.[875] Hata hivyo, umoja huu haujengwi kwa kutumia silaha, vitisho wala matumizi mabaya ya madaraka, bali utokane na matokeo ya ule “mfano wa hali ya juu kabisa wa umoja ambao ni mfano wa jinsi Mungu alivyo, yaani Mungu mmoja, katika Nafsi tatu. Hicho ndicho tunachomaanisha sisi Wakristo tunapotumia lile neno “ushirika.”[876] Haya ni mafanikio makubwa ya msukumo wa uhuru wa kimaadili na kiutamaduni.[877] Ujumbe huu wa Kikristo umekuwa na uwezo wa kuwafanya wanadamu waelewe kuwa watu wana maendeleo ya kuungana si tu kwa sababu ya kujiunga na mashirika au vyama: kama vile vya kisiasa, kiuchumi au vile vinavyotoa maslahi ya kimataifa, lakini ni kutokana na mapenzi yao ya kushirikiana wakijua fika kuwa “wao ni wanafamilia hai wa familia nzima ya wanadamu.”[878] Jumuiya ya kimataifa haina budi ijidhihirishe tena na tena na kwa uwazi zaidi kwa chombo halisi cha umoja ambacho Muumba wetu alikipa ridhaa yake “Umoja wa familia ya wanadamu umekuwepo muda wote kwa sababu jamii yake ni binadamu ambao wote wana hadhi iliyo sawa. Kwa sababu hiyo, kutakuwa daima na madhumuni ya kweli ya kukuza manufaa kwa wote ambayo ni manufaa kwa familia yote ya binadamu.”[879]

 

II. KANUNI ZA MSINGI ZA JUMUIYA YA KIMATAIFA

 

a. Jumuiya ya Kimataifa na Tunu Zake

433. Uwepo wa binadamu kama mhimili wa kati na maelekeo ya asili ya watu na walimwengu wote kwa jumla ya kuanzisha mahusiano kati yao ni sababu za msingi za kuanzisha jamii ya kweli ya kimataifa yenye mpangilio wa kuhakikisha kwamba kuna manufaa kwa watu wote.[880] Pamoja na ukweli kwamba kuna mchakato wa kuanzisha na kuendeleza jamii ya kweli ya kimataifa, umoja wa familia ya binadamu, kwa kweli, haujashika kasi ya kuonekana kuwa kuna umoja kama huo. Hii inasababishwa na vipingamizi vinavyotokana na itikadi ya kizalendo na ya kianasa vinavyopingana na manufaa ya mtu vikiangaliwa katika vipengele vyake mbalimbali vya kimwili na kiroho pamoja na vile vya kibinafsi na vya kijumuiya. Kwa kweli, aina yoyote ya nadharia au muundo, jadi au maadili ya ubaguzi wa kimbari au wa kijamii ni vitu visivyokubalika kabisa katika uundaji wa jumuiya hiyo.[881]

Uwezekano wa kuishi pamoja kati ya mataifa mbalimbali unategemezwa na misingi ileile ambayo ingekuwa miongozo ya uhusiano kati ya binadamu: ukweli, haki, mshikamano wa kweli kimatendo na uhuru.[882] Mafundisho ya Kanisa kuhusu kanuni za kikatiba juu ya jamii ya kimataifa yanasema kwamba mahusiano kati ya watu na jumuiya za kisiasa yanaratibiwa kimantiki, kihaki, kisheria na kwa maafikiano bila vurugu au vita wala aina yoyote ya ubaguzi, vitisho na udanganyifu.[883]

434. Sheria ya kimataifa ni mdhamini wa utaratibu wa kimataifa [884] wenye nia ya kuzifanya jumuiya za kimataifa ziishi pamoja kwa amani kati ya jumuiya za kisiasa zinazohitaji, kila moja peke yake, kuyaendeleza yale yaliyo na manufaa kwa raia wao na kuweka jitihada kwa pamoja kuhakikisha kuwa wanadamu wote[885] wanaelewa kuwa manufaa ya taifa hayawezi kamwe kutenganishwa na yale ya familia nzima ya binadamu.[886]

Jumuiya ya kimataifa ni jumuiya ya kisheria iliyoundwa kwa mujibu wa misingi ya makubaliano ya madola wanachama bila kujiona kuwa dola moja ipo chini au juu ya jingine na bila kujihisi kuwa uhuru wake unaingiliwa na dola jingine.[887] Kuielewa jumuiya ya kimataifa kwa mtindo huu hakuna maana kwa namna yoyote ile kuwa tunakubaliana au hatukubaliani na ile hali halisi ya kuwepo kwa vikundi hivi katika hiyo jumuiya bali tunahimiza uwazi wa kila kikundi katika utendaji wake wa mambo.[888] Kuvijali na kuvihimiza vikundi hivi kunasaidia kuzuia mgawanyiko kati yao na badala yake kunavifanya vijifikirie kiumimi hali inayovifanya viyumbe.

435. Majisterio wanatambua umuhimu wa mamlaka ya kitaifa, kama inavyoeleweka zaidi ya yote ni kama maelezo ya uhuru ambao lazima utawale mahusiano kati ya Madola.[889] Mamlaka inawakilisha dhamana ya taifa katika hisia za kisiasa, kiuchumi, kijamii na hata kiutamaduni.[890] Kukua kwa utamaduni kunakuwa na umuhimu wa namna ya pekee kama chanzo cha uwezo wa kuzuia vitendo vya uchokozi au vitendo vingine vya ukandamizaji unaoweza kuwa na athari kwa uhuru wa nchi. Utamaduni huwa ni dhamana ya kuhifadhi utambulisho wa watu na kuonesha na kukuza ukuu wake wa kiroho.[891]

Hata hivyo, huo ukuu wa kiroho huwa haujakamilika. Mataifa yako huru kuzikataa baadhi ya haki zao kwa kuzingatia manufaa kwa wote na kwa kufahamu kwamba wanaunda “familia ya mataifa”[892] ambayo inahitaji kuaminiana, kutegemeana na kuheshimiana.

Kwa maana hiyo, basi, kuwe na uangalifu wa pekee kwa kuwa hayapo bado makubaliano ya kimataifa yanayohusu “haki za mataifa”[893] ambazo kama zingekuwa zimeandaliwa zingeyashughulikia masuala yanayohusu haki na uhuru katika mazingira ya ulimwengu huu wa leo.

b. Mahusiano katika Msingi wa Mapatano kati ya Taratibu za Kisheria na za Kimaadili

436. Ili kuwa na utaratibu wa kimataifa unaohakikisha kuwa kuna mawasiliano ya kuelewana na ya amani kati ya binadamu na ili kuimarisha utaratibu huo, sheria ileile adilifu inayodhibiti maisha ya binadamu lazima pia iratibu mahusiano kati ya dola moja na dola nyingine. “Uzingatiaji wa sheria hiyo adilifu lazima ufundishwe na ukuzwe na mataifa pamoja na madola yote kwa sauti na nguvu ya pamoja na kwa kiasi ambacho hakuna atakayeuonea shaka au kuupuuzia umuhimu wake.”[894] Sheria hiyo adilifu ya kiulimwengu ambayo imechorwa ndani ya moyo wa kila binadamu lazima ichukuliwe kuwa ni yenye manufaa na isiyofutika ikiwa ni mfano hai wa dhamiri ya ubinadamu, mfano[895] ambao ni msingi wa ulimwengu ujao.

437. Heshima inayotolewa na kila mtu kwa zile kanuni ambazo ni msingi wa kisheria wa muundo unaokubaliana na ule mpango adilifu[896] ni sharti la lazima kwa utengamano wa maisha ya kimataifa. Utafutaji wa utengamano kama huu umehimiza kufanyika taratibu kwa ufafanuzi wa ndani zaidi kuhusu haki ya mataifa[897] (“ius gentium”) unaoweza kuchukuliwa kama “mtangulizi wa sheria ya kimataifa.”[898] Tafakari ya kisheria na ya kitheolojia yenye misingi itokanayo na sheria ya asili imeunda “Kanuni za jumla zitumikazo popote ulimwenguni ambazo zipo juu ya sheria zilizoundwa na kila dola peke yake kwa matumizi katika dola husika.”[899] Kanuni hizi ni kama zile za umoja wa jamii ya binadamu, hadhi na heshima sawa kwa binadamu wote, upingaji wa vita kama njia ya ufumbuzi wa migogoro, wajibu wa kushirikiana ili kupata ufanisi na hali ya kuwa tayari kutekeleza ahadi zilizowekwa (pacta sunt servanda). Kanuni hii ya mwisho ni muhimu sana ili kukwepa “vishawishi vya matumizi ya hoja ya nguvu badala ya nguvu ya hoja.”[900]

438. Ili kukwepa migogoro inayozuka kati ya makundi mbalimbali ya kisiasa ambayo yanaweza kuhatarisha utengamano wa mataifa na usalama wa kimataifa ni jambo la lazima kabisa kutumia kanuni za pamoja zinazojulikana na wote kwa majadiliano na kulikataa kabisa lile wazo kwamba haki inaweza kupatikana kwa njia ya vita.[901] “Kama vita inaweza kumalizika bila kuwa na walioshinda au walioshindwa kwa kuufanya ubinadamu ujiangamize wenyewe, yatupasa kuikataa ile mantiki inayoelekea kukubaliana nayo kwamba mapambano na hata vita yenyewe ni vigezo vya maendeleo na ni hatua ya kusonga mbele kihistoria.”[902]

Hati ya Umoja wa Mataifa haipigi tu matumizi ya nguvu bali inakataza hata matumizi ya vitisho vya matumizi ya nguvu.[903] Sehemu hii iliongezwa kutokana na lile tukio la kusikitisha la Vita Kuu ya Pili. Wakati huo Majisterio haikusita kuonesha vipengele kadhaa muhimu vya kusaidia kujenga upya utaratibu mwafaka wa kimataifa. Utaratibu muafaka huu ni ule wa kila taifa kuwa na uhuru wa kujiona kuwa ni taifa kamili, kuwa na utetezi wa haki ya wanyonge, mgawanyo sawa wa raslimali ya dunia hii, upingaji wa vita na pia uwepo wa mpango madhubuti wa kuacha kutumia silaha, kutovunja makubaliano yaliyokwisha kufikiwa na ukomeshaji wa utesaji kutokana na itikadi ya imani ya mtu.[904]

439. Ili kuwa na uimarishaji wa kipaumbele cha sheria, ile kanuni ya kuaminiana ni ya muhimu sana.[905] Kwa mtazamo huu, hati rasmi lazima ziandaliwe ili zisaidie kufikia maamuzi ya mabishano kwa amani. Hii itasaidia pia kuimarisha uwezo na nguvu zao za madaraka. Michakato ya majadiliano, upatanisho, usuluhishi pamoja na utoaji wa maamuzi, michakato ambayo imo katika sheria ya kimataifa lazima iungwe mkono kwa uanzishwaji wa “chombo cha kisheria chenye mamlaka katika ulimwengu huu wa amani.”[906] Michakato ya mwelekeo huu itaifanya jumuiya ya kimataifa isionekane tu kama mkusanyiko wa madola kwa nyakati fulanifulani tu za uhai wao, bali kama kiunzi ambacho kina uwezo wa kutanzua matatizo kwa amani. “Kama ilivyo katika sheria za ndani za kila Dola, mfumo wa ulipizaji kisasi katika jamii na hasa ulipizaji kisasi ule wa jino kwa jino umeshindwa kuendelea kuwepo kutokana na utawala wa sheria. Kwa hiyo, basi mwelekeo huohuo sasa unahitajika kwa haraka katika jumuiya ya kimataifa.[907] Kwa kifupi, sheria ya kimataifa haina budi ihakikishe kuwa sheria ya wale wenye mabavu inashindwa kufanya kazi.[908]

 

III. MUUNDO WA JAMII YA KIMATAIFA

 

a. Manufaa ya Mashirika ya Kimataifa

440. Kanisa ni mwenzi katika safari ya kuelekea kwenye “Jumuiya” ya kweli ya kimataifa iliyochukua mwelekeo dhahiri baada ya kuanzishwa kwa Jumuiya ya Umoja wa Mataifa hapo mwaka 1945. Umoja huu wa Mataifa “umetoa mchango mkubwa wa kuikuza hadhi ya utu wa binadamu, uhuru wa wanadamu na matakwa ya maendeleo na hivyo kuupalilia uwanja wa maendeleo ya maarifa na ustawi wa jamii kwa minajili ya ujenzi wa amani.”[909] Kwa jumla, Mafundisho ya Kanisa kuhusu masuala ya kijamii yanaangalia mashirika ya serikali mbalimbali kuwa yana msimamo wa kujenga hasa yale yanayofanya kazi katika sekta maalumu.[910] Hata hivyo, wakati fulanifulani hutokea wasiwasi wa kuyaona mashirika hayo kuwa hayayashughulikii matatizo yanayojitokeza kwa njia inayokubalika.[911] Majisterio wanapendekeza kwamba mahitaji ya binadamu yashughulikiwe katika maisha ya kijamii na katika maeneo yenye umuhimu wa pekee ili mataifa na watu wote waishi pamoja kwa amani.[912]

441. Wasiwasi wa Papa kuhusu familia ya binadamu kuishi kwa amani na kwa mpangilio unaofaa unamfanya asisitize uundaji wa “namna fulani ya mamlaka ya kimataifa inayojulikana na kukiriwa na watu wote ambayo itakuwa na uwezo pamoja na nguvu ya kulinda usalama, haki na uzingatiaji wa sheria kwa niaba ya wengine wote.[913] Jinsi mambo yanavyozidi kuendelea, pamoja na maafikiano katika maeneo kadhaa, watu muda wote wametambua na kukiri umuhimu wa kuwa na mamlaka inayojishughulisha na matatizo ya kiulimwengu yatokanayo na utafutaji wa yale yenye manufaa kwa watu wote. Ni kitu cha muhimu kwamba mamlaka ya namna hii inapatikana kwa maafikiano na kamwe si kwa kulazimisha na wala isieleweke kuwa ni mamlaka inayofananafanana na “Dola ya Kimataifa yenye mamlaka ya hali ya juu sana.”[914]

Mamlaka ya kisiasa inayofanya shughuli zake kwa kiwango cha jamii ya kimataifa inatakiwa ifuate utaratibu wa kisheria izingatie manufaa ya wote na iheshimu ile kanuni ya auni.” Isieleweke kuwa mamlaka hiyo ya juu ya jamii ya kiulimwengu ina nia ya kuzuia au kuweka wigo wa utendaji wa kazi wa ile mamlaka iliyo chini yake na wala haina nia ya kuiondoa; hasha, nia yake ni kuunda msingi thabiti wa kiulimwengu na kuweka mazingira yatakayowezesha mamlaka ya kila jumuiya ya kisiasa, raia wao na mashirika mengine kutekeleza shughuli zao na kutafuta haki zao kwa usalama zaidi.[915]

442. Kutokana na utandawazi wa matatizo, suala linalohusu uhamasishaji wa kisiasa kwa kiwango cha kimataifa unaofuatilia malengo ya amani na maendeleo kwa kukubali na kuziafiki hatua zilizoratibiwa, limekuwa jambo lenye umuhimu zaidi kuliko ilivyokuwa hapo awali.[916] Majisterio inatambua kwamba uhuru uliopo kati ya watu na kati ya mataifa unachukua hali ya kiuadilifu na ni kipengele muhimu cha kusaidia kufanya maamuzi ya kiuchumi, kiutamaduni, kisiasa na kidini katika masuala ya mahusiano katika ulimwengu huu wa kisasa. Katika muktadha huu inatumainiwa kuwa kutakuwa na mapitio ya mashirika ya kimataifa, mchakato unaodhaniwa kwamba utaudhoofisha ushindani wa kisiasa na utayakataa matamanio yote ya kuyaendesha mashirika haya ambayo yapo kwa manufaa ya wote [917] na kwa lengo la kufanikisha kufikia “kiwango cha juu zaidi cha mpangilio wa kimataifa.”[918]

Kuna umuhimu wa pekee kwa miundo ya serikali mbalimbali kutekeleza majukumu yao ya kurekebisha na kutoa maelekezo katika maeneo ya kiuchumi kwa kuwa upatikanaji wa manufaa kwa wote limekuwa lengo ambalo haliwezi kufikiwa na kila dola kivyake hata kama dola hiyo ina nguvu, mali na uwezo wa kisiasa.[919] Wakala wa kimataifa lazima watoe uhakikisho wa upatikanaji usawa ambao ni kigezo muhimu cha msingi wa haki kwa wote kushiriki katika mchakato wa maendeleo kamili, na wakati huohuo wakiheshimu zile tofauti zinazokubalika kihalali.[920]

443.  Majisterio wanatoa tathmini iliyo bayana kwa mashirika yale yaliyoundwa katika jamii ya kiraia ili kuyaweka sawa maoni ya umma katika utambuzi wake wa vipengele mbalimbali vya maisha ya kimataifa, ikisisitizwa zaidi kuheshimu haki za binadamu kama ilivyoonekana katika mashirika ya kibinafsi yaliyoanzishwa hivi karibuni. Baadhi ya mashirika haya yana wanachama kutoka pande zote za dunia na yote yakiwa na azma ya kufuatia kwa uangalifu na bila upendeleo kinachotokea kimataifa katika eneo hili nyeti.[921] Serikali zijisikie kuhimizwa na misimamo ya watu mbalimbali inayokusudia kutekeleza kwa dhati yale maadili ya kimsingi ya jumuiya ya kimataifa, hasa kwa ishara mbalimbali za mshikamano na za amani zinazojionesha kwa matendo ya watu binafsi waliojihusisha na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali na vyama vingine kwa ajili ya kutetea haki za binadamu.[922]

b. Hadhi ya Kisheria ya Kiti cha Kitume

444. Kiti cha Kitume,[923] kinafaidika na udhahania (subjectivity) kamili, kama mwenye mamlaka kamili ya kutenda mambo ambayo kisheria ni ya kwake. Kiti cha Kitume kinatekeleza uwezo kamili nje ya mipaka yake (nchi) unaotambulika ndani ya muktadha wa jumuiya ya kimataifa ambayo inaonyesha utekelezaji huo ndani ya Kanisa na inaonyeshwa hivyo kwa kuwa na umoja ulio katika mpangilio na uhuru. Kanisa linatumia njia za kisheria zilizo za lazima au zinazosaidia katika kutekeleza utume wake.

Shughuli za kimataifa za Kiti cha Kitume zinadhihirishwa kwa namna iliyo wazi na vipengele kadhaa tofauti kama hivi vifuatavyo: Haki ya ujumbe mshiriki na ujumbe mwakilishi matumizi ya ‘ius contrahendi’ katika masharti ya mikataba; ushirikishwaji katika mashirika yanayozihusu serikali mbalimbali kama mashirika yale yanayosaidiwa na Umoja wa Mataifa na uwezo wa kuanzisha mazungumzo ya kuleta suluhu kunapotokea migogoro. Shughuli hii inalenga kwenye utoaji wa huduma kwa jumuiya ya kimataifa isiyoegemea upande wowote kwa kuwa haina maslahi ya binafsi isipokuwa kuleta manufaa kwa familia nzima ya binadamu. Katika mazingira haya, Kiti cha Kitume hasa kinatoa msaada kwa wanadiplomasia wake.

445. Huduma ya kidiplomasia ya Kiti cha Kitume ambayo ni huduma kongwe na ya kuaminika ni chombo ambacho hakifanyi kazi kwa ajili Uhuru wa Kanisa tu, lakini pia kwa ajili ya ulinzi, na ukuzaji wa hadhi ya utu wa binadamu pamoja na uhamasishaji na uendelezaji wa mpango wa kijamii wenye misingi yake katika tunu za haki, ukweli, uhuru na mapendo. Kwa hulka ya haki ya kimaumbile ambayo tunayo katika ujumbe wetu wa kiroho na kuendelezwa na mfumuko wa matukio ya kihistoria kwa karne nyingi, tunatuma pia mabalozi wetu katika nchi mbalimbali zenye uhusiano na Kanisa Katoliki au nchi zile ambazo Kanisa Katoliki limo kwa namna moja au nyingine. Ni kweli kabisa kwamba madhumuni ya Kanisa na yale ya Dola ni ya mpangilio tofauti na yote ni mashirika yaliyokamilika kila moja kwa hiyo linatumia njia na namna zake, na ni huru katika utekelezaji wa shughuli zao. Lakini ni kweli pia kwamba mashirika haya yote mawili yamejitolea kutoa huduma kwa kitu kilekile kimoja, yaani mtu aliyeitwa na Mungu kuelekea kwenye uzima wa milele na ambaye amewekwa duniani ili kwa msaada wa neema za Mwenyezi Mungu aupate huo uzima wa milele kutokana na mastahili ya kazi yake yanayomletea uzima katika mpangilio wa amani wa kijamii.”[924] Manufaa ya watu na yale ya jumuiya za kibinadamu yanahudumiwa kwa mazungumzo kati ya Kanisa na mamlaka ya kiraia, kitu ambacho kinaonekana pia katika masuala ya masharti ya maelewano ya pande hizo mbili. Mazungumzo kati ya pande hizo mbili yanaelekea kujenga na kuimarisha mahusiano ya maelewano pamoja na ushirikiano wa pande zote mbili. Mazungumzo haya yanasaidia pia kuzuia kama si kumaliza kabisa mabishano yanayoweza kujitokeza hapo baadaye. Madhumuni yake ni kutoa mchango kwa mambo ya maendeleo ya kila mtu na ya binadamu wote kwa jumla katika masuala ya haki na amani.

 

IV. USHIRIKIANO WA KIMATAIFA KWA AJILI YA MAENDELEO

a. Ushirikiano wa Kuhakikisha Haki ya Maendeleo

446. Ufumbuzi wa matatizo ya maendeleo unahitaji ushirikiano wa jumuiya za kisiasa.  “Jumuiya za kisiasa zinahimizana na kulazimishana na zinatufanya tukiri kwamba kila moja inakuwa na mafanikio katika maendeleo yake kwa kutoa mchango wake kwa ajili ya maendeleo ya jumuiya zingine. Ili kweli mambo yawe hivyo, ni muhimu kuwe na maelewano na ushirikiano.”[925] Inaweza kuonekana kuwa si rahisi kukiondosha kiwango cha chini cha maendeleo ya watu kama isivyo rahisi kuibatilisha hukumu ya kunyongwa hasa ukizingatia kuwa haya si matatizo yanayotokana na uchunguzi tu mbaya wa kibinadamu bali ni pia matokeo ya “kiuchumi, kifedha na utaratibu wa kufanya mambo”[926] pamoja na “miundo ya dhambi”[927] inayozuia ukamilifu wa maendeleo ya binadamu na ya watu wote kwa jumla.

Matatizo haya lazima, hata hivyo yakabiliwe kwa maamuzi ya kweli na ya dhati kwa sababu maendeleo si hamu tu ya kupata kitu bali ni haki [928] ya kukipata kitu hicho na kama ilivyo kwa kila haki, upo vilevile wajibu unaoendana na utafutaji wa haki husika. “Ushirikiano katika kumwendeleza mtu kwa jumla na kumwendeleza kila binadamu ni wajibu wa kila mtu kwa manufaa ya wote na ni lazima uchangiwe na pande zote nne za dunia; Mashariki na Magharibi, Kaskazini na Kusini.”[929] Kama Majisterio wanavyosema, haki ya maendeleo ina misingi yake katika kanuni zifuatazo: umoja wa asili na majaliwa yanayofanana na familia ya kibinadamu; usawa wa binadamu; ukomo wa mazuri ya ulimwengu na dhana ya maendeleo kwa ujumla wake; wa uwepo wa binadamu kama mhimili na nguzo ya mshikamano.

447. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanashauri na kuhimiza kuwa kuwe na ushirikiano ili kuziwezesha nchi maskini kuweza kuingia katika soko la kimataifa. Hadi miaka ya hivi karibuni tu ilidhaniwa kuwa nchi maskini zingeweza kuendelea kwa kutegemea rasilimali zao tu na kujitenga na soko la kimataifa. Lakini uzoefu umebainisha kuwa dhana hii ilikuwa potofu kutokana na ukweli uliojitokeza kwamba nchi zilizokuwa na dhana hii zimedorora na zimerudi nyuma kimaendeleo. Nchi zilizoonesha maendeleo ni zile zilizojihusisha na shughuli za kiuchumi katika kiwango cha kimataifa. Kwa hivyo, inaonekana kuwa tatizo kubwa ni lile la kujipenyeza na kulifikia soko la kimataifa si kwa kuangalia upande mmoja tu wa ile kanuni ya matumizi ya rasilimali ya nchi hizi bali kwa kuzingatia matumizi mwafaka ya rasilimali hizo.”[930] Kati ya sababu zinazosababisha maendeleo duni na umaskini uliokithiri ni pamoja na ile hali ya kukosa uwezo wa kulifikia soko la kimataifa[931] ni ujinga wa kutojua kusoma na kuandika, ukosefu wa sehemu za kuhifadhia chakula kwa usalama, ukosefu wa majengo na huduma, hatua zisizoridhisha za kuhakikisha kuwa kuna huduma za msingi za afya, ukosefu wa maji salama na safi ya kunywa, rushwa, kutotengamaa kwa taasisi za umma na kwa maisha na mambo ya kisiasa kwa jumla. Katika nchi nyingi, kuna uhusiano kati ya umaskini na kukosekana kwa uhuru, uwezekano wa upatikanaji wa ari kwa masuala ya kiuchumi na uongozi wa kitaifa wenye uwezo wa kuunda mfumo mzuri wa elimu na mawasiliano.

448. Ari ya kuwa na ushirikiano wa kimataifa inahitaji uelewa wa wajibu wa kuutafuta na kuupata mshikamano pamoja na kuonesha haki na wema kwa watu wote na si ile fikra tu ya soko.[932] Kwa kweli kuna “kitu kinachomhusu na kumgusa mtu kutokana na ule ukweli kuwa yeye kama mtu ana hadhi ya hali ya juu sana.”[933] Ushirikiano ni njia ambayo jumuiya yote ya kimataifa ni lazima ifuate “kwa mujibu wa maana halisi ya manufaa kwa wote kuihusu familia yote ya binadamu.”[934] Matokeo mengi ya kutia moyo yanatokana na ukweli huu, kwa mfano kule kuongezeka kwa imani kuwa nchi na watu maskini wana uwezo wa kufanya mambo na wanaweza pia kuwa na mgawanyo sawa wa mali inayozalishwa.

b. Vita dhidi ya Umaskini

449. Mwanzoni mwa Milenia Mpya, umaskini wa mabilioni ya watu wanaume kwa wanawake limekuwa “suala moja kubwa linalotoa changamoto kwa dhamiri zetu za kibinadamu na za Kikristo.”[935] Umaskini unaleta tatizo kubwa linalojitokeza kisheria katika sura zake mbalimbali zikiambatana na athari zake kadhaa. Umaskini huo unaainishwa na kukua kusikokuwa na uwiano na kusikotambua “haki sawa ya watu wote kuchukua nafasi yao” kwenye meza ya dhifa ya pamoja.”[936] Umaskini kama huu unafanya isiwezekane kuufanya ule ubinadamu kamili unaotegemewa na kufuatiliwa na Kanisa kwa madhumuni ya kuwafanya watu na binadamu wote kwa jumla “kuonekana binadamu zaidi”[937] na kuishi katika mazingira yenye ubinadamu zaidi.[938]

Vita dhidi ya umaskini inalifanya Kanisa lihamasishwe zaidi na liongoze mapendo yake kwa watu maskini.[939] Katika ufundishaji wake kuhusu masuala ya jamii, Kanisa halichoki kusisitiza tena na tena kanuni fulanifulani za msingi za mafundisho haya na kanuni ya kwanza kabisa ikiwa ile ya ukomo wa mazuri ya kidunia.[940] Katika kuweka msisitizo wa kanuni ya mshikamano, Mafundisho ya Kanisa kuhusu masuala ya kijamii inadai uendelezaji wa “kile ambacho ni chema kwa ajili ya wote na kwa ajili ya kila mmoja, kwa sababu, kwa kweli kila mmoja anawajibika kwa mwenzake.”[941] Kanuni ya mshikamano hata mshikamano ule unaopinga umaskini inatakiwa daima iendane, kwa uwiano unaofaa na kanuni ile ya auni ambao kwa msaada wake inawezekana kuendeleza moyo wa kuwa na ari ya utendaji ambao ni msingi muhimu wa maendeleo yote ya kijamii na kiuchumi katika nchi maskini.[942] Maskini wasionekane “kama ni tatizo bali waonekane kama watu wanaoweza kuwa wajenzi wakuu wa maisha yenye ubinadamu zaidi kwa wote.”[943]

c. Deni la nje

450. Haki ya kupata maendeleo isipuuzwe wakati masuala yanayohusiana na migogoro ya madeni ya nje ya nchi maskini yanaposhughulikiwa.[944] Vyanzo changamania vya aina nyingi ndio chimbuko la migogoro ya madeni. Katika kiwango cha kimataifa huwa kuna mabadilikobadiliko ya kima cha mabadilishano ya fedha, bahatisho la fedha, ukoloni mamboleo wa kiuchumi na kila nchi inayodaiwa huwa imejaa rushwa na ina matumizi mabaya ya fedha za umma na ya fedha za mikopo. Matatizo na mateso makubwa yasababishwayo na masuala ya kimuundo na yale ya tabia za wahusika yanawapata watu wa nchi maskini zenye madeni ambao, kwa kweli, hawana uhusiano wowote, na wala hawawajibiki na kuwepo kwa hali hii. Jumuiya ya kimataifa haiwezi kupuuzia ukweli huu. Pamoja na msisitizo unaowekwa kuwa madeni haya lazima yalipwe, kuna haja pia ya kutafuta njia muafaka na zisizohatarisha “haki za kimsingi za watu za kujikimu na za kuongeza kasi ya maendeleo yao.”[945]

 

SURA YA KUMI

UTUNZAJI WA MAZINGIRA

I. VIPENGELE VYA BIBLIA

 

451. Uzoefu hai wa uwepo wa Kimungu katika historia ni msingi wa imani ya watu wa Mungu. “Tulikuwa watumwa wa Farao katika nchi ya Misri; Bwana akatutoa kutoka Misri kwa mkono wa nguvu” (Kum. 6: 21). Historia inaturuhusu kupata fununu ya mambo yaliyopita na kumwona Mungu akifanya kazi yake. Mungu anaweza kusema kuwa “Mtu wa kabila la Mwarami ambaye hakuwa na makazi alikuwa baba yangu (Kum 26: 5); kwa watu wake Mungu anaweza kusema: “Nilimchukua baba yenu Ibrahimu kutoka ng’ambo ya pili ya mto” (Yos 24: 3).  Kumbukumbu hii ya nyakati zilizopita inatufanya tuweze kuangalia kwa matumaini yale yajayo ambayo yana muhimili wake kwenye agano na ahadi ambazo Mungu anaendelea kuzifanya upya.

Imani ya Waisraeli ambayo kwa sasa bado inaishi hapa ulimwenguni, haichukuliwi kama dhana isiyofaa au kama kitu kibaya, bali ni kama zawadi ya Mungu aliyoikabidhi kwa mamlaka ya binadamu yenye utendaji na uwajibikaji. Hali ya asili ambayo ni kazi ya ubunifu wa Mungu haina ushindani wowote wa hatari. Ni Mungu aliyeumba vitu vyote, na kuhusu chochote kile kilichoumbwa “Mungu aliona kuwa ilikuwa vyema kufanya hivyo” (taz. Mwa 1: 4, 10, 12, 16, 21 na 25). Kwenye kilele cha kazi ya uumbaji huu ambacho “kilikuwa kizuri sana” (Mwa 1: 31), Mungu alimweka mtu. Kati ya viumbe vyote vilivyoumbwa na Mungu ni mtu tu, mwanaume na mwanamke ndio walioumbwa na Mungu “kwa mfano wake” (Mwa 1: 27). Bwana alivikabidhi vyote vilivyoumbwa naye uwajibikaji na akaviamuru viangalie muafaka na maendeleo yao (Mwa 1: 26 – 30). Mapatano haya maalumu na Mungu yanaiweka wazi ile nafasi ya upendeleo aliyoitoa Mungu kwa hao watu wawili wa kwanza, kuwa mume na mke katika utaratibu wa uumbaji.

452. Uhusiano wa mtu na ulimwengu ni sehemu ya utambulisho wa ubinadamu wake. Uhusiano huu kwa namna nyingine tena ni matokeo ya uhusiano wa ndani zaidi kati ya mtu na Mungu. Bwana amemfanya binadamu kuwa mwenzi kwa njia ya mazungumzo. Ni katika mazungumzo tu na Mungu, binadamu anaupata ukweli wake unaomwezesha kupata msukumo na kanuni za kufanya mipango ya baadaye ya ulimwengu, ambayo huwa ni bustani aliyompa Mungu ailime na aitunze (taz. Mwa 2: 15). Wajibu huu wa mtu mwenye hadhi ya juu haukuweza kuondolewa hata na dhambi pamoja na ukweli kwamba dhambi ilipunguza uzito wake kwa maumivu na mateso (taz. Mwa 3: 17 – 19).

Uumbaji daima ni kitu cha sifa katika sala ya Waisraeli “Ee Bwana, jinsi yalivyo mengi matendo yako! Kwa hekima umevifanya vyote pia (Zab. 104: 24). Ukombozi unaeleweka kama ni uumbaji mpya unaojenga ule upatanisho ambao dhambi ilikuwa imeuharibu. “Tazama mimi naumba mbingu mpya na nchi mpya” (Isa 65: 17) asema Bwana ambamo “mwitu huwa shamba lenye kuzaa matunda. haki itabaki katika shamba lenye kuzaa matunda. watu wangu watakaa katika makazi yenye amani (Isa 32: 15 – 18).

453. Ukombozi wa uhakika kabisa anaoutoa Mungu kwa binadamu wote kwa kupitia Mwanae haufanyiki nje ya dunia hii. Baada ya kujeruhiwa kwa dhambi, dunia inatakiwa ijikane kabisa (taz. 2 Pet. 3: 10) ili iwe dunia mpya (taz. Isa 65: 17; 66: 22; Ufu 21: 1) na mwisho kabisa pawe pahali pale ambamo “haki yakaa ndani yake” (2 Pet. 3: 13).

Katika shughuli zake za kiuchungaji, Bwana Yesu anatumia vitu vya asili. Yeye si tu kwamba ni mkalimani mahiri wa hali ya asili au hulka ambayo aliiongelea kwa mifano na mafumbo lakini pia anaimiliki (Mt. 14: 22 – 33; Mk. 6: 45 – 52; Lk. 8: 22 – 25; Yn. 6: 16 – 21). Bwana wetu anaitumia hali hii ya asili katika mpango wake wa ukombozi. Anawaomba wafuasi wake waviangalie vitu, wayaangalie majira ya mwaka na wawaangalie watu na wajione kama watoto wanaojua na kuamini kwamba hawataachwa na Baba yao mwenye Busara na anayeona mbali (taz. Lk. 11: 11- 13). Badala ya kujifanya watumwa wa vitu, wafuasi wa Yesu yawapasa wajue namna ya kuvitumia vitu hivi ili kuwe na mahusiano mazuri na kuwe na udugu (taz. Lk. 16: 9 – 13).

454. Kuingia na kuonekana kwa Yesu Kristo katika historia ya ulimwengu, kunafikia kilele chake katika Fumbo la Pasaka, wakati maumbile yanaposhiriki katika drama ya kumkataa Mwana wa Mungu na hatimaye katika ushindi wake wa kishindo wa ufufuko (taz. Mt. 27: 45, 51; 28: 2). Kwa kuvuka kupitia kifo na kukinaksisha kifo hicho kwa ufufuo, Yesu anazindua dunia mpya ambamo kila kitu kinatawaliwa na yeye Mwenyewe (taz. I Kor. 15: 20 – 28) na anaunda upya mahusiano yale mapya ya mpangilio na upatanifu, yaliyokuwa yameharibiwa na dhambi. Kujulikana kwa hali ya kutokuwa na urari ambako kupo kati ya mtu na maumbile kungefuatiwa na utambuzi wa kupitia kwa Yesu upatanisho wa mtu na ulimwengu kwa Mungu, kwamba kila binadamu anayetambua mapendo ya Kimungu anaweza kuona kwa mara nyingine tena amani iliyokuwa imepotea – imepatikana. “Kwa hiyo mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita; tazama! Yamekuwa mapya” (2 Kor 5: 17). Maumbile yaliyokuwa yameumbwa na Neno, yamepatanishwa na Mungu na kupewa amani mpya kwa Neno lilelile lililokuwa amani mpya (Kor. 1: 10 – 20).

455. Si tu kwamba hali ya mtu ya ndani imekamilishwa kwa mara nyingine tena bali maumbile yake yote ya kimwili yameguswa kwa uwezo wa wokovu wa Kristo. Uumbaji wote unashiriki katika ukamilishaji tena wa uumbaji huo unaobubujika kutoka kwenye Fumbo la Bwana la Pasaka, ingawa bado unasubiri ukombozi kamili kutoka uharibifu unaokuja (taz. Rum. 8: 19 – 23) kwa mategemeo ya kuwa na “Mbingu mpya na nchi mpya” (Ufu 21: 1) matukio ambayo ni mwisho wa nyakati, ukamilishaji wa wokovu. Kwa wakati huu uliopo, hakuna kilicho nje ya wokovu huu. Maisha yake yawayo yote, Mkristo anaitwa kumtumikia Kristo, kuishi kadiri ya maelekezo yake, akiongozwa na upendo ambao ni kanuni ya maisha mapya yanayoirudisha nyuma dunia na binadamu kwenye majaliwa yao ya asili. “Bila kujali kama. dunia, au uzima, au mauti; vile vilivyopo sasa, au vile vitakavyokuwepo; yote ni vyenu; nanyi ni wa Kristo na Kristo ni wa Mungu” (1 Kor. 3: 22 – 23).

 

II. MTU NA VITU VYOTE VILIVYOUMBWA

456. Maono ya kibiblia yanawapa Wakristo msukumo kuhusu matumizi ya dunia na hasa zaidi sana kuhusu maendeleo ya kisayansi na ya kiteknolojia. Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatikano ulikiri kuwa mtu “anakitolea hukumu na haki kile ambacho kwa kulingana na uwezo wake wa kufikiri, anaushinda ulimwengu yakinifu kwa kuwa anashiriki katika mwanga wa akili ya Kimungu.”[946] Mababa wa Mtaguso walikiri maendeleo yaliyofikiwa na walitoa shukrani zao kwa jinsi binadamu alivyokuwa ameamua kutumia vipaji vyake kwa karne na karne bila kuchoka, katika masuala ya sayansi jarabati, masomo ya teknolojia au masomo ya sanaa na sayansi za kijamii.[947] Leo “hasa kwa msaada wa sayansi na teknolojia, binadamu ameongeza sana uwezo wake kwa karibu maumbile yote na anaendelea kufanya hivyo.”[948]

Kwa binadamu “aliyeumbwa kwa mfano wa Mungu, alipokea amri na mamlaka ya kuidhibiti dunia na vitu vyote vilivyomo, na kuutawala ulimwengu kwa haki na utakatifu, mamlaka ya kujihusisha mwenyewe na kuvihusisha vitu vyote kwa ujumla wake kwake yule ambaye alipaswa akiriwe kama ndiye Bwana na Muumbaji wa vyote. Hivyo, kwa kuvifanya vitu vyote vidhibitiwe na binadamu, ulimwengu wote utalistaajabia jina la Mungu. Kwa karne na karne, binadamu wamejitahidi kuyaboresha mazingira yao kwa juhudi ya kila mmoja peke yake na kwa juhudi ya pamoja. Kwa waamini, suala hili limefikia ukomo; likizingatiwa kwa lenyewe, shughuli hii ya binadamu inakubaliana kabisa na mapenzi ya Mwenyezi Mungu.”[949]

457. Matokeo ya sayansi na teknolojia ni dhahiri na ni ya kutia moyo. “Si sahihi kufikiri kwamba kazi zilizofanywa kwa kutumia akili na jitihada za mtu zinapingana na uwezo wa Mungu na kwamba kiumbe chenye uwezo wa kufikiri ni mpinzani wa Muumba. Wakristo wanaamini kwamba ushindi wa taifa la binadamu ni dalili ya neema ya Mungu na ustawi wa mtindo au mpango wake wa siri.”[950] Mababa wa Mtaguso vilevile wanasisitiza ule ukweli kwamba “jinsi uwezo wa mtu unavyoongezeka, vivyo hivyo uwajibikaji wake yeye mwenyewe binafsi na ule wa kijamii unavyozidi kupanuka,”[951] na kwamba kila tendo la binadamu lilingane na uzuri mwafaka wa watu kwa mujibu wa mpango wa utashi wa Mungu.[952] Kwa maana hiyo, Majisterio imerudia kusisitiza tena na tena kwamba Kanisa Katoliki halipingi maendeleo kwa namna yoyote ile.[953] Badala yake linaelewa na kuamini kuwa “sayansi na teknolojia ni matokeo ya ajabu ya ubunifu wa mtu aliopewa na Mungu kwa kuwa matokeo hayo ya ajabu yametuwezesha kufanya mambo mengi ya kushangaza na sisi sote tunashukuru kwa manufaa hayo tuyapatayo.”[954] Kwa sababu hiyo, “kama watu wanaomwamini Mungu, watu walioona kuwa maumbile aliyoyaumba yalikuwa ‘mazuri,’ tunaifurahia teknolojia hii na maendeleo ya kiuchumi ambayo watu kwa kutumia akili yao wamefanikiwa kuyafikia.”[955]

458. Fikra za Majisterio kuhusu sayansi na teknolojia kwa jumla zinaweza pia kutumika kwa masuala ya mazingira na kilimo. Kanisa linatambua na kukiri “manufaa yanayopatikana na yanayoweza bado kupatikana kutokana na mafunzo na matumizi ya biolojia ya kimolekuli yaliyojaliziwa na masomo mengine kama vile masomo ya genetiki na matumizi yao katika kilimo na viwanda.”[956] Kwa kweli, teknolojia “ingeweza kuwa chombo kisicho na gharama katika kutatua matatizo mazito kama yale yanayohusu njaa na magonjwa kwa kuzalisha aina ya hali ya juu na nzuri zaidi ya mimea na kwa kuzalisha aina bora ya madawa.”[957] Ni jambo muhimu, hata hivyo, kukumbushana juu ya dhana ya “matumizi sahihi” kwa kuwa tunajua kwamba uwezo huu unaweza pia kuwa na madhara kwa binadamu ukitumika vibaya, au kwa maendeleo yake ukitumika vizuri.[958] Kwa sababu hii, “kuna umuhimu wa kuwa na busara ya kuchunguza kwa makini maumbile, hatima na uwezo wa aina mbalimbali za kiteknolojia.”[959] Kwa hiyo, wanasayansi hawana budi “kutumia utafiti na utaalamu wao wa kiufundi kwa kutoa huduma kwa binadamu.”[960] Hata hivyo, utaalamu huu lazima udhibitiwe na wautumie kwa manufaa ya binadamu na kwa kuzingatia kanuni ambazo zinaleta heshima ya hali ya juu kwa binadamu.[961]

459. Kitu muhimu cha kukumbuka kwa matumizi ya uvumbuzi wa kisayansi na wa kiteknolojia ni heshima ya uvumbuzi huo kwa watu wote, wanaume na wanawake ambayo lazima pia iambatane na msimamo muafaka na wa ulazima kwa viumbe hai vingine. Hata kama kuna mawazo ya kuvisababishia mabadiliko, “maumbile ya kila kimojawapo na mahusiano ya pande zote mbili lazima vizingatiwe kwa muundo wenye mpangilio unaokubalika.”[962] Kwa maana hiyo, matokeo ya kuogofya ya utafiti wa kibiolojia yanaleta wasiwasi mkubwa kwa vile “hatuna bado uwezo wa kukadiria machafuko ya kibiolojia ambayo yangesababishwa na utumiaji wa kijenetiki usio na mpangilio mzuri na uendelezaji usiofaa wa aina ngeni za mimea na uhai wa viumbe, achilia mbali majaribio yasiyokubalika kuhusu asili ya uhai wenyewe wa binadamu[963] Kwa kweli “sasa inajulikana wazi kuwa matumizi ya uvumbuzi huo katika nyanja za viwanda na kilimo yamesababisha madhara ambayo yatadumu kwa muda mrefu ujao. Ukweli huu umesababisha hali ya kusikitisha ya kutufanya tukiri kwamba hatuwezi kujiingiza katika eneo moja la mfumo wa ikolojia bila kujali matokeo ya kujiingiza huku katika maeneo mengine na kwa ustawi wa vizazi vijavyo.”[964]

460. Mtu, kwa hiyo, asisahau kwamba “uwezo wake wa kuubadili na kwa maana nyingine, kuumba ulimwengu kwa kazi yake mwenyewe. uko daima katika karama za mwanzo na za asili za vitu ambavyo vipo.”[965] Asiitumie “dunia kiholela na jinsi apendavyo kama vile haikuwa na mahitaji yake yenyewe na haikuwa na madhumuni kutoka kwa Mungu ambayo kwa kweli binadamu anaweza kuyaendeleza lakini kamwe asiyasaliti.[966] Anapofanya hivyo “badala ya kutekeleza majukumu yake kama mshirika wa Mungu katika uumbaji, mtu anajiweka mwenyewe badala ya Mungu na hivyo kuishia katika kujifanya Mungu na hapo huuharibu ulimwengu badala ya kuutawala.”[967]

Iwapo mtu anayaingilia mazingira bila kuyatumia vibaya au kuyaharibu, tunaweza kusema kwamba “hayaingilii kwa nia ya kuyabadilisha bali anayaendeleza katika mpangilio wa uumbaji uliokusudiwa na Mungu. Wakati akifanya kazi katika eneo hili ambalo wazi kabisa ni nyeti, mtafiti anashikilia na kufuata mtindo wa Mungu. Mungu alimtaka mtu awe mfalme wa uumbaji.”[968] Mwisho, ni Mungu mwenyewe anayewapa watu, wanaume na wanawake, heshima ya kushiriki katika kazi ya uumbaji kwa nguvu yake ya maarifa na akili yao.

 

III. UPEO WA MGOGORO KATIKA UHUSIANO KATI
YA MTU NA MAZINGIRA

 

461. Ujumbe wa Kibiblia na Majisterio wanawakilisha vigezo muhimu vya tathmini ya matatizo ya uhusiano yaliyopo kati ya mtu na mazingira.[969] Sababu za msingi za matatizo haya zinatokana na ile hali ya binadamu ya kujifanya kuwa ana uwezo usio na masharti wa kuvitawala viumbe bila kujali mambo mengine ya kimaadili ambayo kwa namna nyingine lazima yavipambanue vitendo vyote vya kibinadamu.

Hali ya kuelekea kwenye “ugonjwa unaochukuliwa kama [970] unyonyaji wa mali ya uumbaji ni matokeo ya mchakato wa kihistoria na wa kiutamaduni wa muda mrefu. Hali tuliyo nayo kwa wakati huu wetu wa sasa unashuhudia ongezeko la uwezo wa mtu kuingilia kati mabadiliko yanayotokea. Kipengele cha kutaka na kuchukua rasilimali kimepata nguvu na kimeshika kasi ya kusambaa hadi kufikia kiwango cha kutishia ile hali nzuri ya mazingira na ya ukarimu wake; mazingira ambayo ni kama ‘rasilimali’ huthubutu kuyatishia mazingira ambayo ni ‘makazi’ ya rasilimali hiyo. Kutokana na uwezo pamoja na mbinu zitumikazo katika mabadiliko haya ya kiteknolojia, huonekana mara nyingine kuwa uwiano kati ya mtu na mazingira umefikia upeo wa hali ya juu wa matatizo.”[971]

462. Maumbile huonekana kama chombo kilicho mikononi mwa mtu ambacho lazima akitawale kwa ufundi hasa kwa ufundi wa njia ya kiteknolojia. Dhana ya hali ya kupungua kwa kitu ikaanza kuingia upesiupesi vichwani mwa wanasayansi – dhana iliyoonekana kuwa haikuwa sahihi – kwamba ukubwa usio na mipaka wa nishati na rasilimali unaweza kupatikana na kuboreshwa kwa haraka na kwamba matokeo hasi ya uendelezaji wa mpango wa maumbile ya asili unaweza kutumiwa kwa urahisi. Dhana hii ya kupungua kwa kitu inayachukulia maumbile ya kiulimwengu kwa mujibu wa nadharia inayoamini kuwa asili ya ulimwengu na vitu vyote vilivyomo ni matatizo na kuyaeleza maendeleo kama ufujaji. Kutenda na kuwa na kitu huonekana kuwa ni bora zaidi kuliko uwepo wa kitu, na imani hii huleta matokeo mabaya ya utengano wa kibinadamu.[972]

Mitazamo kama hii haitokani na utafiti wa kisayansi wala wa kiteknolojia, bali hutokana na imani iliyokithiri isiyofaa juu ya matokeo ya kisayansi na pia nadharia potofu ya wasomi wachache wenye uwezo wa kumiliki vyombo vya utafiti. Maendeleo ya kisayansi na ya kiteknolojia hayaondoshi yale maendeleo ya kufanya vitu kupita kiasi na wala maendeleo haya si chanzo cha kujiondoa kwenye dini kwa maudhi yanayosababishwa kwa kuikataa dini na sheria zote za ubinadamu. Kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia udadisi wa kutaka kuyajua zaidi mambo haya huongezeka na kusababisha ongezeko la kumheshimu zaidi binadamu na kuuheshimu uumbaji wenyewe.

463. Uelewa sahihi wa mazingira unasaidia kuzuia maumbile yasifanywe kuwa chombo cha kupatia faida tu na kuendeleza unyonyaji. Hapohapo, maumbile yasitawaliwe kiasi cha kuifanya heshima ya binadamu mwenyewe idhalilike. Hali kama hii huonekana pale maumbile na dunia yenyewe zinapotukuzwa mithili ya Mungu kama ionekanavyo wazi katika vikundi fulani vya kiikolojia vinavyopania kutambuliwa kimataifa katika masuala yao ya kiikolojia wanayoyaamini.[973]

Majisterio inapata mvuto wa kupinga dhana ya kuyaona mazingira katika msingi ulio katika maumbile asili (ecocentrism) na katika viumbe hai (biocentrism) kwa kuzingatia ukweli kuwa “inapendekezwa kwamba tofauti ya asili ya uwepo (ontological) na mambo yahusianayo na tunu (axiological) kati ya watu na viumbe wengine hai iondolewe/isiwepo, kwani wigo wa eneo la uhai unachukuliwa katika umoja wa viumbe bila kutofautisha tunu. Hivyo wajibu mkuu wa mwanadamu unaweza kuondolewa kwa faida ya kujali usawa wa ‘hadhi’ ya viumbe wote hai”.[974]

464. Mtazamo wa mtu na vitu kutojihusianisha na Mungu imeleta makatao ya dhana ya uumbaji na kudhani kuwa kuwepo kwa mtu na asili/maumbile ni kitu kinachojitegemea kabisa. Uhusiano unaounganisha ulimwengu na Mwenyezi Mungu umeharibika. Kuharibika kwa uhusiano huu kumemfanya mtu kwa namna fulani atengwe na ulimwengu na kwa namna ya msingi kumeiharibu sura yake. Binadamu wanadhani kuwa hawana uhusiano wa karibu na mazingira wanamoishi. Matokeo ya dhana hii yapo wazi sana: ni ule uhusiano alio nao mtu na Mungu wake ndio unaoyaweka wazi mahusiano yake na wenzake. Hii ndiyo sababu iliyoufanya utamaduni wa Kikristo daima uvitambue viumbe vinavyomzunguka mtu na uvikiri kuwa vitu hivi ni zawadi kutoka kwa Mungu na hivyo kuna ulazima wa kuvilea na kuvitunza kwa kuonesha shukrani kwa Muumba. Wabenediktini na Wafransiskani katika namna ya kuishi kwao kitawa wameshuhudia uhusiano huu ambao ni wa karibu sana kati ya mtu na mazingira yake ya kibinadamu, uhusiano ambao unamsukuma na kumfanya aviheshimu vitu vyote vinavyomzunguka.[975] Kuna haja ya kuendelea kusisitiza zaidi na zaidi ili kuonesha jinsi uhusiano huu ulivyo wa karibu kati ya ikolojia ya kimazingira na “ikolojia ya kibinadamu.”[976]

465. Majisterio yanatilia mkazo uwajibikaji wa binadamu katika kuyafanya mazingira yawe safi na salama kwa wote.[977] “Iwapo binadamu leo watafanikiwa kuutumia uwezo wao wa kisayansi kwa kuzingatia maadili yanayokubalika, watafanikiwa kuyafanya mazingira wanamoishi watu yawe makazi mazuri ya kuishi. Na wataweza pia kuviondosha vyanzo vya uchafuzi wa mazingira, watajihakikishia vilevile kwamba kuna hali nzuri ya afya na makazi ya vikundi vidogovidogo vya watu, na hata kwa makazi makubwa ya binadamu. Teknolojia yenye uwezo wa kuleta uchafu inaweza pia kuwa na uwezo wa kuondosha uchafu. Uzalishaji wenye uwezo wa kulimbikiza unaweza pia kuwa na uwezo wa kugawa kwa haki. Lakini hivi vyote vinawezekana tu pale maadili yanayoheshimu maisha na utu wa binadamu kwa minajili ya vizazi vya leo na vya kesho yanapotawala na kuongoza.”[978]

 

IV. UWAJIBIKAJI WA WOTE

 

a. Mazingira ni ya Manufaa Kwa Watu Wote

466. Utunzaji wa mazingira unatoa changamoto kwa binadamu wote. Suala la kukiheshimu kile kinacholeta manufaa kwa wote ni wajibu wa pamoja[979] na unawahusu wote kwa kuzuiwa wasizitumie zile aina mbalimbali za viumbe hai na vile visivyo hai kama wanyama, mimea na vitu vya asili kama wapendavyo kwa mahitaji yao ya binafsi ya kiuchumi bila woga wa kuadhibiwa.[980] Huu ni wajibu ambao lazima uzingatiwe ipasavyo kutokana na ukweli wa kuwepo kwa maafa makubwa ya kiikolojia hapa ulimwenguni na ulazima wa kupambana nayo kiulimwengu kwa sababu viumbe vyote vinajitegemea kwa mujibu wa utaratibu uliopangwa na Mwenyezi Mungu. “Mtu lazima azingatie hulka ya kila kiumbe na pia ile ya mahusiano ya muungano wake katika utaratibu wa kimfumo ambao ndio ‘ulimwengu’”[981]

Mtazamo huu una umuhimu wa aina yake pale mtu anapofikiria manufaa ya kimazingira kuhusu hali ya kuwa na tofauti ya matumizi kiuhai ambayo lazima yashughulikiwe kiuwajibikaji na yahifadhiwe kwa uangalifu kwa sababu yana manufaa makubwa kwa binadamu wote katika mazingira ya mahusiano ya karibu yanayofungamanisha sehemu mbalimbali za mfumo wa ikolojia. Kuhusu hilo, kila mtu anaweza kuona, kwa mfano, umuhimu wa Amazoni, moja ya sehemu mashuhuri sana za maumbile ya asili katika ulimwengu huu, kutokana na kuwa na matumizi ya aina nyingi ya uendelezaji wa uhai, ukweli ambao unaufanya ukanda huo uonekane kuwa ni wa lazima kwa uwiano wa kimazingira wa sayari nzima.[982] Misitu inawezesha uwepo wa uwiano asilia ambao ni muhimu kwa maisha.[983] Uharibifu utokanao na uunguzaji misitu moto ovyo ovyo na mara nyingine kwa makusudi, huyafanya maeneo yageuke jangwa kwa haraka na hivyo kusababisha upungufu wa akiba ya maji na kuhatarisha maisha ya wananchi, wenyeji wa asili wa sehemu hizo na yale ya vizazi vijavyo. Mashirika na watu binafsi lazima wajione kuwa wanawajibika kuuhifadhi urithi wa misitu na inapolazimika kukuza na kuendeleza programu za kutosha za kupanda miti upya.

467. Uwajibikaji katika masuala ya mazingira ambayo ni urithi wa watu wote, hauhusu tu mahitaji ya sasa bali pia yale ya baadaye. “Tumerithi kutoka vizazi vilivyopita na tumefaidi kutokana na kazi za wale wa rika letu: Kwa mantiki hiyo tunawajibika kwa hao wote, na hatuwezi kukataa kujihusisha na wale wajao kuipanua familia hii ya binadamu.[984] Huu ni wajibu ambao vizazi hivi vya sasa vinao kwa vizazi vya baadaye,[985] wajibu ambao unaihusu kila Serikali pamoja na jumuiya ya kimataifa.

468. Uwajibikaji katika masuala ya mazingira ungeonekana pia waziwazi zaidi katika ngazi za kisheria. Kuna umuhimu kwa jumuiya ya kimataifa kuweka kanuni za kufanana ambazo zingefuatwa na Nchi kudhibiti kwa ukamilifu vitendo vyote vinavyoathiri mazingira na kulinda mfumo wa ikolojia kwa kuzuia matukio hatari. “Serikali pia ingejishughulisha ndani ya mipaka ya nchi yake kuzuia uharibifu wa angahewa na wa ile sehemu ya dunia ambapo uhai wawezekana kuwepo, kwa kufuatilia pamoja na mambo mengine, matokeo ya maendeleo ya kiteknolojia na ya kisayansi. (na) kuhakikisha kwamba raia zake hawaathiriwi na uchafuzi hatari au takataka zenye sumu.[986]

Maandalizi yale yatakayokuwemo katika kanuni hii ya kisheria isemayo, “haki ya kuwa na mazingira asilia ambayo ni salama na yenye kuleta afya” [987] yanaendelea vizuri. Maandalizi ya kanuni hii yamechochewa na wasiwasi uliooneshwa na maoni ya umma katika kufundisha namna ya kutumia bidhaa zilizotengenezwa kulingana na mahitaji ya vitu bora na katika kufikiria namna ya kuwaadhibu wale wanaochafua mazingira. Lakini hatua za kisheria peke yake hazitoshi.[988] Hatua hizi ni lazima ziende sambamba na uongezekaji wa uwajibikaji pamoja na mabadiliko ya dhati ya tabia na namna ya kuishi.

469. Mabingwa wa masuala haya walioitwa kutoa maamuzi yanayohusu afya na athari za kimazingira wanajikuta mara nyingine wanakwama kuamua kutokana na data walizo nazo kuhitilafiana au kuwa pungufu. Kutokana na tatizo hili, linakuwa jambo la busara kufanya tathmini kwa kuzingatia misingi ya “Kanuni ya tahadhari” ambayo haina ulazima wa kutumia kanuni yenyewe bali miongozo fulani fulani yenye madhumuni ya kuidhibiti ile hali ya kutokuwa na uhakika. Hii inaonesha kuwa kuna haja ya kuwa na maamuzi ya muda ambayo yanaweza kurekebishwa wakati kweli mpya zinapopatikana. Maamuzi haya lazima yawe na uwiano kwa kuzingatia vipengele vile vilivyotangulia kutolewa kwa hatari zingine. Sera za kibusara zinazotegemea ile kanuni ya tahadhari zinadai kwamba maamuzi ya chaguzi mbadala zinazoweza kuwepo yafikiriwe kwa kutegemea ulinganishi wa hatari na faida zilizoonekana hapo awali pamoja na uamuzi wa kutoingilia kati. Mtazamo huu wa kitahadhari unaungana na ule msisitizo wa kufanyika kwa jitihada ya kupata taarifa na elimu zaidi kwa sababu sayansi haiwezi kupata majibu ya harakaharaka kuhusu kutokuwepo au kukosekana kwa hatari. Hali hii ya mazingira ya kutokuwa na uhakika na pia ule ufumbuzi wa muda inadhihirisha kuwepo kwa umuhimu wa pekee wa kuufanya mchakato wa kutoa maamuzi uwe wa wazi.

470. Programu za maendeleo ya kiuchumi lazima zizingatie kwa uangalifu “haja ya kuheshimu hulka na mambo yake yanayojirudia kimsimu” [989] kwa sababu rasilimali si nyingi na nyingine ikishachakaa au ikishatumika haiwezi kuwepo au kufanywa ionekane mpya tena. Mwenendo wa kasi ya unyonyaji uliopo hivi sasa unatishia na kuhatarisha sana upatikanaji wa rasilimali kwa sasa na hata kwa hapo baadaye.[990] Ili ufumbuzi wa tatizo la ikolojia upatikane, ni lazima shughuli za kiuchumi ziheshimu zaidi mazingira zikitafuta uwiano muafaka kati ya mahitaji ya maendeleo ya kiuchumi na yale ya kuyalinda mazingira. Kila shughuli ya kiuchumi inayotumia rasilimali lazima pia ihusike na ulindaji wa mazingira na iangalie mbele ili ione gharama inayohitajika ambayo ni “kitu muhimu cha gharama halisi ya shughuli ya kiuchumi.”[991] Kwa mtazamo huu, mmoja anazingatia mahusiano yaliyopo kati ya shughuli za binadamu na mabadiliko ya hali ya hewa ambayo katika changamania lao la hali ya juu lazima yafuatiliwe kwa wakati muafaka na mara kwa mara kwa ngazi za kisayansi, kisiasa na kisheria, kitaifa na kimataifa. Hali ya hewa ni kitu chenye manufaa na ni lazima ilindwe. Kitu hicho chenye manufaa kinawakumbusha walaji na wale walio katika sekta ya viwanda kukuza zaidi hali ya uwajibikaji kwa mienendo yao.[992]

Uchumi unayaheshimu mazingira hautakuwa na lile lengo moja tu la kuongeza na kudunduliza faida hadi kufikia upeo wake wa juu kabisa kwa sababu ulindaji wa mazingira hauwezi kuhakikishiwa kwa njia moja tu ya kufanya hesabu ya gharama na faida kutokana na fedha iliyopatikana. Mazingira ni moja ya mafao yale ambayo hayawezi kulindwa na kukuzwa kikamilifu kwa nguvu za soko.[993] Kila nchi na hasa nchi zile zilizoendelea lazima ziwe macho na zitambue kwa haraka wajibu wake na zifikirie jinsi mali asilia inavyotumika. Kuwe na uhimizaji wa dhati wa kutafuta njia zingine mpya za kusaidia upunguzaji wa athari za kimazingira katika uzalishaji na utumiaji wa bidhaa.

Kutakuwa na hoja ya kuwa na uangalifu wa pekee kuhusu masuala ya rasilimali za kinishati.[994] Rasilimali zile zisizoweza kukarabatika au kutengenezeka tena ambazo hutumiwa na nchi zilizokwisha kuendelea sana na zile zilizoendelea hivi karibuni tu kiviwanda, lazima zitumike kwa kutoa huduma kwa binadamu wote. Kwa mtazamo wa kimaadili unaozingatia usawa na mshikamano wa vizazi kadhaa, itakuwa pia lazima kuendelea, kwa kupitia mchango wa jumuiya ya kisayansi, kupata vyanzo vipya vya nishati pamoja na kutafuta rasilimali mbadala na pia kuongeza viwango vya nishati ya nyuklia.[995] Matumizi ya nishati katika hali yake kama hiyo inayohusu maendeleo ya mazingira, inahitaji uwajibikaji wa kisiasa wa Serikali, jumuiya ya kimataifa na watendaji wa masuala ya uchumi. Uwajibikaji kama huo lazima ufafanuliwe kwa uwazi zaidi na pia uwe kwa wakati wote kwa manufaa ya wote.

471. Uhusiano uliopo kati ya watu wa makabila ya asili na ardhi yao pamoja na rasilimali, unastahili kushughulikiwa kwa namna ya pekee kwa sababu hii ni alama ya msingi sana inayowatambulisha na kuwatofautisha na kuwapambanua watu hawa.[996] Kutokana na shauku kubwa ya uanzishaji na uendelezaji wa ukulima wa mashamba makubwa kwa kutumia mashine na pia kutokana na mchakato wa kuchangamana pamoja na uanzishaji wa miji, wengi wa watu hao wamekwisha poteza au wapo katika hatari ya kupoteza sehemu zao za ardhi wanamoishi.[997] Ardhi kwa watu hao ni kiini kinachofungamana na umaana wa kuishi kwao.[998] Haki za watu wa makabila ya asili lazima zilindwe ipasavyo na ifaavyo.[999] Watu hawa wanaonesha mfano wa kuishi kimuafaka na mazingira ambayo wamefikia kuyaelewa vizuri na kuyalinda.[1000] Uzoefu wao wa pekee ambao ni rasilimali isiyofidika kwa binadamu ipo katika hatari ya kupotea kabisa pamoja na mazingira ambayo ndimo walimotoka au ndio asili yao.

b. Matumizi ya Bioteknolojia

472. Katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na maswali mengi yenye kuhitaji majibu ya harakaharaka kuhusu matumizi ya namna mpya ya bioteknolojia katika maeneo ya kilimo, ufugaji wa wanyama, shughuli za madawa na utunzaji wa mazingira. Njia mpya ambazo zinaweza kutumiwa na mbinu za kisasa za kibiolojia na za kibiojenetiki ni chanzo cha matumaini na shauku kwa upande mmoja lakini pia ni chanzo cha wasiwasi kwa upande mwingine. Matumizi ya aina mbalimbali ya bioteknolojia, ukubalifu wake kimaadili, matokeo yake kwa afya ya binadamu na kwa mazingira na uchumi ni masuala yanayohitaji uchunguzi wa kina na majadiliano makali. Haya ni maswali yanayoelekea kuzua malumbano yanayowahusu wanasayansi na watafiti, wanasiasa na watunga sheria, wachumi na wanamazingira pamoja na wazalishaji na pia walaji. Wakristo nao wanayajadili matatizo haya kwa sababu wanafahamu fika umuhimu wa faida na manufaa yanayohatarishwa.[1001]

473. Msimamo wa Kikristo kuhusu uumbaji haupingi ukubalifu wa binadamu katika kuingilia kati hulka, pamoja na viumbe vingine hai, mradi tu kunakuwa na uwajibikaji.[1002] Kwa kweli, maumbile si kitu kinachostahili heshima ya kimungu na ambacho mtu hawezi kukisogelea. Kinyume na mawazo haya, hulka ni zawadi iliyotolewa na Muumba wetu kwa jumuiya ya binadamu na kuikabidhi kwa akili na uwajibikaji wa kiakili wa watu wanaume na wanawake. Kwa sababu hiyo binadamu hafanyi kosa la jinai anapoingilia kati na kuzibadilibadili kidogo baadhi ya sifa zao bainifu kwa kuzingatia utaratibu, uzuri na manufaa ya kila kiumbe kwa chenyewe na shughuli zake katika mfumo wa ikolojia. Uingiliaji kati wa binadamu unaoviharibu viumbe hai au mazingira ya asili lazima ushutumiwe, lakini ule unaoiendeleza unastahili sifa. Ukubalifu wa matumizi ya mbinu za ufundi wa kibiolojia na kibiojenetiki ni upande mmoja tu wa tatizo la kimaadili. Kama ilivyo kwa kila tabia ya binadamu, ni muhimu pia kufanya tathmini ya kwelikweli kuhusu manufaa halisi pamoja na hasara zinazoweza kujitokeza siku za baadaye. Ni jambo lisilokubalika kuyachukulia kijuujuu, bali uwajibikaji wa kutosha katika masuala yanayogusa uwanja wa uingiliaji kati kiteknolojia na kisayansi. Masuala haya yenye nguvu na msukumo na ambayo yameenda kwa viumbe hai yanaweza kuleta athari za kudumu.

474. Bioteknolojia za kisasa zina uwezo wa kuingilia masuala ya kijamii ya mahali, ya taifa na hata ya kimataifa. Kwa hiyo, ni lazima vitathminiwe kwa kuzingatia vigezo vya kimaadili ambavyo daima hutoa mwongozo wa shughuli za binadamu na mahusiano yao katika maeneo ya kijamii, kiuchumi na kisiasa.[1003] Zaidi ya yote vigezo vinavyohusu haki na mshikamano lazima vizingatiwe. Watu binafsi na vikundi vinavyojishughulisha na mambo ya utafiti pamoja na wale wanaotaka kuitumia teknolojia hii kibiashara lazima wazingatie vigezo hivi. Kwa vyovyote vile, lazima kuwe na uangalifu ili kukwepa kutumbukia katika kosa la kuamini kuwa uenezaji wa faida zitokanazo na hizi teknolojia mpya za kibioteknolojia zinaweza kuleta ufumbuzi wa matatizo ya umaskini na kudumaa kwa maendeleo, mambo ambayo yanazikabili nchi nyingi hapa duniani.

475. Katika hali ya mshikamano wa kimataifa mengi yanaweza kufanyika kuhusiana na matumizi ya hizi bioteknolojia mpya. Kwanza kabisa tunaweza kuwa na urahisishaji wa mabadilishano ya kibiashara yenye usawa na yasiyo na mzigo wa masharti, yasiyo na haki ya ukuzaji wa maendeleo ya watu walio katika hali ngumu sana. Bila hivyo hautakuwa wa kweli na wa manufaa iwapo utaishia katika ubadilishanaji wa bidhaa tu. Ni jambo la lazima na la msingi kukuza maendeleo huru ya kisayansi na ya kiteknolojia ambayo ni ya muhimu na ya lazima kwa watu hawa; lakini hapohapo ikiendelezwa pia elimu ya ubadilishanaji wa maarifa kisayansi na kiteknolojia kwa nchi changa zinazoendelea.

476. Mshikamano una pia maana ya kuziomba nchi changa zinazoendelea ziwajibike na kuwaomba hasa viongozi wa kisiasa wa nchi hizo kuandaa sera za kukuza biashara zitakazowafaa watu wao na zitakazowawezesha kuwa na ubadilishanaji wa teknolojia itakayoboresha afya na hali ya upatikanaji wa chakula chao. Katika nchi kama hizo lazima kuwe na ongezeko la uwekezaji katika masuala ya utafiti, mkazo ukiwekwa zaidi katika yale maeneo bayana na maeneo yanayoonesha mahitaji ya wananchi wa nchi hizo. Ikumbukwe kuwa tafiti zingine zenye uwezekano wa kuwa na manufaa katika maeneo ya bioteknolojia hazihitaji uwekezaji wa hali ya juu sana. Kutokana na hilo, litakuwa jambo la kufaa kuwa na wakala wa kitaifa watakaowajibika kuyalinda yale yenye manufaa kwa wote kwa kutumia kwa uangalifu zile mbinu za jinsi ya kukabiliana na hatari.

477. Wanasayansi na mafundi sanifu wanaojihusisha na eneo hili la bioteknolojia wanaombwa kufanya kazi kwa juhudi na maarifa katika kuyatafutia ufumbuzi matatizo ya upatikanaji wa chakula na yale yanayohusu afya. Wasisahau kuwa shughuli hii inavihusu viumbe hai na vile ambavyo si hai. Viumbe hivi vyote ni urithi wa binadamu na vinakusudiwa kubaki kwa vizazi vijavyo. Kwa waamini ambao wana jadi za kiitikadi za kiimani wangeweza kusema kuwa hii ni zawadi ya Muumba wetu aliyoikabidhi kwa akili na uwezo wa kufikiri wa binadamu ambavyo navyo pia ni zawadi kutoka mbinguni. Inategemewa kwamba wanasayansi watatumia uwezo walio nao katika utafiti wanaoufanya kwa shauku na kwa dhamiri safi na yenye uaminifu.[1004]

478. Wajasiriamali na wakurugenzi wa wakala wanaojihusisha na huo utafiti pamoja na uzalishaji na uuzaji wa bidhaa zitokanazo na bioteknolojia mpya wasifikirie faida kwa upande wao tu, lakini pia wafikirie manufaa ya tafiti hizo kwa watu wote. Kanuni hii ambayo ina ukweli kwa kila aina ya shughuli za kiuchumi, zina ukweli wa aina yake kwa mambo ya upatikanaji wa chakula, madawa, hali ya afya na masuala ya mazingira. Kwa maamuzi yao, wajasiriamali na wakurugenzi wa sekta hii wanaweza kutoa miongozo ya maendeleo katika maeneo ya bioteknolojia yenye kutia moyo kama vile vita dhidi ya njaa hasa katika nchi maskini, vita dhidi ya magonjwa na vita ya kuusalimisha mfumo wa ikolojia ambao unachukuliwa kama baba mlezi wa sisi sote.

479. Wanasiasa, watungaji sheria na viongozi wengine wa umma wanawajibika katika kutathmini yale yanayoweza kuwa na manufaa na pia kuwa na faida na yale yenye kuelekea kuwa na hatari kutokana na matumizi ya hizo bioteknolojia. Maamuzi yao ya kitaifa au kimataifa yasiamrishwe na vikundi fulani vyenye nia ya kuyafaidi maamuzi hayo. Mamlaka za umma ziwahimize pia watu wenye ujuzi kutoa maoni yao yanayoweza kusaidia kufikia maamuzi ya kuwafaa wote.

480. Viongozi katika sekta ya mawasiliano na habari wanayo pia kazi muhimu ambayo lazima waifanye kibusara na bila kupendelea upande huu au ule. Jamii inatazamia kupata taarifa iliyokamilika na isiyo na upendeleo wowote. Taarifa kama hiyo, itawasaidia wananchi kuwa na maoni sahihi kuhusu bidhaa za kibioteknolojia zinazozalishwa kwa kuwa wao ndio watumiao bidhaa hizo. Kishawishi cha kuzipokea taarifa za kijuujuu zilizochochewa na shauku kubwa chumvi mno au taarifa zenye mshtuo na zisizo na sababu lazima ziepukwe.

c. Mazingira na Mgawanyo wa Kushirikishana Rasilimali

481. Kuhusu suala la ikolojia, Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanatukumbusha kuwa mali yote iliyo hapa duniani iliumbwa na Mungu ili kila mmoja aitumie kwa busara. Lazima kuwe na mgao ulio sawa wenye haki na upendo. Msisitizo huu wa kuwa na mgao ulio sawa na wa haki umetokana na ile hali inayojitokeza ya kuhodhi rasilimali hiyo. Uroho unaooneshwa na baadhi ya watu au na vikundi vya watu ni kinyume na utaratibu wa uumbaji.[1005] Matatizo ya ikolojia yanayojitokeza siku hizi, kwa kweli, yanauhusu ulimwengu mzima na hivyo yanaweza kupatiwa ufumbuzi tu kwa ushirikiano wa kimataifa. Ushirikiano huu ndio unaoweza kuwa na uhakika zaidi wa kuyatatua matatizo haya ya kiikolojia yanayohusu matumizi ya rasilimali za dunia hii.

482. Janga linalotokana na hali ya jinsi mazingira yalivyo na kuwepo kwa umaskini limesababishwa na vitu vingi tata ambavyo haviwezi kupatiwa maelezo rahisi na ya moja kwa moja. Ufumbuzi wake unaweza kupatikana kwa kutumia ile kanuni inayofuatilia na kuona ukomo na hatima ya mali hizo. Kanuni hii inatoa mwanya wa mwelekeo wenye misingi ya kimaadili na ya kiutamaduni. Janga hili la kimazingira linaloukumba ulimwengu hivi sasa, linawaathiri hasa wale ambao umaskini wao wa kupindukia umetokana na mambo kadhaa kama vile kuishi katika sehemu zenye mmomonyoko wa ardhi na zilizogeuka jangwa kwa sababu ya kufyeka misitu, kujihusisha katika mapambano ya kutumia silaha na kulazimika kuzihama nchi zao au kutokana na sababu za kukosa nyenzo za kiuchumi na za kiteknolojia za kujilinda na majanga hayo.

Idadi kubwa ya watu hawa maskini wanaishi katika sehemu zenye uchafuzi, pembezoni (viungani) mwa miji mikubwa au wanaishi katika sehemu za makazi ya muda au katika majengo yasiyo salama ambayo yako katika hatari ya kuporomoka muda wowote ule. Unapotokea uwezekano wa kuwatafutia mahali pengine pazuri zaidi pa kuishi, zitolewe taarifa mapema zinazochanganua makazi yanayotolewa ili kukwepa kuongeza matatizo juu ya mateso na kila inapowezekana wahusika wenyewe wahusishwe katika michakato hii yote.

Ni muhimu pia kukumbuka hali ya nchi zile zinazoonekana kama zinaadhibiwa kutokana na sheria za kimataifa zisizo na haki na pia nchi za nje. Katika hali kama hii, hakuna ujanja wa kuifanya njaa na umaskini visiyaharibu mazingira.

483. Ule uhusiano wa karibu uliopo kati ya maendeleo ya nchi maskini sana hapa ulimwenguni, mabadiliko ya idadi ya watu na matumizi endelevu ya mazingira visiwe visingizio vya chaguzi za kisiasa na za kiuchumi zinazopingana na hadhi ya utu wa binadamu. Katika nchi zilizoendelea kuna “kushuka kwa vima vya uzazi vyenye matokeo hasi kwa umri wa kuzeeka kwa watu ambako hakuwezi hata kujirekebisha kwenyewe kibiolojia.”[1006] Hali ni tofauti katika nchi zinazoendelea ambako kiwango cha ongezeko la idadi ya watu kinapanda. Ingawa ni kweli kwamba mgao usio na uwiano kati ya watu na upatikanaji wa rasilimali unazuia maendeleo na matumizi endelevu ya mazingira, hata hivyo, ifahamike kwamba ongezeko la idadi ya watu ni sehemu muhimu ya maendeleo.[1007] “Kuna makubaliano yaliyoenea na yanayoelekea kukubalika yasemayo kwamba sera ya idadi ya watu ni sehemu moja tu ya mkakati mzima wa maendeleo. Kwa sababu hiyo, ni muhimu kwamba mazungumzo yoyote ya sera za idadi ya watu yazingatie maendeleo halisi na yale yaliyosanifiwa kuhusu mataifa na kanda mbalimbali za hapa ulimwenguni. Hapohapo haiwezekani kutogusia maana halisi ya neno hili ‘maendeleo’. Maendeleo yote yanayostahili kuitwa maendeleo yawe yale yaliyokamilika, yaani yawe kwa manufaa halisi ya kila mtu na kwa chochote kinachomhusu mtu huyu.”[1008]

484. Ile kanuni ya jumla ya madhumuni ya matumizi ya bidhaa inayahusu pia maji ambayo yanazungumziwa vilevile katika Maandiko Matakatifu kuwa ni alama ya kutakasa (taz. Zab 51: 14; Yn.13.8) na ya uzima (taz. Yn. 3: 5; Gal 3: 27). “Kama zawadi iliyotolewa na Mungu, maji ni kitu cha muhimu kwa kutufanya tuishi. Kwa hiyo, kila mmoja ana haki ya kuyatumia.”[1009] Mwongozo wa matumizi ya maji hayo na wa kuhusu huduma zingine zitolewazo nayo hasa kwa wale wanaoishi katika hali ya umaskini, uwe ule wa kujali kuwa maji yanakidhi haja ya kila mtu. Kutopatikana kabisa au kupatikana kwa wasiwasi kwa maji salama ya kunywa kunaathiri afya ya idadi kubwa ya watu na mara nyingi huwa sababu ya milipuko ya magonjwa, mateso ya ainaaina, migogoro mingi inayoongeza umaskini na hata vifo. Ili kupata ufumbuzi unaofaa kwa tatizo hili, “lazima kuwe na mazingira yanayosaidia kuweka vigezo vyenye misingi ya kuheshimu na pia kujali haki na hadhi ya utu wa binadamu wote.”[1010]

485. Kwa jinsi hulka na umuhimu wa hulka hiyo ulivyo, maji hayawezi kuchukuliwa tu kama inavyochukuliwa bidhaa nyingine yoyote ile, bali ni lazima maji yatumiwe kwa busara na kwa ushirikiano. Kijadi, usambazaji wa maji ni kati ya majukumu yale yaliyokabidhiwa kwa wakala wa umma kwa sababu maji hutoa manufaa kwa watu wote. Hata kama usambazaji wake unakabidhiwa kwa sekta binafsi, maji bado yanabaki kuwa kitu kinacholeta manufaa makubwa. Haki ya kupata maji,[1011] kama ilivyo haki ya kupata vitu vingine, ina misingi yake katika hadhi ya utu na kamwe si katika aina yoyote tu ya ukadiriaji wa kiasi cha kitu chenye manufaa ya kiuchumi. Bila maji maisha huwa hatarini. Kwa hiyo, haki ya kupata maji safi na salama ya kunywa ni haki ya wote na haiwezi kutenganishwa na maisha yao.

d. Mitindo Mipya ya Namna ya Kuishi

486. Matatizo makubwa ya kiikolojia yanahitaji mabadiliko ya kifikra yenye kuleta matokeo ya kufaa kuhusu upokeaji na utumiaji wa mitindo hiyo mipya ya namna ya kuishi.[1012] Vigezo vinavyosaidia walaji kuichagua na wawekezaji kuwekeza katika mitindo hiyo mipya ni “utafutaji wa ukweli, uzuri, wema na ushirikiano wa pamoja kwa manufaa ya wote.”[1013] Mitindo hii mipya ya maisha, lazima iwe na kiasi na ukadiri na pia ijiwekee malengo ya kuwa na nidhamu ya viwango vya kuvifikia katika jamii husika. Kuna hoja ya kuiachilia mbali ile mantiki ya utumiaji tu na ukuzaji wa aina ya kilimo na ile ya uendelezaji wa viwanda inayokubaliana na utaratibu wa uumbaji na utoshelezaji wa mahitaji ya msingi ya binadamu wote. Mitazamo hii inayokubaliana na utambuzi mpya wa uhuru wa wakazi wote wa dunia itachangia katika kuviondosha vile vyanzo vya aina mbalimbali vya maafa ya kiikolojia na itakuwa na uwezo wa kuitika na kusaidia kwa haraka pale maafa ya aina hii yanapowakumba watu au nchi.[1014] Lile tatizo la kiikolojia lisifutwe kwa sababu tu ya yale matazamio ya kutisha yanayowakilishwa na uharibifu wa kimazingira; lakini yawe, zaidi ya yote, yenye kutoa hamasa ya mshikamano wa kweli ulioenea duniani pote.

487. Hali ambayo mtu anayefanya kitu kwa mujibu wa uumbaji lazima, kimsingi aioneshe, ni ile ya kutoa shukrani. Kwa kufanya hivyo, kwa kweli, analifunua lile fumbo lililoumbwa na Mungu ambalo bado anaendelea kulitunza. Pale anapouweka kando uhusiano wake na Mungu, hulka hupoteza ile maana yake halisi na hufukarishwa. Wakati hulka hii inapofichuliwa tena na kuwa katika hali yake ya ukiumbe, hapo njia za mawasiliano na hiyo hulka hupatikana tena, uwazi na wingi wa maana yake huonekana na hivyo hutuwezesha kuingia katika ufalme wa hilo fumbo. Ufalme huu unamfungulia mtu njia ielekeayo kwa Mungu Muumba wa mbingu na nchi. Ulimwengu unajiweka wenyewe mbele ya macho ya mtu kama shahidi wa Mungu pale ambapo uwezo wake wa kuokoa na wenye busara ya kuona mbali unapojifunua na kujiweka wazi.

 

SURA YA KUMI NA MOJA

UHAMASISHAJI WA AMANI

I. VIPENGELE VYA BIBLIA

 

488. Pamoja na ukweli kuwa amani ni zawadi aliyopewa binadamu na Mungu kwa mujibu wa utaratibu aliojiwekea mwenyewe, amani hiyo, kimsingi ni sifa inayomwelekea Mwenyezi Mungu; “Bwana ni amani.” (Amu 6: 24). Uumbaji ambao ndio unaufanya utukufu wa Mungu uonekane, unalenga kwenye amani. Mungu aliumba vitu vyote vilivyopo. Uumbaji wa aina yoyote huunda kitu kimoja ambacho ni kizuri na chenye maumbile ya kupendeza (taz. Mwa 1: 4, 10, 18, 21, 25, 31). Misingi ya amani iko katika uhusiano ambao uko kati ya Mungu mwenyewe na viumbe vyake. Uhusiano huu unajitokeza na kuonekana katika mambo yale ambayo ni maadilifu (taz. Mwa 17: 1). Kutokana na kitendo ambacho binadamu alikitenda kwa utashi wake huru kinyume na utaratibu alioupanga Mungu, ulimwengu umeshuhudia umwagikaji wa damu na utengano. Vurugu na vitendo vya kutumia nguvu vimejitokeza katika mahusiano ya watu kati yao wenyewe (taz. Mwa 4: 1 – 16) na mahusiano kati ya jamii (taz. Mwa 11: 1 – 9). Amani na vurugu, tujuavyo, haviwezi kukaa pamoja: na palipo na vurugu, Mungu hawezi kuwa mahali hapo (taz. 1 Nya 22: 8 – 9).

489. Kwa mujibu wa ufunuo wa kibiblia, neno amani lina maana pana zaidi kuliko ile ya kutokuwepo tu kwa vita. Neno hili amani linawakilisha ukamilifu wa maisha (taz. Mal. 2: 5). Pamoja na ukweli kuwa hii ni kazi ya mikono ya wanadamu, zawadi hii ni kati ya zile zawadi kubwa kabisa anazowapa Mungu watu wake wote, wanaume na wanawake, kwa mujibu wa utaratibu aliojiwekea: “Bwana akuinulie uso wake, na kukupa amani” (Hes. 6: 26). Amani hii inazaa matunda (Isa 48: 19), afya njema (taz. Isa 48: 18), ustawi (taz. Isa 54: 13,) hali ya kutokuwa na woga (taz. Law 26: 6) na furaha ya hali ya juu (taz. Mit 12: 20).

490. Amani ni lengo la maisha katika jamii kama ilivyofafanuliwa waziwazi kabisa na maono ya Kimasiha: Wakati ambapo watu wote watatembea kuelekea kwenye nyumba ya Bwana, yeye atawafundisha njia zake, nao watatembea wakifuata njia hizo za amani (taz. Isa 2: 2 – 5). Ahadi ya kipindi cha Kimasiha ni ile inayoizunguka hali yote ya asili ya kimaumbile (taz. Isa 11: 6 – 9) na Masiha mwenyewe kuitwa Mwana Mfalme wa amani” (Isa 9: 5). Popote pale ambapo amani yake inatawala na popote penye amani hii ingawa kwa kiasi kidogo tu hakuna atakayethubutu na kufanikiwa kuwafanya watu wa Mungu wawe na woga (taz. Sef 3: 13). Hapo ndipo amani itakuwa ya kudumu kwa sababu mfalme anapotawala kwa mujibu wa haki ya Mungu, uadilifu, unastawi na amani kujaa tele “hata mwezi utakapokoma.” (Zab 72: 7). Mungu anatamani kuwapa amani watu wake: “anaongelea kuhusu amani na watu wake, na watakatifu wake na pia na wale wanaoikimbilia katika mioyo yao” (Zab 85: 9). Katika kumsikiliza Mungu anachowaambia watu wake kuhusiana na amani, mtunga zaburi anayasikia maneno yafuatayo:” “Fadhili na kweli zimekutana, haki na amani zimebusiana” (zab 85: 11).

491. Mhusika wa utekelezaji wa ahadi ya amani ionekanayo katika Agano lote la kale ni Yesu. Amani, kwa kweli, ni ishara ya Kimasiha inayoshika vitu vingine vyote vyenye manufaa ya ukombozi. Lile neno la Kiyahudi “Shalom” linaonesha “ukamilifu” huu ikifuatiliwa na maana ya neno lenyewe kwa kuzingatia elimu ya asili na historia ya neno hili (taz. Isa 9: 5nk; Mik 5: 1 – 4). Ni dhahiri kabisa kwamba ufalme wa yule Masiha ni ufalme wa amani (taz. Ayu 25: 2; Zab 29: 11; 37: 11; 72: 3, 7; 85: 9; 11; 119: 165; 125: 5; 128: 6; 147: 14; Wim 8: 10; Isa 26: 3, 12; 32: 17f., 52: 7; 54:10; 57; 19; 60: 17; 66: 12; Hag 2: 9; Zek 9: 10 na wengine). Yesu “ni amani yetu” (Efe 2: 14). Amevunja ukuta wa uhasama kati ya watu akiwapatanisha na Mungu wao (taz. Efe 2: 14 – 16). Huu ni unyenyekevu wenye kuleta matokeo mazuri ambao Mtakatifu Paulo anautumia kuonesha jinsi ile hamasa kali inavyowachochea Wakristo kuwa na maisha ya kujitolea na kueneza amani.

Siku kabla ya kufa kwake, Yesu alizungumza juu ya uhusiano wake wa mapendo na Baba na nguvu yenye uwezo wa kuwaunganisha, ambao mapendo haya yanatoa kwa wafuasi wake. Haya ni mazungumzo ya kuaga yanayoonesha maana ya maisha yake kwa kina na yanaweza kuchukuliwa kama muhtasari wa mafundisho yake yote. Zawadi ya amani ni muhuri wa wosia wake wa kiroho. “Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapayo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo” (Yn 14: 27). Maneno ya Bwana Mfufuka hayawi tofauti. Kila wakati anapokutana na wafuasi wake wanapokea kutoka kwake salamu na zawadi ya amani. “Amani iwe nanyi” (Lk 24: 36; Yn. 20: 19, 21, 26).

492. Amani ya Kristo, kwanza kabisa ni upatanisho wa Baba ulioletwa na uchungaji wa Yesu ambao aliukabidhi kwa wafuasi wake. Uchungaji huu unaanza na utangazaji wa amani: “Na nyumba yoyote mtakayoingia, semeni kwanza, Amani iwemo nyumbani humu” (Lk 10: 5; taz. Rum 1: 7). Amani ni upatanisho wa mtu na kaka zake na pia na dada zake, kwa kuwa katika sala ile ambayo Yesu alitufundisha, sala ya “Baba yetu,” msamaha tunaomwomba Mungu atupe unahusishwa na msamaha ule tunaowapa kaka zetu na dada zetu: “utusamehe madeni yetu, kama sisi nasi tuwasameheavyo wadeni wetu” (Mt. 6: 12). Kwa aina hizi mbili za upatanisho, Wakristo wanaweza kuwa wapatanishi na kwa hivyo kushiriki katika Ufalme wa Mungu kufuatana na kile ambacho Yesu mwenyewe anatangaza katika Heri Mlimani: “Heri wapatanishi, maana hao wataitwa wana wa Mungu” (Mt 5: 9).

493. Kufanya kazi kwa ajili ya kukuza na kuendeleza amani hakuwezi kutenganishwa na kazi ya kutangaza Injili ambako, kwa kweli, ni kutangaza “habari njema ya amani” (Mdo 10: 36; taz. Efe 6: 15) kunakoelezwa kwa watu wote, wanaume na wanawake. Katikati ya hiyo “Injili ya amani” (Efe 6: 15) linabakia lile fumbo la msalaba, kwa sababu amani ni matunda ya sadaka ya Kristo (taz. Isa 53: 5) - “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, alichubuliwa kwa maovu yetu. Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.” Yesu msulubiwa ameshinda mgawanyiko, ameimarisha tena amani na upatanisho kwa njia dhahiri kabisa ya msalaba “na akiisha kuufisha ule uadui kwa huo msalaba” (Efe 2: 16) na kuleta wokovu wa ufufuko kwa binadamu.

 

II. AMANI: TUNDA LA HAKI NA MAPENDO

494. Amani ni kitu chenye thamani kubwa,[1015] na ni wajibu wa kila mtu kuwa nayo.[1016] Amani hii ipo kwa kuzingatia ule utaratibu wa kirazini na wa kimaadili wenye mizizi yake ndani ya Mungu mwenyewe ambaye ndiye asili ya vitu vyote na ni ukweli wenyewe na wema wa hali ya juu sana.[1017] Amani haina maana ya kutokuwepo tu kwa vita na wala haimaanishi kuwepo tu kwa uwiano muafaka wa nguvu kati ya maadui.[1018] Amani ina misingi yake katika uelewa sahihi wa binadamu [1019] wenye misingi muhimu iliyojikita katika haki na upendo. Ikieleweka katika maana yake pana kama kitu kile kinachoheshimu uwiano wa aina yoyote ile wa binadamu.

“Amani ni tunda la haki” [1020] (taz. Isa 32: 17), ikieleweka katika maana pana kuwa ni kuheshimu uwiano wa vipengele vyote vya mtu mwanadamu. Kunakuwa na tishio la amani pale mtu anapopewa baadhi tu ya yale anayopaswa kuyapata kama binadamu, pale hadhi yake isipoheshimiwa na pale maisha yake ya kiraia yasipoelekezwa kwenye manufaa kwa wote. Ulinzi wa ukuzaji wa haki za binadamu ni muhimu kwa ujenzi wa jamii yenye utulivu na amani na yenye maendeleo yaliyokamilika kwa kila mmoja na kwa watu wote kwa ujumla wao pamoja na mataifa.[1021]

Amani pia ni tunda la mapendo. “Amani ya kweli na ya kudumu huwa zaidi ni matokeo ya mapendo kuliko haki, kwa sababu kazi ya haki ni kuondoa tu vikwazo vya amani yaani madhara yaliyotendeka au uharibifu uliotokea. Amani kwa yenyewe ni tendo ambalo hutokana na mapendo tu.”[1022]

495. Amani hujengwa siku hadi siku katika utafutaji wa utaratibu muafaka uliopangwa na Mungu[1023] na huweza kustawi pale tu watu wote wanapotambua kuwa kila mmoja wao anawajibika katika kuiendeleza.[1024] Ili kuzuia migongano na vurugu ni lazima kabisa amani ianze kuota mizizi kama kitu cha thamani ndani ya moyo wa kila mtu. Kwa njia hii amani inaweza kuenea katika familia, katika mashirika mbalimbali yaliyo ndani ya jamii na hatimaye kuihusisha jumuiya yote ya kisiasa.[1025] Katika mazingira yaliyotulia yenye upatanifu na yanayoheshimu sheria, utamaduni wa kuwa na amani ya kweli unaweza kukua na kuenea katika jumuiya nzima ya kimataifa. Amani kwa hiyo, ni tunda la “upatanifu ulioundwa na Mungu mwenyewe katika jamii ya wanadamu. Amani ni lazima ichochewe na watu wakati wanapokuwa katika harakati za kujiendeleza ili wajipatie haki zaidi.”[1026] Hali kama hii ya ukamilifu wa amani[1027] “haiwezi kupatikana hapa duniani bila kuulinda ustawi wa jamii na watu kubadilishana mawazo na vipaji vyao.”[1028]

496. Vurugu kamwe si jibu. Kutokana na imani yake kwa Kristo na baada ya kuufahamu fika ujumbe wake, Kanisa linatangaza “kwamba vurugu ni kitendo kiovu na cha kihuni kisichomfaa mtu, na hivyo, hakikubaliki kwani hakiwezi kuleta ufumbuzi wa matatizo. Vurugu ni uongo mtupu kwa kuwa ni kitendo kinachokwenda kinyume na imani yetu na pia kinyume na ukweli wa ubinadamu wetu. Vurugu hukiharibu kile inachojidai kukitetea yaani hadhi ya utu, uhai na uhuru wa binadamu.”[1029]

Ulimwengu wa kisasa unahitaji pia manabii wasio na silaha za kivita ambao mara nyingi hudharauliwa.[1030] “Wale wasiopenda vurugu na umwagikaji damu. Kwa nia ya kulinda haki za binadamu, wanatumia njia zile ambazo wanyonge wanaweza kuzipata, na wanatoa ushahidi wa mapendo ya kiinjili alimradi wanafanya hivyo bila kuingilia haki na wajibu wa watu wengine na pia vyama vingine. Wanatoa ushahidi ulio halali kabisa kuhusu hali mbaya na ya hatari ya kimwili na kiroho inayosababishwa na utumiaji wa nguvu wenye kuleta uharibifu na hata vifo.”[1031]

 

III. KUSHINDWA KWA AMANI: VITA

497. Majisterio inalaani “unyama wa vita[1032] na inataka vita iangaliwe kwa mtazamo mpya.[1033] Kwa kweli, ni jambo lisiloweza kufikirika kwa urahisi kuwa katika enzi hii ya atomu, vita inaweza kutumika katika masuala ya kuleta haki.”[1034] Vita ni “balaa”[1035] na njia isiyofaa kwa kutatua na kumaliza matatizo yanayozuka kati ya mataifa. “Jambo hili halijatokea na halitatokea,[1036] kwa sababu vita inazua migogoro mingine mipya yenye utata zaidi.[1037] Inapozuka, vita huwa “mauaji ya kinyama yasiyo ya lazima”[1038] na “tukio lisiloweza kurudi nyuma tena”[1039] linalohatarisha hali ya sasa ya binadamu na kutishia hali yake ya baadaye. “Hakuna kinachopotea kwa kuwa na amani, lakini kinyume chake ni kwamba kila kitu kinaweza kupotea kwa vita.[1040] Madhara yanayosababishwa na mapambano ya kutumia silaha hayawi ya kimwili tu bali pia ya kiroho.[1041] Hatimaye, vita ni “kushindwa kwa utu wa kweli wa ubinadamu wote,”[1042] “vita daima ni kushindwa kwa ubinadamu:”[1043] “kamwe kusiwe tena na watu wanaopambana na wenzao, kamwe. kusiwe na vita tena, kusiwe na vita tena.”[1044]

498. Utafutaji wa ufumbuzi mbadala wa kutatua migogoro ya kimataifa inayohusu vita leo, limekuwa suala muhimu na linalohitaji kushughulikiwa kwa haraka sana. Umuhimu huu unatokana na ukweli kwamba ule uwezo mkubwa wa kufanya uharibifu ambao hata nchi ndogo zinaweza kuwa nao na pia yale mahusiano ya karibu sana ya watu wa ulimwengu mzima, yanafanya kuwe na ugumu au kusiwe na uwezekano kabisa wa kuzuia madhara ya hiyo migogoro.”[1045] Kwa hiyo, ni jambo la muhimu kutafuta sababu za migogoro hii ya kivita hasa ile inayohusiana na masuala ya haki, umaskini na unyonyaji ambazo zinahitaji uingiliaji kati ili kuziondoa.” Kwa hiyo, neno jingine linaloweza kutumika badala ya ‘amani’ ni maendeleo. Kama vile kulivyo na uwajibikaji wa pamoja wa kuzuia vita, kuwe pia na uwajibikaji wa pamoja wa kukuza maendeleo.”[1046]

499. Nchi haziwi na njia za kutosha kujilinda muda wote na kujihami zenyewe kikamilifu. Hali hii ndiyo inayofanya kuwe na umuhimu wa kuwa na vyama vya kimataifa na vya nchi mbalimbali au mabara ambavyo hufanya kazi kwa kushirikiana kumaliza migogoro na kukuza amani pamoja na kuanzisha mahusiano ya kuaminiana yanayowafanya watu wasifikirie matumizi ya vita.[1047] “Kuna kila sababu ya kuwa na matumaini. kwamba kwa kukutana pamoja na kuwa na majadiliano, watu wanaweza hatimaye kuyatambua vizuri zaidi yale yanayowaunganisha ambayo yanatokana na maumbile ya asili waliyo nayo wote. Moja ya mahitaji muhimu sana ya maumbile yao ya asili ni hili kwamba kinachotawala kati yao na wale wenye uhusiano nao si woga bali ni mapendo; na ni mapendo yale yanayoelekea kujitokeza katika ushirikiano wa aina mbalimbali wa kuaminiana na pia wenye kuleta faida nyingi.”[1048]

a. Kujitetea Kihalali

500. Vita ya uchokozi kwa asili ni mbaya, ni kinyume na maadili. Kunapozuka vita katika nchi fulani, viongozi wa nchi hiyo iliyoshambuliwa wana wajibu na haki ya kujihami hata kwa kutumia silaha.[1049] Kwa mujibu wa sheria inayokubalika kihalali, matumizi ya nguvu lazima yazingatie masharti fulani: “Madhara yaliyosababishwa na uchokozi huo kwa taifa au jumuiya ya kimataifa yawe ya kudumu, mazito na yaliyothibitika kuwa ni ya kweli. Njia zingine zote zilizojaribiwa kuuzima uchokozi huo ziwe zimeonekana kutofaa na kuwe na matumaini makubwa ya kufanikiwa. Matumizi ya silaha yasisababishe madhara na fujo kubwa zaidi kuliko madhara na fujo zile zinazokusudiwa kukomeshwa. Uwezo wa uharibifu wa vifaa hivi vya kisasa vinavyotumika unahusika sana na utoaji wa tathmini ya sharti hili. Hivi ni vigezo vya mapokeo vilivyoorodheshwa katika mafundisho yajulikanayo kama ‘vita halali na ya haki.’ Ili tathmini ya masharti haya ikubalike ni lazima iwapitie wale wenye busara na hekima katika masuala yenye manufaa kwa wote ili waidadisi na hatimaye watoe maoni yao.”[1050]

Kama uwajibikaji huu unahalalisha umilikaji wa njia za kutosha za kutumia haki hii ya kujilinda, madola bado yanawajibika kufanya chochote yawezayo “kuhakikisha kuwa yale masharti ya amani yanakuwepo si katika nchi zao tu bali ulimwenguni pote.”[1051] Ni muhimu kukumbuka kuwa, “ni kitu kimoja kupigana vita kwa madhumuni ya kujihami, lakini ni kitu tofauti kuitawala nchi nyingine kwa mabavu. Kuwa na uwezo wa kivita hakuhalalishi utumiaji wa nguvu kwa malengo ya kisiasa au ya kijeshi na wala haina maana kwamba baada ya kuzuka vita kwa wahasimu hao kuchukua silaha sawia.”[1052]

501. Hati ya Umoja wa Mataifa iliyotayarishwa na kuandikwa baada ya maafa ya Vita Vikuu vya Pili ilikuwa na madhumuni ya kuvikinga vizazi vijavyo kutokana na balaa la vita. Misingi ya hati hii ni ya kemeo na makatazo ya jumla ya kukimbilia kutumia nguvu kwa kumaliza migogoro kati ya Madola. Hata hivyo, kuna aina mbili za kesi ambazo hazihusiki. Kesi ya kwanza ni ile inayohusu ulinzi ambao ni halali na ya pili inahusu zile hatua zinazochukuliwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa katika eneo lake la uwajibikaji katika kudumisha amani. Katika kila moja ya hizi mtumiaji wa haki ya kujilinda lazima aheshimu “ile mipaka ya kimapokeo ya ulazima na uwiano.”[1053]

Kwa hiyo, kujiingiza katika vita yenye malengo ya kuzuia maafa bila kuwa na ushahidi wa kutosha wa ulazima wa kuwa na mashambulio ya haraka na ya kidharura hakuwezi kukwepa maswali ya kisheria na ya kimaadili. Uhalali wa kimataifa wa kutumia nguvu za majeshi ulio na malengo ya kimsingi na uliochunguzwa kwa makini unaweza kutolewa tu na chombo chenye uhalali wa kisheria kinachotambua zile hali maalumu za tishio la amani na hivyo kuidhinisha uingiliaji wa uhuru wa nchi ambao kwa kawaida huwa ni wa Dola.

b. Kulinda Amani

502. Masharti ya ulinzi unaokubalika kihalali kunafanya kuwepo kwa majeshi ya kivita yanayolinda amani katika nchi pia kuwe halali. Wale wanaotetea usalama na uhuru wa nchi wakiwa na msimamo huu wanatoa mchango halisi na wa kweli wa utunzaji wa amani.[1054] Yeyote anayetoa huduma katika majeshi ya nchi, anafanya hivyo kwa kutetea ukweli, haki na kile kilicho bora hapa ulimwenguni. Wengi wa watu wa aina hii ni wale waliojitoa mhanga kwa kuyalinda hayo manufaa na kuwalinda wale wasio na hatia. Kitu kinachojitokeza kwa wazi kabisa siku hizi ni lile ongezeko la wanajeshi wanaojiunga na vikosi vya kimataifa vilivyoanzishwa na Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kutoa huduma za kihisani au kwa kulinda amani.[1055]

503. Kila mwanajeshi anawajibika kimaadili kuzipinga na kuzikataa amri zinazodumisha na kuendeleza uhalifu dhidi ya sheria ya kimataifa na kanuni za sheria hiyo.[1056] Wanaolitumikia jeshi wanawajibika moja kwa moja kwa vitendo vyao wanavyovifanya vya ukiukaji wa haki za raia na watu kwa jumla au ukiukaji wa kanuni za sheria za kimataifa za uhisani. Vitendo kama hivi haviwezi kuhalalishwa kwa madai kuwa wanatii amri za wakubwa.

Wale wanaopinga kutoa huduma jeshini wanapolazimika kufanya hivyo kwa sababu haziendani na maadili yao kuhusu utumiaji wa nguvu au kwa sababu wanapinga kushiriki katika migogoro au mapigano fulani maalumu lazima wawe tayari kukubali kupokea aina mbadala ya utoaji wa huduma. “Ni jambo sahihi kabisa kuwa na namna fulani ya kiungwana ya kuwasaidia wale wanaopinga kutumia silaha kwa madai kwamba kufanya hivyo kunapingana na maadili yao. Wanajeshi kama hao wanaweza kutoa huduma zingine za kijamii mradi tu wanakubali kufanya hivyo.”[1057]

c. Wajibu wa Kuwalinda Wasio na Hatia

504. Haki ya utumiaji wa nguvu kwa nia ya kutoa ulinzi halali inahusiana na wajibu wa kuwalinda wahanga wasio na hatia ambao hawawezi kujilinda wenyewe na vitendo vya uchokozi. Katika migogoro inayojitokeza siku hizi ambayo mara nyingi hujitokeza katika nchi moja husika, miongozo ya sheria ya kimataifa lazima iheshimiwe kikamilifu. Mara nyingi sana inatokea kwamba raia wanashambuliwa na mara nyingine raia hao huwa ndio wanaoelekezewa mitutu ya bunduki. Wakati mwingine wanauawa kinyama au kuhamishwa kutoka nchi na makazi yao kwa visingizio vya “usafishaji wa kikabila”[1058] kitu ambacho kamwe hakikubaliki. Katika mazingira ya kuhuzunisha kama haya, msaada wa kimataifa utolewe na uwafikie wale walengwa, lakini msaada huu usitumike kwa kuwarubuni na kuwapa vishawishi. Wema, uhisani na huruma kwa binadamu vipewe kipaumbele na si matakwa ya wale wanaohusika na migogoro hiyo.

505. Ile kanuni ya ubinadamu iliyochorwa ndani ya dhamiri ya kila mmoja ni pamoja na wajibu wa kuwalinda raia kutokana na madhara ya vita. “Ulinzi wa kiwango cha chini kabisa cha hadhi kwa kila binadamu unaohakikishiwa kwa mujibu wa sheria ya kimataifa kuhusu misaada ya uhisani, mara nyingi, unakiukwa kwa visingizio vya matakwa ya kisiasa au ya kijeshi ambayo kamwe yasipewe umuhimu zaidi ya heshima ya binadamu. Leo tunatambua kuwa kuna haja ya kuwa na muafaka mpya kuhusu kanuni za ufadhili wa kimataifa na uimarishaji wa misingi yake ili kuzuia kujitokeza tena kwa ukatili na dhuluma.[1059]

Aina moja ya wahanga wa vita ambayo ni ya pekee ni ile ya wakimbizi waliolazimishwa na wapiganaji kuzikimbia sehemu zao za jadi walizozoea kuishi na kwenda nje ya nchi zao na kuishi huko kama wakimbizi. Kanisa linakuwa karibu nao si kwa uwepo wake wa kiuchungaji tu na utoaji wa misaada ya kimwili bali pia kwa ahadi zake za kutetea ubinadamu wao. “Kujihusisha kwetu na masuala ya wakimbizi lazima kutusukume kuzitambua kanuni zile zinazotambuliwa kimataifa kuhusu haki za binadamu na kuomba kwamba wakimbizi wenyewe nao wahakikishiwe utambuzi wa haki hizi zinazowahusu.[1060]

506. Jaribio la kuvifuta kabisa vikundi vya kitaifa, kikabila au vile vya lugha fulani ni uhalifu mbele ya Mungu na mbele ya ubinadamu wenyewe. Wale wanaohusika na uhalifu wa aina hii watajibu mbele ya haki.[1061]
Karne ya ishirini imeshuhudia uhalifu wa kutisha wa maangamizi ya vikundi vya watu: kutoka maangamizi ya Waarmenia hadi yale ya Waukraini, yale ya watu wa Kambojia na yale yaliyoshamiri katika Afrika na katika nchi za Balkani. Kati ya hayo yote yale maangamizi makuu ya Wayahudi ya Shoah yanaonekana kuwa ya kutisha mno. “Siku za Shoah ulikuwa usiku usiosahaulika katika historia na ulikuwa uhalifu usio na kifani dhidi ya Mungu na ubinadamu.”[1062]

Jumuiya ya Kimataifa kwa ujumla wake inawajibika kimaadili kuingilia kati, kwa niaba ya vikundi vile ambavyo uhai wao unatishiwa au haki zao za kimsingi za ubinadamu zinakiukwa kwa kiwango cha hali ya juu. Madola yakiwa wanachama wa jumuiya ya kimataifa hayawezi kunyamaza kimya na kujifanya kama hayahusiki; “ni halali kabisa na ni wajibu wao kuchukua hatua madhubuti za kumnyang’anya yule mchokozi silaha,”[1063] iwapo njia zingine zote hazifui dafu. Kanuni ya kutokuingilia mambo ya ndani ya nchi nyingine haiwezi kuchukuliwa kama sababu ya kuzuia uvamizi kwa nia ya kuwalinda wahanga wasio na hatia.[1064] Hata hivyo, hatua zinazochukuliwa kwa kufanya hivyo lazima ziheshimu sheria ya kimataifa na ile kanuni ya msingi ya usawa kati ya Madola.

Katika jumuiya ya kimataifa kuna pia Mahakama ya Jinai ya Kimataifa yenye jukumu la kutoa adhabu kwa wale wanaohusika na makosa mazito kama yale ya uangamizaji wa kabila au taifa, uhalifu dhidi ya ubinadamu, makosa ya vita, uchokozi wa kuvamia nchi na makosa mengine yanayohusiana na vita. Majisterio inahimiza wakati wote utumiaji wa chombo hiki.[1065]

d. Hatua Dhidi ya Wale Wanaotishia Amani

507. Vikwazo, kwa kufuata utaratibu uliofafanuliwa na chombo cha kimataifa kilichopo sasa, vina nia ya kurekebisha mwenendo wa serikali ya nchi inayokiuka kanuni za kuishi pamoja au inayofanya matendo ya ukandamizaji kwa watu wake. Madhumuni ya vikwazo hivi lazima yafafanuliwe kwa uwazi na hatua zinazochukuliwa lazima zifanyiwe tathmini za mara kwa mara bila upendeleo na vyombo halali vya jumuiya ya kimataifa ili kuhakikisha kama vinaleta matokeo yanayotarajiwa na jinsi matokeo hayo yanavyowagusa raia. Lengo hasa la hatua hizi ni kufungua milango ya mazungumzo na majadiliano. Vikwazo kamwe visitumike kama njia ya kutoa adhabu kwa idadi yote ya watu. Si sawa kama idadi yote ya watu na hasa wale ambao wanapaswa kulindwa kwa usalama wao wanateseka kutokana na vikwazo hivi. Vikwazo vya kiuchumi ndivyo hasa vinavyotakiwa kutumika na vitumike kwa uangalifu sana na viwe na vigezo madhubuti vya kisheria na kimaadili.[1066] Vikwazo vya kiuchumi viwe vya muda mfupi na vilete matokeo muafaka au la visitumike kabisa.

e. Upunguzaji wa Silaha za Vita

508. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanapendekeza kuwa upunguzaji wa silaha za vita uwe wa kijumla, uliodhibitiwa na wenye usawa unaolingana.[1067] Kasi ya uongezekaji wa silaha za vita inatishia amani. Kanuni ya kujitosheleza ambayo inasema kuwa ‘kila nchi inaweza kuwa na mbinu zile tu za lazima kwa kujihami kihalali’ izingatiwe na nchi inayonunua silaha pia na wale wanaozitengeneza na kuziuza.[1068] Kuhodhi silaha za vita kwa namna yoyote ile au kuziuza silaha hizi ovyo ovyo tu hakuwezi kutetewa kisheria. Matukio kama haya lazima pia yatathminiwe kwa kuangalia vigezo vya kimataifa kuhusu ule mkataba wa kuzuia uenezaji wa silaha za nyuklia, utengenezaji, biashara na matumizi ya aina mbalimbali ya silaha. Silaha za vita haziwezi kuchukuliwa kama bidhaa zingine zinazotumika katika ubadilishanaji kwenye masoko ya kimataifa na ya nyumbani.[1069]

Aidha, Majisterio imefanya tathmini ya kimaadili kuhusiana na mazingira yanayoweza kuzuia uenezaji wa silaha za vita. Ulimbikizaji wa silaha za vita ambao unaonekana kuwa njia isiyofaa kwa kuzuia uzukaji wa vita kwa kweli; unaweza kabisa kuwafanya maadui wa vita wasite kuanzisha mapigano. Watu wanaiona njia hii kuwa ni nzuri na inaweza kuleta matokeo yanayotegemewa katika kuhakikisha kuwa kuna amani kati ya mataifa. Hata hivyo, njia hii inawafanya baadhi ya watu wawe na wasiwasi hasa pale wanapoiunganisha na kuihusisha na masuala ya maadili. Mashindano ya silaha hayatoi uthibitisho wa kuwa na amani. Pamoja na kuwa na uwezo wa kuviondolea mbali vyanzo vya vita, njia hii inaweza pia kuvikuza.[1070] Sera za uzuiaji wa silaha za nyuklia, kama zile za kipindi cha vita baridi na propaganda lazima zibadilishwe na badala yake kuwe na hatua madhubuti za upunguzaji wa silaha za vita kwa njia ya mazungumzo na majadiliano.

509. Silaha za maangamizi ya idadi kubwa ya watu bila kujali kama maangamizi haya yanafanywa kwa njia za kibiolojia, kikemikali au za kinyuklia huwa ni tishio kubwa kwa ulimwengu. Wale wanaomiliki silaha za aina hii wanawajibika kwa namna kubwa sana mbele ya Mungu na mbele ya binadamu wote.[1071] Kuna malengo yenye uhusiano wa karibu sana kati ya ile kanuni ya mkataba wa kuzuia ueneaji wa silaha za nyuklia na zile hatua za upunguzaji wa silaha kama hizo na pia ule upigaji marufuku wa majaribio ya nyuklia. Malengo haya lazima yakabiliwe upesi inavyowezekana kwa kutumia hatua za ngazi ya kimataifa.[1072] Amri ya kupiga marufuku uendelezaji, utengenezaji, ulimbikizaji na utumiaji wa silaha za kibiolojia na kikemikali pamoja na masharti ya kuziharibu zinakamilisha zile kanuni zilizowekwa kimataifa za uzuiaji wa silaha za hatari kama hizo[1073] ambazo zinalaaniwa na Majisterio. Majisterio husema wazi kwamba “kitendo chochote cha vita chenye nia ya kuangamiza kabisa miji au maeneo makubwa ya ardhi pamoja na watu wake ni uhalifu mbele ya Mungu na binadamu. Kitendo kama hiki kinastahili kulaaniwa kwa kauli moja na bila kusita.”[1074]

510. Upunguzaji wa silaha za vita lazima uwe pamoja na upigaji marufuku wa silaha zenye kuleta madhara makubwa au zinazoshambulia kidharura bila utaratibu wa kueleweka. Silaha hizo ni kama zile za mabomu ya ardhini yanayoendelea kuleta madhara kwa kipindi kirefu hata baada ya kumalizika kwa uhasama. Nchi zile zinazotengeneza, kuuza na kuendelea kutumia silaha hizo zinahusika moja kwa moja na ucheleweshaji wa kuziondosha kabisa silaha hizo za mauaji.[1075] Jumuiya ya kimataifa lazima iendelee na juhudi yake ya uondoshaji wa mabomu haya ya ardhini na iendeleze pia ushirikiano katika elimu na mafunzo ya ufundi na nchi zile ambazo hazina uwezo wa kuyaondosha mabomu haya kwa haraka na zisizo na uwezo wa kutoa msaada kwa wahanga wa haya mabomu hayo.

511. Hatua zifaazo zahitajika kudhibiti utengenezaji, uuzaji, uingizaji na utoaji nje ya nchi silaha ndogondogo na zana za vita zinazosababisha mara nyingi kuzuka kwa vurugu. Uuzaji na usafirishaji wa zana za vita huwa tishio kubwa la amani. Silaha hizi huua na mara nyingi hutumika kwa migogoro ya ndani ya nchi na kati ya nchi moja na nyingine. Upatikanaji wa silaha hizi kirahisi hufanya migogoro mipya iongezeke na ile ya zamani ipambe moto zaidi. Nchi zinazoweka amri kali za kuzuia uhamishaji wa silaha nzito za vita na kamwe hazizuii uuzaji na usafirishaji wa silaha ndogondogo na zana nyepesi au nchi zinazofanya hivyo mara chache tu hufanya kuwe na kupingana kwa mambo kusikokubalika. Ni jambo la lazima na la haraka kwa serikali kuchukua hatua zinazofaa kudhibiti utengenezaji, ulimbikizaji, uuzaji na ufanyaji biashara ya silaha[1076] ili kuzuia ueneaji upesi wa hizo silaha hasa kati ya wapiganaji ambao si wa nchi husika.

512. Kuwatumia watoto na vijana kama askari katika mapambano ya kijeshi pamoja na ukweli kwamba umri wao mdogo ni kizuizi tosha cha kuwafanya wasiwe kuruta lazima kulaaniwe. Kwa kulazimishwa kwa nguvu kushiriki katika mapambano ya vita au kujiamulia wenyewe kufanya hivyo bila kujua matokeo ya uamuzi huo, watoto hawa hawanyimwi tu elimu na utoto wao wa kawaida, bali pia wanafundishwa kuua. Huu ni uhalifu katika mapambano ya silaha ya aina yoyote ile, lazima ukomeshwe na wakati huohuo watoto wale waliofanywa maaskari lazima wapewe kila aina ya msaada wa kuwatunza, kuwapa elimu na kuwawezesha kuishi maisha ya kawaida.[1077]

f. Kuushutumu Ugaidi

513. Ugaidi ni moja ya aina mbaya sana ya vurugu inayotishia jumuiya ya kimataifa leo; unajenga chuki, kifo na hamu ya kulipisa kisasi [1078] Ulipoanza kujitokeza, ugaidi ulikuwa wa kinyemela wenye vitendo vya hila na vya uchokozi vinavyofanana na vile vya mashirika yaliyo na siasa kali na yenye nia ya kufanya uharibifu na mauaji ya watu. Lakini sasa ugaidi unakuwa ni mfumo wenye ujanja wa kisiasa uliotanda na kuenea kisirisiri katika nchi nyingi. Mfumo huu wa ugaidi unaweza pia kutumia teknolojia ya kisasa. Mara nyingi una njia kemkem za kujipatia fedha zinazouwezesha kufanikisha mipango ya kuwashambulia watu wasio na hatia ambao huwa wahanga wa vitendo vya ugaidi.[1079] Vitendo vya ugaidi vinaelekeza mashambulizi yake ya ugaidi kwa makazi ya kawaida ya watu na vitendo hivi haviwi na malengo ya kijeshi kwa kuzingatia utaratibu wa vita uliotangazwa rasmi. Ugaidi hutokea na kutendeka usiku bila kujali zile sheria za kuzuia mapambano ambazo watu wameziweka kwa mujibu wa ile sheria ya kifadhila ya kimataifa. “Mara nyingi mbinu za kigaidi huchukuliwa au huonekana kama mikakati mipya ya vita.”[1080] Tusisahau pia kutilia maanani vyanzo vinavyoweza kusababisha mitindo ya aina hii ya kudai kile kinachofikiriwa ni haki ya mtu ambayo haikubaliki. Kuupiga vita ugaidi kuna maana ya kuwajibika kimaadili  kwa kuweka masharti yatakayozuia utokeaji na uendelezaji wake.

514. Ugaidi unastahili kulaaniwa kabisa kwa kuwa unayadhalilisha maisha ya binadamu. Ikumbukwe kuwa binadamu daima ni ukomo wa mambo na si njia ya kuufikia ukomo huo. Matendo ya ugaidi yanaondoa hadhi yote ya ubinadamu na ni uvunjaji wa sheria dhidi ya ubinadamu huo. ”Kwa hiyo, mtu anaweza kujihami mwenyewe na vitendo vya ugaidi kwa mujibu wa sheria.”[1081] Hata hivyo, haki hii ya kujihami haiwezi kutumiwa bila kufuata utaratibu wa kisheria na wa kimaadili kwa sababu jitihada ya kupambana na ugaidi lazima ifanyike kwa kuheshimu haki za binadamu na zile kanuni za nchi inayojitawala yenyewe kisheria.[1082] Utambulisho wa yule anayetuhumiwa kuwa na hatia lazima uthibitishwe kwa sababu uhalifu daima ni wa mhusika mwenyewe peke yake na hivyo kikundi cha dini yake, taifa au kabila lake hakiwezi kuhusishwa moja kwa moja na ugaidi wake. Ushirikiano wa kimataifa dhidi ya vitendo vya ugaidi “usiwe tu kwa kutumia nyenzo za vikosi vya jeshi. Ni muhimu kwamba matumizi ya nguvu hata pale inapokuwa lazima kufanya hivyo yawe pamoja na kufanya uchambuzi wa kina ili kubaini wazi sababu za vitendo hivi vya ugaidi.[1083] Kitu kingine kinachohitajika ni kwa wanasiasa na wasomi[1084] kujiona kuwa wanawajibika katika masuala ya ugaidi na hivyo wasaidie kutafuta na kupata ufumbuzi kwa nini, kwa mfano, mazingira ya aina hii yanaelekea kusababisha vitendo vya ugaidi kuliko ya aina ile: “uandikishaji wa magaidi huwa rahisi zaidi katika mazingira ambayo yanaruhusu haki za raia kukandamizwa na udhalimu kuvumiliwa kwa kipindi cha muda mrefu.”[1085]

515. Kitendo cha mtu kujitangaza wenyewe kuwa ni gaidi ni cha kumtukana na kumkashifu Mungu.[1086] Katika hali kama hii si mtu tu, bali hata Mungu anakashifiwa na mtu anayejidai kuwa ana ukweli wote wa Mungu. Afadhali mtu atafute ukweli kuliko kujidai kuwa anao na kumbe hana. Kuwaona wale wanaokufa wakati wa kufanya matendo ya kigaidi kama mashahidi kunaharibu maana ya “kifo cha kishahidi.” Kifo cha kishahidi ni kile kinachompata mtu anayekuwa radhi kufa badala ya kumkataa Mungu na kuukataa upendo wake. Kifo cha kishahidi hakiwezi kuwa cha mtu anayeamua kujiua mwenyewe eti kwa jina la Mungu.

Haipo dini inayovumilia matendo ya kigaidi wala inayoeneza imani ya kigaidi au inayounga mkono ugaidi.[1087] Lingekuwa jambo la manufaa kama dini zote zingeshirikiana kuviondosha vyanzo vya ugaidi na kukuza urafiki kati ya watu.[1088]

 

IV. MCHANGO WA KANISA KWA AJILI YA AMANI

516. Ukuzaji na uendelezaji wa amani ulimwenguni ni sehemu muhimu ya ujumbe wa Kanisa wa kuendeleza kazi ya ukombozi hapa duniani. Kwa kweli, Kanisa katika Kristo ni “sakramenti au alama na chombo cha amani ambacho kipo hapa ulimwenguni kwa ajili ya ulimwengu.”[1089] Ukuzaji wa amani ya kweli ni dalili ya imani ya Kikristo katika yale mapendo ambayo Mungu anayo kwa kila binadamu. Kutoka imani ya ukombozi katika mapendo ya Mungu, dunia inajitokeza kwa mwonekano mpya na inajitokeza pia njia mpya ya kuwasogelea wengine bila kujali iwapo hao wengine ni mtu mmoja mmoja au watu wengi kwa pamoja. Hii ni imani inayobadilisha na kuyafanya maisha yaonekane mapya baada ya kupata msukumo wa amani ambayo Kristo aliwaachia wafuasi wake (taz. Yn 14: 27). Baada ya kuguswa na imani hii, Kanisa linakusudia kukuza umoja wa Wakristo na ushirikiano mzuri kati ya waamini wa dini zingine. Tofauti ya dini kamwe isiwe sababu ya migogoro. Ule utafutaji wa amani kwa pamoja kwa upande wa waamini ni chanzo muhimu cha umoja wa watu.[1090] Kanisa linawasihi watu binafsi mmoja mmoja, watu wote kwa jumla, Madola na mataifa kuwa pamoja katika kuimarisha amani ikiweka msisitizo wa pekee wa nafasi muhimu ya sheria ya kimataifa.”[1091]

517. Kanisa hufundisha kwamba amani ya kweli hupatikana kwa njia ya kusamehe na kwa upatanisho.[1092] Si rahisi kwa mtu kusamehe, pale anapokabiliwa na matatizo makubwa yanayotokana na mapambano ya vita kwa kuwa vurugu kama hizo hasa “zinapokuwa zimekithiri na kuonesha ukali mkubwa wa mateso ya hali ya juu”[1093] zinamwachia mtu maumivu makali. Mateso haya yanaweza kupozwa tu kwa pande zote husika kufikiria kwa dhati na kwa kina njia zinazoweza kuyaondoa matatizo yaliyopo na kuwa na msimamo madhubuti na wa ujasiri wa kujutia yale yaliyopita. Uzito wa hayo yaliyopita ambayo hayawezi kusamehewa unaweza kupokelewa tu pale msamaha wa pande zote mbili unapotolewa na kupokelewa. Huu ni mchakato mrefu na mgumu, lakini hata hivyo si kitu ambacho hakiwezi kupatikana.[1094]

518. Tendo la pande mbili zisizoelewana kusameheana lisiondoe haja ya kutafuta haki na wala lisizibe njia inayoelekea kwenye ukweli. Kwa kweli, huu ni muda mzuri na unaofaa ambao unaweza kutumiwa na vyanzo, vyenye nia ya kuanzisha vyombo vya kimataifa vya kisheria. Kwa mujibu wa kanuni ya mamlaka ya kisheria ya kiulimwengu ikiongozwa na utaratibu wa kiutendaji ambao unaheshimu haki za mshtakiwa na za wahanga, vyombo hivyo vya sheria vinaweza kuuyakinisha na kuubainisha ukweli wa uhalifu uliotendeka wakati wa mapambano ya kivita.[1095] Hata hivyo, ili mahusiano yaweze kuimarika kiasi cha kuyafanya mawazo ya upande mmoja yakubaliwe na upande wa pili kwa nia ya kuwa na upatanisho, ni lazima kudadisi na kupata taarifa zaidi ya ile taarifa ya tabia tu ya kiuhalifu ya kutenda na kutotenda kosa na utaratibu wa ulipaji wa fidia.[1096] Ni lazima, hata hivyo, kukuza na kuendeleza heshima ya kuwa na haki kwa masuala ya amani. Haki hii inafanya kuwe na matumaini ya ujenzi wa jamii ambamo kuna miundo ya ushirikiano badala ya ile miundo ya matumizi ya mabavu kwa madhumuni ya kufikia yale ambayo ni ya manufaa kwa wote.[1097]

519. Kanisa hutumia sala katika harakati zake za kutafuta amani. Sala huufungua moyo na kuuweka wazi, si tu kwa uhusiano wake wa karibu na Mungu, bali pia kwa uhusiano na wengine wenye heshima, uelewa, taadhima na mapenzi mema.[1098] Sala inaongeza ujasiri na inatoa msaada kwa “wote ambao ni marafiki wa amani,” [1099] na pia wale wapendao amani na wanaojitahidi kuikuza amani hiyo katika mazingira yao wanamoishi. Sala ya Liturujia ni “kilele ambako tendo la Kanisa huelekea na hapohapo ni chanzo na asili ya nguvu zake.”[1100] Kwa namna ya pekee adhimisho la Ekaristi, “chanzo na kilele cha maisha ya Kikristo,” [1101] ni chemchemi ya uwajibikaji wa kweli wa Kikristo kwa ajili ya amani.[1102]

520. Siku za kuadhimisha Amani Ulimwenguni huwa wakati mzuri sana wa sala kwa ajili ya kuikuza na kuiendeleza amani na pia huwa muda muafaka wa kutoa ahadi ya kuujenga ulimwengu wa amani. Papa Paulo VI alianzisha siku hizi za amani kwa madhumuni ya kuwafanya watu angalau “kwa siku hizi maalumu mwaka unapoanza, kuyaelekeza mawazo yao kwenye masuala yanayohusu amani.”[1103] Ujumbe wa Papa kwa siku hizi maalumu za amani ulimwenguni huonesha chanzo na njia ya kuendeleza Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii na jinsi Kanisa linavyoendelea siku zote kuikuza amani na kazi yake ya kiuchungaji ya kukuza amani.” Amani hujieleza yenyewe kwa njia ya amani tu, na haiwezi kamwe kutenganishwa na madai ya haki. Amani hii inakuzwa na kuendelezwa kwa kujitoa sadaka, upole, huruma na mapendo ya kila mtu.[1104]

 

SEHEMU YA TATU

“Kulingana na Kanisa, ujumbe wa Kijamii wa Injili lazima usichukuliwe katika nadharia, lakini zaidi ya yote, uwe ndio msingi na mvuto kwa utendaji.”

(Centesimus Annus, 57)

 


SURA YA KUMI NA MBILI

MAFUNDISHO KUHUSU JAMII NA UTENDAJI
WA KANISA

I. KAZI YA KICHUNGAJI KATIKA NYANJA YA KIJAMII

 

a. Mafundisho kuhusu Jamii na Utamadunisho wa Imani

521. Kwa kutambua nguvu ya Ukristo ya kufanya upya hata mambo ya utamaduni na ya jamii,[1105] Kanisa linatoa mchango wa mafundisho yake katika kujenga jumuiya ya wanadamu kwa kueleza maana ya kijamii ya Injili.[1106] Mwishoni mwa karne ya kumi na tisa Majisterio ya Kanisa kwa mpangilio ilishughulikia masuala muhimu ya kijamii ya wakati huo, ikiunda “kielelezo cha daima cha Kanisa. Kwa maana Kanisa lina kitu cha kusema kuhusu hali ya pekee ya wanadamu kibinafsi na ya kijumuiya, na katika ngazi ya kitaifa na ya kimataifa. Kanisa hutengeneza mafundisho halisi kwa hali hizo, yaliyo katika mkusanyiko wa muundo unaoliwezesha kufanyia uchambuzi mambo ya jamii, kuyahukumu, na kuonesha njia ya kufuata ili kupata ufumbuzi sahihi wa matatizo husika.[1107] Kuingilia kati kwa Papa Leo XIII katika uhalisi wa mambo ya kijamii na kisiasa ya wakati wake kwa njia ya Rerum Novarum “imelipa Kanisa kuwa na kama ‘hadhi ya kiraia,’ katika mabadiliko ya mambo ya maisha ya jamii, na msimamo huo hadhi hiyo imethibitishwa baadaye.”[1108]

522. Katika mafundisho yake kuhusu jamii, Kanisa limetoa hasa mtazamo kamili wa binadamu na kufahamu kikamilifu hali yake binafsi ya kijamii. Anthropolojia ya Kikristo hufunua hali ya kutoweza kukiuka hadhi ya kila mtu, na kuweka mambo ya kazi, uchumi, siasa katika mtazamo halisi wa mwanzoni, unaotia mwanga katika tunu za binadamu, na pamoja kuhimiza na kutegemeza jitihada ya ushahidi wa Kikristo katika nyanja mbalimbali za maisha ya kibinafsi, kiutamaduni na kijamii. Kutokana na “malimbuko ya kwanza ya Roho” (Rum 8:23), Wakristo wana “uwezo wa kutekeleza sheria mpya ya upendo (taz. Rum 8:1-11). Kwa njia ya huyo Roho aliye ‘arbuni ya urithi wetu’ (Efe 1:14), mtu mzima anafanywa upya toka ndani, hata kwa kufikia ‘ukombozi wa mwili wetu’ (Rum 8:23).[1109] Ndiyo sababu mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii huonesha jinsi msingi wa kimaadili wa utendaji wa kiraia umekuwa maendeleo kamili ya binadamu, na inalingana na kanuni kwa utendaji wa kijamii unaoelekea katika manufaa ya kweli ya wanadamu, na juhudi imekusudiwa kuweka nafasi itakayowezesha kila mtu kuridhisha wito wake kamili.

523. Anthropolojia hii ya Kikristo inaleta uhai na kuitegemeza kazi ya kichungaji ya utamadunisho wa imani na kazi hiyo inayokusudia kufanya upya ndani, kwa njia ya nguvu ya Injili, vigezo vya hukumu vya mtu wa kisasa, tunu zinazotegemeza uamuzi wake, namna ya kufikiri na mifano ambayo maisha yake yanachukua sura yake. ”Kwa njia ya utamadunisho, Kanisa, kwa upande wake, linaeleweka zaidi kama ishara na ni chombo cha kufaa kweli kwa utume wake.”[1110] Ulimwengu wa leo una pengo kati ya Injili na utamaduni, kwa sababu ya mtazamo wa kiulimwengu wa wokovu, unaotaka kupunguza hata Ukristo kuwa “hekima ya kibinadamu tu, sayansi ya uongo ya ustawi.”[1111] Kanisa hutambua kuwa linapaswa kupiga “hatua kubwa mbele katika juhudi zake za uinjilishaji, na kuingia katika awamu mpya ya historia katika kazi ya kimisionari, kazi ambayo ina sifa ya kubadilikabadilika.”[1112] Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yanasimama katika mtazamo huo wa kichungaji: “Uinjilishaji mpya’ ambao dunia ya kisasa inahitaji sana na kwa haraka.. ambao lazima uhusishe pamoja na mambo mengine muhimu, utangazaji wa mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii.”[1113]

b. Mafundisho Kuhusu Jamii na Kazi ya Kichungaji ya Kijamii

524. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii ni lengo lisiloepukika linaloyakinisha tabia, mfano, uwezo wa kuelewa na kuendeleza kazi ya kichungaji katika uwanja wa jamii. Ni maelezo ya huduma ya uinjilishaji wa kijamii, inayolenga kuangaza, kuchochea, na kutegemeza ustawi kamili wa utu wa binadamu, kwa njia ya matendo ya kuleta ukombozi wa Kikristo katika hali yake ya kidunia na hali yake ya juu kupita dunia. Kanisa liko na linafanya kazi katika historia. Linafanya kazi kati ya jamii na tamaduni za nyakati zake, ili litekeleze utume wa kutangaza upya ujumbe wa Kikristo kwa mataifa yote, katika mazingira halisi yaliyo na magumu yake, pamoja na mapambano na changamoto. Linafanya hivyo kusudi imani iwaangaze, ili wapate kufahamu ukweli kwamba “ukombozi wa kweli ni kwa mtu mwenyewe kujikana binafsi kwa upendo wa Kristo.”[1114] Huduma ya Kanisa ya kichungaji ya kijamii ni maelezo hai na halisi ya utambuzi mkamilifu wa utume wa uinjilishaji wake katika mambo ya kijamii, kiuchumi, kiutamaduni na ya kisiasa ya hapa duniani.

525. Ujumbe wa kijamii wa Injili lazima uongoze Kanisa katika aina mbili za kazi yake ya kichungaji: kwanza kusaidia wanaume na wanawake kugundua ukweli na kuchagua njia wanayopaswa kufuata, na pili kuwatia moyo Wakristo kutoa ushuhuda kwa roho ya utumishi wa Injili katika uwanja wa utendaji wa kijamii. “Leo hasa, hata Neno la Mungu haliwezi kutangazwa na kusikilizwa, lisiposindikizwa na ushuhuda wa nguvu ya Roho Mtakatifu, anayefanya kazi katika amali ya Wakristo kwa kutoa huduma kwa kaka na dada zao, ikiwa uhai wao na maisha ya baadaye viko hatarini.”[1115] ‘Hitaji la uinjilishaji mpya husaidia Kanisa kufahamu kuwa “leo hasa, zaidi ya ilivyowahi kutokea. ujumbe wake kuhusu jamii utapata kuaminika mara kutokana na ushuhuda wa matendo kuliko matokeo yake ya mantiki ya ndani na matumizi endelevu ya maneno.”[1116]

526. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii hutoa vigezo vya kimsingi kwa ajili ya kazi ya kichungaji katika uwanja wa jamii: kutangazwa Injili; kuweka ujumbe wa Injili katika mazingira halisi ya jamii; kupanga amali zinazokusudiwa kwa kufanya upya mambo; na kuyalinganisha na madai ya maadili ya Kikristo. Uinjilishaji mpya wa jamii, awali ya yote, hudai utangazaji wa Injili: Mungu humwokoa kila mtu katika Yesu Kristo. Ni tangazo hili ndilo hufunua mtu kwa yeye mwenyewe na hiyo lazima iwe kanuni ya kutafsiri mambo ya jamii. Kwa kutangaza Injili, hali ya kijamii ni muhimu na isiyoepukika, lakini si peke yake tu. Ni hali inayofunulia nafasi nyingi mbalimbali za wokovu wa Kikristo, hata ikiwa haiwezekani kulinganisha kikamilifu na kiuhakika mambo ya jamii na Injili. Ijapo hufanikiwa hata kwa namna ya ajabu, haiwezi kuepuka mipaka ya uhuru wa kibinadamu na mashaka juu ya mambo ya mwisho kwa kila kilichoumbwa.[1117]

527. Juu ya yote, kazi ya kijamii ya Kanisa katika sekta ya jamii, inapaswa kutoa ushuhuda wa ukweli wa utu wa binadamu. Anthropolojia ya Kikristo huruhusu utambuzi wa masuala ya kijamii ambao hauwezi kupata ufumbuzi wa kufaa, ikiwa tabia ipitayo yote ya utu wa binadamu, inayofunuliwa kwa njia ya imani, hailindwi.[1118] Amali ya kijamii ya Wakristo lazima ichukue mvuto kutoka katika kanuni ya kimsingi ya umuhimu wa utu wa binadamu.[1119] Sharti la kukuza upekee kamili wa binadamu, hudai Wakristo kuazimu tunu zile za hali ya juu zinazoongoza kila jamii inayoratibiwa na inayozalisha. Tunu hizo ni ukweli, haki, upendo na uhuru.[1120] Kazi ya kichungaji katika mambo ya jamii lazima ijitahidi kuhakikisha kuwa kufanywa upya kwa maisha ya umma kunaendana na heshima ya kweli ya tunu hizo. Kwa njia hii, ushuhuda wenye mbinu mbalimbali wa Kanisa hujitahidi kustawisha utambuzi wa manufaa ya kila mtu na ya watu wote sawa kama chanzo cha maendeleo ya kila namna ya maisha katika jamii.

c. Mafundisho Kuhusu Jamii na Malezi

528. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii ni rejea ya lazima kwa ajili ya malezi ya Kikristo yaliyo kamilika kabisa. Mkazo wa Majisterio katika kupendekeza mafundisho hayo kama chemchemi ya uvuvio kwa kazi ya utume na kazi ya kijamii hutokana na kuwa na uhakika kwamba ni chemchemi ya ajabu ya malezi.“ Hii ni kweli hasahasa kwa waumini walei ambao wanahusika katika nyanja mbalimbali za maisha ya jamii na umma. Zaidi ya hayo, ni muhimu mno wawe na ujuzi sahihi na kamili. wa mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii.”[1121] Utajiri huu wa ujuzi wa Mafundisho hayo haufundishwi na kueleweka vya kutosha. Hii kwa upande mmoja ni sababu ya kushindwa kuonekana katika mwenendo wa watu.

529. Tunu ya malezi ya mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii inadai kuangaliwa zaidi katika katekesi.[1122] Katekesi ni mafundisho yaliyo katika utaratibu wa Mafundisho ya Kanisa katika ukamilifu, kwa nia ya kuwatayarisha waamini kwa maisha kamili ya kiinjili.[1123] Lengo la mwisho la katekesi “si kufanya watu wajue tu bali pia wawe katika umoja na udugu wa karibu kabisa, kwa undani, na Yesu Kristo.”[1124] Kwa njia hii, inawezekana kutambua kazi ya Roho Mtakatifu, ambaye kutoka kwake inakuja zawadi ya maisha mapya katika Kristo.[1125] Ikieleweka katika mwanga huu, kwa huduma yake ya kulea katika imani, kwa kujali katekesi lazima isishindwe “kuangaza inavyotakiwa mambo kama kazi ya mtu kwa ajili ya kupata uhuru wake kamili, kujenga jamii yenye mshikamano na udugu zaidi, na kupambana kwa ajili ya haki na kujenga amani.”[1126] Kwa kufanya hivyo, lazima Majisterio kuhusu jamii iwe imewasilishwa: historia yake, yaliyomo, na methodolojia yake. Kusoma hati au nyaraka za kijamii, katika mazingira ya Kikanisa, hutajirisha kujifunza na kuelekeza, kwa njia ya misaada ya nyanja mbalimbali ya utaalamu, na ufundi uliomo katika jumuiya.

530. Ndani ya katekesi hasa ni muhimu kwamba mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii yaelekee kwenye kazi inayomotisha utekelezaji wa uinjilishaji na kufanya mambo ya kiulimwengu kuwa ya kibinadamu. Kwa kweli, kwa njia ya mafundisho haya, Kanisa linadhihirisha kinadharia na kwa vitendo ujuzi unaowezesha kutegemeza jitihada ya kubadili maisha ya kijamii, kwa kusaidia kikamilifu zaidi kulingana na mpango wa Mungu. Katekesi ya kijamii inalenga kuwalea wanaume na wanawake, ambao kuhusu utaratibu wa maadili, wanapenda uhuru wa kweli, watu ambao “wanatengeneza uamuzi wao katika mwanga wa ukweli, wanaelekeza utendaji wao na nia ya kuwajibika, na kutaka yaliyo kweli na ya haki katika kusaidiana na wengine.”[1127] Ushuhuda wa maisha ya Kikristo una nguvu sana kama tunu ya malezi: “Kwa namna ya pekee maisha ya utakatifu unaong’aa katika watu wengi wa Taifa la Mungu, wanyenyekevu na wasioonekana, imekuwa njia rahisi na ya kuvutia sana kwa kutambua mara moja uzuri wa ukweli, na nguvu ya ukombozi ya upendo wa Mungu, na tunu ya uaminifu bila masharti kwa matakwa yote ya sheria ya Bwana, hata katika mazingira magumu sana.”[1128]

531. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii lazima yawe msingi wa kazi ya malezi ambayo ni nzito na ya kudumu, hasa kwa waamini walei. Malezi hayo sharti yazingatie wajibu wao katika jamii ya raia. “Malezi yanamhusu mlei, bila kusubiri tu kupokea amri na miongozo. Ni kuchukua hatua kwa hiari na kuwa na roho ya Kikristo katika mawazo, desturi, sheria na miundo ya jumuiya wanamoishi.”[1129] Hatua ya kwanza ya malezi ya Wakristo walei yanapaswa kuwa ni kuwasaidia waweze kufanya vizuri kazi ya kila siku katika nyanja za kiutamaduni, kijamii, kiuchumi na kisiasa, na kukuza hisia ya wajibu kwa ajili ya huduma kwa watu wote.[1130] Hatua ya pili inahusu malezi ya utambuzi wa kisiasa ili kutayarisha Wakristo walei kutekeleza uwezo wao wa kisiasa. “Walio na kipaji cha kufanya kazi ngumu ijapo ya heshima, yaani kazi ya kisiasa, au wale ambao vipaji vyao huweza kukuzwa katika suala hili, wanapaswa kuwa tayari kufanya hivyo, na kusahau yanayowafaa wao wenyewe na faida yao ya kidunia. Hawa wanapaswa kuingia katika siasa.”[1131]

532. Taasisi za elimu za Kikatoliki zinaweza, na tena zinapaswa kutekeleza huduma yenye thamani ya malezi, wakijitolea kwa namna ya pekee kwa kutamadunisha ujumbe wa Kikristo, yaani, kukutanisha, kwa faida, Injili na matawi mbalimbali ya ujuzi. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii ni njia ya lazima kwa malezi halisi ya Kikristo kwa upendo, haki na amani, na pia kwa ukomavu wazi wa wajibu wa maadili na kijamii, katika nyanja mbalimbali za kitamaduni na kitaaluma.

Majuma ya Kijamii” ya Wakatoliki ni wakati ambao Majisterio daima imekaziwa, ni mifano muhimu ya fursa ya malezi. Ni nyakati za kufundisha na kuleta ukomavu kiimani kwa waamini walei, wanaoweza kutoa mchango wao wa hali ya juu kwa utaratibu wa kidunia. Nchi kadhaa wanaona Majuma hayo kama kweli karakana za utamadunisho kwa kubadilishana mawazo na mang’amuzi, kujadili matatizo yaliyopo na kutambua njia mpya za kiutendaji.

533. Si jambo la kupuuza azma ya kutumia mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii kwa malezi ya mapadre na waseminari, ambao katika mazingira ya matayarisho yao kwa utume, lazima wastawishe ujuzi kamili wa mafundisho ya Kanisa na masuala ya kijamii ya wakati wao wa leo. Idara ya Elimu Katoliki imetoa waraka, Mwongozo wa Kufundisha mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii katika Malezi ya Mapadre,[1132] ambao unatoa maelekezo na mapendekezo kwa ajili ya mpango wa kufaa na sahihi wa masomo kwa ajili ya mafundisho hayo.

d. Kustawisha Dialogia

534. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii ni chombo cha kufanya dialogia kati ya jumuiya za Wakristo na jumuiya ya kiraia na kisiasa. Ni chombo kinachofaa cha kustawisha na kukuza mielekeo murua ya ushirikiano uwezao kuleta manufaa kulingana na mazingira. Uwajibikaji wa mamlaka za kiraia na kisiasa, huitwa kuhifadhi wito wa binafsi na wa wito wa kijamii wa wanadamu kadiri ya maeneo yao, na kwa njia ziwawezeshazo katika mafundisho kuhusu jamii, wanaweza kupata msaada muhimu na kuwa chemchemi tajiri ya uvuvio.

535. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii pia ni chombo kifaacho kweli kwa ajili ya dialogia na kusaidiana katika uwanja wa ekumeni. Hiyo imekwisha fanyika mahali pengi na kwa ngazi pana kuhusu kutunza hadhi ya utu wa binadamu, kustawisha amani, mapambano dhidi ya vitendo na balaa za dunia ya leo, kama njaa na umaskini, kutojua kusoma, mgawanyo usio sawa wa mali ya dunia na kukosa makazi. Ushirikiano huu katika mengi huongeza uwezo wa kutambua kuwa wote ni ndugu katika Kristo, na hurahisisha safari kuelekea uekumeni.

536. Katika mapokeo ya jumla ya Agano la Kale, Kanisa Katoliki linaweza kuingia katika dialogia na ndugu Wayahudi, ambayo linafanya pia kwa njia ya mafundisho yake kuhusu jamii, ili kujenga pamoja, nyakati za baadaye za haki na amani kwa watu wote, kama wana na mabinti wa Mungu yule mmoja. Urithi huu mmoja wa kiroho hulisha pande zote na kuwezesha kuheshimiana,”[1133] na juu ya msingi huo inawezekana kufikia mapatano mapana zaidi kuhusu kuondoa kila aina ya ubaguzi na kulinda heshima ya binadamu.

537. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii pia yana sifa za wito wa daima kwa dialogia kati ya wadau wa dini za dunia ambao kwa pamoja wataweza kutafuta namna za kufaa za kushirikiana. Dini inahusika kushughulikia kupata amani, inayotegemea wajibu wa wote kwa ustawi mkamilifu wa binadamu.[1134] Katika nia ya mikusanyiko ya sala iliyofanyika huko Assisi,[1135] Kanisa linaendelea kuwaalika waamini wa dini nyingine kuzungumza na kutia moyo kila mahali ushuhuda wa kweli wa tunu hizo ambazo familia nzima ya wanadamu inashirikishana.

e. Wenye Kuhusika na Uendeshaji wa Kazi ya Kichungaji ya Kijamii

538. Taifa zima la Mungu lina kazi ya kutenda pale Kanisa linapotekeleza utume wake. Kwa njia mbalimbali na kwa njia ya kila mshiriki kadiri ya vipaji na namna yake ya kutenda iliyo ya pekee kwa kila wito, taifa la Mungu lazima waitikie wajibu wa kutangaza na kutoa ushuhuda wa Injili (taz. 1 Kor 9:16), kwa kutambua kuwa “uendeshaji wa misioni ni kazi ya Wakristo wote.”[1136]

Kazi ya kichungaji katika sekta ya jamii imekusudiwa kwa Wakristo wote, wanaoitwa kuwa watendaji thabiti wa kutoa ushuhuda wa mafundisho kuhusu jamii na kuwa wahusika kikamilifu wa mapokeo thabiti ya “kazi yenye kuzaa matunda ya mamilioni ya watu, ambao, wakichochewa na Majisterio kuhusu jamii, wamejitahidi kufanya mafundisho hayo kuwa mwongozo katika kuhusika na ulimwengu.”[1137] Kutenda binafsi au pamoja na wengine katika vikundi mbalimbali, vyama, au taasisi, Wakristo wa leo wanadhihirisha “harakati kubwa katika kulinda utu wa binadamu na himaya ya hadhi ya binadamu.”[1138]

539. Katika Kanisa mahalia, wajibu wa kwanza kwa jitihada ya kichungaji ya kuinjilisha mambo ya kijamii, humwangukia Askofu, akisaidiwa na mapadre, watawa wanaume kwa wanawake, na walei. Kwa kuhusika kwa namna ya pekee na mambo ya mahali, Askofu ni mhusika wa kustawisha na kueneza mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii, kwa kupitia taasisi zinazostahili.

Kazi ya kichungaji ya Askofu huonekana katika huduma ya mapadre wanaoshiriki utume wa kufundisha wa Askofu, kutakatifuza na kuongoza jumuiya ya Wakristo. Kwa njia ya programu za malezi zinazofaa, mapadre lazima wapate kujua mafundisho kuhusu jamii na kusaidia wanajumuiya wao kutambua haki na wajibu zao za kuwa watendaji wa mafundisho hayo. Kwa njia ya maadhimisho ya sakramenti, hasa ya Ekaristi na upatanisho, padre anasaidia waamini kuishi kadiri ya wajibu wao kijamii, kama tunda la fumbo la wokovu. Angepaswa kuamsha na kuchochea kazi ya kichungaji katika uwanja wa jamii, akishughulikia zaidi kwa namna ya pekee malezi na kusindikiza kiroho Wakristo walei waliomo katika maisha ya kijamii na kisiasa. Padre anayeshughulikia huduma ya kichungaji katika vyama mbalimbali vya Kikanisa hasa vile vilivyojitolea kwa utume wa kijamii, ana wajibu wa kustawisha ukuzaji wa vikundi hivyo kwa njia ya mafundisho ya kufaa kuhusu jamii.

540. Kazi ya kichungaji katika sekta ya jamii ni pamoja na kazi ya wale waliowekwa wakfu kadiri ya karama zao za pekee. Ushuhuda wao unaong’aa, hasa katika mazingira ya umaskini mkubwa, ingekuwa ukumbusho kwa watu wote wa tunu za utakatifu na huduma ya ukarimu kwa jirani. Zawadi kamili ya binafsi ya watawa wanaume kwa wanawake imetolewa katika maisha ya sala ya kila mmoja kama ishara inayoelezeka na kueleweka na ya unabii ya mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii. Kwa kujitoa na nafsi zao kikamilifu kwa ajili ya huduma ya fumbo la upendo wa Kristo kwa wanadamu na kwa ulimwengu, watawa wanatanguliza na kuonesha katika maisha yao wenyewe kiasi cha sura ya hali mpya ya wanadamu ambayo mafundisho hayo ya jamii yanashauri: Katika usafi wa moyo, umaskini na utii, waliojiweka wakfu wanakuwa katika huduma ya upendo ya kichungaji, hasa kwa sala, ambayo kwayo wanatazama mpango wa Mungu kwa ajili ya ulimwengu na wanamwomba Bwana kufungulia mioyo ya watu wote, kukaribisha ndani yao zawadi ya upendo mpya wa binadamu, ndilo tunda la sadaka ya Kristo.

 

II. MAFUNDISHO KUHUSU JAMII NA UWAJIBIKAJI WA WALEI

 

a. Waamini Walei

541. Sifa muhimu kwa mwamini mlei anayefanya kazi katika shamba la Bwana (taz. Mt 20:1-16) ni tabia ya kidunia kama wanafunzi wa Kristo, inayotendeka kwa namna ya pekee katika dunia. “Ni kazi yake mlei kutafuta Ufalme wa Mungu akishughulikia mambo ya kiulimwengu, na kuyaelekeza kadiri ya mapenzi ya Mungu.”[1139] Kwa njia ya Ubatizo, mlei ameingia katika mwili wa Kristo na kuwa mshiriki wa maisha yake na utume wake kadiri ya utambulisho wao pekee. “Neno ‘mlei’ hapa hueleweka kama waamini wote. Wale walio katika Madaraja Matakatifu na wale walio watawa katika shirika lililokubaliwa na Kanisa, yaani, waamini ambao, kwa Ubatizo wamejiunga na Mwili wa Kristo, ni watu wa Taifa la Mungu na kwa namna yao wanashiriki kazi ya Kristo kuhani, nabii na mfalme, na kwa uwezo wao wanajitahidi kutekeleza utume wa Wakristo wote katika Kanisa na katika ulimwengu.”[1140]

542. Utambulisho wa mwamini mlei huanza na kulishwa na sakramenti za Ubatizo, Kipaimara na Ekaristi. Ubatizo unamfananisha mtu na Kristo, Mwana wa Baba, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote, aliyetumwa kama Mwalimu na Mkombozi. Kipaimara kinamfanya mtu binafsi kuwa na sura ya Kristo, aliyetumwa kuhuisha hulka na kila kiumbe kwa njia ya kumimina Roho Mtakatifu. Ekaristi inamfanya mwamini mshiriki katika sadaka moja na ya pekee ambayo Kristo alimtolea Baba, katika mwili wake, kwa wokovu wa ulimwengu.

Wakatoliki walei ni wanafunzi wa Kristo, wakianza na sakramenti, yaani, kwa nguvu ambayo Mungu alitenda ndani yao, akiwatilia chapa ya mfano wa kweli wa Mwanae Yesu Kristo. Ni kutoka katika kipaji cha kimungu cha neema, na sio kwa idhini ya mtu, kwamba mtu mlei amepewa vipaji au sifa zinazodhihirishwa kwa namna yake, vya unabii, ukuhani na ufalme.

543. Ni wajibu wake mwamini mlei kutangaza Injili kwa ushuhuda wa mfano wake wa maisha yaliyosimikwa katika Kristo na kwa kuishi katika mambo ya wakati huu duniani: familia, jitihada ya mwanataaluma katika ulimwengu wa kazi, utamaduni, sayansi, utafiti; utekelezaji wa wajibu wa kijamii, kiuchumi na kisiasa. Mambo yote ya kilimwengu ya wanadamu – yawe ya binafsi na pia ya kijamii, pamoja na mazingira mbalimbali na hali ya kihistoria, na vilevile miundombinu na taasisi – katika muktadha ambamo Wakristo walei wanaishi na kufanya kazi. Mambo hayo ni mahali ambamo upendo wa Mungu hupokelewa; jitihada ya mwamini mlei inaafikiana na mtazamo huo na inadhaniwa kama sura ya Upendo wa kiinjili; “kwa sababu mwamini mlei kuingia na kuwa mtendaji katika ulimwengu si kitu kinachohusika na anthropolojia na jamii tu, bali kwa namna ya pekee, ni ukweli halisi wa kitheolojia na Kikanisa pia.”[1141]

544. Ushuhuda wa mwamini mlei huzaliwa katika kipaji cha neema, iliyotambuliwa, kulishwa na kukomaa.[1142] Motisha hiyo inafanya jitihada katika ulimwengu wenye maana na ni kinyume na sifa za utendaji ulio wa pekee wa misingi ya binadamu ya wasiomtaka Mungu, ambayo yakosa msingi wa hatima na inabanwa katika mipaka ya nyakati za dunia. Mtazamo wa mambo ya mwisho, ni ufunguo unaoruhusu kuwa na ufahamu halisi wa mambo ya binadamu. Kutoka mtazamo wa mema ya milele, mwamini mlei anaweza kushughulikia katika utendaji wa duniani kadiri ya kanuni ya ukweli halisi. Hali bora ya maisha na uzalishaji mali kwa wingi zaidi, sio vipimo vya kutosha kupima utimilifu kamili wa utu wa binadamu katika maisha haya, na zina nafasi ndogo zaidi tunapotazama maisha ya baadaye, “kwa sababu upeo wa binadamu haubanwi na utaratibu wa ulimwengu; kuishi katika mstari wa historia ya wanadamu, anatunza ukamilifu wa lengo lake la milele.”[1143]

b. Maisha ya Kiroho ya Waamini Walei

545. Waamini walei wanaitwa kukuza maisha ya kiroho halisi ambamo wanazaliwa upya, kama wanaume na wanawake wapya, waliotakatifuzwa na wenye wajibu wa kutakatifuza, waliozama katika fumbo la Mungu na waliosimikwa katika jamii. Maisha hayo ya kiroho yatajenga ulimwengu kadiri ya Roho wa Yesu. Yatawezesha watu kuona kupita mipaka ya historia, bila kujitenga nayo, na kustawisha upendo wenye ari kwa Mungu bila kuacha kuwatazama ndugu zao, wanaoweza kuwaona kama Bwana awaonavyo na kuwapenda kama Baba anavyowapenda. Njia hii ya kiroho hufungulia dhana hizi mbili: maisha ya kiroho ya ndani na utendaji wa kijamii, ambayo inajidhihirisha kama maisha ya kujitolea yanayoleta umoja, maana, na tumaini katika maisha ambayo kwa sababu nyingi mbalimbali yana mgongano na yamesambaratika. Wakiongozwa na maisha hayo ya kiroho waamini walei wanaweza kutoa mchango wao “katika kutakatifuza ulimwengu, toka ndani kama chachu, kwa kutekeleza wajibu zao za pekee. Hivyo, hasa kwa ushuhuda wa maisha yao wenyewe. wanaweza kumdhihirisha Kristo kwa wengine.”[1144]

546. Waamini walei lazima waimarishe maisha yao ya kiroho na ya kimaadili, kwa kuongeza zaidi na zaidi uwezo wao wa kuendeleza wajibu zao za kijamii. Kukazia zaidi nia zao za ndani na kujipatia mtindo wa kufaa wa kazi yao katika sekta za jamii na siasa kumeleta matokeo ya malezi endelevu ya kuelekea hasa kupata ulingano kati ya maisha, katika sura zake zote, na imani. Katika mang’amuzi ya waamini, kwa kweli, “hayawezi kuwemo maisha mawili yanayoandamana sawia: kwa upande mmoja yale yanayoitwa maisha ya ‘kiroho’, na tunu zake na masharti yake; na kwa upande mwingine, yale yanayoitwa maisha ya ‘kiulimwengu’, yaani maisha katika familia, kazini, mahusiano ya kijamii, madaraka katika maisha ya umma na utamaduni.”[1145]

Kuweka imani na maisha pamoja hudai kufuata njia kwa utaratibu unaooneshwa na mambo ya kimsingi na ya pekee ya kuishi Kikristo: Neno la Mungu kama mwongozo; maadhimisho ya Liturujia ya Mafumbo ya Kikristo, sala binafsi, mang’amuzi halisi ya Kanisa yaliyohimizwa na malezi pekee ya kuchagua miongozo ya kiroho; mazoezi ya fadhila za kijamii na jitihada ya kudumu kwa ajili ya malezi ya kiutamaduni na kitaaluma.

c. Kutenda kwa Busara

547. Waamini walei wanapaswa kutenda kadiri ya amri za busara, fadhila inayowezesha kutambua wema halisi katika kila hali, na kuchagua njia sahihi ya kufikia. Kwa sababu ya fadhila hiyo, kanuni za maadili zinaambatana kwa kila nafasi inavyofaa. Tunaweza kutambua nafasi tatu tofauti za kutumia busara kwa kupambanua na kutathmini hali, kushauri maazimio na kuhimiza utekelezaji kwa wakati wake. Hatua ya kwanza ni kutafakari na kushauriana shauri ili suala lijadiliwe na kutafuta maoni ya lazima. Hatua ya pili ni kutathmini, na jambo linachambuliwa na kuamuliwa katika mwanga wa mpango wa Mungu. Hatua ya tatu, ile ya kukata shauri, inategemea hatua zilizotangulia na inawezesha kuchagua kati ya hatua mbalimbali zinazoweza kuchukuliwa.

548. Busara inawezesha kufanya maamuzi yaliyo ya maana, na jinsi yalivyo, na kutambua wajibu tunaopaswa kwa matokeo ya hatua iliyochukuliwa. Maoni yaliyoenea sana yanaweka busara na ujanja, na kujitafutia faida, na kutoamini, au na woga au kuyumba, haya si sawa na ufahamu sahihi wa fadhila hiyo. Busara ni sifa ya utendaji kwa kutumia akili na inasaidia katika kuamua kwa hekima na ujasiri namna ya kutenda inayopaswa kufuatwa, hivyo busara inakuwa ndio kipimo cha fadhila nyingine.[1146] Busara husisitiza wema wa wajibu na kuonesha jinsi gani mtu anaweza kuutekeleza. Kwa uchambuzi wa mwisho, ni fadhila ambayo inadai umakini mkomavu wa fikra na uwajibikaji kwa ufahamu halisi wa hali ya pekee na kuchukua uamuzi kadiri ya utashi ulio sahihi.[1147]

d. Mafundisho kuhusu Jamii na Vyama vya Walei

549. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii lazima yawe sehemu kamili ya malezi endelevu ya waamini walei. Mang’amuzi huonesha kuwa kazi hii ya malezi kwa kawaida inawezekana katika vyama vya kikanisa vya walei, ambavyo vinajibu “kigezo cha kikanisa” sahihi.[1148] Vikundi na vyama vina nafasi yao pia katika malezi ya waamini walei. Kwa kweli vina uwezo, kila kimoja katika mtindo wake, ya kudhibiti malezi kwa njia ya mang’amuzi yaliyoshirikishwa kwa undani katika maisha ya kitume, na tena kuwa na nafasi ya kujumuika, kufanya malezi kuwa kweli na ya namna yake pekee ambayo wanachama wao wanapokea kutoka kwa watu wengine na jumuiya.”[1149] Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii husisitiza na kuangaza kazi ya vyama, miamsho ya vikundi vya walei vilivyojikabidhi kufanya kuwa upya sekta mbalimbali za utaratibu wa ulimwengu.[1150] “Ushirikiano wa Kanisa, uliomo tayari na ukifanya kazi katika utendaji wa mtu binafsi, unapata hali ya pekee katika walei wanaofanya kazi kwa pamoja katika vikundi, yaani, katika utendaji unaofanyika pamoja na wengine wakiwa na ushirikiano wa kuwajibika katika maisha na utume wa Kanisa.”[1151]

550. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii ni muhimu hasa kwa vyama vya kikanisa vilivyo na kazi ya kichungaji katika jamii, kama lengo lao. Vyama hivyo hudhihirisha alama ya kutazamiwa kwa sababu mbele ya maisha ya jamii kuwemo kwao kunatazamiwa kuwa na tabia ya kuwa viungo vya Kanisa; hiyo inaonesha umuhimu na tunu ya sala, kutafakari na dialogia kwa kuelekea katika kustawisha mambo ya jamii. Ni lazima kukumbuka kuwa kuna tofauti, iliyomo, “kati ya utendaji wa Wakristo, kutenda binafsi au kwa pamoja kwa nia yao kama raia wanaoongozwa na mwongozo wa dhamira yakinifu ya Kikristo, na utendaji wao wanapotenda pamoja na wachungaji wao kwa niaba ya Kanisa.”[1152]

Vyama mbalimbali vilivyo na tabia yao pekee, vinavyokusanya watu pamoja kwa niaba ya wito wao wa Kikristo na utume katika taaluma fulani au uwanja wa utamaduni, wana kazi muhimu na ya thamani wakitayarisha Wakristo waliokomaa. Kwa mfano, Chama cha Madaktari Wakatoliki wanalea waliojiunga nacho kwa njia ya uchambuzi kuhusu masuala mengi ambayo sayansi ya utabibu, baiolojia na sayansi nyingine mbele ya uwezo wa ushindani wa madaktari vilevile kwa upande wa dhamiri yao binafsi na imani. Tunaweza kusema hivyohivyo kuhusu vyama vya walimu Wakatoliki, wanasheria, wafanyabiashara, wafanyakazi, na tena vyama vya wanamichezo Wakatoliki na vya ikolojia, n.k. Katika muktadha huu, mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii huonesha kwamba ni njia ya kufaa kwa ajili ya kulea dhamiri ya watu binafsi na utamaduni wa nchi.

e. Huduma Katika Sekta Mbalimbali za Maisha ya Kijamii

551. Kuwemo kwa walei katika maisha ya kijamii kunadhihirishwa na huduma, ishara na ashirio la upendo, mambo yanayoonekana katika familia, utamaduni, kazi, uchumi na siasa kadiri ya hali zake husika. Wakiitikia mahitaji mbalimbali katika maeneo yao ya kazi, walei wanaume kwa wanawake huonesha ukweli wa imani yao, na vilevile kuhusu ukweli wa mafundisho ya Kanisa mintarafu jamii, yanayoonekana ukweli jinsi wanavyoyaishi kimatendo ili kupata ufumbuzi wa matatizo katika jamii. Kwa kweli, mafundisho kuhusu jamii yanaaminika wazi zaidi kutokana na ushuhuda wa utendaji kuliko kwa uzito endelevu wa ndani au mantiki yake.[1153]

Kwa kuingia katika Milenia ya tatu ya kipindi cha Kikristo, waamini walei wanajidhihirisha kwa njia ya ushuhuda wao, kwa watu wote ambao wanawabeba kulingana na wito muhimu wa wakati huu wetu. “Kwa kuchota katika hazina ya mafundisho ya Kanisa, maazimio ya Mtaguso yanakusudiwa kwa watu wote, wawe wanamwamini Mungu ama wasiomwamini wazi; wanakusudiwa kuwasaidia kutambua kwa undani zaidi lengo la maisha yao, kufanya kazi kulingana zaidi na hadhi ya binadamu iliyo ya juu kabisa, kujitahidi kuweka msingi imara zaidi ya udugu wa wote na kuitika miito inayodai ya nyakati zetu kwa ukarimu na jitihada ya pamoja ya upendo.”[1154]

1. Huduma kwa Binadamu

552. Kati ya maeneo ya uwajibikaji wa walei, huduma kwa utu wa binadamu inakuwa ndio kipaumbele. Kustawisha hadhi ya kila mtu, iliyo hazina kuliko zote katika wanaume na wanawake, ni “kazi muhimu ya lazima, kwa namna fulani, kazi iliyo kiini na ya kuunganisha, ya huduma ambayo Kanisa, na Waamini walei ndani yake, wanaitwa kukabidhi familia ya watu.”[1155]

Aina ya kwanza ya jukumu hilo ni jitihada na bidii ya kujifanya upya moyoni, kwa sababu historia ya wanadamu huongozwa sio na shuruti isiyojulikana, bali kutokana na wingi wa wahusika, ambao matendo yao huru yanajenga sura ya utaratibu wa kijamii. Taasisi za kijamii haziwezi kujidhaminisha bila msukumo wa lazima, manufaa ya wote; “kujifanya upya kwa roho ya Kikristo”[1156] lazima kutanguliwe na jitihada ya kuboresha jamii “kadiri ya nia ya Kanisa, katika misingi imara ya haki za kijamii na hisani ya kijamii.”[1157]

Kutokana na wongofu wa mioyo ni kwamba linaibuka suala la kujali wengine, wanaopendwa kama ndugu. Kujali huku hutusaidia kufahamu masharti na jitihada ya kurekebisha taasisi, miundo na hali ya maisha yaliyo kinyume na hadhi ya binadamu. Basi, walei inawabidi kufanya kazi kwa pamoja, kwa wongofu wa mioyo yao na kuboresha miundo, wakitambua hali ya kihistoria na kutumia vifaa vinavyoruhusiwa ili hadhi ya kila mwanaume na mwanamke iheshimiwe kweli na kustawishwa katika taasisi.

553. Kustawisha hadhi ya binadamu hudai awali ya yote kukiri haki isiyoweza kukiukwa ya uhai, toka kutungwa mimba hadi kifo cha kawaida, ya kwanza kati ya haki zote na sharti kwa haki nyingine ya binadamu.[1158] Kujali hadhi ya binadamu hudai, hasa, kwamba hali ya kidini ya binadamu itambuliwe. “Hiyo si sharti ‘kuhusu mambo ya imani,’ bali ni sharti linayofungamana kabisa na ukweli halisi wa mtu binafsi.”[1159] Kutambua kweli haki ya uhuru wa dhamiri na uhuru wa dini ni moja ya mema ya hali ya juu sana na moja ya wajibu anaopaswa kila mtu anayetaka kweli kuthamini mema ya kila binadamu na ya jamii.[1160] Katika muktadha wa utamaduni wa leo, kuna hitaji la haraka sana la kulinda ndoa na familia, linalotekelezwa kikamilifu kwa kukubali kwa nia tunu muhimu na pekee ya mambo hayo mawili kwa ajili ya maendeleo halisi ya jamii ya wanadamu.[1161]

2. Huduma katika Utamaduni

554. Utamaduni ni eneo muhimu kwa uwepo wa Kanisa na Wakristo binafsi. Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatikano unaangalia mwelekeo wa kutenga imani ya Kikristo na maisha ya kila siku kama moja ya makosa makubwa zaidi ya siku hizi.[1162] Bila mtazamo wenye tabia ya kuchunguza asili ya mambo, kosa la kumtamani Mungu katika kujijali mwenyewe tu na kujithamini, na wingi wa njia katika mtindo wa maisha ya anasa; kukipa kipaumbele uchunguzi wa tafiti ya teknolojia na sayansi kama ndio lengo katika vyenyewe; kutia mkazo katika kinachoonekana, na shauku ya sura ya kuonekana, ufundi na ujuzi katika mawasiliano: yote haya lazima yaeleweke katika mtazamo wa kiutamaduni na kuzihusianisha na suala muhimu la utu wa binadamu, ambao ni ukuzaji wake mkamilifu, wa uwezo wa binadamu wa kuwasiliana na kujihusisha na watu wengine, na uchunguzi wa daima wa binadamu wa kutaka kujibu maswali makuu yanayojitokeza katika maisha yote. Lazima kukumbuka kuwa “Utamaduni ni kitu ambacho kwa njia yake binadamu, kama binadamu, anakuwa binadamu zaidi, na ana nafasi zaidi ya kukua ‘kuwa binadamu.’[1163]

555. Kuustawisha utamaduni wa kijamii na kisiasa ukiongozwa na Injili lazima uwe uwanja wenye umuhimu wa pekee kwa waamini walei. Historia ya hivi karibuni imeonesha udhaifu na kushindwa kwa mitazamo ya utamaduni wa pamoja iliyotawala muda mrefu, hasa katika ngazi ya jamii na siasa. Katika uwanja huo, hasa, katika miaka baada ya Vita Vikuu vya Pili, Wakatoliki katika nchi mbalimbali waliohusika katika ngazi za juu, inaoonesha kwa wazi sana leo, kudumu kwa mvuto wao na katika urithi wao wa tunu. Kujihusisha katika mambo ya jamii na siasa kwa Wakatoliki, kwa kweli kamwe hakukubanwa katika kubadili miundo tu, kwa sababu kujihusisha kwao kumechukua nafasi kwenye misingi ya utamaduni unaopokea na kusikiliza hoja kutoka katika imani na maadili, na kuyachukua kama msingi na lengo la kupanga mipango. Utambuzi huo unapokosekana, Wakatoliki wenyewe wanasambaratika kiutamaduni na makusudi yao yanakuwa hayatoshelezi na hivyo yamebanwa. Kipaumbele cha haraka leo kipo katika kudhihirisha urithi wa mapokeo ya Kikatoliki, tunu zake, na yaliyomo, na urithi wote wa kiroho, kiakili na kimaadili. Ni kufanya utamaduni uwe wa kisasa Imani katika Yesu Kristo, aliyejidhihirisha kama “njia na ukweli na uzima” (Yn 14:6), huhimiza Wakristo kujitolea kwa nia thabiti na ya daima, iliyo katika mtazamo mpya wa kujenga utamaduni wa kijamii na kisiasa unaoongozwa na Injili.[1164]

556. Ukamilifu mtimilifu wa utu wa binadamu na manufaa ya jamii nzima ni malengo muhimu ya utamaduni;[1165] basi, hali ya kimaadili ya utamaduni ni kipaumbele katika utendaji wa kijamii ya walei. Kushindwa kuangalia hali hiyo kwa urahisi, hugeuza utamaduni kuwa chombo kinachofanya ubinadamu kuwa duni. Utamaduni unaweza kugeuka kuwa tasa na kuelekea uharibifu “unapogeuka na kuwa na mtazamo finyu na kutaka kudumisha njia mbaya za kuishi kwa kukataa mabadiliko yoyote kuhusu ukweli wa mtu.”[1166] Kuunda utamaduni wa kuwatajirisha wanaume na wanawake hudai, kinyume chake, kuwajibika kwa mtu kamili, ambaye, katika eneo la utamaduni, hujidhihirisha kwa ubunifu, akili, ufahamu wake wa ulimwengu na utu wa binadamu; zaidi pia, ni yule ambaye anatumia vizuri uwezo wake wa kujidhibiti, kujitoa sadaka, ushirikiano na kuwa tayari kustawisha manufaa kwa wote.[1167]

557. Kujihusisha kijamii na kisiasa kwa mwamini mlei katika uwanja wa utamaduni, leo huenda kwenye mielekeo ya pekee. Wa kwanza ni kutaka kuhakikisha haki ya kila mmoja ya utamaduni wa kibinadamu na kiraia “kulingana na hadhi ya binadamu, bila ubaguzi wa kitaifa, kijinsia, nchi, dini, au mazingira ya kijamii.”[1168] Haki hii inamaanisha haki ya familia na watu kuwa huru na kufungua shule; uhuru wa kushiriki njia za mawasiliano ya kijamii pamoja na kuepuka kila aina ya ukiritimba na udhibiti wa kiitikadi wa uwanja huo; uhuru wa kutafiti, kushirikishana maoni, hoja na majadiliano. Kwenye kiini cha umaskini wa watu wengi sana ziko pia njia mbalimbali za kukosesha watu utamaduni na kushindwa kutambua haki za utamaduni. Kuwajibika katika elimu na malezi ya binadamu daima ndio shughuli ya kwanza ya utendaji kijamii wa Wakristo.

558. Changamoto ya pili ya wajibu wa Mkristo ni kuhusu yaliyomo katika utamaduni, yaani ukweli. Suala la ukweli ni muhimu kwa utamaduni kwa sababu “umekuwa wajibu wa kila mtu, ambamo tunu za akili, utashi, dhamiri na udugu ni za kwanza.”[1169] Anthropolojia sahihi ni vigezo vya kuangazia na kuhakikisha kila aina ya kihistoria ya kiutamaduni. Kuwajibika kwa Wakristo katika uwanja wa utamaduni ni kinyume na mitazamo iliyo na upungufu na yenye itikadi potofu kuhusu mtu na uhai. Nguvu ya kuwa wazi katika ukweli inahakikishwa hasa na ukweli kwamba ”tamaduni mbalimbali kimsingi ni njia mbalimbali za kukabiliana na suala la maana ya kuishi binadamu.[1170]

559. Wakristo lazima wafanye kazi ili tunu kamili ya hali ya kidini ya utamaduni ionekane. Hii ni muhimu na ya haraka kwa ajili ya ubora wa maisha ya watu, ya mtu binafsi na ya jamii. Suala litokalo katika fumbo la maisha na kuhusu fumbo lililo kubwa zaidi la Mungu kwa kweli ni kiini cha kila utamaduni, hilo linapofutwa, utamaduni na maisha ya maadili ya mataifa yanaharibika.[1171] Hali ya kidini ya kweli na halisi ni sehemu muhimu ya binadamu na inamruhusu kufungulia utendaji wake mbalimbali kwenye upeo ambamo zinapata lengo na mwelekeo. Tabia ya kidini au kiroho ya binadamu inaoneshwa katika aina inayochukuliwa na utamaduni, ambao inaupa uhai na mvuto. Kazi zisizohesabika sana za kila wakati hutoa ushahidi huu. Hali ya kidini ya mtu au taifa inapokanushwa na kukataliwa, utamaduni wenyewe unaanza kufifia, mara nyingine hutoweka kabisa.

560. Katika ustawi wa utamaduni halisi, walei watatilia maanani vyombo vya habari, wakichunguza hasa yote yaliyomo kuhusu chaguzi au maamuzi yasiyohesabika ambayo watu wanafanya. Maamuzi hayo, japo yanabadilika kati ya kundi na kundi na toka mtu hadi mtu, yote yana uzito wa maadili na yanapaswa kupimwa katika mwanga huo. Kusudi kuweza kuchagua inavyofaa, lazima kufahamu kanuni ya utaratibu wa maadili na kutekeleza kiaminifu.[1172] Kanisa linashirikisha mapokeo marefu ya hekima, inayotoka na Ufunuo wa Mungu na tafakari ya wanadamu,[1173] ambayo kitheolojia inarekebisha “maoni ya ‘wasioamini Mungu,’ maoni ambayo humnyima mtu kuwa na utambuzi wa kiroho na kumjengea mitizamo ya kupenda anasa ambayo humshawishi mwanadamu kujisikia huru katika kila sheria na Mungu mwenyewe”[1174] Badala ya kuhukumu njia za mawasiliano ya kijamii, mapokeo hayo yanawekwa kwa ajili ya kuzihudumia: “Utamaduni wa hekima ya Kanisa unaweza kuokoa utamaduni wa upashanaji habari usiwe ni mkusanyiko wa habari zisizo na maana.”[1175]

561. Mwamini mlei anaangalia upashanaji habari kama nafasi na chombo chenye nguvu ya mshikamano:” Mshikamano ni matokeo ya upashanaji habari ulio sahihi na safi na usambazaji huru wa mawazo kunakohifadhi ujuzi na heshima ya wengine.”[1176] Si hivyo kwa upashanaji habari unaotumika katika kujenga na kutegemeza mtindo wa uchumi unaohifadhi choyo na tamaa ya mali. Kusahau hali ya ukosefu mkubwa wa haki kwa makusudi, pamoja na mateso ya watu, inaonyesha kuchagua kwa namna isiyoweza kukubalika kabisa.[1177] Miundo ya upashanaji habari na siasa na usambazaji wa teknolojia ni vipengele vinavyosaidia kuwafanya watu fulani kuwa “matajiri wa habari” na vilevile kuwafanya watu wengine “maskini wa habari” wakati ambapo kufanikiwa na hata kunusurika hutegemea upashanaji. Kwa njia hii, upashanaji habari mara nyingi husaidia katika kukosa haki na kukosa usawa ambayo husababisha mateso. Mawasiliano na teknolojia ya upashanaji habari, pamoja na mafunzo katika matumizi yake, lazima zilenge kuondoa hali ya kukosa haki na usawa.

562. Wanataaluma katika uwanja wa upashanaji habari si peke yao walio na wajibu wa maadili. Wanaotumia vyombo vya habari nao pia wana wajibu. Wafanyakazi wa upashanaji habari wanaojitahidi kutimiza wajibu wao unaostahili na kuwa na wapokeaji/wasikilizaji wanaotambua wajibu wao. Wajibu ya kwanza ya watumiaji ni kuchunguza na kupekua ili kuchagua. Wazazi, familia, na Kanisa wana masharti dhahiri wasiyoweza kuepuka. Kwa wale wanaofanya kazi, kwa uwezo mbalimbali katika uwanja wa upashanaji wa kijamii, onyo la Mt. Paulo linasikika kwa sauti na uwazi: “Basi, uvueni uongo, mkaseme ukweli kila mtu na jirani yake; kwa maana tu viungo, kila mmoja kiungo cha wenzake. Neno lolote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia” (Efe 4:25. 29). Kwa kumtumikia binadamu kwa kujenga jumuiya ya watu yenye misingi kwenye mshikamano, haki na upendo, na kueneza ukweli kuhusu uzima wa binadamu na kutekeleza hatima yake katika Mungu, imekuwa kiini kuhusu maadili katika upashanaji.[1178] Katika mwanga wa imani, mawasiliano ya wanadamu yanaweza kuonekana kama safari toka Babeli hadi Pentekoste, au zaidi, kama jitihada binafsi ama za kijamii ya kushinda hali ya kuanguka kwa mawasiliano (taz. Mwa 11:4-8), kuwafungulia watu kipaji cha lugha (taz. Mdo 2:5-11), kwa mawasiliano kama ilivyorekebishwa na nguvu ya Roho Mtakatifu aliyetumwa na Mwana.

3. Huduma katika Uchumi

563. Wakikabiliwa na muktadha wa uchumi wa leo ulio katika hali ngumu kueleweka, walei wanaongozwa katika matendo yao na kanuni za Majisterio kuhusu jamii. Ni lazima kanuni hizo zijulikane na kupokelewa katika uwanja wa utendaji wa kiuchumi, zinapodharauliwa, hasa kanuni za umuhimu wa binadamu, ubora wa utendaji wake unalegalega.[1179]

Uwajibikaji wa Wakristo utatafsiriwa katika jitihada ya tafakari ya utamaduni inayoelekea kwenye upambanuzi wa mifano ya siku hizi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Kwa kubana suala la maendeleo kuwa kama suala la tekniki tu kutanyima maudhui yake ya kweli, ambayo kumbe yanahusu “hadhi ya mtu binafsi na ya watu.”[1180]

564. Wataalamu wa uchumi, wale wanaofanya kazi katika uwanja huu na viongozi wa siasa lazima waone umuhimu wa haraka wa kufikiri upya uchumi, wakiangalia, kwa upande mmoja, umaskini mbaya sana wa mali wa mabilioni ya watu na, kwa upande mwingine, ukweli kwamba “miundo ya kiuchumi, kijamii na kiutamaduni haujawezesha kutosheleza mahitaji ya maendeleo ya kweli.”[1181] Mahitaji wanayodaiwa kuwa nayo kwa ufanisi wa kiuchumi lazima yalingane na yale ya ushirikiano katika siasa, na haki ya kijamii. Kwa kweli, inamaanisha kuwa mshikamano lazima uwe sehemu kamili ya mtandao wa kuunganisha uchumi, siasa na jamii, ambao leo ustawi wa utandawazi unaimarisha.[1182] Katika jitihada hiyo ya kufikiri upya, kwa nia ya kupata matokeo mazuri katika mazingira ya kiuchumi, vikundi vyenye mvuto wa Kikristo vinavyofanya kazi katika uwanja wa uchumi: wafanyakazi, wafanyabiashara na wachumi wana kazi muhimu ya kufanya.

4. Huduma katika Siasa

565. Kwa mwamini mlei kujihusisha na siasa kunastahili na inadai jitihada ya Mkristo kuwatumikia wengine.[1183] Kushughulikia manufaa kwa wote kwa roho ya utumishi, ukuzaji wa haki kwa kuangalia hasa mazingira ya umaskini na mateso, kujali kujitegemea binafsi katika mambo ya dunia, kanuni ya kusaidiana, ustawi wa dialogia na amani katika hali ya mashirikiano: hivyo ni vigezo vinavyopaswa kusukuma waamini walei katika utendaji wao wa kisiasa. Waamini wote, ikiwa wana haki na wajibu kama raia, wanapaswa kuheshimu mwongozo wa kanuni hizo. Uangalifu wa pekee unatakiwa kwa wale wanaoshika nafasi katika taasisi wakihusika na masuala yenye matatizo ambayo wote wanahusika nayo, ikiwa ni katika serikali ya mahali au ya nchi na ya kimataifa.

566. Kazi inayokwenda pamoja na uwajibikaji katika taasisi ya kijamii na kisiasa inadai wajibu mkubwa na dhahiri wa kuweza kuonesha wazi hitaji la pekee la hali ya kimaadili katika maisha ya kijamii na kisiasa kwa njia ya kushiriki katika midahalo ya kisiasa, na katika maamuzi ya utendaji. Uangalifu usiotosheleza katika mambo ya maadili husababisha kupunguza hadhi ya binadamu ya maisha katika jamii na taasisi za kijamii na kisiasa, na kwa hiyo kuimarisha, “miundo ya dhambi”[1184] “Kuishi na kutenda kadiri ya dhamiri kuhusu masuala ya siasa haimaanishi kukubali misimamo ya kisiasa inayoingizwa kutoka nje ya wigo wa siasa, bali hasa njia ambamo Wakristo hutoa mchango wao kimatendo ili, kwa njia ya maisha ya kisiasa, jamii iwe yenye haki zaidi na kuimarisha zaidi hadhi na utu wa binadamu.[1185]

567. Katika mazingira ya jitihada ya kisiasa ya walei, uangalifu pekee unatakiwa kwa kuwatayarisha waamini kutumia mamlaka waliyo nayo, hasa wanapokabidhiwa wajibu hizo na raia wenzao kadiri ya kanuni za demokrasia. Lazima waoneshe shukrani kwa mfumo wa demokrasia “kiasi kwamba inahakikisha ushiriki wa raia katika kufanya maamuzi ya kisiasa, kuhakikisha kwamba wataongozwa katika kuchagua na kuwawajibisha wale wanaowatawala, na kuwabadili kwa njia ya amani inapotakiwa.”[1186] Lazima wakatae taasisi zenye siri zinazotaka kushawishi au kuathiri taasisi halali zinazofanya kazi vizuri. Kutumia madaraka lazima kuwe na tabia ya utumishi wa kutumia katika mazingira ya sheria ya maadili ili kufikia manufaa ya umma. Wanaotumia madaraka ya kisiasa lazima waone kuwa nguvu ya raia wote inaongozwa kwenye manufaa kwa wote;[1187] na wanapaswa kafanya hivyo sio kwa mtindo wa utawala wa mabavu, bali kwa kutumia nguvu ya tabia njema pamoja na uhuru.

568. Mwamini mlei anaitwa kuainisha hatua ambazo zinazochukuliwa katika mazingira ya siasa ili zielekeze utendaji wa kanuni na tunu zilizo sahihi kwa maisha katika jamii. Wito huo kwa mbinu za utambuzi,[1188] kwa mtu binafsi na kwa jumuiya, unajengwa kwa kufuata mbinu asili za kimsingi: ujuzi wa mazingira, yanayofanyiwa uchambuzi kwa msaada wa sayansi ya kijamii na vyombo vingine vya kufaa; utafiti kwa mpango wa mambo hayo katika mwanga wa ujumbe usiobadilika wa Injili na mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii, kutambua mambo yaliyochaguliwa kwa nia ya kuhakikisha kuwa hali itaendelea vizuri. Ikiwa jambo limechunguzwa kwa utaratibu na maelezo ya kufaa, inawezekana kuamua wazi na kwa ufanisi. Lakini, tunu pekee yake tu lazima zisiongoze kufikia maamuzi hayo, kwa sababu hakuna suala linaloweza kutatuliwa mara moja na basi. “Imani ya Kikristo haikudai kamwe kushurutisha muundo usio na uwezo wa kubadilika katika masuala ya kijamii na kisiasa, ikijua kuwa hali ya kihistoria inawataka wanaume na wanawake kuishi katika mazingira yasiyo kamilifu, na ambayo pia huweza kubadilika haraka.”[1189]

569. Mazingira pekee katika kutumia utambuzi hupatikana katika uendeshaji wa mfumo wa kidemokrasia, unaoeleweka kwa wengi leo katika mtazamo wa namna ya asiyesadiki au kutegemeza hisia ya watu ambazo zinaongoza kusadiki kwamba ukweli ni kitu kinachoamuliwa na walio wengi, na kutegemea maoni ya siasa.[1190] Katika hali hii, utambuzi unatakiwa hasa ikiwa unatumika mintarafu ukweli na usahihi wa habari, utafiti wa kisayansi, maamuzi ya kiuchumi, yanayoathiri maisha ya watu maskini sana. Vilevile, hudai inapohusika na mambo mintarafu wajibu wa kimaadili za kimsingi na zisizoepukika, kama utakatifu wa uhai, ndoa isiyotenguliwa, ustawi wa familia iliyosimikwa juu ya ndoa kati ya mwanaume na mwanamke.

Katika mazingira hayo vigezo fulani vya kimsingi vinafaa: kutofautisha, na pamoja, kuunganisha kati ya utaratibu wa kisheria na ule wa kimaadili; uaminifu katika utambulisho wa mtu mmoja na watu kwa pamoja, nia ya kujiingiza katika dialogia na watu wengine; hitaji, katika uamuzi wa kijamii na harakati za Wakristo, kuhusu kushika tunu tatu zisizotengana – tunu za kimaumbile, kuhusu kujitegemea kihalali kwa mambo ya dunia; tunu za kimaadili, zinazostawisha utambuzi wa hali ya kimaadili ya undani wa kila suala la kijamii na kisiasa; tunu zipitayo maumbile, ili kutimiza wajibu wake katika roho ya kiinjili ya Yesu Kristo.

570. Wakati – katika eneo la mambo yahusuyo wajibu za msingi za kimaadili – maamuzi ya kisheria au kisiasa yanayopendekezwa au yanayoamuliwa kinyume na tunu na kanuni za Kikristo, Majisterio hufundisha kuwa “dhamira ya Kikristo iliyolelewa vizuri hairuhusu mtu kupiga kura kwa programu ya siasa, au sheria binafsi inayopinga maudhui ya imani na maadili.”[1191] Ikiwa haiwezekani kuepuka utekelezaji wa programu hizo za kisiasa au kuzuia au kutangua sheria hizo, Majisterio hufundisha kuwa mbunge ambaye upinzani wake kwa programu au sheria hizo ni wazi na kujulikana na wote, anaweza kukubali kihalali maamuzi hayo kwa nia ya kuzuilia madhara yanayosababishwa na hizo programu au sheria, na kupunguza matokeo mabaya kwa ngazi ya utamaduni na maadili ya umma. Kwa hiyo, mfano maarufu wa mambo hayo unahusu sheria ya kuruhusu utoaji mimba.[1192] Kura ya mbunge, kwa vyovyote, haiwezi kuhesabiwa kama kibali cha sheria isiyo haki, bali kama kushiriki kupunguza matokeo mabaya ya sheria iliyokusudiwa, na uzito wake hutegemea tu wale walioshughulikia kuitengeneza.

Wakikabiliwa na mambo mengi yanayohusu wajibu za maadili za kimsingi na za lazima, lazima kukumbuka kuwa ushuhuda wa Kikristo unapaswa kuchukuliwa kama sharti la kimsingi linaloweza kusababisha mtu hata kutoa uhai kwa ajili ya upendo na heshima ya kibinadamu.[1193] Historia ya karne ishirini zilizopita, kama vile ya karne iliyopita imejaa mashahidi kwa ajili ya ukweli wa Kikristo, ushahidi wa imani, matumaini na upendo uliosimikwa katika Injili. Kifodini ni ushahidi wa mtu aliyefananishwa binafsi na Kristo msulibiwa, ukielezewa kwa namna muhimu ya kumwaga damu yake, kadiri ya mafundisho ya Injili; ikiwa “chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, . hutoa mazao mengi” (Yn 12:24).

571. Wajibu ya kisiasa wa Wakatoliki mara nyingi uko katika mazingira ya “kujitawala” ya Dola, yaani, kutofautisha kati ya maeneo ya siasa na dini.[1194] Utengano huo “ni tunu iliyofikiwa na kukubaliwa na Kanisa Katoliki, na imekuwa urithi wa ustaarabu wa nyakati zetu.”[1195] Mafundisho Katoliki ya maadili, lakini, hukataa wazi kabisa mtazamo wa kujitawala unaochukuliwa kama uhuru wa kutoka au kutozingatia sheria ya kimaadili; ‘uhuru’ wa namna hii unahusu, awali ya yote, tabia ya mtu anayeheshimu ukweli unaotokea katika ufahamu wa kimaumbile kuhusu maisha ya binadamu katika jamii, hata kama kweli hizo zinaweza kufundishwa katika dini pekee, kwa sababu ukweli ni mmoja.”[1196] Hamu halisi ya kutafuta ukweli, kwa kutumia vifaa kisheria ili kuustawisha na kulinda kweli za kimaadili kuhusu maisha ya kijamii – haki, uhuru, heshima kwa uhai na kwa haki za binadamu wengine - ni haki na wajibu wa wahusika wote wa jumuiya ya kijamii na kisiasa.

Majisterio inapoingilia kati masuala ya maisha ya kijamii na kisiasa, hayakosi kuangalia masharti ya uhuru unaotazamwa kwa namna iliyo sahihi, kwa sababu “Majisterio haitaki kutumia mamlaka ya kisiasa au kuondoa uhuru wa maoni ya Wakristo kuhusu masuala ya kidunia. Kumbe, inamaanisha – kama ilivyo kazi yake pekee – kufundisha na kuangaza dhamira ya waamini, hasa wale wanaohusika na maisha ya kisiasa, ili matendo yao daima yafae ustawi mkamilifu wa binadamu na manufaa kwa wote. Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii sio kujipenyeza katika serikali ya nchi binafsi. Ni shauri la wajibu wa walei Wakatoliki kujiamini kimaadili, kunakopatikana katika dhamiri ya mtu, iliyo moja na isiyogawanyika.”[1197]

572. Kanuni ya kujitegemea inadai heshima ya kila dini kwa upande wa Dola, ambayo “huhakikisha uendeshaji huru wa ibada, na utendaji wa kiroho, kiutamaduni, na misaada ya upendo ya jumuiya za waamini. Katika jamii ya watu mchanganyiko, kutoegemea dini katika mambo ya nchi huruhusu mawasiliano kati ya mapokeo ya dini mbalimbali ya nchi.”[1198] Kwa bahati mbaya, hata katika jamii za kidemokrasia, bado kuna hali ya kukosa kuvumiliana na kustahiana na hiyo hukataa kutambua umuhimu wa dini katika siasa na utamaduni. Kutostahimili huko hutaka kuzuia utendaji wa Wakristo katika eneo la kijamii na kisiasa kwa sababu Wakristo wanajitahidi kushika ukweli unaofundishwa na Kanisa na wanatii wajibu wa kimaadili wa kutenda kwa kulingana na dhamiri zao. Nia hizo zinakwenda mbali, hata kimsingi, kiasi kwamba wanakataa msingi wa maadili ya kimaumbile. Mambo hayo huondoa maadili na kuleta matokeo wazi ya mwenye nguvu kushinda juu ya mdhaifu, haikubaliwi kamwe katika mfumo wa utawala wa wengi, kwa sababu hubomoa kila msingi wa kweli wa kila jamii ya binadamu. Katika mwanga wa hali hii ya mambo, “kuweka kando Ukristo. hakuwezi kuleta faida katika nyakati za baadaye za jamii, au kwa maridhiano kati ya watu; mwisho itahatarisha msingi wenyewe wa kiroho na kiutamaduni wa ustaarabishaji.”[1199]

573. Eneo maalumu la utambuzi kwa upande wa mwamini mlei linahusu kuchagua vyombo vya siasa, yaani kuwa mwanachama wa chama au aina nyingine za kushiriki siasa. Uchaguzi unaoandamana na tunu, na kuangalia mazingira halisi. Kwa vyovyote, uchaguzi unaoamuliwa lazima usimikwe katika upendo na kuelekea kutekeleza kwa manufaa ya wote.[1200] Ni vigumu kwa imani ya Kikristo kupokelewa katika kikundi kimoja tu cha jamii au ushirika wa kisiasa kudai kwamba chama kimoja au muungano wa kisiasa unaendana kikamilifu na masharti ya imani au ya maisha ya Kikristo na kungeweza kuwa ni kufanya kosa la hatari. Wakristo hawawezi kupata chama kinachoridhisha kikamilifu masharti ya kimaadili yanayotokana na imani na ya kuwa mwanakanisa. Kuwa mshiriki katika ushirika wa kisiasa hakuwezi kuwa wa itikadi, lakini kila mara uwe wa kuchunguza; kwa njia hii chama na uwanja wake wa kisiasa itakuwa salama zaidi kwa kutekeleza kwa manufaa ya wote pamoja na lengo la kiroho la binadamu.[1201]

574. Utofautishaji ambao lazima ufanyike, kwa upande mmoja kati ya masharti ya imani na hiari za kijamii – kisiasa na kwa upande mwingine kati ya chaguzi zinazofanywa na Mkristo binafsi na kama jumuiya, inamaanisha kwamba, kuwa mwanachama wa chama au shirika la kisiasa lazima kuonekane kama uamuzi wa binafsi, halali walau katika mipaka ya vyama vile au misimamo ambayo haipingani na imani ya Kikristo na tunu zake.[1202] Lakini, kuchagua chama, ushirika wa kisiasa, watu ambao watakabidhiwa maisha ya umma, wakati huohuo kuhusisha dhamiri ya kila mmoja, hakuwezi kamwe kuwa uchaguzi wa mtu peke yake. “Ni wajibu ya jumuiya ya Kikristo kuchunguza kwa makini hali iliyo na upekee ya nchi yake, kwa kuangazwa na mwanga wa Maneno yasiyobadilika ya Injili na kutokeza kanuni za kutafiti, miongozo ya kuhukumu, na maelekezo ya utendaji kutoka katika Mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii.”[1203] Kwa vyovyote “hairuhusiwi kwa yeyote kubainisha mamlaka ya Kanisa kwa maoni binafsi tu”;[1204] waamini wanapaswa hasa “kujaribu kuongozana kwa dialogia ya kweli katika roho ya upendano na kutamani kwa hamu ya juu zaidi ya yote manufaa kwa wote.”[1205]

 

HITIMISHO

KWA USTAARABU WA UPENDO

 

a. Msaada Ambao Kanisa Hutoa kwa Watu wa Leo

575. Katika jamii ya kisasa, watu wanang’amua zaidi na zaidi mahitaji ya kuona maana mpya. “Mtu daima anatamani kujua walau kidogo kisicho wazi, maana ya maisha yalivyo, harakati zake, na kifo chake.”[1206] Ni vigumu kuona masharti ya kujenga maisha ya kesho katika mazingira ya mahusiano ya kimataifa yaliyo mchanganyiko na kutegemeana ambayo pia ni ya kila siku zaidi na zaidi yenye vurugu na kukosa amani. Maisha na kifo vinaonekana kuwa mikononi mwa maendeleo ya sayansi na teknolojia, zinazokwenda haraka kuliko uwezo wa binadamu kusisitiza lengo lake la mwisho na kupima gharama yake. Hali nyingi zinadokeza kwamba “kutoridhika kunakoongezeka kuhusu mali ya dunia zinazopatikana kati ya watu wa nchi tajiri, kunaharibu haraka ndoto nyingi za paradisi hapa duniani. Watu wanatambua zaidi na zaidi haki zao kama binadamu, haki zilizo za wote na zisizokiukwa, na wanatamani mahusiano ya kibinadamu na ya haki zaidi.”[1207]

576. Kwa maswali hayo kuhusu maana na lengo la maisha ya binadamu, Kanisa linajibu kwa kutangaza Injili ya Kristo, inayokomboa hadhi ya binadamu kutoka katika maoni yanayobadilikabadilika na kuhakikisha uhuru wa wanaume na wanawake kwa jinsi isiyoweza sheria yoyote ya watu. Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatikano unaonesha kuwa utume wa Kanisa katika dunia ya leo ni kusaidia kila binadamu kumtambua Mungu aliye lengo la mwisho la maisha yake. Kanisa linajua vema kuwa “Mungu peke yake, ambaye yeye anatumikia, anaweza kushibisha shauku kali ya moyo wa binadamu, kwa sababu ulimwengu na unachotolea hakiwezi kumridhisha.”[1208] Mungu peke yake, aliyeumba binadamu kwa mfano wake na kumkomboa kutoka katika dhambi, anaweza kujibu kikamilifu kwa njia ya Ufunuo uliotendeka katika Mwanae aliyejifanya mtu. Injili, kwa kweli, “hupasha habari na kutangaza uhuru wa wana wa Mungu, na kuvunja kila kifungo cha dhambi, inaheshimu kabisa hadhi ya dhamiri na uhuru wake wa kuchagua; haikosi kamwe kutia moyo kutumia vipaji vya binadamu katika utumishi wa Mungu na wa watu, na hatimaye, inahimiza kila mmoja kwa upendo wenye huruma kwa wote.”[1209]

b. Kuanza Upya toka Imani katika Kristo

577. Imani katika Mungu na katika Yesu Kristo inaangaza kanuni za kimaadili zilizo peke yao msingi usiobadilika kamwe, imara na shwari, wa utaratibu wa ndani na nje, wa binafsi na wa umma, ambao pekee unaweza kuzalisha na kuthibitisha ufanisi wa Dola.” [1210] Uhai katika jamii lazima usimikwe juu ya mpango wa Mungu, kwa sababu “hali ya kitheolojia hutakiwa kwa kutafsiri na kutatua matatizo ya siku hizi katika jamii ya binadamu.”[1211] Katika hali iliyopo ya kutisha ya aina za unyonyaji na kukosa haki ya kijamii, kuna hisia kali iliyoenea sana ya mahitaji ya mageuzi mapya ya kibinafsi na ya jamii ya kimsingi, yanayoweza kuhakikisha haki, mshikamano, uaminifu na uwazi. Kweli, kuna njia ndefu na ngumu mbele; kuleta mabadiliko mapya hayo hudai nguvu sana, hasa kwa ajili ya wingi na uzito wa mambo yanayosababisha na kuharibu hali ya kukosa haki iliyomo kwa wakati huu duniani. Lakini, kama historia na mang’amuzi binafsi huonesha, si vigumu ndani ya mambo hayo kutambua sababu zilizo hasa za “kiutamaduni” kutokana na mtazamo wa pekee wa kumwona binadamu, jamii na dunia. Naam, katika kiini cha suala la utamaduni tunakuta hisia ya maadili, ambayo kwa upande wake imesimikwa na kukamilika katika hisia ya kidini.”[1212] Kuhusu “Suala la Kijamii” tusidanganywe na “upuuzi wa kutarajia kuwa, tukikabili changamoto kubwa za nyakati zetu, tutaweza kupata njia ya kanuni ya kutenda muujiza. La, hatutaokolewa na Kanuni bali na Kristo na uhakika anaotupa: Mimi ni pamoja nanyi! Basi, sio jambo la kutunga ‘programu mpya’. Programu iko tayari: ni mpango unaopatikana katika Injili na kuishi katika Mapokeo hai, ni sawa kama ilivyokuwa daima. Hatimaye, ina kiini chake katika Kristo mwenyewe, ambaye anajulikana, kupendwa na kuigwa, na hivyo katika yeye tunaweza kuishi uzima wa Utatu Mtakatifu, na pamoja naye kugeuza historia hadi utimilifu wake katika Yerusalemu ya Mbinguni.”[1213]

c. Matumaini Thabiti

578. Kanisa linawafundisha wanaume na wanawake kuwa Mungu huwapa nafasi ya kushinda maovu na kufikia mema. Bwana aliwakomboa watu wote “mlinunuliwa kwa thamani.” (1Kor6:20). Maana na msingi wa jukumu la Kikristo katika dunia zinasimikwa katika hakika hiyo, inayoamsha matumaini ijapo dhambi imetia dosari kubwa katika historia ya watu. Ahadi za Mungu zinahakikishia kuwa dunia haifungiki juu yake mwenyewe, bali ni wazi kwa Ufalme wa Mungu. Kanisa linajua matokeo ya “siri ya kuasi” (2 The 2:7), lakini pia linajua kuwa “katika kila mwanadamu kuna vipaji na nguvu, na ‘wema’ kimsingi (taz. Mwa 1:31), kwa sababu binadamu ni mfano wa Muumba, na yumo chini ya mvuto wa wokovu wa Kristo, ambaye ‘amejiunga kwa namna fulani na kila mtu’ na kwa sababu kazi yenye nguvu ya Roho Mtakatifu ‘hujaza ulimwengu’ (Hek 1:7)."[1214]

579. Tumaini la Kikristo linatia nguvu sana jukumu la kujihusisha katika eneo la kijamii, kwa sababu huleta kujiamini kwa kuweza kujenga dunia bora zaidi, hata kama haitapatikana kamwe “paradisi hapa duniani”.[1215] Wakristo, hasa walei, wanahimizwa kutenda ili “nguvu ya Injili ing’ae katika maisha ya kijamii na ya familia ya kila siku. Wanajimudu kama watoto wa ahadi, na hivyo kama Mashujaa, katika imani wanatumia vizuri wakati huu (taz. Efe 5:16; Kol 4:5), na kwa subira wanangoja utukufu utakaokuja (taz. Rum 8:25). Basi, wasifiche matumaini hayo ndani ya mioyo yao, bali wayaoneshe kwa njia ya uongofu wa daima na kwa kushinda ‘juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho’ (Efe 6:12)."[1216] Tumaini hili la kidini linaloongoza uwajibikaji huu laweza kutokubaliwa na wote, lakini mvuto wa kimaadili kutoka tumaini hilo ndio sehemu inayokutanisha Wakristo na watu wote wenye mapenzi mema.

d. Kujenga “Ustaarabu wa Upendo”

580. Kusudi la sasa hivi la mafundisho ya Kanisa kuhusu jamii ni kudokeza kanuni na tunu zinazoweza kutegemeza jamii inayostahili binadamu. Kati ya kanuni hizo, mshikamano hubeba nyingine zote, kwa namna fulani. Hudhihirisha “moja ya kanuni za kimsingi ya mitazamo ya Kikristo ya taasisi za kijamii na kisiasa.”[1217]

Mwanga wa kuangaza kanuni hizo unatokana na umuhimu wa upendo, “ishara inayojulisha wanafunzi wa Kristo (taz. Yn 13:35)."[1218] Yesu anatufundisha kuwa “sheria ya kimsingi ya ukamilifu wa binadamu, na tena mageuzi ya ulimwengu, ni amri ya upendo”[1219] (taz. Mt 22:40; Yn 15:12; Kol 3:14; Yak 2:8). Mwenendo wa binafsi ni kweli wa kibinadamu unapotoka katika upendo, huonesha upendo na kuelekea upendo. Hivyo, ukweli huo hufaa kwa eneo la jamii; Wakristo wanapaswa kuwa wazi kabisa na ni mashahidi wa hayo, na hawana budi kuonesha kwa maisha yao jinsi upendo ulivyo nguvu pekee (taz. 1 Kor 12:31-14:1) inayoweza kuongoza kwa ukamilifu wa binafsi na kijamii, na kuruhusu jamii kupiga hatua kuelekea wema.

581. Upendo lazima uwemo na kukoleza kila mahusiano ya kijamii.[1220] Inatakiwa hasa kwa wale walio na madaraka kwa manufaa ya watu. “Wanapaswa kuustawisha ndani yao na kuuamsha kwa wengine, upendo, mkuu na malkia wa fadhila. Kwa maana, matokeo mazuri tunayotamani sote yanaletwa hasa kwa kumimina wingi wa mapendo, upendo ule wa kweli wa Kikristo unaotimiliza sheria yote ya Injili, ukiwa tayari kujitolea sadaka mwenyewe kwa ajili ya wengine, na ni dawa salama dhidi ya kiburi cha dunia na kujipenda binafsi kupita kiasi.”[1221] Upendo huu sharti uitwe “upendo kijamii”[1222] au “upendo wa kisiasa”[1223] na lazima uwakumbatie wanadamu wote.[1224] “Upendo kijamii”[1225] ni kinyume cha ubinafsi na umimi. Kuangalia maisha ya jamii peke yake kama wafanyavyo watu katika mtazamo wa kisosholojia, tusisahau kwamba maendeleo kamili ya mtu binafsi na ya jamii yanaathiriana. Ubinafsi, basi, ni adui aliye hatari sana kwa jamii iliyo katika utaratibu. Historia hufundisha jinsi mioyo inavyoharibika, kama wanaume na wanawake, wasipoweza kutambua tunu nyingine au mambo mengine ya kufaa mbali na mali ya dunia, shauku inayotawala ambayo inazuia uwezo wao wa kujitolea.

582. Ili jamii iwe zaidi na tabia ya kibinadamu, kumstahili binadamu, upendo katika maisha ya jamii – siasa, uchumi na utamaduni – lazima upate tunu mpya, kwa kuwa sheria daima na ya hali ya juu, kwa kila utendaji. “Ikiwa haki kwa yenyewe inafaa kwa ajili ya ‘usuluhishi’ kati ya watu kuhusu ugawaji kati yao wa mali kwa usawa, upendo na upendo tu (pamoja na ule upendo wenye ukarimu tunaouita ‘huruma’) unaoweza kurudisha binadamu kuwa mwenyewe.”[1226] Mahusiano ya wanadamu hayawezi kuongozwa kwa kipimo cha haki tu. “Wakristo wanajua kuwa upendo ni sababu ya Mungu kuingia katika uhusiano na mtu. Na ni upendo unaodai toka kwa mwanadamu kama jibu lake. Kwa hiyo, upendo pia ni njia maalumu na ya staha hasa ya mahusiano kati ya watu. Upendo, basi, lazima ukoleze kila sekta ya maisha ya watu na kufikia utaratibu wa kimataifa. Wanadamu tu, ambamo hutawala ‘ustaarabu wa upendo’ wataweza kufurahia amani sahihi na ya kudumu.[1227] Kwa upande huu, Majisterio hupendekeza sana ushirikiano kwa sababu unaweza kuhakikisha manufaa ya umma na kusaidia maendeleo kamili ya binadamu: upendo ”hufanya mtu kumwona jirani kama nafsi nyingine.”[1228]

583. Upendo tu unaweza kugeuza kabisa mwanadamu.[1229] Mageuzi hayo hayakusudii kuvuta kabisa hali ya kidunia na kuwa kitu cha kiroho kisicho na mwili.[1230] Wale wanaofikiri kuweza kuishi fadhila ya kimungu ya upendo bila kujali sehemu yake ya kimaumbile, inayochukua wajibu za haki, wanajidanganya. Upendo ni amri kuu ya kijamii. Unaheshimu wengine na haki zao. Unadai mazoea ya haki na upendo pekee unatuwezesha kuishi upendo. Upendo hustawisha maisha ya kujitolea: ‘Mtu ye yote anayetaka kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na ye yote atakayeiangamiza, ataiponya” (Lk 17:33)."[1231] Wala upendo hauwezi kupata ukamilifu wake katika hali ya duniani tu ya mahusiano ya wanadamu na kijamii, kwa sababu kwenye uhusiano na Mungu tu, unapata utimilifu wake. “Karibu na mwisho wa maisha, nitafika mbele yako mikono mitupu, kwa sababu siombi, ee Bwana uhesabu kazi zangu. Haki zetu zote kuwa si kamili mbele ya macho yako. Basi, nataka nivalishwe katika haki yako tu na kupokea kutoka upendo wako na kuishi nawe milele.”[1232]


 
[1] Cf. John Paul II, Apostolic Letter Novo Millennio Ineunte, 1: AAS 93 (2001), 266.
[2] John Paul II, Encyclical Letter Redemptoris Missio, 11: AAS 83 (1991), 260.
[3]  Catechism of the Catholic Church, 2419.
[4] John Paul II, Apostolic Letter Novo Millennio Ineunte, 50-51: AAS 93 (2001), 303-304.
[5] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 41: AAS 80 (1988), 571-572.
[6] Cf. John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Ecclesia in America, 54: AAS 91 (1999), 790.
[7] Cf. John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Ecclesia in America, 54: AAS 91 (1999), 790; Catechism of the Catholic Church, 24.
[8] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 55: AAS 83 (1991), 860.
[9] John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Christifideles Laici, 15: AAS 81 (1989), 414.
[10] Second Vatican Ecumenical Council, Decree Christus Dominus, 12: AAS 58 (1966), 678.
[11] Second Vatican Ecumenical Council, Dogmatic Constitution Lumen Gentium, 31: AAS 57 (1965), 37.
[12] Cf. Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 4: AAS 63 (1971), 403.
[13] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 92: AAS 58 (1966), 1113-1114.
[14] Second Vatican Ecumenical Council, Dogmatic Constitution Dei Verbum, 2: AAS 58 (1966), 818.
[15] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 3: AAS 58 (1966), 1026.
[16] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 3: AAS 58 (1966), 1027.
[17] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 10: AAS 58 (1966), 1032.
[18] John Paul II, Address at General Audience (19 October 1983), 2: L’Osservatore Romano, English edition, 24 October 1983, p. 9.
[19] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 44: AAS 58 (1966), 1064.
[20] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 3: AAS 58 (1966), 1026.
[21] Second Vatican Ecumenical Council, Dogmatic Constitution Lumen Gentium, 1: AAS 57 (1965), 5.
[22] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 30: AAS 58 (1966), 1050.
[23]  Catechism of the Catholic Church, 1789, 1970, 2510.
[24]  Catechism of the Catholic Church, 2062.
[25]  Catechism of the Catholic Church, 2070.
[26] John Paul II, Enyclical Letter Veritatis Splendor, 97: AAS 85 (1993), 1209.
[27] These laws are found in Ex 23, Deut 15, Lev 25.
[28] Cf. John Paul II, Apostolic Letter Tertio Millennio Adveniente, 13: AAS 87 (1995), 14.
[29] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 13: AAS 58 (1966), 1035.
[30] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Dogmatic Constitution Dei Verbum, 4: AAS 58 (1966), 819.
[31] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 10: AAS 58 (1966), 1033.
[32] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Dogmatic Constitution Lumen Gentium, 9: AAS 57 (1965), 12-14.
[33] John Paul II, Apostolic Letter Mulieris Dignitatem, 7: AAS 80 (1988), 1666.
[34] John Paul II, Apostolic Letter Mulieris Dignitatem, 7: AAS 80 (1988), 1665-1666.
[35] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 40: AAS 80 (1988), 569.
[36] John Paul II, Apostolic Letter Mulieris Dignitatem, 7: AAS 80 (1988), 1664.
[37] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 24: AAS 58 (1966), 1045.
[38] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 12: AAS 58 (1966), 1034.
[39] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 22: AAS 58 (1966), 1043.
[40] Second Vatican Ecumenical Council, Dogmatic Constitution Dei Verbum, 5: AAS 58 (1966), 819.
[41] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 22: AAS 58 (1966), 1043.
[42] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 22: AAS 58 (1966), 1043.
[43]  Catechism of the Catholic Church, 1888.
[44] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 38: AAS 80 (1988), 565-566.
[45] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 28: AAS 58 (1966), 1048.
[46]  Cf. Catechism of the Catholic Church, 1889.
[47] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 37: AAS 58 (1966), 1055.
[48] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 36: AAS 58 (1966), 1054; Second Vatican Ecumenical Council, Decree Apostolicam Actuositatem, 7: AAS 58 (1966), 843-844.
[49] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 36: AAS 58 (1966), 1054.
[50] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2244.
[51] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Dogmatic Constitution Dei Verbum, 2: AAS 58 (1966), 818.
[52] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 41: AAS 83 (1991), 844.
[53] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 41: AAS 83 (1991), 844-845.
[54] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 76: AAS 58 (1966), 1099.
[55] Second Vatican Ecumenical Council, Dogmatic Constitution Lumen Gentium, 1: AAS 57 (1965), 5.
[56] Second Vatican Ecumenical Council, Dogmatic Constitution Lumen Gentium, 5: AAS 57 (1965), 8.
[57] John Paul II, Encyclical Letter Redemptoris Missio, 20: AAS 83 (1991), 267.
[58] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 76: AAS 58 (1966), 1099; Catechism of the Catholic Church, 2245.
[59] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 76: AAS 58 (1966), 1099.
[60] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 40: AAS 58 (1966), 1058.
[61] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2244.
[62] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 40: AAS 58 (1966), 1058.
[63] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Gaudium et Spes, 11: AAS 58 (1966), 1033.
[64] Cf. Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 37: AAS 63 (1971), 426-427.
[65] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Redemptor Hominis, 11: AAS 71 (1979), 276: ‘‘The Fathers of the Church rightly saw in the various religions as it were so many reflections of the one truth, ‘seeds of the Word,’ attesting that, though the routes taken may be different, there is but a single goal to which is directed the deepest aspiration of the human spirit.’’
[66] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 38: AAS 58 (1966), 1055-1056.
[67] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 39: AAS 58 (1966), 1057.
[68] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 39: AAS 58 (1966), 1057.
[69] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Redemptor Hominis, 13: AAS 71 (1979), 283-284.
[70] Cf. John Paul II, Apostolic Letter Novo Millennio Ineunte, 16-28: AAS 93 (2001), 276 285.
[71] John Paul II, Encyclical Letter Redemptoris Mater, 37: AAS 79 (1987), 410.
[72] Congregation for the Doctrine of the Faith, Instruction Libertatis Conscientia, 97: AAS 79 (1987), 597.
[73] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 1: AAS 58 (1966), 1025-1026.
[74] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 40: AAS 58 (1966), 1057-1059; John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 53-54: AAS 83 (1991), 859- 860; John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 1: AAS 80 (1988), 513-514.
[75] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 32: AAS 58 (1966), 1051.
[76] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 54: AAS 83 (1991), 859.
[77] Cf. Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 13: AAS 59 (1967), 263.
[78] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 40: AAS 58 (1966), 1057-1059.
[79] John Paul II, Encyclical Letter Redemptor Hominis, 14: AAS 71 (1979), 284.
[80]  Catechism of the Catholic Church, 2419.
[81] Cf. John Paul II, Homily at Pentecost for the First Centenary of Rerum Novarum, (19 May 1991): AAS 84 (1992), 282.
[82] Cf. Paul VI, Apostolic Exhortation Evangelii Nuntiandi, 9, 30: AAS 68 (1976), 10-11; John Paul II, Address to the Third General Conference of Latin American Bishops, Puebla, Mexico (28 January 1979), III/4-7: AAS 71 (1979), 199-204; Congregation for the Doctrine of the Faith, Instruction Libertatis Conscientia, 63-64, 80: AAS 79 (1987), 581-582, 590- 591.
[83] John Paul II, Encyclical Letter Redemptor Hominis, 8: AAS 71 (1979), 270.
[84] Second Vatican Ecumenical Council, Dogmatic Constitution Lumen Gentium, 48: AAS 57 (1965), 53.
[85] Cf. Paul VI, Encyclical Letter Evangelii Nuntiandi, 29: AAS 68 (1976), 25.
[86] Paul VI, Encyclical Letter Evangelii Nuntiandi, 31: AAS 68 (1976), 26.
[87] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 54: AAS 83 (1991), 860.
[88] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 41: AAS 80 (1988), 570-572.
[89] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 5: AAS 83 (1991), 799.
[90] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 54: AAS 83 (1991), 860.
[91] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2420.
[92] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 42: AAS 58 (1966), 1060.
[93] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 41: AAS 80 (1988), 570-572.
[94] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 54: AAS 83 (1991), 860.
[95] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Declaration Dignitatis Humanae, 14: AAS 58 (1966), 940; John Paul II, Encyclical Letter Veritatis Splendor, 27, 64, 110: AAS 85 (1993), 1154-1155, 1183-1184, 1219-1220.
[96] John Paul II, Message to the Secretary-General of the United Nations, on the occasion of the thirtieth anniversary of the Universal Declaration of Human Rights (2 December 1978): AAS 71 (1979), 124.
[97] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 5: AAS 83 (1991), 799.
[98] Cf. Paul VI, Apostolic Exhortation Evangelii Nuntiandi, 34: AAS 68 (1976), 28.
[99]  Code of Canon Law, canon 747, § 2.
[100] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 3: AAS 73 (1981), 583-584.
[101] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 41: AAS 80 (1988), 571.
[102] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 41: AAS 80 (1988), 571.
[103] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 41: AAS 80 (1988), 572.
[104] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 59: AAS 83 (1991), 864-865.
[105] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Fides et Ratio: AAS 91 (1999), 5-88.
[106] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Declaration Dignitatis Humanae, 14: AAS 58 (1966), 940.
[107] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Veritatis Splendor, 13, 50, 79: AAS 85 (1993), 1143-1144, 1173-1174, 1197.
[108] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 59: AAS 83 (1991), 864.
[109] In this regard, the foundation of the Pontifical Academy of Social Sciences is significant; in the motu proprio establishing the Academy one reads: ‘‘Social science research can effectively contribute to improving human relations, as has been shown by the progress achieved in various sectors of society especially during the century now drawing to a close. This is why the Church, ever concerned for man’s true good, has turned with growing interest to this field of scientific research in order to obtain concrete information for fulfilling the duties of her Magisterium’’: John Paul II, Motu Proprio Socialium Scientiarum (1 January 1994): AAS 86 (1994), 209.
[110] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 54: AAS 83 (1991), 860.
[111] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 59: AAS 83 (1991), 864.
[112] Second Vatican Ecumenical Council, Dogmatic Constitution Lumen Gentium, 12: AAS 57 (1965), 16.
[113] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2034.
[114] Cf. Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 3-5: AAS 63 (1971), 402-405.
[115] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2037.
[116] Cf. Congregation for the Doctrine of the Faith, Instruction Donum Veritatis, 16-17, 23: AAS 82 (1990), 1557-1558, 1559-1560.
[117] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 53: AAS 83 (1991), 859.
[118] Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 13: AAS 59 (1967), 264.
[119] Cf. Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 4: AAS 63 (1971), 403-404; John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 41: AAS 80 (1988), 570-572; Catechism of the Catholic Church, 2423; Congregation for the Doctrine of the Faith, Instruction Libertatis Conscientia, 72: AAS 79 (1987), 586.
[120] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 25: AAS 58 (1966), 1045-1046.
[121] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 76: AAS 58 (1966), 1099-1100; Pius XII, Radio Message for the fiftieth anniversary of Rerum Novarum: AAS 33 (1941), 196-197.
[122] Cf. Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 190; Pius XII, Radio Message for the fiftieth anniversary of Rerum Novarum: AAS 23 (1931), 196-197; Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 42: AAS 58 (1966), 1079; John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 41: AAS 80 (1988), 570-572; John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 53: AAS 83 (1991), 859; Congregation for the Doctrine of the Faith,  Instruction Libertatis Conscientia, 72: AAS 79 (1987), 585-586.
[123] John Paul II, Encyclical Letter Redemptor Hominis, 14: AAS 71 (1979), 284; cf. John Paul II, Address to the Third General Conference of Latin American Bishops, Puebla, Mexico (28 January 1979), III/2: AAS 71 (1979), 199.
[124] Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 42: AAS 59 (1967), 278.
[125] Paul VI, Apostolic Exhortation Evangelii Nuntiandi, 9: AAS 68 (1976), 10.
[126] Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 42: AAS 59 (1967), 278.
[127] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2039.
[128] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2442.
[129] Cf. John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Christifideles Laici, 15: AAS 81 (1989), 413; Second Vatican Ecumenical Council, Dogmatic Constitution Lumen Gentium, 31: AAS 57 (1965), 37.
[130] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 43: AAS 58 (1966), 1061-1064; Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 81: AAS 59 (1967), 296-297.
[131] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 453.
[132] Beginning with the Encyclical Pacem in Terris of John XXIII, the recipient is expressly identified in this manner in the initial address of such documents.
[133] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 3: AAS 80 (1988), 515; Pius XII, Address to Participants in a Convention of the Catholic Action movement (29 April 1945), in Discorsi e Radiomessaggi di Pio XII, vol. VII, 37-38; John Paul II, Address at the international symposium ‘‘From Rerum Novarum to Laborem Exercens: towards the year 2000’’ (3 April 1982): Insegnamenti di Giovanni Paolo II, V, 1 (1982), 1095-1096.
[134] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 3: AAS 80 (1988), 515.
[135] Cf. Congregation for the Doctrine of the Faith, Instruction Libertatis Conscientia, 72: AAS 79 (1987), 585-586.
[136] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 3: AAS 80 (1988), 515.
[137] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 46: AAS 83 (1991), 850-851.
[138] Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 42: AAS 63 (1971), 431.
[139] Cf. Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 179; Pius XII, in his Radio Message for the fiftieth anniversary of Rerum Novarum: AAS 33 (1941), 197, speaks of ‘‘Catholic social doctrine’’ and, in the Encyclical Letter Menti Nostrae of 23 September 1950: AAS 42 (1950), 657, of ‘‘the Church’s social doctrine.’’ John XXIII retains the expression ‘‘the Church’s social doctrine’’ (Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 [1961], 453; Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 [1963], 300-301) and also uses ‘‘Christian social doctrine’’ (Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 [1961], 453) or even ‘‘Catholic social doctrine’’ (Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 [1961], 454).
[140] Cf. Leo XIII, Encyclical Letter Rerum Novarum: Acta Leonis XIII, 11 (1892), 97-144.
[141] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 3: AAS 73 (1981), 583-584; John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 1: AAS 80 (1988), 513-514.
[142] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2421.
[143] Cf. Leo XIII, Encyclical Letter Rerum Novarum: Acta Leonis XIII, 11 (1892), 97-144.
[144] Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 20, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, p. 24.
[145] Cf. Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno, 39: AAS 23 (1931), 189; Pius XII, Radio Message for the fiftieth anniversary of Rerum Novarum: AAS 33 (1941), 198.
[146] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 5: AAS 83 (1991), 799.
[147] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 5: AAS 83 (1991), 799.
[148] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 56: AAS 83 (1991), 862.
[149] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 60: AAS 83 (1991), 865.
[150] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 60: AAS 83 (1991), 865.
[151] Leo XIII, Encyclical Letter Rerum Novarum: Acta Leonis XIII, 11 (1892), 143; cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 56: AAS 83 (1991), 862.
[152] Cf. Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 177-228.
[153] Cf. Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 186-189.
[154] Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 21, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, p. 24.
[155] Cf. Pius XI, Encyclical Letter Non Abbiamo Bisogno: AAS 23 (1931), 285-312.
[156] The official German text can be found in AAS 29 (1937), 145-167.
[157] Pius XI, Address to Belgian Radio Journalists (6 September 1938), in John Paul II, Address to international leaders of the Anti-Defamation League of B’nai B’rith (22 March 1984): L’Osservatore Romano, English edition, 26 March 1984, pp. 8, 11.
[158] The official Latin text can be found in AAS 29 (1937), 65-106.
[159] Cf. Pius XI, Encyclical Letter Divini Redemptoris: AAS 29 (1937), 130.
[160] Cf. Pius XII, Christmas Radio Messages: on peace and the international order, 1939, AAS 32 (1940), 5-13; 1940, AAS 33 (1941), 5-14; 1941, AAS 34 (1942), 10-21; 1945, AAS 38 (1946), 15- 25; 1946, AAS 39 (1947), 7-17; 1948, AAS 41 (1949), 8-16; 1950, AAS 43 (1951), 49-59; 1951, AAS 44 (1952), 5-15; 1954, AAS 47 (1955), 15-28; 1955, AAS 48 (1956), 26-41; on the order within nations, 1942, AAS 35 (1943), 9-24; on democracy, 1944, AAS 37 (1945), 10-23; on the function of Christian civilization, 1 September 1944, AAS 36 (1944), 249-258; on making a return to God in generosity and brotherhood, 1947, AAS 40 (1948), 8-16; on the year of the great return and of great forgiveness, 1949, AAS 42 (1950), 121-133; on the depersonalization of man, 1952, AAS 45 (1953), 33-46; on the role of progress in technology and peace among peoples, 1953, AAS 46 (1954), 5-16.
[161] Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 22, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, p. 25.
[162] Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 22, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, p. 25.
[163] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 267-269, 278-279, 291, 295-296.
[164] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 401-464.
[165] Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 23, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, p. 26.
[166] Cf. John XXIII Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 415-418.
[167] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 257-304.
[168] John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris, Title: AAS 55 (1963), 257.
[169] John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 301.
[170] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 294.
[171] Cf. Cardinal Maurice Roy, Letter to Paul VI and Document on the occasion of the tenth anniversary of Pacem in Terris, L’Osservatore Romano, English edition, 19 April 1973, pp. 1-8.
[172] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes: AAS 58 (1966), 1025-1120.
[173] Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 24, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, p. 28.
[174] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 1: AAS 58 (1966), 1026.
[175] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 40: AAS 58 (1966), 1058.
[176] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 24: AAS 58 (1966), 1045.
[177] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 25: AAS 58 (1966), 1045.
[178] Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 24, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, p. 29.
[179] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Declaration Dignitatis Humanae: AAS 58 (1966), 929-946.
[180] Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 76-80: AAS 59 (1967), 294-296.
[181] Cf. Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio: AAS 59 (1967), 257-299.
[182] Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 25, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, p. 29.
[183] Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 21: AAS 59 (1967), 267.
[184] Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 42: AAS 59 (1967), 278.
[185] Cf. Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens: AAS 63 (1971), 401- 441.
[186] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens: AAS 73 (1981), 577-647.
[187] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis: AAS 80 (1988), 513-586.
[188] Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 26, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, p. 32.
[189] Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 26, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, p. 32.
[190] Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 26, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, p. 32.
[191] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 39: AAS 80 (1988), 568.
[192] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus: AAS 83 (1991), 793-867.
[193] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 10: AAS 83 (1991), 805.
[194] Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 27, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, p. 33.
[195] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 4: AAS 58 (1966), 1028.
[196] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 1: AAS 80 (1988), 514; cf. Catechism of the Catholic Church, 2422.
[197] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 22: AAS 58 (1966), 1042.
[198] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Redemptor Hominis, 14: AAS 71 (1979), 284.
[199] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1931.
[200] Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 35, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, p. 39.
[201] Pius XII, Radio Message of 24 December 1944, 5: AAS 37 (1945), 12.
[202] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 11: AAS 83 (1991), 807.
[203] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 453, 459.
[204]  Catechism of the Catholic Church, 357.
[205] Cf. Catechism of the Catholic Church, 356, 358.
[206]  Catechism of the Catholic Church, title of Chapter 1, Section 1, Part 1; cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 12: AAS 58 (1966), 1034; John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 34: AAS 87 (1995), 440.
[207] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 35: AAS 87 (1995), 440-441; Catechism of the Catholic Church, 1721.
[208] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 12: AAS 58 (1966), 1034.
[209] Cf. Catechism of the Catholic Church, 369.
[210] John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 35: AAS 87 (1995), 440.
[211] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2334.
[212] Cf. Catechism of the Catholic Church, 371.
[213] Cf. John Paul II, Letter to Families Gratissimam Sane, 6, 8, 14, 16, 19-20: AAS 86 (1994), 873-874, 876-878, 899-903, 910-919.
[214] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 50-51: AAS 58 (1966), 1070-1072.
[215] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 19: AAS 87 (1995), 421-422.
[216] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2258.
[217] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 27: AAS 58 (1966), 1047-1048; Catechism of the Catholic Church, 2259-2261.
[218] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Fides et Ratio, proem: AAS 91 (1999), 5.
[219] Cf. Catechism of the Catholic Church, 373.
[220] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 34: AAS 87 (1995), 438-440.
[221] Saint Augustine, Confessions, I, 1: PL 32, 661: ‘‘Tu excitas, ut laudare te delectet; quia fecisti nos ad te, et inquietum est cor nostrum, donec requiescat in te.’’
[222] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1850.
[223]  Catechism of the Catholic Church, 404.
[224] John Paul II, Apostolic Exhortation Reconciliatio et Paenitentia, 2: AAS 77 (1985), 188; cf. Catechism of the Catholic Church, 1849.
[225] John Paul II, Apostolic Exhortation Reconciliatio et Paenitentia, 15: AAS 77 (1985), 212 213.
[226] John Paul II, Apostolic Exhortation Reconciliatio et Paenitentia, 16: AAS 77 (1985), 214. The text explains moreover that there is a law of descent, which is a kind of communion of sin, in which a soul that lowers itself through sin drags down with it the Church and, in some way, the entire world; to this law there corresponds a law of ascent, the profound and magnificent mystery of the communion of saints, thanks to which every soul that rises above itself also raises the world.
[227] John Paul II, Apostolic Exhortation Reconciliatio et Paenitentia, 16: AAS 77 (1985), 216.
[228] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1869.
[229] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 36: AAS 80 (1988), 561-563.
[230] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 37: AAS 80 (1988), 563.
[231] John Paul II, Apostolic Exhortation Reconciliatio et Paenitentia, 10: AAS 77 (1965), 205.
[232] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 22: AAS 58 (1966), 1042.
[233] Cf. Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 26-39: AAS 63 (1971), 420-428.
[234] Pius XII, Encyclical Letter Summi Pontificatus: AAS 31 (1939), 463.
[235] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 13: AAS 83 (1991), 809.
[236] Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 27: AAS 63 (1971), 421.
[237] John Paul II, Encyclical Letter Redemptor Hominis, 14: AAS 71 (1979), 284.
[238] Cf. Fourth Lateran Ecumenical Council, Chapter 1, De Fide Catholica: DS 800, p. 259; First Vatican Ecumenical Council, Dei Filius, c. 1: De Deo rerum omnium Creatore: DS 3002, p. 587; First Vatican Ecumenical Council, canons 2, 5: DS 3022, 3025, pp. 592, 593.
[239] John Paul II, Encyclical Letter Veritatis Splendor, 48: AAS 85 (1993), 1172.
[240] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 14: AAS 58 (1966), 1035; cf. Catechism of the Catholic Church, 364.
[241] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 14: AAS 58 (1966), 1035.
[242] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 14: AAS 58 (1966), 1036; cf. Catechism of the Catholic Church, 363, 1703.
[243] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 15: AAS 58 (1966), 1036.
[244]  Catechism of the Catholic Church, 365.
[245] Saint Thomas Aquinas, Commentum in tertium librum Sententiarum, d. 27, q. 1, a. 4: ‘‘Ex utraque autem parte res immateriales infinitatem habent quodammodo, quia sunt quodammodo omnia, sive inquantum essentia rei immaterialis est exemplar et similitudo omnium, sicut in Deo accidit, sive quia habet similitudinem omnium vel actu vel potentia, sicut accidit in Angelis et animabus’’; cf. Saint Thomas Aquinas, Summa Theologiae, I, q. 75, a. 5: Ed. Leon. 5, 201-203.
[246] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 26: AAS 58 (1966), 1046-1047.
[247] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 27: AAS 58 (1966), 1047.
[248] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2235.
[249] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 24: AAS 58 (1966), 1045; Catechism of the Catholic Church, 27, 356 and 358.
[250]  Catechism of the Catholic Church, 1706.
[251] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1705.
[252] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 17: AAS 58 (1966), 1037; cf. Catechism of the Catholic Church, 1730-1732.
[253] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Veritatis Splendor, 34: AAS 85 (1993), 1160-1161; Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 17: AAS 58 (1966), 1038.
[254] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1733.
[255] Cf. Gregory of Nyssa, De Vita Moysis, II, 2-3: PG 44, 327B-328B: ‘‘unde fit, ut nos ipsi patres quodammodo simus nostri... vitii ac virtutis ratione fingentes.’’
[256] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 13: AAS 83 (1991), 809-810.
[257] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1706.
[258] John Paul II, Encyclical Letter Veritatis Splendor, 35: AAS 85 (1993), 1161-1162.
[259]  Catechism of the Catholic Church, 1740.
[260] Congregation for the Doctrine of the Faith, Instruction Libertatis Conscientia, 75: AAS 79 (1987), 587.
[261] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1749-1756.
[262] John Paul II, Encyclical Letter Veritatis Splendor, 86: AAS 85 (1993), 1201.
[263] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Veritatis Splendor, 44, 99: AAS 85 (1993), 1168-1169, 1210-1211.
[264] John Paul II, Encyclical Letter Veritatis Splendor, 61: AAS 85 (1993), 1181-1182.
[265] Cf. Encyclical Letter Veritatis Splendor, 50: AAS 85 (1993), 1173-1174.
[266] Saint Thomas Aquinas, In Duo Praecepta Caritatis et in Decem Legis Praecepta Expositio, c. 1: ‘‘Nunc autem de scientia operandorum intendimus: ad quam tractandan quadruplex lex invenitur. Prima dicitur lex naturae; et haec nihil aliud est nisi lumen intellectus insitum nobis a Deo, per quod cognoscimus quid agendum et quid vitandum. Hoc lumen et hanc legem dedit Deus homini in creatione’’: Divi Thomae Aquinatis, Doctoris Angelici, Opuscola Theologica, vol. II: De re spirituali, cura et studio P. Fr. Raymundi Spiazzi, O.P., Marietti ed., Taurini - Romae 1954, p. 245.
[267] Cf. Saint Thomas Aquinas, Summa Theologiae, I-II, q. 91, a. 2, c: Ed. Leon. 7, 154: ‘‘partecipatio legis aeternae in rationali creatura lex naturalis dicitur.’’
[268] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1955.
[269] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1956
[270] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1957.
[271]  Catechism of the Catholic Church, 1958.
[272] First Vatican Ecumenical Council, Dei Filius, c. 2: DS 3005, p. 588; cf. Pius XII, Encyclical Letter Humani Generis: AAS 42 (1950), 562.
[273] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1960.
[274] Cf. Saint Augustine, Confessions, 2, 4, 9: PL 32, 678: ‘‘Furtum certe punit lex tua, Domine, et lex scripta in cordibus hominum, quam ne ipsa quidem delet iniquitas.’’
[275] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1959.
[276] John Paul II, Encyclical Letter Veritatis Splendor, 51: AAS 85 (1993), 1175.
[277] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 19-20: AAS 87 (1995), 421-424.
[278] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 13: AAS 58 (1966), 1034-1035.
[279] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1741.
[280] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Veritatis Splendor, 87: AAS 85 (1993), 1202-1203.
[281] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1934.
[282] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 29: AAS 58 (1966), 1048-1049.
[283] Cf. Paul VI, Encyclical Letter Octogesima Adveniens, 16: AAS 63 (1971), 413.
[284] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris, 47-48: AAS 55 (1963), 279-281; Paul VI, Address to the General Assembly of the United Nations (4 October 1965), 5: AAS 57 (1965), 881; John Paul II, Address to the Fiftieth General Assembly of the United Nations (5 October 1995), 13: L’Osservatore Romano, English edition, 11 October 1995, p. 9-10.
[285] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 84: AAS 58 (1966), 1107-1108.
[286] Cf. Paul VI, Address to the General Assembly of the United Nations, 5: AAS 57 (1965), 881; Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 43-44: AAS 59 (1967), 278-279.
[287] John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Christifideles Laici, 50: AAS 81 (1989), 489.
[288] John Paul II, Apostolic Letter Mulieris Dignitatem, 11: AAS 80 (1988), 1678.
[289] John Paul II, Letter to Women, 8: AAS 87 (1995), 808.
[290] John Paul II, Sunday Angelus (9 July 1995): L’Osservatore Romano, English edition, 12 July 1995, p. 1; cf. Congregation for the Doctrine of the Faith, Letter to the Bishops of the Catholic Church on the Collaboration of Men and Women in the Church and in the World: L’Osservatore Romano, English edition, 11/18 August 2004, pp. 5-8.
[291] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 22: AAS 73 (1981), 634.
[292] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 22: AAS 73 (1981), 634.
[293] John Paul II, Message for the International Symposium on the Dignity and Rights of the Mentally Disabled Person, 5 January 2004, 5: L’Osservatore Romano, English edition, 21 January 2004, p. 6.
[294] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 12: AAS 58 (1966), 1034; Catechism of the Catholic Church, 1879.
[295] Cf. Pius XII, Radio Message of 24 December 1942, 6: AAS 35 (1943), 11-12; John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 264-265.
[296]  Catechism of the Catholic Church, 1880.
[297] The natural social disposition of men and women also makes it evident that the origin of society is not found in a ‘‘contract’’ or ‘‘agreement,’’ but in human nature itself; and from this arises the possibility of freely creating different agreements of association. It must not be forgotten that the ideologies of the social contract are based on a false anthropology; consequently, their results cannot be – and in fact they have not been – profitable for society or for people. The Magisterium has declared such opinions as openly absurd and entirely disastrous: cf. Leo XIII, Encyclical Letter Libertas Praestantissimum: Acta Leonis XIII, 8 (1889), 226-227.
[298] Congregation for the Doctrine of the Faith, Instruction Libertatis Conscientia, 32: AAS 79 (1987), 567.
[299] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 25: AAS 58 (1966), 1045-1046.
[300] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 26: AAS 80 (1988), 544-547; Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 76: AAS 58 (1966), 1099-1100.
[301]  Catechism of the Catholic Church, 1882.
[302] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Declaration Dignitatis Humanae, 1: AAS 58 (1966), 929-930.
[303] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 41: AAS 58 (1966), 1059-1060; Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 32, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, pp. 36-37.
[304] John Paul II, Address to the 34th General Assembly of the United Nations (2 October 1979), 7: AAS 71 (1979), 1147-1148; for John Paul II, this Declaration ‘‘remains one of the highest expressions of the human conscience of our time’’: Address to the Fiftieth General Assembly of the United Nations (5 October 1995), 2: L’Osservatore Romano, English edition, 11 October 1995, p. 8.
[305] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 27: AAS 58 (1966), 1047-1048; Catechism of the Catholic Church, 1930.
[306] Cf. John XIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 259; Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 22: AAS 58 (1966), 1079.
[307] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 278-279.
[308] John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 259.
[309] John Paul II, Message for the 1999 World Day of Peace, 3: AAS 91 (1999), 379.
[310] Paul VI, Message to the International Conference on Human Rights, Teheran (15 April 1968): L’Osservatore Romano, English edition, 2 May 1968, p. 4.
[311] John Paul II, Message for the 1999 World Day of Peace, 3: AAS 91 (1999), 379.
[312] John Paul II, Message for the 1999 World Day of Peace, 3: AAS 91 (1999), 379.
[313] John Paul II, Message for the 1998 World Day of Peace, 2: AAS 90 (1998), 149.
[314] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 259-264.
[315] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 26: AAS 58 (1966), 1046-1047.
[316] Cf. Paul VI, Address to the General Assembly of the United Nations (4 October 1965), 6: AAS 57 (1965), 883- 884; Paul VI, Message to the Bishops Gathered for the Synod (26 October 1974): AAS 66 (1974), 631-639.
[317] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 47: AAS 83 (1991), 851-852; cf. also Address to the 34th General Assembly of the United Nations (2 October 1979), 13: AAS 71 (1979) 1152-1153.
[318] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 2: AAS 87 (1995), 402.
[319] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 27: AAS 58 (1966), 1047-1048; John Paul II, Encyclical Letter Veritatis Splendor, 80: AAS 85 (1993), 1197-1198; John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 7-28: AAS 87 (1995), 408- 433.
[320] Second Vatican Ecumenical Council, Declaration Dignitatis Humanae, 2: AAS 58 (1966), 930-931.
[321] John Paul II, Encyclical Letter Redemptor Hominis, 17: AAS 71 (1979), 300.
[322] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 259-264; Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 26: AAS 58 (1966), 1046-1047.
[323] John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 264.
[324] John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 264.
[325] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 33: AAS 80 (1988), 557-559; John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 21: AAS 83 (1991), 818-819.
[326] John Paul II, Letter on the occasion of the fiftieth anniversary of the outbreak of the Second World War, 8: L’Osservatore Romano, English edition, 4 September 1989, p. 2.
[327] John Paul II, Letter on the occasion of the fiftieth anniversary of the outbreak of the Second World War, 8: L’Osservatore Romano, English edition, 4 September 1989, p. 2.
[328] Cf. John Paul II, Address to the Diplomatic Corps (9 January 1988), 7-8: L’Osservatore Romano, English edition, 25 January 1988, p. 7.
[329] John Paul II, Address to the Fiftieth General Assembly of the United Nations (5 October 1995), 8: L’Osservatore Romano, English edition, 11 October 1995, p. 9.
[330] John Paul II, Address to the Fiftieth General Assembly of the United Nations (5 October 1995), 8: L’Osservatore Romano, English edition, 11 October 1995, p. 9.
[331] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 47: AAS 83 (1991), 852.
[332] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Redemptor Hominis, 17: AAS 71 (1979), 295-300.
[333] Paul VI, Encyclical Letter Octogesima Adveniens, 23: AAS 63 (1971), 418.
[334] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 54: AAS 83 (1991), 859-860.
[335] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 41: AAS 58 (1966), 1060.
[336] Cf. John Paul II, Address to Officials and Advocates of the Tribunal of the Roman Rota (17 February 1979), 4: Insegnamenti di Giovanni Paolo II, II, 1 (1979), 413-414.
[337] Cf. Code of Canon Law, canons 208-223.
[338] Cf. Pontifical Commission ‘‘Iustitia et Pax,’’ The Church and Human Rights, 70-90, Vatican City 1975, pp. 45-54.
[339] John Paul II, Encyclical Letter Sollecitudo Rei Socialis, 41: AAS 80 (1988), 572.
[340] Paul VI, Motu Proprio Iustitiam et Pacem (10 December 1976): L’Osservatore Romano, 23 December 1976, p. 10.
[341] Cf. Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 29-42, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, pp. 35-43.
[342] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 453.
[343] Congregation for the Doctrine of the Faith, Instruction Libertatis Conscientia, 72: AAS 79 (1987), 585.
[344] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 1 AAS 80 (1988), 513-514.
[345] Cf. Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 47, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, p. 47.
[346] Second Vatican Ecumenical Council, Gaudium et Spes, 26: AAS 58 (1966), 1046; cf. Catechism of the Catholic Church, 1905-1912; John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 417-421; John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 272-273; Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 46: AAS 63 (1971), 433-435.
[347] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1912.
[348] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 272.
[349] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1907.
[350] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 26: AAS 58 (1966), 1046-1047.
[351] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 421.
[352] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 417; Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 46: AAS 63 (1971), 433-435; Catechism of the Catholic Church, 1913.
[353] Saint Thomas Aquinas places ‘‘knowledge of the truth about God’’ and ‘‘life in society’’ at the highest and most specific level of man’s ‘‘ inclinationes naturales’’ ( Summa Theologiae, I-II, q. 94, a. 2: Ed. Leon. 7, 170: ‘‘Secundum igitur ordinem inclinationum naturalium est ordo praeceptorum legis naturae ... Tertio modo inest homini inclinatio ad bonum secundum naturam rationis, quae est sibi propria; sicut homo habet naturalem inclinationem ad hoc quod veritatem cognoscat de Deo, et ad hoc quod in societate vivat’’).
[354] Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 197.
[355] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1910.
[356] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 74: AAS 58 (1966), 1095-1097; John Paul II, Encyclical Letter Redemptor Hominis, 17: AAS 71 (1979), 295-300.
[357] Cf. Leo XIII, Encyclical Letter Rerum Novarum: Acta Leonis XIII, 11 (1892), 133-135; Pius XII, Radio Message for the fiftieth anniversary of Rerum Novarum: AAS 33 (1941), 200.
[358] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1908.
[359] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 41: AAS 83 (1991), 843-845.
[360] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 69: AAS 58 (1966), 1090.
[361] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 31: AAS 83 (1991), 831.
[362] Cf. Pius XII, Radio Message for the fiftieth anniversary of Rerum Novarum: AAS 33 (1941), 199-200.
[363] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 19: AAS 73 (1981), 525.
[364] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 42: AAS 80 (1988), 573.
[365] Pius XII, Radio Message for the fiftieth anniversary of Rerum Novarum: AAS 33 (1941), 199.
[366] Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 22: AAS 59 (1967), 268.
[367] Congregation for the Doctrine of the Faith, Libertatis Conscientia, 90: AAS 79 (1987), 594.
[368] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 31: AAS 83 (1991), 832.
[369] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 71: AAS 58 (1966), 1092-1093; cf. Leo XIII, Encyclical Letter Rerum Novarum: Acta Leonis XIII, 11 (1892), 103-104; Pius XII, Radio Message for the fiftieth anniversary of Rerum Novarum: AAS 33 (1941), 199; Pius XII, Radio Message of 24 December 1942: AAS 35 (1943), 17; Pius XII, Radio Message of 1 September 1944: AAS 36 (1944), 253; John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 428-429.
[370] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 6: AAS 83 (1991), 800-801.
[371] Leo XIII, Encyclical Letter Rerum Novarum: Acta Leonis XIII, 11 (1892), 102.
[372] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 14: AAS 73 (1981), 613.
[373] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 69: AAS 58 (1966), 1090-1092; Catechism of the Catholic Church, 2402-2406.
[374] Cf. Leo XIII, Encyclical Letter Rerum Novarum: Acta Leonis XIII, 11 (1892), 102.
[375] Cf. Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 22-23: AAS 59 (1967), 268-269.
[376] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 430- 431; John Paul II, Address to the Third General Conference of Latin American Bishops, Puebla, Mexico (28 January 1979), III/4: AAS 71 (1979), 199-201.
[377] Cf. Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 191-192, 193-194, 196-197.
[378] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 69: AAS 58 (1966), 1090.
[379] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 32: AAS 83 (1991), 832.
[380] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 35: AAS 83 (1991), 837.
[381] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 69: AAS 58 (1966), 1090-1092.
[382] Cf. Pontifical Council for Justice and Peace, Towards a Better Distribution of Land. The Challenge of Agrarian Reform (23 November 1997), 27-31: Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 1997, pp. 28-31.
[383] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 27-34, 37: AAS 80 (1988), 547-560, 563-564; John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 41: AAS 83 (1991), 843-845.
[384] Cf. John Paul II, Address to the Third General Conference of Latin American Bishops, Puebla, Mexico (28 January 1979), I/8: AAS 71 (1979), 194-195.
[385] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 42: AAS 80 (1988), 572-573; cf. John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 32: AAS 87 (1995), 436-437; John Paul II, Apostolic Letter Tertio Millennio Adveniente, 51: AAS 87 (1995), 36; John Paul II, Apostolic Letter Novo Millennio Ineunte, 49-50: AAS 93 (2001), 302-303.
[386] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2448.
[387]  Catechism of the Catholic Church, 2443.
[388]  Catechism of the Catholic Church, 1033.
[389] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2444.
[390]  Catechism of the Catholic Church, 2448.
[391]  Catechism of the Catholic Church, 2447.
[392] Saint Gregory the Great, Regula Pastoralis, 3, 21: PL 77, 87: ‘‘Nam cum qualibet necessaria indigentibus ministramus, sua illis reddimus, non nostra largimur; iustitiae potius debitum soluimus, quam misericordiae opera implemus.’’
[393] Second Vatican Ecumenical Council, Decree Apostolicam Actuositatem, 8: AAS 58 (1966), 845; cf. Catechism of the Catholic Church, 2446.
[394]  Catechism of the Catholic Church, 2445.
[395] Cf. Leo XIII, Encyclical Letter Rerum Novarum: Acta Leonis XIII, 11 (1892), 101-102, 123.
[396] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1882.
[397] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 15: AAS 80 (1988), 529; cf. Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 203; John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 439; Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 65: AAS 58 (1966), 1086-1087; Congregation for the Doctrine of the Faith, Instruction Libertatis Conscientia, 73, 85-86: AAS 79 (1987), 586, 592-593; John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 48: AAS 83 (1991), 852-854; Catechism of the Catholic Church, 1883-1885.
[398] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 49: AAS 83 (1991), 854-856; John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 15: AAS 80 (1988), 528-530.
[399] Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 203; cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 48: AAS 83 (1991), 852-854; Catechism of the Catholic Church, 1883.
[400] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 48: AAS 83 (1991), 854.
[401] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 48: AAS 83 (1991), 852-854.
[402] Cf. Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 22, 46: AAS 63 (1971), 417, 433-435; Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 40, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, pp. 41-42.
[403] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 75: AAS 58 (1966), 1097-1099.
[404] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1913-1917.
[405] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 423- 425; John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 14: AAS 73 (1981), 612-616; John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 35: AAS 83 (1991), 836-838.
[406] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 44-45: AAS 80 (1988), 575-578.
[407] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 278.
[408] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 46: AAS 83 (1991), 850-851.
[409] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1917.
[410] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 30-31: AAS 58 (1966), 1049-1050; John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 47: AAS 83 (1991), 851-852.
[411] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 44-45: AAS 83 (1991), 848-849.
[412] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 15: AAS 80 (1988), 528-530; Pius XII, Christmas Radio Message of 24 December 1952: AAS 45 (1953), 37; Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 47: AAS 63 (1971), 435-437.
[413] There can be associated to the concept of interdependence the classical theme of socialization, repeatedly examined by the Church’s social doctrine; cf. John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 415-417; Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 42: AAS 58 (1966), 1060-1061; John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 14-15: AAS 73 (1981), 612-618.
[414] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 11-22: AAS 80 (1988), 525-540.
[415] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1939-1941.
[416] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1942.
[417] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 36, 37: AAS 80 (1988), 561-564; cf. John Paul II, Apostolic Exhortation Reconciliatio et Paenitentia, 16: AAS 77 (1985), 213-217.
[418] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 38: AAS 80 (1988), 565-566.
[419] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 38: AAS 80 (1988), 566; cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 8: AAS 73 (1981), 594-598; John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 57: AAS 83 (1991), 862-863.
[420] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 17, 39, 45: AAS 80 (1988), 532-533, 566-568, 577-578. International solidarity too is required by the moral order; peace in the world depends in large part on this: cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 83-86: AAS 58 (1966), 1107-1110; Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 48: AAS 59 (1967), 281; Pontifical Commission ‘‘Iustitia et Pax,’’ At the Service of the Human Community: an Ethical Approach to the International Debt Question (27 December 1986), I, 1, Vatican Polyglot Press, Vatican City 1986, p. 11; Catechism of the Catholic Church, 1941, 2438.
[421] Solidarity, though not yet with that explicit name, is one of the basic principles of Rerum Novarum (cf. John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 [1961], 407). ‘‘What we nowadays call the principle of solidarity ... is frequently stated by Pope Leo XIII, who uses the term ‘friendship,’ a concept already found in Greek philosophy. Pope Pius XI refers to it with the equally meaningful term ‘social charity’. Pope Paul VI, expanding the concept to cover the many modern aspects of the social question, speaks of a ‘civilization of love’” (John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 10: AAS 83 [1991], 805). Solidarity is one of the basic principles of the entire social teaching of the Church (cf. Congregation for the Doctrine of the Faith, Instruction Libertatis Conscientia, 73: AAS 79 [1987], 586). Starting with Pius XII (cf. Encyclical Letter Summi Pontificatus: AAS 31 [1939], 426-427), the term solidarity is used ever more frequently and with ever broader meaning: from that of ‘‘law’’ in the same encyclical to that of ‘‘principle’’ (cf. John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 [1961], 407), that of ‘‘duty’’ (cf. Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 17, 48: AAS 59 [1967], 265-266, 281) and that of ‘‘value’’ (cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 38: AAS 80 [1988], 564-566), and finally that of ‘‘virtue’’ (cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 38, 40: AAS 80 [1988], 564-566, 568-569).
[422] Cf. Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 38, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, pp. 40-41.
[423] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 32: AAS 58 (1966), 1051.
[424] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 40: AAS 80 (1988), 568: ‘‘ Solidarity is undoubtedly a Christian virtue. In what has been said so far it has been possible to identify many points of contact between solidarity and charity, which is the distinguishing mark of Christ’s disciples (cf. Jn 13:35).’’
[425] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 40: AAS 80 (1988), 569.
[426] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1886.
[427] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 26: AAS 58 (1966), 1046-1047; John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 265-266.
[428] Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 43, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, p. 44.
[429] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 36: AAS 58 (1966), 1053-1054.
[430] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 1: AAS 58 (1966), 1025-1026; Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 13: AAS 59 (1967), 263-264.
[431] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2467.
[432] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 265-266, 281.
[433] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 61: AAS 58 (1966), 1081-1082; Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 35, 40: AAS 59 (1967), 274-275, 277; John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 44: AAS 80 (1988), 575-577. For social reform, ‘‘the primary task, which will affect the success of all the others, belongs to the order of education’’: Congregation for the Doctrine of the Faith, Instruction Libertatis Conscientia, 99: AAS 79 (1987), 599.
[434] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 16: AAS 58 (1966), 1037; Catechism of the Catholic Church, 2464-2487.
[435] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 17: AAS 58 (1966), 1037-1038; Catechism of the Catholic Church, 1705, 1730; Congregation for the Doctrine of the Faith, Instruction Libertatis Conscientia, 28: AAS 79 (1987), 565.
[436]  Catechism of the Catholic Church, 1738.
[437] Cf. Congregation for the Doctrine of the Faith, Instruction Libertatis Conscientia, 26: AAS 79 (1987), 564-565.
[438] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 42: AAS 83 (1991), 846. This statement is made in the context of economic initiative, but it appears correct to apply it also to other areas of personal activity.
[439] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 17: AAS 83 (1991), 814-815.
[440] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 289-290.
[441] Cf. Saint Thomas, Summa Theologiae, I-II, q. 6: Ed. Leon. 6, 55-63.
[442]  Catechism of the Catholic Church, 1807; cf. Saint Thomas Aquinas, Summa Theologiae, II-II, q. 58, a. 1: Ed. Leon. 9, 9-10: ‘‘iustitia est perpetua et constans voluntas ius suum unicuique tribuendi.’’
[443] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 282-283.
[444] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2411.
[445] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1928-1942, 2425-2449, 2832; Pius XI, Encyclical Letter Divini Redemptoris: AAS 29 (1937), 92.
[446] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 2: AAS 73 (1981),580-583.
[447] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 40: AAS 80 (1988), 568; cf. Catechism of the Catholic Church, 1929.
[448] John Paul II, Message for the 2004 World Day of Peace, 10: AAS 96 (2004), 121.
[449] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 39: AAS 80 (1988), 568.
[450] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 39: AAS 80 (1988), 568.
[451] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 265-267.
[452] John Paul II, Message for the 2004 World Day of Peace, 10: AAS 96 (2004), 120.
[453] John Paul II, Encyclical Letter Dives in Misericordia, 14: AAS 72 (1980), 1223.
[454] John Paul II, Encyclical Letter Dives in Misericordia, 12: AAS 72 (1980), 1216.
[455] John Paul II, Encyclical Letter Dives in Misericordia, 14: AAS 72 (1980), 1224; cf. Catechism of the Catholic Church, 2212.
[456] Saint Thomas Aquinas, Summa Theologiae, II-II, q. 23, a. 8: Ed. Leon. 8, 72; cf. Catechism of the Catholic Church, 1827.
[457] Paul VI, Address to the Food and Agriculture Association on the twenty-fifth anniversary of its foundation (16 November 1970): Insegnamenti di Paolo VI, vol. VIII, p. 1153.
[458] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 12: AAS 58 (1966), 1034.
[459] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1605.
[460] John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Christifideles Laici, 40: AAS 81 (1989), 469.
[461] The Holy Family is an example of family life: ‘‘May Nazareth remind us what the family is, what the communion of love is, its stark and simple beauty, its sacred and inviolable character; may it help us to see how sweet and irreplaceable education in the family is; may it teach us its natural function in the social order. May we finally learn the lesson of work’’: Paul VI, Address at Nazareth (5 January 1964): AAS 56 (1964), 168.
[462] John Paul II, Letter to Families Gratissimam Sane, 17: AAS 86 (1994), 906.
[463] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 48: AAS 58 (1966), 1067-1069
[464] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Decree Apostolicam Actuositatem, 11: AAS 58 (1966), 848.
[465] John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Christifideles Laici, 40: AAS 81 (1989), 468.
[466] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 39: AAS 83 (1991), 841.
[467] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 39: AAS 83 (1991), 841.
[468] John Paul II, Letter to Families Gratissimam Sane, 7: AAS 86 (1994), 875; cf. Catechism of the Catholic Church, 2206.
[469] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 47: AAS 58 (1966), 1067; cf. Catechism of the Catholic Church, 2210.
[470] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2224.
[471] Cf. Holy See, Charter of the Rights of the Family, Preamble, D-E, Vatican Polyglot Press, Vatican City 1983, p. 6.
[472] Cf. John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 45: AAS 74 (1982), 136-137; Catechism of the Catholic Church, 2209.
[473] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 48: AAS 58 (1966), 1067-1068.
[474] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 48: AAS 58 (1966), 1067.
[475] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1603.
[476] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 48: AAS 58 (1966), 1067.
[477] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1639.
[478] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1603.
[479] Cf. John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 13: AAS 74 (1982), 93-96.
[480] John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 19: AAS 74 (1982), 102.
[481] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 48, 50: AAS 58 (1966), 1067-1069, 1070-1072.
[482] Cf. John Paul II, Letter to Families Gratissimam Sane, 11: AAS 86 (1994), 883-886.
[483] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 50: AAS 58 (1966), 1070-1072.
[484]  Catechism of the Catholic Church, 2379.
[485] Cf. John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 12: AAS 74 (1982), 93: ‘‘For this reason the central word of Revelation, ‘God loves his people,’ is likewise proclaimed through the living and concrete word whereby a man and a woman express their conjugal love. Their bond of love becomes the image and the symbol of the covenant which unites God and his people (cf. Hos 2:21; Jer 3:6-13; Is 54). And the same sin which can harm the conjugal covenant becomes an image of the infidelity of the people to their God: idolatry is prostitution (cf. Ezek 16:25), infidelity is adultery, disobedience to the law is abandonment of the spousal love of the Lord. But the infidelity of Israel does not destroy the eternal fidelity of the Lord, and therefore the ever faithful love of God is put forward as the model of the faithful love which should exist between spouses (cf. Hos 3).’’
[486] John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 13: AAS 74 (1982), 93-94.
[487] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 48: AAS 58 (1966), 1067-1069.
[488] John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 47: AAS 74 (1982), 139; the quotation in the text is taken from Second Vatican Ecumenical Council, Dogmatic Constitution Lumen Gentium, 31: AAS 57 (1965), 37.
[489] John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 48: AAS 74 (1982), 140; cf. Catechism of the Catholic Church, 1656-1657, 2204.
[490] Cf. John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 18: AAS 74 (1982), 100-101.
[491] John Paul II, Letter to Families Gratissimam Sane, 11: AAS 86 (1994), 883.
[492] John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 43: AAS 74 (1982), 134.
[493] John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 43: AAS 74 (1982), 134.
[494] John Paul II, Message to the Second World Assembly on Ageing, Madrid (3 April 2002): L’Osservatore Romano, English edition, 24 April 2002, p. 6; cf. John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 27: AAS 74 (1982), 113-114.
[495] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 48: AAS 58 (1966), 1067-1069; Catechism of the Catholic Church, 1644-1651.
[496]  Catechism of the Catholic Church, 2333.
[497]  Catechism of the Catholic Church, 2385; cf. Catechism of the Catholic Church, 1650-1651, 2384.
[498] John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 20: AAS 74 (1982), 104.
[499] The respect owed to the sacrament of Marriage, as well as to the married couples themselves, their families and the faith community, forbids pastors regardless of motivation and pretext - even pastoral - from setting up any kind of ceremony for the divorced who wish to remarry. Cf. John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 20: AAS 74 (1982), 104.
[500] Cf. John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 77, 84: AAS 74 (1982), 175-178, 184-186.
[501] Cf. John Paul II, Letter to Families Gratissimam Sane, 14: AAS 86 (1994), 893-896; Catechism of the Catholic Church, 2390.
[502] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2390.
[503] Cf. Congregation for the Doctrine of the Faith, Letter on the Pastoral Care of Homosexual Persons (1 October 1986), 1-2: AAS 79 (1987), 543-544.
[504] John Paul II, Address to the Tribunal of the Roman Rota (21 January 1999), 5: L’Osservatore Romano, English edition, 10 February 1999, p. 3.
[505] Cf. Congregation for the Doctrine of the Faith, Document on Some Considerations Concerning the Response to Legislative Proposals on the Non-Discrimination of Homosexual Persons (23 July 1992): L’Osservatore Romano, 24 July 1992, p. 4; cf. Congregation for the Doctrine of the Faith, Declaration Persona Humana (29 December 1975), 8: AAS 68 (1976), 84-85.
[506] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2357-2359.
[507] Cf. John Paul II, Address to Spanish Bishops on their Ad Limina Visit (19 February 1998), 4: L’Osservatore Romano, English edition, 11 March 1998, p. 5; Pontifical Council for the Family, Family, Marriage and ‘‘De facto Unions’’ (26 July 2000), 23, Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2000, pp. 40-43; Congregation for the Doctrine of the Faith, Considerations Regarding Proposals to Give Legal Recognition to Unions Between Homosexual Persons (3 June 2003), Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2003.
[508] Congregation for the Doctrine of the Faith, Considerations Regarding Proposals to Give Legal Recognition to Unions Between Homosexual Persons (3 June 2003), 8, Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2003, p. 9.
[509] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 71: AAS 87 (1995), 483; Saint Thomas Aquinas, Summa Theologiae, I-II, q. 96, a. 2 (“Utrum ad legem humanam pertineat omnia vitia cohibere”): Ed. Leon. 7, 181.
[510] John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 81: AAS 74 (1982), 183.
[511] Holy See, Charter of the Rights of the Family (24 November 1983), Preamble, E, Vatican Polyglot Press, Vatican City 1983, p. 6.
[512] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1652.
[513] John Paul II, Letter to Families Gratissimam Sane, 6: AAS 86 (1994), 874; cf. Catechism of the Catholic Church, 2366.
[514] John Paul II, Letter to Families Gratissimam Sane, 11: AAS 86 (1994), 884.
[515] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 39: AAS 83 (1991), 842.
[516] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 92: AAS 87 (1995), 505-507.
[517] John Paul II, Letter to Families Gratissimam Sane, 13: AAS 86 (1994), 891.
[518] John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 93: AAS 87 (1995), 507-508.
[519] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 50: AAS 58 (1966), 1070-1072; Catechism of the Catholic Church, 2367.
[520] Paul VI, Encyclical Letter Humanae Vitae, 10: AAS 60 (1968), 487; cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 50: AAS 58 (1966), 1070-1072.
[521] Cf. Paul VI, Encyclical Letter Humanae Vitae, 14: AAS 60 (1968), 490-491.
[522] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 51: AAS 58 (1966), 1072-1073; Catechism of the Catholic Church, 2271-2272; John Paul II, Letter to Families Gratissimam Sane, 21: AAS 86 (1994), 919-920; John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 58, 59, 61-62: AAS 87 (1995), 466-468, 470-472.
[523] Cf. John Paul II, Letter to Families Gratissimam Sane, 21: AAS 86 (1994), 919-920; John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 72, 101: AAS 87 (1995), 484-485, 516- 518; Catechism of the Catholic Church, 2273.
[524] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 51: AAS 58 (1966), 1072-1073; Paul VI, Encyclical Letter Humanae Vitae, 14: AAS 60 (1968), 490-491; John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 32: AAS 74 (1982), 118-120; Catechism of the Catholic Church, 2370; Pius XI, Encyclical Letter Casti Connubii (31 December 1930): AAS 22 (1930), 559-561.
[525] Cf. Paul VI, Encyclical Letter Humanae Vitae, 7: AAS 60 (1968), 485; John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 32: AAS 74 (1982), 118-120.
[526] Cf. Paul VI, Encyclical Letter Humanae Vitae, 17: AAS 60 (1968), 493-494.
[527] Cf. Paul VI, Encyclical Letter Humanae Vitae, 16: AAS 60 (1968), 491-492; John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 32: AAS 74 (1982), 118-120; Catechism of the Catholic Church, 2370.
[528] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 50: AAS 58 (1966), 1070-1072; Catechism of the Catholic Church, 2368; Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 37: AAS 59 (1967), 275-276.
[529] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2372.
[530] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2378.
[531] Cf. Congregation for the Doctrine of the Faith, Instruction Donum Vitae (22 February 1987), II, 2, 3, 5: AAS 80 (1988), 88-89, 92-94; Catechism of the Catholic Church, 2376-2377.
[532] Cf. Congregation for the Doctrine of the Faith, Instruction Donum Vitae (22 February 1987), II, 7: AAS 80 (1988), 95-96.
[533] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2375.
[534] Cf. John Paul II, Address to the Pontifical Academy for Life (21 February 2004), 2: L’Osservatore Romano, English edition, 3 March 2004, p. 7.
[535] Cf. Pontifical Academy for Life, Reflections on Cloning: Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 1997; Pontifical Council for Justice and Peace, The Church and Racism. Contribution of the Holy See to the World Conference against Racism, Racial Discrimination, Xenophobia and Related Intolerance, 21, Vatican Press, Vatican City 2001, p. 22.
[536] Cf. John Paul II, Address to the Eighteenth International Congress of the Transplantation Society (29 August 2000), 8: AAS 92 (2000), 826.
[537] John Paul II, Letter to Families Gratissimam Sane, 10: AAS 86 (1994), 881.
[538] Holy See, Charter of the Rights of the Family, art. 3 c, Vatican Polyglot Press, Vatican City 1983, p. 9. The United Nations Universal Declaration of Human Rights (10 December 1948) affirms that ‘‘the family is the natural and fundamental group unit of society and is entitled to protection by society and the State’’ (article 16,3).
[539] Holy See, Charter of the Rights of the Family, Preamble, E, Vatican Polyglot Press, Vatican City 1983, p. 6.
[540] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Declaration Gravissimum Educationis, 3: AAS 58 (1966), 731-732; Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 52: AAS 58 (1966), 1073-1074; John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 37, 43: AAS 74 (1982), 127-129; Catechism of the Catholic Church, 1653, 2228.
[541] Cf. John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 43: AAS 74 (1982), 134-135.
[542] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Declaration Gravissimum Educationis, 3: AAS 58 (1966), 731-732; Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 61: AAS 58 (1966), 1081-1082; Holy See, Charter of the Rights of the Family, art. 5, Vatican Polyglot Press, Vatican City 1983, pp. 10-11; Catechism of the Catholic Church, 2223. The Code of Canon Law devotes canons 793-799 and canon 1136 to this right and duty of parents.
[543] John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 36: AAS 74 (1982), 127.
[544] John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 36: AAS 74 (1982), 126; cf. Catechism of the Catholic Church, 2221.
[545] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Declaration Dignitatis Humanae, 5: AAS 58 (1966), 933; John Paul II, Message for the 1994 World Day of Peace, 5: AAS 86 (1994), 159-160.
[546] John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 40: AAS 74 (1982), 131.
[547] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Declaration Gravissimum Educationis, 6: AAS 58 (1966), 733-734; Catechism of the Catholic Church, 2229.
[548] Holy See, Charter of the Rights of the Family, art. 5 b, Vatican Polyglot Press, Vatican City 1983, p. 11; cf. Second Vatican Ecumenical Council, Dignitatis Humanae, 5: AAS 58 (1966), 933.
[549] Congregation for the Doctrine of the Faith, Instruction Libertatis Conscientia, 94: AAS 79 (1987), 595-596.
[550] Second Vatican Ecumenical Council, Declaration Gravissimum Educationis, 1: AAS 58 (1966), 729.
[551] Cf. John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 43: AAS 74 (1982), 134-135.
[552] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 52: AAS 58 (1966), 1073-1074.
[553] John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 37: AAS 74 (1982), 128; cf. Pontifical Council for the Family, The Truth and Meaning of Human Sexuality: Guidelines for Education within the Family (8 December 1995), Libreria Editrice Vaticana 1995.
[554] John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 26: AAS 74 (1982), 111-112.
[555] John Paul II, Address to the General Assembly of the United Nations (2 October 1979), 21: AAS 71 (1979), 1159; cf. John Paul II, Message to the Secretary-General of the United Nations on the occasion of the World Summit for Children (22 September 1990): AAS 83 (1991), 358-361.
[556] John Paul II, Address to the Committee of European Journalists for the Rights of the Child (13 January 1979): L’Osservatore Romano, English edition, 22 January 1979, p. 5.
[557] Cf. Convention on the Rights of the Child, which came into force in 1990 and which the Holy See has ratified.
[558] Cf. John Paul II, Message for the 1996 World Day of Peace, 2-6: AAS 88 (1996), 104-107.
[559] John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 44: AAS 74 (1982), 136; cf. Holy See, Charter of the Rights of the Family, art. 9, Vatican Polyglot Press, Vatican City 1983, p. 13.
[560] Holy See, Charter of the Rights of the Family, art. 8 a-b, Vatican Polyglot Press, Vatican City 1983, p. 12.
[561] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 10: AAS 73 (1981), 601.
[562] Leo XIII, Encyclical Letter Rerum Novarum: Acta Leonis XIII, 11 (1892), 104.
[563] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 10: AAS 73 (1981), 600-602.
[564] Cf. Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 200; Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 67: AAS 58 (1966), 1088-1089; John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 19: AAS 73 (1981), 625-629.
[565] Cf. Leo XIII, Encyclical Letter Rerum Novarum: Acta Leonis XIII, 11 (1892), 105; Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 193-194.
[566] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 19: AAS 73 (1981), 625- 629; Holy See, Charter of the Rights of the Family, art. 10 a, Vatican Polyglot Press, Vatican City 1983, p. 14.
[567] Cf. Pius XII, Allocution to Women on the Dignity and Mission of Women (21 October 1945): AAS 37 (1945), 284-295; John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 19: AAS 73 (1981), 625-629; John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 23: AAS 74 (1982), 107-109; Holy See, Charter of the Rights of the Family, art. 10 b, Vatican Polyglot Press, Vatican City 1983, p. 14.
[568] Cf. John Paul II, Letter to Families Gratissimam Sane, 17: AAS 86 (1994), 903-906.
[569] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 19: AAS 73 (1981), 625-629; John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 23: AAS 74 (1982), 107-109.
[570] John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 45: AAS 74 (1982), 136.
[571] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2211.
[572] Cf. John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 46: AAS 74 (1982), 137-139.
[573] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 6: AAS 73 (1981), 591.
[574] John Paul II, Encyclical Letter Redemptor Hominis, 1: AAS 71 (1979), 257.
[575] John Paul II, Encyclical Letter Redemptor Hominis, 8: AAS 71 (1979), 270.
[576] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2427; John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 27: AAS 73 (1981), 644-647.
[577] Cf. Saint John Chrysostom, Homily on Acts, in Acta Apostolorum Homiliae 35,3: PG 60, 258.
[578] Cf. Saint Basil, Regulae Fusius Tractatae 42: PG 31, 1023-1027; Saint Athanasius, Life of Saint Antony, ch. 3: PG 26, 846.
[579] Cf. Saint Ambrose, De Obitu Valentiniani Consolatio, 62: PL 16, 1438.
[580] Cf. Saint Irenaeus, Adversus Haereses, 5, 32, 2: PL 7, 1210-1211.
[581] Cf. Theodoret of Cyr, On Providence, Orationes 5-7: PG 83, 625-686.
[582] John Paul II, Address during his Pastoral Visit to Pomezia, Italy (14 September 1979), 3: L’Osservatore Romano, English edition, 1 October 1979, p. 4.
[583] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 2: AAS 73 (1981), 580-583.
[584] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 1: AAS 73 (1981), 579.
[585] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 3: AAS 73 (1981), 584.
[586] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 6: AAS 73 (1981), 589-590.
[587] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 6: AAS 73 (1981), 590.
[588] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 6: AAS 73 (1981), 592; cf. Catechism of the Catholic Church, 2428.
[589] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 31: AAS 83 (1991), 832.
[590] Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 200.
[591] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 16: AAS 73 (1981), 619.
[592] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 4: AAS 73 (1981), 586.
[593] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 12: AAS 73 (1981), 606.
[594] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 12: AAS 73 (1981), 608.
[595] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 13: AAS 73 (1981), 608-612.
[596] Cf. Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 194-198.
[597] Leo XIII, Encyclical Letter Rerum Novarum: Acta Leonis XIII, 11 (1892), 109.
[598] Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 195.
[599] John Paul II, Ecyclical Letter Centesimus Annus, 32: AAS 83 (1991), 833.
[600] John Paul II, Ecyclical Letter Centesimus Annus, 43: AAS 83 (1991), 847.
[601] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 11: AAS 73 (1981), 604.
[602] Cf. John Paul II, Address to the Pontifical Academy of Social Sciences (6 March 1999), 2: L’Osservatore Romano, English edition, 17 March 1999, p. 3.
[603] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 41: AAS 83 (1991), 844.
[604] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 14: AAS 73 (1981), 616.
[605] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 9: AAS 58 (1966), 1031-1032.
[606] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 14: AAS 73 (1981), 613.
[607] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 43: AAS 83 (1991), 847.
[608] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 32 AAS 83 (1991), 832-833.
[609] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 19: AAS 73 (1981), 625- 629; John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 9: AAS 83 (1991), 804.
[610] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 67: AAS 58 (1966), 1088-1089.
[611] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2184.
[612]  Catechism of the Catholic Church, 2185.
[613]  Catechism of the Catholic Church, 2186.
[614] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2187.
[615] Cf. John Paul II, Apostolic Letter Dies Domini, 26: AAS 90 (1998), 729: ‘‘In celebrating Sunday, both the ‘first’ and the ‘eighth’ day, the Christian is led towards the goal of eternal life’’.
[616] Cf. Leo XIII, Encyclical Letter Rerum Novarum: Acta Leonis XIII, 11 (1892), 110.
[617]  Catechism of the Catholic Church, 2188.
[618]  Catechism of the Catholic Church, 2187.
[619] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 26: AAS 58 (1966), 1046-1047; John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 9, 18: AAS 73 (1981), 598-600, 622-625; John Paul II, Address to the Pontifical Academy of Social Sciences (25 April 1997), 3: L’Osservatore Romano, English edition, 14 May 1997, p. 5; John Paul II, Message for the 1999 World Day of Peace, 8: AAS 91 (1999), 382-383.
[620] Cf. Leo XIII, Encyclical Letter Rerum Novarum: Acta Leonis XIII, 11 (1892), 128.
[621] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 10: AAS 73 (1981), 600-602.
[622] Cf. Leo XIII, Encyclical Letter Rerum Novarum: Acta Leonis XIII, 11 (1892), 103; John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 14: AAS 73 (1981), 612-616; John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 31: AAS 83 (1991), 831-832.
[623] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 16: AAS 73 (1981), 618-620.
[624] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 18: AAS 73 (1981), 623.
[625] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 43: AAS 83 (1991), 848; cf. Catechism of the Catholic Church, 2433.
[626] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 17: AAS 73 (1981), 620-622.
[627] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2436.
[628] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 66: AAS 58 (1966), 1087-1088.
[629] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 12: AAS 73 (1981), 605-608.
[630] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 48: AAS 83 (1991), 853.
[631] Paul VI, Address to the International Labour Organization (10 June 1969), 21: AAS 61 (1969), 500; cf. John Paul II, Address to the International Labour Organization (15 June 1982), 13: AAS 74 (1982), 1004-1005.
[632] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 16: AAS 83 (1991), 813.
[633] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 10: AAS 73 (1981), 600.
[634] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 10: AAS 73 (1981), 600-602; John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 23: AAS 74 (1982), 107-109.
[635] Cf. Holy See, Charter of the Rights of the Family, art. 10, Vatican Polyglot Press, Vatican City 1983, pp. 13-14.
[636] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 19: AAS 73 (1981), 628.
[637] John Paul II, Letter to Women, 3: AAS 87 (1995), 804.
[638] Cf. John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 24: AAS 74 (1982), 109-110.
[639] Cf. John Paul II, Message for the 1996 World Day of Peace, 5: AAS 88 (1996), 106-107.
[640] Leo XIII, Encyclical Letter Rerum Novarum: Acta Leonis XIII, 11 (1892), 129.
[641] John Paul II, Message for the 1998 World Day of Peace, 6: AAS 90 (1998), 153.
[642] John Paul II, Message to the Secretary-General of the United Nations on the occasion of the World Summit for Children (22 September 1990): AAS 83 (1991), 360.
[643] Cf. John Paul II, Message for the 2001 World Day of Peace, 13: AAS 91 (2001), 241; Pontifical Council “Cor Unum” - Pontifical Council for the Pastoral Care of Migrants and Itinerant People, Refugees: a Challenge to Solidarity, 6: Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 1992, p. 10.
[644] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2241.
[645] Cf. Holy See, Charter of the Rights of the Family, art. 12, Vatican Polyglot Press, Vatican City 1983, p. 14; John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 77: AAS 74 (1982), 175-178.
[646] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 66: AAS 58 (1966), 1087-1088; John Paul II, Message for the 1993 World Day of Peace, 3: AAS 85 (1993), 431-433.
[647] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 21: AAS 73 (1981), 634.
[648] Cf Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 23: AAS 59 (1967), 268-269.
[649] Pontifical Council for Justice and Peace, Towards a Better Distribution of Land: The Challenge of Agrarian Reform (23 November 1997), 13: Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 1997, p. 18.
[650] Cf. Pontifical Council for Justice and Peace, Towards a Better Distribution of Land. The Challenge of Agrarian Reform (23 November 1997), 35: Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 1997, p. 33.
[651] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 19: AAS 73 (1981), 625-629.
[652] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 19: AAS 73 (1981), 625-629.
[653] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 19: AAS 73 (1981), 629.
[654] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 15: AAS 83 (1991), 812.
[655] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 18: AAS 73 (1981), 622-625.
[656] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 19: AAS 73 (1981), 625-629.
[657] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 19: AAS 73 (1981), 625-629.
[658] Cf. Leo XIII, Encyclical Letter Rerum Novarum: Acta Leonis XIII, 11 (1892), 135; Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 186; Pius XII, Encyclical Letter Sertum Laetitiae: AAS 31 (1939), 643; John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 262-263; Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 68: AAS 58 (1966), 1089-1090; John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 20: AAS 73 (1981), 629-632; John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 7: AAS 83 (1991), 801-802.
[659] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 19: AAS 73 (1981), 625-629.
[660]  Catechism of the Catholic Church, 2434; cf. Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 198-202: ‘‘The Just Wage’’ is the title of Chapter Four (nos. 65-76) of Part Two.
[661] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 67: AAS 58 (1966), 1088-1089.
[662] Leo XIII, Encyclical Letter Rerum Novarum: Acta Leonis XIII, 11 (1892), 131.
[663]  Catechism of the Catholic Church, 2435.
[664] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 68: AAS 58 (1966), 1089-1090; John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 20: AAS 73 (1981), 629-632; Catechism of the Catholic Church, 2430.
[665] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 20: AAS 73 (1981), 632.
[666]  Catechism of the Catholic Church, 2435.
[667] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 20: AAS 73 (1981), 629.
[668] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 20: AAS 73 (1981), 630.
[669] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 20: AAS 73 (1981), 630.
[670] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2430.
[671] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 68: AAS 58 (1966), 1090.
[672] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 20: AAS 73 (1981), 631.
[673] Cf. John Paul II, Address to the International Conference for Union Representatives (2 December 1996), 4: L’Osservatore Romano, English edition, 11 December 1996, p. 8.
[674] John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 8: AAS 73 (1981), 597.
[675] John Paul II, Message to the Participants in the International Symposium on Work (14 Sepember 2001), 4: L’Osservatore Romano, English edition, 17 October 2001, p. 3.
[676] Cf. John Paul II, Address to the Pontifical Academy of Social Sciences (27 April 2001), 2: AAS 93 (2001), 599.
[677] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 10: AAS 73 (1981), 600-602.
[678]  Catechism of the Catholic Church, 2427.
[679] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 35: AAS 58 (1966), 1053; Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 19: AAS 59 (1967), 266-267; John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 20: AAS 73 (1981), 629-632; John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 28: AAS 80 (1988), 548-550.
[680] Cf. John Paul II, Message to the Participants in the International Symposium on Work (14 September 2001), 5: L’Osservatore Romano, English edition, 17 October 2001, p. 3.
[681] John Paul II, Greeting after the Mass for the Jubilee of Workers (1 May 2000), 2: L’Osservatore Romano, English edition, 10 May 2000, p. 4.
[682] John Paul II, Homily at the Mass for the Jubilee of Workers (1 May 2000), 3: L’Osservatore Romano, English edition, 10 May 2000, p. 5.
[683] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 25-27: AAS 73 (1981), 638-647.
[684] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 31: AAS 80 (1988), 554-555.
[685] Cf. The Shepherd of Hermas, Liber Tertium, Allegory I: PG 2, 954.
[686] Clement of Alexandria, Homily What Rich Man Will Be Saved?, 13: PG 9, 618.
[687] Cf. Saint John Chrysostom, Homiliae XXI de Statuis ad Populum Antiochenum Habitae, 2, 6-8: PG 49, 41-46.
[688] Saint Basil the Great, Homilia in Illud Lucae, Destruam Horrea Mea, 5: PG 31, 271.
[689] Cf. Saint Basil the Great, Homilia in Illud Lucae, Destruam Horrea Mea, 5: PG 31, 271.
[690] Cf. Saint Gregory the Great, Regula Pastoralis, 3, 21: PL 77, 87. Title of § 21: “Quomodo admonendi qui aliena non appetunt, sed sua retinent; et qui sua tribuentes, aliena tamen rapiunt.”
[691] Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 190-191.
[692] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 63: AAS 58 (1966), 1084.
[693] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2426.
[694] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 40: AAS 80 (1988), 568-569.
[695] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 36: AAS 80 (1988), 561.
[696] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 65: AAS 58 (1966), 1086-1087.
[697] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 32: AAS 80 (1988), 556-557.
[698] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 41: AAS 83 (1991), 844.
[699] Cf. John Paul II, Message for the 2000 World Day of Peace, 15-16: AAS 92 (2000), 366-367.
[700] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 28: AAS 80 (1988), 548.
[701] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 42: AAS 83 (1991), 845-846.
[702]  Catechism of the Catholic Church, 2429; cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 63: AAS 58 (1966), 1084-1085: John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 48: AAS 83 (1991), 852-854; John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 15: AAS 80 (1988), 528-530; John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 17: AAS 73 (1981), 620-622; John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 413-415.
[703] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 15: AAS 80 (1988), 529; cf. Catechism of the Catholic Church, 2429.
[704] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 16: AAS 83 (1991), 813-814.
[705] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 32: AAS 83 (1991), 833.
[706] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 32: AAS 83 (1991), 833.
[707] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 43: AAS 83 (1991), 847.
[708] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 422-423.
[709] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 35 AAS 83 (1991), 837.
[710] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2424.
[711] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 35: AAS 83 (1991), 837.
[712] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 43: AAS 83 (1991), 846-848.
[713] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 38: AAS 83 (1991), 841.
[714]  Catechism of the Catholic Church, 2269.
[715]  Catechism of the Catholic Church, 2438.
[716] John Paul II, Catechesis at General Audience (4 February 2004), 3: L’Osservatore Romano, English edition, 11 February 2004, p. 11.
[717] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 17: AAS 80 (1988), 532.
[718] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 32: AAS 83 (1991), 833.
[719] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2432.
[720] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 35: AAS 83 (1991), 837.
[721] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 32: AAS 83 (1991), 832-835.
[722] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Laborem Exercens, 19: AAS 73 (1981), 625-629.
[723] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 36: AAS 83 (1991), 838.
[724] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 36: AAS 83 (1991), 840.
[725] Concerning the utilization of resources and goods, the Church’s social doctrine offers its teaching regarding the universal destination of goods and regarding private property; cf. Chapter Four, Part III of the present document.
[726] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 34: AAS 83 (1991), 835.
[727] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 40: AAS 83 (1991), 843.
[728] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 41: AAS 83 (1991), 843-845.
[729] Cf. Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 41: AAS 63 (1971), 429-430.
[730] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 34: AAS 83 (1991), 835-836.
[731] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 40: AAS 83 (1991), 843; cf. Catechism of the Catholic Church, 2425.
[732] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 39: AAS 83 (1991), 843.
[733] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 15: AAS 83 (1991), 811-813.
[734] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 48: AAS 83 (1991), 853; cf. Catechism of the Catholic Church, 2431.
[735] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 15: AAS 83 (1991), 811.
[736] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 48: AAS 83 (1991), 852-853; cf. Catechism of the Catholic Church, 2431.
[737] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 48: AAS 83 (1991), 852-854.
[738] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 48: AAS 83 (1991), 852-854.
[739] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 30: AAS 58 (1966), 1049-1050.
[740] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 433-434, 438.
[741] Cf. Pius XI, Encyclical Letter Divini Redemptoris: AAS 29 (1966), 103-104.
[742] Cf. Pius XII, Radio Message for the fiftieth anniversary of Rerum Novarum, 21: AAS 33 (1941), 202; John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 49: AAS 83 (1991), 854-856; John Paul II, Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 45: AAS 74 (1982), 136-137.
[743] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 40: AAS 83 (1991), 843.
[744] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 36: AAS 83 (1991), 839-840.
[745] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 36: AAS 83 (1991), 839.
[746] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 36: AAS 83 (1991), 839.
[747] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 36: AAS 83 (1991), 839.
[748] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 37: AAS 83 (1991), 840.
[749] Cf. John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Ecclesia in America, 20: AAS 91 (1999), 756.
[750] Cf. John Paul II, Address to members of the ‘‘Centesimus Annus - Pro Pontifice’’ Foundation (9 May 1998), 2: L’Osservatore Romano, English edition, 27 May 1998, p. 6.
[751] John Paul II, Message for the 1998 World Day of Peace, 3: AAS 90 (1998), 150.
[752] Cf. Paul VI, Populorum Progressio, 61: AAS 59 (1967), 287.
[753] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 43: AAS 80 (1988), 574-575.
[754] Paul VI, Populorum Progressio, 57: AAS 59 (1967), 285.
[755] John Paul II, Message for the 2003 World Day of Peace, 5: AAS 95 (2003), 343.
[756] Paul VI, Populorum Progressio, 59: AAS 59 (1967), 286.
[757] John Paul II, Address to the Pontifical Academy of Social Sciences (27 April 2001), 4: AAS 93 (2001), 600.
[758] John Paul II, Address to the Pontifical Academy of Social Sciences (11 April 2002), 3: L’Osservatore Romano, English edition, 24 April 2002, p. 10.
[759] Cf. John Paul II, Address to members of the Italian Christian Workers’ Associations (27 April 2002), 4: L’Osservatore Romano, English edition, 12 June 2002, p. 11.
[760] Cf. John Paul II, Address to the Pontifical Academy of Social Sciences (25 April 1997), 6: L’Osservatore Romano, English edition, 14 May 1997, p. 5.
[761] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 58: AAS 83 (1991), 864.
[762] Cf. Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 43-44: AAS 63 (1971), 431-433.
[763] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2440; Paul VI, Populorum Progressio, 78: AAS 59 (1967), 295; John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 43: AAS 80 (1988), 574-575.
[764] Paul VI, Populorum Progressio, 14: AAS 59 (1967), 264.
[765] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2437-2438.
[766] Cf. John Paul II, Message for the 2000 World Day of Peace, 13-14: AAS 92 (2000), 365 366.
[767] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 29: AAS 83 (1991), 828-829; cf. Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 40-42: AAS 59 (1967), 277-278.
[768] John Paul II, Address at General Audience (1 May 1991): L’Osservatore Romano, English edition, 6 May 1991, p. 3. Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 9: AAS 80 (1988), 520-523.
[769] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 14: AAS 80 (1988), 526-527.
[770] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 39: AAS 83 (1991), 842.
[771]  Catechism of the Catholic Church, 2441.
[772] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 36: AAS 83 (1991), 838-839.
[773]  Catechism of the Catholic Church, 1884.
[774] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 266-267, 281-291, 301-302; John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 39: AAS 80 (1988), 566-568.
[775] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 25: AAS 58 (1966), 1045-1046; Catechism of the Catholic Church, 1881; Congregation for the Doctrine of the Faith, Doctrinal Note on Some Questions Regarding the Participation of Catholics in Political Life (24 November 2002), 3: Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2002, p. 8.
[776] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 25: AAS 58 (1966), 1045.
[777] John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 258.
[778] John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 450.
[779] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 74 AAS 58 (1966), 1095-1097.
[780] Pius XII, Christmas Radio Message of 24 December 1944: AAS 37 (1945), 13.
[781] Pius XII, Christmas Radio Message of 24 December 1944: AAS 37 (1945), 13.
[782] Pius XII, Christmas Radio Message of 24 December 1944: AAS 37 (1945), 13.
[783] John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 266.
[784] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 283.
[785] John Paul II, Message for the 1989 World Day of Peace, 5: AAS 81 (1989), 98.
[786] John Paul II, Message for the 1989 World Day of Peace, 11: AAS 81 (1989), 101.
[787] John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 273; cf. Catechism of the Catholic Church, 2237; John Paul II, Message for the 2000 World Day of Peace, 6: AAS 92 (2000), 362; John Paul II, Address to the Fiftieth General Assembly of the United Nations (5 October 1995), 3: L’Osservatore Romano, English edition, 11 October 1995, p. 8.
[788] John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 274.
[789] John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 275.
[790] Cf. Saint Thomas Aquinas, Sententiae Octavi Libri Ethicorum, VIII, lect. 1: Ed. Leon. 47, 443: ‘‘Est enim naturalis amicitia inter eos qui sunt unius gentis ad invicem, inquantum communicant in moribus et convictu. Quartam rationem ponit ibi: Videtur autem et civitates continere amicitia. Et dicit quod per amicitiam videntur conservari civitates. Unde legislatores magis student ad amicitiam conservandam inter cives quam etiam ad iustitiam, quam quandoque intermittunt, puta in poenis inferendis, ne dissensio oriatur. Et hoc patet per hoc quod concordia assimulatur amicitiae, quam quidem, scilicet concordiam, legislatores maxime appetunt, contentionem autem civium maxime expellunt, quasi inimicam salutis civitatis. Et quia tota moralis philosophia videtur ordinari ad bonum civile, ut in principio dictum est, pertinet ad moralem considerare de amicitia.’’
[791] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2212-2213.
[792] Cf. Saint Thomas Aquinas, De Regno. Ad Regem Cypri, I, 10: Ed. Leon. 42, 461: ‘‘omnis autem amicitia super aliqua communione firmatur: eos enim qui conueniunt uel per nature originem uel per morum similitudinem uel per cuiuscumque communionem, uidemus amicitia coniungi... Non enim conseruatur amore, cum parua uel nulla sit amicitia subiecte multitudinis ad tyrannum, ut prehabitis patet.’’
[793] ‘‘Liberty, equality, fraternity’’ was the motto of the French Revolution. ‘‘In the final analysis, these are Christian ideas.’’ John Paul II affirmed during his first visit to France: Homily at Le Bourget (1 June 1980), 5: AAS 72 (1980), 720.
[794] Cf. Saint Thomas Aquinas, Summa Theologiae, I-II, q. 99: Ed. Leon. 7, 199- 205; Saint Thomas Aquinas, Summa Theologiae, II-II, q. 23, ad 1um: Ed. Leon. 8, 168.
[795] Paul VI, Message for the 1977 World Day of Peace: AAS 68 (1976), 709.
[796] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2212.
[797] John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 259.
[798] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 73: AAS 58 (1966), 1095.
[799] John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 269; Leo XIII, Encyclical Letter Immortale Dei, in Acta Leonis XIII, V, 1885, 120.
[800] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1898; Saint Thomas Aquinas, De Regno. Ad Regem Cypri, I, 1: Ed. Leon. 42, 450: ‘‘Si igitur naturale est homini quod in societate multorum uiuat, necesse est in omnibus esse aliquid per quod multitudo regatur. Multis enim existentibus hominibus et unoquoque id quod est sibi congruum prouidente, multitudo in diuersa dispergetur nisi etiam esset aliquid de eo quod ad bonum multitudinis pertinet curam habens, sicut et corpus hominis et cuiuslibet animalis deflueret nisi esset aliqua uis regitiua communis in corpore, quae ad bonum commune omnium membrorum intenderet. Quod considerans Salomon dixit: ‘Ubi non est gubernator, dissipabitur populus.’”
[801] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1897; John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 279.
[802] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 74: AAS 58 (1966), 1096.
[803] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 46: AAS 83 (1991), 850-851; John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 271.
[804] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 74: AAS 58 (1966), 1095-1097.
[805] John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 270; cf. Pius XII, Christmas Radio Message of 24 December 1944: AAS 37 (1945), 15; Catechism of the Catholic Church, 2235.
[806] John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 449-450.
[807] John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 450.
[808] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 269-270.
[809] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1902.
[810] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 258-259.
[811] Cf. Pius XII, Encyclical Letter Summi Pontificatus: AAS 31 (1939), 432-433.
[812] John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 71: AAS 87 (1995), 483.
[813] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 70: AAS 87 (1995), 481-483; John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 258-259, 279-280.
[814] Cf. Pius XII, Encyclical Letter Summi Pontificatus: AAS 31 (1939), 423.
[815] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 70: AAS 87 (1995), 481- 483; John Paul II, Encyclical Letter Veritatis Splendor, 97, 99: AAS 85 (1993), 1209-1211; Congregation for the Doctrine of the Faith, Doctrinal Note on Some Questions Regarding the Participation of Catholics in Political Life (24 November 2002), 5-6, Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2002, pp. 11-14.
[816] Saint Thomas Aquinas, Summa Theologiae, I-II, q. 93, a. 3, ad 2um: Ed. Leon. 7, 164: ‘‘Lex humana intantum habet rationem legis, inquantum est secundum rationem rectam: et secundum hoc manifestum est quod a lege aeterna derivatur. Inquantum vero a ratione recedit, sic dicitur lex iniqua: et sic non habet rationem legis, sed magis violentiae cuiusdam.’’
[817] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 270.
[818] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1899-1900.
[819] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 74: AAS 58 (1966), 1095-1097; Catechism of the Catholic Church, 1901.
[820] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2242.
[821] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 73: AAS 87 (1995), 486-487.
[822] John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 74: AAS 87 (1995), 488.
[823] Saint Thomas Aquinas, Summa Theologiae, II-II, q. 104, a. 6, ad 3um: Ed. Leon. 9, 392: ‘‘principibus saecularibus intantum homo oboedire tenetur, inquantum ordo iustitiae requirit.’’
[824]  Catechism of the Catholic Church, 2243.
[825] Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 31: AAS 59 (1967), 272.
[826] Congregation for the Doctrine of the Faith, Instruction Libertatis Conscientia, 79: AAS 79 (1987), 590.
[827] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2266.
[828] John Paul II, Address to the Italian Association of Judges (31 March 2000), 4: AAS 92 (2000), 633.
[829] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2266.
[830] John Paul II, Address to the International Committee of the Red Cross, Geneva (15 June 1982), 5: L’Osservatore Romano, English edition, 26 July 1982, p. 3.
[831] John Paul II, Address to the Italian Association of Judges (31 March 2000), 4: AAS 92 (2000), 633.
[832] John Paul II, Address to the Italian Association of Judges (31 March 2000), 4: AAS 92 (2000), 633.
[833] John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 27: AAS 87 (1995), 432.
[834]  Catechism of the Catholic Church, 2267.
[835]  Catechism of the Catholic Church, 2267.
[836] John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 56: AAS 87 (1995), 464; cf. also John Paul II, Message for the 2001 World Day of Peace, 19: AAS 93 (2001), 244, where recourse to the death penalty is described as “unecessary.”
[837] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 46: AAS 83 (1991), 850.
[838] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 46: AAS 83 (1991), 850.
[839] John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 70: AAS 87 (1995), 482.
[840] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 44: AAS 83 (1991), 848.
[841] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2236.
[842] Cf. John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Christifideles Laici, 42: AAS 81 (1989), 472-476.
[843] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 44: AAS 80 (1988), 575-577; John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 48: AAS 83 (1991), 852-854; John Paul II, Message for the 1999 World Day of Peace, 6: AAS 91 (1991), 381-382.
[844] John Paul II, Message for the 1998 World Day of Peace, 5: AAS 90 (1998), 152.
[845] John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Christifideles Laici, 41: AAS 81 (1989), 471-472.
[846] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 75: AAS 58 (1966), 1097-1099.
[847] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 260.
[848] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Decree Inter Mirifica, 3: AAS 56 (1964), 146; Paul VI, Apostolic Exhortation Evangelii Nuntiandi, 45: AAS 68 (1976), 35-36; John Paul II, Encyclical Letter Redemptoris Missio, 37: AAS 83 (1991), 282-286; Pontifical Council for Social Communications, Communio et Progressio. 126-134: AAS 63 (1971), 638-640; Pontifical Council for Social Communications, Aetatis Novae, 11: AAS 84 (1992), 455-456; Pontifical Council for Social Communications, Ethics in Advertising (22 February 1997), 4-8: L’Osservatore Romano, English edition, 16 April 1997, pp. I-II.
[849]  Catechism of the Catholic Church, 2494; cf. Second Vatican Ecumenical Council, Decree Inter Mirifica, 11: AAS 56 (1964), 148-149.
[850] Pontifical Council for Social Communications, Ethics in Communications (4 June 2000), 20, Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2000, p. 22.
[851] Cf. Pontifical Council for Social Communications, Ethics in Communications (4 June 2000), 22, Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2000, pp. 23-25.
[852] Cf. Pontifical Council for Social Communications, Ethics in Communications (4 June 2000), 24, Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2000, pp. 26-28.
[853] Leo XIII, Encyclical Letter Rerum Novarum: Acta Leonis XIII, 11 (1892), 134.
[854] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1910.
[855] Cf. Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 203; Catechism of the Catholic Church, 1883-1885.
[856] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 49: AAS 83 (1991), 855.
[857] Second Vatican Ecumenical Council, Declaration Dignitatis Humanae, 1: AAS 58 (1966), 929.
[858] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Declaration Dignitatis Humanae, 2: AAS 58 (1966), 930-931; Catechism of the Catholic Church, 2106.
[859] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Declaration Dignitatis Humanae, 3: AAS 58 (1966), 931-932.
[860] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2108.
[861]  Catechism of the Catholic Church, 2105.
[862] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Declaration Dignitatis Humanae, 2: AAS 58 (1966), 930-931; Catechism of the Catholic Church, 2108.
[863] Second Vatican Ecumenical Council, Declaration Dignitatis Humanae, 7: AAS 58 (1966), 935; Catechism of the Catholic Church, 2109.
[864] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Declaration Dignitatis Humanae, 6: AAS 58 (1966), 933-934; Catechism of the Catholic Church, 2107.
[865] Cf. John Paul II, Message for the 1999 World Day of Peace, 5: AAS 91 (1999), 380-381.
[866] John Paul II, Apostolic Exhortation Catechesi Tradendae, 14: AAS 71 (1979), 1289.
[867] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 76: AAS 58 (1966), 1099; cf. Catechism of the Catholic Church, 2245.
[868] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 47: AAS 83 (1991), 852.
[869] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 76: AAS 58 (1966), 1099.
[870] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 1: AAS 58 (1966), 1026.
[871] Cf. Code of Canon Law, canon 747, § 2; Catechism of the Catholic Church, 2246.
[872] Cf. John Paul II, Letter to the Heads of State Signing the Final Helsinki Act (1 September 1980), 4: AAS 72 (1980), 1256-1258.
[873] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Dogmatic Constitution Lumen Gentium, 1: AAS 57 (1965), 5.
[874] Cf. Pius XII, Address to Catholic Jurists on the Communities of States and Peoples (6 December 1953), 2: AAS 45 (1953), 795.
[875] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 42: AAS 58 (1966), 1060-1061.
[876] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 40: AAS 80 (1988), 569.
[877] Cf. John Paul II, Address to the Fiftieth General Assembly of the United Nations (5 October 1995), 12: L’Osservatore Romano, English edition, 11 October 1995, p. 9.
[878] John XXIII, Encylical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 296.
[879] John XXIII, Encylical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 292.
[880] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1911.
[881] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Declaration Nostra Aetate, 5: AAS 58 (1966), 743-744; John XXIII. Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 268, 281: Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 63: AAS 59 (1967), 288; Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 16: AAS 63 (1971), 413; Pontifical Council for Justice and Peace, The Church and Racism. Contribution of the Holy See to the World Conference against Racism, Racial Discrimination, Xenophobia and Related Intolerance, Vatican Press, Vatican City 2001.
[882] Cf. John XXIII, Encylical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 279-280.
[883] Cf. Paul VI, Address to the United Nations (4 October 1965), 2: AAS 57 (1965), 879-880.
[884] Cf. Pius XII, Encyclical Letter Summi Pontificatus, 29: AAS 31 (1939) 438-439.
[885] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 292; John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 52: AAS 83 (1991), 857-858.
[886] Cf. John XXIII, Encyclical Letter in Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 284.
[887] Cf. Pius XII, Christmas Radio Message on a Just International Peace (24 December 1939) 5: AAS 32 (1940) 9-11; Pius XII, Address to Catholic Jurists on the Community of States and of Peoples (6 December 1953) 2: AAS 45 (1953), 395-396; John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 289.
[888] Cf. John Paul II, Address to the Fiftieth General Assembly of the United Nations (5 October 1995), 9-10: L’Osservatore Romano, English edition, 11 October 1995, p. 9.
[889] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 289-290; John Paul II, Address to the Fiftieth General Assembly of the United Nations (5 October 1995), 15: L’Osservatore Romano, English edition, 11 October 1995, p. 10.
[890] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 15: AAS 80 (1988), 528-530.
[891] Cf. John Paul II, Address to UNESCO (2 June 1980), 14: L’Osservatore Romano, English edition, 23 June 1980, p. 11.
[892] John Paul II, Address to the Fiftieth General Assembly of the United Nations (5 October 1995), 14: L’Osservatore Romano, English edition, 11 October 1995, p. 10; cf. also John Paul II, Address to the Diplomatic Corps (13 January 2001), 8: L’Osservatore Romano, English edition, 17 January 2001, p. 2.
[893] John Paul II, Address to the Fiftieth General Assembly of the United Nations (5 October 1995), 6: L’Osservatore Romano, English edition, 11 October 1995, p. 8.
[894] Pius XII Christmas Radio Message (24 December 1941 ): AAS 34 (1942) 16.
[895] John Paul II, Address to the Fiftieth General Assembly of the United Nations (5 October 1995), 3: L’Osservatore Romano, English edition, 11 October 1995, p. 8.
[896] John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 277.
[897] Cf. Pius XII, Encyclical Letter Summi Pontificatus: AAS 31 (1939) 438-439; Pius XII, Christmas Radio Message (24 December 1941): AAS 34 (1942) 16-17; John XXIII Encylical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 290, 292.
[898] John Paul II, Address to the Diplomatic Corps (12 January 1991), 8: L’Osservatore Romano, English edition, 14 January 1991, p. 3.
[899] John Paul II, Message for the 2004 World Day of Peace, 5: AAS 96 (2004), 116.
[900] John Paul II, Message for the 2004 World Day of Peace, 5: AAS 96 (2004), 117; cf. also John Paul II, Message to the Rector of the Pontifical Lateran University (21 March 2002), 6: L’Osservatore Romano, 22 March 2002, p. 6.
[901] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 23: AAS 83 (1991), 820-821.
[902] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 18: AAS 83 (1991), 816.
[903] Cf. Charter of the United Nations (26 June 1945), art. 2.4; John Paul II, Message for the 2004 World Day of Peace, 6: AAS 96 (2004), 117.
[904] Cf. Pius XII, Christmas Radio Message (24 December 1941): AAS 34 (1942), 18.
[905] Cf. Pius XII, Christmas Radio Message (24 December 1945): AAS 38 (1946), 22; John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 287-288.
[906] John Paul II, Address to the International Court of Justice, The Hague (13 May 1985), 4: AAS 78 (1986), 520.
[907] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 52: AAS 83 (1991), 858.
[908] John Paul II, Message for the 2004 World Day of Peace, 9: AAS 96 (2004), 120.
[909] John Paul II, Message for the 2004 World Day of Peace, 7: AAS 96 (2004), 118.
[910] Cf. John XIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 426, 439; John Paul II, Address to the 20th General Conference of FAO (12 November 1979), 6: L’Osservatore Romano, English edition, 26 November 1979, p. 6; John Paul II, Address to UNESCO (2 June 1980), 5, 8: L’Osservatore Romano, English edition, 23 June 1980, pp. 9-10; John Paul II, Address to the Council of Ministers of the Conference on Security and Cooperation in Europe (CSCE) (30 November 1993), 3, 5: L’Osservatore Romano, English edition, 8 December 1993, pp. 1-2.
[911] Cf. John Paul II, Message to Nafis Sadik, Secretary General of the 1994 International Conference on Population and Development (18 March 1994): AAS 87 (1995), 191-192; John Paul II, Message to Gertrude Mongella, Secretary General of the United Nations Fourth World Conference on Woman (26 May 1995): L’Osservatore Romano, English edition, 31 May 1995, p. 2.
[912] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 84: AAS 58 (1966), 1107-1108.
[913] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 82: AAS 58 (1966), 1105; cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 293; Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 78: AAS 59 (1967), 295.
[914] John Paul II, Message for the 2003 World Day of Peace, 6: AAS 95 (2003), 344.
[915] John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 294-295.
[916] Cf. Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 51-55 and 77-79: AAS 59 (1967), 282-284, 295-296.
[917] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 43: AAS 80 (1988), 575.
[918] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 43: AAS 80 (1988), 575; cf. John Paul II, Message for the 2004 World Day of Peace, 7: AAS 96 (2004), 118.
[919] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 58: AAS 83 (1991), 863-864.
[920] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 33, 39: AAS 80 (1988), 557-559, 566-568.
[921] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 26: AAS 80 (1988), 544-547.
[922] John Paul II, Message for the 2004 World Day of Peace, 7: AAS 96 (2004), 118.
[923] Cf. Code of Canon Law, canon 361.
[924] Paul VI, Apostolic Letter Sollicitudo Omnium Ecclesiarum: AAS 61 (1969), 476.
[925] John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 499; cf. Pius XII, Christmas Radio Message (24 December 1945): AAS 38 (1946), 22.
[926] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 16: AAS 80 (1988), 531.
[927] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 36-37, 39: AAS 80 (1988), 561 564, 567.
[928] Cf. Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 22: AAS 59 (1967), 268; Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 43: AAS 63 (1971), 431-432; John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 32-33: AAS 80 (1988), 556-559; John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 35: AAS 83 (1991), 836-838; cf. also Paul VI, Address to the International Labour Organisation (10 June 1969), 22: AAS 61 (1969), 500-501; John Paul II, Address to the Participants in the European Convention on the Church’s Social Teaching (20 June 1997), 5: L’Osservatore Romano, English edition, 23 July 1997, p. 3; John Paul II, Address to Italian Business and Trade-Union Leaders (2 May 2000), 3: L’Osservatore Romano, English edition, 10 May 2000, p. 5.
[929] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 32: AAS 80 (1988), 556.
[930] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 33: AAS 83 (1991), 835.
[931] Cf. Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 56-61: AAS 59 (1967), 285-287.
[932] Cf. Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 44: AAS 59 (1967), 279.
[933] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 34: AAS 83 (1991), 836.
[934] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 58: AAS 83 (1991), 863.
[935] John Paul II, Message for the 2000 World Day of Peace, 14: AAS 92 (2000), 366; cf. John Paul II, Message for the 1993 World Day of Peace, 1: AAS 85 (1993), 429-430.
[936] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 33: AAS 80 (1988), 558; cf. Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 47: AAS 59 (1967), 280.
[937] Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 6: AAS 59 (1967), 260; cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 28: AAS 80 (1988), 548-550.
[938] Cf. Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 20-21: AAS 59 (1967), 267-268.
[939] Cf. John Paul II, Address to the Third General Conference of Latin American Bishops, Puebla, Mexico (28 January 1979), I/8: AAS 71 (1979), 194-195.
[940] Cf. Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 22: AAS 59 (1967), 268.
[941] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 38: AAS 80 (1988), 566.
[942] Cf. Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 55: AAS 59 (1967), 284; John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 44: AAS 80 (1988), 575-577.
[943] John Paul II, Message for the World Day of Peace 2000, 14: AAS 92 (2000), 366.
[944] Cf. John Paul II, Apostolic Letter Tertio Millennio Adveniente, 51: AAS 87 (1995), 36; John Paul II, Message for the 1998 World Day of Peace , 4: AAS 90 (1998), 151-152; John Paul II, Address to the Conference of the Inter-Parliamentarian Union (30 November 1998): Insegnamenti di Giovanni Paolo II, XXI, 2 (1998), 1162-1163; John Paul II, Message for the 1999 World Day of Peace, 9: AAS 91 (1999), 383-384.
[945] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 35: AAS 83 (1991), 838; cf. also the document At the Service of the Human Community: an Ethical Approach to the International Debt Question, published by the Pontifical Commission “Iustitia et Pax” (27 December 1986), Vatican City 1986.
[946] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 15: AAS 58 (1966), 1036.
[947] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 15: AAS 58 (1966), 1036.
[948] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 33: AAS 58 (1966), 1052.
[949] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 34: AAS 58 (1966), 1052.
[950] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 34: AAS 58 (1966), 1053.
[951] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 34: AAS 58 (1966), 1053.
[952] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 35: AAS 58 (1966), 1053.
[953] Cf. John Paul II, Address given at Mercy Maternity Hospital, Melbourne (28 November 1986): L’Osservatore Romano, English edition, 9 December 1986, p. 13.
[954] John Paul II, Meeting with scientists and representatives of the United Nations University, Hiroshima (25 February 1981), 3: AAS 73 (1981), 422.
[955] John Paul II, Meeting with employees of the Olivetti workshops in Ivrea, Italy (19 March 1990), 5: L’Osservatore Romano, English edition, 26 March 1990, p. 7.
[956] John Paul II, Address to the Pontifical Academy of Sciences (3 October 1981), 3: L’Osservatore Romano, English edition, 12 October 1981, p. 4.
[957] John Paul II, Address to the participants in a convention sponsored by the National Academy of Sciences, for the bicentenary of its foundation (21 September 1982), 4: L’Osservatore Romano, English edition, 4 October 1982, p. 3.
[958] John Paul II, Meeting with scientists and representatives of the United Nations University, Hiroshima (25 February 1981), 3: AAS 73 (1981), 422.
[959] John Paul II, Meeting with employees of the Olivetti workshops in Ivrea, Italy (19 March 1990), 4: L’Osservatore Romano, English edition, 26 March 1990, p. 7.
[960] John Paul II, Homily during Mass at the Victorian Racing Club, Melbourne (26 November 1986), 11: Insegnamenti di Giovanni Paolo II, IX, 2 (1986), 1730.
[961] John Paul II, Address to the Pontifical Academy of Sciences (23 October 1982), 6: Insegnamenti di Giovanni Paolo II, V, 3 (1982), 892-893.
[962] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 34: AAS 80 (1988), 559.
[963] John Paul II, Message for the 1990 World Day of Peace, 7: AAS 82 (1990), 151.
[964] John Paul II, Message for the 1990 World Day of Peace, 6: AAS 82 (1990), 150.
[965] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 37: AAS 83 (1991), 840.
[966] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 37: AAS 83 (1991), 840.
[967] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 37: AAS 83 (1991), 840.
[968] John Paul II, Address to the 35th General Assembly of the World Medical Association (29 October 1983): L’Osservatore Romano, English edition, 5 December 1986, p. 11.
[969] Cf. Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 21: AAS 63 (1971), 416-417.
[970] Paul VI, Apostolic Letter Octogesimo Adveniens, 21: AAS 63 (1971), 417.
[971] John Paul II, Address to participants in a convention on “The Environment and Health” (24 March 1997), 2: L’Osservatore Romano, English edition, 9 April 1997, p. 2.
[972] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 28: AAS 80 (1988), 548-550.
[973] Cf., for example, Pontifical Council for Culture - Pontifical Council for Interreligious Dialogue, Jesus Christ the Bearer of the Water of Life. A Christian Reflection on the ‘‘New Age’’, Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2003, p. 33.
[974] John Paul II, Address to participants in a convention on “The Environment and Health” (24 March 1997), 5: L’Osservatore Romano, English edition, 9 April 1997, p. 2.
[975] John Paul II, Address to participants in a convention on “The Environment and Health” (24 March 1997), 4: L’Osservatore Romano, English edition, 9 April 1997, p. 2.
[976] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 38: AAS 83 (1991), 841.
[977] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 34: AAS 80 (1988), 559-560.
[978] John Paul II, Address to participants in a convention on “The Environment and Health” (24 March 1997), 5: L’Osservatore Romano, English edition, 9 April 1997, p. 2.
[979] Cf. John Paul II, Encyclcal Letter Centesimus Annus, 40: AAS 83 (1991), 843.
[980] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 34: AAS 80 (1988), 559.
[981] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 34: AAS 80 (1988), 559.
[982] John Paul II, Apostolic Exhortation Ecclesia in America, 25: AAS 91 (1999) 760.
[983] Cf. John Paul II, Homily in Val Visdende (Italy) for the votive feast of St John Gualberto (12 July 1987): Insegnamenti di Giovanni Paolo II, X, 3 (1987) 67.
[984] Paul II, Encyclical Letter Populorum Progressio, 17: AAS 59 (1967), 266.
[985] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 37: AAS 83 (1991), 840.
[986] John Paul II, Message for the 1990 World Day of Peace, 9: AAS 82 (1990), 152.
[987] John Paul II, Address to the European Commission and Court of Human Rights, Strasbourg (8 October 1988), 5: AAS 81 (1989), 685; cf. John Paul II, Message for the 1999 World Day of Peace, 10: AAS 91 (1999), 384-385.
[988] Cf. John Paul II, Message for the 1999 World Day of Peace, 10: AAS 91 (1999), 384-385.
[989] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 26: AAS 80 (1988), 546.
[990] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis,34: AAS 80 (1988), 559-560.
[991] John Paul II, Address to the Twenty-Fifth General Conference of FAO (16 November 1989), 8: AAS 82 (1990), 673.
[992] Cf. John Paul II, Address to a study group of the Pontifical Academy of Sciences (6 November 1987): Insegnamenti di Giovanni Paolo II, X, 3 (1987) 1018-1020.
[993] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 40: AAS 83 (1991), 843.
[994] Cf. John Paul II, Address to the participants at the Plenary Assembly of the Pontifical Academy of Sciences (28 October 1994): Insegnamenti di Giovanni Paolo II, XVII, 2 (1994) 567-568.
[995] Cf. John Paul II, Address to the participants at a Symposium on physics (18 December 1992): Insegnamenti di Giovanni Paolo II, V, 3 (1982), 1631-1634.
[996] Cf. John Paul II, Address to the Indigenous Peoples of the Amazon, Manaus (10 July 1980): AAS 72 (1980), 960-961.
[997] Cf. John Paul II, Homily at the Liturgy of the Word with the Indigenous Peoples of the Peruvian Amazon Valley (5 February 1985), 4: AAS 77 (1985), 897-898; cf. also Pontifical Council for Justice and Peace, Towards a Better Distribution of Land: The Challenge of Agrarian Reform (23 November 1997), 11, Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 1997, p. 17.
[998] Cf. John Paul II, Address to the Indigenous Peoples of Australia (29 November 1986), 4: AAS 79 (1987), 974-975.
[999] Cf. John Paul II, Address to the Indigenous Peoples of Guatemala (7 March 1983), 4: AAS 75 (1983), 742-743; John Paul II, Address to the Indigenous Peoples of Canada (18 September 1984), 7-8: AAS 77 (1988), 421-422; John Paul II, Address to the Indigenous Peoples of Ecuador (31 January 1985), II,1: AAS 77 (1985), 861; John Paul II, Address to the Indigenous Peoples of Australia (29 November 1986), 10: AAS 79 (1987), 976-977.
[1000] Cf. John Paul II, Address to the Indigenous Peoples of Australia (29 November 1986), 4: AAS 79 (1987), 974-975; John Paul II, Address to Native Americans (14 September 1987), 4: L’Osservatore Romano, English edition, 21 September 1987, p. 21.
[1001] Cf. Pontifical Academy for Life, Animal and Plant Biotechnology: New Frontiers and New Responsibilities, Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 1999.
[1002] Cf. John Paul II, Address to the Pontifical Academy of Sciences (23 October 1982), 6: Insegnamenti di Giovanni Paolo II, V, 3 (1982), 892-893.
[1003] Cf. John Paul II, Address to the Pontifical Academy of Sciences (3 October 1981): AAS 73 (1981), 668-672.
[1004] Cf. John Paul II, Address to the Pontifical Academy of Sciences (23 October 1982): Insegnamenti di Giovanni Paolo II, V, 3 (1982), 889-893. John Paul II, Address to the participants in a convention sponsored by the National Academy of Sciences, for the bicentenary of its foundation (21 September 1982): Insegnamenti di Giovanni Paolo II, V, 3 (1982), 511-515.
[1005] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 69: AAS 58 (1966), 1090-1092; Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 22: AAS 59 (1967), 268.
[1006] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 25: AAS 80 (1988), 543; cf. John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 16: AAS 87 (1995), 418.
[1007] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 25: AAS 80 (1988), 543-544.
[1008] John Paul II, Message to Nafis Sadik, Secretary General of the 1994 International Conference on Population and Development (18 March 1994), 3: AAS 87 (1995), 191.
[1009] John Paul II, Message to Cardinal Geraldo Majella Agnelo on the occasion of the 2004 Brotherhood Campaign of the Brazilian Bishops’ Conference (19 January 2004): L’Osservatore Romano, English edition, 17 March 2004, p. 3.
[1010] John Paul II, Message to Cardinal Geraldo Majella Agnelo on the occasion of the 2004 Brotherhood Campaign of the Brazilian Bishops’ Conference (19 January 2004): L’Osservatore Romano, English edition, 17 March 2004, p. 3.
[1011] Cf. John Paul II, John Paul II, Message for the 2003 World Day of Peace, 5: AAS 95 (2003), 343; Pontifical Council for Justice and Peace, Water, an Essential Element for Life. A Contribution of the Delegation of the Holy See on the occasion of the 3rd World Water Forum, Kyoto, 16-23 March 2003.
[1012] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 36: AAS 83 (1991), 838-840.
[1013] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 36: AAS 83 (1991), 839.
[1014] Cf. John Paul II, Address to the UN Centre, Nairobi, Kenya (18 August 1985), 5: AAS 78 (1986), 92.
[1015] Cf. John Paul II, Message for the 1986 World Day of Peace, 1: AAS 78 (1986), 278-279 .
[1016] Cf. Paul VI, Message for the 1969 World Day of Peace: AAS 60 (1968), 771; John Paul II, Message for the 2004 World Day of Peace, 4: AAS 96 (2004), 116.
[1017] John Paul II, Message for the 1982 World Day of Peace 4: AAS 74 (1982), 328.
[1018] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 78: AAS 58 (1966), 1101-1102.
[1019] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 51: AAS 83 (1991), 856-857.
[1020] Cf. Paul VI, Message for the 1972 World Day of Peace: AAS 63 (1971), 868.
[1021] Cf. Paul VI, Message for the 1969 World Day of Peace: AAS 60 (1968) 772; John Paul II, Message for the 1999 World Day of Peace, 12: AAS 91 (1999), 386-387.
[1022] Pius XI, Encyclical Letter Ubi Arcano: AAS 14 (1922), 686. In the Encyclical, reference is made to Saint Thomas Aquinas, Summa Theologiae, II-II, q. 29, a. 3, ad 3um: Ed. Leon. 8, 238; cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 78: AAS 58 (1966), 1101-1102.
[1023] Cf. Paul VI, Encylical Letter Populorum Progressio, 76: AAS 59 (1967), 294-295.
[1024] Cf. Paul VI, Message for the 1974 World Day of Peace: AAS 65 (1973), 672.
[1025] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2317.
[1026] John Paul II, Address to the Diplomatic Corps (13 January 1997), 3: L’Osservatore Romano, English edition, 15 January 1997, pp. 6-7.
[1027] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 78: AAS 58 (1966), 1101; cf. Catechism of the Catholic Church, 2304.
[1028] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 78: AAS 58 (1966), 1101.
[1029] John Paul II, Address at Drogheda, Ireland (29 September 1979), 9: AAS 71 (1979), 1081; cf. Paul VI, Apostolic Exhortation Evangelii Nuntiandi, 37: AAS 68 (1976), 29.
[1030] Cf. John Paul II, Address to the Pontifical Academy of Sciences (12 November 1983), 5: AAS 76 (1984), 398-399.
[1031]  Catechism of the Catholic Church, 2306.
[1032] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 77: AAS 58 (1966), 1100; cf. Catechism of the Catholic Church, 2307-2317.
[1033] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 80: AAS 58 (1966), 1103-1104.
[1034] John XXIII, Encylical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 291.
[1035] Leo XIII, Address to the College of Cardinals: Acta Leonis XIII, 19 (1899), 270-272.
[1036] John Paul II, Meeting with Officials of the Roman Vicariate (17 January 1991): L’Osservatore Romano, English edition, 21 January 1991, p. 1; cf. John Paul II, Address to the Latin-Rite Bishops of the Arabian Peninsula (1 October 1990), 4: AAS 83 (1991), 475.
[1037] Cf. Paul VI, Address to Cardinals (24 June 1965): AAS 57 (1965) 643-644.
[1038] Benedict XV, Appeal to the Leaders of the Warring Nations (1 August 1917): AAS 9 (1917), 423.
[1039] John Paul II, Prayer for peace during General Audience (16 January 1991): Insegnamenti di Giovanni Paolo II, XIV, 1 (1991), 121.
[1040] Pius XII, Radio Message (24 August 1939): AAS 31 (1939) 334; John Paul II, Message for the 1993 World Day of Peace, 4: AAS 85 (1993), 433-434; cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 288.
[1041] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes 79: AAS 58 (1966), 1102-1103.
[1042] John Paul II, Message for the 1999 World Day of Peace, 11: AAS 91 (1999), 385.
[1043] John Paul II, Address to the Diplomatic Corps (13 January 2003), 4: L’Osservatore Romano, English edition, 15 January 2003, p. 3.
[1044] Paul VI, Address to the General Assembly of the United Nations (4 October 1965), 5: AAS 57 (1965), 881.
[1045] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 51: AAS 83 (1991), 857.
[1046] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 52: AAS 83 (1991), 858.
[1047] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 288-289.
[1048] John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 291.
[1049] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2265.
[1050]  Catechism of the Catholic Church, 2309.
[1051] Pontifical Council for Justice and Peace, The International Arms Trade. An ethical reflection (1 May 1994), ch. 1, 6: Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 1994, p. 13.
[1052] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 79: AAS 58 (1966), 1103.
[1053] John Paul II, Message for the 2004 World Day of Peace, 6: AAS 96 (2004), 117.
[1054] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 79: AAS 58 (1966), 1102-1103; Catechism of the Catholic Church, 2310.
[1055] Cf. John Paul II, Message to the Third International Meeting of Military Ordinaries (11 March 1994), 4: AAS 87 (1995), 74.
[1056] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2313.
[1057] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 79: AAS 58 (1966), 1103; cf. Catechism of the Catholic Church, 2311.
[1058] John Paul II, Sunday Angelus (7 March 1993), 4: L’Osservatore Romano, English edition, 10 March 1993, p. 1; John Paul II, Address to the OSCE Council of Ministers (30 November 1993), 4: AAS 86 (1994), 751.
[1059] John Paul II, Address at General Audience (11 August 1999), 5: L’Osservatore Romano, English edition, 25 August 1999, p. 6.
[1060] John Paul II, 1990 Message for Lent, 3: L’Osservatore Romano, English edition, 12 February 1990, p. 5.
[1061] Cf. John Paul II, Message for the 1999 World Day of Peace, 7: AAS 91 (1999), 382; John Paul II, Message for the 2000 World Day of Peace, 7: AAS 92 (2000), 362.
[1062] John Paul II, Address at the Regina Coeli (18 April 1993), 3: L’Osservatore Romano, English edition, 21 April 1993, p. 12; cf. Commission for Religious Relations with Judaism, We Remember. A Reflection on the Shoah (16 March 1998), Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 1998.
[1063] John Paul II, Message for the 2000 World Day of Peace, 11: AAS 92 (2000), 363.
[1064] Cf. John Paul II, Address to the Diplomatic Corps (16 January 1993), 13: L’Osservatore Romano, English edition, 20 January 1993, p. 9; cf. John Paul II, Address to the International Conference on Nutrition sponsored by FAO and WHO (5 December 1992), 3: AAS 85 (1993), 922-923; John Paul II, Message for the 2004 World Day of Peace, 9: AAS 96 (2004), 120.
[1065] Cf. John Paul II, Sunday Angelus (14 June 1998): L’Osservatore Romano, English edition, 17 June 1998, p. 1; John Paul II, Address to participants in the World Congress on Pastoral Promotion of Human Rights (4 July 1998), 5: L’Osservatore Romano, English edition, 29 July 1998, p. 8; John Paul II, Message for the 1999 World Day of Peace, 7: AAS 91 (1999), 382; cf. also Pius XII, Address at the Sixth International Congress of Criminal Law (3 October 1953): AAS 45 (1953), 730-744.
[1066] Cf. John Paul II, Address to the Diplomatic Corps (9 January 1995), 7: L’Osservatore Romano, English edition, 11 January 1995, p. 6.
[1067] John Paul II, Message for the fortieth anniversary of the United Nations (14 October 1985), 6: L’Osservatore Romano, English edition, 14 November 1985, p. 4.
[1068] Cf. Pontifical Council for Justice and Peace, The International Arms Trade. An ethical reflection (1 May 1994), ch. 1, 9-11, Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 1994, p. 14.
[1069] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2316; John Paul II, Address to the World of Work, Verona, Italy (17 April 1988), 6: Insegnamenti di Giovanni Paolo II, XI, 1 (1988), 940.
[1070]  Catechism of the Catholic Church, 2315.
[1071] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 80: AAS 58 (1966), 1104; Catechism of the Catholic Church, 2314; John Paul II, Message for the 1986 World Day of Peace, 2: AAS 78 (1986), 280.
[1072] Cf. John Paul II, Address to the Diplomatic Corps (13 January 1996), 7: L’Osservatore Romano, English edition, 17 January 1996, p. 2.
[1073] The Holy See is a party to juridical instruments dealing with nuclear, biological and chemical weapons in order to support such initiatives of the international community.
[1074] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 80: AAS 58 (1966), 1104.
[1075] Cf. John Paul II, Message for the 1999 World Day of Peace, 11: AAS 91 (1999), 385-386.
[1076] Cf. John Paul II, Message for the 1999 World Day of Peace, 11: AAS 91 (1999), 385-386.
[1077] Cf. John Paul II, Message for the 1999 World Day of Peace, 11: AAS 91 (1999), 385-386.
[1078] Cf. Catechism of the Catholic Church, 2297.
[1079] Cf. John Paul II, Message for the 2002 World Day of Peace, 4: AAS 94 (2002), 134.
[1080] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 79: AAS 58 (1966), 1102.
[1081] John Paul II, Message for the 2002 World Day of Peace, 5: AAS 94 (2002), 134.
[1082] Cf. John Paul II, Message for the 2004 World Day of Peace, 8: AAS 96 (2004), 119.
[1083] John Paul II, Message for the 2004 World Day of Peace, 8: AAS 96 (2004), 119.
[1084] John Paul II, Message for the 2004 World Day of Peace, 8: AAS 96 (2004), 119.
[1085] John Paul II, Message for the 2002 World Day of Peace, 5: AAS 94 (2002), 134.
[1086] Cf. John Paul II, Address to Representatives from the World of Culture, Art and Science , Astana, Kazakhstan (24 September 2001), 5: L’Osservatore Romano, English edition, 26 September 2001, p. 7.
[1087] Cf. John Paul II, Message for the 2002 World Day of Peace, 7: AAS 95 (2002), 135-136.
[1088] Cf. ‘‘Decalogue of Assisi for Peace,’’ 1, in the letter addressed by John Paul II to Heads of State and of Government on 24 February 2002: L’Osservatore Romano, English edition, 6 March 2002, p. 12.
[1089] John Paul II, Message for the 2000 World Day of Peace, 20: AAS 92 (2000), 369.
[1090] Cf. John Paul II, Message for the 1988 World Day of Peace, 3: AAS 80 (1988), 282-284.
[1091] Cf. John Paul II, Message for the 2004 World Day of Peace, 9: AAS 96 (2004), 120.
[1092] Cf. John Paul II Message for the 2002 World Day of Peace, 9: AAS 94 (2002), 136-137; John Paul II, Message for the 2004 World Day of Peace, 10: AAS 96 (2004), 121.
[1093] John Paul II, Letter on the occasion of the fiftieth anniversary of the outbreak of the Second World War (27 August 1989), 2: L’Osservatore Romano, English edition, 4 September 1989, p. 1.
[1094] Cf. John Paul II, Message for the 1997 World Day of Peace , 3 and 4: AAS 89 (1997), 193.
[1095] Cf. Pius XII, Address to the Sixth International Congress on Criminal Law (3 October 1953): AAS 65 (1953) 730-744; John Paul II, Address to the Diplomatic Corps (13 January 1997), 4: L’Osservatore Romano, English edition, 15 January 1997, p. 7. John Paul II, Message for the 1999 World Day of Peace, 7: AAS 91 (1999), 382.
[1096] Cf. John Paul II, Message for the 1997 World Day of Peace, 3, 4, 6: AAS 89 (1997), 193, 196-197.
[1097] John Paul II, Message for the 1999 World Day of Peace, 11: AAS 91 (1999), 385.
[1098] Cf. John Paul II, Message for the 1992 World Day of Peace, 4: AAS 84 (1992), 323-324.
[1099] Paul VI, Message for the 1968 World Day of Peace: AAS 59 (1967), 1098.
[1100] Second Vatican Ecumenical Council, Constitution Sacrosanctum Concilium, 10: AAS 56 (1964), 102.
[1101] Second Vatican Ecumenical Council, Constitution Lumen Gentium, 11: AAS 57 (1965), 15.
[1102] The eucharistic celebration begins with a greeting of peace, the greeting of Christ to his disciples. The Gloria is a prayer for peace for all the people of God on the earth. Prayer for peace is made through the anaphora at Mass: an appeal for the peace and unity of the Church, for the peace of the entire family of God in this life, for the advancement of peace and salvation in the world. During the communion rite the Church prays that the Lord will “grant us peace in our day” and remembers Christ’s gift that consists of his peace, invoking “the peace and unity of his Kingdom.” Before communion, the entire assembly exchanges a sign of peace and the assembly prays that the Lamb of God, who takes away the sins of the world will “grant us peace.” The eucharistic celebration concludes with the assembly being dismissed in the peace of Christ. There are many prayers that invoke peace for the world. In these, peace is sometimes associated with justice, for example, as in the opening prayer for the Eighth Sunday in Ordinary Time, in which the Church asks God to guide the course of world events in justice and peace, according to his will.
[1103] Paul VI, Message for the 1968 World Day of Peace: AAS 59 (1967), 1100.
[1104] Paul VI, Message for the 1976 World Day of Peace: AAS 67 (1975), 671.
[1105] Cf. Congregation for the Clergy, General Directory for Catechesis, 18, Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 1997, pp. 21-22.
[1106] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Redemptoris Missio, 11: AAS 83 (1991), 259-260.
[1107] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 5: AAS 83 (1991), 799.
[1108] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 5: AAS 83 (1991), 799.
[1109] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 22: AAS 58 (1966), 1043.
[1110] John Paul II, Encyclical Letter Redemptoris Missio, 52: AAS 83 (1991), 300; cf. Paul VI, Apostolic Exhortation Evangelii Nuntiandi, 20: AAS 68 (1976), 18-19.
[1111] John Paul II, Encyclical Letter Redemptoris Missio, 11: AAS 83 (1991), 259-260.
[1112] John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Christifideles Laici, 35: AAS 81 (1989), 458.
[1113] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 5: AAS 83 (1991), 800.
[1114] John Paul II; Encyclical Letter Redemptoris Missio, 11: AAS 83 (1991), 259.
[1115] Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 51: AAS 63 (1971), 440.
[1116] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 57: AAS 83 (1991), 862.
[1117] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 48: AAS 80 (1988), 583-584.
[1118] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 76: AAS 58 (1966), 1099-1100.
[1119] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 453; John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus 54: AAS 83 (1991), 859-860.
[1120] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Pacem in Terris: AAS 55 (1963), 265-266.
[1121] Cf. John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Christifideles Laici, 60: AAS 81 (1989), 511.
[1122] Cf. Congregation for the Clergy, General Directory for Catechesis, 30, Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 1997, pp. 30-32.
[1123] Cf. John Paul II, Apostolic Exhortation Catechesi Tradendae, 18: AAS 71 (1979), 1291-1292.
[1124] John Paul II, Apostolic Exhortation Catechesi Tradendae, 5: AAS 71 (1979), 1281.
[1125] Cf. Congregation for the Clergy, General Directory for Catechesis, 54, Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 1997, p. 54.
[1126] John Paul II, Apostolic Exhortation Catechesi Tradendae, 29: AAS 71 (1979), 1301-1302; cf. also Congregation for the Clergy, General Directory for Catechesis, 17, Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 1997, p. 21.
[1127] Second Vatican Ecumenical Council, Declaration Dignitatis Humanae, 8: AAS 58 (1966), 935.
[1128] John Paul II, Encyclical Letter Vertatis Splendoris, 107: AAS 85 (1993), 1217.
[1129] Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 81: AAS 59 (1967), 296-297.
[1130] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 75: AAS 58 (1966), 1097-1098.
[1131] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 75: AAS 58 (1966), 1098.
[1132] 30 December 1988, Vatican Polyglot Press, Rome 1988.
[1133] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Declaration Nostra Aetate, 4: AAS 58 (1966), 742-743.
[1134] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 32: AAS 80 (1988), 556-557.
[1135] 27 October 1986; 24 January 2002.
[1136] John Paul II, Encyclical Letter Redemptoris Missio, 2: AAS 83 (1991), 250.
[1137] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 3: AAS 83 (1991), 795.
[1138] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 3: AAS 83 (1991), 796.
[1139] Second Vatican Ecumenical Council, Dogmatic Constitution Lumen Gentium, 31: AAS 57 (1965), 37.
[1140] Second Vatican Ecumenical Council, Dogmatic Constitution Lumen Gentium, 31: AAS 57 (1965), 37.
[1141] John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Christifideles Laici, 15: AAS 81 (1989), 415.
[1142] Cf. John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Christifideles Laici, 24: AAS 81 (1989), 433-435.
[1143] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 76: AAS 58 (1966), 1099.
[1144] Second Vatican Ecumenical Council, Dogmatic Constitution Lumen Gentium, 31: AAS 57 (1965), 37-38.
[1145] John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Christifidelis Laici, 59: AAS 81 (1989), 509.
[1146] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1806.
[1147] The exercise of prudence calls for a progressive formation in order to acquire the necessary qualities: “memory” as the capacity to remember one’s own past experience with objectivity, without falsification (cf. Saint Thomas Aquinas Summa Theologiae, II-II, q. 49, a. 1: Ed. Leon. 8, 367); “docilitas” (docility) that allows one to learn from others and to profit from their experience on the basis of an authentic love for truth (cf. Saint Thomas Aquinas Summa Theologiae, II-II, q. 49, a. 3: Ed. Leon. 8, 368-369); “solertia” (diligence), that is, the ability to face the unexpected with objectivity in order to turn every situation to the service of good, overcoming the temptation of intemperance, injustice, and cowardice (cf. Saint Thomas Aquinas Summa Theologiae, II-II, q. 49, a. 4: Ed. Leon. 8, 369-370). These cognitive dispositions permit the development of the necessary conditions for the moment of decision: “providencia” (foresight), which is the capacity of weighing the efficacy of a given conduct for the attainment of a moral end (cf. Saint Thomas Aquinas Summa Theologiae, II-II, q. 49, a. 6: Ed. Leon. 8, 371) and “circumspectio” (circumspection), or the capacity of weighing the circumstances that contribute to the creation of the situation in which a given action will be carried out (cf. Saint Thomas Aquinas Summa Theologiae, II-II, q. 49, a. 7: Ed. Leon. 8, 372). In the social context, prudence can be specified under two particular forms: “regnative” prudence, that is, the capacity to order all things for the greatest good of society (cf. Saint Thomas Aquinas Summa Theologiae, II-II, q. 50, a. 1: Ed. Leon. 8, 374), and “political” prudence, which leads citizens to obey, carrying out the indications of authority (cf. Saint Thomas Aquinas Summa Theologiae, II-II, q. 50, a. 2: Ed. Leon. 8, 375), without compromising their dignity as a human person (cf. Saint Thomas Aquinas Summa Theologiae, II-II, qq. 47-56: Ed. Leon. 8, 348-406).
[1148] Cf. John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Christifideles Laici, 30: AAS 81 (1989), 446-448.
[1149] John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Christifideles Laici, 62: AAS 81 (1989), 516-517.
[1150] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961) 455.
[1151] John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Christifideles laici, 29: AAS 81 (1989), 443.
[1152] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 76: AAS 58 (1966), 1099.
[1153] Cf. John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961) 454; John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 57: AAS 83 (1991), 862-863.
[1154] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 91: AAS 58 (1966), 1113.
[1155] John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Christifideles Laici, 37: AAS 81 (1989), 460.
[1156] Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 218.
[1157] Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 218.
[1158] Cf. Congregation for the Doctrine of the Faith, Instruction Donum Vitae, (22 February 1987): AAS 80 (1988) 70-102.
[1159] John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Christifideles Laici, 39: AAS 81 (1989), 466.
[1160] Cf. John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Christifideles Laici, 39: AAS 81 (1989), 466.
[1161] Cf. John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Familiaris Consortio, 42-48: AAS 74 (1982), 134-140.
[1162] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 43: AAS 58 (1966), 1062.
[1163] John Paul II, Address to UNESCO (2 June 1980), 7: L’Osservatore Romano, English edition, 23 June 1980, p. 9.
[1164] Cf. Congregation for the Doctrine of the Faith, Doctrinal Note on Some Questions Regarding the Participation of Catholics in Political Life (24 November 2002), 7: Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2002, p. 15.
[1165] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 59: AAS 58 (1966), 1079-1080.
[1166] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 50: AAS 83 (1991), 856.
[1167] Cf. John Paul II, Address to UNESCO (2 June 1980), 11: L’Osservatore Romano, English edition, 23 June 1980, p. 10.
[1168] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 60: AAS 58 (1966), 1081.
[1169] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 61: AAS 58 (1966), 1082.
[1170] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 24: AAS 83 (1991), 822.
[1171] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 24: AAS 83 (1991), 821-822.
[1172] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Decree Inter Mirifica, 4: AAS 56 (1964), 146.
[1173] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Fides et Ratio, 36-48: AAS 91 (1999), 33-34.
[1174] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 55: AAS 83 (1991), 861.
[1175] John Paul II, Message for the 1999 World Day of Social Communications, 3: L’Osservatore Romano, English edition, 3 February 1999, pp. 1-2.
[1176]  Catechism of the Catholic Church, 2495.
[1177] Cf. Pontifical Council for Social Communications, Ethics in Communications (4 June 2000), 14, Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2000, pp. 14-16.
[1178] Cf. Pontifical Council for Social Communications, Ethics in Communications, 4 June 2000, 33, Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2000, p. 40.
[1179] Cf. Congregation for the Doctrine of the Faith, Doctrinal Note on Some Questions Regarding the Participation of Catholics in Political Life (24 November 2002), 3: Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2002, p. 8.
[1180] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 41: AAS 80 (1988), 570.
[1181] John Paul II, Message for the 2000 World Day of Peace, 14: AAS 92 (2000), 366.
[1182] Cf. John Paul II, Message for the 2000 World Day of Peace, 17: AAS 92 (2000), 367-368.
[1183] Cf. Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 46: AAS 63 (1971), 433-436 .
[1184] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 36: AAS 80 (1988), 561-563.
[1185] Congregation for the Doctrine of the Faith, Doctrinal Note on Some Questions Regarding the Participation of Catholics in Political Life (24 November 2002), 6: Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2002, p. 13.
[1186] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 46: AAS 83 (1991), 850.
[1187] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 74: AAS 58 (1966), 1095-1097.
[1188] Cf. Congregation for Catholic Education, Guidelines for the Study and Teaching of the Church’s Social Doctrine in the Formation of Priests, 8, Vatican Polyglot Press, Rome 1988, pp. 13-14.
[1189] Congregation for the Doctrine of the Faith, Doctrinal Note on Some Questions Regarding the Participation of Catholics in Political Life (24 November 2002), 7: Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2002, pp. 15-16.
[1190] Cf. John Paul II, Centesimus Annus, 46: AAS 83 (1991), 850-851.
[1191] Congregation for the Doctrine of the Faith, Doctrinal Note on Some Questions Regarding the Participation of Catholics in Political Life (24 November 2002), 4: Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2002, p. 9.
[1192] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Evangelium Vitae, 73: AAS 87 (1995), 486-487.
[1193] Cf. John Paul II, Post-Synodal Exhortation, Christifideles Laici, 39: AAS 81 (1989), 466-468.
[1194] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 76: AAS 58 (1966), 1099-1100.
[1195] Congregation for the Doctrine of the Faith, Doctrinal Note on Some Questions Regarding the Participation of Catholics in Political Life (24 November 2002), 6: Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2002, p. 11.
[1196] Congregation for the Doctrine of the Faith, Doctrinal Note on Some Questions Regarding the Participation of Catholics in Political Life (24 November 2002), 6: Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2002, p. 12.
[1197] Congregation for the Doctrine of the Faith, Doctrinal Note on Some Questions Regarding the Participation of Catholics in Political Life (24 November 2002), 6: Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2002, pp. 12-13.
[1198] John Paul II, Address to the Diplomatic Corps (12 January 2004), 3: L’Osservatore Romano, English edition, 21 January 2004, p. 3.
[1199] Congregation for the Doctrine of the Faith, Doctrinal Note on Some Questions Regarding the Participation of Catholics in Political Life (24 November 2002), 6: Libreria Editrice Vaticana, Vatican City 2002, p. 14.
[1200] Cf. Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 46: AAS 63 (1971), 433-435.
[1201] Cf. Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 46: AAS 63 (1971), 433-435.
[1202] Cf. Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 50: AAS 63 (1971), 439-440.
[1203] Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 4: AAS 63 (1971), 403-404.
[1204] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 43: AAS 58 (1966), 1063.
[1205] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 43: AAS 58 (1966), 1063.
[1206] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 41: AAS 58 (1966), 1059.
[1207] John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 451.
[1208] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 41: AAS 58 (1966), 1059.
[1209] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 41: AAS 58 (1966), 1059-1060.
[1210] Pius XII, Encyclical Letter Summi Pontificatus: AAS 31 (1939), 425.
[1211] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 55: AAS 83 (1991), 860-861.
[1212] John Paul II, Encyclical Letter Veritatis Splendor, 98: AAS 85 (1993), 1210; cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 24: AAS 83 (1991), 821-822.
[1213] John Paul II, Apostolic Letter Novo Millennio Ineunte, 29: AAS 93 (2001), 285.
[1214] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 47: AAS 80 (1988), 580.
[1215] John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961), 541.
[1216] Second Vatican Ecumenical Council, Dogmatic Constitution Lumen Gentium, 35: AAS 57 (1965), 40.
[1217] John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 10: AAS 83 (1991), 805-806.
[1218] John Paul II, Encyclical Letter Sollicitudo Rei Socialis, 40: AAS 80 (1988), 568.
[1219] Second Vatican Ecumenical Council, Pastoral Constitution Gaudium et Spes, 38: AAS 58 (1966), 1055-1056; cf. Second Vatican Ecumenical Council, Dogmatic Constitution Lumen Gentium, 42: AAS 57 (1965), 47-48; Catechism of the Catholic Church, 826.
[1220] Cf. Catechism of the Catholic Church, 1889.
[1221] Leo XIII, Encyclical Letter Rerum Novarum: Acta Leonis XIII, 11 (1892), 143; cf. Benedict XV, Encyclical Letter Pacem Dei: AAS 12 (1920), 215.
[1222] Cf. Saint Thomas Aquinas, QD De caritate, a. 9, c; Pius XI, Encyclical Letter Quadragesimo Anno: AAS 23 (1931), 206-207; John XXIII, Encyclical Letter Mater et Magistra: AAS 53 (1961) 410; Paul VI, Address to FAO (16 November 1970), 11: AAS 62 (1970), 837-838; John Paul II, Address to the Members of the Pontifical Commission “Iustitia et Pax” (9 February 1980), 7: AAS 72 (1980), 187.
[1223] Cf. Paul VI, Apostolic Letter Octogesima Adveniens, 46: AAS 63 (1971), 433-435.
[1224] Cf. Second Vatican Ecumenical Council, Decree Apostolicam Actuositatem, 8: AAS 58 (1966), 844-845; Paul VI, Encyclical Letter Populorum Progressio, 44: AAS 59 (1967), 279; John Paul II, Post-Synodal Apostolic Exhortation Christifideles Laici, 42: AAS 81 (1989), 472-476; Catechsim of the Catholic Church, 1939.
[1225] John Paul II, Encyclical Letter Redemptor Hominis, 15: AAS 71 (1979), 288.
[1226] John Paul II, Encyclical Letter Dives in Misericordia, 14: AAS 72 (1980), 1223.
[1227] John Paul II, Message for the 2004 World Day of Peace, 10: AAS 96 (2004), 121; cf. John Paul II, Encyclical Letter Dives in Misericordia, 14: AAS 72 (1980), 1224; Catechism of the Catholic Church, 2212.
[1228] Saint John Chrysostom, Homilia De Perfecta Caritate, 1, 2: PG 56, 281-282.
[1229] Cf. John Paul II, Apostolic Letter Novo Millennio Ineunte, 49-51: AAS 93 (2001), 302-304.
[1230] Cf. John Paul II, Encyclical Letter Centesimus Annus, 5: AAS 83 (1991), 798-800.
[1231]  Catechism of the Catholic Church, 1889.
[1232] Saint Thérèse of the Child Jesus, Act of Offering in Story of a Soul, tr. John Clarke (Washington, D.C.: ICS 1981, p. 277), as quoted in Catechism of the Catholic Church, 2011.